You are on page 1of 20

KISWAHILI KIDATO CHA PILI

UONGOZI KATIKA JAMII:(LEADERSHIP IN OUR COMMUNITY)


SHUGHULI:
MSAMIATI WA VIONGOZI:
1. Katika makundi,
(a) Tajeni viongozi wanaopatikana katika shule yenu.
(b) Elezeni majukumu ya kila kiongozi?
Viongozi wa Shule:
KIONGOZI JUKUMU
1. Mwalimu Mkuu Anaongoza shughuli zote shuleni.
2. Naibu Mwalimu Mkuu Ni msaidizi wa Mwalimu Mkuu.
3. Mkurugenzi wa masomo Anasimamia shughuli za masomo shuleni.
4. Mshauri Anashauri wanafunzi kuhusu masomo yao na kazi
5. Mwalimu wa darasa Anafundisha na kusimamia shughuli za darasa
6. Kapteni wa michezo Anawakilisha wanafunzi wote shuleni.
7. Kapteni wa bweni Anadumisha nidhamu darasani
8. Mpishi mkuu Anaangalia saa na kuchunga wakati kwa vipindi vya masomo
9. Mhasibu Anatunza pesa za shule.
10. Kiranja mkuu Anawakilisha wanafunzi wote shuleni
11. Kiranja wa darasa Anashughulikia na mambo ya darasa
12. Mdhibiti wa muda Anachungulia wakati wa vipindi

SHUGHULI
1. Katika makundi,
(a) Tajeni viongozi mbali mbali katika jamii yenu.
(b) Eleza majukumu ya voiongozi hawa.
Viongozi Wa Shule Viongozi Wa Kijiji/ Kata/ Mtaa Viongozi Wa Taifa
Mwalimu mkuu Mwenyekiti wa kijiji Rais
Naibu Mwalimu Mkuu Makamu wa mwenyekiti Makamu wa rais
Mwalimu wa zamu Katibu Spika wa bunge
Mkurugenzi wa masomo Diwani Jaji/ Hakimu mkuu
Mwalimu mshauri wa wanafunzi Mjumbe Waziri mkuu
Kiranja mkuu wa shule Meya Waziri
Kiranja wa darasa Katibu wa mji Mbunge
Mpishi mkuu Halmashauri ya kijiji Mkuu wa majeshi
Mhasibu wa shule Halmashauri ya mji Mkuu wa polisi
Mkutubi wa maktaba ya shule Mkuu wa askari wa majeshi

1
MAELEZO YA MAJUKUMU YA VIONGOZI:
SHUGHULI
1. Katika makundi,
(a) Tajeni majukumu matano ya Mwalimu Mkuu.
(b) Elezeni majukumu ya Spika wa bunge la taifa.
(c) Orodhosheni majina ya viongozi watano katika jamii na kueleza majukumu yao.
(d) Elezeni umuhimu wa viongozi katika jamii.
Majibu
1. Mwalimu Mkuu
(a) Kudumisha nidhamu shuleni. (to ensure that there is discipline in school)
(b) Kutunza mali ya shule. (to protect school properties)
(c) Kutunza pesa za shule na matumizi yake, (proper planning and allocation of school
resources)
(d) Kuandikisha wanafunzi shuleni. (admitting of new students at school)
(e) Kuratibu na kusimamia shughuli zote shuleni. (to supervise all school activities)
2. Majukumu ya Spika wa Bunge
(a) Mwenyekiti wa shughuli za bunge. (chairperson of parliament)
(b) Mratibu wa shughuli za bunge.
(c) Kuongoza vikao vya bunge.
(d) Kuongoza shughuli ya kutunga sharia.
(e) Kutangaza matokeo ya kura bungeni.
Umuhimu Wa Viongozi Katika Jamii
 Kudumisha Amani.
 Kupanga na kutekeleza miradi ya serikali.
 Kutatua mizozo
 Kuwajibika kwa mahitaji ya jamii.
 Kudumisha utulivu na maendeleo.
Majukumu ya viongozi katika jamii:
SHUGHULI:
Katika makundi,
(a) Tajeni majukumu ya kiranja wa darasa.
 Kudumisha usafi darasani.
 Kudumisha nidhamu darasani.
 Kutunza vifaa vya darasa.
 Kukusanya vitabu vya wanafunzi na kupeleka kwa mwalimu ili visahihishwe.
 Kufunga na kufungua darasa.
 Kuwakilisha darasa katika shughuli zote za shule.

