Professional Documents
Culture Documents
Magogoni Has Fallen
Magogoni Has Fallen
(Magogoni Imeanguka)
MAGOGONI
HAS
FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
1 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
MAGOGONI
IMEANGUKA
Kimepigwa chapa kwa mara ya kwanza Tanzania, mwaka 2023
copyright© 2023 Aziz Hashim
2 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
MAGOGONI
IMEANGUKA
3 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
sha yake.”
“Siyo hivyo, kingine mwanaume wake naye anaonekana usiku
tu, tena anaingia kwa machale kwelikweli na anatoka alfajiri. Huu
ni mwezi wa pili sasa lakini hata sura zao hakuna anayezijua hapa
mtaani.”
“Bado sioni kama kuna tatizo mpaka halo, hapa ni mjini mke
wangu, kila mtu na maisha yake, mambo ya kufuatiliana hayana
maana kabisa.”
“Kwa hiyo ninachokueleza hakina maana si ndiyo?”
“Siyo hivyo, sijaona kama kuna tatizo katika maelezo uliyonipa,
umefanya jambo zuri kuniambia lakini kama nilivyokueleza, sija-
ona tatizo hapo.”
“Tatizo lipo! Juzi usiku nilipotoka kwenda kukinga maji uani,
nimeona kundi la kama watu nane hivi, wanawake kwa wanaume
wakiingia mle ndani. Nahisi kuna jambo linaloendelea ambalo
tunatakiwa kuwa nalo makini sana, pengine siyo watu wazuri.”
“Hebu ngoja kwanza, ulitoka usiku wa saa ngapi?”
“Kama saa nane hivi, si unajua maji yalikuwa yamekatika wiki
yote hii, sasa usiku nikaanza kuyasikia yakitoka, nikaona bora ni-
kakinge vyombo ili hata yakikatika tena tusihangaike, wewe hush-
indi nyumbani huijui shida tunayoipata maji yanapokatika,” wa-
nandoa wawili vijana, walikuwa wakijadiliana jioni moja wakiwa
chumbani kwao ndani ya nyumba ya vyumba viwili walivyokuwa
wanaishi.
Mwanaume, Denis Mtama alikuwa akifanya kazi ya uandishi wa
habari za uchunguzi huku mkewe, Hope akiwa ni mfanyabiashara
4 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
5 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
6 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
7 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
8 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
9 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
10 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
kwake.
Baada ya kuwasili kazini, kwa kuwa tayari jambo alilokuwa
analifuatilia lilikuwa na ishara ya kutishia usalama wa taifa, ilibidi
atoe taarifa kwa mtu maalum aliyekuwa anawasiliana naye mara
kwa mara kama ‘informer’ na kumjuza kilichokuwa kinaendelea.
***
Mtihani wangu wa kwanza baada ya kuwa nimerejea maso-
moni kutoka nchini Israel, ilikuwa ni wimbi la matukio ya uporaji
magari, uvamizi wa vituo vya polisi na kuporwa silaha lakini yote
tisa, kumi ilikuwa ni mauaji yaliyokuwa yanatingisha katika mae-
neo ya Mkuranga, Kibiti na Rufiji.
Nasema ulikuwa ni mtihani mkubwa kwa sababu ndani ya muda
mfupi niliofanya kazi, nilitokea kuaminiwa na viongozi wangu wa
ngazi za juu kabisa na kila tatizo lililokuwa linatokea, mimi ndiye
niliyekuwa nafikiriwa haraka kwamba naweza kuwa na mbinu za
kujua nini cha kufanya.
Sina haja ya kujitambulisha sana, wengi tayari mnanijua, Kenny
hapa, au Snox lakini kwa kuwa sasa hivi nilikuwa nimepanda
ngazi, wengi walikuwa wanapenda kuniita Chief na taratibu jina
hilo lilianza kuwa maarufu kuliko hata lile la Snox.
Hatua ya kwanza ilikuwa ni kujaribu kuyatazama matatizo yote
matatu na kujua ni kwa namna gani yalikuwa na uhusiano, na-
maanisha ujambazi wa kupora magari, matukio ya kuvamia vituo
vya polisi na mauaji ya watu yaliyojawa na utata mkubwa yali-
yokuwa yakiendelea Kibiti, Mkuranga na Rufiji.
Waliokuwa wananiamini hawakuwa wanakosea, mafunzo nili-
11 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
12 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
13 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
kulieleza.
Sasa hili kundi la pili, lenyewe lilikuwa na namna ya tofauti
kabisa ya kufanya uhalifu wao. Kwanza, matukio ya uporaji
wao wa magari, yalikuwa yakihusisha mauaji. Yaani wao wa-
likuwa wakilitaka gari, basi hakuna mjadala, ni aidha uwape
wakuache au uuawe kisha walichukue.
Mbinu hii ilikua ngeni kabisa na ile iliyokuwa inatumiwa
na wezi wa kawaida wa magari ambao wala hawakuwa na
shida ya kuondoa uhai wa mtu wala kujeruhi, hawa wenyewe
walikuwa wakiwafunga kamba madereva na kwenda kuwa-
telekeza mafichoni bila kuwadhuru hata kidogo.
Lakini pia kulikuwa na tofauti nyingine kubwa ambayo
ilizidi kunipa wasiwasi ambayo ni aina ya magari yaliyokuwa
yanaibwa. Inafahamika kwamba wezi wa kawaida wa magari,
huwa wanayalenga magari ya kifahari hasa matoleo mapya
yanayopendwa zaidi.
Lakini kundi hili la pili, lenyewe lilikuwa likiyalenga
magari yenye uwezo mkuba wa kupita hata katika maeneo
ambayo hakuna barabara nzuri, yaani wao walikuwa wanazi-
lenga zaidi gari za kazi. Kwa wale wenye uelewa wa magari
watakuwa wanaelewa ninaposema magari ya kazi namaanisha
ya aina gani.
Kwa kifupi ni yale matoleo ya magari kama Toyota Land-
cruiser, Nissan Patrol, Land Rover na ya aina hiyo. Ilikuwa ni
dhahiri kwamba magari hayo hayaendi kuuzwa kwa sababu
14 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
15 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
16 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
tunaweza kuchelewa.”
“Ni sahihi kabisa, hata mjumbe wa serikali ya mtaa ninaoishi
alikuwa na haraka ya kutaka kuwasiliana kwanza na polisi lakini
nikamzuia kwa sababu kuna jambo kubwa ambalo nimelihisi,”
alisema, nikashusha pumzi ndefu na kuanza kumhoji kwa undani.
Maelezo yake yote yalikuwa yakinaswa moja kwa moja na vifaa
maalum na vya kisasa vya mawasiliano nilivyokuwa nimevivaa
mwilini ambavyo isingekuwa rahisi kwa mtu yeyote kuviona au
hata kuvihisi.
Maelezo aliyonipa yalinifanya nipate shauku kubwa ya kwanza
kufika kwenye nyumba aliyokuwa ananielezea lakini pia kuweka
vijana wa ‘rada’ ambao wangenisaidia kulitazama suala hilo kwa
karibu zaidi.
Baada ya maelezo na mtoa taarifa wangu, tulitoka pamoja na
kwenda mpaka kwenye gari langu, tukaondoka pamoja kuele-
kea ‘field’ nikiwa na maana ya eneo la tukio. Kwa kuwa sikuwa
naifahamu vizuri mitaa ya Kijitonyama, ilibidi yeye ndiyo anion-
goze, nikawa nafuata maelekezo yake na hatimaye tukafika eneo
husika.
Mwonekano wa mazingira ya nje ya nyumba hiyo, ilionesha
dhahiri kwamba kuna jambo lisilo la kawaida lililokuwa linaende-
lea ndani ya nyumba hiyo, tukapita taratibu huku nikiwa makini
kutazama kila kitu.
“Mimi naishi hapo gengeni, nashukuru kwa kunifikisha nyum-
bani!”
“Hapana, hutakiwi kushuka ili usije ukajihatarisha, hatakiwi
17 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
18 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
wanaweza kutusaidia?”
“Umejuaje kama mimi ni mwandishi wa habari?”
“Aaah! Dennis, hivi ukisikia neno serikali huwa unalichuku-
liaje?”
“Lakini hata jina langu pia sijakwambia mahali popote katika
mazungumzo yetu! Umelijuaje?”
“Najua kila kitu kukuhusu wewe kwa sababu hii ni kazi yangu,”
nilisema huku nikijaribu kutabasamu kwa sababu ilionesha mtoa
taarifa wangu bado alikuwa mgeni kwenye kazi yake na pengine
hata hakuwa ananijua vizuri kama alivyojinasibu mwenyewe
mwanzo.
Basi nilirudi naye mpaka Mlimani City, nikamuacha palepale
nilipomkuta na kuchomoa noti kadhaa na kumkabidhi. Haukuwa
utaratibu wetu kupeana fedha kienyeji namna hiyo lakini nililaz-
imika kufanya hivyo kama njia ya kutafuta ukaribu zaidi na mtoa
taarifa wangu.
“Muda wowote ukihisi upo kwenye hatari yoyote nipigie simu,”
nilimwambia, akashusha pumzi ndefu na kunishukuru.
Niliondoka na moja kwa moja nilirudi ofisini ambapo kitu cha
kwanza ilikuwa ni kuwaita vijana wangu wawili ambao nilikuwa
nawaamini sana kwenye kazi. Niliwapa maelekezo yote na ku-
waeleza nini kinachotakiwa kufanyika haraka iwezekanavyo.
Kilichofuatia baada ya hapo ilikuwa ni utekelezaji wa haraka,
taarifa za akina nani waliokuwa wanaishi ndani ya nyumba ile
na kwa nini walikuwa wakijifichaficha muda wote. Maelekezo
yangu ilikuwa ni kuhakikisha taarifa zote muhimu zinapatikana
19 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
20 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
umemuona?”
“Mh! Hebu nionyeshe vizuri ni yupi?” Dennis alimwambia
mkewe huku wote wakisogea dirishani, wakawa wanachungulia
kule gengeni ambapo mkewe alimuonesha mhusika mwenyewe
aliyekuwa akimzungumzia.
Alikuwa ni msichana ambaye kiumri hakuwa na zaidi ya miaka
26 na mwonekano wake haukuwa ukifanana na kazi aliyokuwa
akiifanya. Japokuwa alijitahidi kuvaa nguo zilizochokachoka
lakini rangi ya ngozi yake ilionesha kabisa siyo mtu anayefanya
kazi za kutembea juani au siyo mtu ambaye alikuwa na maisha
magumu kama mwenyewe alivyokuwa akitaka kuwaaminisha
watu.
“Mkubalie!”
“Nimkubalie kivipi sasa? Yaani mtu anakuja tu huko simjui
halafu nimkubalie, au mnajuana?”
“Hapana sijuani naye kwa chochote!”
“Sasa kwa nini unasema nimkubalie? Au ndiyo mke mwenzan-
gu nini?” alisema mke wa Dennis na kuanza kuchachamaa aki-
taka aeleweshwe.
“Sasa mimi nikueleweshe nini wakati mimi ndiyo kwanza
namuona? Mimi nimekushauri umkubalie kwa sababu sisi bin-
adamu tumeagizwa upendo, kama mtu amekuja kukulilia shida,
na biashara yake haiingiliani na yako kwa nini umzuie? Kwani
wewe huwa unauza matunda?”
“Hapana lakini sijui kwa nini moyo wangu una wasiwasi naye.
Ananihojihoji maswali ambayo siyaelewei.”
21 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
22 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
“Unamaanisha nini?”
“Namaanisha kwamba pengine kile tunachokihofia tayari seri-
kali imeshakiona na sasa inakifanyia kazi kwa karibu.”
“Kwani ulienda kutoa taarifa polisi?”
“Hapana, kwani umeona polisi wamekuja hapa?”
“Sasa ni nini hiki? Najua unajua lakini hutaki kuniambia!”
23 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
24 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
2
K
WA kutumia vijana maalum, niliendelea kufua-
tilia kwa karibu taarifa tulizopewa na mtoa taarifa
wetu asubuhi ya siku hiyo na kitu ambacho niliona
kinaweza kufaa zaidi, ilikuwa ni kuweka watu wa
kufuatilia nyendo za watu waliokuwa wanaishi
kwenye nyumba ile kama walikuwepo, kwa muda wa saa ishirini
na nne.
Hiyo ilikuwa mbinu ya kwanza lakini mbinu nyingine ambayo
hii ilikuwa ya kitaalamu zaidi, ilikuwa ni kufuatilia mawasiliano
yote yaliyokuwa yanatoka au kuingia katika eneo la Mtaa wa Ki-
jitonyama Kisiwani.
Nasema hii ni mbinu ya kitaalamu zaidi kwa sababu hata watu
waliosomea teknolojia ya mawasiliano, hawawezi kuwa na ujuzi
wa kuelewa namna unavyoweza kuchuja mawasiliano ya maelfu
ya watu mpaka kumpata yule uliyekuwa unamtaka kisha ukaanza
25 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
26 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
27 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
28 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
29 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
Kazi zote mbili ziliendelea kufanyika kwa pamoja, ile timu ili-
yokuwa ikifuatilia kila kitu eneo la tukio kwa usiri wa hali ya juu,
iliendelea kusonga mbele kuelekea kwenye hatua ya kukamilisha
kazi lakini pia upande wa pili mimi na vijana wangu pia tulikuwa
tunaendelea na kazi ya kuhakikisha tunaweza kuzi-track simu zote
tatu zilizokuwa zinatumika kufanyia mawasiliano.
Kitu ambacho watu wengi hawakijui, kuna tofauti kubwa kati
ya matukio ya ujambazi na matukio ya ugaidi na hata namna ya
akuyashughulikia kuna tofauti kubwa pia.
Naweza kusema kwamba kwetu sisi tuna bahati kubwa sana
kwamba matukio ya kigaidi ambayo yameshatokea ni machache
na hata madhara yake siyo makubwa sana ukilinganisha na nchi
kama Kenya, Somalia, Sudan, Libya na nchi nyingine kwa bara la
Afrika.
Hata hivyo, bahati hiyo inakwenda sambamba na ukweli
mwingine mchungu kwamba kwa sababu matukio kama hayo ni
nadra sana kutokea, hata utayari wa vyombo vya ulinzi na usala-
ma kuyashughulikia huwa ni wa kiwango cha chini mno.
Utayari uliopo mara nyingi huwa ni ule wa kupambana na ma-
tukio ya ujambazi au uvamizi wa mipaka ya nchi na hili ni tatizo
kubwa sana ambalo watu waliopata nafasi ya kwenda kusoma na
kupata mafunzo nje, huwa wanakumbana nalo wawapo mafun-
zoni kwa sababu wanakuwa hawaelewi chochote!
Hicho ndicho kilichonikuta hata mimi nilipokuwa masomoni
nchini Israel lakini namshukuru Mungu kwamba niliweza ku-
pata mafunzo ya vitendo kutoka kwa wataalam wa masuala ya
30 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
31 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
32 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
33 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
“Vipi tena?”
“Umechelewa kidogo kuna mafundi wa Dawasco walikuja hapa
mtaani eti wanakagua watu wanaojiunganishia maji kinyemela.”
“Kwani mpaka leo kuna watu wanajiunganishia maji?”
“Mh! Sidhani kwa sbabu sijawahi kusikia, kila mtu mwenye
bomba analipa bili, sasa unaweza kujiunganishia maji halafu
ukawa unalipa bili?”
“Enhee, kwa hiyo hapo sasa stori ni nini?”
“Ujue hayo maswali yako ya kuwa unanihoji kama upo kutafuta
habari huwa siyapendi,” alisema mke wa Dennis na kusababisha
wote wacheke. Kazi yake ya uandishi wa habari za uchunguzi
ilikuwa imemuathiri kisawasawa.
“Sasa si wakawa wameenda hapo nyuma kwa mzee Msomali,
wakawa wanataka kwenda kukagua mita, mzee akawa mkali
kama pilipili, kukatokea bonge la ugomvi watu wakajaa!”
“Khaa! Yaani sijaelewa! Mafundi wa Dawasco wamekuja ku-
kagua mita, halafu mzee Msomali akawa hataki!”
“Wewe naye, mi ninapokusimulia akili zako huwa unaziweka
wapi? Ndiyo! Wamekuja kukagua mita, wameanzia nyumba
nyingine ambapo walikuwa wanakagua vizuri tu, walipofika kwa
Msomali kabla hawajahamia huu upande wetu huku ndiyo timb-
wili likatokea.”
“Sasa kwa nini huyo mzee alikuwa hataki waingie?”
“Kila mtu amebaki na mshangao maana amechachamaa vibaya
mno, eti anasema hapo nyumbani kwake wezi wamekuwa waki-
ingia na kumuibia spea za magari yake uani ndiyo maana hamua-
34 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
35 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
36 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
37 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
38 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
39 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
40 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
41 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
42 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
market).
Picha ambayo niliipata kwa haraka ni kwamba watu waliokuwa
wakiishi mle ndani, japokuwa walikuwa wakiishi maisha ya
ukimya na kujifichaficha, lakini walikuwa na uwezo mkubwa wa
kifedha kutokana na mazingira ya mle ndani.
Kulikuwa na choo na bafu ambavyo vilijitenga lakini vyote vi-
kiwa ni vya ndani kwa ndani, nikahakikisha kote kwamba hakuna
mtu kisha nikarudi na kuanza kuchunguza vizuri dari kuanzia
kule tulikoingia, kwenye vile vyumba tulivyokagua, sebuleni
mpaka chooni.
Ilikuwa ni muhimu kwanza kuchunguza kila kitu kwa ukaribu
kabla ya kwenda kumalizia katika vile vyumba viwili vilivyoku-
wa vimefungwa. Baada ya kujiridhisha, sasa tulirudi kwenye vile
vyumba viwili na niliona ni vyema kuanza na kile chumba amba-
cho kilikuwa kimefungwa mlango kwa ndani.
Kabla ya kutumia nguvu, nilijaribu kwanza kutumia diplomasia
kwa kugonga taratibu na kuwataka waliokuwa ndani wafungue
na kujisalimisha wenyewe. Nilizungumza kwa mara ya kwanza
kwa sauti ambayo nilikuwa na uhakika kwamba inasikika vizuri
kabisa hata kwa mtu aliyepo ndani lakini hakukuwa na majibu
yoyote.
Niligonga kwa mara ya pili lakini bado hakukuwa na majibu,
nikagonga mara ya tatu na ya mwisho huku nikiwaandaa vijana
wangu kwa ajili ya kuvunja mlango. Ajabu ni kwamba tulisikia
mlango ukifunguliwa kutoka ndani, wote tukarudi nyuma na
kukaa ‘standby’.
43 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
44 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
3
K
WA umakini wa hali ya juu, niliingia ndani ya
chumba hicho bastola ikiwa mkononi, nikawa
naangaza kitu kimoja baada ya kingine kwa
umakini mkubwa, hakukuwa na kitu chochote cha
kutia mashaka zaidi ya kitanda, kabati la nguo na
meza ndogo ya kujipambia lakini pia kama ilivyokuwa sebuleni,
chumba chote kilikuwa kimetandikwa mazulia.
Nilihakikisha pia kama uvunguni mwa kitanda hakukuwana
mtu, nikakagua pia kwenye dari ili kuwa na uhakika kama haku-
namtu aliyepanda na kujificha lakini hakukuwa na dalili zozote.
Nilitoka na kutoa ishara kwamba chumba hicho nacho kifun-
45 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
46 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
47 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
48 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
49 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
50 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
vipi kwenye chumba kama kile na kwa nini muda wote milango
ilikuwa imefungwa. Ambacho hakuna kati yetu ambaye alikuwa
amekigundua ni kwamba kumbe hawakuwa wasichana wadogo
kama ambavyo ungeweza kuwaona kwa harakaharaka.
Nitaeleza vizuri zaidi kwa nini nasema hivyo lakini kilicho-
fanyika pale, ilikuwa ni kwa yule mwanamke kuzungumza nao
kwa lugha waliyokuwa wanaelewana, kisha akageuka na kunio-
neshea ishara mimi, nadhani alikuwa anawatambulisha kwangu,
nikatingisha kichwa kama ishara ya kukubali utambulisho huo.
Yule mwanamke akanisogelea na kunisemesha kwa sauti ya
chini:
“Hawa ni mabinti zangu, hawana baya lolote, wanatumika bila
ridhaa zao, nakuomba sana kama ambavyo umesema utanilinda
mimi, uwalinde na wao! Walikuwa na silaha tayari kupambana
lakini nimewaomba wazishushe chini, naomba wakukabidhi kama
ishara ya uaminifu kati yetu,” alisema yule mwanamke kwa sauti
ya chini akiwa amenisogelea.
Nilishtuka mno aliponiambia kwamba kumbe walikuwa na si-
laha na walishakuwa tayari kwa chochote ili kujilinda, akawageu-
kia kisha akawapa ishara wainuke na kuweka chini silaha zao.
Kila mmoja alikuwa na bunduki ya AK47 iliyokatwa kitako na
kuifanya ibebeke kirahisi na kwa jinsi walivyokuwa wamevaa,
isingekuwa rahisi kwa mtu yeyote kugundua kwamba walikuwa
na silaha.
Japokuwa nilikuwa na ujasiri wa hali ya juu, nilijikuta mapigo
ya moyo wangu yakinienda mbio kuliko kawaida kwa sababu
51 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
52 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
53 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
54 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
55 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
56 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
57 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
58 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
59 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
60 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
yao, akili yangu ilitua kwenye picha iliyokuw aimetundikwa uku-
tani ndani ya kile chumba walichokuwemo wale wasichana.
Sijui ni machale au ndiyo kuiva kwenye medani kwa sababu
nilipoitazama tu ile picha, kuna kitu kiliniambia akilini mwangu
kwamba niishushe pale ilipokuwa imetundikwa na kuichunguza
zaidi.
Ilikuwa ni picha iliyochorwa kwa mkono ikionesha mandhari ya
kama jangwa hivi pamoja na ngamia kadhaa, picha ambazo watu
wengi hupenda kuzibandika ukutani kwa jinsi zinavyovutia.
Nilipoishusha pale ukutani, akili ya haraka ilinituma niigeuze
upande wa nyuma, nikakutana na kitu ambacho sikuwa nime-
kitegemea kabisa.
Kulikuwa na karatasi nyingine kadhaa zote zikiwa na ukubwa
kama ile picha lakini zikiwa zimewekwa kwa mfumo maalum un-
aowezesha kufunua ukurasa mmoja baada ya mwingine.
Ile iliyokuwa juu kabisa, ilikuwa na mchoro kama wa ramani
ya jengo fulani kubwa, ukiwa na maelezo yote muhimu kama
ambavyo ramani za majengo makubwa zinavyokuwa, ikionesha
milango ya kuingilia na kutokea, madirisha, mifumo ya mabomba
ya maji safi pamoja na maji taka na taarifa nyingine muhimu.
Niliitazama kwa makini, akili yangu ikanituma kwamba haukuwa
mchoro mgeni kwenye macho yangu ingawa kwa harakaharaka
sikuweza kukumbuka ni mchoro wa nini. Nikafungua ukurasa wa
pili! Lahaula, nilikutana na picha iliyochorwa kwa mkono ya jengo
la Ikulu ya Magogoni ya jijini Dar es Salaam.
Ninaposema Ikulu ya Magogoni namaanisha ikulu hiihii ambayo
ndipo anapoishi mheshimiwa rais! Inaitwa Ikulu ya Magogoni kwa
61 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
sababu ule mtaa ilipo, unaitwa kwa jina hilohilo na wengi wa-
napoitaja Magogoni, huwa wanamaanisha ikulu.
Nilishindwa kuelewa picha ya ikulu, tena ikiwa imechorwa kwa
mkono na kwa ustadi wa hali ya juu, ilikuwa inafanya nini ndani
ya nyumba hiyo waliyojaa watu hatari? Kabla sijafunua ukurasa
uliokuwa unafuatia, ilibidi nirudie kwanza kutazama ule mchoro
kwenye ukurasa wa kwanza!
Kile nilichokuwa nimekihisi mwanzo ndicho kilichokuwa kime-
tokea, ulikuwa ni mchoro wa ramani ya ikulu, ukiwa na taarifa zote
muhimu kuhusu sehemu hiyo nyeti na inayolindwa zaidi ukiachana
na benki kuu!
