Professional Documents
Culture Documents
Taarifa Kwa Umma Kuhusu Nemc
Taarifa Kwa Umma Kuhusu Nemc
b.
c.
3.
NEMC kama chombo muhimu nchini kilichopewa jukumu la kusimamia
utekelezaji wa Sheria ya Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira inatarajiwa kazi
zake zifanyike kwa ufanisi wa kiwango cha juu kulingana na majukumu
yaliyoko kwa mujibu wa Sheria. Hivyo, kwa mapungufu yanayojitokeza Mhe.
Makamba, ndani ya wiki moja ataunda jopo la wataalamu wasiozidi watano ili
kutathmini utendaji wa NEMC na changamoto mbali mbali katika usimamizi
wa hifadhi ya mazingira na kuishauri Serikali ipasavyo.
4.
Ili kuimarisha ufanisi na udhibiti wa utendaji wa NEMC, ndani ya wiki
moja litatolewa Tangazo litakalokuwa na mambo yafuatayo: Anwani ya barua
pepe (email), Nukushi (fax), Namba ya simu, Namba ya Whatsapp ili mtu yeyote
mwenye malalamiko au aliyewahi kuombwa rushwa ama chochote na
watumishi wa NEMC ambacho ni kinyume na maadili ya kazi yao atoe taarifa
mara moja ili uchunguzi ufanyike na hatua zichukuliwe.
5.
Kutokana na mapungufu yanayojitokeza katika utekelezaji wa Tathmini ya
Athari kwa Mazingira, ndani ya wiki moja, NEMC ipitie upya orodha ya
wataalamu na taasisi elekezi zilizosajiliwa na kufuta wataalamu na taasisi zote
ambazo zimekuwa zikikiuka maadili ya kazi zao likiwemo suala la kuwasilisha
taarifa zilizo chini ya viwango, kuchelewesha kazi za wateja wao na
kutowasiliana na wateja wao kuhusu hatua za utekelezaji wa maombi yao.
6.
Ndani ya wiki tatu uitishwe mkutano wa dharura wa Bodi ya NEMC
kujadili na kufanya maamuzi juu ya changamoto za utendaji katika Baraza.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA MAKAMU WA RAIS
08.01.2016