Professional Documents
Culture Documents
Kiswahili - 1
Kiswahili - 1
MAELEKEZO
1. Karatasi hii ina sehemu A na B zenye jumla ya maswali nane (08)
2. Jibu maswali yote ya sehemu A na maswali matatu (3) kutoka sehemu B.
Swali la Tano (05) ni la lazima.
3. Zingatia maagizo ya kila sehemu na ya kila swali.
4. Simu za mikononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba
cha mtihani.
5. Andika Namba yako ya Mtihani katika kila ukurasa wa kijitabu cha kujibia.
1
SEHEMU A (alama 40)
Jibu maswali yote katika sehemu hii
1. Soma kifungu cha habari kifuatacho kwa makini kisha jibu kwa usahihi maswali
yanayofuata.
Baadhi ya wananchi walianza kuamini kuwa huo ndio ulikuwa mtindo wa maisha, wakaanza
kujivunia na kufurahia vitendo vyao vya uovu. Wakaanza kudhihaki uadilifu na wema.
Wanawake vimulimuli wakaanza kuvaa mavazi yasiyo nadhifu bila kimuyemuye. Wakaanza
kukosa huruma na kutamani honoraria kwa kila kazi wanayopewa kuitekeleza, iwe kwa
watoto yatima au kanisani. Ubinafsi umeshamiri, wanawake walioteuliwa na Mungu ili wazae
na kulea watoto wamekuwa ndio watu wasio na huruma: mitaroni, makorongoni, mtoni na
vichakani vichanga kutupa.
2
Maswali
a) Andika kichwa cha habari kisichozidi maneno matano.
b) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyolumika katika habari uliyosoma.
i. Vimulimuli
ii. Kimuyemuye
iii. Honoraria
iv. Akajinasibu
v. Ukiritimba
2. Kwa kutumia mifano kutoka katika lugha ya kiswahili, toa hoja tano kubainisha tofauti
kati ya mofimu na silabi.
3. Fafanua kwa mifano maridhawa dhana zifuatazo kama zinavyotumika katika lugha ya
kiswahili
i. Umilisi wa lugha
ii. Chagizo
iii. Uambishaji wa kisarufi
iv. O-rejeshi
v. Kitenzi kishirikishi
4. Eleza kwa mifano kuntu mambo matano (5) yanayoweza kupelekea mtu kuwa mlumbi
wa lugha katika jamii.
3
SEHEMU B (ALAMA 60)
Jibu maswali matatu (03) kutoka sehemu hii. Swali la tano (05) ni la lazima.
5. Ukiwa kama mtaalamu mbobevu wa taaluma ya tafsiri na ukalimani eleza kwa mifano
kuntu mbinu sita (6) za kutathmini matini.
6. Wewe kama mdau wa elimu, andika insha yenye maneno yasiyopungua 350 na
yasiyozidi 400 kuhusu umuhimu wa Mtaala Mpya wa Elimu ambao jamii itanufaika
endapo utatekelezwa kikamilifu nchini Tanzania kuanzia mwaka 2024. Toa hoja tano
(5).
7. Kwa kutumia mifano kutoka katika Lugha ya Kiswahili, eleza ni kwa namna gani lugha
moja inaweza kusababisha kuibuka kwa utofauti katika lugha hiyo hiyo miongoni mwa
watumiaji. Tumia hoja sita (6) zenye mifano madhubuti.