Professional Documents
Culture Documents
Kitabu Cha Sala Na Nyimbo-1
Kitabu Cha Sala Na Nyimbo-1
NIA NJEMA 9
SALA YA MATOLEO 9
BABA YETU 9
SALAMU MARIA 10
KANUNI YA IMANI 10
AMRI ZA MUNGU 10
AMRI ZA KANISA 11
SALA YA IMANI 11
SALA YA MATUMAINI 11
SALA YA MAPENDO 11
SALA YA KUTUBU 12
MALAIKA WA BWANA 12
MALKIA WA MBINGU 13
SALA YA JIONI 13
KUTUBU 14
KABLA YA KULA 15
Mt. Yohana Mtume - ii
KISHA KULA 15
KUOMBA NA KUSIFU 15
TUNAUKIMBILIA 16
8. EE BWANA TWAKUOMBA 81
28. EE MARYAMU 93
NIA NJEMA
Kumheshimu Mungu wangu namtolea roho yangu, ni-
fanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike. Wazo, neno,
tendo lote namtolea Mungu pote, Roho, mwili, chote
changu, Pendo na uzima wangu, Mungu wangu nitamp-
enda, wala dhambi sitatenda. Jina lako nasifia, utakalo
hutimia, kwa utii navumilia, teso na matata pia. Nipe
Bwana, neema zako niongeze sifa yako. Amina.
SALA YA MATOLEO
Ee Yesu, kwa mikono ya Bikira Maria, na kwa muungano
na sadaka yako kuu, ninakutolea sala, matendo, ma-
sumbuko na furaha zangu zote za leo. Ee Yesu, ufalme
wako utufikie.
BABA YETU
Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe, Ufalme
wako ufike, utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku. Utusamehe makosa
yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usi-
tutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina.
Mt. Yohana Mtume - 9
SALAMU MARIA
Salamu Maria, umejaa neema, Bwana yuu nawe,
umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu, mzao wa
tumbo lako, amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa
Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa
kwetu. Amina
KANUNI YA IMANI
Nasadiki kwa Mungu, Baba mwenyezi, mwumba wa
mbingu na dunia. Na kwa Yesu Kristu, Mwana wa pekee,
Bwana wetu; aliyetungwa kwa Roho Mtakatifu,
akazaliwa na Bikira Maria, akateswa kwa mamlaka ya
Ponsyo Pilato, akasulubiwa, akafa, akazikwa; akashukia
kuzimu; siku ya tatu akafufuka katika wafu; akapaa
mbinguni; amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi;
toka huko atakuja kuwahukumu wazima na wafu.
Nasadiki kwa Roho Mtakatifu, kanisa takatifu katoliki,
ushirika wa Watakatifu, maondoleo ya dhambi, ufufuko
wa miili, na uzima wa milele. Amina.
AMRI ZA MUNGU
1. Ndimi Bwana Mungu wako, usiabudu Miungu wen-
gine.
2. Usitaje bure jina la Mungu wako.
3. Shika Kitakatifu siku ya Mungu.
4. Waheshimu baba na mama, upate miaka mingi na
heri duniani.
5. Usiue.
6. Usizini.
7. Usiibe.
8. Usiseme uwongo.
AMRI ZA KANISA
1. Hudhuria Misa takatifu Dominika na sikukuu
zilizoamriwa.
2. Funga siku ya Jumatano ya majivu; usile nyama siku
ya ljumaa Kuu.
3. Ungama dhambi zako zote walau mara moja kila
mwaka.
4. Pokea Ekaristi Takatifu hasa wakati wa Paska.
5. Saidia kanisa katoliki kwa zaka.
6. Shika sheria katoliki za ndoa.
SALA YA IMANI
Mungu wangu, nasadiki maneno yote linayosadiki, lina-
yofundisha kanisa Katoliki la Roma: Kwani ndiwe uli-
yetufumbulia hayo, wala hudanganyiki, wala udanganyi.
Amina.
SALA YA MATUMAINI
Mungu wangu, natumaini kwako nitapewa kwa njia ya
Yesu Kristu, neema zako duniani na utukufu mbinguni,
kwani ndiwe uliyeagana hayo nasi, nawe mwamini. Ami-
na.
