Professional Documents
Culture Documents
TANGAZO
MIGODI YA DHAHABU YA GEITA, BULYANHULU, BUZWAGI NA
NORTH MARA KUANZA KULIPA USHURU WA HUDUMA KWA
KIWANGO CHA 0.3% YA MAPATO GHAFI KWA
HALMASHAURI ZA WILAYA NA MIJI
Wizara ya Nishati na Madini inapenda kutangazia umma kuwa
mgodi wa dhahabu wa Geita unaomilikiwa na kampuni ya
AngloGold Ashanti; na migodi ya Bulyanhulu, Buzwagi na North
Mara inayomilikiwa na kampuni ya Acacia Mining, imeanza kulipa
ushuru wa huduma kwa kiwango cha asilimia 0.3 (0.3%) ya mapato
ghafi kwa Halmashauri husika. Halmashauri zitakazonufaika na
malipo hayo ni: Mji wa Geita; Wilaya ya Geita; Mji wa Kahama;
Wilaya ya Msalala; na Wilaya ya Tarime. Malipo hayo yanaanza
tarehe 1 Julai, 2014. Malipo hayo yanafuatia makubaliano kati ya
Serikali na Kampuni zinazomiliki migodi husika kufanya
marekebisho kwenye Mikataba ya Maendeleo ya Uchimbaji Madini
(Mining Development Agreement - MDA) baina ya Serikali na Migodi
ya Geita, Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara kuhusu ulipaji wa
ushuru wa 0.3% ya uzalishaji kulingana na Sheria ya Local
Government Finance Act, Cap.290 Revised Editions of 2002 badala
ya Dola za Marekani 200,000 kwa mwaka zilizokuwa zikilipwa
awali.