Professional Documents
Culture Documents
Iremsa Kiswahili
Iremsa Kiswahili
OFISI YA RAIS
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
UMOJA WA SHULE ZA MCHEPUO WA KIINGEREZA MKOANI IRINGA
(IREMSA)
ii. _______________________________________________________________
iii. _______________________________________________________________
iv. _______________________________________________________________
v. _______________________________________________________________
SEHEMU D: UTUNGAJI
4. Weka alama za uandishi katika sehemu zilizoachwa wazi
Mfano: Unaitwa nani?
SEHEMU E: UFAHAMU
5. Soma kwa makini hadithi ifuatayo kisha jibu maswali yanayofuata
Hapo zamani za kale kulitokea mgogoro mkubwa sana kati ya ndege na
wanyama. Juhudi zote za kumaliza mgogoro huu zilionekana kugonga mwamba
na hatimaye vita ilianza. Wakati majeshi hayo mawili ya wanyama na ndege
yakijiandaa kupigana, popo alisita kuchagua upande wa kujiunga nao kivita. Jeshi la
ndege lilifika nyumbani kwa popo na kumwambia “ Twende vitani ewe popo ndege
mwenzetu”
Popo alikataa na kusema “ Mimi ni mnyama na si ndege kama ninyi”.
Baadaye jeshi la wanyama nalo lilifika nyumbani kwa popo na kumwambia “
Twende vitani ewe popo mnyama mwenzetu”. Popo alikataa tena na kujibu “ Mimi
ni ndege na wala si mnyama kama ninyi”. Basi kukawa na ngurumo za kutisha za
wanyama shupavu kama vile simba, duma na tembo, na ndege shupavu kama vile
tai na mbuni. Majike wenye ndama na majike wenye makinda walihisi kiama chao
kimefika.
Kwa bahati nzuri sana, katika dakika za mwisho kuelekea vita, muafaka
ulifikiwa kati ya pande hizo mbili na vita ikaepukwa. Kukawa na amani badala ya
mapigano. Makundi yote mawili yakawa na shamrashamra za kusherehekea
kuepukana na mgogoro. Kuona hivyo, popo naye alitamani kuwa sehemu ya
shamrashamra hizo. Alikwenda kwa ndege akitaka kujiunga nao lakini ndege
walimfukuza. Baadayae akaenda kwenye kundi la wanyama nao walimfukuza. Popo
akabaki kuwa njia panda kwani hakuruhusiwa kujiunga na kundi la ndege au kundi
la wanyama.
MASWALI
i. Mgogoro uliotokea hapo zamani uliwahusu akina nani?
__________________________________________________
ii. Nini maana ya nahau kugonga mwamba kama ilivyotumika katika hadithi
hapo juu?________________________________________
iii. Neno kiama katika hadithi hapo juu lina maana gani?
_____________________________________________________
iv. Neno lipi katika hadithi uliyosoma hapo juu lina maana sawa na neno
shangwe?__________________________________________
Kwanini?________________________________________________