You are on page 1of 4

Imani Ya Nike / The Nicene Creed

  Nasadiki kwa Mungu mmoja, Baba Mwenyezi, Muumba wa mbingu na dunia, na


vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana.
 
Nasadiki Bwana mmoja, Yesu Kristo, Mwana wa pekee wa Mungu, amezaliwa na
Baba mbele ya kuwa ulimwengu, Mungu kutoka Mungu, mwanga kwa mwanga,
Mungu kweli kwa Mungu kweli, amezaliwa, hakuumbwa, Mwenye umungu
mumoja na Baba.
Vitu vyote viliumbwa naye. Alishuka toka mbinguni, kwa ajili ya sisi watu, na kwa
ajili ya wokovu wetu; alitwaa mwili kwa tendo la Roho Mtakatifu, katika Bikira
Maria, akawa mtu. Akasulibiwa kwa ajili yetu, wakati wa Pontio Pilato, akateswa,
akazikwa, Akafufuka kisha siku tatu, kama ilivyoandikwa; akapanda mbinguni,
anakaa kwa mukono wa kuume kwa Baba.
Ndipo atarudi kwa utukufu, kuwahukumu wazima na wafu, na ufalme wake
hautakuwa na mwisho.
 
Nasadiki kwa Roho Mtakatifu, Bwana na Mtoa uzima, aliyetoka kwa Baba na
Mwana, anayeabudiwa na kutukuzwa, pamoja na Baba na Mwana, aliyesema kwa
manabii
 
Nasadiki Kanisa, moja, takatifu, katoliki, lililotoka kwa Mitume.
Ninasadikia ubatizo mmoja kwa kuondolewa kwa dhambi. 
Nangojea ufufuko wa wafu na uzima wa milele utakaokuja.  Amina.

SALAM, MALKIA! / Hail, Holy Queen / Salve Regina

Salam, Malkia! Mama mwenye huruma uzima tulizo matumaini yetu. Salam!
Tunakusihi ugenini sisi wana wa Eva. Tunakulilia tukilalamika na kuhuzunika
huku bondeni kwenye machozi. Haya basi mwombezi wetu utuangalie kwa macho
yako ya huruma, Na mwisho wa ugeni huu utuonyeshe Yesu mzao mbarikiwa wa
tumbo lako. Ee mpole, Ee mwema, Ee mpendelevu Bikira Maria.

Matendo Ya Rozari Takatifu


MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)
Tendo la kwanza; 
Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. 
Tumwombe Mungu   atujalie unyenyekevu.

Tendo la pili; 
Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti.  
Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.

Tendo la tatu; 
Yesu anazaliwa Betlehemu.  
Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara

Tendo la nne; 
Yesu anatolewa hekaluni.  
Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.

Tendo la tano; 
Maria anamkuta Yesu hekaluni.  
Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.

MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)

Tendo la kwanza; 
Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu.  
Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.

Tendo la pili; 
Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu.  
Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.

Tendo la tatu; 
Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. 
Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.

Tendo la nne; 
Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu.  
Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
Tendo la tano;
Yesu anakufa Msalabani. 
Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.

MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)

Tendo la kwanza; 
Yesu anafufuka.  
Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.

Tendo la pili; 
Yesu anapaa mbinguni. 
Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.

Tendo la tatu; 
Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. 
Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.

Tendo la nne; 
Bikira Maria anapalizwa mbinguni. 
Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.

Tendo la tano; 
Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni.  
Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.

MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)

Tendo la kwanza; 
 Yesu anabatizwa Mto Jordani. 
Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
Tendo la pili; 
Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana.  
Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.

Tendo la tatu; 
Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. 
Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.

Tendo la nne; 
Yesu anageuka sura. 
Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.

Tendo la tano; 
Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia.  
Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.

You might also like