Kwa kawaida, picha na michoro yoyote ya ikulu huwa ni mion-
goni mwa vitu ambavyo kwa kitaalamu huitwa ‘classified docu-
ments’ ikiwa na maana ya nyaraka za siri ambazo ni kundi fulani
dogo la watu wachache ndilo pekee linaloruhusiwa kuziona!
Sasa kama ni hivyo, watu hawa waliweza kupata nyaraka nyeti
na muhimu kiasi hicho? Tena ikiwa na maelezo ambayo mengine
hata mimi mwenyewe sikuwa nayajua? Na kwa nini walikuwa na
michoro hii? Walikuwa wanapanga kufanya nini? Sikupata majibu,
ikabidi niendelee kuzipekua zile karatasi.
Kulikuwa na mchoro mwingine wa kutokea juu ambao nao uli-
kuwa unaonesha eneo lote la ikulu na maeneo ya jirani, ukiwa na
majina ya mitaa na barabara zote kuizunguka ikulu.
Kama hiyo haitoshi, kulikuwa pia na picha zilizokuwa zinaone-
sha mandhari ya ndani ya ikulu na zilikuwa takribani nane, zikiwa
zimekuwa ‘scanned’ na kuunganishwa kwenye karatasi moja.
62 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
63 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
64 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
65 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
66 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
67 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
68 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
4
W
AKATI nikisimamia hilo, nilipokea simu
kutoka kwa kiongozi wa Kikosi cha Kudhibiti
na Kupambana na Ugaidi (Anti Terror Squad-
ron- ATS) akinitaarifu kwamba nimechaguliwa
kuwa ‘field commander’ wa kikosi hicho, ikiwa
na maana sawa na kile alichoniambia mkurugenzi, kwamba mimi
ndiye nitakayekuwa kiongozi wa oparesheni hiyo kwa jumla.
Nilishusha pumzi ndefu kwa sababu mambo yalikuwa yakienda
na kubadilika kwa kasi kubwa mno kiasi kwamba ungeweza
kudhani upo kwenye ndoto ya kutisha! Sikuyaogopa majukumu
makubwa niliyokuwa nimepewa, akili zangu zilikuwa ni kwa
namna gani nitaweza kukimbizana na kasi ya mambo.
Kama nilivyokuwa nimepanga, jambo la msingi kabisakwa
69 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
70 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
ukuta mrefu.
Ukuta huo ulikuwa umezibwa kwa miti mingi iliyopandwa nje na
ndani ya ukuta na kitu pekee ambacho kilikuwa kikionekana kwa
urahisi, lilikuwa ni geti kubwa jeusi kwenye lango kuu la kuingilia
na ndiyo maana wengi tulipenda kupaita getini.
Kumbe tayari taarifa juu ya tulichokibaini zilikuwa zimeshaenea
kila sehemu na vikosi vyote vilikuwa vimewekwa kwenye hali ya
utayari, wenyewe huwa tunaita ‘Alert’.
Hakukuwa na muda wa kupoteza, lile gari lililokuwa na silaha
kwa maana ya bunduki, lenyewe ndilo lilikuwa la kwanza kuwasili,
likafuatia lile lililokuwa na malighafi za kutengeneza mabomu na
la mwisho ndiyo lile nililokuwa naliendesha mimi ambalo nilikuwa
nimepanda na vijana wangu na breki ya kwanza ikawa ni nje ya
ofisi za kitengo cha Kikosi cha Kudhibiti na Kupambana na Ugaidi
(Anti Terror Squadron- ATS).
Kitengo hiki ndicho kilichokuwa kinahusika na masuala yote
yanayohusiana na masuala ya ugaidi na kiliundwa rasmi baada ya
tukio la shambulio la ugaidi lililotokea Ubalozi wa Marekani jijini
Dar es Salaam na Nairobi.
Kwa wanaokumbuka vizuri matukio hayo ya mashambulizi ya
kigaidi ubalozini yalitokea Agosti 7, 1998 na kusababisha Afrika
Mashariki na dunia nzima kuzizima, wahusika wakuu wakiwa ni
kundi la kigaidi la Al Qaeda.
Watu 213 walifariki na wengine 4,500 kujeruhiwa jijini Nairobi,
Kenya wakati kwa Tanzania watu 11 waliaga dunia na wengine 85
walijeruhiwa vibaya na huo ndiyo ukawa mwanzo wa marekebi-
71 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
72 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
73 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
74 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
75 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
76 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
77 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
78 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
79 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
80 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
81 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
82 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
83 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
84 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
85 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
86 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
87 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
88 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
89 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
90 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
91 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
92 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
Nilichokigundua harakaharaka, ni kwamba mzee huyu wa Ki-
somali naye alikuwa na mafunzo na alikuwa akishirikiana kwa
karibu na watu waliokuwa nyuma ya pazia kwa sababu hata namna
alivyokuwa akijikoholesha pale, ni kwamba kuna ujumbe alikuwa
akiufikisha kwa njia ya kikohozi kumpa taarifa yule aliyekuwa ana-
zungumza naye.
“Sasa kwa kuwa umekataa kutoa ushirikiano kwa hiyari yako,
tutakulazimisha utoe ushirikiano kwa shuruti na na kuhakikishia
utafurahi na nafsi yako,” nilisema huku nikisimama kwa jazba.
Sikutegemea kama anaweza kuleta masihara kiasi hicho katika
suala nyeti kama lile na moyoni nikajiapiza kwamba nitamfunza
adabu, tena kwa mikono yangu mwenyewe kwa sababu ilishaone-
sha wazi kwamba hakuwa tu akishirikiana na magaidi, bali yeye
mwenyewe alikuwa gaidi na ndiyo maana hata alikuwa amepan-
dikizwa ‘chip’ ya mawasiliano kwenye mkono wake.
Niliposimama tu, vijana wangu wawili waliingia na nikawapa
maelekezo kwamba kitu cha kwanza inatakiwa ‘chip’ yake ya mko-
noni ikatolewe na kuhifadhiwa kisha apelekwe kwenye mahabusu
ya chini ya ardhi mpaka nitakaporejea.
Nilitoka kwenye kile chumba na kuwaacha vijana wangu waki-
tekeleza kile nilichowaambia na moja kwa moja nikaingia kwenye
kile chumba cha pili walichokuwa wamekaa viongozi wa idara
mbalimbali wakisikiliza kila kilichokuwa kinaendelea.
“Tunafanyeje!”
“Tumehafanikiwa kunasa location ya mahali alipo huyo ali-
yekuwa anazungumza naye, anatakiwa kwenda kukamatwa haraka
93 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
iwezekanavyo,” nilisema huku nikikiweka vizuri kifaa changu cha
mawasiliano sikioni ili kuzungumza na vijana wa Cyber ambao
ndiyo waliokuwa wakifanya kazi ile.
“Weka location kwenye ‘screen 2’,´nilisema wakati nikiungumza
nao, nadhani wote mle ndani hawakuwa wamenielewa harakaharaka
nilimaanisha nini na muda mfupi baadaye, ‘screen’ kubwa iliyokuwa
upande wa juu kabisa wa kile chumba, iliwaka, nikawataka watu
wote waitazame kwa makini.
Ilifungua ramani, zile zinazotumika na ‘satelite’, watu wote
wakatulia wakiitazama, mimi pia nikatulia kwa sababu bado sikuwa
nimeelewa yuko wapi. Ramani iliendelea kujifungau huku wote
tukitupia macho na mwisho ikatulia. Mawasiliano yalionesha kwam-
ba simu ile ilikuwa katika eneo la Kibiti mkoani Pwani.
“Ngoja kwanza kuna kitu sijakielewa hapa,” alisema mkurugenzi
huku akisimama, akionesha kushangazwa na kile kilichokuwa kina-
onekana pale kwenye ramani.
“Eneo lote la Mkiru kuna mauaji yasiyoeleweka yanayoendelea
kwa kasi,” alisema, akiwa na maana kwamba Mkiru ni kifupisho
cha Mkuranga, Kibiti na Rufiji, hivyo ndivyo eneo hilo tulivyokuwa
tunaliita kwa lugha za kioparesheni.
Akaendelea: “Halafu hapa tunaoneshwa mtuhumiwa tunayemsaka
yupo Kibiti muda huu! Kwa hiyo inamaanisha wale wanaofanya
matukio ya kihalifu kule ikiwa ni pamoja na kuwaua viongozi wa
serikali wa vijiji na mitaa na kuvamia vituo vya polisi wapo kwenye
‘misheni’ moja na hawa wanaotaka kuvamia ikulu?”
“Siyo kwamba wapo pamoja, bali ni kwamba ni watu haohao, ni
94 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
95 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
96 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
97 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
98 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
99 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
5
K
ILA kitu kilifanyika kwa kasi kubwa na umakini
wa hali ya juu, vijana wangu wote wakawa wame-
shatoa ‘mabomba’ kuelekeza kwenye lile gari. Kwa
umakini mkubwa nikasogea mpaka upande wa
dereva, nikamuona akiwa amenyanyua mikono juu
huku akionesha kuwa na wasiwasi usioelezeka.
“Teremka!” nilitoa amri, kweli akatii na kuteremka huku mikono
yake ikiwa juu, nikampokea juujuu na kumlaza kwenye lami huku
nikimuwekea goti mgongoni, nikafanikiwa kumdhibiti na kum-
funga pingu kwa nyuma.
Vijana wangu nao walikuwa ‘sharp’ kwelikweli, wakawaterem-
sha watu wengine wawili waliokuwa upande wa pili wa dereva
mwendo.
Kile nilichokuwa nakihisi kuanzia mwanzo sasa kilikuwa kinaan-
za kujidhihirisha! Mpaka hapo nilishakuwa na uhakika kwamba
yale matukio ya mauaji na uporaji wa silaha kwenye vituo vya
polisi yalikuwa na uhusiano na ule mpango wa kuivamia ikulu na
mpaka hapo ilionesha kwamba waliokuwa wanafanya matukio
hayo, ndiyo haohao waliokuwa wanapanga kuvamia ikulu.
Nilihisi kichwa kikiwa kinapata moto, nikamuelekeza kutuma
taarifa hizo makao makuu na muda huohuo na mimi nikawa na-
wasiliana na viongozi wangu na kuwaeleza mambo tuliyokuwa
tunaendelea kuyabaini ili kuweka rekodi sawa.
Haukupita muda mrefu tukawa tayari tumeshaingia Jaribu Mpak-
ani, nikaanza kupunguza mwendo wakati tukianza kuingia kwenye
mji huo mdogo uliochangamka kiasi.
Kilichonipa matumaini makubwa, ni kwamba wakati tukiingia
kwenye mji huo, tulikuta kuna kizuizi cha askari wenye silaha
wakiwa wamezuia magari yote yaliyokuwa yanatokea upande wa
kusini, wakifanya ukaguzi gari moja baada ya jingine.
Tulipokaribia kile kizuizi, nilitoa ishara kwa kutumia taa, askari
wenye silaha waliokuwa wametanda barabarani wakiendelea na
ukaguzi wakafungua upande mmoja wa kizuizi ili tupite, vijana
wangu waliokuwa nyuma nao wakapunguza mwendo na badala ya
kupita, niliwasha taa nyingine kuonesha kwamba tunasimama.
Muda mfupi baadaye msafara wetu ukawa umesimama kando ya
barabara, nikateremka na kutembea kikakamavu kuwaelekea wale
askari.
nilivyoagiza.
“Haya tupe chetu tugawane!”
“Ngojeni kwanza tujiridhishe kama ndiyo yeye!” nilisema huku
nikimuinamia yule mwanaume aliyekuwa amekalishwa chini, akio-
nesha kuwa na hofu kubwa isiyo na kifani.
Kwa kuwa binafsi sikuwa namjua mtuhumiwa anafananaje,
ilibidi nimnyanyue pale chini, nikamfunga pingu kisha nikaanza
kumkokota kuelekea kule tulikokuwa tumepaki magari yetu. Lengo
lilikuwa ni kutaka yule dereva athibitishe kama ndiye yule tuli-
yekuwa tunamtafuta.
“Siyo mwenyewe!” alisema yule dereva wa gari la mihogo, wale
vijana wakawa ni kama hawaamini, wakarudia kumtazama vizuri.
Ni kweli naye alikuwa na asili ya Kisomali lakini yeye hakuwa
mrefu kama maelezo ya awali yaliyotolewa na hata kiumri huyu
alionesha kuwa bado kijana mdogo.
“Kweli jamani, niliwaambia lakini!” alisema mmoja kati yao, ha-
rakaharaka wakatawanyika na kuingia tena mitaani, wakamuacha
yule mtuhumiwa pale kwenye mikono yangu, nikaanza kumchun-
guza kwa umakini bila kumsemesha chochote.
Sijui kwa nini akili yangu ilinituma kwamba hata kama yule de-
reva amesema siyo yule mtuhumiwa ambaye tulikuwa tunamsaka
kwa udi na uvumba, bado huyu naye anaweza kuwa ni walewale.
“Unaitwa nani!”
“Naitwa Ishmael afande!”
“Unaishi wapi?”
“Naishi Temeke!”
wa.
Lakini ghafla, yule kijana alishtuka akiwa ni kama haamini
alichokuwa anakiona mbele yake. Kilichomshtua ilikuwa ni baada
ya kumuona yule kijana mwingine wa Kisomali ambaye tulikuwa
tumesaidiwa kumpata na wale vijana wa pale.
“Vipi, mbona umeshtuka?”
“Huyu hapa ni ndugu yake, yeye anakujua vizuri zaidi kule ku-
liko hata mimi,” alisema kwa msisitizo akimnyooshea kidole yule
kijana ambaye alikuwa amedhibitiwa vizuri na vijana wangu.
“Una uhakika?”
“Nina uhakika afande, muulize mwenyewe kama nadanganya!”
alisema, nikashusha pumzi ndefu, nikaikamata vizuri bastola am-
bayo kwa muda wote huo ilikuwa mkononi.
“Kwa hiyo kumbe muda wote unaniektia hapa si ndiyo?” nilise-
ma huku nikimkamata yule kijana kwa nguvu na kumsukuma
mpaka kwenye ‘bodi’ la gari, nikamkaba kwa nguvu huku mkono
mmoja nikimgusisha bastola.
“Utasema ukweli, iwe ni kwa hiyari yako au kwa lazima, hau-
wezi kutupotezea muda hapa,” nilisema kwa jazba huku nikizidi
kumkandamiza kwa nguvu nikiwa nimemkaba.
6
“
KWENYE flash kuna nini?” nilisema huku nikiwa bado
nimemkaba kwa nguvu, akaonesha ishara kwamba
nimuachie atasema mwenyewe.
“Kuna kazi nilitumwa kuja kuprint.”
“Kazi gani?”
“Sijui ni kazi gani, mimi nimetumwa tu na nimeambiwa hatakiwi
mtu yeyote kujua zaidi ya mtu wa steshenari tu.”
“Umetumwa na nani?”
“Kiongozi wetu!”
“Kiongozi wenu? Kiongozi wenu wewe na nani?” nilizidi kum-
bana lakini alionesha kutokuwa na majibu, nikaona tusizidi kupo-
teza muda, ilitakiwa tuondoke haraka kuelekea huko wanakosema
“Ndiyo!”
“Silaha mnapata wapi?”
“Sijui lakini huwa zinaletwa!”
“Kuna njia nyingine ya kuingia au kutoka zaidi ya hii?”
“Ndiyo, kuna njia ya upande wa pili, hiyo ndiyo hutumika sana
nyakati za mchana, hii hutumika nyakati za usiku!”
“Sasa nataka uniongoze twende mpaka huo upande wa pili!”
“Wataniua! Wakishajua nipo na nyinyi wataniua!”
“Tutakulinda!”
“Hamna uwezo wa kunilinda, wakiamua jambo lao hakuna
anayeweza kuwazuia!”
“Ilikuwaje ukafika huku na kujiunga nao?”
“Ni habari ndefu ambayo siwezi kuielezea hapa, walikuja kutu-
chukua Mombasa mimi na wenzangu.”
“Wenzako akina nani?”
“Vijana wenzangu, tuliletwa kama kumi!”
“Jumla kuna watu wangapi?”
“Ni wengi, wanafika arobaini!”
“Kiongozi wenu ni nani?”
“Kwa hapa ni Abdulwaheed lakini kuna viongozi wengine wa juu
ambao huwa wanakuja na kuondoka!”
“Si ulisema humfahamu wewe?”
“Nisamehe! Niliogopa kueleza ukweli.”
“Kwa hiyo mwanzo uliogopa kusema ukweli lakini sasa hivi
huogopi tena si ndiyo?”
“Siyo hivyo! Sasa hivi najua kama nisipowaeleza ukweli sote
saidia hasa baada ya kuona amekaa eneo lile kwa muda mrefu.
Ndiyo maana baada tu ya kugundua kwamba alikuwa na kifaa
hicho, hatua ya kwanza ilikuwa ni kukichomoa na kukitupa lakini
kwa kuwa tayari tulishapoteza muda eneo lile, nilikuwa na uhakika
kwamba lazima wenzake watakuwa wameshatukaribia.
Hicho ndicho kilichotokea kwa sababu milio ya pikipiki iliposiki-
ka tu, wale wenzake ambao ilionesha walikuwa wanatulia ‘timing’
ya kutuzunguka, walichomoka kutoka mafichoni na kuanza kufyat-
ua risasi lakini walikuwa tayari wamechelewa.
Kingine kilichofanya nizuie vijana wangu wasijibu mapigo ni
milio ya silaha zilizokuwa zinatumika. Kwa uzoefu niliokuwa nao,
kabla sijaenda masomoni na baada ya kurudi, nilikuwa na uwezo
wa kutambua aina ya silaha kwa kusikia mlio wake tu hata kama ni
kwa mbali.
Ilionesha wazi kabisa wale wenzake walikuwa wamejihami
kwa bunduki za kivita na kanuni ni kwamba unapopambana na
mtu anayetumia silaha ya kivita, tena kwa kukushtukiza, hutakiwi
kuzubaa eneo hilo kwani sekunde moja tu inaweza kubadilisha kila
kitu.
Uzuri ni kwamba wale bodaboda wote walikuwa ‘sharp’ kwelik-
weli, wakawa wanavuta mafuta kwa nguvu na kusababisha boda-
boda ziwe zinakimbia kwa kasi kubwa kwelikweli, wakati mwing-
ine tukinusurika kugonga miti au kuanguka kutokana na ubovu wa
barabara.
Dakika chache tu baadaye tayari tulikuwa tumefika pale kwenye
kile kijito ambacho tuliyaacha magari yetu. Tukashuka kwenye
nzito.
Kama nilivyowahi kueleza kuwa kikosi hiki ni miongoni mwa
vikosi ambavyo huwa havionekani sana mitaani na siku waki-
onekana, basi ujue kuna jambo zito! Tayari nilishapewa mamlaka
ya kukiongoza kikosi hicho tangu tukiwa Dar es Salaam kwa
sababu kilikuwa kinatoka ndani ya kitengo ingawa pia kilikuwa na
maafisa wengine kutoka jesi la polisi hususan kitengo cha FFU.
Muda mfupi baadaye kikosi chote kilikuwa kimeshawasili na
magari kupaki pembeni ya barabara, mengine upande wa kushoto
na mengine upande wa kulia. Kwa kuwa walishapewa maelekezo
ya kupokea maagizo kutoka kwangu, walipofika tu, viongozi
wanne waliokuwa na vyeo vya juu kuliko wenzao, walikuja na
kunipigia saluti.
Hakukuwa na muda wa kupoteza, kwa msaada wa vijana wa
Cyber na teknolojia ya mawasiliano, tulianza kuzipitia picha za
satellite ili kuisoma vizuri ile kambi walikokuwa wamejichimbia
wale wahalifu, wakiongoza na Abdulwaheed.
Niliwaelekeza kila kitu tulichokutana nacho, nikawaonesha yule
kijana wa Kisomali ambaye bado alikuwa kwenye mikono yetu
na kuwaeleza mambo mengi ambayo hawakuwa wakiyajua kisha
baada ya hapo, nikaanza kuwapa mipango ya nilichokuwa nimeki-
panga.
Kwa kuwa ilishaonesha kwamba wale wahalifu walikuwa wame-
jipanga kisawasawa na hatutakiwi kuingia kichwakichwa, nil-
ishauri kwamba tunatakiwa kuendelea kuisoma ile kambi mpaka
usiku kisa ndiyo tutaivamia.
7
N
ILITAKA recconasance ifanyike kwa njia zote mbele,
kwa kutumia teknolojia kama vile kwa kutazama picha
za satellite na kunasa mazungumzo ya simu ya eneo
husika, lakini pia ilikuwa inatakiwa watu waende eneo
la tukio na kufanya ujasusi.
Nilipowaeleza kuhusu suala hilo, niliona wote wakitazamana, hapa
ndipo linapokuja tatzo.
Nimeeleza na naendelea kueleza kwamba nchi nyingi za ulimwengu
wa tatu zinapata sana shida kupambana na ugaidi kwa sababu hazina
watu wenye uzoefu wa kupambana na magaidi na kwa bahati mbaya
sana wengi huwa wanashindwa kuwatofautisha magaidi na majambazi
somali.
Harakaharaka niliwasiliana na wale wenzetu tuliokuwa tumewaa-
cha pale kwenye ile shule ya msingi wakiwa wanajiandaa. Tuli-
hitaji kuongeza nguvu haraka iwezekanavyo ili kuwadhibiti wale
wanaume ambao tungewatumia kama chambo kutekeleza zoezi
lile kuanzia ndani kama nilivyokuwa nimeelekezwa na baba yake
Saima.
Kwa kuwa vikosi vyote vilikuwa tayari, hakukuwa na muda
wa kupoteza, takribani vijana wangu sita na wengine sita kutoka
kitengo cha kupambana na ugaidi walichomoka na ndani ya muda
mfupi tu, wakawa tayari wamefika usawa wa barabarani kutokea
pale tulipokuwepo.
Ilikuwa ni lazima wakae kwa kule mbali ili wasije wakaamsha
hofu kwa wale watuhumiwa na kuharibu mpango mzima.
“Wewe utabaki hapahapa, ukijaribu kutoroka kitakachokukuta
tusilaumiane,” nilisema huku nikichomoa funguo ya pingu na ku-
fungua upande mmoja, nikamfungua mkono mmoja kisha nikam-
funga kwenye mguu mmoja.
Nilifanya hivyo kwa sababu katika hali ya kawaida, hakuna mtu
ambaye angeweza kukimbia akiwa amefungwa mkono na kuun-
ganishwa na mguu, na hata kama angejaribu, asingeweza kufika
mbali.
“Chief, anaweza kutoroka huyu,” alisema mmoja kati ya wale
vijana wa kikosi kazi niliokuwa nao, nikatingisha kichwa kum-
hakikishia kwamba hawezi kwa sababu hata sisi tukiwa mafunzoni,
tulikuwa tukipewa mafunzo hayo na ilikuwa ni mpaka mtu aliye-
fuzu kwa kiwango cha juu kabisa ndiyo anayeweza kutoroka akiwa
amefungwa mkono na mguu kwa pingu.
Pikipiki zilikuwa nne ikiwa na maana kwamba wale vijana nao
walikuwa wanne, lakini sisi tulikuwa watatu, mimi na wale vijana
wawili wa kikosi maalum, kwa hiyo ilitakiwa umakini mkubwa ku-
hakikisha kwamba hakuna yeyote kati yao anayetoroka kwa sababu
kwa kufanya hivyo, tungeharibu mpango mzima.
Niliwapa ishara wenzangu kwamba kila mmoja ashughulike
na mmoja na mimi nitashughulika na wawili na kitu cha kwanza
tulichotakiwa kukifanya, ilikuwa ni kuwaweka chini ya ulinzi kwa
kushtukiza.
Baada ya kila mmoja kunielewa nilichomaanisha, tulianza kuso-
gea kwa mwendo wa kunyata, tukiwa tumekaribia pale, mmoja kati
yao aliingia ndani kwenda kuchukua mzigo, jambo ambalo lilirahi-
sisha kazi kwa sababu sasa kila mmoja alitakiwa kushughulika na
mtu mmoja.
