Sautiza watanzania leo zinasikika duniani kote kwa viongozi wanchi na dunia ambapo wananchi wanadai viongozi watimize ahadi zao juu ya afya ya uzazi kwa kina mama, watoto na vijana. Watanzania wana mchango mkubwa sana katika uzinduziwa ripoti hii ya dunia ambayo inazinduliwa wiki hii katika nchi mbalimbali duniani ikitoa wito wa uwajibikaj i na ushiriki wa wananchi katika ngazi zote katika hudumaza afya. Ripoti hii ni harakati za kipekee kwani zaidi ya mikutano 100 ya sauti za wananchi imefanyika katika nchi 20 mwaka 2015. Watu wa rika zote, kutoka katika aina tofauti za maisha wamesafiri kutoka katika vijiji na miji yao ili kushiriki katika mikutano hii maalum ya kidiplomasia na iliyowazi ili kukutana na wanasiasa, watoa huduma za afya na waandishi wa habari. Wananchi waliongea na kuuliza maswali, viongozi walisikiliza na kujibu ili kuitikia matakwa ya uhitaji wa ushirikishaji na uwajibikaji wa nchi zao katika huduma za kina mama, watoto na vijana.
Tukio: Uzinduzi wa Ripoti ya Sauti za Wananchi
Tarehe:25/09/2015 Muda: Saa nne na nusu hadi saa tano na nusu asubuhi (4:30-5:30) Mahali: Ofisi za Muungano wa Utepe Mweupe wa Uzazi Salama 164C Msasani Beach, Kinondoni S.L P 65543, Dar es Salaam Parua Pepe: rose.mlay@gmail.com Simu : +255 754 316 369 Mitandao ya kijamii: #CitizenPost
Mikutano ya Sauti za Wananchi pia ilifanyika katika wilaya na miji mikuu
ikiwemo Muheza, Kilindi, Handeni, Korogwe, Jiji la Tanga na Dar es Salaam. Pia mikutano hiyo ilitangazwa na ITV na Radio One ambapo wananchi kutoka sehemu mbalimbali za nchi walipata nafasi ya kuchangia na kuuliza maswali kwa viongozi wao. Pia wananchi waliweza kuchagua wawakilishi wao-kwa mara ya kwanza kabisa-ili wazungumze kwenye mkutano wa afya wa dunia uliofanyika mwezi Mei mwaka huu huko Geneva. "Suala kubwa kabisa la kusisimua katika (Mkutano wa afya wa dunia) ilikua ni kwa mara ya kwanza kabisa katika historia ya Shirika la Afya
duniani na Baraza lake, mkutano ulioongozwa na asasi ya kiraia
ulifanyika ili kuimarisha uwajibikaji wa kisiasa kwa afya ya dunia hasa kwa afya ya kina mama na watoto. Muungano wa Utepe Mweupe pamoja na serikali za Bangladesh na Sweden ziliitisha majadiliano ya kwanza ya dunia kati ya wanachi na serikali. Lilikua ni suala la kihistoria. Majadilia no haya ya sauti za wananchi msingi wake ni mikutano ya sauti za wananchi liyofanyika katika nchi 20 ambapo asasi za kiraia ziliweza kukubalika katika kuimarisha hali ya afya duniani -kwa wakati ujao" Richard Horton,Mhariri Mwandamizi, Lancet. Katika moja ya vipengele vya ripoti ya sauti za wananchi mbacho kina akisi mapendekezo yaliyotolewa na wananchi waTanzania,mwananchi kutoka Tanga, Peter Katuka anasema; 'Tuna sera nzuri lakini hazitekelezwi. Kwa mfano, sera ya serikali inasema kwamba kuwe na zahanati katika kila kijiji na kituo cha afya katika kila kata' Mapendekezo ya wananchi kwa viongozi; 1. Kuakisi sauti za wananchi katika vipaumbele vya sera na kuchukua hatua ilikuboresha afya ya ya uzazi kwa kina mama, watoto na vijana. 