SALA YA MAPENDO
Mungu wangu, nakupenda zaidi ya chochote; kwani ndi-
we mwema, ndiwe mwenye kupendeza. Nampenda na
SALA YA KUTUBU
Mungu wangu, nimetubu sana dhambi zangu, kwani
ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukizwa
na dhambi. Basi sitaki kukosa tena, nitafanya kitubio,
naomba neema yako nipate kurudi. Amina.
MALAIKA WA BWANA
Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria.
Naye akapata mimba kwa Roho Mtakatifu.
Salamu, Maria, ........... .
MALKIA WA MBINGU
Malkia wa mbingu furahi, Aleluya.
Kwani uliyestahili kumchukua, Aleluya.
Amefufuka alivyosema, Aleluya.
Utuombee kwa Mungu, Aleluya.
Furahi, shangilia, ee Bikira
Maria.Aleluya. Kwani, hakika Bwana
amefufuka. Aleluya.
SALA YA JIONI
(Jichunguze kidogo)
KISHA KULA
-Nakushukuru Mungu wangu, kwa chakula ulichonipa,
nipate nguvu za kukutumikia vema. Am ina.
KUOMBA NA KUSIFU
Mungu wangu, nawaombea watu wa nchi hii, wapate
kusikia maneno yako na kukupenda wewe Bwana Mun-
gu wetu.
TUNAUKIMBILIA
Tunaukimbilia, ulinzi wako, mzazi Mtakatifu wa Mungu,
Usitunyime tukiomba katika shida zetu, utuokoe kila
tuingiapo hatarini, ee Bikira mtukufu mwenye baraka.
Amina
Kumbuka
Kumbuka, ee Bikira Maria mpole sana, haijasikika bado
hata mara moja kwamba ulimwacha mtu aliyeukimbilia
ulinzi wako, Akiomba msaada na maombezi yako. Kwa
matumaini hayo nlnakukimbilia wewe, Ee mama, Bikira
wa Mabikira, ninakuja kwako ninasimarna mbele yako
nikilalamika mimi mkosefu. Ee mama. wa Neno la Mun-
gu usikatae maneno yangu, bali upende kuyasikia na
kuyasikiliza, Amina.
Salamu Malkia
Mt. Yohana Mtume - 23
Salamu Malkia mama mwenye huruma; uzima, tulizo na
matumaini yetu salamu. Tunakusihi ugenini hapa sisi
wana wa Eva. Tunakulilia, tunakulalamikia na kuhuzu-
nika bondeni huku kwenye machozi. Haya basi,
mwombezi wetu -Utuangalie kwa macho yako yenye hu-
ruma, na mwisho wa ugeni huu, -Utuonyeshe Yesu na
mzao mbarikiwa wa tumbo lako.
Ee mpole, Ee mwema Ee mpendelevu Bikira Maria.
1. Baba Yetu
2. Salamu Maria
3. Nasadiki
4. Baba wa Milele, ninakutolea MWILI na DAMU, ROHO
na UMUNGU wa Mwanao Mpenzi, Bwana wetu Yesu
Kristu kwa kulipia dhambi zetu na dhambi za dunia
nzima
5. Kwa ajili ya Mateso makali ya Yesu, Utuhurumie sisi
na dunia nzima.
Kumaliza
Mt. Yohana Mtume - 26
Mungu Mtakatifu, Mtakatifu Mwenye Enzi Mtakatifu
Uishiye milele, utuhurumie sisi na dunia nzima. x 3
Maria ametusaidia,
Maria anataka kutusaidia,
Maria anaweza kutusaidia,
Maria atatusaidia.
3. Kwenye chembe kubwa:
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,
Kama mwanzo na sasa, na siku zote, na milele.
Amina.
Maria ametusaidia,
Maria anataka kutusaidia,
Maria anaweza kutusaidia,
Maria atatusaidia.
Wimbo:
Umekosa nini we Yesu
Kushitakiwa bure kwa Pilato
Wenye kustahili hukumu
Si wewe, si wewe Bwana, ni sisi.
