Professional Documents
Culture Documents
Sintaksia Ya Kiswahili
Sintaksia Ya Kiswahili
TANZANIA
SWALI: Kulikoyela Kahigi au Kulikoyela Kahigi na Mugyabuso Mulokozi ndio washairi nguli
kifani kuliko mshairi yeyote wa Kiswahili. Thibitisha hoja hii kwa mifano dhahiri ya mbinu
zake/zao tatu za kifani au kanusha kwa mifano thabiti.
Kwa mujibu wa Mulokozi na Kahigi (1982). Wao wanafasiri kuwa ushairi ni sanaa
iliyopambanuliwa kwa mpangilio maalumu wa maneno fasaha na yenye muwala kwa lugha ya
mkato, picha, sitiari au ishara katika usemi, maandishi au mahadhi ya wimbo ili kuleta wazo au
mawazo, kufunzu au kueleza tukio au hisia fulani kuhusu maisha au mazingira ya binadamu kwa
njia igusayo moyo
Kwa mujibu wa Abedi (1954). Ushairi au utenzi ni wimbo, hivyo kama shairi haliimbiki
halina maana
Kwa mujibu wa Shaban Robert (1958). Ushairi ni sanaa inayopambanuliwa kama nyimbo,
mashairi au tenzi zaidi ya kuwa sanaa ya vina, ushairi una ufasaha wa maneno machache au
muhtasari, mawazo, maoni na fikra za ndani zinazoelezwa kwa muhtasari wa ushairi huvuta
moyo kwa namna ya ajabu
Kezilahabi J. M(1976). Ushairi ni tukio, hali au wazo ambalo limeoneshwa kwetu kutokana
na upangaji mzuri wa maneno fasaha yenye mizani kwa kifupi ili kuonesha ukweli fulani wa
maisha
Kwa ujumla, ushairi ni utungo ambao hutungwa kwa kutumia lugha teule ambayo agalau
huwa lugha mkato na lugha fishe, fauku ya hayo, utungo huu huwa na muwala yaani mtiririko au
mpangilio mzuri wa mawazo kutoka neno moja hadi lingine
0
Kwa mujibu wa Sw. M. Wikipedia. Org(2022). Fani ni mbinu anayoitumia mwandishi wa ila
kufikisha ujumbe uliowakusudia hadhira
Kwa mujibu wa Senkoro(2011). Anasema fani ni katika fasihi ni ule ufundi wa kisanaa
anaotumia msanii katika kazi katika kazi yake, ni ufundi wa msanii katika kuumba umbo la kazi
ya fasihi kutokana na ubunifu wake. Anaendelea kusema, fani ni ufundi ambao msanii anautumia
katika kufikisha ujumbe ujumbe kwa jamii
Mbinu za kifani zimegawanyika katika vipengele tofautitofauti kama vile muundo, mtindo,
matumizi ya lugha, wahusika, mandhari/muktadha. Katika swali letu limetutaka kutumia mbinu
tatu za kifani ambapo tumependekeza muundo, mtindo na matumizi ya lugha
Kulikoyela K. Kahigi na Mugyabuso Mulokozi sio washairi nguli kifani katika uandishi
wa mashairi ya Kiswahili kwa sababu hawajazingatia vipengele mbalimbali vya kifani kama vile
muundo wa shairi, mtindo wa shairi pamoja na matumizi ya lugha katika uandishi wa mashairi
yao ambayo ni diwani ya MAGEUZI iliyoandikwa na Kulikoyela K. Kahigi na diwani ya TENZI
TATU ZA KALE iliyoandikwa na Mugyabuso Mulokozi
Katika kipengere cha muundo; muundo ni umbo na mpangilio wa kazi ya fasihi, katika
ushairi wa Kiswahili, mashairi huwa na miundo mbalimbali inayohusisha idadi ya mistari
(vipabde au mishororo katika kila ubeti, mathalani mashairi ya tathimina, tathinia, tathilitha,
tarbia, takhimisa, tasdisa, usaba, unane, utisa na ukumi: Senkoro 2011). Pia muundo wa ushairi
wa Kiswahili huhusisha vipengele mbalimbali kama vile mshororo, vina, mizani, beti kituo au
