Professional Documents
Culture Documents
Ushairi Maswali Na Majibu
Ushairi Maswali Na Majibu
atikaschool.org/ushairi-maswali-na-majibu
0 Comments
1/25
Fukuto lanipa neno, neno hili kutamka
Kutamka wazi vino, vino subira kutaka
Kutaka imani mno, mno n’sipate wahaka
Wahaka wa matukano, matukano na mashaka.
Maswali
a) Kwa nini nafsi neni inaomba subira na amani? (al.2)
b) Shairi hili ni la aina gani kwa kuzingatia (al.4)
(i) Mpangilio wa maneno
(ii) Mpangilio wa vina.
c) Kwa kutolea mifano eleza mbinu mbili za lugha zilizotumika katika shairi. (al.4)
d) Andika ubeti wa tatu kwa lugha nathari. (al. 4)
e) Kwa kutolea mifano, eleza jinsi uhuru wa kishairi ulivyotumiwa kutekeleza arudhi. (al.6)
Majibu
(a) Ili asiwe na wasiwasi ya kutukanwa na huhiniwa aepuke kufanyiwa mabaya. 1 x 2 =2
( c) (i) Tashbihi
- Hafifu kama muwele
- Tele mithili kitoto.(al.2)
(ii) Uradidi/Takriri
- Subira’
- Bora, kombora, ukora
- Kiburi, kudhuri n.k.(al.2)
Read More
0 Comments
USHAIRI MASWALI NA MAJIBU MODEL18012023003
18/1/2023
0 Comments
Mkatanimkatika, harithihatorithiwa
Sinaninalolishika, walaninalochukuwa
Mlimwengukanipoka, hata tone la muruwa!
Mrithininiwanangu?
2/25
Sinango’ombesinambuzi,sinakondesinabuwa
Sinahatamakaazi, mupasayokuyajuwa
Sinamazurimakuzi, jinsinilivyoachiwa
Mrithininiwanangu?
Sinakazisinabazi, ilawingiwashakawa
Sinachembeyamajazi, mnonikukamuliwa
Nakwa’cheniupagazi, mgumukwenuku’tuwa
Mrithininiwanangu?
Sinasikuachajina, mkatahatasifiwa
Hatanifanye la mana, mnonikulaumiwa
Poleniwanangusana, sinakwenu cha kutowa
Mrithininiwanangu?
Sinaleosinajana, sinakeshokutwaliwa
Sinazizisinashina, walatawikuchipuwa
Sinawanangu mi sana, la kwacha nakuraduwa
Mrithininiwanangu?
Sinai la keshokwenu,wenyewekuiongowa
Muwanekwanyingi,mbinumwendepasikupuwa
Leo siyo, keshoyenu, kamamutajikamuwa
Mrithininiwanangu?
(Kina cha maisha A.S.Mohammed)
MASWALI
a) Elezahaliyamzungumzajikatikashairihili ( alama 4)
b) Elezadhamirakuuyamshairikulitungashairihili (alama 2)
c) Ni nanianayezungumziwananafsinenikatikashairihili? (alama 2)
d) Elezatoniyashairihili (alama 2)
e) Fafanuambinutatuzalughazlizotumiwakatikashairihili (alama 3)
f) Tambuabahariyashairihiliukizingatia. (alama4)
a. Mizani
b. Vina
g) Andikaubetiwamwishokwalughayanathari/tutumbi. (alama 3)
MAJIBU
a) Hali yamzungumzaji. (al 4)
- maishayenyeumaskinimkubwa.
- maishayasiyokuwanamatumaini.
- maishayaliyokosathamani.
- maishayenyekusikitisha.
b) Dhamirakuuyamshairi (al 2)
- kuwahimizawanawemaishaniilikuhakikishamaishamemaya baadaye kwa vile
haliyasasaniyakimaskini.
d) toniyashairi (al 2)
- masikitiko
- kutamauka/kukosamatumaini
- yakuhuzunisha
e) mbinutatuzalughazilizotumika. (al 3)
- sitiari – mkatanimkatika
- Balagha – mrithininiwanangu?