Kwa kasi ya kimbunga tuliwavamia pale, silaha zikiwa mikononi
na kuwaweka chini ya ulinzi kimyakimya. Kwa jinsi tukio lilivyo-
fanyika kwa haraka, kila mmoja alijikuta akiwa chini, tukawapiga
pingu na kuwatuliza chini.
Kufumba na kufumbua yule mmoja aliyekuwa ameingia ndani,
baada ya kusikia purukushani alitoka mbio nje na kutaka kuleta
upinzani lakin naye alijikuta akichotwa mtama na kuanguka chini
kama mzigo, akafungwa pingu na kulazwa pale chini kama wen-
zake.
“Msaada! Majambazi, jamani tumeva...” mmoja kati yao alijaribu
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Twende!” nilisema huku nikimpa ishara ya kuingia ndani. Kwa
kuwa nyumba haikuwana umeme, ilibidi nichomoe tochi ndogo
lakini yenye mwanga mkali na kumulika ndani.
Kule ndani kweli kulikuwa na watoto watatu wa kike na wawili
wa kiume wakiwa wanamsaidia mmwanamke huyo kupika maan-
dazi na mikate. Sebule ilikuwa kama ‘bakery’ ya mikate, wakash-
tuka kuona mama yao akiingia na mimi akiwa amefungwa pingu,
nikatoa amri ya wote kutoka nje, kweli wakatii huku wakitetemeka.
Kule nje walipokelewa na vijana wangu, mimi nikamtaka yule
mwanamke anipitishe chumba kimoja baada ya kingine kuhakiki-
sha kama kweli hakukuwa na mtu mwingine mle ndani.
Nilipekua kila sehemu mpaka uvunguni mwa vitanda lakini haku-
kuwa na mtu, nikatoka naye mpaka nje na kumtaka afunge mlango
mkubwa kwa funguo. Alifanya hivyo na kwa kuwa tayari wale
wenzetu walishapewa maagizo ya kusogea eneo la tukio, tayari
walishafika na kuzingira eneo lote.
Niliagiza nyumba yote ifanyiwe upekuzi wa kina ili kuanga-
lia kama kuna chochote ambacho kinaweza kutusaidia, wale
watuhumiwa wanne pamoja na yule kijana wa Kisomali, niliagiza
wapelekwe pale kwenye ile kambi ya muda pale shuleni kwa ajili
ya mahojiano ya kina, yule mwanamke na wanaye nikaapizwa
wapelekwe kwenye kituo kidogo cha polisi kilichokuwa kwenye
mji ule, kwanza kwa ajili ya usalama wao lakini pia kwa ajili ya
mahojiano ya kina.
huohuo.
Baada ya kila kitu kukamilika, ndipo nilipoanza kuwafafanulia
watu wote waliokuwa wanahusika kwenye misheni ile, mpango
uliokuwa ndani ya kichwa changu na jinsi tutakavyovamia.
Kwa jinsi nilivyochora mpango mzima, kila mmoja alikuwa
anatingisha kichwa kuonesha kuniunga mkono kwa sababu kila
kitu kilikuwaakimepangiliwa kwa ufasaha wa hali ya juu. Mimi
na vijana wawili niliokuwa nawaamini kwa ushupavu, tulitakiwa
kuondoka kwa zile pikipiki wakati vikosi vingine vikiondoka kwa
magari kupita njia tofauti na yetu ili kwenda kuizingira kambi
kisha kusubiri amri kutoka kwangu. Safari ikaanza.
Nilikuwa makini kuhakikisha vikosi vyote vinafanya kazi kwa
kufuata maelekezo yangu na kwa umakini mkubwa kwa sababu
kama alivyokuwa ameniambia baba yake Saima, hatukutakiwa
kumpoteza yeyote kati yetu katika misheni ile.
Ili kuhakikisha kwamba hakuna anayeleta uzembe, nilikuwa
nawasiliana na vikosi vyote kila baada ya muda mfupi, na mimi pia
nikawa nawasiliana na watu wa teknolojia ya mawasiliano (IT) na
wale wa Cyber ili kuhakikisha tunapata taarifa za kila kilichokuwa
kinaendelea.
Kama nilivyoeleza awali, vikosi vyote vilikuwa vimegawa-
nywa kwa mfumo maalum wa kwenda kuizunguka kambi yote
ili mashambulizi yatakapoanza, basi yaanzie kutokea ndani kama
tulivyokubaliana kisha yafuatie kwenye pande zote za kuizunguka
kambi ile.
Majira ya kama saa saba hivi, tayari vikosi vyote vilikuwa tayari
Hata hivyo, kuna kitu hakikuwa sawa! Eneo lote lilikuwa kimya
kabisa na hakukuwa na upinzani ambao ulioneshwa. Ndani ya
muda mfupi tu, vikosi vyote vilikuwa vimeshaingia eneo hilo huku
vingine vikibaki kulinda usalama kuizunguka kambi yote ili ku-
hakikisha hakuna mtu hata mmoja anayetoroka.
Harakaharaka niliinuka pale chini nilipokuwa nimejiegamiza na
kutoa ishara, vikosi vyote vikajipanga katika namna ya kuwekeana
kitu kinachoitwa ‘cover’, nikatoa ishara ya kugawanyika kwenye
makundi na kuingia kwenye nyumba zote zilizokuwa eneo lile,
mimi nikiongoza kuelekea kwenye nyumba ambayo ilionekana
kuwa kubwa kuliko zote.
Bado ukimya ulikuwa umetawala, nikaukanyaga mlango wa
lile jengo kubwa na kujibana pembeni kwa sekunde kadhaa kisha
nikawa wa kwanza kuingia, bunduki ikiwa mkononi huku tochi
yenye mwanga mkali niliyokuwa nimeivaa ikimulika mle ndani.
Hakukuwa na mtu yeyote! Nikatoa taarifa kupitia vifaa vya
mawasiliano na kutaka majibu kutoka kwa vikosi vingine, majibu
yakawa ni yaleyale! Hakukuwa na mtu yeyote kwenye jengo hata
moja!
“Haiwezekani! Haiwezekani!” nilisema nikiwa ni kama siamini
kabisa kilichokuwa kinatokea! Inawezekanaje misheni iliyopan-
giliwa kwa umakini mkubwa kiasi hicho ifeli kizembe namna
hiyo? Viongozi wangu wangenionaje? Lilikuwa ni doa kubwa sana
ambalo lilinifanya mapigo ya moyo yawe yananienda mbio kuliko
kawaida.
ile na kuvitaka vikosi vyote turudi mpaka kwenye ile kambi kisha
maelekezo mengine yatatolewa kuanzia hapo. Kila mmoja alikuwa
amechoka kisawasawa, kwanza uchovu wa kutolala usiku kucha,
kutembea umbali mrefu maporini lakini kubwa ilikuwa ni kush-
indwa kufanikisha misheni ile.
Basi ilibidi kila mmoja atii, tukaanza kurudi ambapo mpaka in-
afika saa mbili za asubuhi, vikosi vyote vilikuwa vimerejea kwenye
ile kambi tuliyoivamia usiku ule. Wale niliowapa jukumu la ku-
fanya upekuzi eneo lile, walikuwa wamefanya kazi yao kwa weledi
wa hali ya juu.
Ushahidi wa kila aina ulikuwa umekusanywa na kuwekwa kwe-
nye masanduku maalum kwa ajili ya uchunguzi wa kitaalamu zaidi
ikiwa ni pamoja na kujaribu kuwatambua baadhi ya watu walio-
kuwa kwenye kambi ile.
Nikiwa naendelea kuangalia ushahidi uliokusanywa, nilipokea
simu ya moja kwa moja kutoka kwa mkurugenzi. Kitendo cha simu
yake kuita moja kwa moja kwenye simu yangu, kilinishtua kwa
sababu kwa kawaida tunapokuwa kwenye misheni kama hizo, ma-
wasiliano huwa yanafanyika kwa kupitia mfumo wa mawasiliano
kupitia vifaa maalum ambapo wote mliopo kwenye misheni husika
mnakuwa mnasikia kila kinachoendelea.
“Unatakiwa kurudi haraka na timu yako! Huko wabaki watu
wachache kwa ajili ya kuendelea kufanya ‘monitoring’ kwa
karibu,” alisema mkurugenzi, huku sauti yake ikionesha kuwa na
mchecheto usio wa kawaida.
Kwa kuwa neno lake lilikuwa ni amri, kilichofuatia baada ya
8
K
WANZA alianza kwa kuichambua ile ripoti iliyo-
tolewa na ubalozi kwa kina na kwa utaalamu wa
hali ya juu, mambo mengi ambayo hayakuwa yame-
bainika awali, yakawekwa wazi.
Akaendelea kuchambua maelezo niliyoyatoa na
mwisho akaja na hitimisho kwamba tunatakiwa kujua ni wapi
kilipo kitovu cha shughuli za watu hao na tukishalijua hilo, itakuwa
ni rahisi zaidi kuwazidi akili.
Ilibidi atumie ubao maalum uliokuwa mle ndani, akawa anachora
kwa kutumia ‘marker pen’ akijaribu kuonesha kile alichokuwa
anakihisi.
Alianza kwa kuanisha njia kuu zinazoingia Dar es Salaam aki-
“Magogoni ni lini?”
“Usiku wa Ijumaa.”
“Ijumaa ipi?”
“Ya keshokutwa!”
“Unafahamu nini kuhusu Selous?”
“Ngome kuu!”
“Location?”
“ Mashariki mwa Stiglers Gorge, Kilometa nne kutoka kwenye
maporomoko!”
“Utabaki ukiwa unaning’inia mpaka nitakapaoenda kuhakiki-
sha kwanza Kariakoo kama ulichokisema ni sahihi na kama siyo
sahihi, utabaki hivyohivyo mpaka tutakapoenda na kurudi Selous!”
nilimwambia, akatingisha kichwa harakaharaka kukubali. Mpaka
hapo nilikuwa na uhakika kwamba alichokisema kilikuwa ni kweli.
Nilisogea kwenye ile swichi, nikabonyeza ile swichi, ‘hook’
ikashuka kidogo chini na kumuwezesha miguu yake kukanyaga
sakafuni, nikamsikia akishusha pumzi ndefu akiwa ni kama haami-
ni kama nimemfanyia ‘fair’ kiasi kile.
Harakaharaka nilikusanya vitu vyangu kikiwemo kifaa maalum
cha kurekodia sauti kilichokuwa kinarekodi maelezo yote ali-
yokuwa akiyatoa yule mzee wa Kisomali. Nilizima taa na kufanya
chumba chote kiwe na giza totoro, nikamuacha palepale na kutoka
nje.
Niliona ni kama hatua ninazopiga zinanichelewesha, nikawa
nakimbia huku nikiendelea kuvaa vizuri vifaa vyangu vya ma-
wasiliano, nikielekea kwenye ile ofisi walipokuwepo mkurugenzi
na timu nzima.
“Uko sawa?”
“Niko sawa chief! Kuna taarifa mpya,” nilisema baada ya kuin-
gia kwenye chumba hicho na kudakwa juujuu na mkurugenzi wetu
ambaye alionekana kuwa na shauku kubwa kuliko wengine wote
waliokuwepo ndani ya chumba hicho.
“Nyumba namba 320 Mtaa wa Aggrey! Kuna duka la simu liit-
walo Tawheed Phone and Accessories,” nilisema huku nikihema.
Watu wote wakatulia wakiwa wamenizunguka, wakiwa na
shauku kubwa ya kutaka kusikia nitakachokisema.
“Hicho ndiyo kituo mipango yote inapofanyika, ikiwa ni pamoja
na kukusanya na kuunda silaha zitakazotumiwa na walipuaji wa
kujitoa muhanga ambao ndiyo waliopangwa kufanya shambulizi
Magogoni,” nilisema, nikaona kila mtu amepigwa na butwaa.
“Tukio limepangwa kufanyika usiku wa Ijumaa, maana yake ni
kwamba tuna siku nne tu kuanzia leo kama taarifa za kiintelijensia
zilivyoeleza,” nilisema, hofu ikazidi kutanda kwenye moyo wa kila
mmoja.
“Kuhusu Selous, kama tulivyobaini awali, huko ndiko ilipo
ngome yao kuu. Mashariki mwa Stiglers Gorge, kilometa nne
kutoka kwenye maporomoko ya Mto Rufiji!” nilisema na kuhitimi-
sha, ukimya ukapita mle ndani, kila mtu akitafakari yake.
“Nashauri kikosi kilichotakiwa kwenda Selous, kianzia kwanza
Kariakoo Mtaa wa Aggrey!” alisema baba yake Saima huku akini-
tazama, mkurugenzi naye akaunga mkono hoja hiyo na karibu kila
aliyekuwa mle ndani akakubalianana kilichosemwa.
madirisha ya chuma.
“Fungua tafadhali,” nilisema huku nikitoa kitambulisho, wale
wauzaji waliokuwa wamejifungia upande wa ndani, wakawa
wanatetemeka, nao wakiwa ni kama hawajui ni nini kilichokuwa
kinaendelea.
Binti mmoja mdogo ambaye alionekana kuwa ndiye aliyekuwa
akihusika na kupokea fedha kwa wateja na kuwapa risiti, alifungua
mlango mkubwa huku akitetemeka kuliko kawaida, nikawa wa
kwanza kuingia kule ndani walikokuwa wakihifadhia fedha.
“Simama!” nilimuamuru yule binti aliyefungua geti, akasimama
huku akitetemeka kuliko kawaida.
“Hakikisha mauzo yako yote na vitu vya thamani vimefungiwa
kwenye droo zake, sisi siyo majambazi kama nilivyokueleza,”
nilisema, harakaharaka yule binti akafanya kama nilivyomuele-
keza, maburungutu ya fedha yaliyokuwa yamekaa kihasarahasara
yakafungiwa kwenye droo kisha nikatoa ishara kwa vijana wangu
nao kuingia upande ule.
“Najua kuna mlango wa kutokea upande wa pili, nataka ufungue
haraka,” nilimwambia huku bunduki yangu ikiwa mkononi.
“Haturuhusiwi, ni bosi mwenyewe ndiye anayejua namna ya
kuufungua!”
“Nimekwambia fungua, unataka nitumie nguvu?” nilimtisha
kwa kumnyooshea bastola, akiwa anatetemeka akanionesha kwa
kidole kwenye kabati kubwa la vioo lililokuwa upande wa ukutani,
nikawapa ishara vijana wangu walisogeze.
Walipolisogeza, wote tulipigwa na butwaa kugundua kwamba ni
9
N
ILIRUDI ofisini kwangu na kwa mara ya kwanza
tangu asubuhi ya siku iliyopita, nilipata muda wa
kukaa kwenye kiti changu. Uchovu niliokuwa nao
ulikuwa siyo wa kawaida kwa sababu kama nili-
vyoeleza, sikuwa nimepata muda wa kupumzika
hata kidogo usiku kucha kutokana na suala lililokuwa mbele yetu.
Kichwa kilikuwa kinawaka moto kwelikweli, ni hapo ndipo
nilipokumbuka jambo ambalo huwa linaniokoa sana pale kichwa
kinapokuwa kimechoka kiasi hicho lakini bado nikawa majukumu
mazito yanayonihotaji nitulize akili mbele yangu.
Tahajudi! Wazungu wanaita ‘meditation’. Hii ni mbinu ambayo
niliokuwa nao.
Ukweli ni kwamba yeye ndiye aliyenipa nguvu kule Jangwani,
Kariakoo kwa kuniambia kwamba hata kama tulishindwa kuwaka-
mata wahusika, lakini kitendo cha kugundua maficho yao pekee
ulikuwa ni ushindi.
Nilimweleza kuwa sitaki mtu mwingine yeyote asiyehusika ajue
ni nini kilichokuwa kinaendelea, akakubaliana na mimi kwa asil-
imia mia moja kwa sababu halikuwa jambo geni ‘kitengoni’ kuwa
na misheni za siri ambazo kitaalamu huitwa ‘classified ops’.
Baada ya kupata baraka zake zote, nilirudi kule ukumbini, vijana
wakawa tayari wameshamaliza kula, na mimi nikala harakaharaka
na baada ya hapo, wote tulielekea kwenye chumba cha kubadilishia
nguo.
Wote tukapiga kombati maalum ambazo zingefaa sana kwa maz-
ingira ya hifadhini, baada ya hapo tukachukua vifaa vyote muhimu,
zikiwemo silaha, majaketi ya kuzuia silaha na vifaa vya huduma
ya kwanza na nikawa nawasisitiza kila mmoja kuchukua vifaa vya
kutosha kwa sababu mazoezi yanaweza kuwa marefu na yanayohi-
tahi vifaa halisi vya mapambano.
Baada ya kumaliza kila kitu, tulitoka kwa kupitia mlango wa
nyuma ambako magari matatu yalikuwa yanatusubiri kwa ajili ya
kutupeleka Kunduchi. Kila kitu kilikuwa kinafanyika kimyakimya
kiasi kwamba kuna watu wengi tu pale ndani hawakuwa wanajua
ni nini kinachoendelea.Waliofanikiwa kujua, waliambiwa kwamba
tunakwenda kwenye ‘drill’ na kwa kuwa tayari matangazo ya
kusitisha oparesheni yalikuwa yameshatolewa na uongozi, kila mtu
mbele yetu!
Baada ya kuzungumza na kikosi kizima kwa takribani dakika
kumi, morali ya kila mmoja ilikuwa imepanda kisawasawa, tu-
kagongesheana mikono pale, kila mmoja akiwa na uhakika kwam-
ba tunakwenda kushinda kimyakimya na baada ya hapo, nilianza
kutoa maelekezo ya jinsi oparesheni hiyo itakavyofanyika.
Mbinu zilikuwa ni zilezile, kwanza kuizunguka kambi yote
kimyakimya kisha kuendelea kusubiri mpaka nitakapotoa maele-
kezo ya kuvamia! Nilihakikisha kila mmoja anazo risasi za kutosha
kupambana muda mrefu zaidi kwa sababu nilikuwa najua kazi
haiwezi kuwa nyepesi.
Tukagawana makundi manne kisha tukaanza kusonga mbele
huku tukiwasiliana kwa karibu, kila mmoja akitoa taarifa ya kila
alichokuwa anakiona mbele yake. Kila kitu kilikuwa kinafanyika
kimyakimya, tukawa tunazidi kusonga mbele kuelekea kwenye lile
eneo ambalo taarifa za kiintelijensia zilionesha kwamba ndipo ilipo
kambi yao ndani ya hifadhi hiyo.
Kazi haikuwa nyepesi kwa sababu kama unavyojua, Selous ni
hifadhi ya taifa yenye wanyama wengi wakali, wakiwemo nyoka
wenye sumu kali, simba, chui, tembo wengi achilia mbali fisi we-
nye njaa.
Mpaka inafika saa kumi na mbili jioni, tulikuwa tumeizunguka
kambi yote kwa takribani umbali wa kilometa moja kutoka kila
upande. Tukawa tunazidi kusonga mbele kwa tahadhari kubwa
huku tukiendelea kusubiri giza liingie kwa sababu oparesheni
ilitakiwa kufanyika usiku ili iwe rahisi kwetu kutimiza kile tuli-
chokuwa tumekipanga.
Tuliendelea kusonga mbele, giza likaanza kuingia na kufanya iwe
ya kutisha kwelikweli, fikiria ni usiku na upo kwenye mbuga yenye
wanyama wakali lakini kama hiyo haitoshi, unaenda kupambana na
magaidi!
Mpaka inafika saa tatu za usiku, tulikuwa tumeisogelea kambi ile
kwa umbali wa mita mia moja, umbali ambao sasa ulituwezesha
kuweza kuona kilichokuwa kinaendelea kwenye lile eneo. Kuliku-
wa na pilikapilika nyingi zinazoendelea, moto ukiwa umewashwa
kwenye maeneo kama manne hivi.
Unaweza kusema ni kama zile picha za satelite zilikuwa zimetu-
potosha kidogo kwa sababu picha zilikuwa zinaonesha kama ni
sehemu ndogo tu yenye vibanda kadhaa vya mabati lakini kumbe
haikuwa hivyo.
Eneo zima lenye kambi lilikuwa na ukubwa kama uwanja wa
mpira, kukiwa na vibanda vingi vilivyojengwa kwa miti na nyasi
ingawa vichache ndiyo vilivyokuwa vimejengwa kwa mabati na
hivi ndivyo vilivyoonekana kwenye picha ya satelite.
Kwa jinsi nilivyokadiria ukubwa wa eneo lile, niliamini lazima
idadi ya watu iwe kubwa na harakaharaka nilikadiria kwamba ku-
naweza kuwa na watu zaidi ya 100, tena wenye silaha.
Sisi tupo ishirini, maadui wapo 100, kwa hesabu za harakaharaka
kila mmoja wetu alitakiwa kupambana na si chini ya watu watano!
Haikuwa kazi nyepesi hata kidogo.
Hata hivyo nilipiga moyo konde, nikawa naendelea kuwafafanu-
lia vijana wangu kila kinachoendelea na mbinu za kutumia, tukawa
kuwa imeshatua.
Harakaharaka tukawa tunakimbia kuelekea pale ilipotua huku
kila mmoja akijitahidi kuinama chini kama sheria zinavyoelekeza
unapoisogelea helikopta ambayo haijazima injini na mapangaboi
yanaendelea kuzunguka.
Mimi nilikuwa wa mwisho kupanda, muda huohuo ikanyanyuka
na kuanza kuondoka kwa kasi.
“Kazi nzuri Snox!” ilisikika sauti kutoka upande wa marubani,
ikabidi nitazame vizuri, sikuamini macho yangu kumuona baba
yake Saima akiwa ndiye anayeiendesha helikopta hiyo. Sikuwahi
kujua kama baba yake Saima ni rubani, nikajikuta nikitabasamu.
“Snox nusu mtu nusu chuma,” alisema mkurugenzi na kusa-
babisha wote tuliokuwa ndani ya ile helikopta tucheke. Walikuwa
ni viongozi wangu, tena wa ngazi za juu kabisa lakini kwa jinsi
walivyokuwa wakizungumza na mimi, utafikiri nalingana nao
kuanzia umri mpaka vyeo.
Stori za hapa na pale ziliendelea wakati helikopta ikipasua anga
kwa kasi kubwa, kila mmoja akawa na shauku kubwa ya kutaka
kusikia jinsi tulivyoianza oparesheni ile mpaka muda ule walipoku-
ja kutupa msaada.
Nilikuwa najitahidi kuwafafanulia kwa kina kwa sababu kama
nilivyosema, wote waliokuwa ndani ya helikopta hiyo, walikuwa ni
viongozi, tena wa ngazi za juu!
Akili yangu kwa wakatu huo ilikuwa haijatulia kabisa na japoku-
wa kila mtu alikuwa ananipongeza, bado sikuwa na amani kabisa.
Kitendo cha kumkosa Abdulwaheed, kilinifanya nione ni kama
“Enhee! Imekuwaje?”
“Inaonesha alikuwa anavuja damu nyingi sana kwa sababu kote
alikopita tumekuta michirizi ya damu!”
“Twende kwenye point! Amepatikana hajapatikana?”
“Hajapatikana, tumefanikiwa kuikuta pikipiki aliyoitumia kuto-
rokea lakini eneo tulipoikuta, tumeona matairi ya gari. Inaonesha
alikuja kuchukuliwa na gari lakini akiwa na hali mbaya maana hata
pikipiki yenyewe imelowa damu!”
“Mungu wangu! Kwa hiyo amefanikiwa kutoroka?”
“Ametoroshwa! Amechukuliwa na gari!” ilisikika sauti upande
wa pili, nikajikuta nimeduwaa nikiwa hata sijui niseme nini tena!
Zilikuwa ni habari ambazo kiukweli zilinichanganya na sasa ni-
kawa najua kabisa kazi haijaisha!
Kama kuna watu wameweza kuwasiliana naye na kwenda kum-
chukua na gari huko maporini, maana yake ni kwamba bado mtan-
dao wao hatukuwa tumeumaliza.
“Tunaendelea na uchunguzi wetu kama kuna chopchote tutata-
arifiana,” ilisikika sauti ya yule kijana wangu, nikabaki nimeiweka
simu sikioni, hata sikujua ilikatwa muda gani.
