You are on page 1of 3

SOMO LA KUJITAMBUA

KUJITAMBUA NI NINI ? Neno KUJITAMBUA linatokana na neno TAMBUA lenye


maana ya KUJUA UKWELI WA KITU FULANI KWA KINA , kwahiyo KUJITAMBUA ni
hali ya KUJIJUA VILIVYO KWA KINA . Ingawa watu wengi sana WANAISHI lakini
HAWAJITAMBUI KWA KINA. HUWEZI kuwa MJASIRIAMALI mwenye MAFANIKIO
bila ya KUJITAMBUA. Wakati huo huo HUWEZI KUJITAMBUA BILA KUMJUA
MUNGU. JIULIZE MASWALI HAYA :-- {1}. Kwanini Ulizaliwa ? {2}.Umekuja hapa
duniani kufanya nini ? {3}.Umetokea wapi na unaenda wapi ? AMINI USIAMINI
MATAJIRI ( Watu wenye MAFANIKIO ) duniani kote wanajua kwanini walizaliwa ?
Kwa nini Wanaishi lakini pia wanajua wanakokwenda. Kwahiyo ili UFANIKIWE ni
lazima UJUE UMETOKA WAPI ? NA UNAKWENDA WAPI ? NA KWANINI UPO HAPA
DUNIANI ? Katika MAISHA YA MAFANIKIO ni lazima SIO OMBI kuwa ili Uweze
KUFANIKIWA katika kiwango kikubwa ni lazima uwe umeyapata majibu ya maswali
ya hapo ju

Maama, faida na hasara ya kutojitambua


#KUJITAMBUA NI SOMO LISILOJULIKANA KWA WENGI
Karibu wana FB
Kujitambua ni uelewa wa mtu binafsi kungamua yeye ni nani,anapaswa kufanya
nini, kwa sababu ipi.lini na katka muktadha upi.
Elimu hii ya kujitambua ni adimu mno! Kwani hujikita ndani ya nafsi ya mtu na
kumfanya kuonekana mwenye busara na hekima katika uongeaji ,kimaamuzi na
kimatendo pia bila kufanya hivyo kiunafiki.Pia wapo ambao hujitia ukiziwi,ububu
na wengine kuwa waropokaji ili waonekane wenye elimu ya kujitambua kumbe
hamna kabisa hata chembe ya kujitambua.
Na si wasomi wote hapa duniani na Tanzania ikiwemo ambao hubahatika kuipata
elimu ya kujitambua pamoja na kwamba husoma vitabu mbalimbali ,sehemu
mbalimbali nchi moja na nyingine na kupata vyeti rukuki
(stashada,shahada,shahada ya udhamili n.k) lakini bado hushindwa kupata elimu
ya kijitambua ndio maana baadhi ya watu hutenda matendo ambayo hayaendani na
unavyowaona na unavyowategemea wafanye .
Mfano 1.
-Humu FB kuna baadhi ya watu bado hawana uelewa binafsiri matokeo yake
huchangia hoja kwa maslahi binafsi na si kwa manufaa ya jamii na wengine
huchangia kwa kutumia matusi kwa kudhani wanawakomoa watu ambao hata
hawawafahamu wala hawajawahi kuwaona na hawatakaa wawaone!
Mfano2
Baadhi ya mabosi kutokana na kutojimbua hupenda kumiliki wafanyakazi
wote(hasa wa kike) waliowaajili na kuwatumia kingono bila hata kufikiri faida na
hasara na sababu ya kufanya hivyo na ukioji utaambiwa mapenzi ni upofu wakati
wanaotenda vioja hivyo ndio hujitia upofu.
Pia waweza kuangalia baadhi ya watu wanachosema sicho wanachokifanya mfano
baadhi ya wanaopinga imani za kishirikina ndio watambikaji maarufu! Baadhi ya
watungaji sheria ndio wavunjaji mfano mtu anaua makusudi wala sheria haichukui
mkondo wake na mwingine akiiba kuku hata kama ni mmoja anafungwa miaka
saba (sheria ya wizi wa mifugo).n.k
FAIDA KUU YA KUJITAMBUA.
-Kila akifanyacho mtu anayejitambua hulenga kuchochea na kuleta maendeleo
katika jamii husika.
Ø Kuwa jasiri Au msimamo dhabiti kwa analoamini ni sahihi bila kuyumbishwa na
mtu yoyote.
Ø Kufikia malengo chanya.
Ø Huwa kioo cha jamii (unakuwa barua isomwayo na kila mtu katika jamii).
Ø Kutenda matendo mema (kutetea haki za wanyonge,kupinga ufisadi,n.k) katika
jamii
Ø Hutambua nafasi aliyonayo na jamii humuheshimu bila kushinikizwa mfano
utamskia mtu anamwambia mwenzake “unajua unaongea na mheshiwa?wengine
hulalamika eti pamoja na kutoniita mh, n.k
Ø Mtu huyu huwa sio tegemezi katika jamii..
Ø Huwa ni mtu asiyekuwa na makuu, huwa na matumizi mazuri ya
rasliamali.mfano raslimali watu,ardhi,pesa n.k
Ø Huwa ni mtu wa watu.
Ø Huwa mbunifu (Creative) husoma nyakati.
Ø Huwa anatoa suruhu na sio kulalamika au kulalamikiwa na yeye kuanza
kulaumu na huwa hakati tamaa mpaka siku ya kufa n.k
MADHARA YA KUTOJITAMBUA
-Hathari ni kinyume cha faida tajwa na mjumuisho wa hili;
-Kutojitambua huzorotesha maendeleo kwani mlengwa hufanya mambo hovyo
hovyo).Na hii hupelekea miigogoro kuongezeka katika jamii (Mtu asiyejitambua
huwa chanzo cha migogoro na kero kubwa katika jamii).n.k
HITIMISHO.
Cha kushangaza watu wasiojitambua huwa hawataki msaada wa kuwatoa katika
utumwa wa kutojitambua ndio maana huwa wakali wa kutokubaliana na mkakati
wa anayetaka kuwasaidia ,huku wengi wakibeza na kuweka mbele
vyeo,elimu,umri,pesa,uzuri,umb o n.k japo wengine hukimbilia kujitetea kuwa
binadamu hajakamilika wakati hawako tayari kukamilishwa na wale wenye
kujitambua.Hivyo ni vyema mtu akibahatika kujigundua kuwa ana dalili za
kutojitambua yambidi kujitafakari na kuanza kuchukua taratibu taratibu ili arudi
kwenye mstari

You might also like