- takriri – sina
3/25
f) Bahariyashairiukizingatia. (al 4)
mizani – msuko
vina - ukara
Read More
0 Comments
SWALI NA JIBU LA USHAIRI MODEL16012023001
16/1/2023
0 Comments
Siwe uloandaa,
Harusi ya kukata na shoka,
Masafu ya magari, yakilalama jua kali,
Hadi kanisani kungia, mimbari wa kusimama,
Kasema utamuenzi, hadi yenu mauko?
Vipi jicho lageukia, mitaani vipaa mwitu?
Hukunabia we fidhuli,
Mwanangu utamtunza?
Taandamana naye daima,
Ja chanda na pete?
Hukumwonjesha tamu, ya ulaghai huyuno?
Midisko wampleka, kizingizia mapenzi,
Vipi wamtezea shere, mwangu kumliza?
4/25
(f) Eleza kwa kutoa mifano mbinu za kifasihi zilizotumika katika ushairi huu. (al 3)
(g) Eleza vile mshairi alivyotumia idhini ya kishairi katika utungo huu. (al 3)
(h) Bainisha umuhimu wa maswali ya balagha yaliyotumika katika ushairi huu. (al 2)
(i) Andika ubeti wa tatu kwa lugha tutumbi. (al 4)
majibu
Shairi la pili Majibu
(a)
(i) Hakuna urari wa mishororo katika kila ubeti
(ii) idadi ya vipande hailingani katika kila mshororo
(iii) Hakuna mpangilio maalum wa vina.
(iv) Hakuna urari wa mizani katika kila mshororo 1x2
(b) Masuala yanayoibuliwa na mwandishi.
(i) Dhuluma katika ndoa
(ii) Ukosefu wa uaminifu katika ndoa
(iii) Kutowajibika kwa waume
(iv) Tatizo la ukimwi. 1x2
(c) Nafsineni katika ushairi.
(i) Mtaalam katika masuala ya ndoa;
(ii) Mzazi
(i) Mshauri
(ii) Mlezi 1x1
(d) Toni ya utungo huu.
(i) Malalamishi
(ii) kushauri
(iii) Kuzindua
(iii) Huzuni, hasira (ghadhabu)
(e) Mistari mishata
(i) Hukuja hapa kwa wingi
(ii) Siwe uloandaa.
Mistari kifu.
(i) kusema hapa kwa wingi
(ii) Huachi kulia u waya
(f) Mbinu za kifasihi
(i) maswali ya balagha
(a) Hakuja hapa kwa wingi?
(b) Vipi wangeuza ngoma, mapepo kunipigia?
(c) Vipi wamtezea shere, mwanangu kumuulizia?
(ii) Tashbihi
Taandama naye daima ja chanda na pete
(iii) Utohozi
Walavu
midisko
Nitakipu promisi
(iv) Sitiara / jazanda
Vipaa mwitu – wasichana wengine
Nduli – ugonjwa hatari
Kifaranga – watoto
Miamba – watu mashuhuri
(iv) Kuchanganya ndimi; - nitakipu promise
(vi) Tashihisi / uhuishaji
Masafu ya magari yakilalama jua kali
Vipi jicho lagoukia mitaani vipaa mwitu?
Nadhiri zako za nitakipu promisi, zi wapi mwana
(vii) Nahau / msemo
Kufia kidondani – kupata hasara unapofuata kitu unachokiona cha thamani.
-Kukata na shoka, kucheza shere. 1x3
5/25
(g) Idhini ya kishairi iliyotumika.
(i) kuboronga sarufi / kufinyanga sarufi
Hadi kanisani kuingia – kuingia hadi kanisani
Hadi yenu mauko – hadi mauko yetu
Mwanangu kumuliza – kumuliza mwanangu.
(ii) Insksari.
