You are on page 1of 343

SECRET

SOCIETY
(JAMII YA SIRI)

SEASON 1
MTUNZI: PATRICK.CK

HADITHI HII NI MALI YA MWANDISHI NA HAKI ZOTE


ZIMEHIFADHIWA KWA HIYO HAIRUHUSIWI KUCHAPISHA,
AU KUITUMIA KWA NAMNA NYINGINE HADITHI HII BILA
RUHUSA YA MWANDISHI.HATUA KALI ITACHUKULIWA
KWA YEYOTE ATAKAYEKIUKA MASHARTI HAYA..
SIMULIZI NYINGINE ZA MTUNZI PATRICK.CK

SIMULIZI ZA MAPENZI
1.MISS TANZANIA
2.SERENA
3.BEFORE I DIE
4.BEYOND PAIN
SIMULIZI ZA UPELELEZI
5.PENIELA
6.QUEEN MONICA
7.THE FOOTBALL
8.I DIED TO SAVE PRESIDENT
9.KIAPO CHA JASUSI
10.KIKOSI CHA SIRI
11.SIRI
12.SCANDAL(KASHFA)
13.CAPTURE OR KILL MISSION
MAWASILIANO
0764294499
© 2020 Masimulizi.Haki zote zimehifadhiwa
DAR ES SALAAM
Tayari ni saa kumi na mbili
za jioni Mathew Mulumbi
alipowasili Nikita hotel moja ya
hoteli maarufu jijini Dar es
salaam.Alisimamisha gari katika
maegesho na kushuka akaelekea
ndani ya hoteli.Kabla hajaingia
ndani akasikia mbinja ikipigwa
akageuka na kumuona mtu
amekaa chini ya mwavuli
akatabasamu halafu akabadili
uelekeo akamfuata.Mtu Yule
ambaye umri wake ulipata miaka
hamsini hadi sitini alisimama na
kumpa mkono Mathew Mulumbi
“Karibu sana Mathew
Mulumbi” akasema Yule mzee
“Ahsante sana Profesa
Santala.Shikamoo”
“Marahaba
Mathew.Nimefurahi kukuona
tena.Nimuda mrefu hatujaonana”
akasema mzee Santala
“Ni kweli mzee majukumu
yamekuwa mengi” akajibu
Mathew.Muhudumu akafika mara
moja na kuwahudumia vinywaji
“Samahani sana Mathew
kama kwa namna yoyote ile
nitakuwa nimekusumbua kwa
kukuita hapa kwani nafahamu
wewe ni mtu mwenye mambo
mengi”
“Usijali mzee.Unapoitwa na
mtu kama wewe lazima uache
kila unachokifanya na kwenda
kusikiliza kitu ulichoitiwa”
akasema Mathew
“Nashukuru kwa
hilo.Mathew sitaki kuchukua
muda wako mwingi.Mathew
nimelazimika kukufuata mimi
mwenyewe kuzungumza nawe
.Kwa sasa niko
Arusha.Tumefungua chuo kipya
cha mafunzo ya ujasusi kilichopo
karibu na hifadhi ya Arusha.Nina
wanafunzi hamsini ambao
wanatarajiwa kumaliza mafunzo
ndani ya miezi mitatu ijayo.Vile
vile kuna wanafunzi wengine mia
moja na sabini wakiwa katika
ngazi mbali mbali za
mafunzo”akasema Profesa
Santala
“Hongereni sana kwa hatua
hii kubwa ya kuanzisha chuo cha
kuwafundisha vijana wetu ujasusi
hapa hapa nchini.Nakumbuka
enzi zetu tulikuwa tunakwenda
kujifunza nje ya nchi.Hii ni hatua
kubwa na ya kupongezwa sana”
akasema Mathew
“Ni kweli ni hatua
kubwa.Wanafunzi hao hamsini ni
darasa la kwanza kuhitimu katika
chuo hicho.Ninajisikia fahari
kuwa mkuu wa kwanza wa chuo
hicho” akasema mzee Santala na
kunywa kinywaji chake
“Mathew wanafunzi hao
hamsini wamefundishwa mambo
mengi sana na ninaweza kusema
wameiva ila kuna kitu kimoja
bado ninahitaji wakipate”
“Kitu gani mzee
Santala?Mathew akauliza
“Si somo rasmi ila nataka
vijana hawa wafundishwe nini
maana ya uzalendo wawapo
katika kazi hii ya ujasusi.Si
kwamba hawajafundishwa
uzalendo,wamefundishwa sana
lakini nahitaji wajifunze zaidi
kwa mifano hai.Mathew
nimekufuata kukuomba unisaidie
kuwapa elimu juu ya uzalendo
wanafunzi hawa.Wewe umekuwa
ni jasusi wa kutiliwia mfano
kabisa.Umeshiriki katika misheni
nyingi ndani na nje ya nchi kwa
mafanikio makubwa na hakuna
hata misheni moja ambayo
umewahi kushindwa.Mafanikio
yako yamesababishwa na kila
wakati kuitanguliza mbele
nchi.Hukuwahi kutanguliza
maslahi binafsi katika misheni
zako,kwako ni nchi kwanza”
akasema mzee Santala
“Mzee Santala” akasema
Mathe wna mzee Santala
akamfanya ishara asubiri kwanza
“Mathew nafahamu
unachotaka kukisema.Nafahamu
umejiweka pembeni na mambo ya
ujasusi na unajishughulisha na
biashara lakini bado unaweza
kuwa na msaada mkubwa kwa
taifa.Nataka vijana hawa
wajifunze kupitia kwako nini hasa
maana ya kujitoa kwa ajili ya taifa
lao kama ulivyofanya wewe.
Tafadhali Mathew naomba
usinikatalie katika hili jambo ni
muhimu sana.Tunataka
kutengeneza akina Mathew
Mulumbi wengine ili hata kama
ikitokea Mungu akakuita leo basi
tuwe na vijana wengine ambao
taifa linawategemea katika
ujasusi” akasema mzee Santala na
kumtazama Mathew ambaye
alitafakari kwa muda halafu
akauliza
“Ni muda gani ambao
unataka nikusaidie hilo jambo?
Mathew akauliza
“Wiki mbili zinatosha”
akajibu mzee Santala.Mathew
akafikiri tena kidogo halafu
akasema
“Mzee Santala wewe ni
mmoja wa watu ambao siwezi
kuwakatalia jambo na hasa
linapokuwa jambo lenye maslahi
makubwa kwa nchi kama hili
ulilolitaja.Tatizo sifahamu
nitaanzaje kuwafundisha vijana
hao hicho unachonitaka
nikawafundishe” akasema
Mathew
“Usihofu Mathew.Huna haja
ya kufanya
maandalizi.Unachotakiwa
kufanya ni kuwaeleza ukweli
mtupu ukiwapa mifano ya
misheni ambazo umewahi
kuzifanya nataka wapate picha
namna ya kulitanguliza taifa
mbele pale wawapo kazini au
katika misheni Fulani” akasema
mzee Santala
“Lini unataka nikaanze somo
hilo? Akauliza Mathew
“Jumatatu ijayo” akajibu
mzee Santala
“Nimekuelewa mzee.Leo ni
alhamisi nitafanya maandalizi
siku ya kesho na jumamosi
nitakuja Arusha ili siku ya
jumatatu nianze kazi hiyo”
akasema Mathew
“Nakushukuru sana Mathew
Mulumbi kwa kulikubali ombi
hili”
“Usijali mzee Santala.Tupo
kwa ajili ya taifa na pale
tunapohitajika kufanya jambo
Fulani lenye maslahi kwa taifa
basi hakuna kusita unatii mara
moja.Nitaweka mambo yangu
sawa siku ya kesho na jumamosi
nitakuja Arusha kama
nilivyokueleza” akasema Mathew
Walikuwa na mazungumzo
marefu na ilipotimu saa nne za
usiku wakaagana kila mmoja
akaondoka
“Nimelipokea ombi la
kufundisha vijana kwa mikono
miwili.Ni jambo jema sana kwani
lina maslahi makubwa.Taifa letu
linahitaji sana vijana wa kulilinda
lakini vijana hao lazima wawe
wamepikwa vilivyo wafahamu
thamani yao kw ataifa na wajue
nini wanapaswa kukifanya kwa
taifa lao.Kwa sasa tuko katika
mapambano ya uchumi na tunao
maadui wengi hivyo vijana hawa
lazima wafundwe kupambana
kwa ajili ya taifa lao” akawaza
Mathew Mulumbi akiwa garini
akielekea nyumbani kwake
ARUSHA
Saa mbili asubuhi siku ya
Jumatatu,Mathew Mulumbi
akawasili katika chuo cha ujasusi
kilichojengwa pembezoni mwa
hifadhi ya Arusha.Alipokewa na
profesa Santala
“Mathew Mulumbi karibu
sana katika chuo chetu” akasema
Profesa Santala na kisha
akamzungusha Mathew katika
chuo kile kumuonesha miundo
mbinu mbali mbali ya chuo
“Mnastahili pongezi Profesa
Santala.Chuo ni kizuri
sana.Hakina tofauti na vyuo
tulivyosoma nje ya nchi.Naamini
si muda mrefu wanafunzi kutoka
nchi nyingine barani Afrika
wataanza kuja hapa kujifunza
ujasusi.Hiki ni moja ya chuo bora
kabisa Afrika” akasema Mathew
halafu akaenda kutambulishwa
kwa wahadhiri wengine wa chuo
kile.
Hatimaye muda wa Mathew
kuingia darasani kufundisha
kipindi chake cha kwanza
ukawadia
“Mathew ondoa
hofu.Utaweza” akasema Profesa
Santala kisha akaongozana na
Mathew kuelekea katika darasa
analotakiwa kulifundisha.Profesa
Santala akawasalimu wanafunzi
halafu akawajulisha kuwa kuna
mgeni ambaye atakuwa nao kwa
muda wa wiki mbili
akiwafundisha somo maalum la
uzalendo kwa mifano.
“Anaitwa Mathew
Mulumbi.Yawezekana wengine
mmewahi kulisikia jina hilo basi
leo mmekutana naye ana kwa
ana.Huyu ni jasusi nguli na
atawaelekeza mambo mengi
ambayo mtakwenda kukutana
nayo katika kazi yenu na zaidi
sana uzalendo kwa nchi
yenu.Mtajiuliza kwa nini Mathew
Mulumbi awafundishe uzalendo
wakati mmekuwa mkifundishwa
tangu mlipoingia hapa chuoni?
Mtanijibu pale atakapokuwa
amemaliza kuwapeni
somo.Karibu Mathew” akasema
Profesa Santala na Mathew
akasogea ubaoni
“Kama alivyonitamblisha
Profesa Santala ninaitwa Mathew
Mulumbi.Kwa nusu ya umri
wangu nilionao sasa nimeifanya
kazi hii ya ujasusi hadi
nilipoamua kupumzika na
kuendelea na mambo mengine na
kwa sasa ninajishughulisha na
biashara japo kazi hii iko damuni
na ndiyo maana niko hapa mbele
yenu.Niliingia katika ujasusi
nikiwa bado kijana mdogo sana
na nilikuwa ndiye jasusi mdogo
zaidi kiumri katika shirika la
ujasusi Tanzania.Bado
naikumbuka simu niliyopigiwa
saa sita na dakika tano siku ya
jumanne na mtu aliyejitambulisha
kama mkaguzi wa polisi Damian
Mlanza akanitaka siku inayofuata
nisitoke nyumbani polisi watafika
kuna mambo wanataka kuja
kunihoji.Sikupata usingizi
nikakesha nikijiuliza nimefanya
nini hadi polisi
wanifuate?Nilijiuliza maswali
zaidi ya elfu moja na
kulipopambazuka nikawaeleza
walezi wangu wakanitaka
nikimbie lakini nikawaeleza
sintakimbia kwa kuwa sijafanya
kosa lolote na hakuna sheria ya
nchi niliyovunja.Nilibaki
nyumbani na kweli likafika gari la
polisi wakanichukua bila maelezo
yoyote nikaondoka nao
nikapelekwa kituo cha polisi na
pale nikaingizwa katika chumba
nikakutana na mzee mmoja
ambaye akajitambulisha kuwa
anatoka idara ya ujasusi na
akaniweka wazi kuwa nisihofu
hakuna kosa nililolifanya na
kwamba nimeshinda mtihani wa
kwanza wa kujiamini kwani
ingekuwa ni mtu mwingine
amepigiwa simu kuwa atafuatwa
na polisi na hajui amefanya kosa
gani angetoweka lakini mimi
nilijiamini sikufanya kosa
nikatulia.Huo ndio ulikuwa
mwanzo wangu wa kuingia katika
masuala ya ujasusi.Walipata
taarifa zangu na kuanza
kunifuatilia kwani nikiwa kidato
cha tano niliweza kuchunguza na
kuwabaini watu waliochoma
mabweni ya shule jirani.Vile vile
nikafanikiwa kuwapata watu
walioua mifugo ya shule yetu
hivyo nikaonekana ninafaa sana
katika mambo haya na baada ya
kumaliza kidato cha sita
wakanichukua.Huo ndio ulikuwa
mwanzo wa safari ndefu hadi
hapa nilipo sasa” NdivyoMathew
Mulumbi alivyoanza somo lake
Wakati Mathew Mulumbi
akifundisha,katika chumba cha
mikutano wahadhili walikuwa
kimya wakifuatilia katika runinga
kubwa kile alichokuwa
anakifundisha.Darasa lile lilikuwa
limeunganishwa na vifaa maalum
na mhadhili aliweza kufundisha
hata akiwa ofisini kwake.
Wanafunzi walionekana
kumwelewa sana Mathew kwani
alikuwa anafundisha kwa mifano
iliyowahi kumtokea.Lilikuwa ni
somo lenye msisimko
mkubwa.Madarasa mengine nayo
yaliunganishwa kielektroniki na
kile kilichokuwa kinaendelea
katika darasa la mwaka wa
mwisho.Chuoni kila kitu
kilisimama kwa muda wote
wakimfuatiliaMathew Mulumbi
**********
Mathew Mulumbi alitumia
saa mbili na nusu katika darasa
lake la kwanza kabisa na
alipotoka akapongezwa na kila
mtu pale chuoni.Akiwa katika
mazungumzo na profesa Santala
mara simu yake ikaita.Ilikuwa ni
namba ngeni katika simu yake
akatoka nje na kupokea
“Hallo” akasema Mathew
“Hallo Mathew
Mulumbi”ikasema sauti ya
mwanamke upande wa pili
“Nani mwenzangu? Mathew
akauliza
“Naitwa Linah Mpama
unanikumbuka?akauliza Yule
mwanamke
“Linah? Mathew akashangaa
“Ndiyo.Unanikumbuka
tuliwahi kukutana Arusha japo
imepita miaka mingi? Akauliza
Linah
“Ninakukumbuka
Linah.Siwezi
kukusahau.Nimefurahi leo
umenikumbuka.Unaendeleaje?
Hawajambo wadogo zako Flora
na Jonathan? Mathew akauliza
“Wote wazima kabisa”
“Tena imekuwa vyema
umenipigia.Mimi niko hapa
Arusha kwa siku chache nitakuja
kuwatembelea bado mko Arusha?
Mathew akauliza
“Hapana Mathew hatuko tena
Arusha tumekwisha hama tuko
Dar es salaam” akasema Linah
“Basi nitakaporejea
nitakutafuta tutaonana” akasema
Mathew
“Mathew nimekutafuta nina
shida kubwa nahitajimsaada”
“Msaada upi unahitaji Linah?
“Kuna watu wanataka
kuniua.Niko katika hatari kubwa
na muda wowote naweza
kuuawa” akasema Linah
“Nani wanataka kukuua na
kwa nini?
“Mathew ni jambo kubwa
nitakueleza pale tutakapoonana
lakini kwa sasa naomba utafute
namna ya kunisaidia”
“Linah niko mbali kwa
sasa.Kwa nini usiende kutoa
taarifa katika kituo chochote cha
polisi kilicho karibu yako?
“I Can’t ! akasema Linah
“Kwa nini Linah?
“Mathew please help me.Ni
wewe pekee ambaye ninakuamini
kwamba unaweza kunisaidia na
kuniondoa katika hatari hii
kubwa” akasema Linah
“Linah ningekuwa karibu
ningekusaidia lakini niko
mbali.Kitu gani kinakufanya
usiende kutoa taarifa polisi
kuhusu hao wanaotaka kukuua?
Akauliza Mathew
“It’s because I killed
someone”akasema Linah na
Mathew akastuka
“You killed someone?
Mathew akauliza
“Yes” akajibu Linah na
Mathew akavuta pumzi ndefu
“Mathew please help me !
akalia Linah
“Kwa sasa uko wapi?
“Nimejificha kwa rafiki
yangu” akajibu Linah
“Sawa Linah.Naomba utulie
hapo hapo wakati ninafanya
utaratibu wa kurejea Dar es
salaam leo hii hii kuja
kukusaidia.Tafadhali usiondoke
mahala hapo” akasema Mathew
“Nashukuru sana
Mathew”akasema Linah na
kukata simu.
“Is this true? Akajiuliza
Mathew na kuirejesha kichwani
picha ya msichana mdogo
aliyekutana naye miaka kumi na
tano iliyopita
“Lina Yule niliyekutana naye
miaka ile leo hii ananiambia kuwa
ameua mtu ! haya ni maajabu.I
need to help her.Lazima nirudi
Dar es salaam leo hii hii nikajue
nini kimetokea nione namna ya
kuweza kumsaidia.Hadi
amenipigia mimi simu inaonesha
hana mtu mwingine ambaye
anaweza akamsaidia” akawaza
Mathew na kumfuata Profesa
Santala akamueleza kuwa
amepata dharura na anatakiwa
kurejea Dar es slaam mara moja.
“Hakuna tatizo Mathew
Mulumbi unaweza ukaenda
kutatua tatizo hilo na ukarejea
tena au tutatumia mfumo wa
kielektroniki ili uweze kufundisha
hata ukiwa Dar es salaam”
akasema Profesa Santala
Mathew hakupoteza muda
akaondoka pale chuoni na kuanza
kushughulikia usafiri wa kurejea
Dar es salaam akafanikiwa kupata
nafasi katika ndege ya shirika la
ndege la Tanzania inayoondoka
Arusha saa kumi alasiri.Wakati
akisyubiri muda ufike akaenda
kupumzika hotelin “Angekuwa
ni mtu mwingine nisingekubali
katu kwenda kumsikiliza lakini
Linah lazima nikamsikilize nijue
nini hasa kimemsibu hadi akaua
mtu.Sura ya kimalaika ya binti
Yule bado iko kichwani kwangu
hadi leo na inaniwia ugumu
kuamini eti amemuua mtu”
akawaza Mathew akiwa
anakusanya nguo zake tayari kwa
safari ya kurejea Dar es salaam.
“She was a beautiful kid japo
mambo yake yalikuwa makubwa
kuzidi umri wake.Nilistaajabu
namna alivyofahamu mambo
makubwa ambayo kwa binti wa
umri wake hakupaswa kuyajua”
akawaza Mathew na kurejesha
kumbu kumbu nyuma
MIAKA 15 ILIYOPITA
Ilikuwa ni siku ya Jumanne
Mathew Mulumbi alipowasili
katika jijini Arusha akitokea Dar
es salaam kwa ajili ya kutekeleza
misheni muhimu aliyotumwa na
viongozi wake.Alipokewa na
mmoja wa wafanyakazi wa
shirika la ujasusi ofisi ya Arusha
na kumpeleka katika nyumba
ambako angekaa kwa muda
ambao angekuwepo hapo
Arusha.Ilikuwa ni nyumba nzuri
na kubwa.Ilikuwa na vyumba
vitatu vya kulala,jiko,chumba cha
kulia chakula,sebule
kubwa,chumba cha
maongezi,maktaba ndogo,na
chumba ambacho kingetumika
kama ofisi ya nyumbani bila
kusahau gereji ya gari.Pembeni
kidogo ya nyumba hiyo ya
Mathew kulikuwa na jumba
lingine kubwa la kifahari
Siku ya Jumatano Mathew
alianza rasmi kuifanya kazi
ilimpeleka Arusha.Aliondoka
nyumbani saa mbili za asubuhi na
kurejea nyumbani saa tatu za
usiku.Toka alipofika Arusha
hakupumzika alitoka asubuhi na
kurejea nyumbani usiku.Jumapili
aliamua kupumzika nyumbani
akachukua kitabu chake cha
hadithi akaenda kuketi kandoni
mwa bwawa la kuogelea akiwa
na chupa yake ya mvinyo
pembeni.Akiwa amezama katika
hadithi ile tamu akasikia sauti za
watoto wakimsalimu.
“Shikamoo uncle” Mathew
akageuka na kukutana na sura
zenye tabasamu za watoto wawili
wa kike na kiume ambao bila hata
ufafanuzi lazima ungegundua
kwamba ni mapacha.Walikuwa
wanafanana mno.Mathew
akatabasamu na kucheka kidogo
kwa namna watoto wale
walivyofanana.
"Marahaba hamjambo?
“Hatujambo" wakajibu kwa
pamoja watoto wale
walioonekana wachangamfu
sana.Wakamsogelea Mathew pale
katika kiti wakaa pembeni yake.
“Uncle unaitwa nani?
akauliza mmoja wao
“Ninaitwa Uncle Mathew
Mulumbi.Wewe unaitwa nani?
“Mimi naitwa Flora na huyu
anaitwa Jonathan" akasema
mmoja wao ambaye alionekana
muongeaji sana.
“Nimefurahi
kuwafahamu”akasema Mathew
huku akikifunika kitabu chake.
“Uncle Mathew watoto wako
umewaacha wapi? akauliza
Jonathan.Mathew akacheka
kidogo
"Sina mtoto..." Mathew
akajibu
“Jumba lote hili unaishi
mwenyewe? akauliza tena
Jonathan
“Ndiyo ninaishi mwenyewe"
Mathew akajibu
“Mke wako yuko wapi?
akauliza Flora.Mathew
akastaajabu maswali ya wale
watoto wadogo
“Mnapenda juisi? Akauliza
Mathew
“Ndiyo uncle” wakajibu na
Mathew akawachukua wakaenda
ndani na kuwapatia juisi na
biskuti.Aliwafurahia sana wale
watoto kwa uchangamfu
wao.Kwa muda mfupi watoto
wale walimzoea sana na wakati
akiandaa chakula cha mchana
dada yao akiwaita
“Dada anatuita" akasema
Flora.
Mathew akainuka na
kuelekea nje.Mlangoni alisimama
binti mmoja mweupe aliyevaa
fulana ya mikanda.Chini alivaa
kaptura iliyomfika
magotini.Mathew akastuka baada
ya kukutanisha macho na sura
yenye tabasamu la mstuko la binti
yule.
“Mambo kaka" akasema binti
yule ambaye kiumri yeye na
Mathew hawalingani.Mathew
akababaika kuijibu salamu ya
binti yule.Akabaki akimtazama.
“Kaka nakusalimia" akasema
tena yule binti ambaye
hakuonekana kuwa na wasiwasi
wowote
“Hujambo? Akajibu Mathew
“Sijambo.Kumbe wewe
ndiye uliyehamia humu? akauliza
yule binti huku akiona aibu kwa
mbali
“Ndiyo ni mimi" Mathew
akajibu
“Karibu sana.Mimi naitwa
Linah.Sisi tunaishi nyumba hiyo
ya pembeni.Unaitwa nani?
Akauliza Linah .
“Naitwa Mathew Mulumbi"
akajibu Mathew
“Ouh !.Jina zuri sana"
akasema Linah.
“Karibu ndani Linah”
akasema Mathew
“Nawahitaji akina Flora”
akasema Linah
"Wako humu ndani
wanaangalia katuni.Karibu
ujumuike nasi" akasema Mathew
“Ahsante lakini naogopa
kupigwa” akasema Linah huku
akimfuata Mathew kuelekea
sebuleni
“Upigwe na nani ? Mathew
akauliza
“Na wenye nyumba” akajibu
Linah na kumfanya Mathew
aangue kicheko akamkaribisha
Linah sebuleni
“Unatumia kinywaji gani
Linah? Akauliza Mathew.Linah
akatabasamu na kusema
“Una bia yoyote humu ndani
au mvinyo? Akauliza Linah na
kumfanya Mathew astuke akabaki
akimtazama.
“Mbona umestuka
Mathew.Unashangaa mimi
kunywa bia au mvinyo?Akauliza
tena Linah.Mathew akatabasamu
na kusema
“Ndiyo nimestuka kidogo
kwa sababu vinywaji hivyo ni
vikali na haviwezi kukufaa.Humu
nina Ice cream,juice
mbalimbali,soda na maji”
akasema Mathew.