Wimbo:
Ole msalaba huo mzito
Apagazwa mwana mpenzi wa Mungu.
Mwili waenea mateso
Alipa, alipa madhambi yetu.
Wimbo:
Wimbo:
Wimbo:
Wimbo:
Uso wa Yesu malaika
Betlehemu walikuabudu
Bahati yake Veronika
Kupangusa, kupangusa mfalme wa mbingu.
Wimbo:
Yesu amefufuka
SALA YA MWISHO
(Mbele ya Altare)
TUOMBE
Mt. Yohana Mtume - 46
Ee Mungu, uliye Mwumba wa vitu vyote, tunakuomba usikilize
kwa wema sala zetu sisi taifa lako, utuongoze sote tufuate siku zote
utarati- bu wa mapenzi yako; naye Roho Mtakatifu atutegemeze
mpaka mwisho wa NOVENA hii. Tunaomba hayo kwa njia ya
Kristo Bwana wetu.
W. Amina
TUOMBE
Ee Mungu, unapenda watu wote waokoke, wafikie kweli yako. Tu-
nakuomba upeleke wafanya kazi walio wengi na wema katika
shamba lako. Uwajalie kulihubiri neno lako kwa imani kuu, ili neno
lako lienee na kupokelewa na mataifa yote, wapate nao kukujua
wewe peke yako Mungu wao, Mungu wa kweli. Tunaomba hayo
kwa nguvu ya Roho Mtakatifu anayeliongoza Kanisa lako sasa na
milele
W. Amina.
Bwana alisema kwa kinywa cha Nabii Yoeli: “Katika siku zile za
mwi- sho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho
wangu. Wa- toto wenu, waume kwa wake, watautangaza ujumbe
wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota
ndoto.... Hata wa- tumishi wenu watamiminiwa Roho wangu katika
siku zile, nao watau- tangaza ujumbe wangu" (Mdo. 2: 17-21)
Siku ile ya Pentekoste, baada ya Roho Mtakatifu kulishukia
Kanisa, Mtume Petro aliwakumbusha watu maneno hayo ya Nabii
Yoeli. Na miaka mingi baadaye. Petro aliwaandikia barua wakristu
wa kwanza, akiwaamba "Kila mmoja anapaswa kutumia kipaji
alichojaliwa na Mungu kwa faida ya wengine, kama vile wakili
mwema wa zawadi mbalimbali za Mungu. Anayesema kitu,
maneno yake na yawe kama maneno ya Mungu; anayetumikia
anapaswa kutumikia kwa nguvu aliyojaliwa na Mungu, ili katika
mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristu, ambaye
utukufu na nguvu ni vyake milele na milele"(1 Pet. 4: 10-11)
Mtaguso wa II wa Vatikano ulitukumbusha jambo hilohilo
ulipose- ma: "Roho Mtakatifu anayelitakasa taifa la Mungu kwa
Mt. Yohana Mtume - 49
njia ya Sakramenti amewapa waumini mapaji ya pekee na
kumjalia kila mmoja kadiri apendavyo. Kwa hiyo kila mmoja
amgawie mwenzake kadiri ya vipawa alivyopewa, awe mgawaji
mwaminifu wa neema ya Mungu, alijenge Kanisa zima katika
upendo."
Tunao wajibu wa kutumia vipawa tulivyojaliwa na Roho Mtakatifu
kwa manufaa ya Kanisa zima, na kwa faida ya watu wote.
Tuunganike sote pamoja na wachungaji wetu katika kazi hiyo ya
utume. Tum- wombe nasi Roho Mtakatifu atusaidie kutumia vema
vipawa vyake alivyotujalia katika kazi hiyo ya utume. Tumwombe
basi Roho Mta- katifu atusaidie kutumia vema vipawa vyake
alivyotujalia.
2. Utujalie sisi sote mapaji yako saba, tupate kukutumikia kwa uchaji.
W. Twakuomba utusikie.
TUOMBE
Ewe Roho wa Mungu, ndiwe unayewapa waumini vipawa vyako
kwa kadri unavyotaka. Utujalie tuyapokee na kuyatumia vema
mapaji yako mengi kwa ajili ya utukufu wa Jina lako, na kwa ajili
ya wokovu wa watu wote. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu
Bwana wetu.