Kunambia – ukaniambia
Wanao – wanawako
Tachukua – utachukua
(iii) Lahaja
Huyuno
Mauko
Nitakupiku
Nduli
Maozi
Kuwangia
(iv) kikale
Tezea
Huyuno
Mauko
Nitakupiku
Kuwaingia
Maozi
(iv) Tabdila
Twala twaa
Inkisari – taacha 1x3
(h) Umuhimu wa maswali ya balagha
Kuleta msisitizo wa ujumbe unaoangaziwa
Kumfanyia tashtiti mwanaume kwa yale anayotenda
Kumzindua mwanamume aweze kutekeleza majukumu yake ya ndoa 1x2
(i) Wewe mjeuri uliniahidi ungemtunza mtoto wangu na ungeishi naye daima mapenzi ya dhati lakini
ulimwingiza kwenye mapenzi ya hila kwa kumpeleka disko. Kwa nini unamchezea shere mwanangu
kwa kumliza = 1x4
Read More
0 Comments
SWALI NA JIBU LA USHAIRI MODEL15012023001
15/1/2023
0 Comments
6/25
Tena adili usawa, mgao rasilimali,
Bajeti inapogawa, isawazishe ratili,
Idara zilizoundwa, faidi kila mahali,
Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.
MASWALI
( a) Shairi hili ni la aina gani? Toa sababu (al 2)
(b)
(i) Onyesha aina mbili za uhuru wa kishairi uliotumiwa katika shairi hili (al 2)
(ii) Bainisha umuhimu wa uhuru wa kishairi uliotaja hapo juu (i) (al 2)
(c) Bainisha kipengele kifuatacho cha kimtindo katika shairi hili (al 1)
Usambamba
(d) Eleza toni ya shairi hili. (al 1)
(e) Bainisha nafsineni katika shairi hili (al 1)
(f) Ainisha shairi hili kulingana na:-
(i) Mpangilio wa vina
(ii) Idadi ya vipande katika ubeti (al 2)
(g) Changanua muundo wa ubeti wa nne. (al 3)
(h) Eleza aina mbili za urudiaji katika shairi hili (al 2)
(i) Andika ubeti wa pili kwa lugha nathari. (al 4)
MAJIBU
(a) Tarbia. Lina mishororo mine katika kila ubeti (al 2)
(b
(1) Aina mbili za uhuru wa kishairi
(i) Inkisari – nachoelezea - ninachoelezea
(ii) Kuboronga sarufi
- ya ziada kazi – kazi ya ziada
- wa kila mtu mwende – mwende wa kila mtu
(iii) Tabdila – kusaidiya – kusaidia
patiya – patia
achiya – achia
(iv) Mazida: maali - mali
Muwendo – mwendo 1x2
(b
(2) Umuhimu wa uhuru wa kishairi uliotajwa hapo juu.
(i) Inkisari – kupata urari wa mizani
(ii) Kuboronga sarufi – kupata urari wa vina
(iii) Kuboronga – kuleta mahadhi katika shairi
(iv) Tabdila – kupata urari wa mizani
(v) Mazida – kupata urari wa mizani
(c ) Usambamba
(i) Taifa sio taifa
(ii) Pasi kuwa maadili 1x1
(d) himiza/ nasihi / shawishi = 1x1
(e) mwananchi / raia / mzalendo / mkereketwa =1x1
7/25
(f) kuanisha shairi kulingana na:
(i) mpangilio wa vina
Ukaraguni.
(ii) Idadi ya vipande katika ubeti
Mathnawi 1x2
(g) Muundo wa ubeti wan ne.
(i) Vina vya kati ni ‘a’ na vya nje ni ‘ki’
(ii) Mizani ni kumi na sita katika kila mshororo
(iii) Vipande ni viwili, ukwapi na tao
(iv) Mishororo ni minne
(v) Kibwagizo ni taifa si taifa, pasi kuwa maadili 1x3
(h) Aina mbili za urudiaji
(i) Neno – mf taifa, maadili
(ii) Sauti – mf u, a
(iii) Silabi – mf nde, a, li, ngo
(iv) Sentensi / mshororo – taifa sio taifa, pasi kuwa maadili. 1x2
(i) Ninaanza kwa kuwaelezea kuwa tuwe wazalendo na matendo yetu yaonyeshe tunailinda nchi yetu
kwa mienendo mizuri kwa sababu nchi haikamiliki bila kuwa na matendo mema
Read More
0 Comments
SOMA SHAIRI LIFUATALO KISHA UJIBU MASWALI MODEL25122022001
25/12/2022
0 Comments
8/25
i uwanja wa malofa, lofa mtu mwenye tabu
N
Kusema sana kashifa na moyo kisebusebu
Tunakaribia kuja, kwa kushindwa kujimudu
Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.
