You are on page 1of 4

Namna gani mbinu ya Taswira, imetumika kujenga hisia hasi kwenye riwaya ya Barua

Ndefu​ ​Kama​ ​Hii.

Riwaya ya Barua Ndefu Kama Hii ya Mariama Ba ni riwaya inayoonyesha hali halisi ya
maisha ya wanawake katika jamii ya Afrika ya Magharibi (Senegali) haswa wale
waliozaliwa na kulelewa katika dini ya kiislamu. Mwandishi Mariama Ba anatumia mtindo
wa barua ya kirafiki ambayo ni kati ya mfululilizo wa mazungumzo marefu baina ya
marafiki wawili wapenzi. Halikadhalika, anatumia muundo wa urejeshi ambapo amesuka
matukio kwa kurukia rukia yaani katikati, mwanzo kisha matukio ya usoni. Mtindo huo wa
kipekee na msuko wa visa vya kitabu hiki inakifanya kitabu kimvutie msomaji na kusoma
kwa umakini kila kurasa ili apate kuelewa yale yanayoelezwa. Barua hii ndefu inavuta hisia
za msomaji kwa jinsi Mariama alivyoipa taswira umuhimu mkubwa katika barua hii.
Riwaya hii inazunguka misukosuko wanayopitia wanawake wakisenegali huku
wakikamdamizwa na tamaduni pamoja na dini katika jamii inayowazunguka. Kwa kutumia
taswira, Mariama anaonekana kufaulu katika kuwasilisha maudhui yake ilhali akivuta hisia
kali​ ​kwa​ ​msomaji​ ​yeyote​ ​wa​ ​kitabu​ ​hiki​ ​maridadi.

Taswira ni maneno yaliyopangwa katika kazi ya fasihi na kuchora picha kamili ya kitu, hali,
wazo, dhana au uzoefu fulani wa jamii au sehemu ya jamii katika mawazo ya wanaopokea
kazi hii husika. Mbinu hii ya taswira imetumika sana katika hiki kitabu kwasababu ya asili
ya simulizi hii. Ramatulayi mhusika mkuu anajaribu kumjulisha rafiki yake mpenzi Aisatu
aliyekua Marekani juu ya mambo mbali mbali anayopitia kama mwanamke muisilamu wa
kisenegali huku akiweka wazi hisia na mawazo yake juu ya hayo. Pia, anatafakari na
kupambanua maamuzi aliyochukua na anayoendelea kuyachukua katika maisha yake ya kila
siku. Kuwasilisha hisia hizi kwa wasomaji, Mariama anaipa taswira umuhimu mkubwa
akijaribu kuelezea matukio kadha wa kadha kwa undani mkubwa huku akiacha hisia fulani
kwa msomaji. Hisia hasi ni zile hisia ambazo zinazoondoa furaha, zenye kuleta uchungu,
maumivu au zenye kuchukikiza. Hivyo tutaangalia jinsi hisia hizi zilivyojengwa na taswira
katika​ ​kitabu​ ​hiki​ ​cha​ ​barua​ ​ndefu​ ​kama​ ​hii.

Tukianza na tukio ambalo Ramatulayi analitanguliza katika barua yake, kifo cha Modu.
Ramatulayi anaonekana kuumizwa sana na jambo hili ambalo linamfanya apate mawazo
kadha wa kadha. Jinsi watu wanavyompa pole juu ya kifo cha mume wake, mwandishi
anatumia​ ​ishara​ ​ya​ ​mgeni​ ​na​ ​msulubiwa​ ​kuchora​ ​taswira​ ​inayovutia​ ​hisia​ ​kali​ ​za​ ​huzuni.

​ ​‘...​ ​kwayo​ ​nitabadilika​ ​taratibu,​ ​huku​ ​nikiwa


​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​mgeni​ ​na​ ​msulubiwa​​ ​.’​ ​(Ukurasa​ ​wa​ ​3)

Mgeni ni mtu ambaye amefika sehemu kwa mara ya kwanza na aghalabu hukosa ujuzi juu
ya sehemu hiyo na hivyo hutegemea wenyeji au watu wazoefu wa mahali pale ili kupata
maelezo mbalimbali. Mgeni anaweza kupotea yamkini akikosa msaaada. Msulubiwa, kwa
upande mwingine, ni mtu ambaye anateswa kwa kupewa kazi ngumu au mateso mengine
makali ya kimwili kwa kosa fulani aliloshutumiwa. Taswira ya mtu mgeni anayesulubiwa
inaonyesha mtu ambaye anateswa kwa mashutumu asiyo yajua jambo ambalo linavuta hisia
za hasira kwani ni jambo lakionevu lianaloambatana na maumivu makali. Ramatulayi
kupitia kifo cha mume wake anajiona kama mtu anayeteswa na kuhukumiwa kwa kosa
asilolijua​ ​jambo​ ​ambalo​ ​linampelekea​ ​kusema​ ​maneno​ ​hayo.
Halikadhalika, huku akiwa bado na maumivu juu ya habari za kifo cha mumewe,
Ramatulayi​ ​analaani​ ​mauti​ ​ama​ ​kifo​ ​kama​ ​kitu​ ​kilichomtenganisha​ ​yeye​ ​na​ ​mume​ ​wake.