W. Amina.
TUOMBE
Ee Mungu, utuunganishe sisi kondoo wako tuliotawanyika, tuwe
chi- ni ya Mwanao mpenzi, tupate sote kuushiriki ule utawala wako
wa kweli na haki, utawala wa neema na amani, utawala wa upendo
wako. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu.
W. Amina.
W. Twakuomba utusikie.
3. Utuwezeshe kuendelea katika utakatifu na kutenda mema
kwa imani siku zote za maisha yetu.
W. Twakuomba utusikie.
TUOMBE
Ee Mungu, mbele yako mioyo yote iwazi; wewe wajua yote, wala
haku- na siri iliyofichika mbele yako. Uyatakase mawazo ya mioyo
yetu kwa kutupelekea Roho Mtakatifu, ili tuweze kukupenda na
kukutukuza kama unavyostahili. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu
Bwana wetu.
W. Amina.
TUOMBE
Ee Bwana Mungu wetu, tunakuomba neema ya Roho Mtakatifu itu-
angaze akili na mioyo yetu na kutujaza nguvu ya upendo wako.
Tuna- omba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu.
W. Amina.
TUOMBE
Ee Mungu, Baba wa utukufu, tunaomba utupe Roho wako wa
heki- ma, atuwezeshe kukufahamu vema, atuongoze tuishi maisha
yenye kukupendeza. Utusaidie kupambana na matatizo ya maisha,
tupate kuishi maisha mema hapa duniani na mwishowe tupate
tuzo la heri na furaha yako huko mbinguni. Tunaomba hayo kwa
njia ya Kristu Bwana wetu.
W. Amina.
TUOMBE
Ee Yesu Bwana wetu, uliyesema: Pasipo mimi hamwezi kitu;
umpeleke Roho Mtakatifu atuangaze akili zetu, tupate kufahamu
mapenzi yako na kuyatimiza kwa imani na uchaji. Roho
Mtakatifu atuongoze katika mambo yote, yeye anayeishi na
kutawala nawe pamoja na Baba, daima na milele.
W. Amina.
TUOMBE
Ee Mungu, tunakushukuru kwa neema ulizotujalia, hata tukaweza
kuifanya ibada hii ya Novena takatifu mpaka mwisho. Utujalie
mema yote tuliyoomba; utusaidie kutekeleza yote yale
tuliyokusudia kuten- da. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana
wetu.
W. Amina.
SIKU YA KWANZA
SALA:
Ee Yesu mwenye Huruma nyingi, unayetuonea huruma
na kutusamehe, usizitazame dhambi zetu ila tu matu-
maini tuliyo nayo katika wema wako usio na mipaka;
utupokee sisi sote katika makao ya Moyo wako wenye
huruma na usituache kamwe. Tunakusihi kwa njia ya
upendo wako unaokuunganisha na Baba na Roho Mta-
katifu.
SIKU YA PILI
SALA:
Ee Yesu mwenye Huruma nyingi, uliye asili ya mema
yote, tuongezee neema ya kutenda matendo ya huruma
ili wote wanaotutazama, wamtukuze Baba wa Huruma
aliye juu mbinguni.
SIKU YA TATU
SALA:
Ee Yesu mwenye Huruma nyingi, unayewajalia wote
neema zako tele kutoka katika hazina ya Huruma yako,
utupokee sisi katika makao ya Moyo wako wenye Hu-
ruma na usituache kamwe. Tunakusihi kwa njia ya up-
endo wako wa ajabu ulio nao kwa Baba wa milele.
SIKU YA NNE
Maneno ya Yesu kwa Sista Faustina:
"Uniletee leo wapagani na wote wasionijua bado. Hata
wao niliwafikiria katika mateso yangu makali na bidii
yao ijayo iliufariji Moyo wangu. Uwazamishe katika ba-
hari ya Huruma yangu".