Nilipokuja kurudi kwenye hali yangu ya kawaida, nilitembea
harakaharaka kurudi pale kwenye meza yangu, nikaendelea kuan-
dika ripoti na baada ya kumaliza, ilibidi niongeze na yale maelezo
kwamba Abdulwaheed alikuwa ametoroka. Nilijua hayatawafurahi-
sha viongozi lakini ilikuwa ni lazima kila kitu kisemwe kwa ukweli
na usahihi.
Baada ya kumaliza, niliichukua ile ripoti kwa kutumia ‘USB
10
N
ILIKUJA kuzinduliwa na alarm kwenye simu
yangu, nikaamka harakaharaka na kitu cha kwanza,
ilikuwa ni kwenda bafuni, nikavua nguo zote na
kujimwagia maji ya baridi. Japokuwa usingizi
haukuwa umeisha, lakini angalau nilijihisi kuwa
mwepesi sana, nikatumia takribani dakika kumi bafuni, maji ya
baridi yakiendelea kunimwagikia mwilini kutoka kwenye ‘bomba
la mvua’.
Nilijikausha vizuri, nikavaa nguo zangu kisha nikatoka harakaha-
raka kuelekea ofisini kwangu. Niliwakuta vijana wangu bado wapo
macho, wakawa wananishangaa.
linaweza kuja kusikika masikioni mwangu katika hali tete kama ile
tuliyokuwa nayo kwa wakati huo.
Nilisogea kwenye ile swichi ya ukutani, nikaiwasha, kile chuma
alichokuwa ananing’inia yule mzee wa Kisomali kikawa kinapanda
juu na kusababisha na yeye avutwe juu na kuanza kuning’inia,
kilipofika katika kiwango nilichoona kinatosha, miguu yake ikiwa
haijagusa kabisa chini, nilisogea kwenye lile boksi la vifaa vya
kutesea lililokuwa kwenye meza ya chuma iliyokuwa pembeni.
Harakaharaka nilivaa ‘gloves’ maalum, nikachagua vifaa
nilivyoona vinafaa kwa sababu ilishaonesha dhahiri kwamba
mwendawazimu huyu alikuwa anataka kucheza na akili yangu.
“Nakuomba unisikilize kidogo, dakika yako moja tu ya ku-
nisikiliza inatosha kabisa na baada ya hapo nitakuwa tayari kwa
hatua yoyote utakayoona inafaa!” alisema lakini sikutaka kum-
sikiliza kabisa, ‘kichaa’ kilishaanza kunipanda.
“Usitumie hasira, unaweza kupata majibu ya unachokitafuta bila
hata kutumia nguvu, mimi ni mkubwa kwako kiumri na nilishaku-
onesha utayari wa kukupa ushirikiano na nimekusaidia kuyajua
mengi ambayo hukuwa unayajua, kwa nini hutaki kunisikiliza
kijana wangu?” alisema, nikawa tayari nimeshachukua zana zangu
zote na kumsogelea.
“Sijui chochote kuhusu Plan B lakini naweza kukusaidia kuku-
onesha ni nani anayeweza kuwa anaijua na mahali alipo! Nisikilize
tafadhali kijana wangu!
“Sukari imepanda na nisipopata matibabu ndani ya muda mfupi
tu naweza kurudi kwa Muumba wangu, itakusaidia nini kumtesa
eneo nilipoelekezwa.
Nikasogea mpaka kwenye kituo cha Bajaj kilichokuwa jirani na
pale nilipopaki gari, nikamchukua dereva Bajaj mmoja na ku-
muomba anipeleke katika Kanisa la Mlima wa Moto, tukakubali-
ana bei kisha safari ikaanza.
Niliamua kuchagua Bajaj na siyo bodaboda kwa sababu nilikuwa
na uhakika kwamba kama alichokisema yule mzee wa Kisomali ni
kweli, lazima mahali anapoishi mtu huyo patakuwa na kamera za
ulinzi ambazo zinarekodi kila kinachoendelea kwa hiyo njia nyepe-
si ni kujificha kwenye Bajaj.
Haukupita muda mrefu tukawa tumeshafika kwenye mtaa
nilioelekezwa, mtihani ukawa ni kusoma namba za nyumba kwa
sababu kwa kawaida vibao vya namba za nyumba huwa zinaandik-
wa kwenye vbao vidogo ambavyo ni lazima usogee karibu ndipo
unapoweza kuziona.
“Kaka hebu simama kwanza mara moja,” nilimwambia yule
dereva tukiwa ndiyo kwanza tumeanza kuingia kwenye mtaa huo,
kweli akasimama.
Nikamwambia nimeelekezwa na mwenyeji wangu namba ya
nyumba, nikamuomba akanisaidie kusoma namba za nyumba mbili
zilizokuwa zinafuata ili nipate njia sahihi ya kuhesabu mpaka kwe-
nye nyumba husika.
Bila hata kutafakari kwa kina na kuelewa nilichokuwa nakitaka,
yule dereva alipaki Bajaj yake na kuteremka, akavuka upande wa
pili na kusogea kwenye geti la kwanza, akaisoma namba kwa sauti,
akasogea kwenye geti la pili, napo akaisoma kwa sauti, nikawa
usalama.
Nilibaki nimepigwa na butwaa nikiwa ni kama siamini, kama
yule mfanyabiashara wa kule Mikocheni ndiye kiongozi wa mpan-
go hatari uliokuwa mbele yetu, na bado viongozi wa juu kama
huyu Kamishna wanakutana naye, tena nyumbani kwake, kulikuwa
na tatizo kubwa pengine kuliko mtu yeyote alivyokuwa anafikiria.
Kwa mara nyingine, nilihisi ni kama jambo hilo limekuwa kubwa
kuliko uwezo wangu, nikawasha gari langu nililokuwa nimelipaki
mita chache kutoka kwenye ofisi za ile taasisi, nikaondoka taratibu
huku nikiwa hata sijui nini cha kufanya.
Swali ambalo bado nilikuwa sijalipatia majibu, yule mzee wa Ki-
somali aliniambia kwamba baadhi ya viongozi wetu, tena wa ngazi
za juu kabisa kwa maana ya Kitengo walikuwa wanawasiliana kwa
karibu na viongozi wa misheni ile ya kuiangusha Magogoni.
Niliyemuona, hakuwa anatoka Kitengo japo alikuwa kiongozi wa
juu kabisa, yaani wale viongozi ambao namba moja anapokuwa na
jambo lolote linalohusu masuala ya ulinzi na usalama, basi ndiyo
anaokaa nao meza moja kujadiliana nini cha kufanya.
Sasa hawa viongozi aliowataja huyu mzee wa Kisomali kutoka
Kitengo ni akina nani na uhusika wao ulikuwaje? Ni nani hasa
aliyekuwa anavujisha taarifa za misheni yetu kwa kundi hili hatari
la magaidi? Maswali yalikuwa mengi kuliko majibu na mtu pekee
ambaye niliona anaweza kuwa msaada kwangu kwa wakati huo,
alikuwa ni baba yake Saima.
“Haloo chief!”
“Naam!”
“Upo ofisini?”
“Ndiyo! Nipo.”
“Naomba kuonana na wewe haraka iwezekanavyo! Naomba iwe
nje ya ofisi.”
“Ulitakiwa kuwa nyumbani kupumzika muda huu! Wewe siyo
mashine, unatakiwa kupumzika, mkeo na familia yako inakuhitaji
pia.”
“Baba, siwezi kupumzika na sitapumzika mpaka nitakapoki-
maliza nilichokianza. Ni wewe ndiye uliyenifundisha falsafa hii!”
nilisema, nikasikia baba yake Saima akishusha pumzi ndefu kisha
akaniuliza mahali nilipo.
“Niko njiani natokea Kurasini!”
“Coco Beach!”
“Roger that sir!” nilimjibu kwa ‘code’ za kijeshi nikimaanisha
kukubali kile alichokuwa amekisema, nikakaa vizuri kwenye
usukani na kuanza kukanyaga mafuta kwa kasi kubwa kuelekea
Ufukwe wa Coco.
Baada ya takribani dakika ishirini hivi, tayari nilikuwa nimefika
Coco Beach, nikawa naangaza macho huku na kule, hususani seh-
emu ambayo mimi na baba mkwe wangu, baba yake Saima tulisha-
wahi kukutana kama mara mbili hivi siku za nyuma kwa masuala
ya kikazi.
Niliangaza huku na kule lakini sikumuona na ufukweni hapo
palikuwa na watu wachache kwa muda huo. Nikaenda kupaki gari
kwenye maegesho, ile nateremka tu, nikashtukia mtu ananigusa
begani.
11
J
AMBO lenyewe ni kwamba jeshi la polisi liliitisha mku-
tano na waandishi wa habari makao makuu. Katika mku-
tano huo, kiongozi mmoja wa juu katika jeshi hilo kupitia
kwa waandishi wa habari, alilitangazia taifa kwamba ile
hofu iliyokuwapo ya tetesi za kuwapo na mipango ya
shambulizi la ugaidi, lilikuwa limezimwa.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwatangazia watu wote kwamba
nchi yetu ipo salama! Kulikuwa na tetesi zilizosambaa kwa kasi
kwenye mitandao ya kijamii na kwenye baadhi ya vyombo vya
moja.”
“Ikitokea umegundua kwamba na mimi nahusika, utachukua
uamuzi gani?” aliniuliza swali lingine lililozidi kunichanganya
kichwa changu.
“Haiwezi kutokea!”
“Usiseme haiwezi kutokea, nakuuliza sasa hivi, ikitokea umegun-
dua hivyo utachukua hatua gani?” alisema, safari hii akinitazama
kwa macho yaliyokosa kabisa utulivu, pumzi zikimuenda mbio.
“Nitasimama upande wako, nitakulinda na kukutetea!” nilim-
danganya waziwazi kwa sababu hali aliyokuwa nayo, haikuwa ya
kawaida kabisa!
“Naomba dawa zangu!”
“Dawa zako? Zipi?”
“Naomba dawa zangu za moyo!” alisema huku akianza kutapa-
tapa na kujishika kifuani!
“Chief! Chief!”
“Naomba dawa zangu,” alisema huku akinioneshea kwa kidole
kule kwenye meza yake. Alishindwa kuendelea kusimama, akakaa
kwenye kiti kilichokuwa pembeni ya kile nilichokuwa nimekalia
huku akiendelea kuugulia maumivu makali.
Ilibidi nifanye kama alivyoniambia, nikakimbia upande wa pili
wa meza yake, nikakuta kuna kikopo kilichokuwa na vidonge
ndani yake, nikasoma haraka maelekezo yake na kugundua kwam-
ba vilikuwa ni vidonge vya kuzuia shambulio la moyo na alitakiwa
kuwa anakunywa kimojakimoja kila anapopata shida kwenye moyo
wake.
12
“
AHSANTE! Jambo ambalo sina wasiwasi nalo ni kwam-
ba una moyo mzuri sana! Najivunia kuwa bosi wako!”
alisema kisha akanywa maji kwa wingi kutoka kwenye ile
chupa iliyokuwa pale mezani.
Akaendelea kujiweka vizuri, nikamsogezea viatu vyake
na soksi, nikamsaidia ambapo baada ya muda, alikuwa amerudi
kabisa kwenye hali yake ya kawaida.
“Najua umepatwa na mshtuko kwa sababu siamini kama ulikuwa
unajua kwamba huwa nina matatizo ya moyo!”
“Nilikuwa najua!” nilisema huku nikililazimisha tabasamu kwe-
13
B
ABA yake Saima alikuwa na mawazo ambayo
kimsingi hayakuwa yakitofautiana sana na kile
tulichokuwa tumekizungumza mwanzo japokuwa
yeye aliongeza mbinu za kimedani zaidi. Akasisiti-
za kwamba lazima tufanye kila kinachowezekana
kuhakikisha tunalizuia hilo na akamueleza mkurugenzi kwamba
hiyo ndiyo itakuwa sababu pekee ya namba moja kurudisha uami-
nifu kwake.
Tulijadiliana pia kuhusu suala la ‘double’ ambapo baba yake Sai-
ma alikuwa na taarifa za ndani zaidi na akatuelekeza nini ambacho
kiliamriwa kwa kushirikisha vitengo viwili, sisi pamoja na kikosi
cha ulinzi wa namba moja.
anapata ahueni.
Nilimpa ishara yule dada wa mapokezi aliyenifikisha kwenye
wodi hiyo kwamba arudi kuendelea na majukumu yake, nikamshu-
kuru kwa ishara, akaachia tabasamu hafifu kisha akaondoka haraka.
Mle wodini tukabaki wanne, mimi, dokta Cosmas na wale manesi
wawili, ikabidi nisogee jirani zaidi nikiwa na shauku ya kutaka
kujua ni nini kilichokuwa kimemtokea yule mzee wa Kisomali kwa
sababu mambo yalikuwa yamebadilika ndani ya muda mfupi sana.
“Nilienda kumuangalia kule basement ikiwa ni pamoja na kwen-
da kumpelekea dawa zake za Kisukari.”
“Ulipofika alikuwa na hali gani?”
“Alikuwa na afya njema kabisa na tukawa tunataniana na kuche-
ka wakati nikimpima kiwango cha sukari.”
“Baada ya hapo, nikamchoma sindano ya Insulin kama kawaida
ili kuweka sawa kiwango chake cha sukari kama utaratibu ulivyo,
lakini nikashangaa muda mfupi baadaye hali yake ikibadilika!”
“Mungu wangu!” nilisema, kengele ya hatari ikalia ndani ya
kichwa changu.
“Dawa uliyomchoma iko wapi?” nilimuuliza, akaacha kila
alichokuwa anakifanya na kusogea kwenye mkoba wake, akatoa
kichupa kidogo kilichokuwa na kiasi kidogo cha dawa.
“Ni zilezile ninazomchoma tangu uliponikabidhi kwake!” alise-
ma, akionesha kuchanganyikiwa kabisa.
“Sawa, endelea na kazi!” nilimwambia, harakaharaka akaungana
na wale manesi, wakawa wanaendelea kuhangaika. Yule mzee wa
nilichokuwa nakizungumzia.
“Taarifa ulizokuwa unamvujishia huyo mwanaume ndizo
zilizofanya mpaka leo tushindwe kuudhibiti mtandao hatari wa
magaidi ambao wanataka kuishambulia Magogoni. Bila shaka
sasa unaelewa makosa yako yana uzito kiasi gani. Kibaya zaidi ni
kwamba umekuwa pia ukipata taarifa nyingine nyeti kutoka kwa
mkurugenzi wetu na wewe ukawa unazipeleka moja kwa moja kwa
huyo mwanaume wako. Huu ni uhaini wa kiwango cha juu kabisa
Berthany na adhabu ya uhaini inafahamika.”
“Nisaidie kaka Kenny!”
“Mara ya mwisho umekutana lini na Chriss?”
“Asubuhi ya leo,” alisema, nikashusha pumzi ndefu.
“Sasa nisikilize, kitu cha kwanza utatakiwa kufanikisha Chriss
kukamatwa, tena sasa hivi. Ushirikiano utakaoutoa ndiyo utaka-
oonesha ni kwa kiasi gani unajutia makosa yako.”
“Nipo tayari chief.”
“Nieleze njia rahisi tunayoweza kuitumia kumchukua bila mtu
yeyote kujua kinachoendelea.”
“Muda huu atakuwa kwenye ‘depot’ yao, Kiwalani. Nashauri
twende mpaka Kiwalani, nitampigia simu na kumweleza aje tuon-
ane mara moja, akija basi itakuwa ni rahisi kwenu kumchukua,”
alisema Berthany, nikatafakari kile alichokuwa amekisema na
kuona kina mantiki.
“Tunaondoka pamoja, mguu kwa mguu, ukileta ujuaji wa aina
yoyote tusilaumiane,” nilisema huku nikiinuka, nikatoka na ku-
muacha mle ndani. Ilikuwa ni lazima niende kwanza kuwapanga
kani wa gari.
“Hakukuwa na ulazima wa kufanya hivi, anaweza kushtuka akija
na kuniona.”
“Nina maana yangu, fanya kama nilivyokuelekeza,” nilimwambia
huku nikiingia kwenye siti ya nyuma ya gari lile ambalo lilikuwa
na tinted, nikamtaka aendeshe mpaka nje ya ile ‘depot’, kweli aka-
fanya hivyo huku nikimfuatilia kwa makini kutokea siti ya nyuma,
vijana wangu nao wakafanya kama tulivyokubaliana.
Berthany aliendesha gari mpaka kwenye maegesho ya nje ya
ile ‘depot’, nikampa simu na kumuelekeza aweke ‘loud speaker’
wakati akizungumza naye. Tayari vijana wangu walikuwa wame-
shajipanga kwenye ‘formation’ kama tulivyokubaliana, tayari kwa
kazi.
“Chriss!”
“Mambo baby!”
“Poaa! Upo kazini?”
“Ndiyo! Vipi kuna jipya?”
“Hamna hata jipya, tunaweza kuonana mara moja, nimekuja huku
mitaa ya kazini kwako nikaona nikupitia japo nikuone. Nipo nje
hapa kwenye ‘parking’,” alisema Berthany huku akijitahidi sana
kutoonesha tofauti yoyote kwenye mazungumzo yake.
“Dakika sifuri baby, tena ndiyo vizuri twende tukapate ‘lunch’
pamoja,” alisema mwanaume huyo bila kujua kwamba kumbe
alikuwa amewekwa kwenye mtego.
Muda mfupi baadaye, kijana mmoja mrefu, maji ya kunde mwe-
nye mwili wa mazoezi, alionekana akitoka kwenye lango kuu la
14
“
CHRISTOPHER Ephraim Walusanga,” nilimuita kwa
jina lake kamili.
“Ulizaliwa Desemba 24, 1989 katika Hospitali ya
Mbozi Mission mkoani Mbeya, siku hizi ni mkoa wa
Songwe,” nilisema, akashtuka na kunitazama kwa macho
ya mshangao.
“Ulisoma shule ya msingi Mbozi Mission Primary School na
kuhitimu darasa la saba. Ukaenda kusoma Vwawa Day Secondary
School, ukafukuzwa ukiwa kidato cha tatu kwa sababu ya kuka-
matwa ukiwa unavuta bangi, ni kweli siyo kweli?”
ni yapi.
“Hakuna mtu yeyote ambaye unaweza kumletea maelezo mepesi
namna hiyo halafu akakuamini. Wewe unahesabika kuwa gaidi,
tena gaidi hatari,” niliendelea kumchanganya kichwa ili kuendelea
kumsoma.
“Hapana, mimi siyo gaidi. Mimi nilielekezwa tu kwenda ku-
chukua fedha kwa mhasibu wetu, akanielekeza kuzipeleka mahali
fulani kisha nikapewa huo mzigo wa vichupa vya dawa. Mimi sijui
chochote kinachoendelea zaidi ya kutumika kama dalali tu afande,
sijui nakuapia kwa Mungu.”
“Hivi unafikiri unaweza kunidanganya mtu kama mimi? Hivi
unanifahamu vizuri kweli? Jinsi tulivyokuja kukukamata pekee ku-
napaswa kukufanya ugundue kwamba sisi siyo watu wa kawaida.
“Najua unajua kila kitu ila hapa unatafuta huruma. Nikwambie
tu kwa kifupi ni kwamba taarifa ambazo umekuwa ukimlaghai na
kumtishia Berthany ili akupe, ndizo ambazo zimekuwa zikitumika
na magaidi wanaotaka kuishambulia ikulu. Bila shaka ulisikia
kwamba kuna tukio la ugaidi lilikuwa linataka kutokea, basi wewe
pia umeshiriki kwenye njama zote na ushahidi upo.
“Kwa hiyo kama nilivyokwambia, wewe fikiria uone ni kwa
namna gani utakayoweza kutusaidia kuwapata huyo bosi wako
na wenzake. Ukifanikisha hilo, nakuahidi kwamba nitasimama na
wewe, ukileta ujuaji basi kesi yako ndiyo hiyo na hukumu yake
inafahamika,” nilisema na kutoka, nikamfungia mlango kwa nje na
kurudi ofisini kwangu.
“Nikiwa nimekaribia, akili zangu zilinituma kupitia kwanza kwa
kosa aliyafanya?”
“Hapana, Dokta Cossy ni mtu makini sana, hawezi kufanya
makosa yoyote ya kusababisha uzidiwe ghafla,” nilimtetea Dokta
Cossy kwa lengo la kumtoa wasiwasi yule mzee kwa sababu kama
angegundua ni nini kilichokuwa kimetokea, lazima angeacha kutoa
ushirikiano.
“Amefanya kazi kubwa sana kukupigania, anastahili pongezi,”
nilimwambia, nikamuona akishusha pumzi ndefu na kutuliapale
kitandani.
“Nilijua habari yangu imekwisha,” alisema, nikawa naendelea
kumfariji pale kwa upole.
“Tunaweza kuzungumza?”
“Bila shaka.”
“Mara ya mwisho wakati naagana na wewe uliniambia jambo
kuhusu Abdulwaheed, ukaniambia unajua wapi kwa kumpata.”
“Ndiyo, mambo yanapomuwia magumu, huwa anarudi kujipanga
upya na sehemu zake ni mbili, Kibiti au Mafia.”
“Nawezaje kumpata?”
“Kama unaweza, nenda Kibiti au tuma watu waende, ukifika
stendi ya mabasi, ulizia kwa Ustaadh Fundi, naomba kalamu na
karatasi nikuandikie ujumbe, ataelewa na atakusaidia,” alisema,
nikashtuka nikiwa ni kama siamini kusikia yale aliyokuwa anayas-
ema.
Sikutaka kupoteza muda, nilitoa kalamu, nikajisachi mwilini
kuangalia kama nilikuwa na karatasi, sikuliona, nikaangazaangaza
mle wodini na kuona ‘notebook’ ndogo juu ya droo iliyokuwa
pembeni, nikaichukua.
Ilikuwa ni ya Dokta Cossy, nikachana karatasi moja na haraka-
haraka nikamsogezea yule mzee wa Kisomali. Akaandika maneno
machache kwa lugha ambayo hata sikuielewa kisha chini akaan-
dika namba fulani hivi.
“Mwambie nimekutuma mimi lakini usimwambie kwamba
mnanishikilia, anaweza kuingiwa na hofu na akakataa kutoa ush-
irikiano. Kubwa zaidi, naomba msimpe kashikashi ya aina yoyote,
ni mtu mzuri,” alisema yule mzee.
“Kwa nini unafanya yote haya?”
“Nimeamua kukusaidia, nitatekeleza nadhiri yangu kwa sababu
nimegundua kwamba kwa miaka mingi sikuwa katika mstari
mzuri wa maisha na sasa nimeamua kubadilika,” alisema, nikashu-
sha pumzi ndefu na kunyoosha mkono wangu wa kulia kumpa,
akaupokea palepale kitandani, tukatazamana kwa sekunde kadhaa.
“Nenda harakam, muda hautoshi.”
“Nashukuru, lakini kabla sijaondoka, naomba nikuulize kitu
kingine.”
“Kitu gani?”
“Gilbert Mutasigwa ni nani?”
“Unaniuliza mimi? Nadhani mimi ndiyo nilipaswa kukuuliza
wewe swali hilo,” alisema, akazidi kunichanganya.
“Umemsahau bosi wako?”
“Bosi Mute?” niliuliza kwa mshtuko nikiwa ni kama siamini,
nikamuona akicheka.
“Siku hizi siyo binadamu wa kawaida, mambo mliyomtendea
wanaishi.
“Karibuni,” alisema huku akituoneshea ishara kwenda kukaa
kwenye viti vilivyokuwa vimepangwa vizuri pembeni ya mti wa
mkorosho, akaingia ndani kwake na muda mfupi, kundi la wan-
awake na watoto kama nane hivi, wote wakiwa wamejistiri vizuri
walitoka na kutusalimu.
“Hii ni familia yangu, nimewaita wawasalimu kwa sababu
ukarimu ni jadi yetu, mtatumia nini, maji, juisi au maziwa?”
alisema Ustaadh Fundi ambaye nyumba yake ilikuwa inatosha
kuonesha kwamba alikuwa anaishi maisha fulani ya kujiweza sana
kiuchumi kwa sababu hata wake zake wawili aliotutambulisha,
walikuwa na afya njema, achilia mbali watoto wake.
“Tunashukuru, tumekula tulikotoka!”
