Professional Documents
Culture Documents
MWONGOZO WA
KUUNDA NA
KUTEKELEZA SERA
YA USALAMA NA AFYA
MAHALI PA KAZI
USIMAMIZI NA UDHIBITI WA NYARAKA HII
Mwenye Msimamizi Wafaidika Imepitishwa
Nyaraka na:
Toleo Upitishaji Mkurgenzi wa
Mkaguzi maeneo ya
usalama na afya Bodi ya Ushauri
Mkuu kazi
mahali pa kazi
1.0 Saini
©2021 Tarehe
Mwongozo wa Kuunda na Kutekeleza Sera ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi
YALIYOMO
1. Utangulizi 4
1.1. Muktadhi wa Kisera 5
1.2. Mahitaji ya Kisheria 5
1.3. Malengo ya Mwongozo 5
1.4. Wigo wa Mwongozo 6
1.5. Matumizi ya Mwongozo 6
1.6. Baadhi ya Maneno, Ufupisho na Misemo Iliyotumika 6
5. Kuhusianisha Sera 22
5.1 Utaratibu wa Kuhuisha Sera 22
5.2 Ubora wa Sera 22
Viambata 23
i: Mfano wa Tamko la Sera ya Usalama, Afya na
Ustawi Mahali pa Kazi 23
ii: Mtiririko wa Sera na Utaratibu wa Kuitekeleza 24
iii: Orodha Hakiki ya Kupima Ubora wa Sera 26
iv: Uthaminishaji wa Sera 32
Rejea 35
KUTAMBUA WALIOCHANGIA
KUANDAA MWONGOZO
1. UTANGULIZI
■
Majukumu ya Kiwajibu – Ni yale Majukumu ambayo mhusika
atayatekeleza kama yalivyoainishwa. Mfano wa majukumu ya
aina hii ni wajibu wa kuvaa barakoa kwenye maeneo yenye
vumbi.
■
Majukumu ya Kimamlaka – Ni yale Majukumu yanayomtaka
aliyepo eneo la kazi kuchukua hatua halali zenye lengo la
kuzuia ajali, tukio au ugonjwa utokanao na kazi. Majukumu
haya yanatoa mamlaka ya moja kwa moja ya kudhibiti athari
za vihatarishi katika eneo alipo mhusika. Mfano wa majukumu
ya aina hii ni wajibu wa kutowasha mashine ambayo mikanda
yake haijafunikwa.
■
Mwongozo – Haya ni maelezo yanayofafanua namna ya
kutekeleza jambo au kazi Fulani kwa kutumia lugha rahisi fasaha
na inayoweza kubadirishwa kirahasi kuwa katika vitendo.
2.
UHUSIKA NA MAJUKUMU
YA KILA MDAU
3.
MUUNDO WA SERA YA USALAMA
NA AFYA MAHALI PA KAZI
Aidha, aina ya athari zitokanazo na vihatarishi kama
vilivyofanyiwa tathmini ya vihatarishi mahali pa kazi ni muhimu
kuwa sehemu ya maandalizi ya kutengeneza sera ya usalama
na afya mahali pa kazi.
a. Majukumu ya mwajiri;
Utaratibu wa kutekeleza sera ufafanue majukumu ya kiwajibu
anayotakiwa kuyatekeleza mwajiri Ikiwemo: -
i. Kuhakikisha utekelezaji wa matakwa ya sheria wakati
wote wa uhai wa eneo la kazi unafanyika kwa ufanisi;
ii. Kumlinda mfanyakazi na wadau wengine dhidi ya
vihatarishi vyote vinavyohusiana na eneo la kazi;
iii. Kutengeneza mazingira rafiki yenye staha kwa ajili ya
kufanyia kazi;
iv. Kuwakinga wafanyakazi wanapokuwa kazini dhidi ya
ubaguzi, unyanyasaji, unyanyapaa na udhalilishaji wa
aina yoyote;
v. Kugharamia vifaa na shughuli zote za usalama, afya na
ustawi mahali pa kazi;
vi. Kuhakikisha anashirikiana na mamlaka za usimamizi
Ikiwemo OSHA ili kuwezesha programu za masuala ya
usalama na afya mahali pa kazi zinatekelezeka kwa
ufanisi;
vii. Kubadilishana (sharing) taarifa za usalama na afya kati
ya mwajiri na wadau wakiwemo wafanyakazi hasa haki
za kulindwa dhidi ya vihatarishi mahali pa kazi.
b. Majukumu ya mwajiriwa;
Mwongozo wa kutekeleza sera pia ufafanue majukumu
ya kiwajibu anayotakiwa kutekeleza mwajiriwa Ikiwemo
kuhakikisha kuwa: -
i. Anatii kanuni na kufuata taratibu za usalama, afya na
ustawi mahali pa kazi wakati wote akiwa eneo la kazi;
ii. Anatoa ushirikiano kwa mwajiri katika kutoa na kupokea
taarifa za usalama, afya na ustawi mahali pa kazi kadri
anavyozipata au kuzibaini;
iii. Analinda na kusimamia miundombinu ya kudhibiti athari
za vihatarishi mahali pa kazi;
iv. Kuhakikisha kuwa anajilinda yeye na watu wengine
wanaoweza kuathirika na kazi anazozifanya.