2
(b) Mwenyekiti wa Kijiji.
 husimamia shughuli za uongozi kijijini.
 Kudumisha usalama kijijini.
 Kukata kesi za wanakijiji.
 Kudumisha ushirikiano wa wanakijiji.
 Kuendeleza sera za serikali.
KUPIGA KAMPENI ZA UCHAGUZI:
SHUGHULI:
Katika makundi
(a) Elezeni utaratibu wa kufanya uchaguzi wa kidemokrasia.
(b) Jadili umuhimu wa kampeni za uchaguzi wa kidemokrasia.
(c) Manifesto ina umuhimu gani kwa mgombea uchaguzi na wanajamii kwa jumla?
(d) Jifikirie kwamba wewe ni mgombeaji wa nafasi fulani ya uongozi hapo shuleni. Fanya
kampeni mbele ya darasa kwa kujitambulisha na kuelezea manifesto yako. Tumia lugha ya
kushawishi.
Utaratibu wa kufanya uchaguzi wa kidemokrasia:
 Kuwa na kitambulisho kama mpigaji kura halali.
 Kujisajilisha.
 Jina kupatikana katika kitabu cha usajili.
 Kupiga kura moja kwa yule umtakaye.
 Kupiga kura yako kwa hiari bila kuamuliwa na mtu mwingine.
Baadhi ya sababu za kufanya kampeni za uchaguzi:
 Kueleza manifesto.
 Kujitambulisha kwa wapiga kura.
 Kutoa ahadi za mambo ambayo watawafanyia wapiga kura.
 Kuelimisha wapiga kura kuhusu utaratibu wa uchaguzi.
 Kuwashawishi watu kuwapigia kura.
 Kuwapa nafasi wapiga kura kuwauliza maswali.

Umuhimu wa manifesto:
 Kuonyesha mambo ya kufanywa na mgombea uchaguzi.
 Rekodi ya ahadi kati ya mgombea uchaguzi na wapiga kura.
 Mwongozo wa utekelezaji/ utendaji kazi kwa viongozi.
 Inaonesha uwajibikaji wa kiongozi.

3
SIFA ZA KIONGOZI BORA
SHUGHULI
Katika makundi,
(a) Tajeni sifa za uongozi bora katika jamii.
(b) Elezeni manufaa ya uongozi bora katiak jamii.

SIFA ZA KIONGOZI BORA MANUFAA YA UONGOZI BORA


Muangavu kwa kutenda kazi Huleta Ushirikiano katika jamii
Mwaadilifu kwa kutenda kazi Huleta Umoja katika jamii
Mdhamirifu kwa mipango mipya Huleta Maendeleo katika jamii
Jasiri kwa kutatua matatizo Matumizi bora ya rasilimali
Mbunifu wa miradi na vifaa Huleta Ustaarabu katika jamii
Mvumilivu kwa matatizo Huongeza Uzalendo katika jamii
Mwenye mawasiliano ya wazi Huleta Utulivu na Amani katika jamii
Mwenye maadili mema na mfano mzuri Huleta Upendo katika jamii
Kiongozi anaweza kuwajibika kwa jamii kwa;
 Kujali masilahi ya wanajamii.
 Kutambua mahitaji wa wanajamii.
 Kukutana na wanajamii ili kujua shida na mahitaji yao.
 Kuwashauri na kuwapa mawaidha wanajamii.
 Kuwaletea miradi inayowasaidia kiuchumi.
 Kudumisha umoja na utulivu katika jamii.
 Kupiga na ufisadi, ulevi, uhalifu, chuki, ujinga, utengano n.k.
NGELI YA I – I
Nomino au majina katika ngeli hii ni ya vitu visivyo hesabika. Pia nomino hizi hazibadiliki katika
umoja na wingi.
NO UMOJA WINGI
1 Mvua Mvua
2 Chumvi Chumvi
3 Kahawa Kahawa
4 Saruji Saruji
5 Asali Asali
6 Chai Chai
7 Sukari Sukari
8 Siagi Siagi
9 Furaha Furaha
10 Theluji Theluji
11 Homa Homa
12 Hewa Hewa

4
13 Amani Amani
14 Petrol Petrol
15 Huruma Huruma
16 Subira Subira

NB:
Kwa sababu nomino hizi hasihesabiki, mara nyingi tunatumia maneno; kidogonanyingi kuonyesha
kiasi.
NO UDOGO WINGI
1 Mvua kidogo Mvua nyingi
2 Chumvi kidogo Chumvi nyingi
3 Kahawa kidogo Kahawa nyingi
4 Saruji kidogo Saruji nyingi
5 Asali kidogo Asali nyingi
6 Chai kidogo Chai nyingi
7 Sukari kidogo Sukari nyingi
8 Siagi kidogo Siagi nyingi
9 Furaha kidogo Furaha nyingi
10 Theluji kidogo Theluji nyingi

