Professional Documents
Culture Documents
nusu.
Jesse, Jr, kwa mwavuli wa baba yake alifanikiwa kuwa mwanasiasa anayechanua
na akawa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi, akiwakilisha Chama cha Democrats,
Jimbo la Illinois 2nd District. Obama hajamkinga na jela!
William Jefferson alikuwa kigogo wa kisiasa nchini Marekani. Hivi sasa yupo jela,
akitumia kifungo cha miaka 13 jela, baada ya kukutwa na hatia ya kujihusisha na
vitendo vya rushwa.
Mwaka 2005 akiwa mjumbe wa Baraza la Wawakilishi, Jimbo la Louisiana 2nd
District, alikutwa nyumbani kwake na dola 90,000, shilingi milioni 117 kwa chenji
ya wakati huo. Fedha hizo Jefferson, maarufu kama Bill Jefferson alikuwa
amezificha kwenye friji.
Unaweza kujiuliza ni wangapi leo hii wanakaa nyumbani kwao na fedha nyingi
kiasi hicho hapa nchini. Kuna wanaoishi nyumbani kwao na mabilioni ya shilingi
bila wasiwasi wowote. Hii ndiyo Tanzania!
Marekani, mwanasiasa mkubwa alipokutwa na shilingi milioni 117 moto
ulimuwakia. Umaarufu wake ulipungua, na tangu mwaka 2012 yupo anatumikia
kifungo jela.
Hapa kwetu, yupo ambaye alibainika kuhifadhi shilingi bilioni moja Jersey,
Uingereza, alipoulizwa, alijibu: Hivyo vijisenti tu! Hajawahi kufanywa chochote
tangu mwaka 2008 alipobainika na alipojibu hivyo.
Yupo ambaye amekuwa akizungumzwa kuwa alifanya hamisho kubwa la fedha
kwenye akaunti za nje, tangu mwaka jana kabla ya Uchaguzi Mkuu, mpaka leo
hajawahi kuitwa hata mara moja kuulizwa, uhalali wa miamala aliyofanya.
Taarifa ya Taasisi ya Kudhibiti na Kupambana na Rushwa (Takukuru) pamoja na ile
ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kisha kuthibitishwa na
Bunge la 10, Novemba 2014, iliezwa kuwa ipo miamala ilihamishwa kwa magunia,
masandarusi, lumbesa na viroba Benki ya Stanbic.
Magunia ya fedha, wapi yalipelekwa? Kama siyo kwenye nyumba za watu?
Inaelezwa mgao ulikuwa shilingi bilioni 70. Je, hakuna waliokwenda kuficha
kwenye uvungu wa vitanda vyao noti za mabilioni?
Nakumbusha, Jefferson aliponzwa na shilingi milioni 117 tu, hapa kwetu, watu na
mabilioni yasiyo na maelezo wala hawachukuliwi hatua.
Andrew Theophanous alikuwa kigogo katika Baraza la Wawakilishi nchini
Australia. Makosa ya rushwa yalimpeleka jela miaka sita, na maisha ya kisiasa
yalikoma mwaka 2002 baada ya hukumu. Wenzetu wamezoea, sisi bado sana.
Inapozungumzwa hoja kuhusu Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter
Muhongo ni kwa sababu suala lake lake la kashfa ya Tegeta Escrow halijafungwa.
Wapo watu wanajaribu kusema kuwa Muhongo alipojiuzulu ilitosha, kweli? Mtu
ambaye ndiye kitovu cha wizi mkubwa kufanyika, zaidi ya shilingi bilioni 300,
zikachotwa kihuni, eti siyo jambo zito hilo.
Inavyoonekana ni kwamba Jefferson angepata kashfa hiyo akiwa Tanzania, leo hii
asingekuwa jela. Hata kuziona fedha hizo, nani angethubutu kwenda kumkagua?
Blagojevich kwa Tanzania asingefungwa, tena angekuwa anaendelea kuula
serikalini.
Wakati James Rugemalira anaendelea kudunda, ugawaji wake wa fedha, ni zaidi
ya ule wa mtu wa kati (lobbyist), Jack Abramoff, aliyetikisa Serikali ya Marekani
katika kashfa ya Jack Abramoff CNMI.
Bob Ney, akiwa mjumbe wa Baraza la Wawakilishi, Jimbo la Ohio, kwa Chama cha
Republican, alibainika kupewa fedha na Abramoff, papo hapo ukaibuliwa
uchunguzi wenye maswali mengi, wamepeana fedha za nini?
Hakukuwa na kitu zaidi ya rushwa! Abramoff na Ney, wote walihukumiwa kwenda
jela, miezi 30. Yaani miaka miwili na nusu.
Sisi huku Rugemalira aligawa fedha kama njugu, watu hawahoji. Wengine
wakasema ni za mboga.
Hivi karibuni, kuna maofisa wa serikali walishinda kesi mahakamani baada ya
kuonekana mashtaka dhidi yao hayana kichwa wala miguu.
Yaani unampeleka mtu mahakamani kwa tuhuma za rushwa. Mashtaka yako
yanasema alipewa rushwa na Lugemalira. Jaji, anauliza sasa mbona huyo mtoa
rushwa hamjamleta hapa?
Rushwa hujumuisha mtoaji na mpokeaji. Kama ambavyo Abramoff na Ney
walivyofungwa. Utani wa namna hii ni rahisi kupatikana Tanzania peke yake.
Hivyo, hapa kwetu bado hakujawa na mazoea ya kuwajibishana, ndiyo maana
adhabu hii ya Mramba na Yona naona ina maana kubwa, pengine kuliko
walivyokuwa wanaitumikia gerezani. Nitaeleza!
Lipo kundi kubwa linalalamika kuwa adhabu ni ndogo kuliko kosa. Wanahoji iweje
mfungwa wa kuku afungwe miaka 10, aliyeisababishia serikali hasara ya mabilioni
apewe kifungo cha nje? Ni haki yao kutoa maoni. Nchi huru hii!
Hata hivyo, wote wenye kutoa maoni hayo hawajui maana ya adhabu
wanayoitumikia Mramba na Yona kwa sasa.
Watu hawaadhibiwi kwa lengo la kukomoana tu, bali pia kupitisha mafunzo kwa
jamii ili itambue kuwa kuna malipo ya gharama baada ya kutenda makosa.
Mtoto aliyewaona Mramba na Yona, anapata picha kuwa kumbe nchi inaongozwa
kwa sheria. Ukifanya makosa baadaye lazima utalipia gharama kwa mujibu wa
sheria za nchi. Hii inafundisha zaidi.
Watu ambao wanalingana na babu yake, wanabebeshwa mafagio, chepe na ndoo
za kupigia deki kwa ajili ya kufanikisha usafi, kisha anatambua wanasota kwa