“Watoto wadogo kama hawa
akina Jonathan ndio hawatumii
vinywaji vikali lakini mimi
ninatumia hasa mvinyo” akasema
Linah huku akicheka kichini chini
“Kwa hiyo nikupatie
kinywaji gani Linah? Akauliza
Mathew
“Nashukuru sihitaji chochote
kwa sasa.Kuwa na amani
Mathew” akajibu Linah na
kumfanya Mathew azidi
kumstaajabia binti yule mdogo.
Mathew akaenda kuketi
sofani akaendelea kumfanyia
usaili Linah.
“Anaonekana ni binti mdogo
lakini mambo yake ni tofauti
kabisa na umri wake
ulivyo.Anaongea kwa kujiamini
sana na macho yake makavu hana
aibu hata kidogo.Nilishangaa sana
aliponipa ile salamu.Anapaswa
kunisalimu shikamoo kaka lakini
badala yake akaniambia eti
mambo kaka.Amenistua zaidi
alipohitaji bia au mvinyo.Umri
huu anatumia kilevi !!
Nimeshangaa sana” Akawaza
Mathew
“Mathew sebule yako
nzuri”akasema Linah huku
akitabasamu baada ya kuona
kumekuwa kimya sebuleni.
“Ahsante Linah..” akajibu
Mathew.
“Ana sauti nzuri,sura
nzuri.Kiujumla mtoto huyu ni
mzuri kupindukia.Nasikitika si wa
umri wangu.Naogopa hata kukaa
naye humu ndani wazazi wake
wasije wakaanza kuniletea
matatizo”akawaza Mathew
Wakati Mathew akiendelea
kumtazama Linah kwa kuibia ibia
mara simu ya Linah
ikaita.Akaipokea na kuongea
kidogo kisha akasimama.
“Mathew nawachukua akina
Flora wanapelekwa saluni na
dereva.Nitakuja baada ya muda
mfupi .Au unatoka? Akauliza
Linah.
“Hapana Linah leo ni siku
yangu ya mapumziko,nitakuwepo
nyumbani muda wote.” Akajibu
Mathew.
“Basi vizuri nitarejea baada
ya muda mfupi.Ngoja niwapeleke
hawa watoto” akasema Linah na
kuwashika mikono Jonathan na
Flora akaondoka nao.
“Ama kweli leo nimepatwa
na mshangao.Anasema anarudi
baada ya muda mfupi,sijui
niondoke ili akija
asinikute?Nimemuogopa hata
kukaa karibu naye.Naogopa
iwapo wazazi wake watamkuta
akiwa huku kwangu ninaweza
kuletewa shida.Linah amenizoea
kwa haraka sana mpaka
nimeshangaa.Ninatakiwa
kutokumzoea huyu binti anaweza
akaniletea matatizo” Mathew
alizama mawazoni na mara
mlango ukafunguliwa Linah
akaingia akiwa ameshika mfuko
wa karatasi huku akitabasamu.
“Nimerudi Mathew.Jonathan
na Flora wameenda Saluni
nimebaki peke yangu.Ninahisi
upweke nikiwa peke yangu
ndani” Akasema Linah na
kuuweka ule mfuko wake wa
karatasi mezani.
“Usihofu Linah karibu.Baba
na mama wamesafiri ? akauliza
Mathew
“Unamzungumzia baba
Clemence na mama Blandina?
Akauliza Linah
“Ndiyo” akasema
Mathew.Linah akainama akafikiri
kidogo na kusema
“Wale ni walezi
wangu”akasema Linah
“Wazazi wako wanaishi
wapi? Akauliza tena
Mathew.Linah akanyamaza
kidogo halafu akajibu
“Wazazi wangu walikwisha
fariki” Mathew akastuka kidogo
na kusema
“ouh pole sana Linah.Sikujua
kama umewapoteza wazazi wote
wawili” akasema kwa masikitiko
Mathew.
“Usijali Mathew.Haya ni
mambo ya kawaida na ambayo
yanatutokea sisi sote” akasema
Linah.
“Nilipotambulishwa kwa
mzee Clemence kuwa ndiye
mmiliki wa nyumba hii nikadhani
ndiye baba yako mzazi.”
Akasema Mathew
“Hapana yule ni mlezi
wangu.Sina undugu naye
wowote.Aliwahi kuwa rafiki
mkubwa wa baba kwa hiyo baada
ya wazazi wetu kufariki
akatuchukua na kutulea” akasema
Linah.
“Ndugu zako wengine wako
wapi? akauliza Mathew
“Ndugu pekee
tunayemfahamu ni hawa
wanaotulea wengine wote hatuna
muda nao” akajibu Linah
“Kuna tatizo lolote lilitokea
kati yenu na hao ndugu zenu?
Akauliza Mathew
“Ni historia ndefu kidogo
lakini kwa ufupi tu ni kwamba
baada ya wazazi wetu kufariki
ulitokea mgogoro mkubwa wa
mali na kutuacha masikini.Kama
si huyu mzee kutuchukua na
kutulea yawezekana mimi na
wadogo zangu hivi sasa
tungekuwa watoto wa mitaani
wakati baba yetu alikuwa ni
bilionea”
“Pole sana
Linah..Umekumbana na mikasa
mizito wakati bado mdogo”
akasema Mathew
“Udogo wangu nini Mathew?
Au unanipima kwa umbo?
Akauliza Linah na kumfanya
Mathew acheke kidogo.
“Kwa kweli umbo lako
linaonyesha bado wewe ni binti
mdogo” akasema Mathew na
kumfanya Linah acheke kicheko
kikubwa.
“Usidharau reli
Mathew.Pamoja na wembamba
wake lakini inabeba vitu vizito”
akasema Linah huku akicheka.
“Sijakudharau Linah lakini ni
umbo lako ndilo linaonyesha
kwamba bado ni binti
mdogo.Unaweza ukaniambia una
miaka mingapi?
“C’mon Mathew sitaki
kuzungumzia masuala hayo ya
miaka”akasema Linah na
kumfanya Mathew
atabasamu.Linah akauchukua ule
mfuko wake wa karatasi aliokuja
nao akatoa chupa ya mvinyo na
kuiweka mezani.
“Mathew unatumia kinywaji
hiki? Akauliza Linah .Mathew
akashindwa ajibu nini akabaki
akimkodolea macho hakuyaamini
macho yake
“Mathew unatumia hiki
kinywaji? Akauliza tena
Linah.Mathew akamtazama na
kuuliza
“Linah unatumia hii pombe
kali? Akauliza Mathew
“Ndiyo.Hiki ni kinywaji
changu hasa kwa siku za mwisho
wa wiki na nyakati ambazo huwa
nina furaha.Kwa siku ya leo
ninafuraha kubwa na ndiyo maana
ninataka kunywa kinywaji
hiki.”akasema Linah.Mathew
akaichukua chupa ile akaisoma na
kuirudisha mezani akamtazama
Linah.
“Linah unasoma darasa la
ngapi? Akauliza Mathew
“Usiulize darasa sema kidato
cha ngapi? Darasa ni kwa watoto
wadogo” akasema Linah na
kumfanya Mathew atabasamu
“Leo nimekutana na kiboko
yangu” akawaza Mathew
“Uko kidato cha ngapi?
Akauliza tena Mathew
“Mathew niwapo nyumbani
au katika sehemu za mapumziko
sipendi kuongelea sana masuala
ya shule.Kama hutajali naomba
tafadhali usiniulize masuala ya
shule au maisha binafsi kwa
sasa.Nataka nifurahi.Ila kama
huridhiki kwa mimi kukaa hapa
kwako its ok I can just leave…”
akasema Linah.
“Samahani Linah kama
umekwazika kwa maswali
niliyokuuliza.Hofu yangu mimi
ilikuwa ni kwa walezi wako
wakija na kukukuta huku kwangu
tena ukiwa na chupa ya mvinyo
wanaweza wakaniletea matatizo”
akasema Mathew kwa sauti ya
upole
“Walezi wangu wamekwenda
safari watarudi wiki ijayo"akajibu
Linah
“Kama ni hivyo basi vizuri"
akasema Mathew huku akipiga
hatua kwenda jikoni na kuchukua
glasi mbili na vipande vya
barafu.Akajimiminia mvinyo
katika glasi na kwenda kuketi
sofani.Linah naye akajimiminia
mvinyo akanywa na kukohoa
kidogo halafu akageuza kichwa
na kumtazama Mathew ambaye
alikuwa amemkodolea macho ya
mshangao.
“Mathew mbona
unaniangalia hivyo? Mimi
najisikia vibaya sana
unavyonitazama namna
hiyo.Mathew nina kitu gani cha
ajabu kinachokufanya unitazame
namna hiyo? au unashangaa kwa
mimi kunywa pombe? Sioni kama
ni kitu cha ajabu." akasema Linah
“Linah imenibidi nishangae
kidogo kwa sababu ni mara yangu
ya kwanza kumuona binti wa
umri wako akinywa kinywaji
kikali kama hiki" akasema
Mathew
"Mathew nimekwambia
usiniweke mimi katika kundi la
watoto.Mimi si mtoto mdogo
kama unavyofikiri" akasema
Linah
“Samahani Linah.Usinifikirie
vibaya lakini ninasema hivyo kwa
sababu ninakujali kama mdogo
wangu.Vinywaji vikali kama hivi
havifai kwenu ninyi wanafunzi"
akasema Mathew.Linah akainuka
pale sofani akaifunga ile chupa ya
mvinyo akairudisha katika mfuko
wake wa karatasi akazirusha
nywele zake nyuma na
kumtazama Mathew.
“Nilitegemea ningepata
kampani ya maana toka kwako
badala yake umeanza
kunikashifu.Tayari siku yangu
imeharibika.Kwa heri Mathew”
akasema Linah huku akipiga
hatua kutoka nje.
“Linah usikasirike mdogo
wangu sikuwa na maana mbaya
kukwambia vile”akasema
Mathew lakini Linah hakugeuka
akatokomea zake.
**********
Mathew alistuka saa tatu za
usiku.Alikuwa amelala sana
kutokana na uchovu wa wiki
nzima.Kwa uchovu akainuka na
kukaa kitandani.Wakati
akijinyoosha nyoosha mlio wa
ujumbe mfupi wa maandishi
ukasikika katika simu
yake.Akanyoosha mkono na
kuichukua simu akaanza kuusoma
ujumbe ule ambao ulitoka katika
namba ambazo hakuwa
akizifahamu.
" Mathew nafahamu
nilikuudhi kwa maneno
yangu.Naomba tafadhali kama
nilikuudhi kwa namna yoyote ile
unisamehe na ukubali tuwe
marafiki tena.mwisho naomba
uniruhusu nikupigie simu walau
niisikie sauti yako nzuri yenye
kunipa wazimu....Linah" Mathew
akavuta pumzi ndefu
“Amepata wapi namba zangu
huyu binti? akawaza Mathew
akainuka na kukaa kitandani.Kwa
dakika chache akawa katika
mawazo mengi.Sura ya Linah
ikamjia tena kichwani akausoma
tena ujumbe ule uliotoka kwa
Linah na kutikisa kichwa.
“Nashindwa kumuelewa
huyu mtoto.Nimemfahamu kwa
muda mfupi tu lakini mambo
yake ni makubwa na ya
kushangaza.Kitu kingine cha
kushangaza ni wapi amezipata
namba zangu za simu" akawaza
Mathew halafu akaitupa simu
pembeni akajilaza tena kitandani.
“Inanibidi niwe mwangalifu
sana na huyu mtoto.Mwelekeo
wake si mzuri .Anaweza
akanisababishia matatizo"
akawaza Mathew na kujigeuza
upande wa pili na mara
akastuliwa na sauti ya mlio wa
ujumbe mfupi katika simu
yake.Akageuka na kuichukua
akaufungua ujumbe
ule.Alipousoma akajikuta
akikunja uso.
“Its her again...Huyu binti
anataka kitu gani kwangu?
Natakiwa kumkemea ili apunguze
mazoea na mimi.Ngoja nikatolee
uvivu haka katoto ili kasiendelee
kunizoea." akasema Mathew huku
akiziandika zile namba za Linah
na kupiga.Simu ikaanza
kuita.Mathew alikuwa amekunja
uso kwa hasira
“Hallo Mathew,ahsante kwa
kupiga" ikasema sauti laini ya
Linah.Kabla Mathew hajajibu
Linah akaendelea.
“Mathew samahani kwa
kukusumbua usiku huu.Uko
kitandani? akauliza Linah kwa
sauti laini.Mathew akajikuta
akitabasamu akashindwa ajibu
nini
"Sijui nikajibu nini haka
katoto.Sijui nikafokee kaache
mazoea na mimi...Lakini ngoja
nikasikie kanataka nini" akawaza
Mathew.
Mathew nakuuliza umelala?
akauliza tena Linah
“Sijalala Linah" akajibu
Mathew na kukohoa kidogo
“Pole" akasema Linah
"Pole ya nini? Mathew
akauliza
“Nimekusikia unakohoa.Pole
sana.Kifua kinakusumbua?
akauliza Linah
“Hapana sisumbuliwi na
kifua” akajibu Mathew
“Mathew sema basi hata
ahsante.Mwenzio amekupa pole
na husemi hata ahsante" akasema
Linah kwa sauti laini.Mathew
akatabasamu na kusema
“Ahsante” Kimya kifupi
kikapita halafu Linah akasema
“Unafanya nini muda huu
Mathew?.Mathew akafikiri
kidogo na kujibu.
“Nimejilaza tu hapa
kitandani”
“Uko na nani? akauliza Linah
“Niko peke yangu" akajibu
Mathew halafu akaukunja uso
wake.
“Umevaa nini usiku huu?
akauliza Linah na kumfanya
Mathew abaki kimya akishangaa
“Haka katoto ..!!
“Nijibu basi Mathew umevaa
nini usiku huu? akauliza tena
Linah
"Nimevaa nguo za kulalia"
akajibu Linah.
“Nguo gani? suruali
,kaptura,shati,kanzu au nini?
Mathew akacheka kidogo na
kusema
“Linah naomba unisikilize"
akasema Mathew lakini kabla
hajatamka lolote Linah
akasema
“Naomba kwanza unisikilize
mimi Mathew halafu na mimi
nitakusikiliza.Mimi ndiye
niliyekuwa wa kwanza kukutumia
ujumbe.Nisikilize kwanza
ninachotaka kukwambia halafu na
mimi nitakusikiliza hata kwa
usiku kucha" akasema
Linah.Mathew akazidi kuikunja
sura yake
“Haya sema haraka
unachotaka kuniambia" akasema
kwa sauti ya ukali Mathew.
“Usikasirike Mathew.Nataka
tuongee kirafiki tu.Najua uko
mwenyewe mida hii na mimi niko
mwenyewe.Najua unahisi upweke
mkubwa kwa kuwa peke yako
mida hii na ndiyo maana
nimeamua kukupigia tuongee ili
ufurahi au nimefanya vibaya
Mathew? Akauliza Linah na
kumfanya Mathew atingishe
kichwa chake huku akitabasamu.
“Dah ! Huyu mtoto” akawaza
Mathew.
“Mathew najua unaniona
mimi kama mtoto mdogo labda
kutokana na umbo na muonekano
wangu lakini katika umbo hili hili
na muonekano huu huu ninaweza
nikawa rafiki yako mkubwa na
ambaye nikakufanya ukatabasamu
na kuifurahia dunia" akasema
Linah.
“Linah nani amekupa namba
zangu za simu? akauliza Mathew
kwa sauti ya ukali.
“Mathew kuna kitu kimoja
ambacho ninapaswa
kukukumbusha japokuwa mimi ni
mtoto mdogo kama
unavyonichukulia.Wewe ni
msomaji wa maandiko
matakatifu? akauliza Linah.
“Ndiyo ninasoma" akajibu
Mathew
“Good.Nadhani umesoma
biblia japo kidogo japokuwa
hauonekani kama ni mtu wa
kusoma maandiko.Katika biblia
takatifu agano la kale kitabu cha
mwanzo moja,mstari wa kwanza
hadi wa tano inasema kwamba
Hapo mwanzo Mungu aliziumba
mbingu na nchi.Nayo nchi
ilikuwa ukiwa,tena utupu, na giza
lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya
maji, Roho ya Mungu ikatulia juu
ya uso wa maji. Mungu akasema,
Iwe nuru; ikawa nuru.
Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni
njema; Mungu akatenga nuru na
giza. Mungu akaiita nuru Mchana,
na giza akaliita Usiku.." akasema
Linah na kunyamaza kidogo..
“Unataka kunifundisha nini?
akauliza Mathew akionesha
kuzidi kukerwa na Linah.
“Kuna jambo nataka
nikueleweshe kwa sababu
nikisema nataka kukufundisha
utasema kwamba huwezi
kufundishwa na mtoto" akajibu
Linah
“Linah nimekwisha choshwa
na wewe.Naomba useme
unachotaka kukisema ninahitaji
kupumzika” akafoka Mathew
“Usihofu Mathew
utapumzika,tena utalala usingizi
mnono sana endelea kunisikiliza"
akasema Linah na kunyamaza
kidogo halafu akaendelea.
“Mwenyezi Mungu alikuwa
na makusudi yake alipoumba
usiku.Aliuweka usiku maalum
kwa ajili ya mapumziko ya
viumbe wake wote aliowaumba
na ndiyo maana hata wanyama na
wadudu hupumzika usiku.Kwa
maana hiyo usiku si wakati wa
kukasirika wala kuongea kwa
sauti ya juu ya ukali.Ili kuupa
usiku hadhi yake unapaswa
kuongea lugha nyepesi,kwa
kutumia sauti laini hasa kama
unaongea na mtu wa jinsia ya
tofauti na yako.Kwa hiyo Mathew
nakuomba usiwe na hasira
,tabasamu na uongee na kucheka
na mimi kwa usiku huu.Mathew
nataka tuongee kama
marafiki,japokuwa hatulingani
kiumri lakini hicho si kigezo cha
mimi na wewe kushindwa kuwa
marafiki.Kuna mambo mengi
ambayo tunaweza
tukaongea,tukabadilishana
mawazo na hata kusaidiana
ikibidi" akasema Linah
“Unataka nikusaidie kitu gani
Linah? akauliza Mathew
“Sihitaji unisaidie kitu
chochote kile kwa sababu
ninajitosheleza kwa kila kitu
lakini ninachokiomba toka kwako
ni mimi na wewe kuwa marafiki"
akasema Linah.Mathew akacheka
kidogo na kusema
“Linah unanifurahisha
sana.Mimi na wewe hatuwezi
kuwa marafiki.Kwanza umri wetu
haulingani,pili mimi ni
mfanyakazi na wewe ni
mwanafunzi kwa hiyo tuko katika
dunia mbili tofauti sana.Linah
wewe ni kama mdogo wangu na
si kama rafiki yangu" akasema
Mathew na kumfanya Linah
acheke kwa nguvu.
“Mathew umenifurahisha
sana.Hatuvunji katiba ya nchi
kwa mimi na wewe kuwa
marafiki.Kuna kitu kimoja
ambacho wewe na wengine wengi
huwa
mnajichanganya.Ninapozungumzi
a urafiki sina maana ya kwamba
mimi na wewe tuwe na
mahusiano ya kimapenzi.Achana
na ile dhana kwamba kuwa na
rafiki wa jinsia tofauti basi ni
lazima mjiingize katika masuala
ya ngono" akasema Linah na
kumfanya Mathew atabasamu.
“Haka katoto kanaonekana
kamekomaa sana kiakili.Kana
zungumza mambo makubwa
tofauti na umri wake." akawaza
Mathew.
“Kwa hiyo Mathew mimi na
wewe tunaweza kuwa marafiki
wa kawaida tu japokuwa tuko
katika dunia mbili tofauti kama
ulivyosema." akasema Linah
“Najua kwa muda huu
utakuwa ukiwaza kwamba huyu
mtoto anataka nini
kwangu.Sihitaji chochote toka
kwako Mathew zaidi ya kuwa
marafiki kwa sababu nimeona
kuna vitu vinavyoweza kutufanya
tukawa marafiki wakubwa.Vile
vile ninataka kukusaidia kwa
mambo mawili matatu hivi"
akasema Linah
“Mambo gani hayo ambayo
unataka kunisaidia? akauliza
Mathew huku akitabasamu
“Ninataka kukusadia
kukuondolea upweke ulionao"
akasema Linah na Mathew
akacheka tena kwa nguvu.
“Usinivunje mbavu zangu we
mtoto.Upweke huo unawezaje
kuuondoa? akauliza Mathew
huku akicheka.
“C'mon Mathew naomba
usiniite mimi mtoto wakati hata
wewe bado ni mtoto kwa mama
yako.Naomba tuitane kwa majina
yetu Linah au Mathew.Kuhusu
upweke ninaweza kukusaidia
ukaondokana nao..Niambie
kwanza una mpenzi au huna?
..Akauliza Linah.Mathew akasita
kujibu
“Nijibu Mathew una mpenzi
au huna? akauliza tena Linah
"Ninaye" akajibu
“Yuko wapi ?
“Yuko nje ya nchi" akajibu
Mathew
“Ok Vizuri.Mara ya mwisho
umekutana naye lini? akauliza
Linah
"Miezi kadhaa iliyopita"
“Sawa.Ukimkumbuka sana
huwa unafanya nini?
"Sijakuelewa unamaanisha
nini? akauliza Mathew
“Nina maana kwamba siku
ukiwa na hamu naye,hamu ya
kufanya naye mapenzi si unajua
tena kwa binadamu aliyekamilika
hii ni hali ya kawaida kutokea na
yeye yuko mbali huwa unafanya
nini ? Be honnest with me.."
akasema Linah.Mathew akakaa
kimya.
"Haka katoto kana wazimu
nini? maswali gani haya ya
kuniuliza? akawaza Mathew na
kuikunja sura
“Mathew mbona hunijibu?
akauliza Linah na mara Mathew
akakata simu...
“Hana adabu huyu mtoto !
akasema Mathew kwa hasira na
simu yake ikaita.Akatazama
mpigaji alikuwa ni Linah.
"Ni yeye tena" akasema
Mathew kwa hasira.Akaipokea
simu ile na kusema kwa ukali
“Linah unataka nini kwangu?
Kwa nini unakuwa msumbufu
namna hiyo? akauliza Mathew
kwa ukali.Linah akacheka kidogo
na kusema kwa sauti ndogo..
“Mathew nimekwisha
kueleza kwamba ukifanya hivyo
unavunja taratibu za
usiku.Usipige kelele au kuongea
kwa ukali.Ongea kwa sauti ndogo
yenye kuvutia kama
ninavyoongea mimi" akasema
Linah halafu kikapita kimya
kifupi
“Mathew nakuomba
usikasirike rafiki yangu.Nina
imani huu ni mwanzo wetu mzuri
wa kufahamiana na baada ya
muda utanizoea na utafurahia
sana kuwa na mimi karibu.Kwa
sasa nakuomba taratibu jilaze
kitandani na tuendelee na
maongezi yetu.Pretend niko
pembeni yako tunaongea kama
marafiki wakubwa" akasema
Linah na kumfanya Mathew avute
pumzi ndefu..
“Sijawahi kukutana na mtoto
kama huyu" akawaza Mathew
“Mathew hukunijibu swali
langu nililokuuliza" akasema
Linah
" Swali gani Linah? akauliza
Mathew
“Nilikuuliza kwamba ukiwa
na hamu ya kufanya mapenzi na
mpenzi wako yuko mbali huwa
unafanya nini? Mathew akakata
simu kwa hasira
DAR ES SALAAM
Mathew Mulumbi aliwasili
Dar es salaam na kumkuta dereva
wake akimsubiri uwanja wa
ndege.Akampigia simu Linah na
kumfahamisha kuwa tayari
amekwisha fika Dar es salaam na
Linah akamuelekea mahala alipo
na Mathew akamuelekeza dereva
wake kulekea mahala
alikoelekeza Linah.
“Mathew Mulumbi ! akasema
Linah na kutabasamu baada ya
Mathew Mulumbi kufika katika
nyumba alikokuwa amejificha.