kibwagizo. Lakini katika diwani ya MAGEUZI iliyoandikwa na Kulikoyela K. Kahigi pamoja
na diwani ya TENZI TATU ZA KALE iliyoandikwa na Mugyabuso Mulokozi. Diwani hizi
katika uandishi wake waandishi hawajaweza kuzingatia vipengele mbalimbali vya muundo kama
vile
1
Beti; katika diwani ya MAGEUZI mwandishi Kulikoyela K. Kahigi hajaonesha idadi ya beti
alizoziandika katika diwani yake. Mfano katika shairi la "Ngao za kienyeji" (uk36), Mwandishi
Kulikoyela Kahigi ameshindwa kuonesha idadi kamili ya beti katika shairi hilo. Pia katika shairi
la "Sikuwa na Haja" uk29. Pia katika diwani ya TENZI TATU ZA KALE mwandishi M.
Mulokozi ametumia mabeti mengi katika kichwa kimoja cha tenzi. Mfano katika utendi wa
"Fumo Liyongo" ametumia mabeti 232 ambapo kichwa kimoja cha shairi kinafaa kisizidi mabeti
20
Mishororo; Ni kila idadi ya mistari katika kila ubeti, katika diwani ya “MAGEUZI
mwandishi Kulikoyela Kahigi hajafuata kigezo cha mishororo Katika mashairi yake. Mfano
katika shairi la "Ngao za Kienyeji" (uk36), katika ubeti wa kwanza ametumia mishororo mitano
(takhimisa) lakini ubeti wa pili hajabainisha idadi kamili ya mishororo. Pia katika diwani ya
"TENZI TATU ZA KALE" iliyoandikwa na Mugyabuso Mulokozi katika kigezo cha mishororo
ametumia tarbia tu au mashairi yenye mishororo minne tu, Wakati katika mishororo zipo aina
nyingi za mishororo kama vile tamolisa(mashairi yenye mshororo mmoja), tathinia (mashairi
yenye mishororo miwili), tathilitha (mashairi yenye mishororo mitatu), tarbia (mashairi yenye
mishororo minne) na kadhalika....
Vina na Mizani; Mizani ni idadi kamili ya silabi katika kila mshororo lakini vina vipo
vya aina mbili, vina vya kati na vina vya mwisho. Katika diwani ya MAGEUZI mwandishi
Kulikoyela Kahigi hajaonesha vina vya katika na vina vya mwisho katika mashairi yake na pia
mishororo katika kila ubeti haina idadi kamili ya mizani. Mfano katika shairi la "Ngao za
Kienyeji (uk36)"
NIMEKUJA NA HABARI
Ni diwani yenye mkusanyiko wa mashairi yaliyotungwa kwa ufundi wa hali ya juu ili kuleta
ladha murua kwa wasomaji. Mashairi haya yamegubikwa na mitindo mbalimbali ya utungaji wa
mashairi ikihusisha ukopaji wa kaida kutoka katika tanzu nyingine za fasihi, ili kuleta upekee
katika kazi husika. Diwani hii inaangazia masuala yaliyopo katika jamii kama vile suala la ajira,
uzalendo, ukiushi wa maadili, upokwaji wa haki, uchawi na ushirikina, mfumo wa elimu na
kadhalika
MOYO
Ni diwani iliyosheheni maudhui mseto yaliyowasilishwa kwa fani ya kipekee, ni moja kati
ya diwani chache katika katika fani ya ushairi ambayo mashairi yake yamesheheni maumbo
mbalimbali likiwemo umbo la moyo. Diwani hii imekuwa na mchango mkubwa katika kuonesha
nmaendeleo ya ushairi wa Kiswahili
3
Zifuatazo ni hoja zinazothibitisha kuwa diwani ya "NIMEKUJA NA HABARI"
iliyoandikwa na Zacharia P. Mponzi na Christopher B. Lucas pamoja na diwani ya "MOYO"
iliyoandikwa na Sebastian N. Mbwillow ni baadhi ya diwani zilizozingatia vipengele vya kifani.
