You are on page 1of 8

MUKHTASARI

Familia ya mvulana aliyedungwa jembe kichwani


yaomba usaidizi kumzika mtoto wao
Mtoto wa miaka 14 azuiliwa kwa madai ya
kumchoma kisu shemejiye hadi kufa
Wakili Miguna afichua siku atakayo wasili nchini
Mwalimu aliyenajisi msichana wa miaka 10
amehukumiwa kifungo cha maisha

HABARI KAMILI
Familia ya mvulana wa miaka miwili aliyefariki
katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta alipokuwa
akifanyiwa upasuaji wa kuondoa jembe la uma
lililokuwa kwenye fuvu la kichwa chake inaomba
msaada wa kifedha kwa ajili ya mazishi yake.
Nyanya wa mvulana huyo Asha Njeri alisema kuwa
familia hiyo ni maskini na haiwezi kupata pesa za
kugharamia bili ya hospitali pamoja na gharama za
mazishi. Njeri alikuwa ametembelea familia hiyo
katika kijiji cha Ndula huko Thika Mashariki kabla
ya msiba huo kutokea.
Alisema bintiye, Judy Muthoni, mama wa marehemu
ni mama asiye na mwenzi na mfanyakazi wa
kawaida katika kijiji hicho na kwa hivyo atakabiliwa
na kazi kubwa ya kutafuta pesa zinazohitajika. Bi
Njeri alisema kuwa msiba huo umewasumbua sana
hasa binti yake, aliongeza kuwa binti yake hawezi
hata kuongea kwa sasa.
Njeri alisema yeye na Muthoni hawakuwa nyumbani
ajali hiyo ilipotokea.Marehemu na kaka yake
mkubwa mwenye umri wa miaka mitano walikuwa
wakicheza nje ya nyumba yao pamoja na watoto
wengine wakati mtoto huyo alipopita mbele ya kaka
yake aliyekuwa na jembe la uma na likatua kichwani
kwa bahati mbaya.
Njeri alisema kuwa hawakuwa nyumbani lakini
bado walikuwa ndani ya kijiji, aliongeza kuwa
walipigiwa simu na majirani waliowajulisha kuhusu
ajali hiyo. Majirani, wakiongozwa na Rachael
Harrison ambaye pia ni mfanyakazi wa kujitolea wa
afya katika kijiji hicho, walisema kwamba walisikia
kilio kikubwa cha mtoto huyo na kukimbilia eneo la
tukio na kumkuta kijana huyo akivuja damu nyingi
huku akiwa na jembe kichwani.
Mvulana huyo alikimbizwa katika zahanati ya kijiji
na daktari (aliyetambulika kama Cyrus) alimpa
huduma ya kwanza na kisha kumkimbiza katika
hospitali ya Thika Level 5 kwa gari lake. Mvulana
huyo alipofika hospitalini hali yake iliboreshwa na
CT Scan kuchukuliwa kabla ya kuelekezwa katika
KNH.
Hata hivyo, majirani hao walinyooshea kidole cha
lawama wasimamizi wa KNH kwa kuchukua muda
mrefu kumhudumia mvulana huyo, wakisema kuwa
ni uzembe uliosababisha mvulana huyo asiye na
hatia kufariki alipokuwa akifanyiwa upasuaji.

Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 14 wa


darasa la 4 anayeshtakiwa kwa kumdunga kisu
shemeji yake miezi mitatu iliyopita atasalia katika
gereza la watoto kwa wiki tano zaidi. Mahakama
kuu mjini Eldoret ilitoa uamuzi huo siku ya
Jumatano.
Jaji  Eric Ogola aliagiza kuwa mwanafunzi huyo
aendelee kuzuiliwa katika kituo hicho
kinachosimamiwa na serikali kwa usalama wake wa
kibinafsi hadi itakapothibitishwa kuwa ni salama
kwake kuachiliwa kwa bondi.
Ogola alisema kuwa ameagiza kwamba mshtakiwa
wa kwanza azuiliwe katika gereza la wanawake la
Eldoret GK akisubiri matokeo ya ripoti ya afisa wa
uangalizi wa shule huku mtoto mchanga akizuiliwa
katika makao ya watoto.
Mtoto huyo anashtakiwa pamoja na dadake Lucy
Njeri, 27 na mfanyabiashara wa chang’aa kwa
kumuua shemeji yake kwa kutumia kisu cha jikoni.
Walishtakiwa pamoja kuhusiana na madai ya mauaji
ya Jacob Kioni mnamo Agosti 7 katika mtaa wa
Manyatta huko Moi’s bridge kaunti ya Uasin Gishu.
Mtoto huyo anasemekana kumdunga shemeji yake
kwa kutumia kisu cha jikoni alipokuwa akijaribu
kuwatenganisha marehemu na washtakiwa wenzake
walipokuwa wakipigania kikombe cha chang'aa.
Juhudi za kuwaokoa marehemu hazikufua dafu
kwani alifariki baada ya kuwasili katika hospitali ya
Kaunti Ndogo ya Moi’s bridge. Hakimu aliagiza
kwamba suala hilo litajwe Novemba 17 wakati ripoti
ya afisa wa uangalizi wa sheria itakapotolewa
mahakamani. Jaji Ogola aliagiza washukiwa hao
wapelekwe katika Hospitali ya Rufaa ya Moi mjini
Eldoret kufanyiwa uchunguzi wa kiakili na pia
kutathminiwa umri kabla ya kuwasilisha ombi.