“Hapana, lazima mtie baraka kwenye nyumba yangu, mimi
mgeni yeyote akija hapa lazima ale au kunywa chochote, huo ndiyo
utaratibu wangu,” alisema na kuwageukia wake zake waliokuwa
wamesharudi ndani na kusimama mlangoni kwa ndani.
Akasogea na kukaa kwenye moja kati ya vile viti vilivyokuwa
pale chini ya mkorosho, akatutazama tena mmoja baada ya mwing-
ine.
“Nitawasaidia kwa sababu ya chuki yangu kwa Abdulwaheed
na kundi lake, walikuja kama watu wazuri lakini mwisho wame-
tuingiza sisi wenyeji kwenye matatizo makubwa sana. Wanafanya
mambo tofauti kabisa na maelekezo ya dini yetu ya haki,” alisema
kwa upole, akionesha kuwa na ustaarabu wa hali ya juu unaoletwa
na mtu mwenye hofu ya Mungu.
‘staftahi’.
Kumbe alikuwa ameenda ndani kubadilisha nguo, akatoka akiwa
amevaa tofauti kabisa na jinsi tulivyomkuta awali, miguuni akawa
amevaa mabuti kama ya kijeshi, kofia pana iliyoziba sehemu
kubwa ya kichwa chake na koti refu! Kwa kumtazama tu, ilionesha
kwamba kweli amedhamiria jambo.
Tulimshukuru kwa ‘staftahi’ kisha tukainuka, yeye akatangulia
mbele. Tulitokea kwenye geti kubwa lililokuwa upande wa mbele
wa nyumba ile, tukapata nafasi ya kuitazama vizuri.
Kama nilivyosema, kwa mazingira yale ya kule, ilikuwa ni
nyumba unayoweza kuiita bora, ikiwa imejengwa kwenye eneo
kubwa lenye mandhari nzuri.
Tulitoka mpaka nje, yule mzee akatoa simu na kupiga ambapo
muda mfupi baadaye, Bajaj ilikuja na kusimama kando yetu.
Akatuonesha ishara kwamba tuingie, kisha na yeye akaingia wa
mwisho.
“Ni mbali kidogo na kwa jinsi mlivyovaa, haitaleta picha nzuri
kuonekana mkiwa mmeongozana na mimi mitaani,” alisema Usta-
adh Fundi, tukakubaliana na wazo lake ingawa bado ilibidi tuwe
makini sana na kila kilichokuwa kinaendelea.
15
T
ULITOKA mpaka nje kabisa ya Kibiti, tukaiacha
barabara ya lami na kuingia kwenye barabara ya
vumbi, upande wa kushoto wa Barabara ya Kusini.
Baada ya umbali mrefu, alimpa ishara dereva kwam-
ba asimame na atusubiri hapohapo mpaka tutaka-
porudi.
Akikuuliza mtu yeyote mwambie upo na mimi lakini usiseme
kama nipo na wageni,” alisema Ustaadh Fundi, yule kijana akai-
tikia kwa adabu na safari ikaendelea, safari hii tukitembea kwa
miguu.
Tulipita kwenye mashamba mengi ya korosho na minazi yasiyo-
kulipa kisasi.
“Usiwe na wasiwasi,” nilimwambia na bila kupoteza muda, tu-
kagawana njia za kupita kuelekea kwenye ile nyumba.
Chief Mwaipopo yeye alichagua kusogea moja kwa moja kuele-
kea mbele, mimi nikatakiwa kuzunguka na kutokea upande wa pili
ili asipate mtu yeyote nafasi ya kutoroka. Nilianza kusonga mbele
kuelekea upande tofauti, nikawa najibanza kwenye miti na kuta za
nyumba chakavu kuzuia nisije kuonekana na mtu yeyote.
Niliendelea kusonga mbele na ndani ya dakika zisizozidi tatu ni-
kawa tayari upande wa pili, nikiitazama nyumba ile kutoka kwenye
maficho niliyoyachagua, mita kama ishirini hivi kutoka kwenye ile
nyumba.
Nilimpa ishara Chief Mwaipopo kwa kutumia vifaa maalum vya
mawasiliano, muda huohuo naye akatoka pale alipokuwa ametega
akisubiri ishara kutoka kwangu.
Sijui nini kilitokea lakini ghafla nilisikia filimbi ikipulizwa, kama
zile zinazotumiwa jeshini, nikashtuka sana kwa sababu ilionesha
ni kama tayari wasaidizi wa Abdulwaheed walikuwa wameshtukia
uwepo wetu eneo hilo.
Baada ya filimbi, kilichofuatia ilikuwa ni milio ya risasi lakini
ajabu ni kwamba hazikuwa zinarushwa upande wangu, nikajua
Chief Mwaipopo na Ustaadh Fundi tayari wameingia matatizoni.
Kwa jinsi risasi zilivyokuwa zinarindima, kwanza ilionesha
waliokuwa wakifyatua risasi hizo walikuwa na mafunzo ya ku-
tumia silaha lakini kama hiyo haitoshi, ilionesha kwamba silaha
walizokuwa wanatumia, zilikuwa ni za kivita, mafunzo yangu
suala hilohilo.
“Umemfahamu vipi Ustaadh Fundi?”
“Sikuwa namfahamu kabla ya leo, ila niliunganishwa na yule
mzee wa Kisomali kama nilivyokueleza.”
“Inaonesha anajua mambo mengi sana huyu, ulikuwa unajua
kwamba anamiliki silaha?”
“Siyo tu kumiliki, sikuwa najua pia kwamba anajua kuitumia
lakini pia sikuwa najua anazijua medani za kivita! Hakika amenis-
hangaza sana.”
“Ukimtazama unadhani ni mtu mwema?”
“Mimi pia nilitaka nikuulize swali hilohilo.”
“Nafikiri tunatakiwa kuzungumza naye kwa kina, siyo mtu wa
kawaida ingawa akili zangu zinaniambia kwamba ni mtu mwema.”
“Kwa ushirikiano aliotupa, mimi pia akili zangu zinaniambia
kwamba ni mtu mwema ingawa jambo ambalo bado sijalielewa ni
jinsi alivyokuwa na hasira na Abdulwaheed, inaonesha kuna jambo
kubwa sana alifanyiwa na huyu mwendawazimu.”
“Yote tutayajua baada ya kuzungumza naye na nashauri kwamba
lazima mazungumzo kati yetu na yeye yawe ya kirafiki,” alise-
ma Chief Mwaipopo, nikakubaliana naye kwa kila alichokuwa
anakisema na muda huohuo, ilibidi mimi nitoke na kumfuata Usta-
adh Fundi ambaye alikuwa amekaa pembeni akiwa amejitenga,
akionesha kuwa na mawazo mengi ndani ya kichwa chake.
“Mbona umejiinamia Ustaadh Fundi!”
“Mawazo! Mawazo kijana wangu.”
“Nashindwa nikushukuru kwa namna gani kwa jinsi ulivyoweze-
“Tunaweza kumuamini?”
“Asilimia mia moja! Kumbe miongoni mwa wale mabinti tu-
naowashikilia, mmoja ni mwanaye wa kumzaa na alirubuniwa na
Abdulwaheed kwamba anakwenda kumtafutia kazi mjini,” nilise-
ma, baba yake Saima akawa anatingisha kichwa kuonesha kuelewa
nilichokuwa namueleza.
“Hatuna muda wa kupoteza, tuna dakika kumi kabla ya kupaa
kwenda Mafia!” alisema kisha akanipa ishara kwamba nikaendelee
na majukumu yangu ya kuwaandaa vijana wangu, tayari kwa safari
hiyo.
Harakaharaka niliwakusanya vijana wangu, tukapeana maelekezo
ya mwisho ambapo pia nilimtambulisha kwao Ustaadh Fundi na
kuwaeleza kwamba tutakuwa naye kwenye misheni yetu mpaka
mwisho.
Baada ya kumaliza kuwapa maelekezo ya mwisho, niliwataka
wakae ‘standby’ kwa ajili ya kuondoka, nikamtafutia Ustaadh Fun-
di ‘bullet proof vest’, kizibao maalum kwa ajili ya kuzuia risasi.
“Hujaniambia chochote kuhusu familia yangu!”
“Usijali kuhusu hilo, ipo salama na itakuwa salama, nimeshatoa
maelekezo maana kuna wenzetu wanakuja kwa njia ya barabara
kuongeza nguvu, kila kitu kitakuwa sawa,” nilimwambia ili kumri-
dhisha lakini ukweli ni kwamba sikuwa nimeshafanya mawasiliano
na wenzangu kuhusu kuimarishwa kwa ulinzi nyumbani kwake.
Ilibidi nimfuate baba yake Saima, nikaenda kumueleza kuhusu
suala hilo lakini tofauti na nilivyokuwa nafikiria mimi, alishauri
kwamba suala hilo tuzungumze na jeshi la polisi kwa sababu
pepe.
Pengine unaweza kujiuliza hili linawezekanaje? Nikutoe wasi-
wasi kwamba ni mbinu ya kawaida ambayo huwa inatumika sana
kwa watu maalum kwa sababu za kiusalama.
Hata zinapotokea ziara za viongozi wakubwa duniani kote,
mfano Rais wa Marekani anapokuwa kwenye nchi nyingine kwa
ziara, maafisa usalama wa nchi hiyo huwa wanakawaida ya kuzi-
ma mawasiliano yote ya simu na internet kwa kutumia teknolojia
maalum na hufanya hivyo kwa lengo la kuzuia watu wenye nia
ovu kufanya mawasiliano na kupanga njama zao.
Hata namba moja anapokuwa anafanya ziara kwenye maeneo
korofi hususan kwenye mipaka ya nchi, teknolojia hii pia huwa
inatumika sana, mnashtukia tu simu za mitandao yote haziwezi
kutoka wala kuingia mpaka shughuli inapokamilika.
Hicho ndicho kilichofanyika na baada ya hilo kuwezekana,
tulitakiwa sisi ndiyo tuwe wa kwanza kuhakikisha kama kweli kila
kitu kimeenda sawa. Nilitoa simu yangu ya mkononi, kwenye lile
eneo ambalo ‘network’ ya simu ya mtandao husika husoma, zil-
ionesha kutokuwa na alama yoyote inayoonesha kwamba mtandao
unapatikana eneo hilo.
Kil ammoja alijaribu na majibu yalikuwa yaleyale, mawasiliano
pekee ambayo yalikuwa yanapatikana, ilikuwa ni kupitia mifumo
yetu ya mawasiliano ambayo yenyewe ilikuwa inategemea zaidi
mawasiliano ya ‘satelite’ na siyo minara ya kawaida ya simu za
mikononi au za mezani.
Kwa kuwa sasa tulikuwa na uhakika kwamba hakuna mtu
kwenda gerezani.
Baada ya hilo kukamilika, sisi tuliotakiwa kwenda kule gerezani,
tuliondoka pale kambini na kuelekea kwenye eneo la bandari
ndogo ambapo hapo ndipo ingekuwa kituo chetu cha kuondokea
kwa kutumia usafiri wa boti za mwendo kasi ambazo tayari zili-
kuwa zimeandaliwa kwa ajili ya kutuvusha.
Ikumbukwe kwamba wakati haya yakiendelea, bado hakukuwa
na mawasiliano yoyote yaliyokuwa yanapatikana katika eneo lote
la Mafia kwa sababu mitandao ya simu zote za mikononi, simu za
mezani na intaneti ilikuwa imezimwa.
Saa mbili kamili juu ya alama, safari ilianza. Kulikuwa na boti
tatu ambazo zilituchukua mimi, baba yake Saima, Chief Mwaipo-
po, Ustaadh Fundi aliyeendelea kuwa mtu muhimu kwenye msafa-
ra wetu, wale maafisa wawili wa kitengo waliokuwa wenyeji wetu
pamoja na vijana kumi, jumla tukawa watu 15 pamoja na mana-
hodha watatu ambao kila mmoja alikuwa akiiongoza boti moja.
Hawa manahodha walikuwa ni kutoka kikosi maalum cha askari
wanaofanya kazi ya kulinda rasilimali za bahari ikiwa ni Pamoja na
kupambana na uvuvi haramu.
Bahari ilikuwa tulivu, safari ikaendelea huku boti zote tatu zikiwa
zimeongozana, tukapasua mawimbi na kama baada ya dakika kumi
na tano, tayari tulishawasili kwenye gati maalum lililokuwa linatu-
miwa na maafisa wa gereza, ikiwa ndiyo njia ya kuingia na kutoka
kwenye kisiwa hicho kidogo kilichokuwa sehemu ya Visiwa vya
Mafia, kulipokuwa na gereza maalum la siri alikokuwa anashikili-
wa Mutesigwa.
hilo la siri.
“Itachukua muda gani?” nilimuuliza baba yake Saima baada ya
kuwa ametoka kwenye laini na mkurugenzi.
“Hili ni suala la dharura kwa hiyo naamini ndani ya dakika
chache tu agizo litatoka juu.”
“Sasa huyu atapewaje taarifa wakati tumezima mawasiliano?”
“Tunaweza kuzungumza na wataalamu wetu waachilie ma-
wasiliano kwa dakika chache kisha mitambo izimwe tena.”
“Hapana! Ni hatari sana kwa sababu hizohizo dakika chache wa-
naweza kuzitumia wafuasi wa Mutesigwa kumpa taarifa juu ya kila
kinachoendelea. Lakini pia, suala la kuzima mitambo na kuwasha,
siyo kitu cha papo kwa hapo, ni mchakato unaoweza kuchukua
mpaka dakika arobaini na tano kwa mujibu wa vijana wetu wa
Cyber na IT.”
“Kwa hiyo unashauri nini?” baba yake Saima aliniuliza, tukawa
tunatazamana kwa sababu hata mimi sikuwa na majibu ya haraka-
haraka ya nini cha kufanya.
“Nafikiri amri ikishatoka juu, tunaweza hata kutumia nguvu kuin-
gia, hawawezi kutuzidi nguvu hawa.”
“Hapana! Kazi hizi haziendi hivyo Kenny, unataka kuharibu
mambo sasa,” alisema Chief Mwaipopo ambaye muda wote ali-
kuwa kimya akisikiliza jinsi ninavyolumbana na baba yake Saima.
“Hii inaweza kutusaidia,” alisema Chief Mwaipopo huku akitoa
‘satellite phone’ ndogo aliyokuwa nayo kwenye magwanda yake na
kuiwasha. Nimewahi kueleza kidogo kuhusu hizi simu za satellite
au SAT kama ambavyo tulizoea kuziita.
16
B
AADA ya kama dakika kumi hivi za kuendelea
kusubiri, vifaa vyetu vya mawasiliano vilitoa ishara
kwamba kuna mtu yupo kwenye laini. Alikuwa ni
mkurugenzi ambaye alikuwa akimuita kwenye laini
baba yake Saima, harakaharaka akajibu kwamba
yupo kwenye laini, maelekezo yakaanza kutolewa kwa kutumia
lugha ya uficho.
Niliweza kuelewa vizuri alichokuwa anakisema, akaeleza kwam-
ba namba moja alikuwa ametoa maagizo kwa kamishna kuhusu
sisi kuruhusiwa kuendelea na kazi yetu lakini tatizo ni kwamba
kamishna alirudisha majibu kwamba hampati mkuu wa gereza
kwenye simu.
Wote tulishusha pumzi ndefu kwa sababu sasa kile tulichokuwa
tumekipanga kilikuwa kinaenda kutimia, Chief Mwaipopo akamka-
bidhi ile SAT baba yake Saima ambaye aligeuka haraka na kuele-
kea pale alipokuwa amesimama mkuu wa gereza ambaye alionesha
kukosa utulivu kabisa.
Walizungumza kwa kifupi kisha akampa ile simu, tukamuona
akibofya namba fulani kisha akaiweka simu sikioni na haukupita
muda, simu ikapokelewa upande wa pili. Akawa anazungumza na
upande wa pili na baada ya kama sekunde arobaini hivi, alimrud-
ishia simu baba yake Saima kisha wakawa ni kama wanajadiliana
jambo tena.
Baada ya kujadiliana kwa kifupi, mkuu wa gereza aliwaita askari
wake waliokuwa eneo lile na wakati huohuo baba yake Saima aka-
geuka na kurudi pale tulipokuwa tumesimama.
“Permission granted!” alisema kwa Kiingereza, akimaanisha
kwamba ruhusa ilikuwa imetolewa.
Hakukuwa tena na muda wa kupoteza, harakaharaka tukaanza
kujadiliana namna ya kuifanya kazi ile, tukakubaliana kwamba
vijana sita watabaki nje ambapo watalizunguka gereza kwa upande
wa nje ili kuhakikisha kwamba hakuna mtu anayetoka na sisi wen-
gine tutaingia ndani kwa kuongozana na mkuu wa gereza mwe-
nyewe pamoja na wale askari wake.
Kilichokuwa kinatakiwa kwenda kufanyika ndani, ilikuwa ni
kwenda kumchomoa Mutesigwa ili akajibu tuhuma zilizokuwa
zinamkabili.
makini.
“Kwa kuwa wewe ni kijana wa Mutesigwa, na mimi na Mutesig-
wa tumekuwa na uhusiano mzuri sana baina yetu, nitakuwa sahihi
nikisema kwamba wewe pia ni mmoja kati yetu?”
“Sijakuelewa!”
“Utanielewa usiwe na wasiwasi! Najua ni nini kilichowaleta
huku na ni jambo ambalo tulikuwa tunalitarajia, hata asubuhi ya
leo nilizungumza na Mutesigwa na akaniambia kwamba kwa jinsi
anavyokuja, lazima utakuja hapa gerezani na timu yako. Ambacho
hatukuwa tunakijua ni lini na saa ngapi mtakuja!” alisema, nikawa
naendelea kumtazama kwa makini jinsi alivyokuwa anababaika.
“Bado sijakuelewa!”
“Sikiliza kijana wangu! Ni wewe pekee ndiye unayeweza kuni-
saidia kutoka kwenye huu mtego hatari nilionasa ndani yake,
ukinisaidia mimi utakuwa pia umemsaidia Mutesigwa, tupo tayari
kukupa chochote unachokitaka lakini nakuomba sana utoe ripoti
kwamba huku kilakitu kipo sawa.”
“Kitu gani ambacho kipo sawa?”
“Mlichokuja kukifuata.”
“Unajua tumefuata nini?”
“Najua, najua kwamba...” alisema mkuu wa gereza akiwa anaba-
baika na hofu kubwa iliyokuwa inajionesha dhahiri kwenye uso
wake ilionesha wazi kwamba ni yeye ndiye aliyekuwa akimpa
Mutesigwa nafasi ya kufanya aliyokuwa akiyafanya, huku waki-
udanganya ulimwengu kwamba Mutesigwa alikuwa gerezani.
“Chief Kenny!” sauti ya baba yake Saima ndiyo iliyokatisha
gerezani humo.
“Mutesigwa yuko wapi?” nilirudia kumuuliza mkuu wa gereza,
akawa hana majibu.
Mutesigwa alikuwa mfungwa ambaye vyombo vyote vya ulinzi
na usalama vilikuwa vinajua kwamba yupo gerezani, tena kwenye
gereza maalum lililopo Mafia, tena kisiwani.
Inakuwaje tena tumefika kwenye gereza husika halafu tunakutana
na mapichapicha kama yale, ikionesha wazi kwamba mtuhumiwa
alikuwa akiishi maisha ya kifahari kiasi kile? Lakini yote tisa, kumi
ni wapi alipokuwa Mutesigwa kwa wakati huo? Hakuna aliyekuwa
na majibu.
Ilibidi sisi watatu tusogee pembeni kwanza kwa sababu tuliona
ni kama mkuu wa gereza anataka kutuletea mchezo wa kitoto.
Tulianza kujadiliana pale kuhusu nini cha kufanya, tukakubaliana
kwamba kitu cha kwanza ni lazima tufanye upekuzi wa kina ndani
ya lile jengo ambalo ndilo tuliloelekezwa kwamba Mutesigwa
alikuwa akishikiliwa.
Nilitoa wazo kwamba awali alipokuwa gerezani jijini Dar es
Salaam, Mutesigwa na genge lake walikuwa na kawaida ya kuingia
na kutoka gerezani nyakati za usiku kwa kutumia njia maalum ya
chini ya ardhi, kupitia kwenye chemba za maji machafu.
Kila mmoja alikubaliana na nilichokuwa nimekisema, tu-
kakubaliana kwamba tutachunguza kila kitu hatua kwa hatua ili
tupate majibu kamili.
Lakini pia tulikubaliana kutoa taarifa kwa uongozi wa juu na ku-
toa mapendekezo ya nini kifanyike ambapo jambo la kwanza na la
Kwa akili yake lazima anajua kwamba sisi tunajua yeye yupo ge-
rezani kwa hiyo hahusiki na chochote kinachoendelea uraiani kwa
hiyo hata akijua, pengine ndiyo itakuwa sababu ya yeye kuwahi
kurudi gerezani kwa sababu anaamini yupo salama zaidi akiwa
gerezani kuliko akiwa uraiani,” alisema baba yake Saima, maneno
ambayo kwa mbali yalianza kunishawishi nibadili mawazo yangu.
Tuliendelea kujadiliana mambo mengi, mwisho tukakubaliana
kwamba tukae kwa kusubiri lakini ni lazima tujue akiwa anarudi,
huwa anapitia wapi kuingia gerezani na kuwa makini asije akash-
tukia mchezo kabla hajaingia ndani ya eneo la gereza.
Baada ya muafaka huo kufikiwa, tulikubaliana kwamba mimi
nirudi tena kwa mkuu wa gereza kwenda kuendelea kumdadisi.
Wakati nikitaka kugeuka na kuondoka, Chief Mwaipopo alizung-
umza jambo la maana sana.
“Si amekupa namba za simu za askari ambao ameongozana
nao?”
“Ndiyo, hizi hapa,” nilisema huku nikitoa kikaratasi alichonian-
dikia mkuu wa gereza na kukishika mkono.
“Kwa nini wasipewe vijana wetu wa Cyber na teknolojia ya ma-
wasiliano ili wajaribu kuzitrack hizo namba tujue ni wapi walipo?”
“Lakini si mitandao imezimwa?”
“Vipi kama wametoka nje ya eneo mitandao ilipozimwa?” aliika-
zia hoja yake, wote tukakubaliana kwamba alikuwa amezungumza
kitu cha muhimu sana, harakaharaka hilo likafanyika ambapo baba
yake Saima ndiye aliyewasiliana na wenzetu waliokuwa jijini Dar
es Salaam. Akawatajia namba husika na kazi ya kuzifuatilia namba
wakanitazama.
“Hatushindwi kupambana nao, nguvu yetu ni kubwa!” alisema
Chief Mwaipopo na harakaharaka tukashauriana nini cha kufanya.
Hatua ya kwanza ilikuwa ni kuzima injini za boti zote pamoja na
taa zake, hilo likafanyika, injini zikazimwa pamoja na taa, tukawa
tunaelea kwenye maji huku boti zikitingishwa na mawimbi ya
bahari.
Ajabu ni kwamba, muda mfupi baada ya injini zote kuzimwa
na sisi kumezwa na giza la alfajiri, ile milio ya boti nayo iliacha
kusikika, tukawa tunaendelea kujadiliana nini cha kufanya.
Nilimtazama Mutesigwa, na yeye akanitazama, macho yetu yak-
agongana, nikamuona akitabasamu.
Mpaka hapo nilishapata picha kwamba ni kweli wale walikuwa
ni vijana wengine wa Mutesigwa ambao walikuwa wanatufuatilia
na kitendo cha sisi kuzima boti zetu, kiliwafanya washinddwe kue-
lewa tupo upande gani kwa sababu kulikuwa kimya kabisa, upepo
wa bahari ukiendelea kuvuma.
Niliwatazama vijana wangu, mmoja baada ya mwingine. Ni kwe-
li kwamba wote walikuwa wameiva sana katika medani za kimapi-
gano na ndiyo maana nikawachagua, lakini hakukuwa na yeyote
kati yao ambaye alikuwa na anazijua mbinu za medani kwenye
maji, kwa kifupi ni kwamba wao walikuwa wanajua mapambano
ya nchi kavu zaidi.
