Professional Documents
Culture Documents
Muundo
Muundo
Bahari za Ushairi
Bahari za ushairi ni nyingi sana. Shairi huainishwa katika bahari fulani kulingana na mtindo
wake, umbo lake na matumizi ya lugha.
3. Ukawafi – ni shairi la vipande vitatu (ukwapi, utao na mwandamo) katika kila mshororo.
4. Bantudi – Shairi la vipande vinne (ukwapi, utao, mwandamo na ukingo) katika kila
mshororo.
5. Ukaraguni – shairi ambalo vina vyake vya kati na vya mwisho hubadilika kutoka ubetio
mmoja hadi mwingine.
6. Ukara – shairi ambalo vina vya kipande kimoja havibadiliki kutoka ubeti mmoja hadi
mwingine, lakini vina vya kipande kingine hubadilika. Kwa mfano, vina vya kati
vinafanana kutoka ubeti wa kwanza hadi wa mwisho lakini vina vya kipande cha mwisho
vinabadilika kutoka ubeti mmoja hadi mwingine.
7. Mtiririko – shairi ambalo vina vyake vya mwisho na vya kati havibadiliki kutoka ubeti
wa kwanza hadi wa mwisho.
kwa mfano vina vikiwa ( —ni, —ka) kutoka ubeti wa kwanza hadi wa mwisho.
8. Mkufu/pindu – Shairi ambalo neno la mwisho au kifungu cha mwisho cha maneno
katika ubeti mmoja, hutangulia katika ubeti unaofuatia.
10. Kikai – Shairi lenye kipande kimoja kifupi (chenye mizani chache kuliko kingine) Mfano
(8,4)
Tathmina/umoja
Ni shairi lenye mshororo mmoja kaka kila ube. Mashairi ya aina hii hayapakani kwa
wingi. Vielelezo vifuatavyo vinaashiria aina hii ya shairi.
Tathnia/uwili
Ni shairi lenye mishororo miwili katika kila ubeti. Mashairi haya ingawaje yapo, lakini pia kwa
uchache
Tathlitha/utatu/wimbo
Ni shairi lenye mishororo mitatu katika kila ubeti. Shairi la aina hii wakati mwingine pia huitwa
wimbo. tazama shairi lifuatalo;
Tarbia/unne
Ni shairi lenye mishororo minne katka kila ubeti. Mashairi mengi ambayo yametungwa huwa ni
ya aina hii. Mfano ni kama ufuatao;
Tasdisa/usita
Ni shairi lenye mishororo sita katika kila ubeti. Tazama shairi linalofuata ambalo pia wakati
mwingine hujulikana kama tashlita.
Ewe hisia!
Umeniamshia ndoto niloisahau zamani
Umelimsha mwangu moyoni
nyimbo ya kale
na mdundo usomvutia
ila hayawani wa mwangu rohoni.
Ukumi– ni shairi lenye mishororo kumi katika kila ubeti. Pia shairi hili huitwa ushuri.
Bahari nyingine
Malumbano – Mashairi mawili ambapo mshairi mmoja hutunga shairi akijibu au kupinga utunzi
wa mshairi mwengine.
Ngonjera – Shairi lenye wahusika wawili wanaojibizana. K.m. Ubeti wa kwanza, mwalimu, na
wa pili, mwanafunzi.
Masivina- Ni bahari la shairi lisilo na urari wa vina katika mishororo yake. Hii ina maana kuwa
vina vyake vyote aidha vya kati au vya nje vinatofautiana baina ya mishororo. Vielelezo
vifuatavyo vinaelezea mfano wa bahari hii ya shairi.
Matapeli
Salamu naanza mimi, niwajuvye walimwengu
Muyatege masikiyo, uneni pate lipuka
Pia mutiye manani, asilani musipuze
Kina matapeli ndugu, hutokea kama njozi.
Taabili
Ni shairi ambalo limetungwa kwa nia ya kumsifu mtu aliyeaga dunia.
Mandhuma
Ni bahari ya shairi ambalo upande mmoja (ukwapi) hueleza hoja au huuliza swali na kisha
upande wa pili (utao) hutoa jibu au suluhu ya swali hilo.
Kisarambe
Ni shairi ambalo haswa limejikita kwa maudhui ya kidini. Huweza kuitwa pia
kasida
Sabilia
Ni shairi ambalo halina kibwagizo bali huwa na mstari wa kituo/kiishio/kimalizio.
Togoo
Ni aina ya shairi ambalo limetungwa kwa kusudi la kusifia uzuri wa mahali, mtu au kitu fulani.
Kumbukizi
Ni aina ya shairi ambalo huwakumbusha watu kuhusu matukio mahsusi katika jamii. Matukio
haya yaweza kuwa ya kihistoria, kidini au hata kishujaa. Kwa mfano ujio wa Rais wa Marekani
nchini Kenya, ujio wa Papa Mtakatifu (2015) ni matukio ya kihistoria
Kazi za sanaa huhitaji ubunifu wa hali ya juu. Hali hii hupelekea wakati mwingine watunzi kuenda kinyume na
kaida za matumizi ya lugha kimaksudi. Jambo hili huibua dhana ya uhuru wa kishairi. Uhuru wa kishairi ni idhini
au ruhusa ya mwandishi kutunga shairi kwa namna fulani bila kuzingatia kanuni za kisarufi. Uhuru wa kishairi
huhusisha yafuatayo:
A.Inkisari
.Nalandika-Ninaliandika
Nalisifu-Ninalisifu
Nalitaja-Ninalitaja
Naliweka-Ninaliweka
Lisosetirika-Lisilosetirika
Lilowajibika-Lililowajibika
B.Mazida
Huu ni uhuru wa mshairi wa kuzidisha idadi ya mizani ya maneno ili kuwe na usawa katika idadi
ya mizani.
Wajuzeni-wajuza
Waelimisheni-waelimisha
C.Tabdila.
Huu ni uhuru unaomwezesha mtunzi wa shairi kibadili muundo wa neno ili kutosheleza utamu
au matakwa ya lugha alidhamiria yeye binafsi.
Sheithwani-shetani
Sindani-Sindano
Jenamu-Jehanamu.
D.Utohozi
Huu ni uhuru unaomwezesha mtunzi au mshairi kuiga au kukopa neno au maneno kutoka lugha
nyingine.
Televisheni-Runinga
E.Kuboronga Sarufi
F. Ritifaa
Hii ni mbinu ya kukatiza neno ili kusawazisha mizani. Ritifaa inapo tumika ni kumaanisha
kwamba kuna baadhi ya neno au maneno yaliyoochwa.
Vilugha/vilahaja
– ni matumizi ya msamiati wa lahaja za Kiswahili badala ya Kiswahili sanifu.