You are on page 1of 3

PERFECT STEPS PUBLISHERS

END TERM EXAMS 2015


0721 745374/ 0721 707626 NAIROBI

MUHULA WA MWISHO WA MWAKA 2015

102/3
KISWAHILI
KARATASI YA 3
FASIHI
MUDA: SAA 2 ½

SEHEMU A : TAMTHILIA
Timothy Arege: Mstahiki Meya
Swali la lazima

1. “Fahamu hili. Anayeliogopa tope kumwangukia hawezi kujua njia nzuri ya kulisafisha ……..”
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili. ( alama 4 )
(b) Fafanua sifa za anayerejelewa. ( alama 6 )
(c ) Onyesha jinsi uozo unavyodhihirika katika baraza. ( alama 10)

SEHEMU B : RIWAYA
Ken Walibora : Kidagaa Kimemwozea
Jibu swali la 2 au la 3
2. “…. Lakini wewe kijana si tayari wafanyakazi…..”
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
(b) Fafanua sifa zozote mbili za msemewa. ( alama 4 )
(c ) Kwa kutolea mifano mwafaka, eleza jinsi mbinu ya kinaya ilivyotumiwa
kuelezea hali ya maisha ya msemaji. ( alama 12 )

3. Viongozi wanachangia kuzorota kwa maendeleo katika jamii. Thibitisha ukweli wa


kauli hii kwa mujibu wa riwaya ya Kidagaa Kimemwozea. ( alama 20 )

SEHEMU YA C USHAIRI
Jibu swali la 4 au 5
4. VITA VYA NDIMI
Huyo !Amshike huyo !
Hakuna bunduki wala kifami
Bomu na risasi hata hawazijui
Lakini mno wanashambuliana
Kwa ndimi zilizonolewa kwa makali
Vipande vya matusi silaha zao

Yu imara mmoja wao


Akirusha kombora la neno zito!
Linitingishe adui wake
Na kumgusa hisia kwa pigo kuu
Pigo linalochoma moyoni kama kichomi
Kuchipuza joto la hasira na kisasi
Katika mapigano yaso na kikomo
Filimbi ya suluhu inapulizwa kuwaamua!
Ni nai anayekubali suluhu?
Roho zinakataa katakata
Huku ukaidi ukinyemelea na kutawala kote
Mapandikizi ya watu yakipigana
Vita shadidi visivyo ukomo
Vita vya ndimi!

Magharibi sasa
Jua linapungia mkono machweo
Nalo giza likinyemelea kwa kiburi na
Kasi
Sisikii tena sauti za mIsonyo
Mate ya watesi yamekauka
Makanwa yao yamelemewa na uchovu
Sasa wameshikana mikono
Ishara ya suluhu

Maswali
(a)Hili ni shairi la aina gani? (al.1)
(b) Eleza dhamira ya mshairi (al.2)
(c) Eleza sifa za utunzi alizotumia mshairi (al.3)
(d) Taja tamathali zozote tatu alizotumia mshairi (al.3)
(e) Eleza toni ya mshairi katika beti tatu za awali (al.1)
(f) Eleza hatima ya yanayozungumziwa kwenye shairi (al.2)
(g) Mshairi ametumia alama hisi kwingi. Eleza umuhimu wake (a.2)
(h) Itambue nafsi neni katika shairi (al.1)
(i) Andika mishororo ya kwanza mitatu ubeti wa 4 kwa lugha ya nathari (a.3)
(j) Toa maana ya msamiati huu (al.2)
(i) Kombora
(ii) Misonyo

5. Soma shairi ulilopewa kwa makini kisha ujibu maswali


Mwenye macho wafishasha, wajiona kama ndovu
Kitu kimekulewesha, huutambuwi uovu,
Ngoma yako itakesha, au ni nguvu za povu.
Tangu lini muwerevu, akajinyowa mwenyewe?

Tangu ukipate kitu, ‘megeuka mpumbavu,


Kau hutuamini mtu, ambaye kwamba mtovu,
Wafikiri kisu gutu, hakikati nyama pevu?
Tangu lini muwerevu, akajinyowa mwenyewe?

Wangapi meonekana, mibakhili mishupavu,


Waliyo wakijitona, na wingi usuluhivu,
Leo hawanasi tena, wage ukila maivu.
Tangu lini muwerevu, akajinyowa mwenyewe?

Kupata kusikughuri, ukajidhani mwerevu,


Wa hicho chako kiburi, wewe ni maangavu,
Iko siku itajiri, ujikute kwenye wavu
Tangu lini muwerevu, akajinyowa mwenyewe?

Kila mwenye kukuonya, uiwate ndiya mbovu,


Huchelewi kumuvinya, kumvunda zake mbavu,
Fanya ambayo wafanya, hutajinyowa mashavu,
Tangu lini muwerevu, akajinyowa mwenyewe?

Maswali ya shairi.

(a) Lipe shairi hili kichwa mwafaka. ( alama 1 )


(b) Fafanua toni ya mwandishi. ( alama 2 )
(c) Eleza dhamira katika shairi hili. ( alama 2)
(d) Pambanua umbo la ubeti watatu. ( alama 3 )
(e) Dhihirisha tamathali ya usemi iliyotumiwa katika mloto wa ubeti wa pili. ( alama 2 )
(f) Kwa kutoa mifano , onyesha mbinu ambazo mwandishi ametumia kufanikisha kazi yake kiarudhi
( alama 4 )
(g) Uandike ubeti wa nne kwa lugha ya nathari. ( alama 4 )

(h) Eleza maana za maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika shairi. ( alama 2 )
(i) Kitu
(ii) Mtovu

SEHEMU D : FASIHI SIMULIZI


Jibu swali la 6 au 7.

6. (a) Ni nini maana ya maghani. ( alama 2 )


(b) Eleza sifa nne za maghani. ( alama 8 )
(c ) Fafanua aina tano za maghani. ( alama 10 )

7. (a) Eleza majukumu manne ya maigizo. ( alama 4 )


(b) Eleza sifa tatu za mwigizaji bora . ( alama 6)
(c ) Fafanua vipera hivi vya maigizo
(i) Matambiko ( alama 2 )
(i) Vivugo ( alama 2 )
(ii) Chekechea ( alama 2)
(d) Eleza namna ambavyo jamii ya kisasa inavyoendeleza fasihi simulizi. ( alama 4 )

SEHEMU YA E: HADITHI FUPI


DAMU NYEUSI na KEN WALIBORA na S.A MOHAMMED

8. Eleza kwa tafsili namna maudhui yafuatayo yalivyoendelezwa katika hadithi za


‘Samaki wa nchi za joto’ na ‘Mwana wa darubini.’ (alama 20)
(a) Utabaka
(b) Nafasi ya mwanamke katika jamii.

You might also like