You are on page 1of 8

WAJIBU NA HAKI ZA MWALIMU

(A) WAJIBU MKUU WA MWALIMU


Wajibu mkuu wa mwalimu ambao ndio Nguzo Tano za kazi ya ualimu ni:-
1.KWA MTOTO
2.KWA JUMUIYA
3.KWA MWAJIRI WAKE
4.KWA KAZI YAKE
5.KWA TAIFA

1.KWA MTOTO
Nguzo hii inamtaka mwalimu akubali kwamba wajibu wake mkuu ni kwa mtoto ambaye
amekabidhiwa kumlea na kwamba kwa wakati wote anatakiwa kumwongoza kwa kumkuza
na kumwendeleza kimwili,kiakili na kiroho.

2.KWA JUMUIYA
Nguzo hii inamtaka mwalimu kuijua jumuiya ambamo anaishi na kufanyia kazi na kutii
mamlaka halali na tabia yake mwenyewe kuwa mfano bora kwa wanajumuiya.

3 KWA MWAJIRI WAKE


Nguzo hii inamtaka mwalimu kumtumikia mwajiri wake kwa utii na kwa uaminifu kwa
mujibu wa masharti ya kazi ya ualimu

4.KWA KAZI YAKE YA UALIMU


Nguzo hii inamtaka Mwalimu kufuata kwa wakati wote na kwahali ya juu kabisa Maadili
mema ya kazi ya ualimu pamoja na:-
-kufanya kazi kwa bidii na kwa kufuata utaratibu
-Kuwa mfano mzuri katika tabia wakati wote kwa watoto waliochini ya ulinzi wake na
hata watoto wengine katika jamii.
-kujaribu kila wakati kuinua kiwango cha utendaji nauwezo wa kufanya kazi
-kutotumia vibaya haki zinazoambatana na utumishi wa umma.

5.KWA TAIFA LAKE


-Nguzo hii inamtaka mwalimu kuwa mzalendo na raia mwema na mtii wa sheria za
nchi

na mwelekezaji wa watoto kuwa wazalendo safi na raia wema wa baadae kwa kuzingatia
wajibu wa mwalimu kwa kazi yake ya ualimu
-Mwalimu anategemewa kuwa na tabia na mwenendo mzuri wa kufaa kuigwa na kustahili
kupewa heshima na kuaminiwa na jumuia,wazazi na wanafunzi.
-Mwalimu yeyote anayekwenda kinyume na maadili na masharti ya kazi ya ualimu
anakuwa nimtovu wa nidhamu.
(B) HAKI ZA MWALIMU
LIKIZO YA MWAKA(Annual leave)
-Kwa mujibu wa kanuni za kudumu za watumishi wa umma 2009 kifungu H.5(ii)kikisomwa
pamoja na kanuni za utumishi wa umma,2003 kifungu cha97(i)mtumishi wa umma
anayostahili ya kupewa likizo siku 28 kila mwaka. Aidha kifungu cha 97 (ii) kinaeleza kuwa
likizo ni haki ya mtumishi.
Inapokuwa haitolewi na mwajiri kwa sababu mbalimbali basi mwajiri atawajibika kumlipa
mtumishi mshahara wake wa mwezi. Mtumishi hatopewa likizo ya mwaka hadi amefikisha
miezi 8 tangu kuajiliwa rasmi (kanuni Na.97:za 2003).Mtumishi atapewa usafiri wa likizo
mara moja ndani ya mzunguko wa miaka miwili yeye, mkewe na watoto wane chini ya umri
wa miaka 18 au wategemezi,kanuni Na.97(5).

LIKIZO YA UZAZI (Maternity leave).


Kifungu Na.98(1),2003 Mtumishi wa kike atapewa likizo ya uzazi siku 84 mara moja kila
baada ya miaka (3) kumaliza likizo yake,akijifungua mapacha atastahili likizo ya siku
100,kwa kwa mujibu wa T.S.S,2008,47(1)

Kifungu 98 (2 ) Mtumishi anapojifungua kwa bahati mbaya mtoto akafariki kabla ya miezi
12
Kumalizika. Akipata mimba atastahili likizo ya uzazi siku 84.

Kifungua Na. 98 (3). Mtumishi aliyejifungua astastahili muda wa saa mbili


kwenda kunyonyesha hadi kipindi cha miezi sita (6).
Mtumishi wa Kiume, mkewe akijifungua atapewa likizo ya siku tatu.
(T.S.S 48)

LIKIZO BILA MALIPO.