UTARATIBU WA KUUNDA,
4. KUTEKELEZA NA KUHUISHA
SERA
5. KUHUSIANISHA SERA
VIAMBATA
Wajibu:
■ U
ongozi utafanya kazi kwa kushirikiana na wafanyakazi hasa Kamati za usalama na afya mahali pa
kazi ili kuchukua hatua stahiki zenye lengo la kudhibiti athari za vihatarishi mahali pa kazi;
■ M
eneja na wasimamizi wanawajibika Kuhakikisha wanaowasimamia wanatekeleza majukumu yao
kwenye mazingira rafiki, salama na yasiyo hatari kwa afya. Wajibu huu unajumuisha kutoa Mafunzo
au maelekezo stahiki Sambamba na kufuatilia malalamiko yaliyowafikia Ikiwemo Mapendekezo ya
kufanya maboresho;
■
Wasimamizi, Wafayakazi, Wakandarasi, Watoa huduma na Wageni wanatarajiwa na (JINA LA
KAMPUNI AU ENEO LA KAZI) kutekeleza majukumu yao kwa njia zilizo rafiki kwa afya, usalama na
ustawi wao pamoja na watu wengine;
■
(JINA LA KAMPUNI AU ENEO LA KAZI) imedhamiria Kuwezesha Mafunzo, miundombinu – kazi
na maelekezo yote stahiki ili kuhakikisha utendaji kazi ndani ya himaya ya (JINA LA KAMPUNI AU
ENEO LA KAZI) ni rafiki, salama na usio na hatari za afya au ustawi;
■
Endapo italazimika, (JINA LA KAMPUNI AU ENEO LA KAZI) itachukua hatua za kinidhamu kwa
yule atakayeshindwa kutekeleza wajibu wa kufanya kazi kwa usalama au asiyetii sheria zilizopo za
usalama, afya na ustawi sehemu za kazi Ikiwemo sera na utaratibu kama (JINA LA KAMPUNI AU
ENEO LA KAZI) ilivyoainisha.
Kudhibiti ajali, magonjwa kazini pamoja na uharibifu wa mazingira ni wajibu wa kila mmoja. (JINA LA
KAMPUNI AU ENEO LA KAZI) inatarajia kila mmoja atashirikiana na (JINA LA KAMPUNI AU ENEO LA
KAZI) kwa kuweka juhudi endelevu za kila siku za kusimamia usalama, afya na ustawi mahali pa kazi na
kwamba kila mmoja atapimwa kutokana na matokeo ya juhudi zake.
1. Utangulizi
Elezea Chimbuko la Kuanzisha eneo tajwa la kazi ukionyesha
matarajio yaliyopo ya kukuza uzalishaji kwa kuzingatia ushiriki wa
wadau wa ndani na nje sambamba na uendelevu wa uzalishaji. Pia
onyesha malengo ya kibiashara, kijamii, kiustawi, usalama, afya
na mazingira. Sehemu hii ionyeshe namna sera na sheria za nchi
zitakavyozingatiwa. Aidha, onyesha endapo eneo la kazi tajwa linazo
sera nyingine zaidi ya sera ya usalama na afya mahali pa kazi. Isitoshe,
onyesha namna sera ya usalama na afya mahali pa kazi ilivyo muhimu
ukilinganisha na sera zingine. Utangulizi usizidi maneno 150.
6. Walengwa wa Sera
Ainisha walengwa wote wa sera ya usalama na afya mahali pa kazi
ukionyesha ushiriki wao katika hatua zote za uhai wa sera. Sehemu
hii isizidi maneno 150.
7. Tamko la Sera
Andika tamko rasmi la sera ukiacha nafasi ya kusainiwa na Afisa
Mtendaji wa ngazi ya juu kabisa kwenye eneo la kazi sambamba na
saini ya Mwakilishi wa Usalama na Afya Mahali pa kazi anayewakilisha
kitengo/Idara ambayo ni muhimili (core function) ya eneo la kazi.
Tamko lisizidi maneno 350.
REJEA
Mtendaji Mkuu:
S.L.P 519, Dar es Salaam,
Kiwanja Na. MNY/KMB/565, Kinondoni,
Barabara ya Mahakama,
Simu: +255 (0) 22 2760548, Nukushi: +255 (0) 22 2760552,
Barua Pepe: info@osha.go.tz, Tovuti: www.osha.go.tz