Professional Documents
Culture Documents
4hours Work-Swahili
4hours Work-Swahili
ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Moja; elewa hofu uliyonayo. Kwanza kabisa lazima uielewe hofu uliyonayo,
kwa kuangalia uhalisia wa kile unachohofia, jipe picha ya nini kibaya kabisa
kinaweza kutokea pale utakapochukua hatua. Je utakufa? Je utapata ulemavu
wa kudumu? Na pia jiulize ni kwa uhakika kiasi gani hayo unayofikiria
yatatokea. Unapoelewa kwa kina kile unachohofia, unapunguza nguvu yake,
kwa mfano utagundua kwamba unachohofia siyo kikubwa kama unavyohofia,
kwa mfano kama utaacha kazi na uingie kwenye biashara, hata kama biashara
hiyo itakufa haiwezi kupelekea wewe kufa, bado utakuwa hai na utaweza
kufanyia kazi mambo mengine, ikiwepo hata kurudi kwenye ajira.
Mbili; fanya kile unachohofia kufanya. Njia pekee ya kuishinda hofu ni kufanya
kile unachohofia kufanya, kwa sababu hofu huwa imebeba kile ambacho
unapaswa kukifanya. Unapata hofu kwa sababu kinakuwa ni kitu kipya na
kikubwa kuliko ulivyozoea. Jijengee tabia ya kufanya kitu kidogo unachohofia
kila siku na hilo litakujengea ujasiri wa kukabiliana na hofu nyingine. Tim
anashauri ujijengee tabia ya kuwasiliana na watu maarufu kila siku na
kuhakikisha wanakupa muda wao, ni jambo gumu na ambalo utahofia
kulifanya, lakini ukiweza litakupa ujasiri sana.
Tatu; jua gharama ambayo hofu inakupa. Piga hesabu na ujue ni gharama kiasi
gani hofu zako zinakuingizia, kwa kujua ni vitu gani unakosa kifedha, kimwili na
hata kiakili kwa kutokuchukua hatua. Unahofia kufanya kwa sababu ya kuona
utapoteza, lakini ambacho huoni ni kwamba kwa kutokuchukua hatua,
inakugharimu sana kifedha, kimuda, kiutulivu wa akili na kadhalika. Hebu fikiria
inakugharimu kiasi gani kuendelea kufanya kazi usiyoipenda kwa miaka
mingine kumi badala ya kuchukua hatua sahihi sasa? Ukishaona gharama
ambazo hofu inakuingizia, inakusukuma kuchukua hatua.
KUWA TOFAUTI NI RAHISI KULIKO KUWA KAWAIDA.
Kinachowazuia wengi kuchukua hatua sahihi kwenye maisha yao ni kukubali
kuwa kawaida. Kufanya kile ambacho kila mtu anafanya kwa namna ambayo
wengine nao wanafanya. Hapa unajiweka kwenye ushindani mkali na hivyo
mambo kuwa magumu.
Lakini kama utachagua kuwa tofauti, unaondokana na kundi kubwa la
wanaofanya kawaida na hivyo inakuwa rahisi kwako, kwa sababu ushindani
unakuwa mdogo na nafasi ya wewe kufanya makubwa inakuwa nzuri.
Tim anatushauri tuache kuweka malengo ya kawaida na badala yake tuweke
malengo ambayo siyo ya kawaida. Yaani kama mtu atasikia malengo yako na
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
kukuambia vizuri basi ujue hayo ni ya kawaida. Lakini kama mtu atasikia
malengo yako na kukuambia acha kujidanganya, huwezi kufikia malengo hayo
basi jua una malengo ya tofauti na una nafasi kubwa ya kuyafikia kama
utajituma kweli.
Unapojiwekea malengo makubwa na yasiyo ya kawaida yanakusukuma sana
kuyafikia na hivyo unaweza kuvuka vikwazo na changamoto nyingi. Lakini
unapokuwa na malengo ya kawaida, unaishia kuchukua hatua za kawaida na
changamoto ndogo sana inatosha kukuondoa kabisa kwenye malengo yako.