Kifungu Na.99 (1) cha kanuni za utumishi wa umma 2003. Katibu Mkuu ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma anaweza kutoa likizo bila malipo kama ataridhika na
sababu za maombi ya likizo hiyo. Hata hivyo maombi hayo ni lazima yapitie kwa Mwajiri
kanuni 99(2).

LIKIZO YA UGONJWA.
Kifungu Na.100 (1) cha ushauri wa Daktari, Mamlaka ya ajira inaweza kutoa likizo ya
ugonjwa. Likizo hutolewa miezi sita na mshahara kamili na miezi sita mingine kwa nusu
mshahara.

SABATICAL LEAVE.
Kifungu 101 (1) Likizo hii hutolewa kwa mwajiri ili kukamilisha au kuimarisha
uzoefu.Likizo
hii ni lazima iindhinishwe nakatibu Mkuu Menejimenti ya Utumishi wa Umma.Likizo hii
hupewa Mtumishi si zaidi ya miezi 12 na hutolewa baada ya Mtumishi kufanya kazi
mfululizo
miaka mitano,Kanuni Na.101 (4).
LIKIZO YA KUSTAAFU.(Leave pending retirement)
Kanuni Na 102 za 2003,Mtumishi wa Umma anastahili kuomba likizo ya kujiandaa kustaafu
mwezi mmoja kabla ya tarehe rasmi ya kustaafu kwake.Atastahili kupewa usafiri wa
kumrejesha kwao yeye na familia yake pamoja na mizigo sio chini ya tani tatu kulingana na
daraja lake.

MATIBABU KWA WATUMISHI WA UMMA


Kifungu .K.(i) za kanuni za kudumu 2009 ikisomwa pamoja na kifungu cha 105 cha kanuni
za Utumishi wa umma Mtumishi anastahili kupata matibabu bure. Hata hivyo kuna utaratibu
wa bima ya afya.

Mtumishi akilazimika kusafiri kwenda Hospitali ya Rufaa mwajiri atahusika kugharamia posho
ya kujikimu na nauli.

Vitu muhimu.
-Barua ya rufaa.
-Barua ya ruhusa tota kwa mwajir
-Fomu Appendix K 28$29 Fomu bya madai ya posho.
-Fomu Appendex K/V ya madai ya naului ikiambatana na tiketi K.26
-Kadi ya mahudhurio hospitali
-Sickshhet.

FIDIA YA KUUMIA KAZINI.


-Kanuni Na.111(1-5) inaeleza hatua mbalimbali za kufuata pindi mtumishi anapopatwa na
matatizo kazini.
-Mtumishi anayeumia atalipwa fidia sio chini ya shilingi 1,000,000/= na sio zaidi
zaidi ya shilingi 10,000,000/= kutegemea na hali ya maumivu au kufariki.

-Kifungu ch 110 kinaelezea kwamba mtumishi anapoumia wakati wa kutekelaza


majukumu ya ajira yake anastahili fidia na inamtaka mtumishi kujikinga na hali ambayo
inaweza kuathiri afya yake.

KUJIENDELEZA
-Kanuni Na .103 inaeleza kamba ni wajibu wa mwajiri kuwaendeleza watumishi wake.
-Kutokana na tathimini ya kazi , mwajiri atabainisha mahitaji ya kuendeleza watumishi.
-Watumishi ni lazima wajiendeleze katika fani kwa lengo la kuboresha ufanisi.
-Kuandaa mpango kazi wa mafunzo ka watumishi.
-VTENDO VYOVOTE VINAVYOPINGANA NA UTARATIBU ZA KIUTUMISHI
-UZEMBE UNAOMGHARIMU MWAJIRI
-KUKIUKA MAADILI YA KAZI YA UALIMU (YA UTUMISHI WA UMMA)
Adhabu zake
-kufukuzwa kazi bila Utumishi.
-kufukuzwa kazi na utumishi
-kushushwa cheo.
-kushushwa mshahara si chini ya kiwango ulichoanzia kazi
-kulipa gharama au sehemu ya gharama kwa upotevu au uharibifu uliotokana na uzembe
-karipio
-Onyo
-Kusimamishwa nyongeza ya mshahara.