Matumizi ya vionyeshi na vimilikishi katika ngeli ya I – I


NOMINO VIMILIKISHI VIONYESHI VIVUMISHI VIWAKILISHI
Asali Yangu Hii nzuri itatumiwa
Chai Yangu Hii nyingi Itatosha
Chumvi Yako Hiyo ndogo Ilikwisha
Sukari Yake Hiyo tamu Itanunuliwa
Siagi Yetu Ile nyekundu Itamwagika
Kahawa Yenu Hiyo hudhurungi Inapendeza
Saruji Yao Hiyo nyeupe itauzwa

SHUGHULI:
Tunga sentensi tano kutokana na jedwali hili.
Kukanusha sentensi katika wakati ujao:
KUKUBALI KUKANUSHA
Chumvi itatanunuliwa kesho Chumvi haitanunuliwa kesho
Sukari itawekwa katika maziwa Sukari haitawekwa katika maziwa.
Mvua itanyesha jioni Mvua haitanyesha jioni
Kahawa itawekwa kwenye chai Kahawa haitawekwa kwenye chai
Asali itauzwa jijini Kampala Asali haitauzwa jijini Kampala.

5
FASIHI SIMULIZI: VITENDAWILI
Katika makundi,
(a) Tajeni vitendawili vitano vinavyojulikana sana katika jamii yenu.
(b) Elezeni utaratibu wa kufuata wakati wa kutega na kutegua vitendawili.

Mkondo wa 1
Mtegaji : Kitendawili! Kitendawili!
Msikilizaji: Tega!
Mtegaji: Nyumba yangu haina mlango.
Msikilazaji: Ni jiwe.
Mtegaji: Hapana, umekosea.
Msikilizaji: Ni yai.
Mtegaji: Ndiyo, umepata.

Mkondo wa 2:
Mtegaji : Kitendawili! Kitendawili!
Msikilizaji: Tega!
Mtegaji: Yeye ni mdogo lakini ni mkali.
Msikilazaji: Ni jiwe.
Mtegaji: Hapana, umekosea.
Msikilizaji: Ni mtoto.
Mtegaji: Hapana, umeshindwa. Nipe mji/ nchi.
Msikilizaji: Nimekupa nchi ya Kongo.
Mtegaji: Mimi nitasafiri kwa ndege hadi Kongo. Nikifika huko nitazungumza lugha ya
Lingala, nicheze muziki wa kilingala, nichimbe madini kisha nirudi hapa kwa ndege pamoja na
jibu.
Jibu: Pilipili

6
Mifano:
1. Nyumba yangu haina mlango. (yai)
2. Yeye ni mdogo lakini ni mkali. (pilipili)
3. Kamba yangu ni ndefu lakini haiwezi kufunga kuni. (njia)
4. Kuku wangu anatagia miibani. (miwani)
5. Yeye anajenga lakini hana mikono. (ndege)

NO. KITENDAWILI (RIDDLE) JIBU


1. Nyumba yangu haina mlango (my house has no door) Yai (an egg)
2. Nyumba yangu ina nguzo moja (my house has one pillar) Uyoga (a mushroom)
3. Nina mwanafunzi mzuri asemaye yote ayasikiayo (I have a Kasuku (a parrot)
student who says all that he hears)
4. Sarah ni mzuri lakini ni mkali. (Sarah is good but bitter) Pilipili (pepper)
5. Ziwa la kwetu huoga kando kando. (Our lake we bath on Moto (fire place)
the sides)
6. Nina mtoto kila nimpigapo watu hucheza. ( I have a child, Ngoma ( a drum)
whenever I beat him people dance)
7. Nina mtoto wangu nikimpiga hutoa maziwa. (I have a Papai (a pawpaw)
child; whenever I beat him he produces milk.)
8. Kuku wangu hutagia miibani. (My hen, lays eggs in Nanasi (a pineapple)
thorns.)
9. Anakula kila wakati lakini hashibi. (He eats all the time Kifo (Death)
but he doesn’t get satisfied)
10. Daima namsikia lakini simwoni. (I can feel him but I Upepo (wind)
cannot see him)
11. Popote niendapo, yeye hunifuata. ( Wherever I go, he Kivuli ( a shadow)
follows me)
12. Ni nyoka mrefu lakini hana mkia. (it is a long snake Nyoka ( a snake)
without a tail)
13. Askari ananilinda lakini nikishambuliwa hanisaidii. (He Kivuli (Shadow)
guards me but when they attack me he doesn’t protect me)
14. Juu ni majani, kati ni kuni, chini ni chakula. (Up are Muhogo ( cassava)
leaves, in the middle firewood and down food)
15. Nina kamba ndefu lakini haifungi kuni. ( I have a long Njia ( a route)
rope which cant tie firewood)
16. Cheka uchekwe. ( Laugh and you will be laughed at) Mapengo ( a tooth gap)
17. Kisima cha mfalme hakikauki ( A kings bore hole doesn’t Kinywa (mouth)
dry)
18. Nimevuna shamba kubwa lajini mavuno hayajai mkononi. Nywele ( Hair)
( I have harvested a big garden but my harvest isn’t even a
handful)
19. Tunakwenda na wenzangu lakini tunapofika mimi hukaa Mbwa ( a dog)
mlangoni. (We move with my friends but when we arrive I
remain at the doorway)

