Professional Documents
Culture Documents
Na Mroki Mroki
LEO Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania litaanza vikao
vyake katika Mkutano wa Kumi na Nane wa Bunge hilo mjini
Dodoma.
Wabunge kutoka majimbo na vyama mbalimbali vya siasa
watakutana na kujadili masuala mbalimbali ya kitaifa na
kimataifa kuhusiana na maendeleo ya nchi na utekele\zaji wa
miradi yake mbalimbali yote ikiwa ni kuwaletea maendeleo
wananchi.
Pamoja na mambo mengine hii leo wananchi kupitia luninga zetu
kwa wale watakao pata wasaa wa kutazama watashuhudia kiapo
cha utii kwa Mbunge ambapo Mwanasheria Mkuu wa Serikali
ndugu yangu, George Mcheche Masaju, ataapishwa baada ya
kuteuliwa na
Rais kufuatia kujiuzuru kwa aliyekuwa
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick Mwita Werema.
Hili linafanyika kwa mujibu wa Kanuni ya 24 ya Bunge.
Niimani yamngu kubwa kuwa wabunge wote bila kujali itikadi
zao za kiasiasa watampa ushirikiano mkubwa Masaju katika
utekelezaji wa majukumu yake mapya Bungeni humo na nje ya
Bunge.
Aidha, kwa Mujibu wa Kanuni ya 86 (1) ya Kanuni za Kudumu za
Bunge, jumla ya Miswada Mitatu (3) itasomwa na kupitishwa na
Bunge. Miswada hiyo ni ile ya Sheria ya Usimamizi wa Kodi wa