Vipengele hivyo ni kama vile;
Shairi; Ni utungo wenye mizani 16 katika kila mshororo na wenye mizani 8 katika kila
kipande cha mshororo, mfano katika diwani ya NIMEKUJA NA HABARI shairi la “Fanani na
hadhira” (uk1) ubeti wa kwanza
“Hodi hodi naingia, sipo kupoza dira,
Naomba nipate njia, ila mbona mmefura?
Nataka kusalimia, hamjambo nyi hadhira?
4
Fahari yangu fanani, kazi ipate hadhira”.
Katika mfano huu tunaona kuwa mwandishi ametumia mizani 16 kila mshororo wa ubeti wa
shairi hilo la "fanani na hadhira" pia katika shairi la "tega sikio" (uk2) mwandishi ametumia
shairi lenye mizani 16 katika kila mshororo
Utumbuizo; Ni utungo wa ushairi wenye mizani 14 katika kila mshororo wake wakati
mwingine utungo huu unakuwa hauna idadi kamili ya mizani. Mfano katika diwani ya MOYO
(uk12) shairi la "Mwalimu"
“Hello,
Habari za Leo,
Mjomba hapa nisikilize,
Haya machache nikuelezee,
Haya mafunzo toka kwa Babu"
............(uk5)
Pia katika mfano huu tumeona mwandishi Christopher Lucas hajatumia idadi kamili ya vina na
mizani katika mshororo mmoja kwenda mwingine
Utenzi; Huu ni utungo ambao una mizani nane katika kila mshororo, mara nyingi huwa
ni masimulizi marefu kuhusu maisha au habari. Mfano katika diwani ya NIMEKUJA NA
HABARI, shairi la "Utenzi wa Afrika" (Uk22) mwandishi anasema
Msuko; Huu ni utungo wa ushairi ambao kibwagizo kinakuwa na mizani michache zaidi ya
mishororo mingine. Mfano katika diwani ya MOYO, mwandishi Sebastian N. Mbwillow
ametumia utungo huu katika shairi la "sintofahamu anasema
Sintofahamu................... "(Uk61)
Katika shairi hili la "sintofahamu" mwandishi ametumia utungo huu wa msuko kuanzia ubeti wa
kwanza hadi wa nne. Pia katika diwani ya NIMEKUJA NA HABARI mwandishi ametumia
utungo huu katika shairi la "Zilizo kweli" mwandishi anasema
Mishororo; Katika shairi mishororo ni idadi ya mistari katika kila ubeti wa shairi.
Wamitila (2008) ameainisha aina mbalimbali za mishororo. Kwa kurejelea diwani ya
NIMEKUJA NA HABARI pamoja na diwani ya MOYO waandishi wameweza kutumia aina
mbalimbali za mishororo kama ifuatavyo:-
6
Tathmina; Ni shairi lenye mshororo mmoja. Katika diwani ya NIMEKUJA NA
HABARI katika shairi la "katiba" mwandishi ametumia tathmina kama ifuatavyo
Katika mifano hii tunaona jinsi mwandishi alivyotumia tathmina katika mashairi yake
Tathnia; Ni aina ya shairi ambayo huwa na mishororo miwili katika kila ubeti. Katika
diwani ya NIMEKUJA NA HABARI tathnia imeweza kutumika katika mashairi mbalimbali.