KUTOENDELEA NA MAJUKUMU NA KUPUMZISHWA


Mtumishi anapumzishwa bila kusimamishwa kazi na bila kuathiri maslahi yake..Lengo lake ni
kuzuia kosa lisiendelee kutendeka wakati wa uchunguzi wa awali ukifanyika,(kanuni Na.37)

KUSIMAMISHWA KAZI
Mtumishi husimamishwa kazi na kupewa Hati ya mashtaka. Hatua hii ni baada ya Mamlaka ya
nidhamu kuridhika kuwa kuna tuhuma za ukweli dhidi ya mtumishi husika.(kanuni 38)

KUREKEBISHA MASHTAKA
Mamlaka ya nidhamu inaruhusiwa kurekebisha mashtaka yasiyo sahihi ndani ya siku zisizozidi
30 tangu Mshtakiwa alipopewa mashtaka ya awali (kanuni ya 38(3) )

NUSU MSHAHARA.
Mtumishi aliyesimamishwa kazi anastahili nusu mshahara wake wa mwezi tu kwa kipindi chote
alichosimamishwa kazi.Iwapo mtumishi husika hatapatikanana hatia na hivyo kutofukuzwa kazi
au kutopewa adhabu yoyote atalipwa nusu mshahara wake ambao hakulipwa wakati
aliposimamishwa kazi lakini ameadhibiwa kwa adhabu nyingine, atalipwa robo ya mshahara
wake. (kanuni ya 38-2,5 na 6.)

KUONDOKA KITUONI MTUMISHI ALIYESIMAMISHWA KAZI.


Mtumishi aliye simamishwa kazi haruhusiwi kuondoka kituoni bila kuruhusiwa kwa maandishi
na mamlaka yake ya nidhamu kanuna ya 38 (7)

ATHARI ZA KUFUKUZWA KAZI


Mtumishi akifukuzwa kazi hupoteza haki zake. Hata hivyo mtumishi husika atalipwa pensheni
ya mkupuo iwapo wakati huo alistahili pensheni ya kila mwezi. Aidha, mtumishi aliyetiwa
hatiani kwa makosa ya jinai yanayo husu rushwa au hujuma, atapoteza haki au madai yake
yote.(Kanuni ya 40.2003)
MTUMISHI ANAPOKABILIWA NA KESI YA JINAI.

Mtumishi husika atasimamishwa kazi hadi kesi husika itakapohitimishwa. Hatua za kinidhamu
hazitachukuliwa au kuendelezwa dhidi yake. Masharti na maelekezo yote yako kwenye kanuni
ya 50 na 51

RUFAA
Mtuhumiwa atapewa haki yake ya kukata rufaa kwenye MAMLAKA SAHIHI na MUDA
MUAFAKA. Rufaa kwa walimu imeelezwa kwenye kanuni Na 126 (1 hadi 3) ya kanuni za
mtumishi wa umma,2003.
Muda wa kuwasilisha rufaa ni siku 45 tangu tarehe aliyopata uamuzi wa awali na rufaa ni
lazima iwe kwa maandishi na inayowekwa wazi sababu za kupinga uamuzi na adhabu. Mrufani
anapaswa kuipatia mamlaka yake ya nidhamu nakala ya rufaa.Iwapo hakufanya hivyo mamlaka
ya nidhamu inapaswa kuwasilisha taarifa ya mwenendo wa hatua za nidhamu na maelezo/utetezi
wake dhidi ya sababu za rufaa ndani ya siku 14, nakala kwa Mrufani (kanuni 61)

KUAJIRIWA UPYA KATIKA UTUMISHI WA UMMA


Walimu wanaruhusiwa kuajiriwa upya katika utumishi wa umma baada ya kutumikia adhabu
kwa muda usiopunngua miezi 12.Kanuni Na.120(d) ya kanuni za utumishi wa Umma 2003
imeelekeza kuwa kamati ya mkoa inatoa uamuzi juu ya suala hilo. Uamuzi wa kamati ya
mkoa utawasilishawa kwa katibu wa tume kwa ajili ya kuwaombea kibali cha kuajiriwa upya
walimu hao kwa katibu Mkuu kiongozi.