7
20. Nina watoto wengi lakini nikimpiga mmojawapo wote Sahani (plates)
hulia. ( I have many children but whenever I beat one all
cry)
21. Nilianika mchele juani lakini kulipopambazuka sikuuona. Nyota ( stars)
(I spread rice in the sun to dry but at dawn I never saw it)
22. Nina mgeni nyumbani anayemaliza mafuta. ( I have a Koroboi ( a lamp)
visitor at home who finishes paraffin)
23. Mama, twendeni haraka nyumbani, miguu yake mirefu. Mvua ( Rain)
( Mummy, lets hurry home, his legs are long)
24. Ubwabwa wa mtoto mtamu. (It’s very sweet for children) Usingizi (sleep)
25. Pana visu vingi mkono mmoja tu. (There are very many Ndizi ( a banana bunch)
knives in one hand)
26. Mzazi ana miguu bali mzaliwa hana. (The parent has legs Kuku na yai ( A hen and an
but the child doesn’t have.) egg )
27. Mtoto wangu analia mwituni. (My child is crying in the Shoka (an axe)
forest)
28. Nina watoto wangu wanne ambao wanafukuzana lakini Magurudumu ( tyres)
hawakamatani. (I have four children running after each
otherbut can’t get each other)
29. Nina saa yangu ambayo haijawahi kusimama. ( I have a Moyo ( The heart)
clock that has never stopped)
30. Haukamatiki wala haushikiki. ( It cannot be touched) Moshi ( smoke)
31. Maiti anasema bali waliomchukuwa wamenyamaza. (The Mafiga na chungu
corpse is talking while the people carrying it are silent) (Cooking stones and a pot)
32. Nina wasichana wangu watatu, mmoja akiondoka wengine Mafiga (cooking stones)
hawafanyi kazi. (I have three girls but when one is missing
others can’t work)
33. Nina watoto wanne, lakini akiondoka mmoja wengine Matendeguu (Bed stands)
waliobaki hawawezi kufanya kazi
(I have four children but when one is not there, three can’t
work.)

Faida za vitendawili:
 Kukuza ustadi wa kusema/ kuongea.
 Husaidia kufikiri.
 Ni chemsha bongo.
 Huimarisha utamaduni.
 Kupitisha muda.
 Kupata msamiati.
 Kupata maarifa kuhusu mazingira na utamaduni.

SHUGHULI

8
Katika makundi,
(a) Umewahi kupiga kura au kuona watu katika jamii yako wakipiga kura? Eleza utaratibu wa
kupiga kura kwa kuzingatia yafuatayo.
 I0Ulinzi (askari)
 Vifaa vya kupigia kura. (sanduku, meza, daftari la majina, viti, karatasi, vitabu, kura
zenyewe, kalamu)
 Wasimamizi wa kupiga kura.
 Uga wa kupigia kura.
 Ulingo wa kuzuia watu wasisongamane.
 Ofisi/ nyumba karibu.
 Mifuko

(b) Andika insha kuhusu siku ya uchaguzi shuleni.


SHUGHULI JUMLISHI
Kutakuwa na uchaguzi wa viongozi katika jamii yako kila mara baada ya muda wa viongozi
waliochaguliwa hapo awali kumalizika. Taja aina ya viongozi ambao wanahitajika kuchaguliwa
katika jamii yakokwa ajili ya maendeleo. Pia eleza maandalizi yanayohitajika kwenye kituo cha
kupigia kura siku ya kuchagua mbunge wa eneo lenu.

MADA YA PILI
AFYA NA USAFI
Afya ni hali ya mtu kuwa na uzima bila ugonjwa. Usafi ni hali ya kutokuwa na uchafu.

