Professional Documents
Culture Documents
Ziwa la Tanganyika
Ziwa Tanganyika jinsi inavyoonekana kutoka angani Afrika ya Mashariki Mahali Burundi, Kongo, Nchi zinazopakana Tanzania, Zambia 32,893 km kutegemeana na kiasi Eneo la maji cha mvua kuanzia 3.5 m Kina ya chini Lufubu, Malagarasi, Mito inayoingia Ruzizi Lukuga Mito inayotoka Kimo cha uwiano wa 782 m maji juu ya UB Bujumbura, Kalemie, Miji mikubwa ufukoni Kigoma
Ziwa Tanganyika pamoja na miji muhimu kando lake Ziwa la Tanganyika ni kati ya maziwa makubwa ya Afrika ya kati ikiwa eneo lake ni la pili tu baada ya Viktoria Nyanza katika Afrika na ujazo wa maji yake ya pili duniani baadaya Ziwa Baikal. Jina lake limekuwa tangu 1919 pia jina la koloni ya Kiingereza ya Tanganyika. Ziwa lina ujazo wake mkubwa umetokana na vilindi vyake vinaelekea chini hadi mita 1470. Urefu wa ziwa ni 673 km na upana wake takriban 50 km. Maji ya Ziwa Tanganyika yanajaza ufa kubwa kwenye ganda la dunia ambalo ni sehemu ya bonde la ufa la Afrika ya Mashariki. Eneo la maji ni 32,900 km. Ziwa la Tanganyika limepakana na nchi zifuatazo: Kongo, Tanzania, Burundi na Zambia. Kongo na Tanzania zinatawala sehemu kubwa ya ziwa.
Beseni ya ziwa ni 231,000 km. Mito miwili mikubwa ya Ruzizi na Malagarasi inapeleka maji yao ziwani. Maji yanatoka kwa njia ya mto Lukuga kwenda mto Kongo. Miji mikubwa ziwani ni mabandari ya Kigoma kwa upande wa Tanzania na Kalemie kwa upande wa Kongo. Kila bandari ni pamoja na mwanzo wa njia ya reli. Mji mkubwa kabisa ni Bujumbura mji mkuu wa Burundi.