Professional Documents
Culture Documents
Tafukuri Ndogo Na Fikra Wezeshi
Tafukuri Ndogo Na Fikra Wezeshi
Utangulizi.
USULI
Andiko hili la kitafiti, wezeshi kifikra, lililobeba ndoto njema za wanafunzi Tanzania, ni andiko
lililoandikwa na ndugu Abdul Nondo, Mwanafunzi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam
(UDSM) na Mratibu wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP-Tanzania Students
Networking Programme) Mkoa wa Kigoma kwa kushirikiana na wajumbe wa idara ya Utafiti
na Mafunzo taifa (TSNP Research and Training Departmment)
Pamoja na changamoto tulizonazo katika Mfumo wa Elimu Tanzania ambazo kila siku
Mtandao wa Wanafunzi Tanzania na wadau wa Elimu tumekuwa tukipigania, andiko hili
limetoa majawabu mengi haswa kwa kuzingatia misingi ya haki na wajibu wa Wanafunzi
Tanzania.
Andiko hili wezeshi na amshi kifikra, litawatoa Wanafunzi wengi gizani, litahuisha afya za
wanafunzi kitaaluma, litawapa dira na ndoto murua wanafunzi wa Kitanzania na vile vile
litafanya Wanafunzi wote Tanzania kujikita sana katika wajibu wao na si kusingizia
changamoto tulizonazo katika mfumo wa Elimu Tanzania kama kigezo cha kutofanya vizuri
katika masomo.
Hivyo katika maisha yako yote wewe unayeitwa mwanafunzi, sio kwa bahati mbaya ni kwa
sababu wewe ni msomaji na ni mwanafunzi. Hivyo kama mwanafunzi unajukumu moja tu, ni
jukumu la kusoma ili uitwe “student”. Kama husomi, huna mkakati wowote wa kusoma na
kufanya vizuri wewe utakuwa umesaliti jina lako (Student).
Na hautakuwa na tofauti yoyote na mtu ambaye hasomi yupo mtaani tu au kijiweni hana
kazi yoyote. Katika maisha yako yote mwanafunzi lazima uwe na njia na taratibu zako za
msingi za kukufanya uendelee kuitwa mwanafunzi kwa sababu itafika siku hautaitwa tena
mwanafunzi na lazima uwe umefanya jambo umelivuna kutokana na uwanafunzi wako.
Hivyo basi katika maisha ya mwanafunzi ambaye anapenda kufanikiwa na kufanya vizuri
kuna mambo saba (7) ambayo anatakiwa kuwa nayo katika kutimiza safari yake ya
kitaaluma, kwani mambo hayo ni kama daraja (Bridge) ambalo huunganisha jitihada zake
na mafanikio ya jitihada hizo, kwani unaweza kuwa na jitihada lakini kama hauna mambo
haya saba (7) hauwezi kufanikiwa na kufanya vizuri katika masomo yako au mitihani yako.
Lazima utambue kuwa wewe ni maskini hauna uwezo wowote, na wazazi wako ni
maskini ila wanajibana ili wewe usome na ufanikiwe.
Lazima utambue kuwa kufeli kwako au kufanya kwako vibaya kwa uzembe wa
kutokusoma ni kumsaliti Mungu na wazazi wako, kwani Mungu kupitia vitabu vyake
anaamrisha tusome. Pia wazazi wanajinyima ili usome ila unafeli kwa uzembe wa
kutokusoma ni dhambi pia.
August 2016
Lazima utambue kuwa elimu ndio ufunguo katika mafanikio. Wanafunzi wengi huwa
wakidanganyana kuwa weng wamefanikiwa bila kusoma, ni kweli hawa mara nyingi
ni wale ambao familia zao zina mnyororo wa mafanikio ambapo yeye anaweza
kurithi mali. Je, wewe kwenu kuna mali zozote? Mbali na mali zenu bado Elimu ni
muhimu zaidi ya hizo mali. Kitendo cha kuwa na elimu tu ni zaidi ya mafanikio. Mali
huja baada ya Elimu hivyo Elimu bado ni bora.
Lazima utambue kuwa Elimu yako ni faida kwako, familia yako na taifa lako ambalo
linapambana kukusomesha na hata kukupa mkopo ukifika Elimu ya juu. Hivyo ni
lazima uwe na uchungu wa kupambana ili kufanikiwa kitaaluma.
Self-Estimation (Kujitambua) ni jambo nzuri sana kwani mwanafunzi
akijitambua ni mwanzo mzuri wa kufanya makubwa na kutimiza ndoto zake.