Ni sisi watatu pekee, mimi, baba yake Saima na Chief Mwaipopo
ambao angalau tulikuwa na mafunzo ya mapigano ya kwenye maji,
moyo wangu ukaingiwa na wasiwasi kwamba endapo hao walio-
heri.
Nadhani walipoona kila mtu ameshika ‘chuma’, mimi nikiwa
mbele kabisa, walipata hofu ndani ya mioyo yao, wakazima ha-
raka taa za boti zao zote kisha milio ikawa inasikika kuonesha boti
zimebadili uelekeo na kuacha kuja kule tulikokuwa tukiwasubiri na
kurudi kulekule zilikotoka.
Wote tulishusha pumzi ndefu, nikawaamrisha manahodha tu-
endelee na safari, kwa kasi kubwa kuliko iliyokuwa ikitumika
mwanzo. Nilimgeukia Mutesigwa, nikamuona akiwa ameinamisha
kichwa chake, nadhani kuna jambo alitarajia litatokea lakini hali-
kutokea.
Safari ikaendelea, boti zote zikawa zinafukuzana kwa kasi kub-
wa. Ilikuwa ni lazima tufike nchi kavu haraka iwezekanavyo ili ku-
jihakikishia usalama kwa sababu kama nilivyoeleza, kikosi changu
hakikuwa na utaalamu wa kupambana kwenye maji.
“Watakuwa ni akina nani hawa washenzi wanaotaka kutujaribu?”
alisema baba yake Saima huku akiishusha bunduki yake chini,
watu wote wakashusha bunduki zao, ukimya ukapita, hakukuwa na
aliyekuwa na majibu kwa baba yake Saima.
Safari iliendelea kwa kasi kubwa, giza la alfajiri nalo likawa
linazidi kukimbizwa mbali na nuru ya mapambazuko na hatimaye
tulianza kuona taa kutokea upande wa pili, kuashiria kwamba tu-
libakiza umbali mfupi kabla ya kufika nchi kavu.
Tukiwa tumekaribia kufika ufukweni, milio ya boti ilianza
kusikika tena zikija kwa kasi, nikawahimiza manahodha kuongeza
kasi na kwa bahati nzuri, tulifanikiwa kuwasili kwenye gati ambalo
17
B
AADA ya msafara huo kuondoka, ndipo mimi na
vijana wangu waliokuwa wamesalia, pamoja na Usta-
adh Fundi, tukapanda kwenye helikopta ya mwisho
na safari ikaanza.
Tukiwa angani, nilianza kuwaona wanafunzi wach-
ache wakiwa wanaelekea shuleni, moyoni nikajipongeza kwa sa-
babu kila kitu kilikuwa kimefanyika kwa ustadi wa hali ya juu kiasi
kwamba hata wanafunzi wasingeweza kujua ni nini kilichokuwa
kimetokea.
Kasi ya kuusindikiza msafara wa wale watuhumiwa wote, ilibaki
kwa wale vijana wa kitengo ambao ndiyo waliotupokea.
457 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
“Nitashukuru sana!”
“Lakini hilo litawezekana kama utaendelea kutoa ushirikiano
vizuri kama unavyofanya kuanzia mwanzo.”
“Haina shida baba, kwanza nashukuru kwamba japokuwa nipo
chini ya ulinzi lakini napata huduma zote muhimu, nakushukuru
kwa kutimiza ahadi zako na nakuahidi nitaendelea kutoa ushiriki-
ano.”
“Vizuri! Nataka kujua kuhusu binti aitwaye Zuleikha!” nilimuu-
liza, akawa ni kama ameshtuka kidogo kisha akakaa vizuri.
“Ni miongoni mwa wale mabinti mlionikuta nao mlipokuja
kutukamata!”
“Unafahamu ametokea wapi?”
“Hapana sifahamu kama nilivyokueleza mwanzo, waliletwa pale
na nikapewa jukumu la kuwa nawahudumia na kuwapa huduma
zote muhimu!”
“Ukiacha hao mabinti tuliokukuta nao, kuna wengine ambao
umewahi kuletewa pale ndani?” nilimuuliza, akashusha pumzi
ndefu na kuinua kichwa chake, akiwa ni kama anavuta kumbu-
kumbu, kisha akanigeukia na kunitazama, tukawa tunatazamana.
“Unisamehe sikuwa nimekueleza kila kitu mwanzo!”
“Usijali, unao muda wa kurekebisha hayo yote na wakati wako
ni huu!”
“Ukweli ni kwamba hawa wasichana hawakuwa wa kwanza
kuletwa pale na mume wangu. Kulikuwepo na awamu nyingine
mbili nyuma, kila awamu ilikuwa na wasichana kumikumi la-
kini wenyewe walikuwa wakija kulala tu, hawakuwa wakishinda
pale!”
“Unasema?” nilisema kwa mshtuko. Nikakaa vizuri na kuendelea
kumsikiliza nikiwa ni kama siamini kile alichokuwa amekisema.
“Walikuwa wakija kuchukuliwa usiku, mida ya kuanzia saa tatu
hadi saa nne, kisha wanarudishwa alfajiri wakiwa wamechoka na
kuchafuka sana, wakati mwingine miili yao ikiwa na majeraha
kwenye maeneo mbalimbali.
“Nilipokuwa nawauliza, walikuwa wananiambia kwamba wa-
metoka kwenye mazoezi na hilo lilikuwa linathibitika kwa jinsi
walivyokuwa wakionekana.”
“Mazoezi ya nini?”
“Awali walikuwa wakiniambia kwamba ni mazoezi tu ya kuweka
miili timamu na niliamini lakini walipokuja hawa wa mwisho, ndi-
po nilipoelewa kuwa hayakuwa mazoezi ya kuweka utimamu wa
mwili bali mazoezi ya kijeshi ikiwa ni pamoja na kutumia silaha.”
“Umewahi kuwauliza walikuwa wanaenda kufanyia wapi hayo
mazoezi?”
“Hawakuwa wakijua kwa sababu wote walikuwa ni wageni,
wengine wakiwa ni kutoka nje ya nchi,” alisema, nikashusha pumzi
ndefu, kijasho chembamba kikawa kinanitoka makwapani.
“Sasa hivi wako wapi?”
“Sijui wako wapi? Ilikuwa wakimaliza mafunzo yao wanaondoka
wanaletwa wengine,” alisema, taa nyekundu ikawa imewaka kwe-
nye kichwa changu.
Niliamini kwamba watu wanaoweza kuwa na taarifa hizo, ni
wawili au watatu. Wa kwanza alikuwa ni Abdulwaheed mwe-
18
B
AADA ya kutafakari sana, niliamua kupiga moyo
konde, nikaenda mpaka kwenye chumba chenye
ulinzi wa juu zaidi, alichokuwa ameshikiliwa, nikain-
gia na kuwaagiza vijana wangu wafunge mlango kwa
nje.
Nilipoingia tu, aliinuka haraka sakafuni alipokuwa amekaa,
mikono na miguu yake vikiwa vimefungwa kwa pingu na minyor-
oro. Ilikuwa ni lazima afungwe kwa mtindo huo kwa sababu ali-
kuwa ni ‘high profile criminal’ kwa maana ya mtuhumiwa mwenye
matukio mengi, makubwa na ya kutisha ya kihalifu.
Watu wa namna yake, walikuwa wakiwekwa kwenye vyumba
tofauti na watuhumiwa wengine na kama nilivyoeleza, hata ulinzi
Bosi Mute miaka hiyo, jinsi alivyotokea kuwa mtu muhimu sana
kwenye maisha yangu, jinsi alivyokuja kunibadilisha na kunifanya
niwe mhalifu anayeogopwa na kila kilichoendelea kwenye maisha
yangu, naamini bado kila mmoja anakumbuka.
Kwa hiyo kilichoendelea baada ya hapo, ilikuwa ni yeye kuen-
delea kunitukana na kunikumbusha mambo mengi kuhusu maisha
yangu na mwisho nikaona imetosha sasa.
“Nitakuuliza kwa mara ya tatu na ya mwisho, baada ya hapo
naomba tusilaumiane, Cat Girls ni akina nani?”
“Huna cha kunifanya! Najua unajua kwamba hakuna unachowe-
za kukipata kwangu, na hakuna unachoweza kunitisha nacho,”
alisema kisha akaachia msonyo mkali huku akiendelea kunitazama
kwa macho makali kwelikweli, midomo yake ikimchezacheza kwa
hasira.
“Utaujutia huu muda, utayajutia maneno yako yote unayoni-
tolea,” nilisema huku nikigeuka na kutaka kuondoka.
“Kilichopangwa lazima kitatimia, uliniangusha mara ya kwanza,
ukaniangusha mara ya pili lakini safari hii hutaweza! Siyo wewe
wala serikali ya kidhalimu unayoitumikia, safari hii lazima tuwa-
shikishe adabu,” alisema na kuendelea kunipaka kisawasawa.
Nilitoka moyo wangu ukiwa umenyong’onyea sana, maneno ya
Mutesigwa yalikuwa yamenitonesha donda ndani ya moyo wangu
kwa kunikumbusha mambo mengi katika maisha yangu ambayo
sikuwa nataka kabisa kuyasikia wala kuyakumbuka.
Hali niliyotoka nayo ndani ya chumba alichokuwa amefungiwa
Mutesigwa, iliwashtua mpaka vijana wangu ambao siku zote
alisema.
Maneno yake yalinipa nguvu kubwa mno ndani ya moyo wangu,
nilishusha pumzi ndefu na kupiga funda la kahawa chungu, nikawa
angalau najisikia vizuri, ni kama alikuwa amenitua mzigo mzito
kichwani.
“Nenda kaonane na mkeo lakini unatakiwa kurudi haraka, bado
tuna kazi kubwa ya kuifanya na wewe ndiyo tunayekutegemea.
Msalimu Kamami, mwambie anipigie simu nimemkumbuka?”
alisema na kunifanya nicheke. Kamami ni jina ambalo alikuwa
anapenda kumuita Saima wakiwa nyumbani na alianza kumuita
tangu akiwa binti mdogo.
“Kuhusu huyu mwendawazimu niachie nitashughulika naye,
umesahau kwamba mara zote mimi ndiyo namshughulika naye?
Wewe nenda, ukirudi utayakuta majibu yako yote mezani,” alisema
baba yake Saima, wote tukacheka.
Alichokuwa amekisema ilikuwa ni ukweli, yeye ndiye aliyekuwa
anammudu linapokuja suala la kumhoji, nakumbuka mara ya
mwisho Mutesigwa alipokuwa anacheza na vichwa vyetu, aliin-
gia kwenye chumba alichokuwa amefungiwa na ndani ya dakika
chache, alitoka huku shati lake likiwa limelowa damu, Mutesigwa
akiwa hoi kwa kipigo.
Kwenye suala la kushughulika na wahalifu sugu, baba yake Sai-
ma alikuwa mbobezi na hilo sikuwa na wasiwasi nalo hata kidogo,
japo kwa kumtazama kwa nje usingeweza kudhani kwamba ndani
yake ana roho kama ya simba.
Basi nilimalizia kahawa yangu, nikatoka uso wangu ukiwa na
bulio hilo.
Kikosi cha kwanza kilikuwa ni wasichana waliopewa mafunzo
ya mashambulizi ya kujitoa mhanga na kundi la pili walikuwa ni
vijana wapiganaji waliopewa mafunzo makali ya kijeshi.
Alieleza kwamba mpango uliokuwepo, ni kwamba walipuaji wa
kujitoa mhanga ndiyo ambao walitakuwa kuwa wa kwanza kuanzi-
sha mashambulizi muda utakapowadia, kisha baada ya kufanya
mashambulizi mfululizo, ndipo kundi la pili litakapoingia na kum-
alizia kazi.
Hata hivyo, baada ya kuyasoma maelezo yote, nilibaini kwamba
kuna mambo ya msingi sana Mutesigwa hakuwa ameyazungumza.
Hao vijana waliopewa mafunzo ya kivita ni akina nani na wali-
kuwa wapi kwa sababu akili yangu ilikuwa inanituma kuamini
kwamba tayari tulikuwa tumeivuruga ngome yote, kuanzia kule
Kibiti, Selous mpaka Mafia.
Lakini swali lingine, lilikuwa ni kuhusu hao wasichana waliope-
wa mafunzo ya kushambulia kwa kujitoa mhanga. Nilitaka kujua ni
akina nani na kama ndiyo hao Cat Girls niliokuwa nikiambiwa au
kulikuwa na kundi jingine?
Na kama wapo kweli, wapo wapi na wamepanga kutumia mbinu
gani kuingia Magogoni? Nilishusha pumzi ndefu na kumgeukia
baba yake Saima, naye kumbe alikuwa ametulia akinitazama jinsi
nilivyokuwa napitia taarifa zilizokuwa ndani ya faili lile.
“Una lipi la kusema?”
“Bado vitu vingi havijaelezwa kwa undani lakini kubwa zaidi
haijaelezwa kwamba licha ya oparesheni zote tulizofanya, bado
“Najua kwa siku kadhaa hizi, lazima kuna watu watakuwa wakii-
fanya kazi hiyo, tukifanikiwa kuwabaini watu hao na kuwafuatilia,
tutafanikiwa kuwapata wahusika wa hayo makundi mawili.”
“Tunawezaje kuwabaini?”
“Ni kwa kupitia hizihizi kamera, lazima tufuatilie na kuchunguza
kwa kina kila kitu kilichokuwa kinatokea kwenye mitaa ya kuzun-
guka Magogoni kwa siku hizi tatu mpaka nne zilizopita lakini pia
lazima tuendelee kufuatilia kila kinachoendelea mpaka muda wa
tukio,” alisema.
Kiukweli lilikuwa ni wazo la msingi sana alilolitoa lakini hatu-
kuwa na muda wa kutosha kupitia video zote hizo. Muda tuliokuwa
nao haukuwa unatosha kabisa na ilibidi nimueleze kuhusu hilo.
“Inawezekana kwa kutumia teknolojia. Ni suala la kujua namna
ya kucheza na kamera zote pamoja na servers na kompyuta zinazo-
tumika kuhifadhi taarifa hizo.”
“Unafikiri inaweza kuchukua muda gani?”
“Ikizidi sana ni saa sita!”
“Saa sita? Una uhakika?”
“Ndiyo! Teknolojia imerahisisha sana mambo, nikipewa nafasi
ya kuingia kwenye servers naweza kukuonesha ni kwa namna gani
hilo linawezekana! Ila itabidi niwe na watu wa kunisaidia pamoja
na kompyuta zenye uwezo mkubwa,” alisema, akaniacha nikiwa
nimepigwa na butwaa nikiwa ni kama siamini alichokuwa ameni-
elezea.
Hata hivyo, kwa kuwa yeye alikuwa amebobea kwenye fani hiyo
kuliko mtu mwingine yeyote, ilibidi nikubaliane naye lakini nili-
19
K
AMA nilivyoeleza mwanzo, Jackson Mashewa
alikuwa bado ni kijana mdogo, ukichanganya na
msoto alioupata mafunzoni, alizidi kuonekana
kuwa mdogo lakini alikuwa na akili na ujuzi
mkubwa mno.
“Unadhani hiki unachokifanya kinaweza kutusaidia vipi kuwa-
nasa wahusika kabla hawajaleta madhara?” nilimuuliza.
“Lazima tuwe na ‘keywords’ kwa maana lazima tujue tunatafuta
nini. Inaweza kuwa labda tunajaribu kuangalia nyendo za mtu
fulani ambaye tunamtilia mashaka, lakini pia tunaweza kuwa labda
kabisa utulivu.
“Kumbe maadui zetu wapo karibu yetu kuliko tulivyokuwa
tunafikiria! Nakubaliana na wewe sasa kwamba kumbe kazi bado
ndiyo kwanza imeanza,” alisema huku akivua koti la suti alilokuwa
amevaa, akalegeza na tai aliyokuwa ameivaa.
“Huyu kijana ana akili kubwa sana! Anaweza kutusaidia kutegua
hiki kitendawili kilichopo mbele yetu!” alisema, nikamweleza kila
alichokuwa anakihitaji na yeye akaniambia kwamba tunatakiwa
kumsaidia na kuhakikisha kila anachokitaka kinatimia na kazi ina-
fanyika haraka iwezekanavyo.
“Tunaanzia wapi?” aliniuliza, swali ambalo hata mimi nilikuwa
nataka kumuuliza. Nadhani alikuwa ameniwahi, nikashusha pumzi
ndefu.
“Nafikiri kwanza tumalizie kuwachunguza wageni wote walioa-
likwa kisha kutokea hapo ndipo tunapoweza kuanza kuunganisha
nukta moja hadi nyingine ili kupata picha kubwa iliyojificha,”
nilimwambia.
“Hawa wendawazimu wamejipanga kisawasawa na tukiwachekea
kweli Magogoni itaanguka, inabidi kwanza tuitishe kikao cha
dharura cha viongozi wote ili tujadiliane kwa pamoja nini cha
kufanya. Naamini kila mmoja akitumia akili zake kisawasawa,
tutafanikiwa kuwawahi na kuwadhibiti. Hii ni hatari sana,” alisema
huku akichukua simu yake ya mezani na kuanza kuibofyabofya,
akaniambia nirudi ofisini kwangu na atakaponipigia simu, nielekee
kwenye chumba cha mikutano ya siri bila kupoteza hata dakika
moja, nikatingisha kichwa kukubaliana na alichokisema, nikatoka
chake.
“Kuna binti mmoja walichukuliwa pamoja ingawa yeye alitangu-
lia kwenda mjini. Amesema kwa mafumbo kwamba wamekutana
naye lakini amemueleza kwamba akipata nafasi akamuagie kwao
kwa sababu anajua hatarudi tena na hataendelea kuishi,” alisema,
nikashangaa kidogo kwa sababu sikuwa nimesikia kitu kama
hicho.
Akanifafanulia kwamba kwenye kile kipengele ambacho binti
yake alizungumza kilugha, ndipo alipoyasema maneno hayo,
akanitaka nikirudie kipande hicho, nikarudia na kweli niligundua
kwamba kuna kitu alikitaja lakini sikuwa nimekielewa au pengine
sikuwa nimekitilia maanani.
Alinieleza kwamba hata yeye hakuwa amepata taarifa kamili
lakini kwa kifupi hicho ndicho alichokuwa amemaanisha, nika-
muuliza kama tukimpa nafasi ya kwenda kuoanana na binti yake
anaweza kumhoji zaidi kuhusu hicho alichokisema?
“Zuleikha hana shida, hata wewe anaweza kukueleza lakini ni
mpaka asikie mimi nimeruhusu akwambie,” alisema, wote tu-
kashusha pumzi ndefu, nikawa natafakari cha kufanya kwa sababu
mpaka muda huo bado sikuwa nimemueleza Ustaadh Fundi ni nini
hasa kilichonifanya nikafunga safari.
“Ningeweza kuondoka na kuongozana na wewe lakini bado sid-
hani kama itakuwa salama kwangu na kwa familia yangu, naamini
kila kitu kinaweza kufanyika bila hata ya mimi kusafiri,” alisema
Ustaadh Fundi.
Nilikubaliana naye na kama nilivyokuwa nimepanga, nilitaka na
20
U
KIMYA ulipita kati yetu, nikiwa najaribu kutafuta seh-
emu ya kuanzia kumweleza kile ambacho ndicho hasa
kilichonifanya nifunge safari kuja kuonana naye.
“Taarifa za kiintelijensia zinaonesha bado shambu-
lio la Magogoni lipo palepale, hawa wendawazimu
wamejipanga kisawasawa kuhakikisha wanaiangusha,” nilimwambia,
akawa ni kama hajasikia vizuri nilichokuwa nimekisema, akanitaza-
ma kwa mshangao.
“Inawezekanaje? Abdulwaheed, Mutesigwa wote wapo kwenye
mikono yenu, inawezekanaje tukio likatokea kama lilivyokuwa
limepangwa/”
“Tulichokibaini ni kwamba walikuwa wameshatengeneza mpango
hayajaharibika!
“Kama unakumbuka nilikuambia kuanzia mwanzo kwamba ili
nitimize ahadi yangu ya kukusaidia,lazima tuhakikishe shambulizi
lililopo mbele yetu halitokei! Likitokea maana yake wewe na wen-
zako wote mnakuwa matatizoni na utanipa wakati mgumu sana wa
kutimiza ahadi yangu ya kukusaidia,” nilisema kwa upole huku
nikiwa nimemkazia macho Zuleikha, mtoto wa Ustaadh Fundi ili
anieleze ukweli.
Nilipomkumbusha makubaliano yetu hayo, alishusha pumzi
ndefu kisha akainua uso wake na kunitazama, alipogundua kwam-
ba nilikuwa nimemkazia macho, aliyakwepesha macho yake kisha
akashusha pumzi ndefu.
“Ni kweli!”
“Ni kweli kuhusu nini?”
“Kwamba nilimwambia baba hicho ulichokisema!”
“Ulimwambia nini? Nataka unieleze mwenyewe ili nipate picha
kamili.”
“Kuna rafiki yangu anaitwa Zahara, tumesoma pamoja, wazazi
wake na wazazi wangu wanafahamiana vizuri kwa hiyo amekuwa
kama ndugu yangu,” alisema kwa sauti ya chini, nikakaa vizuri
kwenye kiti nikimtegea sikio kwa umakini.
“Yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kuja mjini na tuliambiwa
kwamba na wao wamekuja kupewa mafunzo kisha watafutiwe
kazi. Yeye na wasichana wenzetu wengine walitangulia kuja
mjini na tulipoona hawarudi, tukaamini kwamba mambo yao
yanawaendea vizuri ndiyo maana hata sisi ikawa rahisi kukubali
kushawishika,” alisema.
“Enhee, ikawaje?”
“Baada ya mimi na wenzangu wengine kuwa tumechukuliwa na
kuletwa mjini, tulishangaa kuona mafunzo tunayopewa hayafanani
na kile tulichokuwa tumeambiwa mwanzo. Kuna sehemu tulikuwa
tunapelekwa kufanya mazoezi ya kijeshi na siku moja ndipo nili-
pofanikiwa kukutana na Zahara!”
“Mlikuwa mnapelekwa wapi kufanya mazoezi?”
“Sipajui, mimi hii ndiyo mara yangu ya kwanza kuja mjini!”
“Enhee, ulipokutana naye akakwambiaje?”
“Akaniambia kwamba yeye na wenzake hawana matumaini ya
kurudi tena nyumbani kwa sababu walikuwa ni kama wametekwa,
wakifundishwa mazoezi ya kijeshi pamoja na kutumia silaha.
Akaniambia wamesikia habari za chinichini kwamba watapelekwa
vitani kwa hiyo haamini kama watarudi salama. Akanitaka nikipata
nafasi nikawape taarifa wazazi wake.”
“Walisikia kwamba wanapelekwa vitani?”
“Ndiyo! Akaniambia wamekuwa wakifundishwa misimamo
mikali ikiwa ni pamoja na kufundishwa ujasiri wa kuvaa mabomu
mwilini na kwenda kujilipua watakapotakiwa kufanya hivyo.”
“Mungu wangu! Enhee, ikawaje?”
“Aliniambia maneno hayo akiwa analia sana, alikuwa na hofu
kubwa ndani ya moyo wake na kuanzia hapo sijawahi kuonana
naye tena!”
“Unampenda rafiki yako?”
“Ndiyo! Nampenda sana.”
gaashangaa!
“Lakini mfumo wake wa uendeshaji ni kama zile nyingine isi-
pokuwa hapa kuna vitu vichache vilivyoongezeka,” nilimwambia,
eti na mimi nikawa mwalimu kwake kwenye vifaa vya kiteknolo-
jia.
Nilikuwa na ujuzi wa kawaida kwa sababu tukiwa mafunzoni
nchini Israel, namna ya kuongoza ndege zisizo na rubani, kuanzia
ndege kubwa mpaka hizo drone za kupigia picha yalikuwa ni ma-
somo ambayo tulijifunza, ingawa ambacho sikuwa nacho ilikuwa
ni uzoefu kwa sababu hata niliporudi sikupata muda wa kutosha
wa kufanyia mazoezi nilichojifunza na hiyo ndiyo sababu iliyoni-
fanya nimchukue Jack.
Basi baada ya kuzungumza mawili matatu na Jack, tuliingia kwe-
nye gari na safari ikaanza. Hakuwa anajua tunaelekea wapi lakini
mimi tayari nilikuwa na ramani yote kichwani.