MSAMIATI WA USAFI
SHUGHULI:
Katika makundi,
(a) Tajeni vifaa mnavyotumia kudumisha usafi pale nyumbani.
(b) Eleza umuhimu wa kudumisha usafi wa kibinafsi, nyumbani na katika jamii.
KIFAA CHA USAFI MATUMIZI YAKE
Wembe Kukata kucha ndefu, kunyoa
Ufagio Kufagia vumbi na takataka
Kitambaa Kufuta kamasi
Dodoki Kuoga mwili
Sabuni Kuoga na kunawa
Kifyekeo Kufyeka nyasi
Pipa Kutia takataka

9
Pasi Kunyosha nguo
Kitana Kuchana nywele
Dawa ya meno Kusafisha meno
Dawa ya viatu Kusafisha viatu.
Karatasi laini Hutumiwa msaalani
Beseni Kunawa, kuoga, kusafisha vyombo
Kioo Kujitazama ili kusafisha uso na mwili
Kabati Kutia vyombo
Jokofu Kutunza vyakula na vinywaji
Kichanja cha vyombo Kuwekea vyombo ili vikauke

Umuhimu wa kudumisha usafi:


 Kujilinda dhidi ya magonjwa.
 Kuwa na afya bora.
 Kutochafua mazingira.
 Kuua wadudu hatari.
 Kulinda mazingira yasichafuke.

(c) Shirikiana kusoma sentensi zifuatazo na mueleze maana yake.


1. Mtoto anapiga mswaki/ anasugua meno.
2. Mvulana ananawa mikono.
3. Shangazi anaoga mwili.
4. Dada anachana nywele.
5. Mama anakata kucha za mtoto.
6. Fatuma anafagia nyumba.
7. Peter anafyeka nyasi.
8. Namubiru anaokota takataka.
9. Mama anachemsha chakula.
10. Oremo anasafisha nguo.
11. Mgeni anafunika chakula.
SEHEMU MSAMIATI WA USAFI
Usafi wa kinywa Kupiga mswaki/ kusugua meno
Usafi wa mikono Kunawa mikono
Usafi wa mwili Kuoga mwili
Usafi wa nywele Kuchana nywele
Usafi wa kucha Kukata kucha kwa wembe
Usafi wa mavazi Kusafisha nguo
Usafi wa nyumbani Kufagia nyumba/ kupiga deki
Usafi wa mazingira Kufyeka nyasi/ kuokota takataka/ kuchoma
Usafi wa chakula na maji Kuchemsha chakula, kufunika, kuchemsha maji,
Kutumia dawa ya maji

10
SHUGHULI
Katika makundi,
(a) Tungeni sentensi mkitumia wa usafi ufuatao.
(i) Oga
(ii) Sugua meno.
(iii) Nawa mikono
(iv) Piga nguo pasi.
(v) Fyeka
MSAMIATI WA AFYA
SHUGHULI:
Katika makundi,
(a) Tajeni msamiati wa afya ambao mnaujua.
(b) Tungeni sentensi kumi mkitumia msamiati wa afya.
(c) Elezeni vifaa vitano vya afya na matumizi yake.
(d) Elezeni vitu vitatu ambavyo vinaweza kudhuru afya yako.

(a) Msamiati wa afya;


Bendeji Daktari
Sindano Machela
Tembe za dawa Kipima joto
Glavu Kiti cha magurudumu
Hospitali
Ambulensi
Sirinji Hudubini

(b) Mifano ya sentensi.


(i) Ninataka dawa.
(ii) Ninaenda hospitalini.
(iii) Anataka kumwona daktari.
(iv) Daktari anatumia kipima joto.
(v) Daktari amemdunga mgonjwa sindano.
(vi) Dawa za tembe ni nzuri.
(vii) Gari la wagonjwa/ ambulensi imenunuliwa.
(viii) Kiti cha magurudumu kimeharibika.
(ix) Mgonjwa amefungwa bendeji.
(x) Daktari anatumia hudubini kuchunguza vidudu kwenye damu.

11
(c) Vifaa na matumizi
Kifaa cha afya Matumizi yake
Kipimajoto Hupima joto la mwili
Machela Kubebea wagonjwa
Gari la wagonjwa Kubeba wagonjwa mahututi
Kiti cha magurudumu Kiti cha mgonjwa mahututi.
Sindano Kuingiza dawa mwilini
Hudubini Kuchunguza vidudu vidogo
Stethoskopu Kusikiliza mapafu na mapigo ya moyo
Glavu Kuvaa mikononi ili kujilinda dhidi ya uchafu
Bendeji Kufungia mahali palipoteguka au chubuka
Uyoka Kuonea sehemu za ndani za mwili
Plasta Kufungia kidonda

(d) Vitu ambavyo vinaweza kuharibu afya yako


 Madawa ya kulevya.
 Sumu
 Vyakula vibaya.
 Vinywaji vya kulevya.
 Kuvuta sigara.
 Ajali.
 Mazingira machafu.
 Msongo wa mawazo.

WADUDU WANAOSABABISHA MAGONJWA:


SHUGHULI
Katika makundi.
(a) Tajeni wadudu hatari wanaoambukiza na kusambaza magonjwa katika jamii.
(b) Tajeni magonjwa ambayo husababishwa na kila mdudu.
MDUDU UGONJWA
Mbu Homa ya malaria
Nzi Kipindupindu/ tumbo kuhara
Mbungo Malale
Kunguni Upele mwilini
Mende Pumu
Chawa Kuumwa kichwa, madoadoa mwilini
Nyuki Kufura kwa mwili.