2. Kuanzishwa kwa mfumo thabiti wa uwajibikaji kutoka ngazi ya serikali ya mtaa hadi taifa. 3.Kuunga mkono wito wa kuwa na mfumo wa uwajibikaji ulio huru na unaoruhusu ushirikishaji katika ngazi ya dunia. Sauti za Jamii zimeimarika zaidi wa kati huu ambao dunia inazindua malengo mapya ya maendeleo, Malengo Endelevu ya Dunia (SDGs) katika baraza la Umoja wa Mataifa huko New York. Wakati huo huo, katibu Mkuu waUmoja wa Mataifa Ban Ki -moon anatangaza mkakati wake wa pili kwa ajili ya afya ya kina mama na watoto. Na haya yote yamekuja sasa kwa sababu tumeona kwamba malengo ya kidunia, kitaifa na ya kijamii yanaweza kufikiwa pale tu sauti za wananchi zitasikilizwa. Na hii ndio sababu wakati viongozi wadunia wanakuta na katika Baraza la Dunia la mwaka 2015 ili kuweka ahadi zao kwa miaka kumi na mitano ijayo, sisi tunasema kwamba "hakuna linalotuhusu sisi wenyewe hatutashiriki" -hii ndio kauli mbiu ya maelfu ya wananchi ambao walishiriki zaidi ya mikutano 100 ya sauti za wananchi duniani (http://www.citizens-post.org/). Wakati huo huo, tarehe 26 Septemba 2015, Ripoti ya Sauti zaWananchi itazinduliwa huko New York na shughuli hii itafanywa na (PMNC)mbele ya viongozi wa dunia na wanachi kutoka sehemu mbalimbali duniani. Pia, huko New York, waandaji wa SAUTI ZA WANANCHI wanaandaa 'Hakuna kinachotusu kama sisi wenyewe hatutashiriki' ili kuonyesha ushiriki wa wananchi katika uwajibikaji katika sekta ya afya na kutoa dondoo juu ya ahadi mpya ya asasi ya kirai katika mkakati wa dunia kwa afya ya kina mama, watoto na vijana. Hii itafanyika siku ya Ijumaa tarehe 25 Septemba.
Kumekua na maendeleo makubwa na ustawi wa afya wakati wa malengo
ya milenia. Hata hivyo mamilioni ya kina mama na watoto wamekua hawafaidiki na na lengo la 4 na la 5 la milenia na muenendo wa sasa unaonyesha kuwa ifikapo mwaka 2030 watoto milioni 4 n awanawake 200,000 watakua wamefariki kutokana na sababu ambazo zingeweza kuzuilika ambazo zinaendana naujauzito na kujifungua. Ili kumalizia agenda ambayo haikumalizwa -ya- kuzuia vifo vya watoto wachanga, kinana mama na watoto ndani ya miaka kumi na tano ijayo inaweza tukutokea kama kutakua na mfumo madhubuti wa uwajibikaji. Ili maendeleo endelevu ya dunia yaweze kufanikiwa, wananchi lazima wawe mbele katika kufanya maamuzi.Asasi za kiraia zina kazi kubwa ya kufanya katika kutengeneza mazingira haya ya maendeleo. Katika wiki hii, mazungumzo ya wanahabari na taarifa kwa umma zitakuwa zikitolewa katika nchi ambazo zilifanya mikutano ya sauti za umma ili kuzindua ripoti hii na mapendekezo yaliyomoili na kutoa mchango katika kuondoa hali ya kutokuwepo kwa mawasiliano ya karibu na mrejesho juu ya vipaumbele vya afya katika ngazi za kitaifa na kimataifa. Imetolewa na Rose Mlay-Mratibu wa Taifa, Muungano wa Utepe Mweupe wa Uzazi Salama Tanzania.
Madhara Yatokanayo Na Ajali Za Barabarani Yamemeendelea Kuwa Sababu Namba Tisa Katika Kusababisha Vifo Vya Watu Wengi Zaidi Duniani Ambapo Inakadiriwa Zaidi Ya Watu Milioni 1