Mfano katika shairi la "Duniani kupeana" (uk32) mwandishi anasema
Pia katika shairi la "najivunia nini" (uk96) tathinia imetumika kama ifuatavyo
Katika mifano hii tunaona jinsi mwandishi alivyoweza kutumia tathinia katika mashairi yake
Tathilitha; Ni aina ya shairi ambayo huwa na mishororo mitatu katika kila ubeti. Katika
diwani ya MOYO mwandishi ametumia tathilitha katika mashairi yake. Mfano katika shairi la
"tegua kitendawili (uk29) mwandishi anasema
7
Katika mfano huu mwandishi ametumia tathilitha, yaani shairi lenye mishororo mitatu. Pia
katika diwani ya NIMEKUJA NA HABARI mwandishi ametumia tathilitha katika mashairi
yake. Mfano katika shairi la pesa (uk115), mwandishi anasema
Pia katika shairi la "fundika" (uk85), shairi la "Mjiajiri shambani" (uk92), shairi la "Mama
Afrika" (uk51) na shairi la "Dunia mgeuko" (uk39) mwandishi ametumia tathilitha katika baadhi
ya mashairi yake. Mfano mashairi tajwa hapo juu
Tarbia; Ni aina ya shairi ambalo huwa na mishororo minne katika kila ubeti wa shairi.
Katika diwani ya MOYO mwandishi ametumia tarbia Katika baadhi ya mashairi. Mfano katika
shairi la "Hautufai" (uk15) anasema
Tua Dua,
Shuka au tua
Nimesimama."
Pia katika mashairi ya "Sote tu watumwa" (uk13), shairi la "Mwalimu"(uk12) na shairi la shairi
la" Karibu tena" (uk4), mwandishi ametumia muundo wa tarbia. Pia Katika diwani ya
NIMEKUJA NA HABARI mwandishi ametumia tarbia Katika baadhi ya mashairi. Mfano katika
shairi la "Fanani na hadhira"(uk1), mwandishi ameonesha muundo huo wa tarbia
Takhimisa; Ni aina ya shairi ambayo huwa na mishororo mitano katika kila ubeti.
Katika diwani ya MOYO mwandishi ametumia muundo huu wa takhimisa katika mashairi
mbalimbali. Mfano katika shairi la "Kwanini waishi" (uk47) mwandishi anasema
Pia katika shairi la "Zoezi zana" (uk97), katika mifano hii waandishi wametumia takhimisa
katika mashairi yao
Tasdisa; Ni aina ya shairi lenye mishororo sita katika kila ubeti. Katika diwani ya
NIMEKUJA NA HABARI mwandishi ametumia muundo wa tasdisa katika baadhi ya mashairi
yake. Mfano katika shairi la "Majeruhi" (uk105), mwandishi anasema
9
Habari kemkem, zipo kwa majeruhi,
Pia katika shairi la" Ardhi inatema" (uk26). Pia katika diwani ya MOYO waandishi ametumia
muundo wa tasdisa katika shairi la "Unatofautiana" (uk57)
Pia katika shairi la" Kama si uchizi ni nini?" ubeti wa nne (uk71) mwandishi ametumia tasdisa
Usaba; Ni aina ya mashairi ambayo huwa na mishororo saba katika kila ubeti wake.
Katika diwani ya MOYO mwandishi ametumia muundo huu katika mashairi mbalimbali. Kwa
mfano katika shairi la "Unatofautiana" ubeti wa tatu (uk57) anasema
Pia katika diwani ya NIMEKUJA NA HABARI mwandishi ametumia muundo wa usaba katika
shairi la "Vituko vya daladala" ubeti wa pili (uk20) anasema
Katika mfano huu tunaona kuwa mwandishi amewaza kutumia usaba katika Shairi Lake
Unane; Ni aina ya mashairi ambayo huwa na mishororo nane katika kila ubeti wake.