HITIMISHO
Lengo la mada hizi ni kuwaelimisha na kuwajengea uwezo Waratibu Elimu Kata , Walimu
wakuu wa shule /Wakuu wa wa shule na Walimu wa walimu wote kwa ujumla katika kutekeleza
majukumu mbalimbali katika maeneo yenu ya kazi kwa kuzingatia sheria ,kanuni,taratibu na
miongozo mbalimbali inayotolewa na serikali katika kuboresha Utumishi wa umma, mara kwa
mara.

POSHO YA KUJIKIMU
Kanunui ya 13 inaeleza kwamba Mtumishi wa Umma aliye ajiliwa anastahili kupewa:-
-Nauli yeye na mkewe, mumewe,watoto na wategemezi wasiozidi 4
-Posho ya kujikimu kwa kiwango na idadi ya siku itakapokuwa imeandaliwa na Katibu
mkuu Ofisi ya Rais menejiment ya Utumishi wa Umma.

KUTIBITISHWA KAZINI.
Kanuni Na.14 za 2003,Mtumishi wa Umma aliye ajiliwa kwa mashariti ya kudumu atakuwa
chini ya matazamio kwa kuzingatia muundo wa Utumishi wake na haitazidi miezi kumi na
miwili.
Mkuu wa kituo/kazi atawajibika kutoa taarifa kwa mamlaka husika kuhusu:-
-Mtumishi kuthibitishwa kazini.
-Mtumishi kuongezewa muda wa matazamio ili kumwezesha kufanya kazi kwa ufanisi.
Utumishi wa Mtumishi kusitishwa.
KUPANDISHWA CHEO (KANUNI NA.15)
Kupandishwa cheo kwa Mtumishi wa Umma kutategemea muda wa utendaji,utendaji wa kazi
uliokidhi malengo (ufanisi wa kazi) na Taaluma ya Mtumishi.
Mtumishi akipandishwa cheo atakuwa kwenye matazamio kwa muda wa miezi 6.Kanuni
Na.16(1).

UHAMISHO.
Mtumishi anapohamishwa hustahili mambo yafuatayo;-
-Posho ya usumbufu 10% ya mshahara wa mwaka (Kanuni za kudumu za 2009L13 1-2).
-Posho ya kujikimu atalipwa siku 14 akiwa na mweza wake na watoto wake 4 chini ya umri
wa miaka 18 na wategemezi 2 kanuni za kudumu 2009L(1-2).
-Usafiri wake na familia yake pamoja na mizigo isio chini ya Tani tatu kutegemea na daraja
lake (kanuni za kudumu za 2010 J1).

UHAMISHO WA KUOMBA.
Mtumishi wa umma hatalipwa chochote anapoomba uhamisho kwa manufaa yake (isipokuwa)
kama amekaa kituo kimoja sio chini ya miaka mitano mfululizo au kama anataka kwenda
kwao kujianda na kustaafu na awe amefanya kazi nje ya mkoa wake si chini ya miaka 10
mfululizo.(L.8 a-b)

KUSTAAFU.
1.Kustaafu kwa hiari.
Itakuwa miaka hamsini na tano, sharti atoe taarifa ya kusudio lake miezi sita kabla ya
kutimiza miaka 55
2.Kustaafu kwa ugonjwa.
Kanuni namba 30,2003 Sheria namba 2 ya pensheni ya itimisho la kazi. Kwa ushauri wa
daktari na jopo la madaktari mamlaka inaweza kupendekeza mwalimu astaafu kwa
ugonjwa.
3.Kustaafu kwa lazima.
Mtumishi wa umma atalazimika kustaafu kwa lazima atimizapo umri wa miaka sitini.
Atawajibika kutoa taarifa miezi sita kabla ili aweze kupata kibali kwa wakati .

-MAFAO YA KUSTAAFU.
-PENSHENI
-MIRATHI
-KIINUA MGONGO CHA MKATABA WA MUDA MAALUM.

PENSHENI.
Pensheni ni mafao ya hitimisho la kazi kwa mtumishi anaye staafu kwa:-
-lazima. Miaka 60.
-kwa hiari. Miaka 55.
-kwa ugonjwa
Pensheni inayolipwa na hazina ni kabla ya 1.7.2004, hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 73 (2)
cha sheria ya mafao ya hitimisho la kazi na 2 ya 1999 NIDHAMU
AINA ZA MAKOSA MA ADHABU ZAKE.