“Linah ! akasema Mathew na
wakatazamana kwa muda
“Nimefurahi kukuona tena
Mathew Mulumbi baada ya miaka
kumi na tano.Ahsante sana kwa
kukubali ombi langu la kuja
kuonana nami na samahani sana
kwa kukuharibia ratiba zako”
akasema Linah na kutikisa kichwa
chake kurudisha nyuma nywele
zake ndefu.Mathew hakujibu
akaendelea kumtazama
“Linah nimelazimika
kukatisha shughuli zangu muhimu
na kurejea Dar es salaam kwa
kuwa ni wewe.Tusipoteze muda
ingia garii tuondoke” akasema
Mathew na Linah akachukua
mizigo yake ikapakiwa garini na
safari ikaanza
“Mathew kuna sehemu
nataka unipeleke lakini nataka
twende mimi na wewe pekee
sihitajimtu mwingine wa tatu”
akasema Linah
“Huyu ni dereva wangu na
hana tatizo lolote”akasema
Mathew\
“I don’t need him ! akasema
Linah na Mathew akamtaka
dereva wake kusimamisha gari
katika hoteli moja akashuka kisha
yeye na Linah wakaendelea na
safari
“Ahsante sana Mathew”
akasema Linah huku akitoa
machozi
“Linah huu si wakati wa
kulia” akasema Mathew
akiendelea kukanyaga mafuta
“Katika maisha yangu
sikutegemea kama ningekutana
tena na Linah.Amekuwa mkubwa
na mrembo sana kinachoniumiza
kichwa nini kimemuingiza katika
masuala ya mauaji? Amepataje
namba yangu ya simu? Akajiuliza
Mathew
“Mathew nataka tupite katika
duka la madawa” akasema Linah
na safari ikaendelea hadi
walipofika katika duka kubwa la
madawa.Tayari kiza kilikwisha
ingia.Linah akachukua vitu
alivyovihitaji katika lile duka la
dawa Mathew akalipa
wakaondoka
Linah akamuelekeza Mathew
mahala anakotaka
waelekee.Wakaliacha gari katika
maegesho ya baa Fulani
wakapanda pikipiki hadi mahala
ambako Linah alielekeza halafu
wakaanza kutembea kwa miguu
na kushika njia ambayo Mathew
hakujua wanaelekea wapi.
Walitembea kimya kimya Linah
akiongoza njia na mara
wakajikuta wamefika katika
makaburi
“Tumefuata nini huku?
Mathew akauliza kwa mshangao
“Relax Mathew” akasema
Linah na kumuongoza Mathew
hadi katikati kabisa mwa eneo lile
la makaburi
“Kuna nini huku Linah?
Akauliza Mathew
“Mathew kuna kitu muhimu
nataka unisaidie kukifanya”
akasema Linah wakiwa juu ya
kaburi
“Mathew Mulumbi nafahamu
wewe ni jasiri hivyo nataka
utumie ujasiri wako
kunisaidia”akasema Linah
“Kitu gani unahitaji
nikusaidie? Akauliza
Mathew.Linah akamtaka asogee
karibu
“Unaiona hii pete kidoleni
kwangu? Akauliza Linah na
kumuonesha Mathew pete katika
kidole chake
“Ndiyo nimeiona”akajibu
Mathew
“Ninataka kuitoa pete hii
katika kidole changu lakini pete
hii haitoki kirahisi hivyo basi
ninataka unisaidie kukata hiki
kidole”
“Kukata kidole? Mathew
akashangaa
“Ndiyo Mathew ninataka
kukikata hiki kidole na usiniulize
sasa hivi kwa nini.Nitakueleza
sababu baadaye.Naomba
unisikilize vizuri” akasema Linah
na kumtazama Mathew kwa
makini
“Wakati wa kukiondoa kidole
hiki kuna mambo yatatokea”
akanyamaza na kumtazama
Mathew
“Mabadiliko gani? Akauliza
Mathew
“Nitabadilika na kuwa
kiumbe wa ajabu lakini pamoja na
mabadiliko hayo naomba
tafadhali usiogope wala kukimbia
hutadhurika.Endelea na zoezi la
kukata kidole usiache” akasema
Linah na Mathew akabaki
anamshangaa
“Mathew tusipoteze muda
zoezi lianze mara moja” akasema
Linah
“Who are you? Akauliza
Mathew
“Mathew ni mimi
Linah.Najua nimekustua kwa
haya niliyokwambia na ndiyo
maana nilikuchagua wewe kwani
ni mtu ambaye utaniamini na
kunisaidia.Let’s do this Mathew!
akasema Lina na kumpatia
Mathew mkasi,akakishika kidole
kilichokuwa na pete na kukibana
kwa mkasi.Mara tu ngozi ya
kidole ilipokatwa na damu
kutoka,ghafla ukasikika upepo
mkali na sauti ya
muungurumo.Mathew akageuka
kutazama pande zote lakini
hakuona kitu chochote aliingiwa
na hofu na mara akaanza kuhisi
mabadiliko katika mkono wa
Linah.Ngozi ilianza kuwa ngumu
na kucha zikabadilika.Linah
alikuwa anaunguruma kwa sauti
nzito ambayo ilimuogopesha
Mathew akamuachia Linah
akaruka pembeni akaanza
kushuhudia mabadiliko makubwa
yakitokea.Linah alikuwa
anabadilika na kuwa kiumbe cha
ajabu chenye umbo kama la
Mamba ambacho kilitoa sauti kali
ya kutisha.Kikapanua mdomo
wake na kuanza kumsogelea
Mathew ambaye alirudi nyuma
kujinusuru
“Kuna mabadiliko
yatatokea.Nitabadilika na kuwa
kiumbe mwingine lakini pamoja
na mabadiliko hayo naomba
tafadhali usiogope wala kukimbia
hutadhurika.Endelea na zoezi la
kukata kidole usiache”Mathew
akayakumbuka maneno ya Linah
“I need to help her ! akawaza
Mathew na kukunja ngumi
akasimama huku kiumbe kile cha
kuogofya kikiendelea
kumsogelea.Japo aliingiwa na
woga lakini hakukimbia na
kiumbe kile kikasimama huku
kikitoa muungurumo.
Mathew akapata ujasiri na
kukisogelea kile kiumbe akaanza
kupambana nacho akafanikiwa
kukiangusha chini.Lilitimka
vumbi kubwa lakini Mathew
aliendelea kuushikilia mkono
wake wa kulia na kufanikiwa
kukikata kile kidole
alichoelekezwa na Linah na mara
tu alipokikata kile kidole
kukatokea vumbi kubwa na
Mathew akapigwa kikumbo
akaanguka chini kama
furushi.Baada ya dakika chache
kukawa kimya na vumbi
lilipotulia Mathew akamuona
Linah akiwa amelala juu ya
kaburi
“Linah ! akaita Mathew na
kuinuka akamfuata.Linah alikuwa
anavuja damu kidoleni huku
akigugumia kwa maumivu
“Linah ! akasema Mathew na
kufungua mfuko wa dawa
waliokwenda nao akamtibu
jeraha.Linah akapata nguvu na
kuinuka akakaa akiweweseka
“Mathew ahsante sana
tunatakiwa kukitafuta kile kidole
chenye pete ulichokikata”
akasema Linah na Mathew
akawasha tochi yake ya simu
wakaanza kukitafuta kidole kile
na wakafanikiwa kukipata kikiwa
kimeanguka pembeni kidogo ya
mahala walipokuwa.Linah
akamuelekeza Mathew
kukichukua kidole kile
akakifunga katika kitambaa
cheupe akatafuta kaburi jipya
akachimba shimo katikati na
kukifukia
“Kazi imemalizika tunaweza
kuondoka” akasema Linah
wakaanza kuondoka mahala pale
huku bado Mathew akiendelea
kumshangaa Linah
“Ama kweli dunia ina
maajabu.Kitu gani kile
kimetokea? Huyu ni Linah Yule
ninayemfahamu au ni kiumbe cha
aina gani? Akajiuliza maswali
akiendelea kumfuata Linah
wakafika katika kituo cha basi
wakachukua piki piki mbili hadi
katika baa walikoacha gari lao
wakaingia na kabla ya Mathew
kuliwasha akaegemea kiti na
kuvuta pumzi ndefu akamtazama
Linah
“Drive ! akasema Linah
“Who are you? Akauliza
Mathew
“Mathew just drive !
akasema Lina na Mathew
akawasha gari wakaondoka
“Kama kweli huyu ndiye
Linah niliyekutana naye Arusha
kitu gani kimemtokea na
kuyabadili maisha yake na kuwa
namna hii? Niliyoyashuhudia ni
mambo ya kutisha sana ambayo
hayasimuliki.Mimi ni jasiri sana
lakini katika muda wote
niliofanya kazi hii ya ujasusi
sijawahi kukutana na mambo ya
kutisha kama haya niliyokutana
nayo muda mfupi uliopita”
akawaza Mathew
**********
Walifika nyumbani kwa
Mathew,akamganga Linah jeraha
lake halafu akampeleka katika
chumba cha wageni kwa ajili ya
kupumzika.Mathew akaingia
chumbani kwake na kujitupa
kitandani
“Mambo niliyoyashuhudia
leo,nilikuwa nikiyatazama katika
filamu na sikujua kama siku moja
ningeweza kuyashuhudia kwa
macho yangu.Huyu kweli ni
Linah Yule ninayemfahamu au ni
kiumbe amechukua umbo lake na
anataka kucheza na akili yangu?
Akajiuliza Mathew na kuinuka
akaenda kuchukua chupa ya maji
akanywa
Alihakikisha kamera zote za
usalama alizozifunga nyumbani
kwake zinafanya kazi vyema
kisha akaenda jikoni kuandaa
chakula.Baada ya kuandaa
chakula Mathew akaenda katika
chumba alimolala Linah taratibu
akaufungua mlango na
kuchungulia ndani bado Linah
alikuwa amelala.
“Who are you? Akajiuliza
Mathew akimtazama Linah na
kutaka kuufunga mlango mara
akasikia Linah akikohoa halafu
akasema
“Come in Mathew” akasema
Linah
“Ouh kumbe umekwisha
amka.Unajisikiaje sasa hivi?
Mathew akauliza na kuingia ndani
“Nina maumivu lakini
nitapona.Ahsante sana Mathew”
akajibu Linah na Mathew
akamtaka wakapate
chakula,Linah akainuka
wakaenda katika chumba cha
chakula wakapata chakula kimya
kimya.Mathew hakutaka kugusia
chochote kuhusu kile kilichotokea
kule makaburini.Alikuwa
anamtazama Linah kwa kuibia
“Mathew nimefurahi sana
kukuona tena baada ya miaka
kumi na tano” Linah akaanzisha
mazungumzo baada ya kuona
kumekuwa kimya sana.
“Ni muda mrefu sana huo na
mengi yametokea” akasema
Mathew na kuendelea kula
taratibu
Baada ya kumaliza kupata
chakula Mathew akamchukua
Linah wakaenda kuketi sehemu
ya juu ya nyumba yake ambako ni
maalum kwa kupumzikia.
“Linah it’s time to talk!
Akasema Mathew
“Mathew kabla ya kukueleza
chochote kwanza nataka
nikushukuru sana kwa kile
ulichokifanya.Sikufanya makosa
kukuchagua wewe na kweli
umenifanyia jambo kubwa sana
ambalo wengine wasingeweza”
akasema Linah
“Nahitaji kufahamu kila kitu
Linah.Mambo niliyoyashuhudia
kwa macho yangu leo yamenipa
hofu na nimekuwa najiuliza
maswali mengi bila majibu je
wewe ni Yule Linah niliyekutana
naye miaka kumi na tano iliyopita
au ni kiumbe amevaa mwili wa
Linah na kutaka kuiteka akili
yangu? Akauliza Mathew
“Mathew I’m
sorry.Nafahamu kilichotokea
kimekupa hofu kubwa sana lakini
mimi ni Linah Yule Yule
unayenifahamu japo maisha
yangu yamekuwa na mabadiliko
makubwa sana na nitakueleza kila
kitu” akasema Linah
“Kabla hujanieleza chochote
nataka kwanza unieleze ukweli
kuhusu mtu ambaye umemuua.Ni
kweli umeua?Nieleze ukweli bila
kunificha” akasema Mathew
“Ni kweli nimeua Mathew”
akasema Linah na kumtazama
Mathew
“Umemuua nani na kwa nini?
Mathew akauliza
“His name was Genes.He
was a nice guy and I loved him so
much.They forced me to kill him
! akasema Linah na kuinamisha
kichwa baada ya muda
akaendelea
“Jambo hili limeniumiza sana
na ndiyo maana ninataka niweke
nukta katika maisha haya.I’m
tired and I can’t do it anymore”
akasema Linah na kuanza
kumwaga machozi.Mathew
akampa kitambaa afute machozi
“Linah naomba unieleze
kuhusu maisha yako kwa miaka
kumi na tano tangu nilipokuacha
wakati ule hadi leo hii” akasema
Mathew.Linah akafikiri kwa
muda na kusema
“Ni mambo mengi
yametokea Mathew Mulumbi
siwezi kukueleza usiku huu
nikayamaliza.Nimepitia mambo
makubwa sana katika kipindi
hiki” akasema Linah
“Nieleze tafadhali” akasema
Mathew na Linah akanywa
mvinyo na kusema
“Nilitegemea safari hii
ningeweza kuyabadili maisha
yangu na kujaribu kuingia katika
mahusiano na mwanaume
niliyempenda kumbe nilikuwa
najidanganya” akasema Linah na
kunyamaza kidogo halafu
akaanza kumueleza Mathew
kuhusu kile kilichotokea

MWAKA 1 ULIOPITA

“Majirani naomba mnisaidie


ananinua!! Sauti ya mwanamke
akilia akiomba msaada ikamstua
Genes aliyekuwa mezani
akinyoosha nguo kwa ajili ya
kuwahi kanisani.Akaizima pasi na
kutulia kwa sekunde kadhaa ili
asikie ni wapi ilikotoka sauti
ile.Kwa mbali akasikia kama sauti
za watu wakizozana.Akapunguza
sauti ya redio ili aweze kusikia
vizuri sauti zile zilitokea
wapi.Aliamini sauti zile za
kuzozana zilitoka katika moja ya
chumba cha wapangaji wenzake
lakini hakuwa na uhakika ni
chumba kipi.Sauti ya mwanamke
akilia ikasikika tena na safari hii
akaamua kuzima kabisa redio
yake ili asikie vizuri.
"Jamani nisaidieni
ananiuaaa!! sauti ile ya
mwanamke ikarudia tena kuomba
msaada.Genes akaitambua sauti
ile,ilikuwa ni ya msichana jirani
yake aitwaye Naomi anayefanya
kazi katika hoteli ya Mbuni
"Naomi na mumewe
wanapigana.Mbona siku zote
wamekuwa wakiishi kwa amani?
akawaza Genes na kufungua
mlango wa chumba chake
akatazama kama kuna mtu yeyote
pale uani ambaye alikuwa
akiufuatilia ugomvi ule lakini
hakukuwa na mtu yeyote.Milango
yote ya vyumba vya wapangaji
wengine ilikuwa
imefungwa.Wakati akijishauri
afanye nini mara akasikia
kishindo kikubwa katika ukuta
uliounganisha chumba cha Naomi
na chumba chake.
"Watauana hawa.Ngoja
nikawaamue" akawaza Genes,na
taratibu akatoka chumbani kwake
na kuelekea katika chumba cha
Naomi.Akajaribu kugonga
mlango kwa nguvu na kisha
akaisikia sauti ya Naomi toka
ndani.
"Ingieni mlango
haujafungwa!
Genes akakinyonga kitasa na
kuingia ndani akajikuta amefunga
breki za ghafla kwa kitu
alichokishuhudia.Naomi na
mumewe Sheddy walikuwa
wakipigana wakiwa wamevaa
nguo za ndani.Kwa sekunde
kadhaa Genes alibaki amesimama
amepigwa na bumbuwazi na
macho yake yalikuwa yameelekea
katika mwili ule
mwororo,mweupe wa Naomi.
Kwa jinsi alivyokuwa
akiheshimiana na Naomi Genes
akaingiwa na woga na kutaka
kurudi nje
"Genes nisaidie anataka
kuniua huyu" Naomi akaomba
msaada.Badala ya kuwaamua
akabaki amemkodolea macho
Naomi.
"Genes nakuheshimu sana
nakuomba tafadhali utoke ndani
mwangu haraka.Usijaribu
kuingilia mambo yasiyokuhusu"
Sheddy mume wa Naomi
akasema kwa ukali akiwa
ameshika kisu mkononi.
"Genes usimsikilize huyu
shetani...nisaidie ataniua! Naomi
akapiga ukelele.
"Sheddy tafadhal........"
Genes akajaribu kutamka kitu
lakini Sheddy akamzuia
"Genes nakwambia toka
humu ndani mwangu haraka
sana.Ugomvi wangu mimi na mke
wangu haukuhusu tafadhali
ondoka haraka sana kabla
sijakufanyia kitu kibaya" Sheddy
akasema kwa ukali huku
ameshika kisu kikali
"Genes nisaidie!! .....Naomi
akalia huku akijitahidi kujitoa
katika mikono ya Sheddy.Genes
akamuonea huruma Naomi
alivyokuwa akilia akashikwa na
hasira
"Sheddy nakuomba tafadhali
usiendelee kumpiga mkeo" Genes
akasema taratibu akijaribu
kumsihi Sheddy amuachie
mkewe.
"Genes naona hujanifahamu
vizuri mimi ni
nani.Nimekwambia ugomvi
wangu mimi na mke wangu
haukuhusu" Sheddy akafoka na
kuanza kumsogelea Genes.Kwa
ufundi wa aina yake Sheddy
akajikuta amedakwa mkono na
kunyang’anywa kisu halafu
akawekwa chini.
"Genes nikiinuka hapa
nitakuua!Unaingilia mambo
yasiyokuhusu kwa nini? Ugomvi
kati yangu mimi na mke wangu
unakuhusu nini? akafoka Sheddy
"Hata kama amekukosea
Sheddy hukupaswa
kumpiga.Kama mwanaume
ulitakiwa uwe na busara ukae
chini na mkeo na muongee kama
mke na mume na kisha
muyamalize matatizo yenu na
maisha yaendelee.Ninamfahamu
Naomi vizuri ni mwanamke
anayejiheshimu sana tofauti na
wanawake wengine hapa
mtaani.Jaribu kukaa na mkeo
muongee na muyarekebishe yale
yote yaliyotokea.Mnapopigana
mnajiabisha ninyi
wenyewe.Tafadhali ndugu yangu
nakuomba kama mwanaume
mwenzako kaa na mkeo na
mjaribu kutafuta suluhu ya
matatizo yenu" Genes akasema
“Sitaki suluhu ya aina yoyote
nimechoka na simtaki tena hapa
kwangu” akasema Naomi na
kukusanya nguo za Sheddy
akaziweka katika sanduku dogo
akalitupa nje.Sheddy akataka
kuleta vurugu lakini Genes
alijitahidi kumdhibiti na
akachukua sanduku lake
akaondoka huku akiahidi kulipa
kisasi
**********
Sauti ya mlango kugongwa
ndiyo iliyomstua Genes toka
usingizini.Tayari ni saa tatu za
usiku.Taratibu akainuka na
kwenda kuufungua mlango
akakutana na Naomi akiwa na
tabasamu lenye aibu kwa
mbali.Genes akapatwa na mstuko
kidogo kwa jinsi Naomi
alivyokuwa amependeza.Kwa
namna alivyokuwa akimuangalia
ni kana kwamba ilikuwa ni mara
ya kwanza anamuona.Naomi pia
aligundua kwamba Genes alikuwa
akimuangalia akaona aibu na
kutazama chini.
"Naomi karibu sana"
akasema Genes
"Genes samahani kwa
kukusumbua" akasema Naomi.
"Usijali Naomi.Karibu ndani"
akasema Genes na kuufungua
mlango zaidi ili Naomi apite.Jioni
hii Naomi alikuwa amependeza
vilivyo ndani ya mavazi
meupe.Huku akiona aibu Naomi
akaingia chumbani kwa
Genes.Mkononi alikuwa
ameshika mfuko mweusi.
"Karibu kiti Naomi" Genes
akamkaribisha Naomi
"Ahsante sana Genes"
akajibu Naomi na kuketi
sofani.Ilikuwa ni mara ya kwanza
kwa Naomi kuingia chumbani
kwa Genes.
" Habari za Jumapili? Genes
akaanzisha maongezi baada ya
kumpatia Naomi kinywaji
"Habari nzuri Genes.Sijui
wewe umeshindaje?
"Nimeshinda salama"
akasema Genes
"Genes nimekuja
kukushukuru kwa msaada wako
wa kumtoa yule jamaa ndani
kwangu.Nilikwisha jaribu kutaka
kumuondoa lakini nikashindwa
kwa sababu kila nilipojaribu
kumwambia simuhitaji tena
alinitishia kuniua ikanibidi kukaa
kimya.Vile vile samahani sana
kwa matusi yote aliyokutukana"
Naomi akasema huku akiangalia
chini.Uso wa Genes ukajenga
tabasamu pana sana.
"Usijali Naomi.Ni mambo ya
kawaida kutokea na wala wewe si
wa kwanza kukorofishana na
mumeo" Akasema Genes na
kumfanya Naomi atabasamu
akainua kichwa na kusema
"Yule hakuwa mume
wangu.Nilikuwa naishi naye
kupoteza wakati lakini lakini
hatukuwa na mipango yoyote ya
mbeleni kwamba tuoane na kuwa
mke na mume" Naomi akasema
" Sikufurahishwa na kitendo
alichokifanya cha kukupiga ndiyo
maana nilipandwa na hasira
nikatakja kumfundisha adabu"
Genes akasema
"Ulifanya kazi kubwa
Genes,bila wewe nadhani
angeniulia ndani kwani tayari
alikwisha pandwa na hasira"
Naomi akasema
"Kwa sasa jitahidi kuishi
mwenyewe na kuyatengeneza
maisha yako" akasema Genes
"Kweli kabisa
Genes.Natakiwa niitumie nafasi
hii kujitengenezea msingi mzuri
wa maisha yangu" akasema
Naomi
"Genes mimi si
mkaaji.Nimekuja kukushukuru
vile vile kuna mzigo huu kidogo
nimekuletea" Akasema Naomi
huku akiinuka sofani.
"Nashukuru sana Naomi.Siku
yoyote muda wowote ukihitaji
msaada wa namna yoyote usisite
kuniambia.Au kama akirudi yule
jamaa na kuanza kukuletea fujo
usiogope kunitaarifu.Si katika
shida tu,hata siku ukijisikia
mpweke na unahitaji mtu wa
kuongea naye na kubadilishana
mawazo mimi niko hapa,usisite
kunigongea mlango au hata
kunipigia simu.Naomba unipatie
namba yako ya simu" Genes
akasema na kisha
wakabadilishana namba na
Naomi akaondoka
Linah akafuta machozi na
kumtazama Mathew
“Hivyo ndivyo nilivyoanza
mahusiano na Genes na
alinifahamu kwa jina la
Naomi,sikutaka kutumia jina
langu la Linah.I hate that name”
akasema Linah na kuinamisha
kichwa
“Nini kilifuata hadi
ukamuua? Mathew akauliza na
Linah akaendelea kumsimulia
**********
" Siamini kama yule kijana
ameondoka nyumbani
kwangu.Namshukuru sana Genes
kama si yeye,Sheddy katu
asingeondoka.Kuna nyakati
najiuliza ni kwa nini nilijiingiza
katika mahusiano na yule
muhuni? Sijui alinipa nini
nikakubali kumpa mwili wangu
auchezee.Sikujua kwamba huko
mtaani watu walikuwa
wakinicheka na kunishangaa
msichana mrembo kama mimi
kuishi na muhuni kama
yule.Naujutia muda wangu
nilioupoteza kwa kijana yule
asiyekuwa na mbele wala
nyuma.I was so stupid" akawaza
Naomi akiwa amejilaza kitandani
na kwa mbali machozi ya majuto
yakamtoka.
"Pamoja na yote yaliyotokea
natamani kupenda tena.Natamani
nimpate mwanaume wa maisha
yangu ambaye nitampenda na
kuishi naye kwa raha furaha na
amani hadi nitakapofika uzee,
mwanaume ambaye atanipenda
atanithamini na
kunijali,mwanaume ambaye
nitajenga naye familia yenye
furaha na upendo
mkubwa.Nikifanikiwa kumpata
mwanaume kama Genes
nitafurahi sana.Kaka yule
ananivutia kwa tabia zake.Ni
mpole,ana heshima,anapenda
watu,na anapendwa na kila
mtu.Anajipenda na ni mtu
mwenye kujituma katika
kujitafutia maendeleo.Nitafurahi
kama ningepata kijana kama
yule" akawaza Naomi na mara
sura ya Genes ikamjia kichwani
akajikuta akitabasamu.