12
Kiroboto
Funza
Mnyoo

(c) Someni sentensi zifuatazo


1. Huyu ni mbu
Mbu anaeneza ugonjwa wa homa ya malaria.
2. Huyu ni nzi
Nzi anaeneza ugonjwa wa tumbo kuhara.
3. Huyu ni mbungo
Mbungo anaeneza ugonjwa wa malale.
4. Huyu ni kunguni
Kunguni husababisha upele mwilini.
5. Huyu ni mende
Mende anasabaisha ugonjwa wa pumu.
6. Huyu ni chawa
Chawa anasababisha kuumwa kichwa na kuwa na madoadoa
7. Huyu ni nyuki
Nyuki anasababisha kufura kwa mwili.

KINGA DHIDI YA MAGONJWA YALETWAYO NA WADUDU


SHUGHULI
Katika makundi,
(a) Eleza jinsi mnavyoweza kuzuia magonjwa mbalimbali.
Magonjwa Jinsi ya kuyazuia
Homa ya malaria  Tumia chandarua unapolala kitandani
 Fyeka nyasi zilizo karibu na nyumba
 Fukia mashimo ya maji yaliyosimama
 Nyunyiza madawa ya kuuwa wadudu
Malale  Nyunyiza dawa inayoua mbu
 Jifunike mwili wote unapolala
 Fyeka nyasi zilizo karibu na nyumba
Kipindupindu  Chemsha maji ya kunywa.
 Funika chakula vizuri
 Nyunyiza dawa ya kuua nzi
Tauni  Ua viroboto kwa dawa ya kunyunyiza
 Dumisha usafi kwa kufagia
 Osha, anika na kupiga pasi matandiko
 Fungua madirisha ili mwanga uingie nyumbani
Pumu  Ua mende kwa dawa ya kunyunyiza
 Funika chakula vizuri

13
 Fagia nyumba
 Fungua madirisha
Kichocho  Usitembee majini bila viatu
 Chemsha maji ya kunywa
Minyoo tumboni  Chemsha maji ya kunywa
 Usile chakula baridi au kilichooza

(b) Eleza njia tano za kinga dhidi ya magonjwa.


 Kulala ndani ya chandarua.
 Kufyeka nyasi karibu na nyumba.
 Kuziba mashimo ya maji yaliyosimama.
 Kufagia nyumba.
 Kudumisha usafi wa mwili.
 Kuosha na kupiga pasi nguo.
 Kuchemsha maji.
 Kuweka chakula kabatini au kwenye jokofu.

(c) Shirikiana katika makundi na kusoma hadithi ifuatayo.


Amos na Hilda ni dada na kaka. Hilda ana umri wa miaka kumi na minne. Anasoma katika kidato
cha pili. Kaka yake Amos ana miaka kumi na mitatu. Anasoma kidato cha kwanza. Wanasomea
katika shule moja ya mseto karibu na nyumbani kwao.
Shule yao ni ya kutwa. Wao pamoja huenda shuleni asubuhi na jioni hurudi nyumbani. Kila siku
Amos huamka asubuhi sana. Yeye hunawa uso wake. Baada ya kupata kiamsha kinywa, yeye
hupiga mswaki. Kisha yeye hufagia chumba chake na kufungua madirisha ili hewa safi kuingia
chumbani.
Hilda pia huamka asubuhi sana. Baada ya kunawa uso yeye huchana nywele zake. Baadaye yeye
huosha vyombo na kuviweka kwenye kichaga cha vyombo ili vikauke. Yeye hupiga deki na
kufagia jikoni. Baadaye hupiga mswaki, oga na kujitayarisha kwenda shuleni.
Wanapofika shuleni, kabla kuingia darasani wao huongozwa na mwalimu wa zamu kuokota
takataka zote shuleni. wanafunzi wengine hupiga deki na kufagia madarasa. Jioni Amos na Hilda
wakirudi nyumbani, huwasaidia wazazi wao na kazi. Hilda humsaidia mamake kufanya usafi
nyumbani. Amos husaidia babake kufanya usafi katika zizi la ngombe na vyumba vya kufugia
kuku.

Siku ya Jumamosi na Jumapili Amos na Hilda hushirikiana na wazazi wao kufagia nyumba,
kufyeka nyasi zilizo karibu na nyumba. Pia wao hufunika mashimo yaliyo karibu na nyumba yao
ili mbu wasije wakazaliana humo. Baada ya shughuli hizo wao huosha nguo zao, shuka za
0vitanda vyao na mikoba ya kubebea vitabu. Amos na Hilda huoga kila siku, hunawa mikono
kabla yao kabla kula chakula na baada ya kutoka msaalani. Wao pia hupiga pasi nguo zao za
nyumbani na sare ya shule.