SALA:
Ee Yesu mwenye Huruma nyingi, uliye nuru ya ulimwen-
gu mzima, uzipokee kwenye makao ya Moyo wako
wenye Huruma roho za wapagani zisizokujua bado; mi-
ali ya neema zako iziangaze ili nazo pamoja nasi
ziitukuze Huruma yako ya ajabu na Wewe mwenyewe
usiziache kamwe.
SIKU YA TANO
SALA:
Ee Yesu mwenye Huruma nyingi, uliye wema kamili,
Wewe hukatai kuwajalia wakuombao mwanga wako; uz-
ipokee kwenye Makao ya Moyo wako wenye Huruma
roho za ndugu zetu wa madhehebu mengine na uzivute
katika mwanga wako ili ziwe na umoja na Kanisa;
usiziache kamwe, bali uzijalie neema ya kuuabudu
ukarimu wa Huruma yako.
SIKU YA SITA
SALA:
Ee Yesu mwenye Huruma nyingi, uliyesema: "Jifunzeni
kwangu, kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa
Moyo", uzipokee roho pole na nyenyekevu pamoja na za
watoto wadogo katika makao ya Moyo wako wa Hu-
ruma. Roho hizi zinastaajabisha mbingu zote na
kumpendeza Baba wa mbinguni kwa namna ya pekee;
ndizo shada yenye harufu tamu iliyopo mbele ya kiti cha
enzi cha Mungu; harufu ambayo yampendeza Baba.
Roho hizi zina makao ya milele Moyoni mwako na daima
zinaimba wimbo wa upendo na Huruma. Baba wa
milele, uzitazame kwa jicho la Huruma roho pole na
nyenyekevy na za watoto wadogo, zilizofungwa katika
makao ya Moyo wa Yesu wenye Huruma. Roho hizi
zafanana sana na Mwanao; harufu tamu ya roho hizo
inapaa kutoka dunia hii na kukifikia kiti chako cha enzi.
Ee Baba wa Huruma na wa Wema wote, ninakusihi kwa
njia ya upendo na upendeleo wako kwa roho hizo,
uibarikie dunia yote ili roho zote ziimbe kwa pamoja sifa
za Huruma yako milele yote. Amina.
SIKU YA SABA
SALA:
Ee Yesu mwenye Huruma nyingi, ambaye Moyo wako ni
upendo kamili, uzipokee kwenye makao ya Moyo wako
wenye Huruma roho ziabuduzo na kutukuza kwa namna
ya pekee ukuu wa Huruma yako. Nguvu yao ni nguvu
ya Mungu mwenyewe, katika masumbuko na magumu
zinasonga mbele zikiitumainia Huruma yako. Roho hizo
zimeungana na Yesu na kuubeba ulimwengu mzima ma-
begani mwao. Roho hizo hazitahukumiwa vikali, bali Hu-
ruma yako itazilinda saa ya kufa kwako.
SIKU YA NANE
Maneno ya Yesu kwa Sista Faustina:
"Leo uniletee roho zilizomo Toharani na kuzizamisha
katika Shimo la Huruma yangu; mito ya Damu yangu
ipoze joto lao. Nazipenda sana roho hizo zote. Zinalipia
fidia kwa Haki yangu. Wewe una uwezo wa kuziletea
unafuu. Tumia rehema zote za Kanisa langu na kuzitoa
kwa ajili yao. Laiti ungejua mateso yao, ungekuwa un-
atoa fidia ya dhambi zao na kulipa madeni yao kwa Haki
ya Mungu".
SALA:
Ee Yesu mwenye Hururna nyingi, uliyesema mwenyewe
kuwa wataka huruma; basi, naingiza kwenye makao ya
Moyo wako wa Huruma roho zilizomo Toharani, zi-
nazokupendeza, ambazo lazima kwanza zitoe fidia kwa
Haki yako. Mito ya Damu na Maji vilivyomwagika kutoka
moyoni mwako viuzimishe moto wa Toharani ili napo pia
Huruma yako itukuzwe.
SIKU YA TISA
SALA:
Ee Yesu mwenye Huruma nyingi, uliye wema kamili,
naingiza katika makao ya Moyo wako wenye Huruma
roho baridi zipate kuota moto wa mapendo yako safi;
roho hizi zinazofanana na maiti na kukuchukiza Wewe.