​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​‘​Mauti​,​ ​njia​​ ​iunganishayo​ ​dunia​ ​mbili​ ​zinazopingana:​ ​moja​ ​yenye


​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​vurugu​ ​na​ ​nyingine​ ​tulivu.’​ ​(ukurasa​ ​wa​ ​3)

Mauti kutumia sitiari imelinganishwa na njia katikati ya dunia ya walio hai ambayo
Ramatulayi anaona ni yenye vurugu na dunia ya wafu ambayo ndiyo tulivu. Taswira hii ya
dunia mbili zinaunganihswa na kifo inazidi kuvuta hisia za uchungu kwani zinaonyesha jinsi
gani Ramatulayi anajihisi mpweke kuachwa peke yake kwenye dunia hii ya walio hai
iliyojaa​ ​machafuko,​ ​mateso​ ​na​ ​ghasia.

Mathalani, taswira yakuonekana inayochorwa na mwandishi ni ile ya kwenye msiba wa


Modu. Picha ya mahali palipojaa watu wengi inachorwa huku kila mtu au kundi wakifanya
mambo yao. Mahali hapa ambapo walikuwa wamekusanyika ili kujumuika na waliofiwa
ambao hisia za zimejawa na majonzi ya kutokwa na mpenda wao, pamegeuzwa kuwa
mahali pa kukutania ndugu au jamaa waliopoteana kwa muda mrefu. Vicheko na kelele za
nguvu vinasikika. Katika ukurasa wote wa nane Ramatulayi anaelezea kiundani matukio
yaliyotukia​ ​kwenye​ ​msiba​ ​huo.

​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​‘Marafiki​ ​ambao​ ​walikuwa​ ​hawajaonana​ ​kwa​ ​siku​ ​nyingi​ ​walikumbatiana


​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​na​ ​kupiga​ ​kelele​ ​kwa​ ​nguvu​ ​’​ ​(ukurasa​ ​wa​ ​8)

Taswira hii inavuta hisia za hasira. Ni kawaida katika jamii yetu ya kiafrika watu kutumia
misiba kama sehemu za kukutania kama kwenye maharusi au sherehe nyinginezo. Walakini,
katika riwaya hii Mariama anatumia lugha kutuonyesha jinsi utamaduni huu unaweza
kumiza​ ​au​ ​kuwakera​ ​watu​ ​kadha​ ​wa​ ​kadha​ ​hasa​ ​wale​ ​wafiwa.

Mbali na hayo, taswira nyingine iliyochorwa na kuibua hisia za hasira ni pale ambapo
malenga-mwimbaji mshirikina Farmata alikuwa anajaribu kumshauri Ramatulayi aachane
na​ ​Modu​ ​na​ ​katika​ ​maongezi​ ​yao​ ​akamfananisha​ ​mwanamke​ ​kama​ ​mpira.

​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​‘Mwanamke​ ​ni​​ ​kama​ ​mpira​.​ ​Arushaye


​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​mpira​ ​huo…’​ ​(Ukurasa​ ​wa​ ​54)
Hapo Farmata anatumia tashbiha kuchora picha ya mwanamke kuwa kama mpira
unaorushwa mchezoni kutoka kwa mchezaji mmoja na kwenda kwa mwingine. Taswira hii
ina chora hisia za huzuni lakini pia hasira. Hii ni kwasababu, mwanamke wa kiafrika
anonekana​ ​kama​ ​chombo​ ​yaani​ ​kwanza​ ​anasifa​ ​ya​ ​kumilikiwa.

Kama mpira, mwanamke humilikiwa na mume wake na ndio maana hukusoma usemi katika
maamuzi ya yale yanayoendelea kaika nyumba, yeye kazi yake ni kufuatwa tu yale
anayoelekezwa na mume wake. Halikadhalika, kama mpira, wanaume huwa hawajali
maumivu ya mwanamke. Mtu akiwa anaupiga mpira anaweza kuudundusha, kuurusha au
kuufanyia chochote anachotaka alimradi anahakikishia ushindi kikundi chake. Lakini pia ni
sifa ilioje kuukamata mpira katika mechi. Vivyo ilivyo na wanawake wa kiafrika ambapo
wanaume hutumia wanawake kama chombo cha kujivunia katika jamii lakini wakiwa
kwenye​ ​mahusiano​ ​nao​ ​huwaumiza​ ​kila​ ​watakavyo​ ​bila​ ​kujali​ ​maumivu​ ​yao.