maswali
(a) Lipe shairi hili anwani ifaayo. (alama 1)
Ulimwengu ni kiwanja
Changamoto ulimwenguni 1 x 1 = alama 1
(b) kwa kutoa mfano, eleza mbinu zozote mbili za lugha zilizotumika katika
shairi.(alama 2)
(b) Istiara/ jazanda – ulimwengu ni kiwanja
Msemo – kutwa kuchwa
Ukinzani/tanakuzi – wenye raha na tabu
Uhuishaji – Kichwa kudanganya shingo (zozote 2x1 = alama 2)
9/25
(i) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi.(alama2)
(i) Malofa:
(ii) Udubu:
( i) Malofa – maskini
(ii) Ndubu – upumbavu (alama 2)
Read More
0 Comments
Soma shairi kisha ujibu maswali MODEL23122022002
23/12/2022
0 Comments
MASWALI
A) Dhamira ya matunzi wa shairi hili ni gani? (Al 2)
B) Bainisha nafsineni katika shairi hili (Al 2)
C) Eleza toni ya shairi hili (Al 2)
D) Changanua muundo wa shairi hili (Al 5)
E) Fafanua maana ya kibwagizo cha shairi hili (Al 2)
F) Eleza mbinu nne ambazo mshairi ametumia kutosheleza mahitaji ya kiarudhi (Al 4)
G) Bainisha bahari ya shairi hili (Al 3)
MONGOZO / MAJIBU
) Dhamira ya mtunzi wa shairi hili ni gani?
a
Kuhimiza watu kutendea wenzao mema wakiwa wangali hai
10/25
) Changanua muundo wa shairi hili
d
i) Lina ubeti 5
ii) Kila ubeti una mishororo minne
iii) Kila mshororo una vipande viwili isipokuwa ubeti wa tano , mshororo wa pili wenye vipande vitatu
iv) Vina vya ndani na vya nje vinabadilika katika ubeti
v) Lina kibwagizo – Nizike ningali hai, n’kifa hutonizika
vi) Kila mshororo una mizani 16
ii) Lahaja
Matozi – machozi
siate – siache
iii)Tabdila
hutonizika – hutanizika
zisipumua – zisipumue
iv) Inkisari
takuwa – nitakuwa
singojee - usingojee
0 Comments
Soma shairi kisha ujibu maswali model23122022001
23/12/2022
0 Comments
11/25
Jana awile jasiri!
MASWALI
afanua ujumbe wa shairi hili (Al 2)
F
a) Eleza muundo wa shairi hili (Al 5)
b) Eleza toni ya shairi hili (Al 2)
c) Ainisha shairi hili kwa kuzingatia (Al 3)
i) Ruwaza ya mistari
ii) Ruwaza ya vipande
iii) Ruwaza ya mizani
d) Eleza mbinu nne ambazo mshairi ametumia kutosheleza mahitaji ya kiarudhi (Al 4)
e) Bainisha sifa mbili za anayezungumziwa katika shairi hili (Al 2)
f) Eleza tamathali mbili za usemi zilizotumiwa katika shairi hili (Al 2)
MWONGOZO / MAJIBU
) Fafanua ujumbe wa shairi hili
a
Shairi linazungumzia jinsi walio na nguvu wasivyowazia walio chini yao na kuwahimiza watu kuzinduka na
kupunguza kelele pamoja na kujishaua
12/25
Read More
0 Comments
YALIMWAGIKA
21/12/2022
0 Comments
YALIMWAGIKA
Lilianza kama wazo, nikawaza,
Niwe na watoto,
Si vikwazo, ghafla mama yao akapatikana,
Kwa rutuba yake,
Akavimba
Kumbe ni mapacha,
furaha!
Majina walishapewa,
Imani kudumu, watazaliwa,
Tungo wakatungiwa,
Amani na Imani,
Baba yao ni malenga
Anatayeita maneno.
Maneno yanaitika.
Nikasubiri.
