You are on page 1of 5

Zeraki Achievers Exam (2021)

102/3 - KISWAHILI - KARATASI YA 3


FASIHI
DISEMBA/JANUARI 2021
Muda: Saa 2½

Jina……………………………………………………. Nambari ya usajili ………………

Jina la Shule…………………………………………... Darasa……………………………..

Sahihi ya Mtahiniwa…………………………………. Tarehe……………………………

MAAGIZO

a) Andika jina lako na nambari yako katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
b) Jibu maswali manne pekee.
c) Swali la kwanza ni la lazima.
d) Maswali hayo mengine matatu yachaguliwe kutoka sehemu nne zilizobakia yaani
tamthilia, Ushairi, Hadithi fupi na Fasihi Simulizi.
e) Usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja.

SWALI UPEO ALAMA

1 20

20

20

20

JUMLA

© Zeraki- 2021 Page 1 of 5


SEHEMU YA A: FASIHI SIMULIZI

1. Swali la lazima
Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali
“Wewe ni mbumbumbu kiasi kwamba ukiona picha yako kwenye kioo unashangaa ulimwona
wapi mtu huyo.”

a. i.Bainisha kipera hiki (alama 1)


ii. Bainisha sifa nne za kipera hiki (alama 4)
iii.Kipera hiki kina faida gani katika jamii yako? (alama 5)
iv)Bainisha changamoto zozote tano zinazoweza kumkumba mtu ambaye angependa
kukusanya data kuhusu kipera hiki. (alama 5)

b. Eleza namna jamii yako inavyojaribu kuhifadhi fasihi simulizi (alama 5)

SEHEMU YA B: TAMTHILIA YA KIGOGO (Pauline Kea)

2. ‘Tusiwaruhusu watu wachache waliojazwa kasumba….kuturejesha ….hatuwezi


kukubali kutawaliwa kidhalimu tena.’

a. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

b. Kwa kumrejelea mzungumzaji wa maneno haya, bainisha unafiki katika kauli hii.
(alama 16)
AU

3. Eleza jinsi mbinu ya taharuki ilivyotumika kufanikisha maudhui katika tamthilia ya


kigogo.(alama 20)

SEHEMU YA C: CHOZI LA HERI (Assumpta K. Matei)


4. “Hakuna amani bila kuheshimu mwanamume”

(a) Eleza muktadha wa dondoo hili (alama 4)


(b) Tambua maudhui yanayodokezwa katika usemi huu. (alama 1)
(c) Huku ukitoa hoja kumi na tano, fafanua nafasi ya mwanamke katika riwaya ya Chozi la
Heri (alama 15)
AU
5.(a) ”Bila hisani,jamii haisimami”.Thibitisha ukirejelea jamii ya Wahafidhina
(alama 10)

© Zeraki- 2021 Page 2 of 5


(b) Baada ya dhiki faraja. Onyesha namna ukweli wa methali hii unavyodhihirika katika
riwaya ya Chozi la Heri (alama 10)

SEHEMU YA D: HADITHI FUPI-TUMBO LISILOSHIBA NA HADITHI


NYINGINE
6.”Kwanza nilimwogopa sana…kwa sababu kila siku alinitishia…”
(a)Fafanua muktadha wa dondoo (alama 4)
(b)Eleza sifa zozote nne za msemaji . (alama 4)
(c)Ni sababu zipi zilichangia msemaji kujikuta katika mikono ya mrejelewa? (alama 4)
(d)Jadili masaibu wanayopitia watoto huku ukirejelea hadithi hii (alama 8)
AU
7. Ukengeushi huzorotesha maendeleo ya kijamii. Jadili kauli hii ukirejelea hadithi ya
‘Mkubwa’. (alama 20)

SEHEMU YA E: USHAIRI

8. Soma shairi hili kisha ujibu maswali yafuatayo.

Nikumbuke mwanangu,
Kila asubuhi unapoamka
Kwenda kazini,
Unapochukua sabuni ya kunukia,
Na dodoki jororo.

Na kopo la koligeti,
Kwenda kukoga hamumuni,
Penye maji ya bomba,
Yaliyochujwa na kutakaswa,
Mororo…

Kumbuka nyakati zile,


Za staftahi ya sima na mtama,
Ndizi na nagwa,
Kwa mchicha na kisamvu,
Na ulipokwenda choo,

© Zeraki- 2021 Page 3 of 5


Ulilia kwa uchungu

Nikumbuke,
Unapotoka nyumbani asubuhi maridadi,
Katika suti ya moto,
Miwani ya pembe,
Viatu vya Paris,
Saa ya dhahabu,
Unapong’oka kwenda kazini,
Katika Volvo,
Katika njia iliyosakafiwa

Kumbuka,
Nyakati zile,
Mimi na mamako,
Tulinyojidamka,
Mara tu kwale wa kwanza,
Alipoanza kukoroma,
Jogoo wa kwanza hajawika,
Mimi nikachukua mundu na panga,
Mamako jembe na shoka,
Tukaelekea porini,
Kufyeka na kuchimbua

Nahubaki wajiandaa kwenda shule…


Nikumbuke,
Saa za jioni,
Unapovalia kitanashati.

Maswali
(a)Thibitisha kuwa utungo huu ni shairi (alama 2)
(b)Fafanua toni ya utungo huu (alama 1)
(c)Huku ukitoa mifano,linganua kati ya mistari toshelezi na mistari mishata (alama 4)
(d) Eleza maudhui yoyote matatu yanayojitokeza kwenye shairi (alama 6)

© Zeraki- 2021 Page 4 of 5


(e)Eleza hulka zozote nne za nasfi nenewa (alama 4)
(f)Bainisha mbinu za kimtindo kwenye vifungu vifuatavyo. (alama 3)
i.Kumbuka nyakati zile
ii.Na kopo la koligeti
iii.Mimi nikachukua mundu na panga

© Zeraki- 2021 Page 5 of 5

You might also like