Manufaa ni makubwa pale palipo na watu wachache, siku zote kileleni kuna
watu wachache kuliko chini, na hewa safi pia kwa sababu hakuna
msongamano. Hivyo hakikisha wewe unakuwa wa tofauti, unalenga kileleni
penye wachache na siyo chini penye kila mtu.
SWALI MUHIMU KUJIULIZA ILI UWE NA MAISHA BORA KWAKO.
Maswali ambayo wengi wamekuwa wanajiuliza ni nini nataka au yapi malengo
yangu. Maswali yote hayo yamekuwa yanawarudisha kwenye mazoea ambayo
wamekuwa wanayaishi maisha yao yote.
Kama unataka kuwa na maisha bora na ya tofauti kwako, basi unapaswa
kuuliza maswali tofauti pia.
Na swali moja ambalo Tim anashauri kila mtu kujiuliza ni kitu gani
kinanisisimua. Hapa unapaswa kujua kile kitu ambacho kinakupa hamasa
kubwa kukifanya, kile ambacho unapenda kweli kukifanya na upo tayari
kukifanya muda wote. Kitu hiki kinakuwa cha tofauti kabisa kwako na ukikijua
na kukifanyia kazi, maisha yako yatakuwa ya tofauti.
Wengi wamezika vile vitu vinavyowasisimua na kuamua kuishi maisha ambayo
wameangiwa na jamii ndiyo maana maisha yao siyo bora. Epuka hilo kwa kujua
kinachokupa hamasa na kukifanya.
SIFA TATU ZA NDOTO UNAYOPASWA KUJIWEKEA.
Badala ya kuweka malengo ya kawaida kama wengine, unapaswa kuwa na
ndoto kubwa ya maisha ambayo unayataka wewe, yenye maana kwako na
yanayokupa nafasi ya kufanya kile unachopenda.
Katika kujiwekea ndoto hiyo, lazima iwe na sifa hizi tatu;
1. Unaweka hatua kwa hatua za kufikia ndoto hiyo. Usiishie tu kujiambia
unataka kufika sehemu fulani, bali jua utafikaje sehemu hiyo.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Kadhalika kwenye kazi, kama unafanya kazi masaa 10 kwa siku, masaa mawili
yanaleta matokeo makubwa kuliko masaa 8, na kama unatekeleza majukumu 5
kwa siku, jukumu 1 lina matokeo makubwa kuliko majukumu 4 yaliyobaki.
Hivyo ni wajibu wako kujua ni sehemu gani sahihi ya kuweka juhudi na muda
wako ili kupata matokeo bora.
KUWA ‘BIZE’ NI UVIVU.
Kama kila muda uko bize, maana yake wewe ni mvivu na huwezi kufanya
maamuzi sahihi kwako. Kwa sababu kama tulivyojifunza, maeneo machache
ndiyo yanayoleta matokeo makubwa. Hivyo kufanya mambo mengi ni dalili
kwamba huwezi kuchagua yale yaliyo sahihi kwako, na huo ni uvivu.
Uchapakazi ni kuchagua mambo machache yenye matokeo makubwa na
kutafanya hayo huku ukipuuza mengine yote. Uvivu ni kujificha nyuma ya
mambo mengi ambayo hayazalishi matokeo yoyote.
Usiwe mvivu, weka vipaumbele vyako sahihi kulingana na sheria ya 80/20 na
kisha toa matokeo mazuri.
SHERIA YA PARKINSON KWENYE MATUMIZI YA MUDA.
Tumeiona sheria ya Pareto (80/20) kwenye kuweka vipaumbele kulingana na
matokeo yanayozalishwa na hivyo tukiweza kuitumia, tutapunguza sana
majukumu yetu.
Ipo sheria nyingine nzuri sana ambayo tukiweza kuifanyia kazi tutapata muda
zaidi. Sheria hiyo ni ya Parkinson.
Sheria hii inasema kwamba jukumu huwa linachukua muda ambao
limepangiwa kufanyika. Kama una masaa mawili ya kufanya jukumu fulani, basi
litafanyika ndani ya masaa mawili, na kama una masaa nane ya kufanya
jukumu hilo hilo, pia litafanyika ndani ya masaa nane.
