You are on page 1of 2

CHUO CHA BIBLIA NA THEOLOGIA-NYAKATO

MTIHANI WA KISWAHILI KWA WAINJILISTI


WA KWANZA SEMISTA YA KWANZA: JULAI 2020.

MUDA: 1 ½

MAELEKEZO:
i) Mthinani huu una sehemu kuu (4) nne A, B, C na D.
ii) Jibu maswali yote katika sehemu A, B na C na swali moja tu kutoka sehemu D.
iii) Majibu yote yaandikwe sehemu husika
iv) Somo na kufuata maelekezo yaliyotolewa kwa kila sehemu na kilia swali.
v) Mwandiko mzuri na mpango bora unatunukiwa.

SEHEMU A: UFAHAMU (10%)

1. Soma shairi hili kisha jibu maswali yanayofuata.

Hale huja, msifuni Mungu katiak patakatifupake,


Msifuni katika anga la uweza wake.
Msifuni kwa matendo yake makuu
Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
Msifuni kwa mvumo wa baragumu
Msifuni kwa kinanda na baragumu
Msifuni kwa matari na kucheza
Msifuni kwa zeze na filimbi
Na kila mwenye pumzi na amsifu Bwana,
Haleluya.

Maswali
i) Ungependa kichwa cha ushairi huu kuwa nini (maneno mawili tu)
__________________________________________________
ii) Utenzi huu umetoka katiak kitabu gani na kifungu gani cha Biblia?
__________________________________________________________________
iii) Mshairi katiak utenzi/shairi hili anataka tujifunze nini katika maisha yetu ya kila
siku? (sentensi 2)
__________________________________________________________________
iv) Nini dhamira kuu ya mwandishi huyu?
__________________________________________________________________
v) Fupisha habari hii kwa kutumia sentensi tatu tu.
__________________________________________________________________
__________________________________________________________________
__________________________________________________________________

SEHEMU B: LUGHA NA UTUMIZI

2. Pigia mstari neon moja tu lisilo landana na maneno yafuatayo.


i) Mwinjilisti, mchungaji, mhasibu, Askofu
ii) Sementi, king’amuzi, mchanga, maji, kibao
iii) Kalamu, karatasi, wino, cherehani, penseli
iv) Mwanza, Dodoma, Moshi, Tabora, Morogoro.

3. Andika vitenzi vinavyotokana na nomino zifuatazo.


Mfano: Mkulima – lima.

i) Mpishi ___________________
ii) Msomi ___________________
iii) Mvuvi ____________________
iv) Mtunzi ____________________

4. Andika aina ya neon mbele ya kila neon ya maneno yafuatayo.


Musa – Nomino.

i) Mwinjilisti ___________________
ii) Fundisha ____________________
iii) Majuzi ______________________
iv) Loh, Ibilisi wewe!! ______________

5. Taja aina (4) nne za sarufi.


a) _____________________
b) _____________________
c) _____________________
d) _____________________

6. Nini maana ya lugha?


________________________________________________________________________
________________________________________________________________________
________________________________________________________________________

SEHEMU C: UANDISHI

7. Wewe ni mwanachuo uliyehitimu uinjilisti katika chuo cha Biblia na Theologia-Nyakato


mwaka jana. Usharika na familya yao wameandaa tafirija ya kukupongeza. Andaa kadi
ya mwaliko kwa marafiki zako na walimu.

SEHEMU D: FASIHI KWA UJUMLA


Jibu swali moja tu.

8. Kwa maelezo na mifano toa tofauti mbili za fasihi andishi na fasihi simulizi.

9. Eleza maana ya fani na maudhui.

********************************************************************

You might also like