Ee Yesu mwenye Huruma, tumia ukuu wa Huruma yako
uzivute roho hizo na kuziweka katikati ya moto wa
mapendo yako, uzijalie upendo mtakatifu kwani Wewe
waweza yote.
Kiit:
Nitajongea Altare yako,
Furaha yangu na heri yangu siku zote.
Kiit:
Nayatamani, nayatamani makao ya Bwana x2
maskani yake Bwana yapendeza kama nini. x2
Kiit:
Nimeingia (hapa) hapa mahali patakatifu. Unipokee
(kwako) unitakase nipate neema. x2
Kiit:
Kwa nyimbo za shangwe: Twendeni wote, twendeni wote,
tumwabudu Bwana. Kwa furaha. Twendeni wote, twendeni
wote, tumwabudu Bwana.
Kiit:
Kikondoo cha Mungu, Mkate wa mbinguni,
Mlishi wa roho yangu, Nakuabudu
Kiit:
Mt. Yohana Mtume - 80
Kweli, kweli, wisho uwe uwingu x 2
8. EE BWANA TWAKUOMBA
Kiit:
Ee Bwana twakuomba upokee vipaji vyetu (x2),
Hivyo vyote ni mali yako,
Tumepata kwa wema wako pokea. (x2)
Kiit:
Mt. Yohana Mtume - 81
Roho yangu Yesu inakutamani,
Njoo kwangu Yesu unipe heri (x2).
Kiit:
Hivi ndivyo wote wenye kumcha Bwana
watakavyobarikiwa naye x2.
Mt. Yohana Mtume - 82
1. Amchaye Bwana atastawi; kama mwerezi wa
Lebanoni.
2. Heri yule amchaye Bwana, na kupendezwa na amri
zake.
3. Wazao wake watakuwa hodari, kizazi cha waadilifu
kitabarikiwa.
Kiit:
Nikupe nini Mungu wangu,
Nikupe nini we Mwokozi,
Nikupe nini Bwana wangu cha kukupendeza (x2)
Kiit:
Roho yangu Yesu inakutamani,
Njoo kwangu Yesu unipe heri (x2).
Kiit:
Ee Baba pokea vipaji hivi,
Sadaka ya Mwanao Mpenzi.
Kiit:
Hiki ni chakula cha mbingu,
Mkate safi kwa wampendao,
Kweli ni uzima wa roho.
Kiit:
Enyi watu wote pigeni makofi,pigeni makoti,
Mshangilie, Mshangilieni mungu kwa sauti ya
shangwe.
Kiit:
Ee Bwana twakuomba upokee vipaji vyetu x2
Hivyo vyote ni mali yako,
Tumepata kwa wema wako pokea.
Kiit:
Ekaristi ni chakula bora,
Yesu Kristo akaa ndani yake,
Atulisha atushibisha daima.
Kiit:
Aulaye mwili wangu, na kuinywa damu yangu,
Asema Bwana, hukaa ndani yangu nami hukaanda-
ni yake.
Kiit:
Yesu asante sana,Yesu asante sana,
Kujifanya chakula, Kujifanya chakula
Kujifanya chakula, Kutuletea shibe alama ya pendo
x2
1. Uloonyesha kwetu ni mapenzi mazito yasiyo na mwi-
sho,
Na wenye sikitiko unawapa tulizo kuwaponyesharoho.
2. Mapenzi yoko Yesu hatuwezi kupima sisi wana wako,
Ulionyesha pendo ukajifanya wewe mlo wetu sote.
3. Kushukuru twashindwa mapenzi ya kulipa roho tun-
ashindwa
Ukae mwangu Yesu nami nikae mwako daima milele.
Kiit:
Tunakushukulu Mama Maria,
Kwa neema unazotujalia,
Asante Mama wa Yesu uliye na huruma,
Uzidi kutuombea mpaka saa ya kufa.