Yale maelezo yaliyotolewa na Zuleikha, mtoto wa Ustaadh Fundi
kuhusu lile eneo walilokuwa wakifanyia mazoezi ambako ndiko
alikokutana na yule mwenzake na kumueleza kile alichokuwa
amenielekeza, yalikuwa yakishabihiana na eneo ambalo nimesha-
wahi kulielezea siku za nyuma na nilikuwa na uhakika kwamba
ndiyo penyewe.
Safari iliendelea tukiwa tunapasua lami ya Barabara ya Baga-
moyo au Ali Hassan Mwinyi. Mwendo niliokuwa naendesha, kama
ilivyo kawaida yangu, haukuwa wa kawaida, nikawa nayapita
magari mengine kwa kasi na baada ya takribani dakika ishirini
hivi, tukawa tumeshafika eneo linaloitwa Mbuyuni, njia panda ya
Kunduchi.
Nikaiacha Barabara ya Bagamoyo na kukata kulia na kuingia
Barabara ya kuelekea Kunduchi. Safari iliendelea mpaka eneo
linaloitwa Mtongani, kwa wenyeji wa maeneo ya Kunduchi
watakuwa wanalijua eneo hilo, nikakata tena kulia na sasa tukawa
tunaendelea Kunduchi Mwisho.
Tulifika mpaka kwenye kituo cha daladala cha Kunduchi, jirani
na geti la hoteli moja kubwa na maarufu iliyopo eneo hilo, nikakata
kushoto na kuingia kwenye barabara ya vumbi, taratibu tukaanza
kuyaacha makazi ya watu.
Dakika kadhaa baadaye, tuliwasili kwenye eneo lenye maka-
buri ya kale ambayo inaelezwa kwamba walizikwa mabaharia wa
Kigiriki miaka mingi nyuma. Haya ndiyo makaburi aliyoyaeleza
Zuleikha na japokuwa mwenyewe hakuwa akijua yapo sehemu
gani, maelezo yake yaliendana kabisa na mwonekano wake.
Ilibidi nitafute sehemu ya kupaki gari kwa sababu sikutaka
uwepo wetu ujulikane na mtu yeyote na eneo hilo barabara yake
ilikuwa mbovu sana, ikiwa imejawa na mchanga mwingi lakini pia
kukiwa na vichaka vingi.
“Huku ni wapi tena?” aliniuliza Jack, akiwa anashangaashangaa,
nikamuonesha ishara kwamba atulie. Kama siyo mwenyeji wa Dar
es Salaam, unaweza kudhani upo mkoani huko kwa jinsi eneo zima
lilivyokuwa.
Nilizima gari baada ya kuwa nimelichomeka vichakani, mahali
ambapo isingekuwa rahisi kwa mtu yeyote kuliona.
Nikamtaka Jack achukue boksi lake lililokuwa na ile ‘drone’,
21
D
RONE za kawaida zinazotumika mitaani, huwa
zikiwashwa, taa za rangi ya kijani, nyekundu na
kijani zikawaka lakini hii ilikuwa inawaka sehemu
moja tu, tena mwanga mweupe ambao ni hafifu
kiasi kwamba ukiwa mbali kidogo, huwezi kuuona.
Ilitengenezwa hivi ili hata ikiwa inafanya kazi angani, isiwe
rahisi kwa mtu yeyote kuigundua. Aliishika rimoti yake, akaibofy-
abofya na yale mapangaboi yakaanza kuzunguka kwa kasi lakini
bila kutoa mlio wowote, nikamuona akizidi kushangaa kwa sababu
zile za mitaani, huwa zinatoa mlio fulani ambao ukiwa mita kad-
haa pembeni unausikia.
Nikampa ishara kwamba ajaribu kuipaisha, kweli akabofyabofa
ile rimoti, ikaanza kupanda juu taratibu, kama helikopta inavyopaa.
573 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
22
N
ILIONA kila mtu mle ndani akitingisha kichwa
chake baada ya mkurugenzi kuwa amemaliza
kuchangia, jambo la msingi akisisitiza kwamba
kuanzia muda huo, eneo lote la Magogoni linataki-
wa kuwa ‘zero ground’ kwa maana macho, masikio
na akili zote za vikosi vyote vya ulinzi na usalama vinatakiwa
kuelekeza nguvu zao hapo.
Wajumbe wengine waliendelea kuchangia, ikaibuka ishu ya
usalama wa namba moja, ikabidi baba yake Saima asimame tena
kutoa ufafanuzi. Alieleza kwamba tayari namba moja alishaon-
dolewa Magogoni na kupelekwa sehemu salama na badala yake,
‘double’ wake ndiye aliyekuwepo na ndiye atakayekuwepo mpaka
muda wa tukio.
Nimeshaeleza sana kuhusu maana ya ‘double’ katika masuala ya
lea kuandika.
Kikao cha dharura na cha siri kilimalizika, viongozi wote waka-
wa wanakuja kwangu na kunipa maneno ya kunitia nguvu, yakawa
yanaingilia sikio moja na kutokea sikio jingine.
“Tunahitaji kuzungumza!” alisema baba yake Saima ambaye
ndiye aliyekuwa wa mwisho kunifuata, akanishika begani na kuni-
tazama.
“Umeingiwa na hofu!” alisema huku akitabasamu, ikabidi na
mimi nizuge na kutabasamu kwa sababu ni yeye pekee ndiye aliy-
enisoma kwa usahihi.
“Usiruhusu hofu ikuingie ndani ya moyo wako! Hutakiwi kuogo-
pa kwa sababu hauna sababu ya kuogopa! Umekuwa imara kuan-
zia hatua ya kwanza nakufahamu, naamini utaendelea kuwa imara
mpaka mwisho wa uhai wako! Nikwambie tu miongoni mwa watu
ambao hawana wasiwasi na wewe hata kidogo, ni mimi! Nakuami-
ni kwamba uwezo aliokujaalia Mungu, ni mkubwa sana na utatu-
vusha salama katika hili! Tuliza akili, tuliza moyo wako, tayari hii
vita tumeshaishinda mezani!
“Vita huwa haipiganwi katika uwanja wa vita! Huwa inapiganwa
mezani kwa hiyo kushinda au kushindwa huwa kunaanzia mezani!
Sisi tumeshaishinda hii mezani,” alisema baba yake Saima kwa
busara za hali ya juu.
“Unatakiwa kurudi nyumbani, ukatumie saa hizi chache na
familia yako, saa kumi na moja na nusu unatakiwa uwe hapa!
Tuondoke!” alisema baba yake Saima huku akinishika mkono, kwa
kiasi fulani nikajihisi kuanza kupata nguvu.
jatokea.
Hoja hiyo pia iliamsha gumzo lingine, nikawaona ‘washua’
wakiwa wanatingisha vichwa na kunipongeza kwa jinsi nilivyoku-
wa nawaza nje ya boksi, nadhani hakuna yeyote kati yao ambaye
alikuwa amewaza namna hiyo kama ambavyo mimi nilikuwa
nimewaza.
Mwisho nikaeleza kuhusu ile nyumba kule Masaki ambayo
taarifa za kiintelijensia zinaonesha kwamba ndipo wanapohifad-
hiwa mabinti ambao ni miongoni mwa watu waliopangwa kufanya
shambulio hilo, tena wakiwa na mafunzo ya kujilipua na kujitoa
muhanga, watu wote wakakaa na kutulia kutaka kusikilia nilikuwa
na mawazo gani.
Niliwaeleza kama ambavyo Jack alikuwa amenishauri kwamba
lazima maafisa ambao tayari walishakuwa eneo la tukio, waongez-
we maradufu kwa ajili ya kufuatilia nyendo za kila mtu anayetoka
kwenye jengo hilo, lakini pia kazi ya kudukua kamera za usalama
(CCTV) ambazo zipo kwenye majengo ya jirani na eneo hilo,
iendelee ili kuchunguza kwa makini ni nini ambacho kimekuwa
kikifanyika kwenye eneo hilo.
Nikaeleza pia kwamba magari yanayoingia au kutoka kwenye
jengo hilo, yatanasishwa vifaa maalum vya GPS ambavyo vimeun-
ganishwa na sumaku, ili kufuatilia nyendo zake, kuona huwa
yanakwenda wapi na wapi.
Nilihitimisha mchango wangu na kukaa, wajumbe wakanipigia
makofi, wengi wakionesha kufurahishwa na mchango wangu, ni-
kawa nimetulia huku nikiwa nimevaa sura ya kazi kwelikweli.
ueleza.
“Basi freshi kaka, karibuni sana muwe wateja wangu!”
“Haina shida kabisa,” nilisema huku nikiendelea na kukimbia
taratibu kurudi kule nilikokuwa nimetokea. Sikutaka kukatisha
kurudi pale nilipowaacha vijana wangu kwanza kwa kuogopa
kushtukiwa, nikakimbia mpaka mwisho wa mtaa upande wa pili,
nikapenye kwenye njia za ndani ya mtaa, nikazunguka na kutokea
pale nilipokuwa nimewaacha vijana wangu.
“Mnaendeleaje?”
“Tumeshafanikiwa kupata ‘access’ ya kamera nne mpaka sasa,
kazi inaendelea!”
“Safi, sasa kuna jambo nataka tujadiliane wote,” nilisema baada
ya kupokea majibu kutoka kwa Jack, wote wakaacha kazi yao na
kunisikiliza.
“Nimepita mtaa mzima, nimebaini kwamba kuna cafe moja ina-
tazama na lile jengo, ni sehemu nzuri ambazo wachache wanaweza
kujibanza na kujifanya wateja wakati mkiendelea kufuatilia kila
kinachoendelea. Mnaonaje?” nilisema, kila mmoja akaunga mkono
hoja niliyoitoa, lakini maswali yakawa ni kutaka kujua kama eneo
hilo linaweza kuwa salama?
“Unaulizia usalama kwenye uwanja wa vita? Usalama wako ni
umakini wako,” nilisema, wote wakakaa kimya. Niliwateua vijana
wawili kwa ajili ya kazi hiyo lakini nikawaeleza kwamba wata-
baki na Jack kwanza mpaka baadaye tutakaporudi kuja kuangalia
wamefikia wapi, Jack akakubali kwa moyo mkunjufu, wale vijana
wawili nao wakakubali.
23
K
ILA mtu alikuwa kimya kabisa ndani ya gari, kitu
pekee kilichokuwa kinasikika, ilikuwa ni ‘keyboard’
zikigongwagongwa na vidole vya vijana wangu kwa
kasi ya cherehani.
Nilipiga gia na baada ya dakika kadhaa, tukawa
tayari tumewasili ‘ground zero’, kama nilivyoeleza awali, jina
hilo lilikuwa ni la kificho kumaanisha Magogoni kwa wakati huo.
Kabla hatujafika eneo la tukio, nilikuwa makini kujaribu kuangalia
maeneo mengine muhimu yanayoizunguka Magogoni.
Jambo ambalo nililibaini ni kwamba oparesheni ile ilikuwa in-
aendeshwa kwa utaalamu wa hali ya juu kwa sababu wananchi wa
kawaida walikuwa wakiendelea na majukumu yao kama kawaida
kuwa zikiendelea.
Tofauti na akina Jack, hawa walitakiwa kuendelea kubaki eneo
hilo kutwa nzima. Shughuli za hapa na pale zikawa zinaendelea
ndani ya eneo la Magogoni, kuhakikisha hakuna chochote kibaya
kinachotokea usiku huo.
Baadhi ya watumishi wa Magogoni, walitakiwa kuendelea na
shughuli zao kama kawaida ili kutomshtua mtu yeyote kuhusu kili-
chokuwa kinaendelea, wakatakiwa kuhakikisha kwamba maandal-
izi yote ya dhifa maalum kati ya namba moja na wafanyabiashara
wakubwa, yanakamilika kwa wakati.
Majira ya saa saba za mchana, maandalizi ya mkutano huo,
yalianza kufanyika na ili kuzidi kuwapumbaza zaidi maadui zetu,
taarifa za kufanyika kwa dhifa hiyo, zilitangazwa kwenye vyombo
mbalimbali vya habari, kuonesha kwamba namba moja atakutana
na kufanya mazungumzo na wafanyabiashara wakubwa nchini.
Taarifa kwenye vyombo vya habari, zilieleza kwamba lengo la
mkutano huo, ni kuangalia namna ya kujenga ushirikiano imara
utakaowezesha taifa kupiga hatua kimaendeleo na wafanyabiashara
hao nao kupata mafanikio makubwa.
Kwa kuwa ilikuwa ni ‘mpango mkakati’, taarifa hiyo pia ilisam-
bazwa kwenye mitandao ya kijamii, gumzo likawa kubwa kuhusu
mkutano huo. Muda ulizidi kusonga mbele, maandalizi ya mkutano
nayo yakazidi kupamba moto.
Kama nilivyoeleza awali, kadiri muda ulivyokuwa unazidi ku-
songa mbele, ndivyo ‘presha’ ilivyokuwa inazidi kupanda ndani ya
mioyo yetu. Haikuwa kwangu peke yangu, nilimuona pia mkuru-
shaliona niwasubiri.
Dakika mbili tu baadaye, tayari walikuwa wamepaki nyuma ya
gari langu, Ustaadh Fundi akateremka kama nilivyomuelekeza na
kuja mpaka kwenye mlango wa dereva, nikashusha kioo na kumpa
ishara kwamba azunguke upande wa pili na kuingia kwenye gari.
Alifanya hivyo, akaingia kwenye gari huku akiwa anahema kwa
kasi mithili ya mtu aliyetoka kukimbia mbio za mita mia moja.
Tulisalimiana kisha nikafungua ‘dashboard’ ya gari, nikatoa
kibunda na kuhesabu noti kadhaa za shilingi elfu kumikumi kwa
lengo la kumlipa dereva. Ajabu ni kwamba Ustaadh Fundi aliniam-
bia ameshamalizana naye, nikataka nimrudishie fedha zake lakini
pia akagoma.
Nilishusha pumzi ndefu na kutazama kwenye ‘side mirror’, nika-
muona yule dereva bodaboda akiondoka zake, kuonesha kwamba
ni kweli alikuwa ameshalipwa chake na Ustaadh Fundi.
“Kwa nini umekataa nisimlipe bodaboda na hutaki nikurudishie
fedha zako?”
“Achana na hayo, hebu tuzungumze mambo ya maana!” alisema
na kunifanya nitabasamu kwa sababu aliyazungumza hayo kwa
lugha ya kimasihara ingawa uso wake haukuwa ukionesha masi-
hara hata kidogo.
“Naomba tuongozane tutaenda kuzungumza vizuri huko tunak-
okwenda!”
“Ni wapi? Sitaki kuonekana kwa namna yoyote ile,” alisema, ni-
kamwambia asiwe na wasiwasi, nikawasha gari na kuingia baraba-
rani, nikazunguka na kuanza kurudi Magogoni.
“Hujaelewa nini?”
“Sijaelewa kila kitu, hebu naomba rudia kunieleza, taratibu,
hatua kwa hatua!” nilimwambia Ustaadh Fundi, akanitazama
machoni, na mimi nikawa namtazama, akashusha pumzi ndefu na
kuanza upya kunielezea kile alichonieleza, safari hii akifafanua
vizuri zaidi.
“Wewe umezipata wapi taarifa hizi?”
“Ina maana huniamini si ndiyo?”
“Sijamaanisha hivyo, nataka tu kujua,” nilimwambia kwa sauti
ya upole, akashusha pumzi nyingine ndefu na kunieleza kwamba
amezipata kutoka kwenye vyanzo vyake vya kuaminika.
“Inawezekanaje umeme ukatike mji mzima mpaka hapa? Hili ni
eneo maalum ambalo limepewa kipaumbele namba moja! Umeme
huwa haukatiki hapa?”
“Leo utakatika! Ikifika saa moja na nusu juu ya alama utakatika!
Kama huamini basi sawa!”
“Hata ikitokea umekatika, taarifa nilizonazo zinaonesha majen-
ereta yanayotumika hapa ya kisasa kabisa na yanakaguliwa mara
kwa mara! Inawezekanaje nayo yakazimika na kusababisha giza
totoro?”
“Swali zuri! Ni kwa sababu kuna nyoka ndani! Kuna mtu au
watu wameuza utu wao! Kuna wasichana ambao wataingia mape-
ma au inawezekana wakawa wameshaingia, naamini hao ndiyo
ambao umeniambia taarifa zaio mnazo! Wataingia kwa gia ya kuja
kupamba pamoja na kutoa huduma za vyakula na vinywaji.
“Hao ndiyo watakaokuja kuchora mchoro wote wa kuharibu
kuwa anasikitika.
Aliisikiliza mpaka mwisho, akawa ni kama amepigwa ganzi
mwili mzima, akabaki ametulia kwa sekunde kadhaa kisha akavuta
pumzi ndefu na kuzishusha.
“Tunahitaji kukutana kwa dharura haraka iwezekanavyo!” alise-
ma, nikajaribu kumkumbusha jambo la muhimu.
“Kuna nyoka kati yetu! Tunawezaje kukutana wote tena? Maana
yake si taarifa zitavuja kwamba tayari tumejua?”
“Unashaurije?”
“Tuitane wachache tu, ikiwezekana watatu au wanne tu, mimi,
wewe, mkurugenzi na Chief Mwaipopo!”
“Haitakuwa na maana kama hatutawashirikisha PSU,” alisema
akimaanisha wale maafisa wa kikosi cha ulinzi wa namba moja.
“Hatuwezi kuwaamini, kwa sababu kama ni nyoka, safari hii
yupo upande wao!”
“Kiongozi wao ni mtu mwenye maadili sana! Nimefanya naye
kazi kwa kipindi kirefu, ni mtu unayeweza kumuamini bila tatizo
lolote,” alisema, nikatingisha kichwa kuonesha kumkubalia.
“Na mtoa taarifa wako lazima awepo ili atufafanulie kwa kina
zaidi, najua kila mmoja ana maswali mengi sana,” alisema, ni-
katingisha kichwa kuonesha kukubaliana na alichokuwa anakise-
ma.
Harakaharaka akabonyeza kigaa chake cha mawasiliano, akazun-
gumza kwa lugha ya kifico (code) akiwataka mkurugenzi na Chief
Mwaipopo kuelekea kwenye ofisi ndogo iliyokuwa ndani, akanipa
ishara na mimi nikamchukue Ustaadh Fundi.
zamu.
“Nafikiri tunatakiwa kuzifanyia kazi taarifa hizi haraka iweze-
kanavyo,” alisema mkurugenzi na tukiwa tunatafakari kila mmoja
kwa nafasi yake, taarifa nyingine mpya ziliingia.
Zilikuwa ni taarifa kutoka kwa wale vijana wetu waliokuwa
wamepangwa kuanzia kule Kunduchi na kwenye barabara zote za
eneo lile.
Zilikuwa ni taarifa kwamba, kuna magari mawili aina ya Coaster,
yametoka kwneye ile kambi kule Kunduchi yakiwa yameongozana,
kila mmoja akajua sasa kazi imeanza.
“Nashauri tuahirishe kikao hiki kwa muda, tujue kwanza ni nini
kinachoendelea,” alisema baba yake Saima, wazo ambalo kila
mmoja alilikubali, tukainuka na kutawanyika, mimi ikabidi kwanza
nimrudishe Ustaadh Fundi kwenye gari ili nipate nafasi ya kufanya
kazi kwa umakini zaidi.
24
T
AARIFA ziliendelea kuingia, hatua kwa hatua. Baada
ya magari yale mawili kutoka Kunduchi, kila afisa
aliyepangwa kwenye eneo lake alikuwa akitoa taarifa
ya kila kinachoendelea, magari manne ya vijana wetu,
yakaanza kuwafuatilia kwa nyuma kwa namna ambayo
isingekuwa rahisi kwa wao kujua kwamba wanafuatilia.
Taarifa zilionesha kwamba baada ya kutoka Kunduchi, waliele-
kea moja kwa moja mpaka eneo liitwalo Mbuyuni ambapo ndipo
ilipo njia panda inayozikutanisha barabara mbili, ile ya Kunduchi na
Barabara ya Morogoro.
“Wameingia Barabara ya Bagamoyo, wakielekea upande wa
Mwenge,” ilisikika taarifa kwenye mfumo wetu wa mawasiliano.
lakini pia yale magari mawili waliyokuja nao hawa mabinti inabidi
yakaguliwe kisawasawa, hatuna muda wa kupoteza,” alisema baba
yake Saima.
Hakukuwa na muda wa kupoteza, nilitoa maagizo kupitia vi-
faa vya mawasiliano kwamba wale wanawake wawili watengwe
haraka na ningependa kwenda kuwahoji mimi mwenyewe wakati
magari yote mawili nayo yakikaguliwa.
Kabla ya kwenda kuwahoji wale wanawake, nilielekea kwanza
kwenye kile chumba maalum walipokuwa wale wasichana wadogo
ambao kama nilivyosema, idadi yao ilikuwa ni thelathini.
“Kiongozi wenu ni nani?” nilivunja ukimya, wasichana wawili
wakanyoosha mikono, nikawapa ishara kwamba wasogee pale nili-
pokuwa nimesimama, wakasogea huku wote tukiwa tumezunguk-
wa na maafisa usalama waliokuwa wamewaweka chini ya ulinzi
mle ndani ya chumba kile kikubwa.
“Ni nini kilichowaleta jioni hii?”
“Tumeambiwa kuna kazi ya kupamba ukumbi wa mikutano la-
kini pia kuwahudumia wageni.”
“Vitambulisho vyenu tafadhali,” nilisema, kila mmoja akatoa kit-
ambulisho chake. Vilikuwa ni vitambulisho vilivyoonesha kwamba
walikuwa wanatoka kwenye kampuni ya ‘cartering’ iitwayo Marti-
soor Catering and Hospitality Company.
Ni kampuni hii ndiyo ambayo duru za kiintelijensia, zilionesha
kwamba ndiyo iliyopangwa na Abdulwaheed na wenzake, ku-
tumika kama njia ya kupenya Magogoni. Ni hawa ndiyo ambao
tulielezwa kwamba ndiyo kwa kifupi wanaitwa ‘Cat Girls’.
25
B
AADA ya mahojiano ya awali kumalizika, niliwaita
vijana wangu walionisaidia kuwapekua wale wan-
awake kule ndani mpaka kubaini kwamba walikuwa
na ‘chip’ zilizopandikizwa kwenye mikono yao.
Ndani ya muda mfupi tu waliwasili, wakawakagua
wote kwa kuanzia na dereva na hawakubaini chochote, gari nalo
likakaguliwa kisawasawa, hakukuwa na chochote chenye kutia
shaka.
ndiyo kiungo muhimu kati ya pande zote na baada ya kila kitu ku-
kamilika, namba moja aliteremshwa kimyakimya kwenye kwenye
gari lake, akaongozwa gizani kuingia ndani.
Makubaliano maalum ya siri ilikuwa ni kwamba hatakiwi mtu
yeyote asiyehusika kujua kilichokuwa kinaendelea kisha apelekwe
kwenye sehemu maalum iitwayo ‘vault’ mpaka tutakapokuwa
na uhakika ni nini kilichokuwa kinaendelea. Nitakuja kufafanua
‘vault’ maana yake ni nini na hutumika wakati gani.
Nadhani hata mwenyewe hakuwa ametegemea kwa alichokutana
nacho na ndiyo maana akalazimika kuwa mpole na nahisi kabisa
ndani ya moyo wake alikuwa anajutia uamuzi wake wa kuvunja
makubaliano kwa sababu eneo hilo halikuwa salama tena!
Nililibaini hilo wakati nikipishana naye koridoni ambapo ali-
poniona, japokuwa ilikuwa ni gizani tukiongozwa na tochi kali
zilizokuwa zinawashwa na kuzimwa, alinionesha ishara fulani am-
bayo niliweza kuilewa vizuri kabisa. Hili pia nitakuja kulifafanua
baadaye.
Basi alipelekwa mpaka ‘vault’, muda wote mimi nikawa na kazi
ya kuingia na kutoka kuhakikisha nakuwa macho na kila kili-
chokuwa kinaendelea, jengo zima bado likiwa gizani huku tukiwa
tunawasiliana kila baada ya sekunde chache kuhakikisha kwamba
kila kitu kinakwenda kama kilivyopangwa.