MASWALI
13/25
a) Eleza jinsi usimulizi ulivyotumika kwenye shairi. (alama 1)
b) Eleza sifa tatu zinazoafiki shairi hili kuwa huru. (alama 3)
c) Shairi hili ni la tanzia. Thibitisha. (alama 1)
d) Tambua mandhari ta tanzia. (alama 1)
e) Tambua nafsineni kwenye ubeti wa kwanza. (alama 1)
f) Eleza toni ya shairi. (alama 2)
g) Onyesha mifano miwili ya matumizi ya sadfa katika shairi. (alama 3)
h) Andika ubeti wa mwisho kwa lugha tutumbi. (alama 4)
i) Eleza maana ya msamiati huu kulingana na shairi. (alama 4)
i.Vijulanga
ii.Susu
iii. Akavimba
iv ..Kiwimbo
YALIMWAGIKA MWONGOZO
).Eleza jinsi usimulizi ulivyotumika kwenye shairi.
A
Ushairi umesimulia safari kabla ya ndoa na katika ndoa.
Read More
0 Comments
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali MODEL21122022001
21/12/2022
0 Comments
14/25
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
Hizi bombo mwaanika, wa ndizini nashtuka,
Peupe mwazianika, kwenye jua kukauka,
Zingine zimeraruka, aibu zinatufika,
Anikeni kwa kuficha, za ndani mkisafisha.
MASWALI
a) Pendekeza kichwa mwafaka katika shairi hili. (alama 1)
b) Eleza toni ya shairi hili. (alama 1)
c) Tambua nafsineni katika shairi. (alama 1)
d) Jadili matumizi ya mitindo ifuatayo ya lugha katika shairi hili.
i. Kinaya (alama 2)
ii. Usambamba (alama 2)
iii. Balagha (alama 1)
e) Onyesha kuwepo kwa uhuru ufuatao katika shairi. (alama 3)
i. Tabdila
ii. Kubananga sarufi
iii. Inkisari
f) Andika ubeti wa mwisho kwa lugha mjazo. (alama 4)
g) Eleza muundo wa shairi hili. (alama 5)
MWONGOZO
1. Pendekeza kichwa mwafaka.
Aibu, Aibu kwetu
15/25
5. Andika ubeti wa mwisho kwa lugha ya mjazo/Nathari.
Mshairi anasema kuwa nguo za ndani zinazoanikwa ovyo/popote,watoto/wana huzipata na kutembea
nazo hata mezani kwa wageni.Hili huleta aibu kubwa na hivyo hushauri watu waanike kwa tahadhari.
Read More
0 Comments
USHAIRI MASWALI NA MAJIBU MODEL16122022002
16/12/2022
0 Comments
a inavyoelezea,katiba ni kielezi,
N
Tutii kwa mazoea, hadi kijacho kizazi,
Kwa hayo nitamwachia, hiyo ya ziada kazi,
Taifa sio taifa, pasi kuwa maadili.
maswali
) Eleza mambo yoyote manne ambayo mshairi anashauri taifa lifanye ili kuwa
a
na maadili. (alama 4)
a) Eleza mambo yoyote manne ambayo mshairi anashauri taifa lifanye ili kuwa na maadili. (alama
4)
16/25
1. Kuwa wazalendo/kuipenda nchi yao
2. Kuwa na umoja/ kuacha ukabila
3. Kuwa na mgao sawa wa raslimali
4. Kuacha tama
5. Kukomesha uhalifu
6. Kuacha maringo
7. Kutii katiba
8. Kuacha ubinafsi na kusaidiana. Zozote 4x1
b) Eleza mtindo wowote ule uliotumika katika shairi hili. (alama 2)
a) Eleza mtindo wowote ule uliotumika katika shairi hili. (alama 2)
Msemo – nipe masikioni- nipe sikio
Jazanda / istiari- kawa upinde
Takriri – kawa mpinde
Tashbihi – kama mtu mswahili
Utohozi – demokrasia, bajeti. Zozote 2x1
Aina =1 2x2 =4
Umuhimu =1
g) Andika ubeti wa pili kwa lugha tutumbi. (alama 4)
aanza kwa kueleza uzalendo kwamba tuipende nchi yetu. Matendo yetu yaonyeshe kuwa tunaipenda
N
nchi yetu.Tabia ya kila mtu ionyeshe msimamo . Nchi haikamiliki bila ya kuwa na matendo mema. 4x1=4
Read More
0 Comments
SIPENDI KUCHEKA - USHAIRI MASWALI NA MAJIBU MODEL16122022001
16/12/2022
0 Comments
SIPENDI KUCHEKA
17/25
ana jambo nanatukiya, kwangu hilo ni muhali
P
Kitenda naona haya, kujishusha yangu hali
Sipendi unipe hidaya, sipendi kutenda hili
Sipendi mimi kucheka
maswali na majibu
a) Hili ni shairi la aina gani? Thibitisha jibu lako kwa kutaja mifano miwili.