"Nahisi kuanza kuvutiwa
kuwa karibu na Genes.Sikuwa
nimegundua kama Genes ni
kijana mcheshi na ambaye
hachoshi kuwa naye karibu.Toka
nimehamia katika nyumba hii
Genes alionesha kutaka kujenga
mazoea na ukaribu nami lakini
nilikuwa nikimkwepa.Wanaume
hawa wenye sura nzuri
ninawaogopa sana kwani
walikwisha niumiza vya kutosha
na ndiyo maana nikaamua kuwa
na Yule kijana asiyejielewa"
Naomi akajigeuza na kuendelea
kuwaza huku akitabasamu
"Nitajaribu kuanza kujenga
mazoea na Genes ambaye nahisi
kuanza kuvutiwa naye
ghafla.Kwa namna
anavyoonekana Genes yuko
tofauti sana na wanaume wengine
walaghai.Toka nimehamia hapa
sijawahi kumuona hata mara moja
Genes ameleta mwanamke hapa
nyumbani.Anajiheshimu sana
huyu kaka na ndiyo maana
ninajikuta nikivutika kuwa naye
karibu.Nataka kufahamu
chimbuko lake,nataka kufahamu
maisha yake,vitu
anavyopenda,vitu asivyopenda na
kikubwa zaidi nataka kufahamu
kama ana mchumba au
hana.Kama hana mchumba basi
anaweza akanifaa sana.Ana kila
sifa ya mwanaume ninayemuhitaji
kwa sasa.Sina haja ya kwenda
mbali kutafuta mawe wakati
dhahabu ninayo hapa karibu"
akawaza Naomi huku
akitabasamu halafu akajifunika
shuka na kujaribu kutafuta
usingizi
Linah akamtazama Mathew
halafu akauliza
“Mathew huvuti sigara?
“Hapana sivuti sigara”
akajibu Mathew
“Nilijenga ukaribu mkubwa
sana na Genes na kadiri
tulivyozidi kuwa karibu ndivyo
nilivyozidi kumpenda hadi
nilipoamua kuwa jasiri na
kumueleza ukweli
wangu.Nilimualika katika sherehe
ya kumuaga mmoja wa
wakurugenzi wa kampuni
niliyokuwa ninafanya kazi na
nilipanga usiku huo tuufungue
ukurasa mpya kati yetu” akasema
Linah na kuendelea kumsimulia
Mathew
**********
Saa ya ukutani ilionyesha
ni saa moja na dakika ishirini za
jioni pale mlango wa chumba cha
Genes ulipogongwa.Genes
akaufungua na kubaki na
mshangao akimshangaa Naomi
alivyopendeza..
"Wow ! Naomi you look like
an angel tonight" akasema Genes
kwa mshangao huku akitabasamu
" Karibu ndani Naomi."
akasema Genes
"Ahsante genes.Nadhani
ndiyo muda wenyewe
huu.Tunaweza kuondoka kama
uko tayari”akasema Naomi na
kutangulia nje.Genes akamalizia
kujiandaa halafu akatoka nje na
kushangaa baada ya kulikuta gari
jipya la kifahari lenye rangi
nyeusi lilikuwa limeegeshwa nje
ya nyumba ile.Wakati Genes
akiangaza kumtafuta
Naomi,mlango ukafunguliwa
akashuka Naomi na Genes
akabaki anashangaa.Naomi
akamtaka kuingia garini akaondoa
gari na kumuacha Genes
akishangaa.
"Naomi sikujua kama wewe
ni dereva mzuri namna hii"
akasema Genes huku
akitabasamu.Naomi akatabasamu
na kusema
"Ninafahamu kuendesha gari
lakini mara nyingi sipendi
kuendesha.Ndiyo maana hata hili
gari huwa ninalihifadhi kwa
kaka"akasema Naomi na
kumfanya Genes azidi kushangaa.
"Hili gari ni lako? akauliza
Genes.
"Ndiyo Genes.Hili ni gari
langu mwenyewe.Kaka yangu
anafanya biashara ya kuagiza na
kuuza magari toka nje ya nchi
nilimuagiza anitafutie gari zuri
akaniletea hili"
"Hongera sana.Ni gari zuri"
akasema Genes.
Safari ikaendelea kimya
kimya.Ni sauti ya muziki
iliyokuwa ikisikika pekee.
Saa mbili na dakika kumi
wakawasili katika ukumbi
inamofanyika sherehe.Nje ya
ukumbi magari mengi yalikuwa
yameegeshwa na watu kadhaa
walikuwa wamesimama nje ya
ukumbi ule wakibadilishana
mawili matatu.Naomi
akasimamisha gari katika
maegesho.Haraka haraka Genes
akashuka na kumfungulia mlango
Naomi akashuka huku
akitabasamu.Genes akamshika
mkono Naomi wakaanza
kuongozana kuelekea
ukumbini.Watu waliokuwa
wamesimama pale nje ya ukumbi
wote wakapigwa na
mshangao.Walikuwa ni
wafanyakazi wenzake na Naomi.
Baada tu kuingia ukumbini
Naomi akakutana na watu wanne
waliokuwa wamesimama karibu
na mlango wa kuingilia na
mikononi mwao walikuwa na
glasi za vinywaji.Wote
walipomuona Naomi akiwa
ameongozana na Genes
wakasitisha maongezi yao
wakabaki wakimtazama kwa
mshangao
" Wow ! Naomi..you are
amazing tonight ! " akasema mzee
mmoja mnene aliyevaa suti ya
kijivu.
Naomi akawasogelea
akawasalimu wote kwa
adabu,Genes naye alifanya kama
alivyofanya Naomi.
" Naomi who is this
handsome man? akauliza yule
mzee mnene ambaye alikuwa
mchangamfu sana.
Naomi akatabasamu na kisha
akasema.
"Anaitwa Genes ni rafiki
yangu" akasema Naomi na
kumtambulisha Genes kwa wale
wakuu wake wa kazi.Wahudumu
waliokuwa wakizunguka na
masinia ya vinywaji walifika pale
walipokuwa wamesimama.Genes
akachukua glasi mbili za mvinyo
mwepesi akampatia moja
Naomi.Maongezi
yakaendelea.Wazee wale
walionekana kuvutiwa sana na
Genes na hawakutaka yeye na
Naomi wandoke pale.Naomi
hakukaukiwa na
tabasamu.Alifurahi kupita
kiasi.Kila mtu aliyemfahamu
alikuwa akimtambulisha kwa
Genes.Kila mtu alimsifu Naomi
kwa kuwa na kijana mzuri kama
Genes.Hakuna aliyefahamu kama
Genes na Naomi ni marafiki wa
kawaida tu na hawakuwa wapenzi
lakini kwa muonekano wao usiku
huu walionekana ni kama
wapenzi waliopendana sana.
Ilipofika saa tatu za usiku
sherehe ikaanza rasmi.Wageni
wote waliokuwa wamesimama
wakaombwa waketi vitini na wale
waliokuwa nje wakaombwa
waingie ndani.Naomi na Genes
wakachagua meza ya peke yao
iliyokuwa pembeni sehemu
lliyokuwa na mwanga hafifu
wakakaa.Wakaangaliana kwa
sekunde kadhaa usoni wote
wakatabasamu.Naomi akatazama
chini halafu akainua kichwa
akataka kusema neno lakini muda
huo huo muhudumu akafika
wakachukua tena glasi mbili za
mvinyo mwepesi.
"Nimefurahi sana Naomi kwa
kunialika katika sherehe
hii.Nimefurahi kuona namna
wafanyakazi wenzako
wanavyokupenda" akasema
Genes
"Genes sifahamu ni kwa nini
nimejikuta nikitokea kuwa
kipenzi cha watu wengi wa hapa
kazini kwetu.Wale wazee
tuliokuwa tukiongea nao ni kweli
wananichukulia mimi kama mtoto
wao.Wananitunza na kuhakikisha
kwamba ninakuwa na furaha siku
zote.Nashukuru Mungu
hawakuwahi kufahamu kwamba
ninaishi na yule muhuni
nyumbani kwangu.Iwapo
wangegundua heshima yangu
ingeshuka mno" akasema Naomi
halafu akainamisha kichwa
alikuwa akiona aibu.
"Naomi samahani kwa
kukuuliza swali kama hili Yule
kijana uliyekuwa ukiishi naye
ulimpenda kwa dhati?
Naomi akainama akafikiri
kisha akasema
"Genes wewe ni rafiki yangu
na sitaki kukuficha kitu.Sikuwa
nikimpenda Yule kijana.Sheddy
alikuwa akifanya kazi katika
kampuni yetu.Alikuwa
mwongozaji watalii.Siku moja
nilikwenda kikazi katika moja ya
hoteli zetu iliyoko nje ya
Arusha.Jioni nikiwa nimepumzika
alikuja yule kijana na kuanza
kuongea na mimi.Alikuwa
akipiga gita huku akiimba
nikafurahi sana.Nilifurahi kupata
mtu wa kuongea naye kwa sababu
nilikuwa nahisi upweke
sana.Toka hapo ndipo urafiki kati
yangu naye ulipoanza.Tulitokea
kuwa marafiki wakubwa
sana.Kwa bahati mbaya kijana
yule alifukuzwa kazi katika
kampuni yetu na hakuwa na
mahala pengine pa kwenda na
kama rafiki yake nikamuonea
huruma na kumpa hifadhi
nyumbani kwangu.Kwa kweli
ninajuta sana kila nikikumbuka
muda nilioupoteza na yule
kijana.Nilikuja kugundua
kwamba alikuwa ni kijana
mlevi,mvuta bangi na mwingi wa
wanawake.Kwa kuwa alifahamu
kwamba mimi sina kauli kwake
alinipeleka alivyotaka.Kila
nilipopata mshahara aliuchukua
na kuupeleka katika starehe.
Sikuwa na kitu cha kufanya zaidi
ya kulia.Nitaendelea kukushukuru
sana kwa kunisaidia kumuondoa
yule muhuni nyumbani kwangu"
akasema Naomi kwa sauti yenye
majuto ndani yake.Genes
akamuangalia kisha akauliza
"Naomi ikiwa atakuja tena na
kukuomba msamaha kwamba
anataka mrudiane utakuwa tayari
kumsamehe? akauliza Genes na
kumfanya Naomi acheke kidogo
"Mimi na yeye tumekwisha
fikia mwisho.Zaidi ya yote
nimeyaanza maisha mapya yenye
furaha na amani.Nimepata
marafiki wapya na mmoja wao ni
wewe ambaye leo hii umenifanya
niwe queen of the night.Genes
kwa kuwa nawe hapa usiku wa
leo kumenizidishia heshima
sana.You are a gentleman.Kila
mtu anakuheshimu.Ahsante sana
kwa kampani yako" akasema
Naomi.Genes akatabasamu na
kusema
"Lakini wafanyakazi
wenzako wote wanafahamu
kwamba mimi ni mchumba
wako.Hakuna anayefahamu
kwamba mimi na wewe ni
marafiki wa kawaida" akasema
Genes na wote wakaangua
kicheko.
"Natamani ingekuwa kweli
kwamba Genes ni mchumba
wangu.Kila mtu hapa anafahamu
kamba Genes ni mchumba
wangu.Ni kijana mtanashati,
anayejiheshimu,mkarimu na zaidi
ya yote ana tabia nzuri.Ana sura
nzuri ya kupendeza,kwa ujumla
kila kitu alichojaliwa kijana huyu
kinanivutia sana.Nitajitahidi ili
aweze kuwa wangu.Genes must
be mine" Akawaza Naomi huku
akimuangalia Genes usoni.
"Mbona unaniangalia hivyo
Naomi? Genes akamstua Naomi
aliyekuwa amemkazia macho.
" Ouh sorry Genes nina
furaha iliyopitiliza usiku wa
leo.Umenifanya nifurahi sana"
akasema Naomi akachukua glasi
yake akanywa funda moja halafu
akamuangalia tena Genes na
kuuliza
"Genes wazazi wako
wanaishi wapi? Genes akakohoa
kidogo akasema
"Wazazi wangu
mimi wanaishi Mbeya ambako
ndiko nyumbani kwetu.Kwa sasa
wamekwisha staafu katika
utumishi wa umma na
wanapumzika wakiufurahia uzee
wao"
"Mko watoto wangapi katika
familia yenu?
"Tuko watoto tisa na mimi ni
mtoto wa saba.Walionitangulia
wote wamekwisha oa na kuolewa
na tayari wana familia zao"
akasema Genes.
"Lini unategemea kuwa na
familia yako na wewe? akauliza
Naomi.Genes akatabasamu na
kusema
"Pindi nikimpata mwanamke
wa ndoto zangu,ambaye
nitampenda na atakayenifanya
nifurahi na kuishi kama mfalme
ndani ya hii dunia" akasema
Genes
"Nipe mimi kazi ya
kukutafutia huyo msichana
unayemtaka.Nitampata ndani ya
siku moja tu" akasema Naomi na
wote wakacheka.
"Vipi kuhusu wewe? Wazazi
wako wanaishi wapi? akauliza
Genes
"Mimi wazazi wangu wote
walikwisha fariki.Walifariki wote
kwa pamoja katika ajaali ya
gari.Katika familia yetu tuko
watoto watatu tu" akasema
Naomi na wote wakacheka
"Pole sana Naomi.Sikujua
kama wazazi wako wote
wamekwisha tangulia mbele za
haki" akasema Genes
"Ahsante sana Genes.Ni
mambo ya kawada kwa binadamu
na hatuna namna ya kukikwepa
kifo" akasema Naomi
wakaendelea na mazungumzo
mengine huku sherehe ikiendelea
Hotuba mbalimbali
zilisomwa huku nyingi ya hotuba
hizo zilikuwa ni za kumpongeza
mkurugenzi anayeondoka kwa
utendaji wake wa kazi
uliotukuka.Baada ya hotuba
kikafuata kipindi cha kukabidhi
zawadi mbali mbali kwa
mkurugenzi anayeondoka na
kisha mkurugenzi mpya
akakaribishwa rasmi halafu
wafanyakazi wote wakajumuika
kwa chakula.Baada ya zoezi la
chakula kukamilika muongozaji
akatanganza kinachofuata ni
muziki.
Saa tisa za usiku sherehe
ikafungwa.Baada ya kuagana na
watu wengine Naomi na Genes
wakaingia katika gari lao na
kuondoka.
"Sherehe ilipendeza sana"
akasema Genes wakiwa garini
lakini Naomi hakujibu kitu.Genes
akakumbuka kwamba Naomi
hakupenda maongezi wakati
akiendesha gari.
Waliiacha barabara
iliyokuwa ikielekea nyumbani
kwao wakachepuka
kushoto.Genes akafikiri Naomi
amepotea njia lakini kila
alipomtazama hakutaka kuamini
kama ni kweli Naomi amepotea
njia.
Baada ya mwendo wa dakika
kumi hivi gari ya Naomi
ikapunguza mwendo na kuwasha
taa ya kushoto kuashiria kwamba
ilikuwa ikielekea katika geti la
hoteli kubwa ya kitalii ya Kobe
Village moja ya hoteli kubwa na
yenye hadhi ya juu katika ukanda
huu wa afrika mashariki.Naomi
akalipeleka gari hadi katika
maegesho kisha akamgeukia
Genes.Akauinua mkono wake wa
kushoto akamshika bega
Genes.Wakatazamana kisha
Naomi akasema
"Genes usiku wa leo tutalala
hapa.."
Genes akamtazama Naomi
asiamini kile alichokisikia.
"Naomi unasemaje? Huku
akitabasamu Naomi akasema
"Genes usiku wa leo tutalala
hapa" akarudia Naomi halafu
akafungua mlango wa gari na
kushuka.Genes ambaye
alionekana kama vile
amemwagiwa maji ya baridi naye
akashuka garini.Naomi
akamshika mkono wakaanza
kupiga hatua kuelekea ndani ya
hoteli ile kubwa ya kifahari.
Naomi alisalimiana na
wahudumu wa
mapokezi.Ilionekana ni kama vile
walikuwa wakifahamiana kwa
sababu baada ya salamu
walitaniana kidogo ikiwa ni
pamoja na kumsifia Naomi namna
alivyopendeza usiku
ule.Mhudumu mmoja akampatia
Naomi kadi ya kufunguliwa
mlango
"Kila kitu ni kama
ulivyoelekeza" akasema
muhudumu yule wakati akimpatia
Naomi ufunguo
"Twende zetu Genes "
akasema Naomi wakaanza
kuondoka kuelekea chumbani.
"Tonight its just me and you
Genes.Siwezi kusubiri zaidi ya
hapa.Uvumilivu umenishinda
.Siwezi kuendelea kuutesa moyo
wangu wakati uwezo wa
kukwambia ukweli
ninao.Vyovyote vile
atakavyonichukulia I don’t
care.Nina kila sababu za kuamini
kwamba Genes ndiye mwanaume
wa maisha yangu.Ana kila kitu
ninachokihitaji toka kwa
mwanaume wa ndoto
zangu.Siwezi kuendelea kupoteza
muda wakati mwanaume ninaye
mikononi mwangu.Siwezi
kusubiri anitamkie yeye.Nataka
asubuhi ya kesho niamke nikiwa
mikononi mwa Genes.Sina hakika
na hisia zake kwangu lakini nina
kila sababu ya kuamini kwamba
hata yeye ananipenda.Nitamuanza
mimi kumweleza na wala
sintaogopa kitu.Nikiendelea
kusubiri wanawake wengine
watamnyakua toka mikononi
mwangu.Sitaki jambo hilo litokee
na ndiyo maana usiku wa leo ni
usiku wa ukweli mtupu.Kuna
msemo usemao try and fail but
don’t fail to try.." akawaza Naomi
wakati wakitembea kimya kimya
kuelekea katika chumba ambacho
watalala kwa usiku huo.
Hatimaye wakafika katika
chumba namba 104.Naomi
akapitisha kadi katika kitasa na
kuufungua ule mlango wakaingia
ndani.
"Karibu ndani Genes"
akasema Naomi .
"Ahsante sana Naomi"
akajibu Genes na kuingia mle
chumbani.Kilikuwa ni chumba
kikubwa na kizuri sana.Naomi
akafunga mlango na kwenda
kuketi katika sofa alilokuwa
ameketi Genes.Akamwangalia
Genes na kutabasamu na kisha
akasema.
"Genes leo nina furaha ya
ajabu sana.Nashindwa nikueleze
vipi ili uweze kunielewa.Furaha
niliyonayo haielezeki.Ninajihisi
ni kama vile ninapaa mawinguni.
" akasema Naomi .Genes
akatabasamu na kusema.
"Naomi nimefurahi sana
kukuona ukiwa na furaha ya
namna hiyo.Toka nimekufahamu
sijawahi hata mara moja kukuona
ukiwa na furaha ya namna
hii.Nitafurahi zaidi kama hilo
tabasamu lako halitatoweka usoni
mwako” akasema Genes huku
akitabasamu.
“Genes furaha hii niliyonayo
leo isingewezekana bila ya
wewe.Wewe ndiye uliyenifanya
leo hii nikawa na furaha ya aina
yake.Katika usiku wa leo
nimepata heshima kubwa toka
kwa wafanyakazi wenzangu na
yote hii ni kwa sababu ya uwepo
wako pembeni yangu.Genes sioni
neno zuri zaidi la kiswahili la
kuonyesha shukrani zangu kwako
zaidi ya ahsante sana.” akasema
Naomi.Genes akatabasamu na
kusema
“Naomi kama
nilivyokwambia awali kwamba
unastahili kuwa na furaha hii
kubwa.Ninafurahi kuwa mmoja
wa watu wenye kuchangia kuleta
tabasamu katika uso
wako.Ninajisikia fahari kubwa
kuwa karibu na mtu kama wewe
..." akasema Genes
Taratibu Naomi akainuka
pale sofani na kuelekea katika
friji.
"Genes unatumia kinywaji
gani usiku huu? akauliza Naomi
huku akilifungua friji.
"Chochote kile ambacho
utapendezwa nikitumie nitafurahi
sana" akasema Genes huku
akiilegeza tai yake.Naomi
akachukua vipande vya barafu
akaweka katika glasi na
kumimina mvinyo.
"Genes kwa furaha
niliyonayo leo naomba
tugonganishe glasi na kutakiana
furaha ya kudumu maishani"
akasema Naomi na kila mmoja
akainua glasi yake juu.
" Kwa furaha ya kudumu
maishani cheers !! " wakasema
wote kwa pamoja na
kugonganisha glasi zao na kila
mmoja akanywa funda
moja.Naomi akaweka glasi
mezani akamtazama Genes kisha
akatabasamu
" Genes najua unajiuliza
mswali mengi sana kwa nini tuko
hapa usiku wa leo.? akasema
Naomi huku akimuangalia Genes
ambaye hakujibu kitu zaidi ya
kutabasamu.Naomi akaendelea
"Genes kwanza kabisa
naomba radhi kwa
kutokufahamisha toka mapema
kuhusu suala la kuja hapa
hotelini usiku huu.Haikuwa
dhamira yangu kufanya hivi
.Sikuwa nimepanga kama nitakuja
hapa hotelini usiku huu .Maamuzi
ya kuja hapa niliyafanya tukiwa
ukumbini hivyo nikamtumia
ujumbe wa simu Latifa rafiki
yangu yule tuliyemkuta
mapokezi, aniandalie chumba
kimoja kwa ajili yangu na mgeni
wangu.Kilichonifanya nifanye
maamuzi hayo ni kutokana na
furaha ya ajabu niliyoipata tukiwa
ukumbini.Nilihisi kama niko
katika dunia nyingine
kabisa.Nilihisi ni kama ninaelea
mawinguni.Wewe ndiye
uliyenifanya nikawa na furaha
kubwa na ya aina yake .Sikutaka
furaha hii iishie ukumbini
pekee.Nilihitaji niendelee
kufurahi zaidi na zaidi nikiwa
nawe.Hii ni sababu kubwa
iliyonifanya niamue kuchukua
chumba na kuja hapa na wewe
baada ya sherehe
kumalizika.Endapo tungerudi
nyumbani kila mmoja
angejifungia chumbani kwake na
kulala na furaha yangu ingeishia
hapo.Genes nimeheshimika na
kuthaminiwa leo kwa sababu
yako.Genes..." Naomi akasita
kuendelea,akamtazama Genes
usoni kisha akachukua glasi yake
ya mvinyo akanywa funda moja
na kusema.
"Genes,kwa muda huu mfupi
ambao nimekuwa nawe kama
rafiki na mtu wangu wa
karibu,naomba nikiri kwamba
ninajiona ni msichana mwenye
mabadiliko makubwa
sana.Najiona niko tofauti sana na
Naomi yule wa kipindi cha
nyuma.Umenifanya nijitambue
zaidi.Kwa sasa ninaiona thamani
yangu na maisha
yangu.Nimekuwa na mtazamo
mpya wa maisha yangu ya sasa
na ya baadae.Ninajiamini
zaidi.Kwa ujumla Genes una
mchango mkubwa katika
mabadiliko haya makubwa ya
maisha yangu kitu
kinachokufanya uwe ni mtu wa
muhimu sana kwangu.Ni sababu
hiyo inayonifanya nijikute
nikihitaji kuwa nawe kila
dakika.Nikiwa nawe najua
nitacheka,nitafurahi na kuhisi
furaha ya ajabu" Naomi
akanyamaza akachukua glasi yake
ya mvinyo akanywa .Genes
akafungua mdomo wake na
kutaka kusema kitu lakini Naomi
akawahi kumzuia
"Let me finish Genes"
akasema Naomi ambaye kwa
usiku huu alionekana kuwa
mwongeaji sana hasa kutokana na
mvinyo ambao amekuwa akinywa
mfululizo.
"Genes nafahamu kwamba
kuwa nawe kila saa kila dakika ni
jambo lisilowezekana kutokana
na majukumu tuliyonayo.Kwa
mfano kuanzia jumatatu
sintakuwepo kwa muda wa mwezi
mmoja.Nitakuwa katika hoteli
yetu mpya iliyofunguliwa
Zanzibar.Kuna shughuli
ninakwenda kuifanya kule.Kwa
maana hiyo kwa muda wa mwezi
mzima sintaiona sura yako.Genes
nimekuzoea sana na kumaliza
mwezi mzima bila kuitia machoni
sura yako kwangu mimi ni kama
mwaka na ndiyo maana nimeona
walau kwa usiku huu mmoja
tukawa pamoja ,tukafurahi
pamoja kwa sababu sintakuona
kwa muda wa mwezi
mzima.Tafadhali Genes naomba
ukubali kwamba utakuwa nami
usiku wa leo na ninaomba
usikasirike kwa maamuzi haya ya
kuja hapa hotelini .Nimefanya
hivi kwa kuogopa pengine
ningekwambia mapema
ungenikatalia.Just for tonight
Genes" Akasema Naomi huku
akimuangalia Genes kwa
huruma.Genes alikaa kimya
akimtazama Naomi.
