Professional Documents
Culture Documents
NENO LA MUNGU
WAKATI WA IBADA YA MISA
JUMAPILI YA NENO LA MUNGU
1. UTANGULIZI
Baada ya kuanza ibada ya misa kama ilivyo kawaida, Kiongozi wa ibada anawaeleza
waamini maana ya sherehe ya leo kama ifuatavyo:
2. TENDO LA TOBA
Kiongozi wa ibada anaweza kutumia tendo la toba kama ifuatavyo:
K: Bwana wetu Yesu, anayetualika kwenye meza ya Neno lake na Ekaristia anatu-
ita tuongoke, hivyo basi tukiri sisi ni wakosefu na kwa imani tuombe huruma ya
Mungu.
K: Bwana Yesu, wewe ni Neno la Mungu aliyefanyika mwili, Bwana utuhurumie.
W: Bwana Utuhumie.
K: Bwana Yesu, uliwaponya vipofu kwa nguvu ya Neno lako, Kristu utuhurumie.
W: Kristu utuhurumie
K: Bwana Yesu, unatukomboa kutoka dhambini, Bwana utuhurumie.
W: Bwana utuhurumie.
K: Mungu mwenyezi atuhurumie, atusamehe dhambi zetu, atufikishe kwenye uzi-
ma wa milele.
W: Amina.
Wimbo wa utukufu.
3. LITANIA YA NENO LA MUNGU
Baada ya msafara wa Neno la Mungu, Kiongozi wa ibada anawaalika waumini wote ku-
likaribisha Neno la Mungu kati yao kwa kuinama, ishara ya heshima. Bado akiwa anaonye-
sha Biblia kwa waumini; Waumini wanaimba Litania ifuatayo:
Padre:
Ndugu wapendwa nawalikeni nyote mnyoshe mkono wa kulia kuelekea
kwenye Biblia. Hii ni Ishara ya uwajibikaji wetu binafsi kutafuta uzima
katika Neno la Mungu.
Padre: Tuombe:
Tumeyasikia maneno yako, Yesu.
Yanatupa furaha na kuleta mwanga na ukweli katika maisha yetu.
Uwepo wako unaleta amani katika ulimwengu
unaosumbuka na uliogawanyika.
Twaomba Neno lako litie katika mioyo yetu upendo wako mkubwa.
Kaa mioyoni mwetu katika familia zetu, jumuiya na nchi yetu.
Tujalie Roho Mtakatifu atusaidie kuelewa Neno lako.
Tunalikaribisha Neno lako lililo miongoni mwetu.
Lifanye liwe kiini cha maisha yetu.
Twaomba Neno lako liangaze yale yote tunayofikiri,
tunayosema na tunayofanya.
Tunaomba lituunganishe wote na pamoja nawe, leo na milele yote.
Wote: Amina.
4. “Roho wa Bwana yu juu yangu, kuwatangazia vipofu kuona tena.” Tuombe ili
kila mmoja wetu aweze kuufungua moyo wake kwa Mungu, anayetuangaza
na Neno lake, na kutongoza kwenye chemichemi ya uzima. Tunaomba…
W: Amina
8. AHADI YA FAMILIA KWA NENO LA MUNGU
(Baada komunyo Padre anawaalika waumini, kuweka ahadi ya kuheshimu,
kusoma na kutafakari Neno la Mungu. Wote wanarudia baada ya Padre):