14
Maswali:
(a) Hilda na Amos wanaitanaje?
(b) Hilda ana miaka mingapi?
(c) Amos anasoma kidato cha ngapi?
(d) Amos hufanya usafi gani anapoamka kila asubuhi?
(e) Hilda akiamka hufanya nini kabla kwenda shuleni?
(f) Wanafunzi hufanya usafi gani asubuhi kabla kuingia darasani?
(g) Baada ya masomo Amos na Hilda huwasaidia wazazi kufanya nini?
(h) Taja usafi ambao Hilda na Amos hufanya wikendi?
(i) Kwa nini Amos na Hilda hufanya usafi?

SHEREHE KATIKA JAMII


Umuhimu wa sherehe
Kufurahia jambo Fulani
Kukumbuka siku/ tukio Fulani
Kutekelezwa matakwa ya kisiasa, kimila na desturi
Mfino ya sherehe
Sherehe Umuhimu wake katika jamii/familia
Noeli/krismasi Kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa bwana yesu
Pasaka Kuadhimisha siku ya kufufuka kwa yesu Kristo
Idi Siku ya maadhimiso ya kumaliza mfungo wa ramadhani au
idada ya Hijja kwa Waislamu
Arusi Ndoa Ya kufunga pingu za maisha
Ubatizo Kupewa jina la kidini kwa wakristo

Kipaimara Kupewa uthibitisho katika dini ya kikristo

Mahafali Kusherehekea kumaliza na kuhitimu masomo

Unyago Sherehe ya waschana kuingizwa katika utu uzima


Jando Sherehe ya wavulana kuingizwa/ kufundishwa utu uzima
Matanga Kuomboleza na kuwaliwaza waliofiwa
Mazishi Shughuli na taratibu kuhusu maziko
Kupewa jina Shughuli ya motto aliyezaliwa kupewa
Ijumaa kuu Kukumbuka siku ya kusulubiwa yesu kristo
Idi fitri Kuadhimisha kwa mwezi mtukufu wa ramadhani
Siku ya kupata uhuru (tarehe 9 Kuadhimisha siku ya kupata uhuru wa uganda
Oktoba kila mwaka)

15
Siku ya wanawake (tarehe 8 Kuandhimisha siku ya wanawake duniani
machi kila mwaka)
Siku ya shahidi wa Uganda ( Kuadhimisha siku ya mashahidi waliokufa kwa imani yao
tarehe 3 juni kila mwaka) yamkidini nchini uganda

UMUHIMU WA KUFANYA SHEREHE KATIKA JAMII


Kufurahia jambo Fulani
Kuadhimisha jambo/tukio Fulani
Kuhimiza masharti ya kimila
Kutimiza matakwa ya kidini
SHEREHE TANO KATIKA FAMILIA NA UMUHIMU WAKE
Arusi: kufunga pingu za maisha kama mume na mke
Kupewa jina: kutimiza mila kwa kutoa jina la kijadi
Ubatizo: kupewa jina la la kidini
Kipaimara: uthibitisho katika dini
Mahafali: sherehe ya kumaliza masomo na kuhitimu
Matanga: kuomboleza na kuwaliwaza waliofiwa
Mazishi: shughuli za maziko
MAMBO YANAYOTENDEKA KWENYE SHEREHE
Kula na kunywa
Dua na maombi
Kucheza ngoma
Kutawadha
Taja sherehe mnazosherehekea nyumbani kwenu
UMUHIMU WA SHEREHE KATIKA JAMII
Kufurahia jambo au tukio Fulani
Kumbukumbu kwa jambo au tukio Fulani
Kutimiza mila za kidini