"Say yes Genes" akasema
Naomi kwa sauti laini yenye
kubembeleza baada ya kuona
Genes hajibu chochote.Genes
akatabasamu na kusema.
"Naomi sipati neno zuri la
kuweza kuielezea furaha
niliyonayo.Furaha hii kubwa
niliyonayo inatokana na mambo
mawili.Kwanza nina furaha
kubwa kukuona ukiwa na furaha
sana siku ya leo.Ninapokuona
ukiwa na furaha kiasi hiki
ninafarijika na kujawa na furaha
mara mbili zaidi yako.Kama
rafiki na mtu wako wa karibu
nitajitahidi kuhakikisha kwamba
furaha hii uliyonayo inadumu
milele.Tabasamu hili la kimalaika
lililoko usoni mwako halikauki
milele" akasema Genes na
kumfanya naomi acheke kicheko
laini na uso wake ukachanua kwa
tabasamu pana sana.
"Thank you Genes you are so
sweet" akasema Naomi.Genes
akatabasamu na kusema .
"Sababu ya pili inayonifanya
nijawe na furaha ni kuwa karibu
nawe .Kwa muda mrefu
nimekuwa nikitafuta nafasi ya
kuwa nawe karibu kama marafiki
nikaikosa kutokana na wewe
kuwa tayari katika
mahusiano.Namshukuru Mungu
kwa sababu nimeipata tena nafasi
hii ya kuwa karibu
nawe.Natamani ukaribu huu
uendelee milele na milele ili
niweze kuufurahia ucheshi
wako,kusuuzika moyo na na
tabasamu lako adhimu,na kama
usemi usemao ukikaa karibu na
waridi na wewe utanukia harufu
ya waridi,ninataka niwe karibu
nawe ewe waridi ili niweze
kunukia.Kuhusu kuwa nawe hapa
hotelini kwa usiku huu nakosa
neno zuri la kukueleza namna
nilivyofurahi kwa nafasi hii
adimu sana. Hukupaswa kuogopa
kunitaarifu kuhusu kuja hapa
hotelini.Nisingeweza kukukatalia
Naomi.Jambo lolote ambalo
linakupa wewe furaha niko tayari
kulifanya" akasema
Genes.Kikapita kimya cha dakika
moja Naomi akasema
"Genes bado hujajibu swali
langu nilikuuliza kwamba uko
tayari kuwa nami kwa usiku huu?
Jibu ndiyo au hapana " akasema
Naomi.Genes akanywa funda
moja la mvinyo halafu akasema
" Naomi hakuna mwanaume
yeyote katika dunia hii anayeweza
kukataa ombi lako la kutaka kuwa
naye hasa kwa usiku kama
huu.Jibu ni ndiyo nitakuwa nawe
kwa usiku huu" akasema
genes.Naomi akainuka kwa
furaha na kwenda kumkumbatia
halafu akaenda kuchukua chupa
ya mvinyo na kujiongezea katika
glasi .
"Naomi kuna jambo nataka
kukuuliza" akasema Genes kwa
sautui yenye wasi wasi fulani
ndani yake.
"Uliza Genes" akajibu Naomi
"Mbona umechukua chumba
kimoja badala ya viwili? Tutalala
vipi? Akauliza Genes huku
akicheka..Naomi naye
akatabasamu na kusema
"Tutalala humu humu
.Chumba hiki ni kikubwa na kina
nafasi ya kutosha kwa watu
wawili.Dhumuni la kutaka
tusirudi majumbani kwetu ni
kutaka kuwa karibu nawe.Kwa
maana hiyo tutalala chumba
kimoja na kitanda kimoja.Are you
scared? Akauliza Naomi kwa
sauti laini huku mkono wake
mmoja ukilisugua sugua bega la
Genes.
"Genes unaogopa kulala na
mimi kitanda kimoja? Akauliza
tena Naomi huku akimuangalia
Genes kwa macho
malegevu.Genes akahisi damu
inaanza kumchemka akayaelekeza
macho yake katika sehemu za
kifua cha Naomi.Kuna kitu
kilimvutia na kumfanya
asiyabandue macho yake
pale.Naomi naye alikuwa kimya
ameyaelekeza macho yake kwa
Genes.Alionekana akihema
haraka haraka.
"Mbona hunijibu
Genes.Unaogopa kulala na mimi
kitanda kimoja?
Genes akayaondoa macho yake
kifuani kwa Naomi akakohoa
kidogo na kusema
" Siogopi Naomi.Nimekosa
neno la kusema.This is a great
suprise to me" Akasema Genes
halafu akameza mate.
"Usijali Genes,hakuna ubaya
wala tatizo lolote kama tukilala
kitanda kimoja.Tunaweza tukalala
bila kufanya hivyo unavyofikiria"
akasema Naomi na kumfanya
Genes acheke kicheko kikubwa
"Genes I can read your
mind.Ninafahamu kitu gani
unawaza" akasema huku
akicheka.Akachukua glasi yake
na kunywa funda moja la mvinyo
halafu akamgeukia Genes.
"Kicheko hicho
kinamaanisha niyasemayo yana
ukweli.Asilimia kubwa ya vijana
wa kiume wakiwa peke yao na
vijana wa kike haijalishi kama ni
wapenzi au ni marafiki,mara
nyingi huwaza kitu kimoja
tu,Ngono.Mawazo yao yote
wanayaelekeza huko.Lakini
inawezekana kabisa kwa mvulana
na msichana wakakaa pamoja
katika chumba kama hiki na
,wakala chakula
pamoja.wakanywa,wakacheka na
kufurahi,wakabadilishana
mawazo juu ya mambo mbali
mbali ya maisha ya kila siku bila
kuhusisha mawazo ya ngono"
akasema Naomi na kumfanya
Genes atabasamu
"Nakubaliana nawe
Naomi.Unachokisema ni kitu cha
kweli kabisa.Kwa upande wangu
mawazo hayakuwa huko
unakofikiri" akasema Genes huku
akicheka.
"Usijali Genes hayo ni
mambo ya kawaida kwa
wanadamu kwa sababu
tumeumbwa na hisia.Wakati wote
mwanaume na mwanamke
wanapokutana Faragha kama
tulivyo mimi na wewe sasa hivi
basi hisia kama hizo lazima
ziwepo hasa kama ni wapenzi au
kama kuna hisia za kimapenzi
kati yao.Sisi si wapenzi,ni
marafiki wa kawaida na sijui
kama kuna hisia zozote za
kimapenzi katika urafiki wetu."
akasema Naomi kisha akaichukua
glasi yake ya mvinyo na kupiga
funda mbili
"Genes..." akaita
Naomi.Genes akainua kichwa na
kumtazama.
"Nahisi joto sana.Nataka
nikaoge nipunguze hili joto"
akasema Naomi huku akiinuka
pale sofani na kuelekea kitandani.
"Naomi ngoja nikupishe ili
uweze kubadili nguo.I'll be
outside" akasema Genes huku
akiinuka.
" Hapana Genes huna haja ya
kutoka.Unaogopa kitu gani?
akasema Naomi huku
akitabasamu
"Siogopi kitu ila si adabu
njema kukaa humu ndani wakati
ukibadilisha nguo." akasema
Genes.
"Usihofu kitu Genes kwani
kitu gani ambacho hujakiona?
Siku ile ulipokuja kuamua
ugomvi wangu na Sheddy
ulinikuta nikiwa na nguo za ndani
pekee ukanitazama mwili wangu
wote sasa leo unaogopa nini?
Huna haja ya kuogopa kitu
Genes..just relax" akasema Naomi
kwa sauti ambayo ilionesha wazi
kwamba tayari alikwisha
lewa.Naomi akamfuata Genes
akamtaka amfungue zipu ya gauni
lake na kuliacha lianguke chini
,akabakiwa na nguo za ndani
pekee.Genes akahisi kama chaji
za umeme zimempitia.Akabaki
ameduwaa akimkodolea macho
Naomi aliyekuwa amesimama
pale kitandani akiwa amebakiwa
na nguo nyeupe za ndani.Naomi
akainama na kuliokota gauni lake
akaliweka kitandani.Kitendo kile
kikayafanya maungo nyeti ya
Genes kupoteza utulivu.
"Tonight you must be mine
Genes.Asubuhi nitaamka nikiwa
mikononi mwako.Sina muda wa
kusubiri zaidi ya hapa" akawaza
Naomi huku akijifunga taulo .
Naomi akaingia bafuni kuoga
na kumuacha Genes pale sofani
akihisi damu
ikimchemka.Kitendo cha Naomi
kuvua nguo mbele yake
kiliufanya mwili wake usisimke
na mapigo ya moyo wake kwenda
kasi.Baada ya kumaliza kuoga
Naomi akatoka bafuni
“I feel much better now”
akasema Naomi.Genes bado
aliendelea kumtazama huku
midomo yake imejaa mate ya
uchu kutokana na umbo la
kutamanisha la Naomi.Kwa hatua
ndogo ndogo Naomi akaenda
kuketi pembeni ya Genes.Taulo
alilokuwa amejifunga likafunuka
kidogo na kuyaacha wazi mapaja
yake meupe na kuzidi kumpa
wakati mgumu Genes.
“Genes hujisikii kwenda
kuoga? Akasema Naomi huku.
“Sihisi joto Naomi” akasema
Genes
Naomi akamsogelea akalivua
koti la genes na kuliweka
pembeni.Halafu akaifungua tai na
kuitupa pembeni.Genes alihisi
kuishiwa nguvu kila mikono laini
ya Naomi ilipomgusa.
“Genes wewe ni kijana
mzuri.Una sura nzuri,una tabia
nzuri,una roho nzuri yaani kila
kitu kwako ni kizuri.Nafurahi
kukufahamu Genes” akasema
Naomi akiwa amekiegemeza
kichwa chake katika bega la
Genes ambae alikuwa
akitabasamu.
“Hata wewe ni msichana
mrembo sana Naomi .Uzuri wako
siufananishi na msichana
mwingine yeyote.Una kila sifa ya
mwanamke mzuri” akasema
Genes na kuufanya uso wa Naomi
uchanue kwa tabasamu kubwa.
“Ahsante sana Genes..”
akasema Naomi huku akijisogeza
karibu zaidi na Genes ambaye
tayari ikulu ilikosa utulivu kwa
mambo aliyokuwa akifanyiwa na
Naomi.
“Genes hivi ni kwa nini
hutaki kuoa? Toka nimekufahamu
sijawahi kukuona ukiwa na
mwanamke.Kijana kama wewe
unatakiwa uwe na mwanamke”
akasema Naomi huku akicheka
cheka.Genes hakujibu kitu.
“Nijibu basi Genes una
mchumba? Naomi akauliza
tena.Genes akageuza shingo na
kumtazama Naomi usoni.
“Sina mchumba Naomi ..”
“ Ouh Genes unasubiri nini
kutafuta mchumba hadi hivi sasa?
Genes akacheka kidogo na
kusema
“Naomi dunia ya sasa
imebadilika sana tofauti na enzi
za wazazi wetu.Siku hizi ni adimu
mno kumpata mtu mwenye
mapenzi ya kweli.Watu
wamekuwa walaghai,wakipenda
mtu kwa kitu alicho nacho na si
kwa moyo wake.Wote wake kwa
waume siku hizi hawana mapenzi
ya kweli.Naogopa kuumizwa na
mapenzi kwa sababu maumivu
yake hayana dawa na huchukua
muda mrefu kupona kwa maana
hiyo bado naendelea kumuomba
Mungu anisaidie niweze kumpata
mwanamke wa ndoto
zangu,mwanamke ambaye
atanipenda mimi kama Genes na
si kwa vitu
nilivyonavyo,mwanamke
atakayenijali na kunithamini hata
nikipata upofu,mwanamke
atakayesimama na mimi katika
kila hali iwe masika na
kiangazi.Kwa bahati mbaya
wanawake wa aina hiyo ni nadra
sana kuwapata zama hizi lakini
nina hakika tayari Mungu
amekwisha nipa mwangaza
kuhusiana na huyo mwanamke
ninayemtaka” akasema genes na
kumfanya Naomi akae kimya
akamuangalia usoni kwa makini
“Kwa nini msichana huyo
nisiwe mimi? Ninakupenda sana
Genes.Ninakupenda mno.Wewe
ni mwanaume pekee ninayetaka
kuwa naye katika maisha
yangu.Mimi ni mwanamke wa
pekee unayepaswa kuwa naye na
si mwingine.Usiku wa leo lazima
nikueleze ukweli wa moyo
wangu” akawaza Naomi
“ Mbona unaniangalia hivyo
Naomi ? akauliza Genes baada ya
Naomi kumuangalia usoni kwa
muda mrefu.
“Napenda tu kuiangalia sura
yako Genes.Huwezi jua ni kwa
kiasi gani nina furahi kuwa nawe
karibu siku ya leo” akasema
Naomi kwa hisia kali
“Genes najua utaniona kama
msichana nisiye na adabu au hii ni
kawaida yangu kulala na
wanaume katika mahoteli lakini
ukweli ni kwamba hii ni mara
yangu ya kwanza na sijawahi
kufanya hivi hata mara
moja.Nimefanya hivi leo hii
kutokana na kutaka ukaribu
zaidi.Nataka niendelee kujihisi
kama niko peponi.Please
Genes.I’m ready for anything
because ..I …I..” Naomi akasita
kuongea.Genes akamtazama
“ Because …..? akauliza
Genes huku akimeza mate..
“Because I love you
Genes…..” akasema
Naomi.Genes akastuka na
kumuangalia Naomi usoni
“Yes I love you Genes.I love
you with all my heart.” akasema
Naomi.Genes akashindwa aseme
nini akabaki akimtazama usoni.
“Genes tafadhali naomba
usinielewe vibaya kukutamkia
kwamba ninakupenda kwa sababu
si tamaduni zetu kwa mwanamke
kumtamkia mwanaume kama
anampenda.Nimeshindwa
kuzizuia hisia zangu.Nimekuwa
nikiubeba mzigo mzito na
nimeona leo hii niutue mzigo huo
kwa kukueleza ukweli.Siko tayari
kuendelea kukaa na suala hili
moyoni bila kukueleza ukweli.”
Akasema Naomi huku
akikipeleka kichwa chake kifuani
kwa Genes.
“ Umekasirika genes ?
akauliza naomi
“ Sijakasirika
Naomi..Nimekosa neno la kusema
kwa maneno mazito
uliyoniambia. “ akasema Genes
na Naomi akajisogeza karibu
zaidi na Genes.Taratibu Genes
akajikuta akiinua mkono wake wa
kushoto na kuupitisha katika
mgongo wa Naomi
akamkumbatia.Wote wawili
walikuwa wakihema haraka
haraka
“ You are mine Genes..you
are all mine…hakuna mwanaume
atakayethubutu kuugusa tena
mwili wangu zaidi yako..Ninahisi
raha ya ajabu sana nikiwa
nawe”akawaza Naomi na mara
taulo alilokuwa amejifunga
kifuani likafunguka na kuanguka
pembeni akabaki mtupu.
“Genes take me to
heaven…..” akasema Naomi kwa
sauti ndogo ya mahaba huku
mkono wake wa kushoto
ukivifungua vifungo vya shati la
Genes na kisha kuanza
kukichezea kifua chake.Naomi
akainua kichwa chake halafu
akamtazama Genes usoni
Taratibu kama wakivutwa na
sumaku wakajikuta
wakiikutanisha midomo yao
Ghafla Genes akastuka kama
mtu aliyekurupuka toka
usingizini.
“Hapana Naomi siwezi
kufanya hivi” akasema genes
huku akiinama na kukishika
kichwa chake
“Why Genes? Akauliza
Naomi..
“Naomi naomba unisamehe
sana.Siko tayari kufanya hivyo
unavyotaka tufanye.Samahani
sana kwa kukuumiza”akajibu
Genes
Naomi akamtazama Genes
halafu akamvuta zaidi kwake na
kuanza kumpiga mabusu
mfululizo.
“ Genes I’m all yours
tonight.Please Genes” akalalama
Naomi huku akimbusu Genes .
Genes akiwa kifua wazi
akafanikiwa kujitoa katika
mikono ya Naomi ,akasimama
huku akihema kwa kasi.Naomi
naye akasimama mwili wake
ulikuwa mweupe na wenye
kutamanisha.Genes akajikuta
akipingana na sauti mbili moja
ikimtaka amtimizie Naomi
matakwa yake na nyingine
ikimtaka asifanye.
“ Genes ninakupenda sana
tafadhali naomba usinifanyie
hivi.Tafadhali genes uonee
huruma moyo wangu unaoumia
kwa penzi lako” Akasema Naomi
huku akitoa machozi.Genes
akajisikia vibaya sana kumuona
Naomi akilia.Taratibu
akamsogelea akalichukua taulo
pale sofani akamfunga
kifuani.Naomi akamkumbatia
Genes kwa nguvu.
“ Genes najua unanifikira
vibaya sana lakini sijali
kitu,vyovyote vile
utakavyonifikiria mimi niko
tayari kwa sababu ninakupenda
Genes.Ninakutaka wewe pekee
katika maisha yangu.” akaendelea
kusema Naomi huku machozi
yakimtoka.Genes akamfuta
machozi na kusema
“ Naomi naomba
unielewe.Sina sababu mbaya
kukataa kufanya mapenzi nawe
kwa usiku wa leo.Ninatamani
sana kufanya nawe mapenzi usiku
kucha lakini kwa usiku wa leo
hapana” akasema Genes
“ Genes yawezekana
umeniona kama kahaba ambaye
ninajilazimisha kwa wanaume na
ndiyo maana unasita kulala na
mimi”Akasema Naomi lakini
Genes akawahi kumkatisha
“Usiseme hivyo
Naomi.Wewe si mwanamke wa
namna hiyo.Ninakufahamu vizuri
ninakufahamu wewe ni msichana
unayejiheshimu na huna tabia
kama hizo.Naomba tafadhali futa
kabisa mawazo kwamba labda
ninakufikiria vibaya.Kamwe
sintathubutu kufanya hivyo”
Akasema Genes.
“Kama hunifikirii mimi ni
kahaba kwa nini hutaki kulala
nami usiku wa leo?Kwa nini
unanifanya nipoteze ile furaha
yote niliyokuwa nayo usiku wa
leo? Akauliza Naomi huku
akiupeleka mkono ikulu kwa
Genes ambako kulikuwa
kumechachamaa
“Naomi kuna jambo ambalo
naomba ulifahamu..” akasema
Genes
“Jambo gani genes.Sitaki
kusikia kitu chochote usiku wa
leo .I want only you.” akasema
Naomi huku akiendelea
kuzichezea nyeti za Genes
“Naomi tumefahamiana si
muda mrefu sana.Urafiki wetu
unazidi kukua siku hadi
siku.Urafiki wetu ni wa dhati na
wa kweli.Naomba kwa faida ya
urafiki wetu tusifanye mapenzi
kwa usiku huu” akasema Genes.
“Why Genes.Kuna tatizo
gani ? Huniamini? Akauliza
Naomi kwa sauti kali.Genes
hakujibu kitu.
"Nijibu Genes. Kwa nini
tusifanye? akauliza tena Naomi
lakini Genes hakujibu kitu
akabaki akimtazama.
"I'm so fool.I'm so stupid"
akajilaumu Naomi.
"Naomi tafadhali usiseme
hivyo.You are not stupid"
"I am a fool " akasema
Naomi huku akifuta machozi na
kwenda kuketi sofani
"You are not Naomi.Naomba
ufute kabisa mawazo hayo.Wewe
ni msichana mzuri mwenye
heshima”
" Thats not true"akasema
Naomi
" Naomi ,sipendi kukuona
ukitoa machozi.Unaiumiza nafsi
yangu sana kila nikikuona ukitoa
chozi.Siku zote nataka kukuona
ukiwa ni mwenye furaha na
tabasamu pana usoni pako."
" Don’t pretend you care
about me" akasema Naomi.
" I'm not pretending
Naomi.Ninakujali sana”akasema
Genes
" Why do you care about me
Genes? akauliza Naomi.
" Because I love you "
akajikuta amesema Genes na
kumfanya Naomi astuke
" Umesemaje Genes?
akauliza Naomi kwa mshangao
" Yes I've just said it.I love
you.I love you so much Naomi"
akasema Genes na mara Naomi
akamrukia na kumkubatia huku
akimbusu mfululizo.Wakaanguka
chini lakini hawakuumia.Usiku
ule ukawa ni mwanzo wa
uhusiano mkubwa kati yao
Kumbu kumbu ile ikamtoa
Linah machozi.Akamtazama
Mathew aliyekuwa akimsikiliza
kwa makini
“Nilimpenda sana Genes na
niliamini ndiye mwanaume wa
maisha yangu na aliponitamkia
kuwa anataka kunioa nilikubali
haraka haraka nikiamini tayari
maisha yangu yamebadilika
kumbe nilikuwa
najidanganya.Baada ya siku mbili
nikapigiwa simu nikapewa
maelekezo ya kumuua haraka
kwani mojaya sharti nililopewa ni
kutokufunga ndoa.Nililia sana
kwani tayari nilikuwa nampenda
Genes lakini sikuwa na namna
nyingine ya kufanya zaidi ya
kufuata maelekezo
niliyopewa,nikamuua Genes”
akasema Linah na kuinamisha
kichwa.Ilionesha wazi kitendo
kile cha kumuua Genes
kilimuumiza sana.
“I shot him five times.Bado
nakumbuka nilivyomshuhudia
akikata roho,Bado nak……”
Linah akashindwa kuendelea
akaanza kulia
“Jikaze Linah nahitaji kujua
kila kitu kilichotokea” akasema
Mathew
“Imeniumiza sana
Mathew.Baada ya kumuua Genes
niliwaza kuhusu hatima ya maisha
yangu na nikagundua kosa
nililolifanya la kumkabidhi
shetani maisha yangu.Nikafikiria
kujitoa uhai kwani sikuona faida
ya mimi kuendelea kuishi hapa
duniani lakini nilipowafikiria
wadogo zangu namna
wanavyonipenda na
kunitegemea,nikawafikiria watu
wengine ambao wako katika
orodha ya wanaotakiwa
kuuawa,nikawafikiria watu wasio
na hatia yoyote wanaouawa kila
siku nikaamua kujitoa kuwasaidia
na siwezi kuwasaidia mimi
mwenyewe nahitaji sana msaada
wako Mathew” akasema
Linah.Mathew akamtazama
halafu akasema
“Nitakusaidia Linah lakini ili
niwe na nguvu ya kukusaidia
ninataka unieleze ukweli mtupu
kuhusu wewe.Who are you?
Tuanzie hapo” akasema
Mathew.Linah akafuta machozi
na kusema
“Mathew mimi ni Linah Yule
Yule ambaye ulimfahamu miaka
kumi na tano iliyopita ila maisha
yangu yamebadilika na sasa mimi
ni muuaji” akasema Linah na
Mathew akastuka kidogo
“Muuaji? Akauliza
“Ndiyo.Niko katika jamii ya
The Red Mambaz”
“Red Mambaz? Ni akina nani
hao? Mathew akauliza
“A secret society” akajibu
Linah na Mathew akashusha
pumzi
“Linah unahitaji msaada
wangu hivyo nahitaji kujua kila
kitu kuhusu hao watu wanaojiita
The Red Mambaz.Ni akina nani
na wako wapi? Mathew akauliza
“Wako hapa
Tanzania.They’re very powerfull
people.Wameushika uchumi wa
nchi,ni wao wenye kuamua nani
awe na nani asiwe Raisi.Ni watu
wenye nguvu sana Mathew hapa
nilipo ninatetemeka kwa woga
kwa kitu nilichowafanyia”
akajibu Linah
“Umesema wao ndio wenye
uwezo hata wa kuamua nani awe
na asiwe Rais.Unamaanisha hata
Rais wetu ambaye tumemchagua
miezi kadhaa iliyopita ni wao
ndio waliomtaka awe Rais?