Serikali imeondoa arifa nyekundu zilizowekwa


kwa wakili Miguna Miguna mnamo Machi 2018.
Wakili huyo alifichua hayo Jumatano akisema sasa
atasafiri kurejea Kenya Oktoba 20.
“Serikali ya William Ruto na Rigathi Gachagua
imeondoa Arifa Nyekundu zilizowekwa dhidi yangu
na Uhuru Kenyatta kinyume cha sheria na
ushirikiano wa Raila Odinga.
Miguna alisema kwenye ukurasa wake wa twitter
kuwa serikali ya William Ruto na Rigathi
Gachagua.imeondoa Arifa nyekundu zilizowekwa
dhidi yake na Uhuru Kenyatta kinyume cha sheria na
ushirikiano wa Raila Odinga. Aliongeza kuwa
kuwasili kwake kutakuwa Octoba 20 6:00 asubuhi.
Kuondolewa kwa marufuku ya kusafiri sasa
kunamaliza kusubiri kwa zaidi ya miaka mitatu kwa
wakili huyo kurejea nyumbani baada ya kufukuzwa
kwa nguvu hadi Kanada mnamo Machi 2018.
Mnamo Septemba 13, Miguna alidai kuwa arifa hizo
nyekundu zingeondolewa siku moja baadaye lakini
hazikutimia.
Aliwaambia Wakenya kwamba Rais William Ruto
alikuwa amemhakikishia kurejea kwake mara tu
arifa hizo nyekundu zitakapoondolewa. Alidai
kuhamishwa kwa nguvu hadi Kanada mnamo Machi
28, 2018.
Hii ilikuwa mara yake ya pili kutolewa nje ya nchi
hadi Kanada, nchi ambayo pia ana uraia halali.
Serikali ilisisitiza kuwa yeye si raia wa Kenya.

Mwalimu katika shule ya kibinafsi jijini Nairobi


ambaye alimshawishi msichana wa miaka kumi
hadi nyumbani kwake kabla ya kumnajisi
amehukumiwa kifungo cha maisha na mahakama ya
Kibera.
James Mawanda alipewa adhabu hiyo Jumatano na
hakimu mkuu wa Kibera Ann Mwangi baada ya
upande wa mashtaka kuthibitisha kesi dhidi yake.
Mwangi alisema kuwa upande wa mashtaka
ulithibitisha kosa la unajisi bila shaka yoyote na
wakati huo amezingatia upunguzaji wa mshtakiwa
na kwa hivyo anamhukumu kifungo cha maisha.
Mwendesha mashtaka aliambia mahakama kuwa
mshtakiwa alitenda kosa hilo katika tarehe tofauti
kati ya Agosti 2018 na 2019 huko Kibera, eneo la
Katwekere ndani ya kaunti ya Nairobi.
Mahakama ilisikia kuwa Mawanda alikuwa na
mazoea ya kumrubuni msichana huyo nyumbani
kwake ili kumfanyia 'mateso'. Mwendesha mashtaka
wa mahakama Jeff Musyoka aliwaita mashahidi
kadhaa waliotoa ushahidi katika kesi hiyo kabla ya
mahakama kujitangaza.
Musyoka aliomba mahakama kumpa mshtakiwa
adhabu kali ili iwe somo kwa watu wengine ambao
wanaweza kufikiria kutenda makosa hayo.
Mshtakiwa alikuwa ameshtakiwa kwa shtaka la pili
la kutenda kitendo kichafu na mtoto mdogo na
makosa mengine kadhaa ya kujaribu kuwanajisi
watoto wengine.
Mahakama, hata hivyo, ilitupilia mbali mashtaka ya
kujaribu kunajisi. Hakimu alisema kutokana na
ushahidi wa mtoto mdogo na wa mashahidi wengine
wakuu waliotoa ushahidi mahakamani hapo ni
dhahiri mshitakiwa alitenda kosa hilo. Wakati akitoa
hukumu hiyo, Hakimu alisema kuwa kosa hilo ni la
kinyama ikizingatiwa kuwa aliyeuawa ni mtoto
mdogo.

MWISHO

You might also like