Kiit:
Kiit:
Mimi ni mtumishi wake Bwana, nitendewe ulivy-
onena x 2
Nitendewe ulivyonena, mimi ni mtumishi wa Bwa-
na (wa Bwana) mimi ni mtumishi wa Bwana ni-
tendewe ulivyonena x 2
28. EE MARYAMU
Kiit:
Salaam, salaam, salaam Maria x 2
Kiit:
Tumaini letu mama (yetu), Mama Maria
tumaini letu mama (yetu), ee mama mwema ndiwe
tumaini letu ewe mama yetu Maria x 2
Kiit:
Mama yetu Maria tunakukimbilia (mama)
sisi wanawako tunaosumbuka ugenini x 2
Mt. Yohana Mtume - 94
1. Utulinde katika shida na taabu zote -Utujalie neema
zako tunapo anguka.
2. Mama yetu mpendelevu -Utusimamie, -Utukinge na
mabaya yote ya mwovu shetani.
3. Twakuomba bila kuchoka ewe mama yetu -Utuinulie
macho yako -Utusikilize.
4. Sala zetu uzifikishe kwa mwanao mpenzi atuondolee
dhambi zetu tulizozitenda.
Kiit:
Ee mama yetu Maria twaomba sana
Ee mama usituache gizani, kwa mwanao tuombee x
2
Kiit:
Mariamu ee zipokee hizo zako heshima
Twakuimba, twakuomba, utuelekee mama
Kiit:
Tunakushukuru Mama Maria,
Kwa neema unazotuombea,
Asante Mama wa Yesu uliye na huruma,
Uzidi kutuombea mpaka saa ya kufa.
Kiit:
Maryam Bikira aliteuliwa na Mungu mwenyezi ku-
shiriki ukombozi wa taifa lake na dunia yote.
Naye akazaa mtoto mwanaume atakayewachunga
mataifa yote kwa fimbo ya chuma na mtoto wake
akanyakuliwa kwangu, na kwa kiti chake cha enzi.
Kiit:
Kwa ishara ya msalaba tuokoe x2
Kiit:
Kristu alijinyenyekeza x2.
Akawa mtii hata mauti na-am mauti ya msalaba x2
Kiit:
Twimbe, twimbe jamani, salamu Yesu msalabani.
Kiit:
Tumekosa, kweli tumekosa, tunaomba Bwana
tusamehe makosa yetu twayatubu.
43. UTUREHEMU:
Mt. Yohana Mtume - 102
Kiit:
Uturehemu ee Bwana kwa kuwa tumetenda
dhambi x2
Kiit:
Ataniita nami nitamwitikia,nitamwokoa, na
kumtukuza X2
Kiit:
Baba mikononi mwako, naiweka roho yangu
Kiit:
Kiit:
Mtazame Mkombozi Msalabani
Alivyotundikwa pasipo na kosa
Ili sisi sote tukombolewe X 2
Kiit:
Mungu wangu, Mungu wangu mbona umeniacha
Kiit:
Kiit:
Kiit:
Kiit:
Kiit:
Kiit:
Kiit:
Yesu wangu niokoe,
( Ulimwegu nilimo ni wa mateso
Nishike mkono wangu Bwana niokoe
Ulikuja duniani kwa wadhambi,
Nitakase kwa damuyo Bwana nitakate
Bwana nakukimbilia ) x 2
Kiit:
Mt. Yohana Mtume - 116
Jiwe walilokata waashi limekuwa jiwe kuu
lapembeni, limekuwajiwe kuu lapembeni.
Kiit:
Ninakulilia. katika unyonge wangu, ewe kinga
yangu
Kiit:
Kesheni kila wakati, ndugu kila wakati, mpate kuo-
koka.
Kiit:
Tumaini letu ni kwa Bwana, kwa maana ana uwezo
wa milele.
Kiit:
Bwana ndiye Mchungaji wangu sitapungukiwa na
kitu
Kiit:
Huo ndio ni mwanzo wa ufalme wa Mungu.
Kiit:
Simama imara jilinde Neno lake Bwana, imara
kesha kila siku uombe utasimama x 2
Kiit:
Tawala Bwana, Tawala Bwana
Kiit:
Tawala tawala, tawala kwetu,
Bwana Yesu.