Mathew akauliza
“Ndiyo Mathew.Hata Rais
wetu Dr Mark Sasile ni mfuasi wa
Red Mambaz.Si yeye tu bali wako
wengi viongozi wa
serikali,viongozi wa dini,wasanii
maarufu,wanamichezo na
wafanya biashara wakubwa.Ni
mtandao mpana sana nitakueleza
kila kitu lakini si kwa usiku huu
nahitaji kutuliza kichwa changu”
akasema Linah
“Dah ! akasema Mathew na
ukimya mfupi ukapita halafu
akasema
“Tuhamie katika kile
kilichotokea kule makaburini.Ni
mambo ya kushangaza
sana.Nimekushuhudia kwa macho
yangu ukibadilikana kuwa katika
umbile la Mamba” akasema
Mathew na kubaki akimtazama
Linah
“Hukupaswa kushuhudia
jambo lile lakini sikuwa na namna
nyingine ya kufanya zaidi ya
kukuacha ulishuhudie.Kwa ufupi
tu ni kwamba unapojiunga na Red
Mambaz unapewa nguvu kubwa
ya kufanya mambo makubwa
ambayo wanadamu wengine
hawawezi.Wanatuambia kwamba
wanatupa nguvu za
kimalaika.Tunaweza kuyabadili
maumbo yetu na kuwa na umbo la
Mamba kama ulivyoshuhudia
kule makaburini.Nguvu hii yote
inatoka katika ile pete iliyokuwa
kidoleni.Ni pete ya ajabu ambayo
ukivalishwa kidoleni haitoki hadi
siku yako ya kufa dipo hutoka na
kuichukua mrithi wako au kama
huna mrithi basi unazikwa
nayo.Ni pete maalum ambayo
inakuunganisha na wenzako na
mkawasiliana kiroho na ukajua
wenzako wako wapi na
wanafanya nini,kwa ufupi ni pete
ya miujiza.Kitu tunachokichunga
ni pete ile kutokugusa
damu.Ulipoanza kukata kidole na
damu ikaangukia katika pete ile
ndipo mambo yalipoanza
kubadilika.Ni mambo ya kutisha
sana Mathew ambayo katika hali
ya kawaida ni vigumu kuamini
kama yanatokea lakini yanatokea
kama ulivyoshuhudia.Katika
ibada zetu kuna wakati ambao
wote hubadilika na kuwa na
maumbo ya Mamba halafu
hurejea katika maumbo ya
binadamu” akasema Linah
“Nini hasa malengo ya
jumuiya hiyo? Akauliza Mathew
“Lengo kuu la hizi jumiya
zote za siri ni kuiharibu
dunia.Hizi ni imani za kishetani
na lengo ni kuifanya dunia iwe ni
sehemu ovu kabisa yenye
kuchukiza machoni pa Mungu
mkuu,kuwafarakanisha
wanadamu na muumba wao kwa
kuwafanya watende mambo
machafu kabisa.Wakati wa
kuapishwa lazima kumkana
kwanza Mungu mkuu na kuahidi
kumuabudu anayeitwa mwenye
mamlaka kuu ambaye ndiye huyo
Red Mamba mkuu.Jamii hizi za
siri huwatumia viongozi wa
serikali kuhalalisha mambo
machafu katika jamii zetu ambayo
ni machukizo mbele za Mungu na
kuyafanya ni mambo
halali.Mfano ni masuala ya
mapenzi ya jinsia moja,utoaji
mimba,zinaa, nk.Haya ni mambo
ambayo kwa jamii nyingi hasa
kwenye nchi kubwa kubwa
yamezoeleka na kuonekana ni ya
kawaida na yanahalalishwa na
watawala ambao wengi ni wafuasi
wa jamii hizi.Mambo hayo
machafu hupewa nguvu na watu
wengine kama
wanamichezo,wanamuziki,matajir
i wakubwa ambao wana wafuasi
wengi duniani ili yaonekane ni
mambo ya kawaida.Katika jamii
zetu za Afrika,mambo haya bado
hayajazoeleka lakini taratibu
yanaanza kupenyeza kwa
kuwatumia viongozi wetu wa
kisiasa,wanamichezo,wanamuziki
na watu wengine wenye
ushawishi mkubwa katika jamii”
akasema Linah
“Inaogopesha sana.Kama
viongozi wetu nao ni wafuasi wa
jamii hii basi lazima wataipeleke
nchi hii katika shimo la moto”
akasema Mathew na kumtazama
Linah
“Ni kweli
unayosema.Tunapelekwa katika
shimo la moto bila kujua
tukidhanini maisha ya kisasa”
akasema Linah
“Baada ya kukata kile kidole
una hakika hawatajua mahala
ulipo? Mathew akauliza
“Sikutaka kuivaa tena ile pete
kwa kuwa ninataka kuachana na
jamii ile na kwa kuwa haivuki
kidoleni kama nilivyokwambia
ndiyo maana nikaamua kukikata
kabisa kidole.Kuivua pete ile ni
ishara kwamba umeyavunja
masharti na hautambuliwi tena
kama mwanajamii lakini
hautaachwa salama.Lazima
uuawe.Umesikia watu maarufu
wamekuwa wakifariki vifo vya
ajabu ajabu na wengi wao
wanafariki wakiwa wazima wa
afya bila kuumwa ugonjwa
wowote.Siri kubwa ni hiyo.Wengi
wa hawa watu maarufu ni wafuasi
wa jamii hiyo na wengi hujiunga
na Red Mambaz wanapokuwa
hawana kitu,wanapewa masharti
na pale wanapopata pesa na
umaarufu wanayaona masharti
hayo ni magumu sana na
kuyavunja na wengine hutaka
kujitoa kabisa katika jamii ndiyo
maana vifo vyao hutokea ghafla
na vingi vinatokana na ajali au
kufariki usingizini.Hivyo ndivyo
itakavyonitokea
mimi.Nimewasaliti na
wataendelea kunisaka kila mahali
usiku na mchana hadi
wahakikishe wameniua” akasema
Linah
“Dah ! Mathew akasema kwa
mshangao
“Ilikuaje Linah ukaingia
katika jamii ya watu hawa?
Ulikuwa na maisha mazuri sana
wakati ule nilipokutana nawe kule
Arusha kitu gani kilikushawishi
hadi ukajiunga nao? Akauliza
Mathew
“Mathew ni hadithi ndefu
sana nitakueleza siku nyingine”
akasema Linah
“Linah wakati ni sasa.Hatuna
wakati mwingine natakiwa kujua
kila kitu sasa hivi.Ilikuaje
ukajiunga nao hadi ukageuka
kuwa muuaji? Watu wangapi
umekwisha waua hadi sasa?
Ulifahamuje kama nimewahi
kufanya kazi shirika la ujasusi?
Hayo yote ninahitaji
kuyafahamu.Maelezo ya kina
yatakayoniwezesha kuifahamu
vyema hii jamii ya siri ya Red
Mambaz yatanisaidia sana kujua
ni namna gani ya kuweza
kukusaidia” akasema Mathew
“Mathew nitaanza na hilo
swali la mwisho ulilouliza kuhusu
nilijuaje kuwa umewahi kufanya
kazi idara ya ujasusi
Tanzania.Tuna kitabu kinaitwa
who is who in Tanzania.Katika
kitabu hicho kumeorodheshwa
majina ya watu wengi kazi zao na
mahala wanakopatikana.Watu
wanaoandikwa katika kitabu
hicho ni wale tu ambao wanaweza
kuwa aidha msaada au hatari kwa
Red Mambaz hivyo ni watu
wanaofuatiliwa kwa ukaribu
mkubwa.Nililisoma jina lako
katika kitabu hicho na ndipo
nilipojua kuwa wewe ni
jasusi.Uliwekewa alama ya kijani
kwa kuwa hukuwa tena katika
shirika la ujasusi na ukiwekewa
alama ya kijani ina maanisha
kuwa wewe si hatari kwa sasa
lakini unaweza kuwa hatari
baadaye.Baada ya kuamua
kuachana na Red Mambaz
sikuona mtu mwingine ambaye
anaweza akanisaidia kutoka
katika jamii hiyo zaidi yako
Mathew ndiyo maana nikakupigia
simu na kukuomba uje
unisaidie.Utanisamehe Mathew
kwa kukuingiza katika jambo hili
la hatari” akasema Linah
“Kweli ni jambo la hatari
sana.Katika kazi yangu ya ujasusi
nimepambana na magaidi na watu
wengine hatari kwa usalama wa
nchi,ni mara ya kwanza kukutana
na jambo kama hili linalohusisha
jamii ya siri.Ni vipi uliweza
kuingia katika jamii hii ya siri?
Akauliza Mathew
“Mathew nitakueleza kila
kitu lakini kuna jambo moja la
muhimu sana ambalo nataka
kukueleza kwa sasa”akasema
Linah
“Jambo gani? Mathew
akauliza
“Kuna sadaka ya damu
inataka kutolewa na hawa
jamaa.Ni damu nyingi inakwenda
kumwagika.Watu wengi
wanakwenda kupoteza maisha
akiwemo Happy binti wa Rais”
“Wamefanya nini watu hao
hadi watolewe sadaka? Nao ni
wafuasi wa Red Mambaz?
Mathew akauliza
“Hapana si wafuasi wa Red
Mambaz.Anayesababisha watu
hao wote wapoteze maisha ni
binti wa Rais anaitwa
Happy.Huyu aliwekwa dhamana
na baba yake Rais Dr Mark
Richard Sasela wakati anajiunga
na Red Mambaz” akasema Linah
“Sijakuelewa Linah.Huyo
Happy aliwekwaje dhamana na
baba yake? Mathew akauliza
“Unapojiunga na Red
Mambaz unapaswa kuweka
dhamana ya mtu au watu
uwapendao inategemea na uzito
wako katika jamii na Dr Mark
alimuweka dhamana mtoto wake
Happy” akasema Linah
“Linah utanisamehe mdogo
wangu lakini nahitaji ufafanuzi
kidogo katika jambo hilo la
dhamana na namna sadaka hiyo
ya damu itakavyotolewa”
akasema Mathew
“Ili ulifahamu kiundani
sualahili,nitakueleza historia
nzima ya Rais Mark namna
alivyojiunga na Red Mambaz
naamini utanielewa” akasema
Linah na kuanza kumsimulia
Mathew namna Dr Mark Sasile
alivyojiunga na Red Mambaz.
DAR ES SALAAM
Hatimaye baada ya heka heka
za miezi miwili ya kampeni za
uchaguzi mkuu wa Rais na
wabunge,Dr Mark Richard Sasela
kutoka chama cha ukombozi
ambaye ni mwanasheria
kitaaluma akatangazwa kuwa
mshindi kwa kupata asilimia 78
ya kura zote ikiwa ni mara ya
kwanza kwa chama cha upinzani
kushinda uchaguzi mkuu tangu
kuanzishwa kwa mfumo wa
vyama vingi nchini Tanzania
Nchi nzima ilizizima kwa
furaha za ushindi huo mkubwa
alioupata Dr Mark.Wafuasi wake
walikesha mitaani wakishangilia
baada ya matokeo kutangazwa.Dr
Mark aliwahi kuhudumu kama
waziri katika serikali
iliyoondolewa madarakani na
alijizolea umaarufu kutokana na
misimamo yake ya kupinga
hadharani vitendo vya rushwa na
ufisadi.Kutokana na tabia yake
hiyo ya kupinga hadharani
vitendo vya rushwa alichukiwa na
wenzake ndani ya chama chake
na kuamua kuhama chama
akahamia katika chama cha
upinzani kilichojulikana kama
chama cha ukombozi.
Katika kampeni za urais na
katika midahalo mbali mbali
aliyoshiriki na wagombea urais
wenzake,Dr Mark aliwakuna watu
wengi kwa namna alivyojieleza
na ahadi alizozitoa kwa wananchi
kama wangempa ridhaa ya
kuongoza nchi.Mikutano yake ya
kampeni ilifurika watu waliotaka
kumsikiliza.Ushindi wake
ulionekana mapema sana kabla
hata ya kura kupigwa
Baada ya ushindi ule
mkubwa,Dr Mark akakabidhiwa
rasmi cheti chake cha ushindi na
maandalizi ya kuapishwa
yakaanza
Akiwa amepumzika
nyumbani kwake usiku akiwa na
baadhi ya viongozi wa chama
chake,Dr Mark akajulishwa kuwa
kuna mgeni anahitaji kumuona
akaelekeza akaribishwe ndani.
“Mheshimiwa Rais mteule
shikamoo” akasema mgeni Yule
ambaye Dr Mark hakuwa
akimfahamu na ilikuwa mara ya
kwanza kuonana naye.Alikuwa ni
kijana nadhifu sana aliyevaa suti
nzuri ya rangi nyeusi na
alionekana ni kijana ambaye
alikuwa anajiweza kimaisha
“Marahaba.Karibu sana”
akasema Dr Mark na
kumuelekeza mmoja wa
watumishi wake kumpeleka
mgeni Yule sebuleni yeye
akamalizia mazungumzo na
viongozi wa chama chake halafu
akaenda kuonana na Yule mgeni
“Karibu sana.Ni mara ya
kwanza tunaonana” akasema
DrMark
“Ndiyo mzee ni mara ya
kwanza tunaonana.Ninaitwa
Edmund Sanjo” Mgeni yule
akajitambulisha kwa kujiamini.
“Karibu sana Mr Edmund
nimefurahi kukufahamu”akasema
Dr Marjk
“Samahani sana mheshimiwa
Rais mteule kwa kukutembelea
muda kama huu” Akaanzisha
mazungumuzo Edmund.
“Bila samahani Mr
Edmund.Kazi hii ni utumishi wa
watu hivyo natakiwa kuifanya
kwa saa ishirini na nne”
Akasema Dr Mark
“Mheshimiwa Rais mteule,
sitaki kuchukua muda wako
mwingi,naomba kama hutajali
tuelekee moja kwa moja katika
jambo la msingi lililonileta hapa
kwako usiku huu” Edmund
akasema.Dr Mark akatikisa
kichwa ishara ya kukubali halafu
akainuka na kumfanyia ishara
Edmund amfuate wakaelekea
katika chumba cha mazungumzo.
“Karibu Mr Edmund”
akasema Dr Mark
“Nashukuru
sana.Mheshimiwa Rais
nimetumwa nikuletee barua hii”
akasema Edmund akaitoa bahasha
katika mfuko wake wa koti na
kumpatia Dr Mark.
“Ninaomba uisome uielewe
na kisha unipe jibu” Edmund
akaongea huku Dr Mark
akiifungua ile bahasha.na kuitoa
karatasi iliyokuwamo mle
ndani,akaanza kuisoma.Ghafla
sura yake ikabadilika na uso
ukakunja ndita.Alipomaliza
akamtazama Edmund kwa hasira
halafu akaitupa karatasi ile
mezani na kugonga meza kwa
mkono wake wa kulia.
“No ! I can’t do that…”
Edmund ambaye
hakuonekana kuwa na wasiwasi
wa aina yoyote ile akatabasamu
kwa mbali halafu akauliza.
“Mzee umeuelewa ujumbe?
“Kijana naomba iwe ni mara
ya kwanza na ya mwisho
kuniletea ujumbe wa kipuuzi
kama huu.Kawaambie hao
waliokutuma kwamba Dr Mark ni
mtu makini,mwenye nguvu na
uwezo wa kufanya lolote
alitakalo.Sihitaji msaada wa mtu
yeyote yule ili niweze
kuongoza.Nimepigiwa kura na
watanzania na ndiyo ambao
nitawatumikia na si mtu au genge
la watu Fulani especially you
devil worshipers.Nakutuma
ukawaambie wakuu wako
kwamba Dr Mark kamwe hawezi
kuwa mtumwa wa
shetani.Ninajiweza,ninamtumaini
Mungu na sihitaji nguvu za
kishetani katika kazi yangu” Dr
Mark akasema kwa ukali.
Edmund akatabasamu na
kusema.
“Tafadhali punguza jazba
mheshimiwa Rais mteule.Naona
ujumbe huu haujauelewa
vizuri.Nipe dakika mbili
nikueleweshe vizuri na ninaomba
unisikilize kwa makini.Kwanza
naomba ufahamu kwamba sisi ni
watu wenye nguvu na
mamlaka.Tuna nguvu na
mamlaka ya kufanya lolote lile
tunalolitaka hapa nchini.Tuna
uwezo wa kumuweka na kumtoa
mtu yeyote
madarakani.Mheshimiwa Rais
mteule kabla ya kampeni za
uchaguzi tulikufuata na kukueleza
nia yetu ya kutaka kukupa nafasi
ya urais kwa sharti la kujiunga
nasi lakini hukuamini kama mtu
kutoka chama cha upinzani
anaweza akashinda uchaguzi na
kuwa Rais na ulitoa ahadi kuwa
kama tukiweza kufanikisha
ukashinda uchaguzi mkuu basi
ungekuwa tayari kujiunga
nasi.Tumetimiza ahadi yetu na
umeshinda uchaguzi sasa ni zamu
yako kutekeleza ahadi
uliyoitoa.Isome vizuri barua hiyo
ina maelekezo yote nini cha
kufanya” akasema Edmund na
kumtazama Dr Mark aliyekuwa
anahema haraka haraka
“ Dr Mark lengo letu sisi ni
kukufanya uwe Rais bora na wa
kihistoria katika nchi hii na
kukumbukwa na vizazi vingi
vijavyo.Tunataka kukupa nguvu
za kiutawala lakini kwa kuwa
umekataa kutimiza ahadi yako
uliyoahidi kabla haujashinda
uchaguzi,mimi nitarejea kwa
walionituma na kuwaeleza kila
kitu ulichoniambia.Nashukuru
sana kwa kunikaribisha na
kuongea nami mheshimiwa Rais
mteule” Edmund akasema huku
akitabasasamu na kisha akaanza
kupiga hatua kuondoka mle
chumbani.Akakinyonga kitasa ili
atoke na mara akasikia sauti ya Dr
Mark
“Wait !!
Edmund akasimama na
kugeuka kumtazama Dr Mark
“Tafadhali rudi tuongee”
Akasema kwa sauti ya chini Dr
Mark.Edmund akarejea ndani.
“Unasemaje Dr Mark?
“Edmund akauliza huku
mkono wake mmoja ameuweka
mfukoni na mwingine ameuweka
mezani
“Tafadhali kaa tuongee”
akasema Dr Mark.Edmund
akavuta kiti na kuketi
“Edmund naomba unisamehe
kwa maneno niliyoyaongea hapo
kabla” akasema Dr Mark
“Mheshimiwa Rais kitu peke
unachotakiwa kukifanya ni
kutekeleza ahadi yako hakuna
kingine tunachoweza
kuzungumza kwa sasa”akasema
Edmund
“Nini kitanitokea kama
sintatekeleza? Akauliza Dr Mark
“Sahau kuhusu nafasi hii
uliyoipata” akasema Edmund na
Dr Mark akacheka kidogo
“Nimeshinda uchaguzi
kihalali kabisa hakuna anayeweza
kutengua ushindi
wangu.Mamilioni ya watanzania
wamenipigia kura” akasema Dr
Mark
“Dr Mark japo
umekabidhiwa cheti cha ushindi
lakini kamwe hautakikalia kiti
hicho na katika siasa utapotea
kama moshi wa
mshumaa.Kumbuka sisi ndiyo
tunaoamua nani awe nani asiwe
Rais.Uchaguzi ni wako Dr Mark”
akasema Edmund na kuingiza
mkono mfukoni akatoa kadi na
kumpatia Dr Mark
“Kadi yangu hiyo hapo kama
utabadili mawazo yako
utanijulisha” akasema Edmund na
kuondoka akimuacha Dr Mark
amesimama amefura hasira
“Huu ni ushindi wangu wa
halali na hakuna wa kunipoka
ushindi! akawaza Dr Mark
akiuma meno kwa hasira
SIKU ILIYOFUATA
Sherehe za ushindi wa Dr
Mark Sasela na chama chake cha
Ukombozi ziliingia mchanga
baada ya wagombea wawili wa
urais kujitokeza na kupinga
ushindi huo mahakamani.Taarifa
hiyo ilimstua sana Dr Mark na
kuyakumbuka maneno ya
Edmund
“Dr Mark japo
umekabidhiwa cheti cha ushindi
lakini kamwe hautakikalia kiti
hicho na katika siasa utapotea
kama moshi wa mshumaa.Ni sisi
ndiyo tunaoamua nani awe nani
asiwe Rais” Dr Mark akahisi
kijasho kinamtoka baada ya
kumbukumbu ile kumjia
“Ni vipi kama wale jamaa
wanachokisema ni cha kweli? Ni
vipi kama mahakama itatengua
ushindi wangu? Ni vipi kama
nitashindwa kukalia kiti hiki cha
urais? Akajiuliza Dr Mark
“Hii yote ni mipango ya wale
jamaa.Sikupaswa kwenda
kinyume na makubaliano yetu.Ni
kweli niliwaahidi kama
wakifanikisha nikashinda
uchaguzi basi nitajiunga nao na
kweli nimeshinda tena kwa
asilimia kubwa na dunia nzima
inashangaa nini
kimetokea.Nilishangaa hata mimi
namna mikutano yangu
ilivyokuwa ikijaa watu.Kila
nilichokitamka watu walikuwa
wanashangilia.Nilipata nguvu na
ujasiri mkubwa wa kusimama
jukwaani na kujieleza na sikujua
nimekuwaje jasiri.Nilikwisha
sahau kuwa nilikuwa nimeingia
makubaliano na jamii ya Red
Mambaz wanisaidie kushinda
uchaguzi.Sasa nimepata picha
kwa nini niligeuka lulu ghafla tu”
akawaza Dr Mark
“Hawa jamaa wana nguvu na
uwezo mkubwa na sitakiwi
kufanya nao mzaha hata kidogo
kwani ninaweza nikaukosa urais
hivi hivi.Siko tayari kuipoteza
nafasi hii ambayo nimeihangaikia
kwa muda mrefu.Haikuwa rahisi
kufika hatua hii.Sintapoteza
chochote kama nitakwenda
kuwaona hawa jamaa na
kutekeleza ahadi yangu” akawaza
Dr Mark na kuichukua ile kadi
aliyopewa na Edmund akampigia
“Dr Mark” akasema Edmund
“Edmund niko tayari”
akasema Dr Mark
“Are you sure? Edmund
akauliza
“Yes I’m sure.Jioni ya leo
njoo nyumbani kwangu” akasema
Dr Mark
“Ahsante Dr Mark” akajibu
Edmund na kukata simu
Saa moja jioni Edmund
alifika katika makazi ya Dr
Mark.Hakukuwa na maongezi
mengi kwani tayari Dr mark
alikwisha fanya maandalizi yote
“Edmund tumekubaliana na
walinzi wangu kwamba
tutaondoka na gari tatu.Moja ya
kwangu na mbili za walinzi
wangu.Tukifika huko mahala
waliko hao wakuu wako
nitaongozana na mlinzi mmoja tu
kwani wamekataa kuniacha peke
yangu” akasema Dr Mark
“Hakuna tatizo Dr Mark.One
more thing,vaa suti nyeusi”
Edmund akasema na Dr Mark
akaelekea chumbani kwake
akavaa suti nyeusi kisha akarejea
akiwa tayari kwa safari
wakaondoka hakuna aliyejua
walikuwa wanaelekea wapi.Wote
walilifuata gari la Edmund.
Dakika arobaini toka watoke
katika makazi ya Dr
Mark,wakawasili katika hoteli
moja kubwa iliyoko nje ya
jiji.Kibao cha hoteli hiyo
kilisomeka kama 6 WAYS
HOTEL.Ilikuwa ni mara ya
kwanza kwa Dr Mark kufika
mahala hapo.Mara tu baada ya
kulivuka geti kulikuwa na
barabara sita zilizokuwa
zikielekea sehemu tofauti za
hoteli hiyo na ndiyo sababu
ikaitwa 6 ways hotel.Edmund
ambaye ndiye aliyekuwa kiongozi
wa msafara ule akaongoza kupita
katika njia ya pili toka kushoto na
magari mengine yote
yakafuata.Eneo lote lilikuwa na
ukimya mkubwa.Baada ya
mwendo wa dakika mbili
wakatokeza nje ya jengo moja
kubwa la duara.Edmund
akasimamisha gari lake nje ya
jengo hilo akashuka.
Dr Mark akashuka garini na
kuongozana na mlinzi mmoja
wakamfuata Edmund aliyekuwa
ameliegemea gari lake akiwasubri
na safari ya kuelekea ndani
ikaanza.Walishuka ngazi
zilizoelekea chini halafu wakafika
katika mlango mmoja
mkubwa,Edmund akawafanyia
ishara wasimame pale.Dr Mark
akahisi msisimko mkubwa
sana.Alihisi kama nywele
zikisisimka na damu kumchemka
kwa namna mahala pale
palivyotisha.Edmund akaelekea
pembeni ya mlango ule uliokuwa
uking’aa sana ambako kulikuwa
na kitu mfano wa madhabahu
iliyojengwa kwa mawe
,akachukua chombo ambacho
ndani yake akaweka unga unga
Fulani ambao Dr Mark na mlinzi
wake hawakuufahamu ni unga wa
nini ,moshi ukaanza kufuka toka
katika kile chombo.Huku
akiongea maneno ambayo Dr
Mark na wenzake hawakuweza
kuyafahamu mara moja Edmund
akauzunguka mlango ule huku
amekishika chombo kile
mkononi.Mara lango lile
likajifungua.Edmund
akakirudisha chombo kile mahala
pake,akainama kidogo huku
akiongea maneno kwa sauti
ndogo halafu akawafanyia ishara
akina Dr Mark wamfuate.