Sera ya menejimenti na ajira katika utumishi wa umma ya mwaka 1999 katika aya za 5.37-37
zimeeleza kuwa KOSA ni kitendo cha utovu wa nidhamu kutokana na kukiuka maadili, kanuni
na masharti ya kazi.

Utaratibu wa kuzingatiwa katika kushughulikia utovu wa nidhamu umeelezwa bayana na


kwamba adhabu zitatolewa kulingana na uzito wa kosa.

Kwa mujibu wa kanuni Na.42 (2) na 43 (2) za kanuni za utumishi wa Umma za mwaka
2003,aina za makosa na adhabu zake zimeainishwa katika nyongeza Na.2.

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHUKUA HATUA ZA NIDHAMU.


(a) Uchunguzi wa awali. Kanuni Na.36

ni lazima mamlaka ya nidhamu ifanye uchunguzi wa awali kabla haijaanza hatua za nidhamu
dhidi ya mtumishi. Hatua hii inasaidia kugundua ukweli kuhusu ukiukwaji na kujiridhisha
kuwa mtumishi amehusika na kuwa kuna uwezekano wa kuthibitisha kosa dhidi yake. Hatua
hii inapunguza uonevu unaoweza kuwepo kwa uchukuaji wa hatua za nidhamu kwa pupa.

(b) makosa na adhabu, kanuni Na.53 na 59.


Makosa madogo madogo (summary proceedings) kanuni Na. 43.
-kuchelewa kufika kazini
-kutokuwepo kazini muda wa kazi
-kutokamilisha kazi.
-uzembe katika kutekeleza majukumu.
-kutotimiza maelekezo ya utendaji kazi.

Adhabu yake
-mara ya kwanza – barua ya onyo
-mara ya pili – karipio
-mara ya tatu – kusimamisha nyongeza ya mshahara.

(c)Makosa makubwa (formal proceedings) kanuni Na.42


-kutofika kazini zaidi ya siku 5
-vitendo vinavyo husu wizi,rushwa
-uzembe uliokithirikatika kutekeleza majukumu
-kujihusisha na kazi nyingine nje ya ofisi saa za kazi.

VITU VYA KUANDAA UNAPOJAZA


1.MKATABA WA AJIRA
- fomu za mkataba nakala 3
- picha za utumishi
-cheti cha taaluma (ualimu) nakala 3
-cheti cha form four/six nakala 3
2.USAJILI PENSHENI
-.barua ya ajira (yenye tsd namba)
-.barua ya kuthibitishwa kazini
-.salary slip halisi
-.picha 2

3.KUSTAAFU
- barua ya ajira ( yenye t sd no)
-barua ya kuthibitishwa kazini
-barua ya kupanda cheo cha mwisho
-salary slip
-picha tatu
-kibali cha kustaafu (ukipate tsd wilaya)
-ujaze fomu za pspf no 6.

4.KUANDAA MIRATHI-MAHITAJI

• -.muhtasari wa wanandugu kumchagua msimamizi wa mirathi


• -.haki ya usimamizi wa mirathi(halisi)
• -.cheti cha kifo(halisi)
• -.barua ya ajira(yenyetsd) nakala
• -.barua ya kuthibitishwa kazini(nakala)
• -.barua ya kupanda cheo cha mwisho(nakala)
• -.salary slip-(halisi)
• -.cheti cha ndoa/ kiapo cha ndoa-(nakala)
• -.kiapo cha mjane/mgane kutunza watoto
• -.vyeti vya kuzaliwa watoto/kiapo(chini miaka 21)
• -.barua toka shuleni kuthibitisha kama mtoto anasoma
• -.picha 8 za msimamizi wa mirathi
• -. picha 3 za kila mtoto wa marehemu
• -. picha 3 za mjane/mgane
• -.kadi za benki za waliopo kwenye mgao(nakala)
• -.fomu na vi ya mgawo wa mirathi(ofisini utapewa)
• -.fomu na8 na 9 za pspf (ofisini utapewa)

VYOTE LAZIMA VIPITIE MAHAKAMANI NA MHURI NA SAINI YA HAKIMU
KILA MTU AVIANDAE AU ATUNZE KUMBUKUMBU ZA UTUMISHI
KWA SABABU NI TOKIO LA KILA MTU

XXXXXXXXXXXX----XXXXXXXXXXXXXXXX----XXXXXXXXXXXXXXX

You might also like