You are on page 1of 3

1) Uhalisia Wa Kijamaa

Hii ni mbinu ya utunzi na uhakiki inayomzingatia binadamu kama uti wa mgongo wa kuwepo
kwa ulimwengu na maana ya ulimwengu ule, hii ni dhana ya njogu na wafula (2007). Kwa
ujumla tunaweza sema kwamba uhalisia wa kijamaa ni nadharia ya uhakiki ianyozingatia
maendeleo ya jamii na maendeleo ya kitabaka ,vilevile nadharia hii huonyesha jinsi uhusiano
kati ya tabaka la mabwenyenye na wachochole huleta mgongano unaosababisha kutokea kwa
mapinduzi . mapinduzi haya huwa ni juhudi na mikakati za wanajamii kupambana na
ukandamizaji wa kilimwengu.

Mihimili yake

Huwa na wahusika wa kimaendeleo na wa kimapinduzi. Hawa ni wahusika wanaonuia kuipindua


na kuibadilisha hali ya maisha . ni wahusika wenye nia ya kumiliki njia kuu za kuzalisha mali
katika jamii yao. Kwa mfano katika riwaya ya kidagaa kimemwozea tunamwona mhusika Amani
vile anavyong’ang’ana na kuhakikisha kuwa Mtemi Nasaba Bora ambaye alikuwa katili na
mfisadi ameondolewa kwenye mamlaka. Kwa hivyo katika riwaya hii, Amani amewekwa kama
mwana mapinduzi na mwanamaendeleo. Katika tamthilia ya kilio cha haki mhusika Lanina
anafanya jitihada zote kuhakikisha kuwa wafanyakazi wengine wachochole kama yeye
wanalipwa vizuri na kwa hivyo anashirikiana na wanamapinduzi wengine kama Dewe na Musa
kumung’oa Delamon.

Husawiri matukio kihistoria ,hutekeleza matendo ya kitabaka. Hufanya hivi kimakusudi au bila
fahamu ,la mno kwao ni kwamba tabaka la wanyonge linajiimarisha ili kujipa mamlaka na nguvu
za kiuchumi ,kwa mfano hata kama Amani na Imani wanateseka kwa muda mrefu katika utawala
wa kidikteta wa Mtemi Nasaba pamoja na wanasokomoko wengi wanajifunga kibwebwe
kukabiliana na hali hiyo na mwishowe wanakuwa washindi.

Uhalisia wa kijamaa huzingatia maslahi ya makabwela . hawa ni fukara wa ulimwengu wenye


nia ya kuimarisha udikteta wa makabwela. Maslahi ya walalahoi huzingatiwa sana kwa kuwa
wahusika wengi kwenye kazi za kifasihi ambazo zinatilia mkazo nadharia ya uhalisia wa
kijamaa. Katika riwya ya kidagaa kimemwonzea tunawaona vile wahusika kama Imani na
Amani wanavyokosa maslahi ya kimsingi kama vile chakula ,lishe bora na nguo za kuvaa.
Amani na Imani wametumiwa na Walibora kuonyesha mashida ambayo yalikuwa
yanawakumba makabwela wa nchi ya Sokomoko. Tunamwona kaburu mmoja wa kiafrika kwa
jina Mtemi Nasaba Bora vile anavyoishi maisha ya raha mustarehe kwa sababu ya kula jasho la
wachochole na pia kuwatumia ili kujizalishia mali. Pia katika tamthilia ya kilio cha haki
tunamwona Delamon vile anavyowatumia wafanyakazi wan chi ile ile kujitajirisha.

Matukio mengi ambayo yanatendeka katika nadharia ya uhalisia wa jamaa yanawahusu


wahusika kitabaka.Wahusika katika nadharia hii uwa wamejigawa katika makundi mawili
ambayo ni kundi au tabaka la juu ambalo ni la matajiri na tabaka la chini ambalo ni la
wachochole. Tabaka la juu ndilo hunyayanyasa tabaka la chini ambalo ni lala walalahoi. Katika
riwaya ya kidagaa kimemwozea tunamwona Mtemi Nasaba Bora na nduguye mwalimu Majisifu
wanavyoishi masha ya juu ilhalii watu kama Amani ,Imani na akina Matuko Weye wanavyoishi
maisha ya kutatanisha na ya hali duni. Tabaka la juu ambalo ni la akina Mtemi Nasaba linapata
kila kitu linaloitaji ilhali tabaka la chini la wanasokomoko hawapati hata vitu vya kimsingi katika
jamii.

Huonyesha matumaini ya kupatikana kwa ushindi baada ya dhiki kuu ya kupigania ukombozi.
Huonyesha kuwa ambaye anakandamizwa yaani mchochole mwishowe huishia kuwa ndiye
mshindi kwenye vita vya ukombozi. Katika tamthilia ya kilio cha haki kundi ambalo
linaongozwa na akina Lanina Musa Na Dewe ndilo linaloshida na katika mwisho wa tamthilia
tunadokezwa vile kaburu Delamon pamoja na wasaliti na vibarakala wake kama Tekeri,Shindo
Na Matovu wanavyouawa.Katika tamthilia ya mstahiki Meya vilevile tunamwona mstahiki meya
pamoja na wanyonyaji wenzake wanavyoshindwa na kundi la wachochole ambalo lilikuwa
limeongozwa na daktari Ziki.

Nadharia ya uhalisia wa kijamaa huelezea hadithi kikweli. Nadharia hiii hueleezea changamoto
zinazomkumba mwanadamu katika harakati zake za maisha. Nadharia hii huonyesha vile
wanajamii huusiana na wenzao ,kwa mfano katika tamthilia ya mstahiki Meya tunaelewa kuwa
katka jamii yetu ama nchi yetu, viongozi wengi wamejitumbukiza kwa siasa chafu za
kuwadhulumu wananchi waliowachagau. Mstahki meya ni mhusika ambaye amewekwa pale
kuonyesha vile viongozi wa nchi za kiafrika ni wafisadi na uwa wanatumia mamlaka yao
kuijinyakulia mali yasiyo halali ,vilevile katika riwaya ya kichwamaji inaonyesha vile jamii zetu
ama nchi zetu zinavyokandamizwa na viongozi wabaya wa serikali kwa mfano tunamwona
Manase akitumia mamlaka yake vibaya kupeana kazi katika afisi yake ya mkuu wa wilaya.

Lugha inayotumiwa na nadharia ya uhalisia wa kijamaa uwa lugha inayoeleweka na wanajamii


ndiposa makabwela waelewe. Lugha hii uwa inaendeleza malengo na mapendekezo ya walio
wengi katika jamii. Wahusika wa kimapinduzi wanapaswa kutumia lugha rahisi inayoeleweka na
jamii ya umaskini anayoipigania.

You might also like