(alama 3)
Shairi huru
Hakuna urari wa vina
Vipande vinatofautiana
Idadi ya mishororo inatofautiana
Mizani haijitoshelezi.
18/25
shairi anasema hapendi maskini akiteswa na mayatimakunyanyaswa naye mnyonge akinyonywa. Hata
M
ikiwa anayewanyanyasa ana nguvu, anajua kuwa hili halitamtikisa
Read More
0 Comments
USHAIRI MASWALI NA MAJIBU MODEL14122022003
14/12/2022
0 Comments
imi
M
Siondoki
Siondoki siondoki
Niondoke hapa kwangu!
Kwa mateke hata na mikuki
Marungu na bunduki, siondoki
apa
H
Siondoki
Mimi ni Pahame!
Niondoke hapa kwangu!
Fujo na ghasia zikizuka
Na kani ya waporaji, siondoki
aki
H
Siondoki
Kwangu siondoki
Niondoke hapa kwangu!
Nawaje; waje wanaokuja
Mabepari wadhalimu, siondoki
amwe
K
Siondoki
Ng’oo hapa kwangu!
Katizame chini mti ule!
Walizikwa babu zangu, siondoki
endi
S
Nende wapi?
Si hapa kitovu changu
Niondoke hapa kwangu
Wangawa na vijikaratasi
Si kwamba hapa si kwangu, siondoki
atu
K
Siondoki
Sihitaji karatasi
19/25
Niondoke hapa kwangu
Yangu mimi ni ardhi hii
Wala si makaratasi, siondoki
Maswali
a) Shairi hili ni la aina gani? Kwa nini (alama 2)
b) Taja masaibu anayopitia mzungumzaji (alama 4)
c) Eleza toni ya shairi hili (alama 2)
d) Eleza muundo wa shairi hili (alama 3)
e) Tambua matumizi ya mbinu ya usambamba (alama 2)
f) Andika ubeti wa tano kwa lugha nathari (alama 4)
g) Tambua idhini moja ya mtunzi (alama 1)
h) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika shairi (alama 3)
(i) Karatasi
(ii) Nimesaki
(iii)kitovu
majibu / mwongozo
. - Ni shairi huru kwa sababu mshairi ametumia (i) mishata mf. katu, eti, niondoke
a
- Shairi lina umbo la paa la nyumba
- Matumizi ya alama za uakifishaji kwa wingi (al. 2)
c . (i) Huzuni
(ii) Ujasiri (2 x 1)
(iii) Uchungu
f. Mshairi anasema kamwe hatoki kwake. Anaashiria chini ya mti waliozikwa babu zake na kusisitiza
kwamba hawezi akaondoka (al. 3)
g. Inkisari –
(i) Sendi – Siendi Nende wapi – Niende wapi
(ii) Kuboroga sarufi mf yangu mimi ni ardhi hii – Ardhi hii ni yangu mimi (1 x 1)
Read More
0 Comments
USHAIRI MASWALI NA MAJIBU MODEL13122022002
13/12/2022
0 Comments
20/25
Huketi mahali tuli, nikaaza peke yangu
Na niazalo ni hili, lililo moyoni mwangu
Naifikiri ajali, siku ya kunyoka kwangu
Naliliya roho yangu, itakufa iyondoke
Maswali
(a) Kwa kuzingatia vina taja bahari ya shairi hili. (alama 1)
Ukara (1x1=1)
(b) Orodhesha mifano ya uhuru wa kishairi iliyotumika na sababu zake. (alama 3)
● Lahaja
Nikaaza – nikawaza (kudhirisha ubingwa / asili / usuli/utamu/ladha
● Tabdila/tafsida
Naliliya – nalilia
(kudumisha mdundo/mapigo ya kisauti / ainisha mapigo)
● Inksari
Niwepuke – niwaepuke
(kudumisha urari wa mizani)
● Kufinyanga lugha kisarufi
Nikisha sanda kutiwa – Nikisha kutiwa sanda.