Na hii ndiyo sababu ambayo huwa inapelekea watu kuahirisha mambo,
wanapokuwa na muda zaidi wanaupoteza, lakini mwisho unapofikia ndiyo
wanasukumwa kuchukua hatua.
Ili kuitumia sheria hii kwa manufaa yako, jiweke muda mdogo wa kukamilisha
majukumu unayojipa. Kama jukumu umezoea kulifanya kwa masaa nane,
jipangie kulifanya kwa masaa manne, na utaona jinsi ambavyo utakamilisha
jukumu hilo ndani ya muda huo mfupi zaidi.
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
Utaona hapa njia zote tatu zinazungumzia bidhaa na siyo huduma, biashara
pekee unayoweza kuifanya na ukawa huru ni ya kuuza bidhaa. Biashara ya
huduma kama ushauri na nyinginezo, zinakuhitaji uwepo wako na hivyo huwezi
kuzifanya kwa namna ambayo utakuwa huru kabisa na muda wako.
BIDHAA RAHISI KWAKO KUZALISHA NA YENYE FAIDA NZURI.
Katika kutaka uhuru wa muda na fedha, kuna bidhaa ambayo unaweza
kuzalisha kwa urahisi na ambayo utaiuza kwa muda mrefu na kuendelea
kuingiza kipato hata kama hufanyi kazi moja kwa moja.
Bidhaa hiyo ni maarifa.
Ukizalisha maarifa, iwe ni kwa mfumo wa kitabu, video au sauti, unaweza
kuuza bidhaa hiyo kwa miaka mingi hata kama huandiki au kuandaa tena
maarifa hayo. Hivyo hii ni sehemu nzuri kwa kila mmoja kuanzia.
Usijiambie kwamba huwezi kuzalisha maarifa kwa sababu wewe siyo mtaalamu
au mwandishi au mengineyo. Unachopaswa kujua ni kwamba, kuna kitu
ambacho wewe unakijua au una uzoefu nacho na wengine hawajui kama
unavyojua wewe.
Hivyo unaweza kuwasaidia watu hao kupitia ujuzi au uzoefu ambao unao na
ukazalisha maarifa ambayo wengine watakuwa tayari kuyalipia na ukauza kwa
muda mrefu kulingana na uwezo wako wa kuwashawishi watu kununua.
NJIA TATU ZA KUZALISHA BIDHAA BORA YA MAARIFA.
Kama ambavyo tumejifunza, bidhaa za maarifa ni rahisi kwako kuzalisha na
utaweza kuziuza kwa muda mrefu, hivyo ni kitu unachopaswa kufanya.
Zipo njia tatu za kuzalisha bidhaa hizi za maarifa.
Njia ya kwanza ni kutengeneza maudhui wewe mwenyewe, hapa utahitaji
kufanya utafiti kupitia kusoma vitabu na kupata maarifa mengine, kisha
kukusanya pamoja yale maarifa ambayo yatamsaidia mtu unayemlenga.
Njia ya pili ni kukusanya maarifa yanayopatikana bure na kisha kuyapaki vizuri
na kuuza kwa wengine kwa njia ambayo ni bora. Haya ni yale maarifa
yanayopatikana bure kabisa, mfano ripoti mbalimbali za kiserikali na maandiko
ambayo hayana hatimiliki.
Njia ya tatu ni kuwatumia wataalamu kuandaa maudhui na wewe kuwalipa
kwa muda wao au kuwapa kamisheni kwa kila maudhui yanayouzwa. Mfano
unaweza kumchangua mtaalamu wa kitu fulani akaandika kitabu au
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
biashara yako kujiendesha bila ya wewe kuwepo, hapo sasa una nafasi ya
kuweza kuwa popote unapotaka kuwa. Hulazimiki tena kuwa kwenye kazia au
biashara yako muda wote, kwa sababu inaweza kujiendesha yenyewe.
Hatua ya nne kwenye kupata uhuru wa maisha yako ni kuwa na uhuru wa
eneo, yaani kutokulazimika kuwa eneo moja, kuwa huru kwenda popote
unapotaka kwenda kwa wakati unaotaka kwenda.
