You are on page 1of 6

FOMU YA MAOMBI

YA KUSHIRIKI MRADI WA VIJANA NA WANAWAKE

(GENERATION FOOD ACCELERATOR - GFA2)

NYANDA ZA JUU KUSINI MWA TANZANIA

MIKOA YA IRINGA NA NJOMBE


1.0 Utangulizi

Mradi huu unasimamiwa na kuendeshwa na shirika la RIKOLTO Afrika Mashariki kwa


kushirikiana na Agriedo hub, Kiota Hub na Agrihub, chini ya program kubwa ya AGRI-
CONNECT inayofadhiliwa na Umoja wa nchi za Ulaya (EU).

Mradi huu utakaoendeshwa kwa kipindi cha mwaka mmoja (2023/2024) ni kwa ajili ya vijana na
wanawake wa Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania (Iringa na Njombe). Mradi umelenga kuibua
na kuboresha biashara bunifu kwenye mnyororo wa thamani wa uzalishaji wa mboga na matunda
pamoja na mifumo ya chakula na lishe. Mradi utaibua vijana na wanawake wajasiriamali wenye
mawazo bunifu ya kibiashara yanayoweza kuendeleza na kukuza usawa wa mnyororo wa
thamani na mifumo ya chakula na lishe katika Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini wa Tanzania
(Iringa na Njombe).

1.1 Vigezo vya kuweza kushiriki

Mshiriki anapaswa kuwa na vigezo vifuatavyo;

 Awe mwenye umri kati ya miaka 18-35.


 Awe ni mkazi wa mkoa wa Iringa au Njombe
 Awe anaweza kusoma, kuzungumza na kuandika lugha ya kiswahili au kiingereza.
 Awe tayari kutenga muda na kushiriki kikamilifu kwenye mradi wa GFA cohort II
 Awe na wazo, sampuli kifani (prototype) au biashara bunifu inayolenga kutatua changamoto
kwenye mnyororo wa thamani wa Mboga na Matunda au Lishe.
 Mwombaji awe na nia na maono ya kukuza na kuendeleza biashara yake kwenye mnyororo
wa thamani wa Mboga na Matunda au Lishe.

1.2 Namna ya kujaza fomu ya maombi

1. Tafadhali jibu maswali yote yaliyopo kwenye fomu hii ya maombi.


2. Zungushia duara au weka tiki katika maswali yanayokutaka kuchagua jibu sahihi.
3. Jibu kwa ufupi na kwa ufasaha kwa maswali ya maelezo.

2.0 Taarifa Binafsi

1. Jina kamili? _________________________________________________________

2. Umri? (a) 18 - 23 (b) 24 - 29 (c) 30 - 35

3. Jinsia? (a) Mwanamke (b) Mwanaume


4. Mkoa unaoishi?

 Iringa ( )
 Njombe ( )

5. Wilaya unayoishi?

 Iringa Mjini ( )
 Iringa Vijijini ( )
 Kilolo ( )
 Mufindi ( )
 Njombe ( )
 Ludewa ( )
 Makete ( )
 Wanging’ombe ( )

6. Namba yako ya simu? ________________________________________________________

7. Barua pepe (kama unayo) _____________________________________________________

8. Mtandao wako wa kijamii (kama unatumia)_______________________________________

9. Hali yako ya Ajira: Nimeajiriwa ( ) Nimeajiajiri ( ) Sina Ajira ( )

10. Kama umeajiriwa, tafadhali andika maelezo mafupi juu ya ajira yako:
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________

3.0 Taarifa za Biashara au Ubunifu

Elezea wazo au biashara yako kwa ufupi;

11. Biashara au ubunifu wako unahusu nini?


___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________

12. Biashara au ubunifu wako umejikita katika eneo gani kati ya haya yafuatayo;

Tafadhali weka tiki kwenye sehemu inayokuhusu


 Uzalishaji wa mboga na matunda ( )
 Uhifadhi wa mazao baada ya mavuno ( )
 Usindikaji wa mboga na matunda ( )
 Usafirishaji na usambazaji wa mboga au matunda ( )
 Usalama wa chakula na ubora wa mboga au matunda ( )
 Sera na sheria wezeshi za uzalishaji na usambazaji wa mboga na matunda ( )
 Teknolojia bora za kulima/ kusindika/ kuhifadhi na kusafirisha mazao ( )
 Pembejeo za kilimo (mbegu, mbolea asilia, viwatilifu asilia, zana za kazi) ( )
 Elimu juu ya lishe bora au kanuni za kilimo bora cha mboga na matunda ( )
 Masoko ya bidhaa za mboga na matunda ( )
 Huduma za kifedha ( )
 Taja mengineyo; ___________________________________