(kudumisha urari wa vina)
*Mwalimu atathmini jibu la mwanafunzi [3 x 1 = 3]
(c) Shairi hili linajitosheleza. Thibitisha kwa kutolea mifano mitatu. (alama 3)
[shairi hujitosheleza kimaana na kimuundo]
(i) Kimaana – ujumbe kwamba nafsineni analilia roo yake siku atakapokufa umejitokeza wazi katika shairi
lote. Kila ubeti wajenga maana hiyo.Ninaililia roho yangu itakapotengana nami baada ya kufa/kifo
change. (4 x 1 = 4)
(ii) Kimuundo; kila kipengee ni hoja.
Kuna urari wa:
● Vina katika ubeti (kivyake)
● Mizani 8:8
● Mishororo minne minne katika kila ubeti
● Vipande: ukwapi na utao (2 x 1= 2)
(d) Andika ya ubeti wa kwanza kwa lugha nathari. (alama 2)
Huwa ninakaa pahali peke yangu na kuwaza.
Kile ninachofikiria kimo moyoni mwangu. Jambo ambalo huwa ninafikiria juu
yake ni kuhusu siku ya kufariki kwangu(bila kutarajiwa / kupangia). [2 x 1 = 2)
(e) Changanua vipengele vya kimtindo vyovyote vitatu katika utungo huu. (alama 3)
(i) Jazanda:
Siku ya kunyoka – siku ya kifo
(ii) Uzungumzi nafsia.
Matumizi ya nafsi ya kwanza: Huketi mahali tuli, nikaaza peke yangu.
(iii) Tashihisi /uhaishaji/uhuishi
Sanda ikisha waswili itakufa iyondoke.
(iv) Mjalizo [ni matumizi kuleta msisitizo sina langu wala changu, [kama nipe nikupe, nishike nikushike]
Sina langu sina changu
(v) Takriri
Sawa sawa
Kibwagizo
21/25
Silabi
(vi) Utohozi
Wanikafini – put in coffin
(3 x 1 = 3)
(f) Dhihirisha matumizi ya taswira. (alama 3)
(i) Taswira Mwendo
wende nami sawa sawa, hadi baiti ya M’ngu / sanda ikisha waswili.
(ii) Taswira oni.
Huketi mahali tuli, nikaaza peke yangu.
(iii) Mguso
Wanitakase muwili
Nitiwe kwa kupokewa, na mikono…..
(iv) Taswira hisi
Naililia roho yangu
Wanitakase muwili
(3 x 1 = 3)
(g) Tolea mifano mitatu ya takriri zilizotumika. (alama 3)
(i) Maana
Nitiwe kwa kupokewa, na mikono ya wenzangu
(ii) fungu la maneno / mshororo
Nalilia roho yangu, itakufa iyondoke
(iii) Takriri silabi
na - naliliya
- naililiya
- naifikiri nk
Takriri ya vina vya mwisho na kati
(iv) Takriri ya neno:
M’ngu
Sanda
Sawa sawa
(3 x 1 = 3)
Read More
0 Comments
USHAIRI MASWALI NA MAJIBU MODEL13122022001
13/12/2022
0 Comments
napotembea anasikiliza
A
Videge vya anga vinavyotumbuiza
Utadhani huwa vimemngojea
Kwa usiku kucha kuja kumwimbia;
Pia pepo baridi kumpepea
Rihi ya maua zikimletea
Nao umande kumbusu miguu;
Na miti yote hujipinda migongo
Kumpapasa, kumtoa matongo;
Na yeye kuendelea kwa furaha
Kuliko yeyote ninayemjua
Akichekelea ha hahaha ha….