KUKOSA UHURU WA ENEO NI UMASIKINI.
Kukosa uhuru wa eneo, yaani kulazimika kuwa eneo moja ambapo huwezi
kusafiri au kwenda unapotaka ni umasikini, haijalishi una fedha au mali kiasi
gani. Uhuru wa kweli ni kuwa huru kwa eneo pia, kama unataka kusafiri
unafanya hivyo bila ya kuwa na kikwazo chochote.
KUPATA UHURU KWENYE KAZI.
Kama tulivyojifunza, mpango huu wa kupata uhuru unawafaa watu wote, yaani
walioajiriwa na waliojiajiri. Lakini kwa walioajiriwa, wanahitaji kupata uhuru wa
eneo kwanza kabla hawajapata uhuru wa kifedha.
Na aliyeajiriwa anaweza kufanya hivyo kwa kuangalia jinsi anavyoweza
kutekeleza majukumu yake ya kazi bila ya kuwa eneo la kazi. Watu huwa
wanafanya kazi masaa 8 kwa siku wakiwa kwenye eneo la kazi, lakini ukiangalia
kwa umakini, muda halisia ambao mtu anafanya kazi hauzidi masaa mawili.
Muda mwingine huwa unapotelea kwenye vikao, kwenye mapumziko ya chai,
chakula, kwenye kubishana au kusubiriana kwa mambo mbalimbali.
Hovyo kwa kuijua kazi yako na kujua majukumu ambayo unapaswa
kuyatekeleza, kazi nyingi zinaweza kufanyiwa nyumbani au sehemu nyingine
kwa msaada wa mtandao wa intaneti. Japo siyo kazi zote, kuna kazi ambazo
lazima mtu awepo eneo la kazi, lakini sehemu kubwa ya kazi, mtu anaweza
kuifanya nje ya eneo la kazi.
Na hivi ndivyo makampuni mengi duniani yanafanya, kuepuka gharama za
kuendesha ofisi, yanaruhusu watu kufanyia kazi zao majumbani, hivyo
wanapewa majukumu wanayopaswa kutekeleza na muda wa kutekeleza na
watu hao wanakuwa huru muda gani wafanye kazi.
Kama mwajiriwa hiki ndiyo kitu unachopaswa kukitengeneza kwenye ajira
yako, kuangalia namna unavyoweza kutekeleza majukumu yako ya kazi bila ya
kuwa eneo la kazi na kisha kumshawishi bosi au mwajiri wako akupe nafasi ya
kujaribu hilo. Nenda kwake ukiwa na mpango kamili, ukionesha jinsi gani
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007
SOMA VITABU TANZANIA WWW.T.ME/SOMAVITABUTANZANIA
HITIMISHO.
Umejifunza mambo muhimu sana kupitia uchambuzi huu wa kitabu cha THE 4-
HOUR WORKWEEK, umejifunza hatua nne za kufikia uhuru kamili wa maisha
yako na jinsi ya kuzifanyia kazi.
Sasa kazi ni kwako kwenda kuyaweka kwenye matendo ili uweze kupiga hatua
na kufanikiwa kwenye maisha yako. Kumbuka haya yote yanawezekana ila
yanahitaji uweke mipango yako mwenyewe na ujipe muda wa kutengeneza
uhuru huu. Japo mwishoni utakuwa huru, lakini mwanzoni lazima uweke kazi
hasa kwenye kujenga misingi ya biashara ambayo itaweza kujiendesha bila ya
wewe. Muhimu ni kuchagua kuyaishi maisha yako na kuacha kuiga maisha ya
wengine.
Kuendelea kupata chambuzi za kina za vitabu na vitabu vilivyochambuliwa,
jiunge na channel ya SOMA VITABU TANZANIA, kwa kufungua
www.t.me/somavitabutanzania
Kupata vitabu mbalimbali vya kujisomea tembelea www.somavitabu.co.tz
JIUNGE KUPATA UCHAMBUZI WA VITABU TUMA UJUMBE KWA TELEGRAM NAMBA 0678 977 007