Katika diwani ya MOYO unane umeweza kujitokeza katika shairi la "Hatutizamani" (uk54)
11
Wamejaa haya, hawaoni mbele! Hatutizamani"
Pia katika diwani ya NIMEKUJA NA HABARI shairi la "Kupe" (uk35) mwandishi ametumia
muundo wa unane. Katika mifano hii tunaona kuwa waandishi wameweza kutumia unane katika
uandishi wa mashairi yao
Utisa; Ni aina ya mashairi ambayo huwa na mishororo tisa katika kila ubeti wake.
Katika diwani ya NIMEKUJA NA HABARI shairi la "Utusamehe" (uk67) anasema
Ukumi; Ni aina ya mashairi ambayo huwa na mishororo kumi katika kila ubeti
wake. Mfano katika diwani ya NIMEKUJA NA HABARI mwandishi ametumia muundo huu wa
ukumi katika shairi la "Eliza" (uk64) anasema
Mtulivu,
12
Mcheshi,
Uliouchanganya na mapozi,
Wavutia,
Mdada,
Pia katika diwani ya MOYO mwandishi ametumia muundo wa ukumi katika shairi la Umri wa
busara" (uk37)
Vina; Katika ushairi wa Kiswahili vina vimegawanyika katika makundi mawili, yaani
vina vya kati na vina vya nje. Katika diwani ya NIMEKUJA NA HABARI pamoja na diwani ya
MOYO, kigezo cha vina kimeweza kuthibitika katika mashairi mbalimbali kama ifuatavyo
Ukara; Ni utungo wa ushairi ambao vina vyake vya nje (utao) hufanana shairi zima,
lakini vina vya kati(ukwapi) hutofautiana kutoka ubeti mmoja hadi mwingine. Katika diwani ya
NIMEKUJA NA HABARI mwandishi ametumia ukara katika shairi la "Nitozeni" (uk19)
.........................................”
.....................................
13
Katika ubeti wa kwanza vina vya kati ni "no" na vina vya kati ni "ngu" lakini vina vya nje katika
beti zote ni "ni". Pia katika diwani ya MOYO mwandishi ametumia ukara katika shairi la
"Tamati" (uk76)
Kikwamba; Ni utungo wa ushairi ambao neno moja huanza katika kila mshororo wa ubeti.
Katika diwani ya NIMEKUJA NA HABARI mwandishi amewaza kutumia kikwamba katika
shairi la "Upendo" (uk9) anasema
Katika shairi hii neno upendo imejirudia katika kila mshororo. Pia katika shairi la "Tunda la
roho" (uk82), mwandishi amewaza kuonesha jinsi neno la kwanza katika kila mshororo wa ubeti
yanavyofanana. Katika diwani ya MOYO mwandishi amewaza kuonesha kikwamba katika shairi
la "Mwalimu" (uk12) anasema
14
“Mwalimu, Tina na shoni wanagombana!
Katika shairi hii la Mwalimu uk12 ubeti wa pili tunaona jinsi neno "Mwalimu linavyojirudia
katika kila mshororo wa ubeti
Mtindo kwa mjibu wa wamitila (2003).katika ushairi wa kiswahili mtindo ni jumla ya mbinu au
sifa zinazomwezesha mwandishi kuwasilia ujumbe wake, huelezea mwandishi anavyounda kazi
yake
Senkoro (1982), anasema mtindo katika kazi ya fasihi ni ile namna ambayo msanii hutunga kazi
hiyo na kuipa sura ambayo kifani na kimaudhui huainisha kanuni au kaida zilizofuatwa (za
kimapokeo) ama ni za kipekee
Mtindo katika ushairi wa kiswahili huzingatia vipengele vikuu viwili ambavyo ni mtindo wa
kisasa na mtindo wa kimapokeo. Waandishi wa diwani hizi mbili ambazo ni diwani ya MOYO
na NMEKUJA NA HABARI wamezingatia mitindo hii kama ifuatavyo:-
