Professional Documents
Culture Documents
Mtihani Wa Kiswahili
Mtihani Wa Kiswahili
TAREHE ...../..../2021
MAELEKEZO:
someni kifungu cha mazungumzo yafuatayo kati ya Mtalii na Mpokeaji wa watalii kisha mjibu maswali
yanayofuata.
Mtalii: Mimi ninaitwa Jane kutoka Ujerumani. Nina lengo la kuzuru mazingira yenu.
Mpokeaji:Sawa. Nchi yetu ina vivutio vingi: mbuga za wanyama, mito, milima mizuri pamoja na nyumba
za kuhifadhia utamaduni wetu. Je, ungependa kuzuru mazingira ya aina gani?
Mtalii: Kwa sasa ningependa kuzuru mojawapo ya mbuga za wanyama. Mna mbuga gani za wanyama ili
niweze kuchagua?
Mpokeaji:(Anachukua ramani) Unaweza kutalii (anamwonyesha ramani) eneo hili la mbuga ya wanyama
ya Akagera, hii ni mbuga ya wanyama ya milima mirefu (Virunga) na sehemu hii ni ya mbuga ya
wanyama ya msitu wa Nyungwe.
Mtalii: Naona kweli kuna mahali pengi pa kutalii. Nimependa sana mazingira ya Akagera na yale ya
milima mirefu ya Virunga. Nafikiria kurudi Rwanda mwaka ujao ili nitalii mahali kwingi. Mpokeaji:Je,
utakaa nchini humu kwa muda gani?
Mtalii: Nina wiki mbili tu na ninataka kuzitumia vizuri. Naomba kujua bei ya kuruhusiwa kuingia katika
mbuga.
Mpokeaji:Aaah! Bei ni nafuu. Ili uingie katika kila mbuga utalipa kiingilio kisha utapewa mwelekezaji wa
watalii katika kila mbuga.
Mpokeaji:Hoteli ni nyingi sana na nzuri. Hizi hapa nambari za simu. Ufikapo mahali panapoitwa
Musanze, piga mojawapo ya nambari hizi ili utengewe chumba cha kulala pamoja na maakuli. Nambari
hii nyingine utaitumia ukiwa mjini Kigali a hii hapa utaitumia ukiwa katika sehemu za Akagera.
Mtalii: Asante sana. Naomba unipe akaunti yenu ili niweze kulipa kiingilio cha mbuga hizo za wanyama.
Je, kuna kampuni ya kutoa huduma za magari ya kutumiwa na watalii?
Mpokeaji:Ndio! Hii hapa orodha ya kampuni hizo, aina za magari ya kutumia na bei zake kwa siku
pamoja na nambari zao za simu.
II. Elezeni maana ya msamiati uliopigiwa mistari katika sentensi hizi kisha mtunge sentensi zenu sahihi
kwa kutumia msamiati huo./Alama 10
1. Mtalii huyu kutoka nchi ya Ujerumani anataka kujua maeneo mazuri ya kuzuru nchini.
3. Mtalii huyu anataka kuzuru wilaya ya Korongi ili aweze kutazama ziwa Kivu.
IV. Kamilisha sentensi zifuatazo kwa kutumia kiulizi ‘-pi’ kwa usahihi./ Alama 5
V. Jaza nafasi zilizo wazi kwa jibu sahihi kutoka kwenye mabano./ Alama 10
VI. Kamilisha jedwali lifuata kwa usahihi ukizingatia wakati uliotimilika. Alama 8
VII. Zibadilishe tungo zifuatazo kwenye kauli taarifa ama kauri asili. Alama 10
A. "Mkulima hakupata hasara bali faida," alisema waziri.
VIII. Soma kauli zifuatazo na useme ikiwa kila kauli ni au si kweli. Alama 10
1. Huwezi kutuma baruapepe kwa simu za mkononi ni baadhi ya vifaa vya teknologia ya mawasiliano.
2. Runinga, redio, faski, komyuta iliyounganishwa na intaneti ili kutuma na kupokea baruapepe.
5. Ni vizuri kuomba ruhusa kabla ya kuenda nje kwa kuwa ni adabu nzuri.
XI. A. Fupisha insha hii katika aya moja tu, yenye misitari mitano. Alama 7.
Maji ni Bora
Maji ni uhai. Mimea, wanyama pamoja na binadamu hawawezi kuishi bila ya kuwepo kwa maji. Maji
yakikosekana ulimwenguni kote, viumbe wote wenye uhai wataangamia. Maji huweza kupatikana katika
bahari, ziwa, bwawa, mto na hata chemchemi. Mvua inaponyesha, watu, wanyama pamoja na mimea
hupata maji ya kutumia.
Maji yana umuhimu mkubwa sana katika maisha ya binadamu. Binadamu hutumia maji kupikia, kunywa,
kufulia nguo, kuogea, kuoshea vyombo na hata kusafishia nyumba. Binadamu huweza kupata chakula
kutoka kwa mimea kwa kuinyunyizia maji hivyo kunawiri na kumpatia binadamu mazao mengi.
Mimea pia hunyunyiziwa dawa za kuwakinga au kutibu magonjwa fulani. Dawa hizi huwa
zimechanganywa na maji.Wanyama pia huhitaji maji ili kuishi na kukua. Wao hunywa maji hayo.
Wanyama hupigwa dawa za kuwakinga dhidi ya magonjwa mbalimbali. Dawa hizo huwa
zimechanganywa kwa maji.
Njia nyingine za burudani ambazo huwavutia watalii wa ndani na nje ya nchi yetu hutumia maji. Kwa
mfano, vidimbwi vya kuogelea na maeneo yaliyo na wanyama wanaoishi majini kama vile mamba,
kiboko na samaki wa aina mbalimbali.
B. Chaguwa Mada moja kati ya hizi tatu ili utunge insha isiyozidi maneno 500. Alama 8.