22/25
Na mimi kubaki kujiuliza
Kuna siri gani inayomliwaza?
Au nikujua au kutojua?
Furaha ya mtu nifuraha gani
Katika dunia inayomhini?
Ukali wa jua wamnyima zao
Soko la dunia la mkaba koo;
Dini za kudhani zamsonga roho
Ayalimia matumbo ya waroho;
Kuna jambo gani linamridhisha?
Kama sikujua ni kutokujua
Laiti angalijua, laitia ngalijua!.
(T. Arege)
MASWALI.
a) Eleza hali ya mzungumziwa katika shairi hili. (alama.4)
b) Huku ukitoa mifano, onyesha aina mbili za uhuru wa kishairi uliotumiwa katika shairi hili. (alama.2)
c) Fafanua aina mbili za taswira ukirejelea ubeti wa pili. (alama.2)
d) Maswali ya balagha katika shairi hili yanasisitiza maudhui yapi? (alama.2)
e) Bainisha vipengele viwili vya kimtindo katika shairi hili. (alama.2)
f) Bainisha aina mbili za urudiaji zilizotumiwa katika shairi hili. (alama.2)
g) Eleza toni ya shairi hili. (alama.2)
h) Bainisha nafsineni katika shairi hili. (alama.1)
i) Eleza muundo wa shairi hili. (alama.3)
MWONGOZO WA USHAIRI.
)i) Mwenyetumaini /tamaa – kubwahamu
a
ii) Mwenyebidii- alfajirina,mapema, kutokwanajasho.
iii) Anayefurahiamandhari – anapotembeaanasikilizavidege….
iv) Mtulivu- kunasiriganiinayomliwaza?
v) Aliyedhulumiwa – soko la dunialamkabakoo.
vii) Aliyeridhika- kunajambogani? (2x2=2)
23/25
iii)
Kilamshororounakipandekimojaisipokuwaubetiwapilimshororowatisanamshororowamwishoubetiwamwisho.
iv) Shairihalinampangiliomaalumwavina
v) Idadiyamizanikatikamishororoinatofautiana. (3x1)
Read More
0 Comments
USHAIRI MASWALI NA MAJIBU MODELI 2362021544
23/6/2021
0 Comments
USHAIRI
Eti
Mimi niondoke hapa
Niondoke hapa kwangu
Nimesaki, licha ya risasi
Vitisho na mauaji, siondoki
Mimi
Siondoki
Siondoki siondoki
Niondoke hapa kwangu!
Kwa mateke hata na mikuki
Marungu na bunduki, siondoki
Hapa
Siondoki
Mimi ni Pahame!
Niondoke hapa kwangu!
Fujo na ghasia zikizuka
Na kani ya waporaji, siondoki
Haki
Siondoki
Kwangu siondoki
Niondoke hapa kwangu!
Nawaje; waje wanaokuja
Mabepari wadhalimu, siondoki
Kamwe
Siondoki
Ng’oo hapa kwangu!
Katizame chini mti ule!
Walizikwa babu zangu, siondoki
Sendi
Nende wapi?
Si hapa kitovu changu
Niondoke hapa kwangu
Wangawa na vijikaratasi
Si kwamba hapa si kwangu, siondoki
Katu
Siondoki
Sihitaji karatasi
Niondoke hapa kwangu
Yangu mimi ni ardhi hii
Wala si makaratasi, siondoki
Maswali
a) Shairi hili ni la aina gani? Kwa nini (alama 2)
b) Taja masaibu anayopitia mzungumzaji (alama 4)
24/25
c) Eleza toni ya shairi hili (alama 2)
d) Eleza muundo wa shairi hili (alama 3)
e) Tambua matumizi ya mbinu ya usambamba (alama 2)
f) Andika ubeti wa tano kwa lugha nathari (alama 4)
g) Tambua idhini moja ya mtunzi (alama 1)
h) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika shairi (alama 3)
(i) Karatasi
(ii) Nimesaki
(iii)kitovu
(al. 3 x 1)
TUMA KWA PRINTA
Read More
0 Comments
25/25