Muda mfupi tu baada ya kuwa amefikishwa ‘vault’, ziliingia ta-
arifa nyingine ambazo zilizidi kutuchanganya! Zilikuwa ni taarifa
za vijana waliokuwa wamejipanga kwenye barabara zote za kuin-
gia na kutoka, ambao walituarifu kwamba eti kulikuwa na mafundi
tatua hili tatizo na mimi naona njia nyepesi kwa sasa, ni kumpigia
simu mkurugenzi wa shirika la umeme, yeye ndiye anayeweza ku-
tuambia tatizo ni nini na kipi kifanyike,” alisema baba yake Saima,
akiingilia majibizano yaliyokuwa yanaendelea kati yetu.
“Ulichokisema ni sawa lakini kwa sababu tunajua itachukua
muda, kwa nini vijana wetu waliosomea ufundi wa umeme wa
majumbani na viwandani wasiitwe haraka kuja kuangalia namna
ya kushughulikia haya majenereta? Tena ikiwezekana waje na jen-
ereta lingine kubwa la ziada haraka iwezekanavyo,” alisema Chief
Mwaipopo, wote tukakubaliana na alichokuwa amekisema kwa sa-
babu alikuwa amefikiri ‘nje ya boksi’ kama wanavyosema vijana.
“Lakini huu pia ni uzembe! Kiongozi wa oparesheni, ulishakuwa
na taarifa kwamba kutatokea hitilafu ya umeme na majenereta
yatashindwa kufanya kazi.
“Kwa nini hukuwasiliana na hao vijana wakafika hapa mapema
na kukaa ‘standby?’, kwa hiyo tulikuwa tunasubiri mpaka tatizo
litokee,” alisema kiongozi wa PSU ambaye ndiyo kwanza alikuwa
amerejea kutoka kumpeleka namba moja sehemu salama kule
ndani.
Lilikuwa ni swali gumu ambalo lilikuwa limeelekezwa kwangu
na kwa sababu alichokuwa amekisema kiongozi wa PSU kilikuwa
ni ukweli ambao upo wazi hata kama alikuwa na chuki dhidi yangu
ambayo hata sijui ilikuwa imesababishwa na nini, nilishindwa cha
kujibu.
“Huu siyo muda wa kulamiana! Narudia tena kusisitiza, huu siyo
muda wa kulaumiana kwa sababu tukianza kuchunguzana hapa,
kinaendelea.
Tukiwa katika hali ile, ghafla tulishtushwa na milio ya risasi,
ambayo ilionesha kurindima kutoka mbali kidogo na pale tulipoku-
wepo, ikitokea upande wa mitaa iliyokuwa jirani na ‘ground zero’,
harakaharaka nikabofya kifaa changu cha mawasiliano kwa lengo
la kutaka kusikia kutoka kwa vijana wangu waliokuwa eneo milio
ile ilikosikika.
Kabla hata sijazungumza chochote, mmoja kati ya vijana wetu
walioripoti kuhusu kuwasili kwa mafundi waliokuwa wanadai
wanakwenda kushughulikia suala la umeme Magogoni, aliripoti
kwamba mafundi wale walikuwa wametoa silaha na kuanza ku-
fyatua hovyo, wakitaka waruhusiwe kupita vinginevyo watawapiga
risasi.
“Permission to engage granted!” alisema baba yake Saima,
nadhani ni baada ya kuona siyo mimi, mkurugenzi wetu wala yule
kiongozi wa PSU anayetoa amri ya nini kifanyike.
Msemo huo wa Kiingereza, huwa unamaanisha kwamba sasa
mnaruhusiwa kuanza kufyatua risasi kujibu mashambulizi pale
mnaposhambuliwa, risasi zikaanza kurindima, safari hii mfululizo.
Milio ile ya risasi ilizua taharuki kubwa si tu kwa wageni walio-
kuwa kule ndani bali kwa kila mtu aliyeisikia. Halikuwa jambo la
kawaida kabisa kusikia milio ya risasi jirani na ‘ground zero’.
26
A
KILI ya haraka ilinicheza kwamba sitakiwi kuen-
delea kuzubaa eneo lile bali kwenda mpaka mstari
wa mbele kuongeza nguvu kwa sababu hiyo ndiyo
ilikuwa maana halisi ya uongozi.
Nilitoka mbio pale tulipokuwa tumesimama na
kukimbilia mpaka getini, vijana wetu kadhaa waliokuwa na silaha,
nao wakawa wananifuata kila mmoja akikimbia huku akiiweka
vizuri silaha yake mkononi.
Tulitoka nje ya geti na kuanza kukimbia kwa tahadhari kubwa
kuelekea kule milio ile ilikokuwa inasikika na kadiri nilivyokuwa
nazidi kusikia milio hiyo, ndivyo ile ‘roho ya kazi’ ilivyokuwa
699 AZIZ HASHIM
MAGOGONI HAS FALLEN
(Magogoni Imeanguka)
inazidi kunipanda.
Muda wote nilikuwa makini kusikiliza ni nini kilichokuwa kinar-
ipotiwa kupitia vifaa vyetu vya mawasiliano, mara ikaingia taarifa
mpya kwamba wale ‘mafundi’ wamevunja kizuizi cha barabarani
na kupita kwa nguvu na magari yao huku wakiendelea kufyatua
risasi.
Sikuwa na wasiwasi kwa sababu nilikuwa na uhakika kwamba
hawatachukua raundi kwa sababu kulikuwa na vizuizi vingine
viwili mbele, nikatoa maelekezo ya vijana wangu kutoruhusu
wendawazimu hao wapite kwenye vizuizi hivyo kwa namna yoy-
ote ile, mimi na vijana wangu tukawa tunazidi kukimbia kuelekea
kule risasi zilizokuwa zinatokea, kila mmoja silaha ikiwa miko-
noni.
Tukiwa tunakaribia kufika kwenye kizuizi cha kwanza kutokea
geti kuu, jambo lisilo la kawaida lilitokea na kunifanya nijihisi ni
kama nataka kuchanganyikiwa.
Zilikuwa ni taarifa nyingine mpya kwamba kuna boti mbili zili-
kuwa zinaonekana kuja kwa kasi kutokea baharini kuja upande wa
nyuma wa Magogoni na maafisa wa kikosi cha wanamaji walipo-
jaribu kuzisimamisha, waliokuwa ndani yake walianza kufyatua
riasi.
“Zinakuja kwa kasi kubwa na taa zote zimezimwa,” alisema afisa
mmoja wa kikosi cha wanamaji kupitia vifaa vya mawasiliano, ni-
kajikuta nimefunga breki za ghafla, vijana wangu nao wakasimama
nyuma yangu na kwa kuwa nao walikuwa wamesikia kinachori-
potiwa, walibaki wakinitazama kusikia nitatoa uamuzi gani, kila
na kuingia ndani?”
“Njoo ujionee mwenyewe,” alisema baba yake Saima ambaye
aliponiona tu nimeingia, licha ya giza lililokuwa limetanda kila
upande, alinifuata na kunisimamisha.
Alipiga hatua ndefu, mikononi mwake akiwa na bunduki na tochi
ndogo yenye mwanga mkali, na mimi nikawa namfuata kwa hatua
ndefundefu, mapigo ya moyo yakidunda mithili ya ngoma.
Alinipeleka mpaka upande wa kushoto wa jengo kubwa, tu-
katembea umbali wa mita kadhaa kwenye bustani nzuri zilizokuwa
zikihudumiwa vizuri, safari yetu ikaishia kwenye chemba ya maji
taka, ambayo mfuniko wake ulikuwa umefunguliwa.
Akamulika ndani na kunitaka nitazame vizuri. Kulikuwa na ngazi
ya chuma ambayo hata sijui iliwekwaje ndani ya chemba hiyo.
Kubwa zaidi, kulikuwa na nguo kadhaa zilizokuwa zimechafuka
na maji taka, zikiwa zimerundikwa kwenye moja ya kona za shimo
hilo.
“Wamebadilisha nguo zao na inaonesha wametoka wakiwa
wamevaa kama maafisa wa humu ndani, na pengine tayari wame-
ingia ndani kabisa mpaka kwenye ukumbi wa mikutano,” alisema
baba yake Saima, nikatingisha kichwa nikiwa ni kama siamini
alichokuwa anakisema.
“Tazama!” alisema huku akimulika na tochi yake na kunionesha
alama za viatu kutoka pale kwenye mfuniko wa ile chemba.
“Huu ni uzembe mkubwa sana umefanyika! Watu wanawezaje
kuingia kirahisi namna hii? Yaani ulinzi wote huu tuliokuwa nao?”
“Na sio tu kuingia, lakini pia kuingia wakiwa na silaha,” alisema
na kazi ikaanza mara moja. Kwa bahati nzuri zaidi, tayari vijana
wa ‘kitengoni’ walikuwa wameshawasili na jenereta la akiba,
wakaunganisha mitambo na ndani ya dakika zisizozidi tan, tayari
umeme ulirudishwa kwenye jengo zima.
Nikaagiza milango yote ambayo ilikuwa ikilindwa kwa mifumo
ya umeme, ‘ilokiwe’ ili asiwepo mtu yeyote ambaye angeweza
kuingia au kutoka bila kutambulika.
Kuwashwa kwa umeme kulitusaidia kuliko maelezo, wale wa-
huni waliokuwa wanajifanya ni mafundi, walidhibitiwa wote na
kufungwa pingu, wakaletwa ndani na kupelekwa kwenye ‘selo’
maalum ya chini ya ardhi iliyokuwa ‘ground zero’.
Lakini pia, kwa kuwa sasa umeme ulikuwepo, taa kubwa zenye
nguvu ziliwashwa upande wa kule baharini ambako wale wahuni
waliokuwa wakijaribu kusogea na boti zao, nao waliweza kud-
hibitiwa kisawasawa na vijana waliokuwa wameapa kufia nchi yao.
Kazi iliyobakia, ikawa ni kwa upande wangu na vijana wangu
wa ndani, kuhakikisha tunawatoa nyoka kabla hawajaleta madhara.
Tulianzia ukumbi wa mikutano ambapo nilitangaza kwamba watu
wote wanatakiwa kutulia sehemu walizokuwa wamekaa na hat-
akiwi mtu yeyote kunyanyuka.
Niliamini kwa wakati huo, teknolojia inaweza kutusaidia kuwa-
baini wahusika kwa haraka bila kutumia nguvu nyingi. Eneo lote la
Magogoni, lilikuwa na kamera maalum ambazo zenyewe zilikuwa
na uwezo wa kufanya kazi hata kwenye giza totoro.
Nikabonyeza kifaa changu cha mawasiliano na kuzungumza na
vijana waliokuwa kwenye ‘control room’, nikawakata watazame
faa vya kisasa vya mawasiliano na vifaa vingine vyote muhimu vya
mawasiliano ya namba moja, hiyo ni kwa mataifa yote duniani na
kadiri taifa linavyokuwa na nguvu za kijeshi na kiusalama, ndivyo
ambavyo hata ‘vault’ zao huwa zinakuwa kubwa na imara zaidi.
Kuta za ‘vault’, hufanya iwe vigumu kwa silaha ya aina yoyote
kupenya. Unaambiwa hata ikitokea ikulu husika ikapigwa kwa
makombora mazito, ndani ya ‘vault’ huwa hakuna kinachoweza
kupenya kwa hiyo usalama wa kiongozi wa nchi, huwa unakuwa
salama kwa asilimia mia moja.
Tukija kwa Magogoni sasa, sitaeleza zaidi kuhusu jinsi ‘vault’
yake ilivyo kwa sababu za kiusalama, lakini kwa kifupi, elewa
kwamba ndiyo sehemu salama zaidi anapoweza kupelekwa namba
moja kunapotokea tatizo lolote lakini pia siyo kila mtu anaweza
kuingia huko. Wengine hufanya kazi kwa miaka mingi bila kujua
kama kuna kitu kama hicho.
Kwa hiyo nilichokifanya, ilikuwa ni kuwasiliana na vijana wa
‘control room’ na kwa kuwa suala lenyewe lilikuwa nyeti, ilibidi
kiongozi wao ndiyo atoe ruhusa ya mimi kuingia kule ndani amba-
po pia ilibidi kiongozi wa PSU naye aidhinishe na yeye ndiye aliy-
etakiwa kuniongoza, nikawa naliona tatizo lingine mbele yangu.
Baada ya kama dakika tatu, mimi na kiongozi wa PSU tulikuwa
kwenye geti la kwanza la kuingia kwenye korido ya kushuka chini
kuelekea kwenye ‘vault’. Hakuna aliyekuwa anamsemesha mwen-
zake, hata sijui hii chuki ilikuwa imetokea wapi.
“Unajifanya mjuaji sana wewe!” alisema kiongozi wa PSU
wakati tukisubiri mlango ufunguliwe huku akinitazama kwa macho
chochote.
Tuliangaza huku na kule lakini hakuna tulichoweza kukiona,
tukawa tunasogea kwa tahadhari kubwa, moshi ukizidi kupungua.
Ghafla niliona kitu kilichozidi kunichanganya kabisa.
Kwenye kona ya chumba kile, mahali kulipokuwa na mlango
wa kuelekea kwenye vyoo vya ndani, kulikuwa na alama za damu
ukutani na pamoja na matundu mengi ya risasi, nikawapa ishara
wenzangu kisha wote tukaanza kusogea kuelekea kwenye mlango
ule, ambao nao ilionesha kwamba umevunjwa.
Tukiwa tunaendelea kusonga mbele kwa tahadhari kubwa, nil-
ishtuka tena baada ya kuona damu zikiwa zinachuruzika kutokea
nyuma ya makabati ya kuhifadhia vitabu na nyaraka mbalimbali
ndani ya chumba hicho.
Nikawapa tena ishara wenzangu, ikabidi tugawane, wawili
waendelee kusogea kule kwenye mlango wa kuingilia chooni
ambao ni mimi na baba yake Saima ambao tulikuwa ‘pair’, kila
mmoja akiwa amemgeuzia mwenzake mgongo, tukisogea mbele
kwa pamoja.
Mkurugenzi ambaye alikuwa ‘pair’ na Chief Mwaipopo, wao
walielekea nyuma ya yale makabati.
“One officer down! I repeat, one officer down!” sauti ya mkuru-
genzi ilisikika kwenye vifaa vya mawasiliano, ikitutaarifu kwamba
afisa mmoja wa usalama alikuwa amepigwa risasi, baada ya kuwa
wamefika kule nyuma ya yale makabati.
Sijui kwa nini lakini akili yangu ilinituma kuamini kwamba
aliyekuwa ameangushwa hawezi kuwa ni miongoni mwetu wala
sikia baba yake Saima akitaka nijibu kama nipo salama, nadhani
walishajaribu kunitafuta mara kadhaa bila mafanikio. Kwa jinsi
alivyokuwa anazungumza, sauti yake ilikuwa ikitetemeka ikione-
sha kuwa yupo kwenye pilikapilika za hali ya juu.
“Kiongozi wa PSU ameasi! Anashirikiana na hawa wendawaz-
imu, wanatushambulia vikali kutokea kwenye chemba, wamemteka
namba moja na inavyoonekana wamemjeruhi,” alisema baba yake
Saima huku akiwa anaonekana ni kama anakimbiakimbia, milio ya
risasi ikawa inasikika zikirindika kwa kasi kubwa.
Yaani ule muda mfupi tu niliokuwa ndani ya bomba, kumbe
mambo yalikuwa yamebadilika kuliko kawaida, nikawa natamani
nimjibu lakini nikawa naogopa kwamba nikifumbua mdomo tu,
nitawashtua wale wendawazimu waliokuwa ndani ya bomba, mita
chache tu kutoka pale tulipokuwepo.
Ilibidi nijaribu kutumia njia ya dharura ya mawasiliano ambayo
haihusishi sauti, nikawa nagonga kwenye spika ya kifaa changu
cha mawasiliano kwa utaratibu maalum, harakaharaka akawa ame-
shanielewa.
Hali ambayo tulikuwa tumefikia sasa ilikuwa ni ile kufa na
kupona kwa sababu risasi zilikuwa zinarindima kisawasawa, kule
kwenye bomba zilikuwa hazisikiki lakini kwenye kifaa cha ma-
wasiliano zilikuwa zinasikika vizuri kabisa.
Harakaharaka nilikivua kile kifaa cha mawasiliano na kuvaa
mask yangu, angalau sasa nikawa napata hewa safi, nikavuta pumzi
ndefu nikiwa bado sijui nini cha kufanya kwa wakati huo.
Nilichokiamua ni kwamba sasa liwalo na liwe, lazima tuwakabili
kila mmoja.
Hoja iliyotolewa na wote waliokuwa wanapinga, ni kwamba
kama shida yao ilikuwa ni kumteka namba moja, jambo ambalo
walikuwa wamefanikiwa, suala la kujisalimisha lilikuwa haliweze-
kani na pengine wangeweza hata kumdhuru.
Mkurugenzi alitoa hoja ambayo hakuna yeyote kati yetu ambaye
alikuwa ameifikiria kwa wakati huo. Alitaka kwamba vijana wa
Cyber wajiridhishe kwanza kama ni kweli namba moja alikuwa
miongoni mwa wale mateka kwa kutumia teknolojia.
Nilieleza awali kwamba miongoni mwa vifaa vya ulinzi alivyo-
navyo namba moja, ni kifaa maalum ambacho kitaalamu kinaitwa
‘transponder chip’, kifaa kidogo sana ambacho lazima namba moja
awe nacho mwilini muda wote.
Kifaa hiki, huwa kinasoma ‘GPS’ kwa ajili ya kujua namba moja
yupo wapi hasa kunapotokea dharura za kiusalama kama hizo.
Awali walikuwa wameshascan na kutoa majibu kwamba alikuwa
ndani ya bomba lakini kwa kuwa sasa tulikuwa tumeshawarudisha
nyuma mpaka kwenye shimo lile, ilikuwa ni lazima warudie tena
kuscan ili tuwe na uhakika kwa asilimia mia moja.
Akaendelea kueleza kwamba endapo tukishapata uhakika, ndipo
sasa tutumie njia ya majadiliano, kwa kitaalamu tunaita ‘negotia-
tion’. Mjadala mwingine ukaibuka kwamba sera za kiusalama,
zilikuwa haziruhusu majadiliano ya aina yoyote na wahalifu hatari
kama magaidi.
Ilibidi nikae kimya kusikiliza mjadala, moyoni nikawa najisemea
kwamba endapo watu wote wangejua ni mazingira ya hatari kiasi
huwa ni za uongo.
Ahadi tamu ambazo huwa zinatumika ni kama kuwapa usafiri
wa kuwawezesha kuondoka salama bila kukamatwa kutoka eneo
la tukio, au kufutiwa mashtaka yote yanayowakabili na wakati
mwingine kuwaahidi kiasi kikubwa cha fedha ili kuwahadaa na
kuwajaza tamaa ili mwisho wa yote wafanye kile ambacho nyie
mnakitaka.
Basi baada ya majadiliano ya hapa na pale, hoja ilipita, ikatakiwa
itafutwe namna ya kuwasiliana kwa sauti na wale wahalifu kuanzia
waliokuwa wamejifungia kule ndani mpaka wale waliokuwa kule
chini, ikakubaliwa kwamba wale waliokuwa na namba moja kule
chini ndiyo ambao wanatakiwa kufanya nao majadiliano.
Nilishaeleza kwamba miongoni mwa waliokuwa wamejifungia
kule ndani, alikuwa ni kiongozi wa PSU ambaye hata sijui nini
kilitokea mpaka akaasi na kuungana na watu waliokuwa wanataka
kuiangusha Magogoni! Yaani mtu ambaye jukumu lake kubwa
ilikuwa ni kuhakikisha usalama wa namba moja, ndiye aliyekuwa
amekengeuka na kuwa mtu hatari kuliko kawaida, akishirikiana na
wale wendawazimu.
Harakaharaka vijana wa Cyber na wale wa IT walifanya mautun-
du yao, mtaalamu wa majadiliano ya kiusalama ambaye kiukweli
sikuwa namjua ni nani, akaanza kuzungumza na sauti yake ikawa
inasikika mpaka kule chini akitumia vifaa maalum vya kiteknolojia
kuzungumza ambapo sauti yake ilikuwa inasikika vizuri kabisa.
Alianza kwa kujitambulisha, akaeleza kwamba tayari wamesha-
wajua watu wote waliokuwa wamevamia Magogoni usiku ule na
Ilibidi nibane pumzi ili nisije nikaishiwa nguvu, namba moja aka-
fanikiwa kushika vyuma vya dirisha na bila kupoteza muda aliji-
rushia kwa ndani, uzito ukapungua mabegani. Kasi ikawa Ustaadh
Fundi ambaye hakuwa akifikia kwenye lile dirisha, ikabidi niiachie
bunduki na kuinua mikono yangu miwili kwa ukakamavu, Ustaadh
Fundi akawa ameshaelewa nini cha kufanya.
Alikanyaga kwenye mikono yangu ambayo nilikuwa nimeiten-
geneza na kuwa kama daraja, akafanikiwa kulishika dirisha, akaji-
vuta na kupanda kwa juu, nikashusha pumzi ndefu, sasa ikawa ni
zamu yangu. Ilikuwa inatakiwa nipande haraka iwezekanavyo ili
kuhakikisha namba moja anaendelea kubaki mgongoni kwangu.
Nikiwa najiandaa kurukia kwenye mkono wa Ustaadh Fundi
ambaye alikuwa ameshajitengeneza na kupata balansi kwenye lile
dirisha, tulishtuka baada ya tochi yenye mwanga mkali kuwashwa
na kunimulika machoni.
Ilibidi nijirushe kwa sababu nilikuwa najua kinachofuata, risasi
mfululizo zikanikosakosa na kutoboatoboa ukuta, Ustaadh Fundi
akajirusha kwa ndani kwa usalama wake.
Hakukuwa na muda wa kupoteza, niliikamata vyema bunduki
yangu na kuanza kujibu mashambulizi, nikafanikiwa kuwaangusha
wanaume watatu wenye miili mikubwa waliokuwa wakija kasi pale
nilipokuwepo huku wakifyatua risasi.
Kukatulia, nikaangaza macho huku na kule na baada ya kujiridhi-
sha, nilimuita Ustaadh Fundi ambaye kumbe alishajiongeza, akawa
ameshafunga kamba pale dirishani, ambayo hata sijui aliipata wapi
kisha akanirushia.
fanya kazi ili kupata kipato cha kuweza kuendesha maisha yao na
familia zao.
Hata hivyo, walikuwepo wachache ambao walikuwa wana jua ni
nini kilichokuwa kinaendelea ingawa nao hawakuwa wakihusika
moja kwa moja. Ni ushahidi huo uliotolewa na wasichana hao
ndiyo uliofanya kazi iwe rahisi.
Wamiliki wa kampuni hiyo iliyokuwa na ofisi zake Kisutu jijini
Dar es Salaam walienda kukamatwa na kuunganishwa na wenzao
waliokuwa wakiendelea kushikiliwa ‘kitengoni’ na kwenye nyum-
ba maalum.
Ni baada ya saa arobaini na nane kuisha, ndipo tulipotangaziwa
kumalizika rasmi kwa oparesheni ile ambayo kama nilivyoeleza,
kuanzia mwanzo mimi ndiye niliyekuwa kiongozi ambapo bila
msaada mkubwa kwa viongozi wangu, hakika isingewezekana
kabisa.
Mkurugenzi ndiye aliyetutangazia sisi viongozi kwamba oparesh-
eni imekamilika na mimi nikatakaiw andiyo niwatangazie vijana
wangu wote kuhusu taarifa zile. Hakukuwa na muda wa kupoteza,
nilitoa taarifa kupitia kifaa cha mawasiliano na kuwataka vijana
wote walioshiriki kwenye oparesheni ile, kukusanyika kwenye
bustani zilizokuwa Magogoni.
Hata wale waliokuwa wakiendelea na doria kwenye maeneo
mengine yote, walitakiwa kuacha kila walichokuwa wakikifanya
na kufika haraka eneo nililokuwa nimewaelekeza.
Walioachwa, ni wale waliokuwa wakiendelea na matibabu pekee,
lakini wengine wote waliitikia wito na ndani ya dakika kadhaa,
MWISHO.