13. Kwa ufupi, elezea tatizo au changamoto iliyopo kwenye tasnia ya mboga na matunda
inayotatuliwa na biashara au ubunifu wako.
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
________________________

14. Elezea kwa jinsi gani suluhisho la biashara yako linavyoweza kutatua tatizo lililotajwa hapo
juu._______________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
_________________________________

15. Chagua hatua ya biashara au ubunifu wako ulipofikia.

 Nina wazo tu la biashara ( )


 Sampuli kifani (mfano wa bidhaa) na inafanya kazi ( )
 Ubunifu uliokamilika na unawatumiaji ( )
 Ubunifu umekamilika na unawateja kiasi ( )
 Ubunifu uliokamilika / nimeshaanza biashara na kuuza ( )

16. Je Ubunifu au biashara yako imesajiliwa?


 Ndiyo ( )
 Hapana ( )
17. Tarehe uliyoanzisha biashara yako?______________________________________________

18. Je biashara au ubunifu wako umesajiliwa katika mamlaka ipi kati ya zifwatazo hapa chini?
 Lessen ya Halmashauri ( )
 BRELA ( )
 TRA ( )
 TCCIA ( )
 TFRA ( )
 TPHPA ( )
 TBS ( )
 SIDO ( )
 Other:______________________________________________________________________________

19. Mtaji wa biashara yako ni shilling ngapi?*


 Sh10,000 - Sh100,000 ( )
 Sh 100,001 - Sh 300,000 ( )
 Sh 300,001 - Sh 700,000 ( )
 Sh 700,001 - Sh 1,500,000 ( )
 Sh 1,500,001 - Sh 3,000,000 ( )
 Sh 3,000,001 - Sh 5,000,000 ( )
 Zaidi ya 5,000,000 ( )

20. Tafadhali eleza kuhusu timu/kikundi chako kwa kutaja majina kamili, jinsia na umri
wao_______________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________

21. Idadi ya wafanyakazi uliowaajiri kwenye biashara yako?

 1-3 ( )
 4-6 ( )
 7-10 ( )
 Other: ( )

22. Kama kuna taarifa za ziada kuhusu biashara au ubunifu wako? Tafadhali elezea
hapa_______________________________________________________________________
4.0 Maelezo ya ziada

23. Je, umeunganishwa na mtandao (internet)?

(a) Ndiyo nimeunganishwa na mtandao una ubora ( )

(b) Ndiyo, nimeunganishwa lakini mtandao hauna ubora ( )

(c) Hapana, sijaunganishwa na mtandao ( )

24. Je, umeshawahi kushiriki kwenye mradi wa GFA katika mwaka uliopita? Ndiyo/Hapana: Kama ndiyo
elezea kwa ufupi? ______________________________________________________________________

25. Ni kwa namna gani ulifahamu juu ya taarifa ya mradi huu wa vijana na wanawake (GFA)?

 ( ) Mitandao ya kijamii
 ( ) Mabango au vipeperushi
 ( ) Matangazo ya radioni
 ( ) Tovuti
 ( ) Marafiki au familia
 ( ) Ofisi za Serikali
 ( ) Njia nyingine tafadhali itaje ___________________________________________

26. Je, una maoni au mawazo ya ziada? (mfano: namna ya ushirikishwaji)

______________________________________________________________________________
______________________________________________________________________________
______________________________________________________________________________
______

Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 20 February 2023, Saa 5:59 usiku. Baada ya kujaza
fomu hii irudishe kwa mtu aliekupatia au ofisi ulipoichukua.

…………………………………….

Taarifa kuhusu washiriki waliochaguliwa, zitatolewa ndani ya kipindi cha wiki 2 mara baada
ya kufungwa kwa tarehe ya kupokea maombi ya usaili. Kwa mawasiliano zaidi tuandikie
kupitia baruapepe; famoustinno@gmail.com au piga simu namba +255 693 90 38 18

You might also like