Pia, taswira nyingine inayojitokeza ni pale ambapo Ramatulayi kwa msaada wa Farmata
anagundua kwamba mtoto wake Aisatu, wajina wa rafiki yake kipenzi anayemuandikia
barua, anaujauzito. Aisatu kwa huzuni na majonzi alimuelezea mama yake ukweli wote hadi
kutaja jina la yule anayehusika na uharibufu huo. Ramatulayi anayejawa na mawazo mengi
ya uchungu na bumbuwazi kubwa, anasema maneno ambayo yanasaidia kuchora taswira ya
kusikitisha​ ​mno​ ​kwa​ ​msomaji.

​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​‘Unakuwa​ ​mama​ ​ili​ ​ukabiliane​ ​na​ ​tufani​’


​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​(ukusasa​ ​112)

Tufani ni dhoruba yenye mwendo wa kuzunguka kwa nguvu sana na mara nyingi huleta
uharibifu wa hali ya juu katika mazingira inapotokea. Kuchorwa kwa taswira ya wanamke
anayekabili tufani peke yake inavuta hisia za kusikitisha lakini za kutishika pia. Tufani
katika muktadha huu imetumika kama ishara kuwakilisha magumu yote aliyoyapitia katika
malezi​ ​ya​ ​watoto​ ​wake.

Mpaka hapo Ramatulayi kama mama wa watoto kumi na mbili, alikuwa ameshapitia
mambo mengi sana. Hii inajumuisha mtoto wake Maliki alipogongwa na pikipiki wakati
anacheza mpira (ukurasa 105-108) , Maudo Falli alipogombana na mwalimu wake wa somo
la fasihi juu ya kumuonea na kumnyima maksi alizostahili kupewa (ukurasa 96-98) au pale
ambapo aligundua kwamba watoto wake Aramu, Yasini na Diyinaba walikuwa
wanajihusisha na tabia chafu kama uvutaji wa sigara na hivyo kuwaaadhibu (ukurasa 101-
104). Hivyo basi, tukio hili la mtoto wake tena aliyeuwa anamatumani makubwa naye
kupata mimba kunamfanya atafakari magumu ambayo mama anapitia huku akijaribu kulea
watoto​ ​wake​ ​katika​ ​njia​ ​ipasayo​ ​bila​ ​kujenga​ ​chuki​ ​bain​ ​ayake​ ​na​ ​wao.

Zaidi ya hapo, Ramatulayi anazidi kutafakari ugumu wakuwa mama au mlezi. Katika barua
yake anaandika methali ambayo tena inachora taswira inayovuta hisia za huzuni pale anapo
jiona kama mtu asiyeweza kumpumzika bali ni kudhoofika tu. Aliwaza haya pale
alipokmbuka kwamba japokuwa anauchovu mwingi, hana budi kufanya kazi za nyumbani
pia​ ​na​ ​tena​ ​kwa​ ​haraka.

​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​‘​ ​Mama​ ​mwenye​ ​watooto​ ​hana​ ​muda​ ​wa​ ​kutalii.


​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​ ​Ila​ ​muda​ ​wa​ ​kufa​ ​anao’​ ​(Ukurasa​ ​101)

Methali hii inamaana kuwa, mwanamke mwenye watoto hawezi kuishi maisha ya
kupumzika au yale ambayo angeyataka kama wafanyavyo watalii. Yaani huishi maisha
huku akisubiria kifo tu na kukosa kufanya yale ambayo yangemfurahisha yeye. Hii ni
kwasababu hutumia muda mwingi kulea na kutunza watoto wake na kusahau kujitunza yeye
mwenyewe. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Ramatulayi ambaye alijikita sana kwenye kulea
watoto​ ​wake​ ​kiasi​ ​cha​ ​kusahau​ ​furaha​ ​yake​ ​yeye​ ​mwenyewe​ ​kama​ ​wamama​ ​wengi.

HITIMISHO​:

Mbinu hii ya taswira kwa kiasi kikubwa imeonyesha ujuzi wa Mariama na kusabibisha
hadhira iweze kuelewa maudhui yake kwa undani kwani ameweza kutumia lugha kugusa
hisia zao kiasi cha msomaji kuhisi maumivu aliyoyapata Ramatulayi kama mwanamke
mjane wa kiafrika mwenye watoto kumi na mbili wa kuwalea lakini pia akijaribu kuvumilia
mila a desturi zinazomkandamiza kama mwanamke katika nafasi hiyo. Hivyo, tumeweza
kujifunza mambo kadha wa kadha juu misusuko suko wanayopitia wanawake hawa lakini
pia​ ​maumivo​ ​wanayoyapata.

Marejeo:

Bâ, Mariama, and c Maganga. ​Barua Ndefu Kama Hii​. Dar es Salaam: Mkuki na Nyota
Publishers,​ ​1994.​ ​Print.

You might also like