Dr Mark na mlinzi wake
wakaingia ndani ya ukumbi
mkubwa ambao ulikuwa na nguzo
kubwa zilizonakshiwa kwa
dhahabu.Ilikuwa ni sehemu yenye
kupendeza na kustaajabisha mno.
Waliupita ukumbi huo na kuingia
katika chumba Fulani ambacho
kilikuwa na kabati
kubwa.Edmund akalifungua na
kutoa vitu mfano wa sura ya mtu
kwa ajili ya kuufunika uso.Yule
mlinzi wa Dr Mark akauliza
“Mheshimiwa haya ni
mambo gani tena?
“Kenneth don’t ask.Fuata
kile ninachokifanya” Dr Mark
akasema kwa sauti iliyojaa wasi
wasi mwingi.Edmund
akawatazama halafu akawaambia
wamfuate.
Walitoka ndani ya chumba
kile na kuufuata ujia uliokuwa na
giza nene halafu wakajikuta
wametokeza mahala palipokuwa
na moshi wenye harufu
nzuri.Sauti za watu zilikuwa
zikisikika.Dr Mark jasho lilizidi
kumtiririka.
“Tunaelekea madhabahu
kuu,toeni viatu vyenu” Edmund
akawaamuru Dr Mark na mlinzi
wake.Haraka haraka wakatoa
viatu na kisha wakaanza
kutembea taratibu wakimfuata
Edmund.Walifika mahala
kulikokuwa na ngazi za
kupanda,wakapanda taratibu.
“Tafadhali msiogope”
Edmund akamwambia Dr Mark
ambaye alikuwa akitetemeka kwa
woga.
Baada tu ya kumaliza
kupanda ngazi zile ghafla pazia la
rangi ya dhambarau likajifungua
na kwa macho yao wakashuhudia
kitu cha ajabu ambacho
hawajawahi kukiona maishani.Dr
Mark akahisi kuishiwa
nguvu,akataka kuanguka lakini
mlinzi wake akamzuia na
kumshika mkono.Mwili wake
ulikuwa ukitetemeka kwa kitu
alichokiona.Mbele yao kulikuwa
na sanamu ya jitu kubwa la
kutisha lenye sura na umbo kama
Mamba.Lilikuwa jeusi na la
kutisha lenye macho makubwa
yaliyong’aa kama moto.Dr Mark
akatetemeka kwa hofu,hakuwahi
kuona kitu cha kutisha namna ile
katika maisha yake.Ghafla
ukatokea mtetemeko katika eneo
lile.Edmund kwa haraka
akawaambia Dr Mark na
mwenzake.
“Fanyeni ninavyofanya
mimi” Edmund akainama na
kusujudu,Dr Mark na mlinzi
wake nao wakafanya vile
alivyofanya Edmund.Wakiwa
bado wameinama wakilisujudia
jitu lile kubwa ,jeusi na la kutisha
Dr Mark akasikia mtu akimgusa
shingo.Taratibu akainua shingo
yake na kukutanisha macho na
mtu mmoja mwenye ndevu nyingi
aliyeufunika uso wake ambaye
alimfanyia ishara ainuke
amfuate.Dr Mark akainuka
japokuwa bado alihisi mwili wote
ukimtetemeka.Mlinzi wake naye
akainuka na kumsaidia kutembea
kumfuata yule mtu ,wakaingia
katika chumba kimoja
kilichokuwa na meza na viti
nane.Akawakaribisha viti na
kuwaomba wasubiri pale.Shati la
Dr Mark lilikuwa limelowa jasho
lililomtiririka kwa uoga aliokuwa
nao..
Baada ya dakika kumi yule
mtu akarejea akiwa ameongozana
na watu wengine
watano.Haikuwa rahisi
kuwatambua kutokana na nyuso
zao kukingwa na zile nyuso za
bandia.Mara tu baada ya kuketi
katika meza ile kubwa yule mzee
akaamuru wote waliokuwamo
mle ndani wavue zile nyuso zao
za bandia na kuziweka mezani.Dr
Mark akapigwa na mshangao
mkubwa kwa sura
alizoziona.Alibaki mdomo wazi
akasindwa aseme nini.Alikuwa
akitazamana na mkuu wa majeshi
aliyekuwa akitabasamu.Mzee
yule aliyeonekana kiongozi wa
jopo lile akaanzisha mazungumzo
na kumtaka mlinzi wa Dr Mark
akasubiri nje hadi
watakapomaliza maongezi.
“Dr Mark napenda kuchukua
nafasi hii kukukaribisha sana
katika hekalu letu.Mbele yako ni
jopo la viongozi wa jamii ya siri
ya watu wenye nguvu na
mamlaka tunajulikana kama Red
Mambaz.Mimi naitwa Hoz.Isack
Lemela ni kiongozi mwandamizi
wa jamii hii hapa nchini
Tanzania.Kwa ufupi tu ni
kwamba Jamii hii ya siri
ijulikanayo kama Red Mambaz
ilianzishwa miaka kadhaa
iliyopita hapa nchini Tanzania ina
wanachama wapatao mia tatu
kwa sasa miongoni mwao wapo
viongozi wa
serikali,wanasiasa,wanamichezo,
wasanii,viongozi wa dini na watu
wengine.Ili uwe mwanachama wa
jamii yetu ya siri lazima uwe ni
mtu mwenye ushawishi au
wadhifa Fulani katika jamii
Lengo kuu la jamii yetu ya siri ni
kuwapa nguvu na mamlaka
wanachama wake.Tunaposema
nguvu na mamlaka tunamaanisha
kuwa na nguvu za kiutawala na
maamuzi katika maeneo yao ya
kiutawala na kuwaweka katika
nafasi za juu kabisa pamoja na
kuwapa mafanikio
makubwa.Wanachama wetu wote
wanapewa uwezo mkubwa wa
kuelewa na kuona mambo mengi
kwa wakati mmoja.Wanao uwezo
wa kuwatambua maadui
zao,ukajua nini kinaendelea wapi
na kwa wakati gani.Wanapewa
nguvu ya kimalaika.Kwa ufupi
naweza kusema sisi ni malaika
tunaoishi duniani” Hoz.Isack
akatulia kidogo akamuangalia Dr
Mark aliyekuwa
akimsikiliza,kisha akaendelea.
“Dr Mark,jana tulimtuma
mjumbe kwako na tunashukuru
kwamba umeupokea ujumbe na
kuuelewa ndiyo maana uko hapa
leo.Sisi tumetimiza ahadi yetu
umeshinda uchaguzi sasa ni zamu
yako kutimiza ahadi.Tumekuita
hapa tunataka kukupa kazi ya
urais kwa miaka mitano.Tunataka
kukufanya uwe ni kiongozi
mwenye nguvu na sauti si
Tanzania bali barani Afrika na
duniani kwa ujumla.Kila
utakachokisema kitakubaliwa na
kusikilizwa.Kabla hatujaendelea
na taratibu nyingine tunataka kwa
ulimi wako utamke kamauko
tayari kujiunga nasi” akasema
Hoz Isack na Dr mark akazidi
kuingiwa na wasiwasi
“Niko tayari kujiunga na Red
Mambaz” akasema Dr Mark
“Ahsante Dr Mark kwa
kutamka maneno hayo.Kuna
mambo mawili yatafanyika usiku
wa leo.Kwanza utakaribishwa
rasmi Red Mambaz na pili
utasimikwa rasmi kama Rais wa
nchi hii.Hapo nina maanisha
kwamba unakabidhiwa rasmi
jukumu la kuiongoza nchi hii kwa
niaba yetu.Wewe ndiye
utakayekuwa ukiyatekeleza yale
yote ambayo utatumwa uyafanye
kwa maana hiyo unatakiwa upewe
nguvu za kutosha kuweza
kuifanya kazi hiyo.Baada ya
usiku wa leo utajikuta ukiwa na
nguvu za ajabu na taswira yako
katika jamii itabadilika.Hakuna
tena mtu yeyote atakayekuwa na
nguvu za kupamba nawe kisiasa”
Hoz.Isack akamwambia Dr Mark
kisha akaingia Edmund na
kumchukua Dr Mark wakaondoka
na kwa kutumia magari wakarejea
katika geri kuu na walipofika
katika njia panda yenye bara bara
zipatazo sita Edmund akaongoza
kupita katika njia namba
nne.Mwendo wa kama mita mia
moja hivi toka waifuate ile bara
bara nambari nne Edmund
akasimamisha gari na kisha
akaenda katika gari la Dr Mark
akamuomba waongee faragha.
“Dr Mark hawa walinzi wako
wanatakiwa waishie
hapa.Hawatakiwi kuendelea zaidi
ya hapa.Kuanzia hapa ni sehemu
ambayo huwa inakuwa na nguvu
za ajabu sana kwa maana hiyo
naomba uwaelekeze kwamba
warudi nyuma na waifuate njia
namba moja itakayowapeleka
hadi hotelini ambako
watajitambulisha kama C6 na
kisha watakirimiwa kila
kitu.Shughuli itakapomalizika
tutawafuata”
Dr Mark akawafuata walinzi
wake garini akaongea nao kwa
dakika tano wakamuelewa na
kugeuza gari wakaelekea
hotelini.Edmund akawaelekeza
Dr Mark na yule mlinzi wake
waingie katika gari lake.Mwendo
wa kama dakika tano hivi gari
likasimama katika geti moja
kubwa jeusi .Edmund akashuka
na kumuamuru Dr Mark na mlinzi
wake mmoja washuke kisha
wakaingia katika kijumba kidogo
kilichokuwa pembeni ya lile
geti.Ndani ya kijumba kile
kulikuwa na beseni la
maji.Edmund akaongea maneno
Fulani na kisha akainua beseni
lile akawaamuru Dr Mark na
mlinzi wake kila mmoja achote
maji yale kwa kutumia kiganja
cha mkono wake na kunawa
usoni.Dr Mark akawa wa kwanza
kunawa maji yale na mara tu
alipoyatia machoni likatokea giza
nene,hakuweza kuona kitu
chochote.Alitaka kupiga kelele na
alipotaka kufumbua mdomo wake
ulikuwa mzito.Baada ya kama
dakika mbili hivi alihisi ni kama
vile alikuwa ameshikwa mkono
na alikuwa akielea
anganiAliogopa mno.Muda mfupi
baadaye akahisi ni kama
amesimama mahala na kisha
akahisi mikono ya mtu ikiyashika
macho yake na mara akaanza
kuona tena.Mbele yake alisimama
mzee mmoja mwenye ndevu
nyingi aliyekuwa amevalia joho
refu jeusi.Mahala hapo palikuwa
na mwanga hafifu japokuwa Dr
Mark aliweza kuyaona mazingira
yake yalikuwa ya miti miti
mingi.Harufu ya ubani ilisikika
eneo lote.Dr Mark alikuwa
akitetemeka kwa woga
“Tafadhali vueni hizo nguo
zenu na mvae nguo zile pale”
Akaamuru mzee yule aliyekuwa
amesimama mbele yao.Dr Mark
na mlinzi wake wakavaa nguo
zile walizoelekezwa wavae
ambazo zilikuwa ni majoho meusi
halafu mzee yule akaamuru
wamfuate.Walitembea kwa
takribani dakika kumi wakiyapita
mawe makubwa na vitu
mbalimbali vyenye maumbo ya
kutisha na hatimaye wakawasili
katika sehemu moja iliyokuwa na
uwanja mpana sana uliozungukwa
na mafuvu ya watu yaliyokuwa
yakitoa mwanga mkali katika
sehemu za macho na kupafanya
mahala hapa paonekane kama
mchana.Katika uwanja huo
kulikuwa na watu wengi wenye
majoho meusi wakiwa
wameinama wakisujudu mbele ya
sanamu ya jitu moja kubwa
iliyokuwa na pembe mbili
kichwani zenye kutoa moto.Dr
Mark akatetemeka
mno.Hakuwahi kuona kitu cha
namna ile katika maisha
yake.Mzee yule aliyekuwa
amewaongoza akapiga makofi
mara tatu na mara watu wote
wakainuka na taratibu akaanza
kuwaongoza akina Dr Mark
kuelekea mbele.
Mlinzi wa Dr Mark
akaondolewa mahala pale na
kupelekwa sehemu nyingine na
Dr Mark akakalishwa katika kiti
kikubwa kilichokuwa kimewekwa
mbele.Wazee wanne
wakajitokeza wakiwa wamevaa
mavazi mekundu .Mzee mmoja
ambaye ndiye aliyeonekana kama
kiongozi wao akainamia sanamu
ya lile jitu lenye pembe
zinazowaka na kuongea maneno
ambayo Dr Mark hakuweza
kuyafahamu na bila kutarajia
sanamu lile likainua mkono wake
na kumuelekezea Dr Mark na
ghafla likatokea tetemeko kubwa
la ardhi eneo lile lililodumu kwa
sekunde kadhaa.Baada ya hapo
mzee yule akamshika mkono Dr
Mark aliyekuwa akitetemeka na
kumuongoza katika madhabahu
ya dhahabu iliyokuwa pembeni
kidogo.Akachukua upanga mmoja
wa dhahabu uliokuwa juu ya ile
madhabahu akampa Dr Mark
aushike
“Dr Mark Sasile,jamii ya
watu wenye nguvu na mamlaka
tukiongozwa na mwenye
mamlaka mkuu tumekubali uwe
mmoja wa wanafamilia hii yenye
nguvu.Kama ilivyo kawaida
yetu,tutafanya kwanza ibada ya
kukukaribisha na kukuunganisha
rasmi na jamii yetu” mzee yule
mwenye sauti ya kukwaruza
akaongea maneno yale na kisha
akagekia madhabahu ile yenye
kung’aa sana akaongea maneno
ambayo Dr Mark hakuyatambua
na baada ya muda mfupi mzee
mmoja akaleta glasi mbili
zilizokuwa zimejaa kimiminika
chekundu na kumpatia Dr Mark
glasi moja.
“Hiki ni kinywaji chetu
kitukufu ambacho kila
mwanafamilia hii lazima
anywe.Hii ni damu iliyotokana na
mimba changa
zinazotolewa.Kinywaji hiki
chenye utukufu na nguvu
kitaingia katika kila seli ya mwili
wako na kuifanya ziwe imara na
nguvu.Naomba unywe tafadhali.”
Mzee yule akamuamuru Dr Mark
ambaye mikono ilikuwa
ikimtetemeka.Kila alipoitazama
damu ile ambayo ilikuwa na
vipande vidogo vidogo vya
nyama alihisi kutaka
kutapika.Mzee yule akamuangalia
Dr Mark kwa macho makali.
“Kunywa tafadhali”
akaamuru yule mzee. Dr Mark
akajaribu kujikaza ili ainywe
damu ile lakini hakuweza.Mikono
ilikuwa ikimtetemeka.Mzee yule
aliyekuwa akiongoza ibada ile
alipoona kwamba Dr Mark
ameshindwa kuinywa damu ile
akasema maneno Fulani kwa sauti
na watu wote waliokuwepo pale
wakaitikia.Waliendelea na
maombi yale kwa nguvu na
ghafla Dr Mark akahisi mkono
wake uliokuwa umeishika ile
glasi ukielekea wenyewe
mdomoni na mdomo ukafunguka
kisha akaanza kuinywa ile
damu.Alipomaliza kunywa damu
ile kukawa kimya kabisa na
alijihisi kama vile ni mtu mpya
kabisa.
Sekunde tano baada ya
kunywa damu ile Dr Mark
akaanza kusikia joto kali la mwili
na ghafla akahisi kama mwili
wake unawaka moto.Alijiona
kama yuko ndani ya bwawa la
moto akiungua.Akapiga ukelele
mkubwa na hatimaye akaanguka
na kupoteza fahamu Akiwa
amelala pale chini hana fahamu
,yakaletwa maji maalum
yaliyokuwa katika beseni
akamwagiwa huku akisindikizwa
na maneno waliyokuwa
wakiyaongea wale wazee.Kisha
mwagiwa maji,ukaletwa moto
uliokuwa ukiwaka katika karai
ukawekwa karibu na kichwa cha
Dr Mark halafu kikaletwa chuma
kimoja chenye mpini wa dhahabu
ambacho kikawekwa ndani ya
moto ule na baada ya dakika mbili
kikaiva na kuwa chekundu .Dr
Mark akiwa bado amelala chini
joho alilovaa likafunguliwa na
kifua chake kikawa wazi .Kile
chuma kilichokuwa kimeiva
ndani ya moto kikatolewa na
akakabidhiwa yule mzee kiongozi
na taratibu akakiweka katika
sehemu ya kulia ya kifua cha Dr
Mark.
“Dr Mark Richard
Sasile,ninakuweka muhuri huu
kama alama ya kukutambulisha
kwamba wewe ni mmoja wa watu
wenye nguvu na mamlaka
duniani.Kwa mamlaka niliyopewa
na mwenye mamlaka mkuu
ninakuingiza rasmi katika jamii
hii ya watu wenye nguvu na
mamlaka katika dunia.Muhuri
huu ninaokutia sasa utakuwa ni
kinga na utambulisho wako na
hautafutika daima.Kwa uwezo na
nguvu nilizopewa nakuamuru Dr
Mark Sasile inuka..!!” Mzee yule
akaamuru kwa sauti kubwa na
taratibu Dr Mark akafumbua
macho na kuinuka akakaa.Upande
wa kulia wa kifua chake
kulipigwa muhuri wa duara wa
dhahabu wenye jina lake.Dr Mark
akajiangalia na kubaki
akishangaa.Mzee yule kiongozi
akamuamuru Dr Mark kusimama
na kumfuata hadi karibu na lile
sanamu la jitu la kutisha.Mzee
yule kiongozi akaongea maneno
Fulani na kisha akamgeukia Dr
Mark
“Dr Mark je unakubali kwa
hiyari yako mwenyewe kujiunga
na jamii ya Red Mambaz? Mzee
yule kiongozi akamuuliza Dr
Mark
“Ndiyo nakubali” akajibu Dr
Mark
“Je uko tayari kufuata
masharti yote yanayompasa
kuyafuata kila mwanajamii wa
Red Mambaz?
“Niko tayari” akajibu Dr
Mark
“Je uko tayari kumkana
Mungu wako unayemuabudu sasa
na kumwangukia,kumsujudia na
kumuabudu mwenye enzi na
mamlaka kuu kwamba ndiye
muweza wa vitu vyote?
“Niko tayari” akajibu Dr
Mark
“Je unakubali kumkabidhi
maisha yako mwenye mamlaka
mkuu ayaongoze?
“Ninakubali” akajibu Dr
Mark
“Dr Mark agano uliloliweka
hivi sasa limekutoa rasmi katika
kundi la watu wenye kumuabudu
Mungu mwingine na kumkubali
mwenye enzi na mamlaka kuu
kwamba ndiye mkuu na mtawala
wa vitu vyote vya dunia.Siku
utakapolivunja agano hili
utakufa” Mzee kiongozi akasema
kisha akamfanyia ishara Dr Mark
asogee mbele na kusimama
pembeni yake karibu kabisa na
sanamu ya lile jitu lenye
kutisha.Mzee kiongozi akampa Dr
Mark karatasi yenye mandishi ya
dhahabu.
“Kinachofuata sasa ni kiapo
mbele ya mkuu wetu mwenye
enzi na mamlaka mkuu” akasema
mzee Kiongozi na kisha akarudi
na kusimama nyuma ya Dr
Mark.Mara eneo lote likaanza
kufuka moshi mwingi wa ubani
na kelele za vitu kama ndege
zikaanza kusikika kwa mbali.Juu
angani radi zikaanza kupiga na
ngurumo kusikika na upepo mkali
ukaanza kuvuma.Dr Mark
alikwisha yazoea mazingira ya
mahala pale na hakuogopa
tena,akaanza kuyasoma
maandishi yaliyomo katika ile
karatasi.Kabla hajatamka neno
lolote radi kubwa ikapiga na
kukichana kitambaa kilichokuwa
kimeifunika nguzo kubwa ya
dhahabu iliyokuwa pembeni ya
sanamu ile ya jitu la kutisha
Majina ya watu mbali mbali
wafuasi wa Red Mambaz
yalikuwa yameandikwa.
“Mimi Mark Richard Sasile
kuanzia dakika
hii,ninakuangukia,nakusujudia na
kukuabudu wewe mwenye
nguvu,enzi na mamlaka mkuu”
alipomaliza kuisoma aya hii
ikapiga radi kubwa sana katika
nguzo ile ya dhahabu na jina lake
la kwanza “Dr Mark ”
likajiandika katika ile nguzo.Dr
Mark akaendelea
“Mimi Mark Richard Sasile
ninakiri kwa kinywa changu
kwamba wewe ndiye mwenye
uwezo na nguvu na hakuna tena
mwingine zaidi yako.Kwa dhati
ya moyo wangu ninajiweka mbele
zako nikiomba nguvu na uwezo
wako vinishukie sasa ili niweze
kuwa mmoja wa wafuasi wako
wenye nguvu hapa duniani”
Baada ya kuisoma tena aya
ya pili radi nyingine kubwa
ikapiga na jina la pili “Richard”
likajiandika katika ile nguzo.Bado
kelele za viumbe mbali mbali
ziliendelea kusikika na upepo
mkali ukivuma.Eneo lote
lilifunikwa na moshi mwingi
mithili ya wingu zito
“Mimi Mark Richard Sasile
,niko tayari kutoa sadaka zangu
mbali mbali kama ninavyopaswa
kufanya na sintasita kufanya
hivyo kila pale nitakapotakiwa
kufanya hivyo”
Radi ya tatu ikapiga na jina la
tatu “Sasile” likajiandika katika
nguzo
“Mimi Dr Mark Richard
Sasile ninakuomba
uniongoze,unisimamie katika kila
jambo ninalolifanya,nilifanye kwa
nguvu zako.Nakuomba unilinde
dhidi ya maadui zangu na unipe
nguvu na uwezo wa kupambana
nao na kuwashinda”
Baada ya hapo zikafuata radi
mfululizo kwa dakika tatu na
kisha kila kitu kikakoma.Taratibu
wingu lililokuwa limelifunika
eneo lile likaanza kutoweka na Dr
Mark akajikuta ni mtu mwenye
mabadiliko makubwa.Alijiona ni
kama ni mtu anayetembea na
nuru.Alijiona aking’aa kama
malaika.Tayari alikuwa ni mmoja
wa wafuasi wa Red Mambaz
Mzee kiongozi akamfuata na
kumpa mkono Dr Mark
“Hongera sana Dr Mark .Sasa
wewe ni mmoja
wetu.Kinachofuata kwa sasa ni
kukuapisha rasmi kama Rais wa
Tanzania na kisha sehemu ya
mwisho kabisa ni kutoa dhamana”
akasema mzee kiongozi na
kumuongoza Dr Mark hadi katika
sehemu moja yenye kibanda kama
kile ambamo mzee mmoja
mwenye ndevu nyingi na joho
refu jekundu alikuwa amekaa.Dr
Mark akaelekezwa na kisha
akashika kitabu kimoja chekundu
katika mkono wake wa kulia
halafu mzee yule akamtaka
kuyarudia maneno
atakayoyasema.
“Mimi Dr Mark Richard
Sasile,mbele ya mwenye enzi na
mamlaka kuu za dunia,kwa utii na
unyenyekevu mkubwa ninaapa
kwamba ninakubali kuwa Rais wa
Tanzania na kwamba nitaifanya
kazi hii kwa nguvu,utii na
uaminifu mkubwa sana chini ya
uongozi wa mwenye mamlaka
kuu na kwamba nitayatekeleza
yale yote atakayoniamuru
kuyafanya kwa niaba yake na
sintapinga hata neno moja
nitakaloamriwa naye.Ewe
mwenye mamlaka kuu naomba
unisaidie”
Dr Mark akamaliza kula
kiapo chake
“Kwa kiapo hiki
ulichokula,kwa niaba ya mwenye
enzi na mamlaka kuu
ninakutangaza rasmi kama Rais
wa Tanzania kutoka katika jamii
ya Red Mambaz” Akasema mzee
yule mwenye ndevu nyingi na
kisha akampa mkono wa pongezi
makofi mengi yakapigwa.
Mzee kiongozi akamfuta Dr
Mark na kumpongeza.