16
UMUHIMU WA SHEREHE MBALIMBALI KATIKA JAMII

SHEREHE KATIKA JAMII UMUHIMU WAKE


Sherehe ya mwaka mpya Tarehe moja januari kila mwaka. Furaha kwa
kufika kwa mwaka mpya
Sherehe ya arusi/ ndoa Siku ya makubaliano kwa kufunga pingu za
maisha
Mafahali Siku ya wanafunzi kusherehekea kumaliza na
kuhitimu masomo
Unyago Siku ya wasichana kuingizwa katika utu uzima
kimila
Jando Siku ya wavulana kuingizwa katika utu uzima
kimila
Kupewa jina Siku ya motto aliyezaliwa kupewa jina lakijadi
Siku ya kuzaliwa Kukumbuka/kuadhimisha tarehe ambapo mtu
alizaliwa
Ubatizo Sakramenti ya kidini ya kikristo ya kubatizwa
jina la kidini
Kipaimara Sakramenti ya kikristo ya kupata uthibitisho
kwa Imani yake
Matanga Kuomboleza na kuliwaza waliofiwa
Mazishi Kutoa heshima ya mwisho kwa marahemu
Pasaka Maadhimisho ya siku ya kufufuka kwa yesu
kristo
Noeli/ krismasi 25 desemba Maadhimisho ya siku ya kuzaliwa kwa yesu
kristo
Ijumaa kuu Kukumbuka siku ya kusulubiwa yesu kristo
Idi fitri Kuadhimisha kwa mwezi mtukufu wa
ramadhani
Idi Kusherhekea kwa kuchinja wanyama kwa dini
ya kiislamu
Siku ya wanawake tarehe 8 machi kila mwaka Kuadhimisha siku ya wanawake duniani
Siku ya kupata uhuru tarehe 9 oktoba kila Kuadhimisha siku ya kupata uhuru wa Uganda
mwaka
Siku ya mashahidi wa Uganda tarehe 3 juni Kuadhimisha siku ya mashshidi waliokufa kwa
kila mwaka Imani yao ya kidini nchini uganda

Shughuli
1. Elezeni sherehe zinazoffanyika kila mwaka katika jamii yako
2. Elezeni sherehe za kisasa na kitamaduni katika jamii yako
3. Tajeni mambo yanayotendeka kwenye sherehe na umuhimu wake
Sherehe za kila mwaka

17
Sherehe ya mwaka mpya, noeli/krismasi
Pasaka
Idi fitri
Idi adhuha
Siku ya uhuru
Siku ya wanawakes
Siku ya mashujaai
Siku ya mashahii waUganda
Sherehe za kisasa
Siku ya kupata uhuru
Siku ya mashujaa
Sherehe za kiutamaduni
Unyago
Jando
Kupewa jina
Matanga
Mazishi
Ndoa
Mambo yanayotendeka kwenye sherehe ni kama vile
Kucheza dansi/ngoma
Kucheza michezo
Kula na kunywa
Kuimba
Magwaride
Mahitaji ya maarusi kwa sherehe ya ndoa
Mavazi rasmi ya maarusi na pete
Keki ya sherehe
Wacheza ngoma

18
Vipaza sauti
Mahema
Vyakula/mapochopocho/vinywaji
Meza na viti
Magari
Wapampe
Wahudumu na wafanyakazi
Maigizo ya sherehe ya ndoa
Bwana arusi
Bibi arusi
Wapambe yaani mpambe wa bwana arusi na mpambe wa bibi arusi
Wacheza ngoma
Wageni
Wazee
Mfawidhi
Maelezo kuhusu maigizo ya ndoa
1. Elezeni tofauti za kufanya maigizo ya sherehe ya ndoa kwa imani tofauti za
kidini na kitamaduni.
 Muvulana kutokamata msichana kiuononi au mkononi
 Mvulana au msichana kutovaa mavazi ya mwenziwe yasiyomstahili
 Imani za kishirikina
 Maigizo kuhitilafiana na imani na maadili ya kitamaduni
2. Tajeni hisia zinazojitokeza wakati wa kufanya maigizo ya sherehe ya ndoa
 Furaha
 Aibu kwa kuvaa mavazi yasiyo ya kawaida
 Fahari kwa kuhisi mtu ni bwana au bibi arusi
3. Ni maandalizi yapi yanayohotajika kwa maigizo ya sherehe ya ndoa
 Mavazi/maleba ya maarusi
 Viti/meza
 Mkate/keki ya sherehe
 Wapampe
 Vyakula na vinywaji
 Mpiga picha

19
4. Tumieni simu ya mwalimu tarakilishi na projekta kutazama picha na video za
sherehe ya ndoa
Tazama video na picha
NDOA NA MASHARTI YAKE
Riadhaa ya mwanamume ni mwanamke
Kutangaza ndoa katika makanisa na misikiti kabla ya kufunga ndoa yenyewe
Kulipa mahari
Kuwepo kwa mashahidi wakati wa kufunga ndoa
Maarusi wasiwe na uhusiano wa kiukoo
Maarusi wawe waliojiheshimu na mwenye kijihifadhi
Ridhaa ya wazazi
Sherehe ya kufunga ndoa ya kidini, kiserikali au kiutamaduni
Kutofanya mapenzi na mtu mwingine asiye mume wala mke wako
MADHARA YA KUSHIRIKI MAPENZI KABLA YA NDOA
Kuambukizwa magonjwa ya zinaa kama vile kaswende, kisonono, vidonda katika sehemu za siri
Kupata ugonjwa hatari wa ukimwi
Kupata ugonjwa wa saratani ya maini

20

You might also like