Mtindo wa kimapokeo, ni mtindo ambao mashairi huandikwa kwa kufuata urari wa vina na
mizani, katika diwani ya NIMEKUJA NA HABARI" shairi la “fanani na hadhira” (Uk.1)
waandishi ametumia shairi la kimapokeo, anasema,
Katika mfano huu tunaona kuwa mwandishi amefata urari wa vina na mizani. Kwani vina vya
kati ni a na vina vya mwisho ni ra
15
Mtindo wa kisasa, ni mtindo ambao mashairi huandikwa pasipo kufuata urari wa vina na mizani
mfano katika diwani ya "NMEKUJA NA HABARI" Mwandishi ametumia mtindo wa kisasa
mfano katika shairi la Tundala Roho” (uk.82)
Pia katika diwani ya "MOYO" mwandishi ametumia mtindo wa kisasa mfano katika shairi la
Katika mifano hiyo hapo juu tunaona kuwa mwandishi ametumia mashairi ya kisasa kwani
ajafata urari wa vina na mizani katika uandishi wake, pia katika shairi la “Filimbi”. (uk53)
pamoja na shairi la “nakumbuka juzi kati” (uk59) ni mfano wa mashairi ambayo hayajazingatia
urari wa vina na mizani (kisasa)
Sitiari, hii ni sawa na tashibiha ambayo hulinganisha vitu au watu bila kutumia kiunganishi
mfano mithili ya, sawa na. Mfano katika diwani ya NIMEKUJA NA HABARI shairi la
“Upendo” (uk.9) ubeti wa 5
Tafsida, ni matumizi ya lugha mwala inayokidhi mwelekeo wa jamii kuhusu miiko na makatazo
ya kutumia lugha za uwazi hasa kutumia uchafu wa matusi mfano katika diwani ya
"NIMEKUJA NA HABARI" shairi la X-Wangu (uk.12) ubeti wa 2
Shairi hili linamzungumzia mwanamke na tabia zake lakini mwandishi ameficha ukali wa
maneno na akaweka tafsida.
Takriri, ni utokeaji wa mara kwa mara wa kurudia maneno kwa malengo maalumu vile vile
katika diwani ya "NIMEKUJA NA HABARI" shairi la Glory (Uk.14)
...............”
Nidaa. ni neno au tamko linalioonesha mchomo wa moyo kwa sababu ya aidha furaha,
mshangao au huzuni. Katika diwani ya "MOYO" shairi la “Kwa Heri Wangu” (uk.2) ubeti wa 4
17
“Masharo wanakufata kwa swaga zao aaa!”
Methali katika ufundi wa utungaji washairi huingiza methali katika kazi zao kwa lengo la aidha
kutoa onyo au msisitizo wa jambo.katika diwani ya "MOYO" shairi la “Karibu Tena” (uk.4)
ubeti wa 3
Ndondo si chururu
Haba na haba
Mdokezo, ni hali inayoonyesha kuendelea kwa kitu au jambo fulani. Hii imejitokeza katika
diwani ya "MOYO" shairi la “Karibu Tena”. (uk 4) ubeti 5
Misemo na nahau, pia mwandishi ameweza kuhusisha misemo na nahau kwenye kazi yake hii
inadhihirisha unguri wake katika utunhaji wa kazi za kishairi na katika diwani ya "MOYO"
shairi la Mwanangu. (uk 19) ubeti 1
...........................”
18
MAREJELEO
Mponzi Z. P & Lucas. C. B(2023). Diwani ya Nimekuja na habari. CBL Company Limited
Mwanza - Tanzania
Mulokozi M. M(2012). Diwani ya Tenzi tatu za kale. Taasisi ya uchunguzi wa Kiswahili (TUKI)
Chuo kikuu Cha Dar es salaam
Mulokozi, M. M na Kahigi K. K(1982). Kutunga Ushairi na Diwani zetu, TPH, Dar es salaam
Wamitila. K. W(2003). Kichocheo cha fasihi simulizi na andishi Nairobi. Focus publishers
19
.
20