“Kwa tukio hili tayari wewe
ni Rais wa Tanzania na
kitakachofanyika siku chache
zijazo kukuapisha ni taratibu za
kiserikali lakini tayari wewe ni
rais wa nchi hii.Twende sasa
katika sehemu ya mwisho ambayo
ni sehemu muhimu sana ya
dhamana” Akasema mzee
kiongozi na kumuongoza Dr
Mark kwenda katika sehemu ya
udhamini.Ilikuwa ni sehemu
iliyotengenezwa kama kitanda na
kabla ya kukifikia kitanda hicho
kulikuwa na karai la moto
uliokuwa ukiwaka.Mzee kiongozi
akakishika chuma kimoja chenye
mpini wa dhahabu na kukiweka
ndani ya ule moto na kuongea
maneno Fulani na kisha
akamgeukia Dr Mark.
“Dr Mark Sasile,kila mtu
anayejiunga na umoja wetu ni
lazima atoe mdhamini
wake.Iwapo itatokea siku moja
umekwenda kinyume na taratibu
na matakwa yetu basi sisi
humchukua mdhamini na
kuinywa damu yake kama ishara
ya kuomba msamaha kwa
mwenye enzi mkuu.Dhamana
huchaguliwa na mwenye enzi
mkuu na hutakiwi kupingana na
maamuzi yake.Kwa maneno hayo
basi tayari mdhamini wako
amekwisha patikana na kwa sasa
unatakiwa uchukue chuma hiki na
kwenda kuutia muhuri wa moto
katika paji lake la uso la
mdhamini wako” Akasema mzee
Kiongozi na kumkabidhi Dr Mark
kile chuma kilichokuwa chekundu
kwa kuungua na moto.Dr Mark
alikuwa akitetemeka mikono
baada ya kukipokea chuma
kile.Hakujua mdhamini wake
aliyechaguliwa alikuwa nani.
“Naomba mdhamini huyo
asiwe ni mwanangu Happy”
Akawaza Dr Mark huku wazee
wale wakimuangalia kwa macho
makali sana.
Taratibu akaanza kutembea
kukiendea kitanda kile ambacho
alielekezwa kwamba alikuwepo
mdhamini wake.Wazee wale
walikuwa wakisemezana jambo
kila Dr Mark alipokuwa akipiga
hatua kuelekea kile kitanda.Hatua
tatu kabla hajakifikia kitanda kile
akasimama na kugeuka akakutana
na sura zilizokunjamana za wale
wazee na kisha akaendelea kupiga
hatua kwa kusita kukiendea kile
kitanda.Alipokifikia akatazama
lakini hapakuwa na mtu yeyote
pale kitandani.Akageuka na
kuwatazama wale wazee.Mzee
kiongozi akamfuata na
kumnong’oneza kitu sikioni.Dr
Mark akavuta pumzi ndefu na
kisha akauinua juu mkono ule
aliokuwa amekishika kile chuma
kilichokuwa chekundu kwa
kuungua na taratibu akaanza
kuushusha mkono wake
chini.Mpaka wakati huo pale
kitandani hapakuwa na mtu
yeyote na wala hakujua mdhamni
wake alikuwa nani.
Ghafla Dr Mark akastushwa
na kitu ambacho hakuwa
amekitazamia
“No ! I can’t do this !!
Akasema Dr Mark kwa hasira na
kukitupa chini kile chuma
alichokuwa amekishika mkononi
Katika kitanda kile alikuwa
amelala Happy binti pekee wa Dr
Mark ambaye ndiye alichaguliwa
na mwenye mamlaka mkuu kuwa
dhamana ya Dr Mark.Upepo
mkali ukaendelea kuvuma na
mara eneo lote likawa jeusi na
radi kuanza kuunguruma.Hali
ikageuka na kuwa ya kutisha
sana eneo lile.
Sauti za kutisha za
miungurumo zikaendelea
kusikika.Upepo mkali ukaendelea
kuvuma na eneo lote
likatikisika.Dr Mark alikuwa
akitetemeka kwa uoga.Alifahamu
kwamba yeye ndiye chanzo cha
yale mambo yote kutokea.Kama
asigekataa kumtia mwanae
muhuri ule wa moto katika paji
lake la uso basi mambo yote yale
yasingetokea.
"Siko tayari kumuingiza
mwanangu katika imani kama
hizi.Bora waniue kuliko kumleta
mwanangu sehemu kama
hii.Kamwe sintamuweka
mwanangu muhuri wa moto"
akasema kwa sauti ndogo Dr
Mark huku akitetemeka na
kujilaumu sana kwa maamuzi
yake ya kujiunga na imani hii..
"Laiti ningejua kama mambo
yako hivi basi nisingejiunga
kabisa na mambo
haya..Nilikuw..............." wakati
akiwaza mzee mmoja akajitokeza
akiwa amebeba mbuzi dume
mweusi mwenye pembe
ndefu,akamuweka mbuzi yule
katika madhabahu ambayo wao
huyatumia kwa ajili ya kutolea
sadaka.Mzee kiongozi akasogea
katika madhabahu ile na
kumchinja yule mbuzi damu
ikasambaa katika madhabahu ile
halafu akainama na kuongea
maneno fulani ambayo Dr Mark
hakuyafahamu na baada ya muda
mfupi hali ikatulia na kuwa
shwari Dr Mark akavuta pumzi
ndefu.
"Ouh Thank you Lord”
akasema Dr Mark baada ya
mambo kutulia.Mzee Kiongozi
akamfuata Dr Mark akamuomba
amfuate.Wakaelekea katika
chumba kimoja kidogo
kilichokuwa na viti viwili
wakakaa.Mzee yule akamtazama
Dr Mark kwa makini sana usoni
kisha akasema
"Dr Mark kwa nini ukafanya
vile?
Dr Mark akakosa neno la
kujibu
"Nakuuliza Dr Mark kwa
nini ukafanya vile? akauliza tena
mzee Kiongozi.Midomo ya Dr
Mark ilikuwa
ikimtetemeka.Hakujua ajibu nini.
"Toka nimejiunga na umoja
huu haijawahi kutokea hata mara
moja mtu akadharau maagizo
aliyopewa na viongozi
wake.Uliapa wewe mwenyewe
kwa mdomo wako kwamba
utakuwa tayari kutekeleza yale
yote ambayo tutakutuma
uyafanye lakini kabla hata
hujaupata urais tayari umekwisha
anza kudharau maagizo ya
viongozi wako.Naomba nikueleze
ukweli kwamba wakuu
wamekasirika sana na kama si
kuwatuliza kwa sadaka ile ya
mbuzi mweusi aliyenona
tungeweza kuangamia sisi
sote.Mungu wetu ni mkali sana na
huwa hana mzaha hata
kidogo.Ukiweka ahadi yako
mbele yake lazima uitimize
vinginevyo adhabu yake huwa
mbaya sana.Adhabu yake ni
kukuondoa duniani wewe na
familia yako yote" akasema mzee
Kiongozi na kumtazama Dr Mark
ambaye alikuwa akitetemeka
"Mkuu naomba msamaha
sana kwa mambo yote
yaliyotokea.Nafahamu kwamba
wewe una uwezo wa kuniombea
msamaha kwa wakuu
wakanisamehe na ninaahidi
kwamba sintarudia tena.Nitafanya
na kutekekeleza yale yote
nitakayoagizwa
kuyafanya.Tafadhali sana naomba
uniombee msamaha" akasema Dr
Mark kwa uoga.
"Nilifanya vile kwa sababu
ninampenda sana binti yangu wa
pekee na sikutaka ashiriki katika
imani hii.Bado ni mdogo na
anahitaji ayafurahie maisha
yake.Tafadhali naomba binti
yangu asidhuriwe na kitu
chochote kile mkuu" akasema Dr
Mark kwa sauti yenye
kitetemeshi.
Mzee kiongozi akafungua
pazia kubwa lililokuwemo katika
kile chumba na mara ikajitokeza
runinga kubwa akaiwasha na
kumwambia Dr Mark aangalie
kwa makini.
Katika runinga wakaonekana
watu wengi sana wakiwa
wamejaa katika uwanja wa
taifa.Wengine walikuwa
wamepanga mstari mrefu
wakipita kutoa heshima zao za
mwisho katika jeneza lililokuwa
limefunikwa bendera ya taifa na
pembeni yake lilizungukwa na
wanajeshi.Dr Mark akamtazama
vizuri mtu aliyelala ndani ya lile
jeneza akagundua kwamba ni
yeye ndiye aliyekuwa amelala
mle ndani.Akastuka sana na
kuuliza
"Hii ina maana gani mkuu ?
"Hii ni siku ya mazishi yako
ya kitaifa" akasema mzee
kiongozi.
"Mazishi yangu ya kitaifa?
akauliza tena Dr Mark kwa wasi
wasi
"Ndiyo.Mazishi yako ya
kitaifa..."
"Mazishi gani wakati bado
sijafa? Dr Mark akauliza
"Hivi ndivyo utakavyokufa”
akasema mzee kiongozi huku
akitumia kifaa cha kubadilishia
picha katika runinga na mara
yakaonekana magari yakiwa
katika msafara yakienda kwa kasi
kubwa na mara likatokea tukio
moja baya.Gari la kati kati
likapasuka matairi ya mbele na
kupinduka.Tukio lile
likasababisha ajali mbaya sana
.Gari zote zilizokuwamo katika
ule msafara zikapata ajali.Damu
nyingi ikamwagika.Watu wengi
wakapoteza maisha
yao.Wanajeshi wakafika eneo lile
la ajali kwa helkopta ya jeshi na
kwa haraka wakaliendea lile gari
lililopasuka matairi na kuwatoa
watu wote waliokuwamo ndani.
"Amekufa" akasema
mwanajeshi mmoja akiwasiliana
na wenzake.Mtu aliyekuwa
amelazwa katika machela ni Dr
Mark.Alikuwa amelala huku
ametapakaa damu.Jasho
likamtoka Dr Mark baada ya
kuiona video ile.
"Sijaelewa video hii ina
maanisha nini? akauliza Dr Mark
kwa mshangao
"This is how you'll die Mark"
akasema mzee kiongozi
"Me? akauliza tena Dr
Mark.Moyo ulikuwa ukimuenda
mbio na kumfanya avute pumzi
ndefu
"Ndiyo Dr Mark.Hivi ndivyo
utakavyokufa kama utashindwa
kufanya yale yote
tutakayokuagiza kuyafanya"
akasema mzee kiongozi.Dr Mark
akapiga magoti na kumuomba
mzee kiongozi.
"Tafadhali mkuu naomba
uniombee msamaha.Niko tayari
kufanya chochote
mtakachonielekeza” akaomba Dr
Mark lakini mzee kiongozi
hakumjali akamwambia atazame
tena katika runinga.Safari hii Dr
Mark alionekana akihutubia
katika ukumbi mkubwa uliokuwa
umejaa watu.Akautambua ukumbi
ule kwamba ni ukumbi wa
mikutano wa umoja wa
mataifa.Akawatambua na baadhi
ya marais.Dr Mark alikuwa
akihutubia na watu wote mle
ukumbini walikaa kimya
wakimsikiliza yeye.Kila baada ya
muda mfupi ukumbi wote
ulikuwa ukimshangilia kwa
nguvu na kusimama kuonyesha
kukubaliana na mambo
aliyoyasema.Picha nyingine
ikajitokeza Dr Mark akiwa ndani
ya boti nzuri ya kifahari akiwa na
mwanamke mmoja ambaye
hakuwa akimfahamu lakini
kulikuwa na kila dalili kwamba
walikuwa ni wapenzi. Walikuwa
wakifurahia maisha huku
wakicheka na kufurahi.Pamoja
nao alikuwepo binti yake wa
pekee Happy akionekana
kusimama na mwanaume mmoja
ambaye alionekaa kama mumewe
wakiwa na mtoto mmoja mzuri
wa kike ambaye alionekana kama
mtoto wao.Sura ya Dr Mark
ikajenga tabasamu pana sana
alipoiona picha ile.
"Hivi ndivyo maisha yako
yatakavyokuwa kama utafanya
kila tutakalokuagiza
kulifanya.Utakuwa ni Rais
mwenye nguvu na utasikilizwa na
kila taifa duniani.Mwanao Sandra
ataolewa na kufanikiwa kupata
mtoto.Maisha yenu yatakuwa na
furaha kila siku." akasema mzee
kiongozi na kumuangalia Dr
Mark namna alivyokuwa
akitabasamu
"I need this life" akasema
kwa furaha Dr Mark
"Ni juu yako kuchagua ni
maisha gani unayataka.Kama
unataka kufa au unataka kuishi
maisha ya furaha siku zote fanya
maamuzi sasa" akasema mzee
kiongozi.
"Mkuu sitaki kufa.Bado
ninataka kuendelea kuishi na
kuwa rais wa Tanzania.Bado
ninataka kuendelea kuishi maisha
mazuri yenye furaha kila siku"
akasema Dr Mark
"Kama umechagua kuendelea
kuishi na kuyafurahia maisha basi
huna budi kufanya yale yote
tutakayokuamuru kufanya.Hii ni
nafasi yako ya mwisho kufanya
tutakavyokuamuru kama
utakwenda kinyume tena na
tunavyotaka sisi basi utakufa
kama ulivyoona katika runinga"
akasema mzee Kiongozi
"Niko tayari sasa kufanya
lolote lile mtakaloniamuru
kulifanya.Nitatekeleza maagizo
yote mtakayoniagiza." akasema
Dr Mark
"Kabla sijakutoa katika
chumba hiki na kukurudisha tena
katika madhababu unaamini
kwamba hutafanya tena mambo
ya ajabu kama uliyoyafanya muda
mfupi uliopita? akauliza mzee
kiongozi
"Nakuahidi mkuu kwamba
sintarudia tena kufanya mambo
kama yale.Nitafanya yale tu
nitakayoamriwa kuyafanya"
akasema Dr Mark kisha wakatoka
mle chumbani na kuelekea katika
eneo la ibada
Mzee kiongozi akaenda
kupiga magoti chini ya lile
sanamu kubwa la jitu la kutisha
ambalo kwa sasa lilibadilika rangi
na kuwa jekundu.Akaongea
maneno ambayo Dr Mark
hakuyaelewa na kisha akarejea
kwa Dr Mark akamtaka asogee
tena pale kwenye madhabahu ya
mawe na akamuweke muhuri wa
moto binti yake Happy .
Dr Mark akakishika kile
chuma chekundu kilichokuwa na
moto mkali akapiga hatua za
taratibu kuelekea mahala
alipokuwa amelala binti yake wa
pekee Happy
Akiwa na chuma kile
mkononi akamtazama binti yake
kwa muda.Kila kitu kilikuwa
kimetulia na hakukusikika mlio
wa kitu chochote hata wadudu.
"I'm sorry Happy" akasema
Dr Mark kisha taratibu
akakishusha chuma kile katika
paji la uso la binti yake Happy.
Baada ya kitendo kile
akapongezwa kisha akapewa
masharti mengine na maelekezo
ya kina kuhusiana na Red
Mambaz halafu akaondoka
**********
Happy Richard Sasile
alikurupuka kutoka usingizini
baada ya kuota ndoto ya
kutisha.Jitu kubwa lenye umbo
kama Mamba lilikuwa
likimfukuza likiwa na chuma
kinachowaka moto.Happy
alijitahidi kukimbia lakini jitu lile
lilikuwa na mbio kumzidi na
Happy akajikwaa akaanguka chini
jitu lile likamsogelea na kumpiga
na kile chuma cha moto usoni na
Happy akaamka.Uso uliloa jasho
na alihisi maumivu makali ya
kichwa.
“Sijawahi kuota ndoto ya
kutisha kama hii ambayo ninaiona
kama kweli.Sehemu lile jitu
liliponipiga na chuma usoni pana
maumivu makali.Nini maana ya
ndoto hii? Akajiuliza Happy na
kuinuka akaenda kuchukua dawa
za kutuliza maumivu akameza
halafu akarudi tena kitandani
akaanza kuitafakari ile ndoto
mwishowe akaamua kuchukua
biblia yake akaanza kuisoma na
taratibu akahisi macho mazito
akalala tena
Asubuhi aliamka mwili wote
ukimuuma na hakujua sababu
nini,Dr Mark akaamuru apelekwe
hospitali lakini hakuna ugonjwa
wowote ulioonekana baada ya
kufanyiwa vipimo hivyo akapewa
mapumziko
“Inaniuma sana kumtoa
mwanangu kwa Red
Mambaz.Hali hii aliyonayo leo
imesababishwa na kile
nilichokifanya jana.Bado
ninatakiwa kumpeleka naye
akavishwe pete lakini sijui
nitaanzaje kumweleza kuhusu
jambo hili na akanielewa”
akawaza Dr Mark
Linah akaongeza mvinyo
katika glasi yake akanywa halafu
akamtazama Mathew
“Hivyo ndivyo Dr Mark
alivyojiunga na Red Mambaz”
akasema Linah
“Mambo haya nilikuwa
nikiyasikia kwa watu
wakiyasimulia lakini sikujua
kama ni mambo ya kweli.Happy
yuko wapi kwa sasa? Mathew
akauliza
“Dr Mark alitakiwa
kumpeleka mwanae Happy katika
madhabahu ya mwenye mamlaka
mkuu lakini hakufanya hivyo
baada ya Happy kukataa kujiunga
na Red Mambaz.Imekwisha pita
mwaka mmoja tangu awe Rais na
hajampeleka Happy kwa mkuu na
hicho kinahesabika kama kitendo
cha dharau kwa mkuu na yeyote
anayemdharau mkuu lazima
afe.Dr Mark alitakiwa afariki kwa
kudharau masharti aliyopewa
lakini akaomba msamaha kwa
mkuu na ili asamehewe anatakiwa
kutoa sadaka ya damu
itakayomfurahisha mwenye
mamlaka mkuu.Dr Mark
amekubali kumtoa sadaka
mwanae Happy na watu wengine
kwani sadaka ya kuomba
msamaha inatakiwa iwe damu ya
watu kuanzia hamsini na
kuendelea” akasema Linah
“Dah ! Huu ni ukatili
usiovumilika” akasema Mathew
“Ni ukatili lakini lazima hilo
lifanyike ama sivyo Dr Mark
atapoteza maisha”akasema Linah
“Lini na wapi sadaka hiyo
itatolewa? Akauliza Mathew
“Happy anaimba kwaya
katika kanisa lao na Rais
amejitolea kuifadhili kwaya hiyo
kwenda nchini Rwanda kushiriki
katika tamasha la uimbaji.Kwa
jumla kwaya hiyo ina watu zaidi
ya sabini na Rais amewakodishia
ndege itakayowapeleka Rwanda
na kuwarudisha
nyumbani.Wanakwaya hao
hawatafika huko wanakoelekea
ndege itaanguka njiani na wote
watafariki dunia na hiyo ndiyo
salama ya Dr Mark” akasema
Linah na kumtazama Mathew
“Mathew kuna nyakati
zimekuwa zikifululiza ajali
mbaya na kuchukua uhai wa watu
wengi.Wakati mwingine ajali hizo
hazitokeiu kwa bahati mbaya bali
ni Red Mambaz wanakuwa kazini
katika kutoa sadaka ya damu kwa
mkuu wao.Mathew hii ni siri
kubwa sana na nimekueleza wewe
kwa kuwa ninakuamini hivyo
jitahidi kufanya kila
linalowezekana kuwaokoa watu
hao ambao wanakwenda kutolewa
uhai wao bila kosa lolote.Wote
hao zaidi ya sabini wataangamia
kwa sababu ya Happy kukataa
kujiunga na Red Mambaz.We
must save them” akasema Linah
“Ni namna gani ndege hiyo
itaangushwa? Mathew akauliza
“Litapelekwa kundi la ndege
wakubwa ambao wataingia katika
injini na kusababisha hitilafu
kubwa na ndege hiyo
itaanguka”akajibu Linah na
Mathew akafikiri kidogo na
kusema
“Linah ilikuaje ukaingia
katika jamii hiyo ya wauaji na
kuyaharibu maisha yako kiasi
hiki? Hukufikiria madhara yake
kabla ya kujiunga na huo
ushetani? Akauliza Mathew
“Mathew nimesema
nitakueleza kila kitu kwa nini
nilijikuta katika jamii ya watu
hao.Sikutegemea kama siku moja
maisha yangu yangebadilika na
kuwa namna hii,sikutegemea
kama siku moja ningetoa roho ya
mtu lakini maisha niliyopitia
yamenilazimisha niwe hivi
nilivyo leo.Ninajutia yale
niliyoyafanya,ninajutia
kuyaharibu maisha yangu lakini
nina nafasi ndogo ninayo bado
kabla hawa jamaa hawajaniua na
ninataka kuitumia nafasi hiyo
kuwasaidia wale wasio na hatia
ambao wako katika orodha ya
kuuawa” akasema Linah Mathew
akamtazama na kusema
“No body is goig to kill you
Linah,I’ll protect you! Akasema
Mathew na Linah akatabasamu
“Mathew hawa jamaa wana
nguvu kubwa na wana mtandao
mrefu pia wanaweza kuingia
sehemu yoyote na wakafanya
chochote.Nilikueleza awali kuwa
kumekuwa na wimbi kubwa la
vijana
hasa,wanamuziki,wanasiasa na
wanamichezo kutafuta mafanikio
na umaarufu mkubwa na
wanapopewa masharti
hukubaliana nayo kuyatekeleza
yote na baada ya kupata
mafanikio na umaarufu hujikuta
wakibeba mzigo mzito wa
kutimiza masharti waliyopewa na
hapo huanza kutafuta njia za
kutoka lakini tayari huwa
wamechelewa kwani mara tu
unapojiunga na jamii yetu
unakuwa umemkabidhi shetani
maisha yako na hakuna namna ya
kuweza kutengua mkataba wako
na shetani hivyo ukivunja
masharti hakuna msamaha ni
kuuawa.Mimi sikujiunga kwa ajili
ya kupata mali wala umaarufu
nilitaka kulipiza kisasi kwa wale
wote waliotutesa mimi na wadogo
zangu na kutusababishia
umasikini mkubwa baada ya
wazazi wetu kufariki.Sikuweka
dhamana mtu yeyote nilijiweka
dhamana mwenyewe ili
nitakapokiuka masharti basi
niuawe mimi mwenyewe na
nikapelekwa nje ya nchi kupatiwa
mafunzo ya uuaji nikarudi nchini
na kuanza kazi yangu
nikafanikiwa kuwamaliza wale
wote waliotudhulumu mali zetu
na kutusababishia umasikini
mkubwa.Baada ya kuimaliza kazi
yangu ndipo nikaamua kuanza
maisha mapya na kutafuta
mwanaume ambaye nitaishi naye
lakini mambo hayakwenda vizuri
kama nilivyokueleza.Sitaki
kuendelea tena na hawa
mashetani ndiyo maana nikakata
kile kidole chenye pete yao japo
si njia ya kuwakimbia lakini
nimekwisha tuma ujumbe kwao
kwamba mimi si mtu wao tena
hata hivyo lazima watanisaka
wanimalize.Miongoni mwao kuna
majasusi na kuna wauaji kama
m…..aaagghhhh !! Linah akatoa
ukelele na kuanguka sofani na
mara ukatokea mlio katika sofa
walilokuwa wamekalia.Risasi
ilimkosa Linah na kupiga sehemu
ya juu sofa baada ya Linah
kuanguka sofani na Mathew kwa
kasi ya ajabu akaruka nyuma ya
lile sofa na kulibinua likaanguka
na kuwakinga.Haraka haraka
akatoa bastola akajaribu
kuchungulia kama angeweza
kumuona mtu yeyote lakini
hakumuona mtu.
“Lazima kuna mdunguaji
amejificha sehemu! akasema
Mathew na kumfuata Linah
aliyekuwa ameshikilia bega lake
“Linah are you okay?
“Nimepigwa risasi ya bega !
akasema Linah
“Kuna mdunguaji yuko
sehemu anatufuatilia.Tunatakiwa
kurejea ndani haraka sana”
akasema Mathew na kuhesabu
mpaka tatu kisha wakainuka na
kukimbilia katika mlango wa
kuingilia ndani wakashuka haraka
haraka huku Linah akiendelea
kuvuja damu
“Mathew mambo
yameanza.Jamaa tayari
wanafahamu niko hapa.Hatuko
salama Mathew” akasema Linah

NDUGUMSOMAJI MAMBO
YAMEANZA TENA,
MATHEW MULUMBI USO
KWA USO NA THE RED
MAMBAZ.
ATAFAULU KUMUOKOA
LINAH ASIUAWE?
ATAFANIKIWA KUMUOKOA
HAPPY NA WANAKWAYA
WENZAKE WASIUAWE ?
ENDELEA KUFUATLIA
SIMULIZI HII

You might also like