Lazima mwanafunzi uwe na dira ya kujua wapi unaelekea na ufahamu nini ufanye, uwe
kama nani anayekuvutia, wapi unataka ufike kitaaluma. Je, Chuo Kikuu? Na ukifika chuo
kikuu unapenda usome nini?. Uwe mwanasheria au usome kilimo, au uwe mwalimu? Ukiwa
na haya maono, Dira kujua wapi unaelekea lazima itakufanya uwe na mikakati (Mission) ya
kutekeleza hii adhma yako, kwani dira yako itasimama kama malengo yako (Objectives).
Hivyo hivyo dira yako itakufanya kuwa na mikakati ya kutekeleza yote unayodhamiria, hivyo
dira (Vision) ni jambo la msingi uwe nalo.
3. MATUMAINI (HOPE)
Hii ni tofauti kabisa na mwanafunzi ambaye anasoma lakini hana matumaini ya kufaulu.
Huyu ni rahisi sana kufeli na kufanya vibaya kwa sababu hatakuwa na mipango yoyote,
wala njia zozote (Strategies) kwa sababu hana matumaini yoyote. Yeye tayari amekata
tama kuwa hawezi kufaulu.
Hii ni kwa sababu ya tamaduni tuliyojijengea kuwa shule yangu wanafunzi huwa wanafaulu
wachache sana na ni wale wanaoongoza darasani. Wanafunzi wengi huangalia matokeo ya
August 2016
nyuma ya shule zao, halafu wanakata tama kuwa hawawezi kufaulu, na sio jambo la
kushangaza kufeli kidato cha nne ni kawaida kwa sababu wengi huwa wanafeli.
Badilika kuanzia leo, kuwa na matumaini, usiangalie mabaya yaliyoko nyuma, yaangalie
kwa njia ya kutorudia mabaya lakini si kwa njia ya kukuvunja moyo.”DON’T GIVE UP!”
Sema “I DON’T GIVE UP AGAIN!”, “I DON’T GIVE UP!” Sema “I CAN PASS”, weka ahadi
na Mungu kuwa utasoma kwa jitihada zote na utafaulu.
Hii ni kwa sababu lazima tufahamu kuwa mambo yote tunayoyafanya ni lazima tumuombe
Mungu na tumuamini Mungu. Mtandao wa wanafunzi Tanzania (TSNP) unapendekeza
kuwa Lazima mwanafunzi aishi katika imani ya kumuomba Mungu ili yote anayoyafanya
yafanikiwe. kama ni Musilamu lazima umuombe Mungu akujalie kwa yote unayoyafanya na
jitihada zako zote. Kama ni Mkristo lazima umuombe Mungu akusaidie.
Pia kumbuka Mungu tayari yeye mwenyewe anasisitiza umuhimu wa Elimu. Ukisoma
vitabu vyake tukufu vyote anasema, mfano:-
DINI YA KIISLAMU:-
“Elimu haipatikani kwa kurithi kwa baba na mama, wala haipatikani ndotoni.
Inapatikana kwa kutafuta usiku na mchana. (Imesemwa na Mwanazuoni).
DINI YA KIKRISTO:-
Biblia inasema:
Mithali 4:13, “Mkamate sana Elimu usimwache aende zake, mshike maana yeye ni
uzima wako”.
August 2016
Hivyo ni wajibu wako kuamini yote anayoagiza Mungu na kama utayadharau haya utakuwa
umemkosea Mungu, na kama hautafanya jitihada basi utapata dhambi kwa sababu utakuwa
unakaidi aagizayo Mungu hivyo ni njia moja ya kwenda motoni.
Ondoa imani potofu eti ukifeli Mungu ndio kapanga, sio kweli na haina ukweli. Mungu
ameagiza tusome na kufaulu, tufanikiwe. Mungu hapendi kuona wewe unaangamia, hivyo
kuanzia leo timiza hili agizo la Mungu.
Mwanafunzi bora ni Yule ambaye ana heshima na nidhamu, nidhamu hii ianze kwa
wazazi, walimu, na hata wanafunzi wenzako. Nidhamu huambatana na Baraka juu ya
mafanikio yako
Epuka kusema:-
Hivyo Mwanafunzi lazima awe mvumilivu (Patient, endurable, tolerant), asiwe mwepesi
kukata tamaa pale anapokumbana na changamoto. Mfano, Wazazi hawana ada
unapata mawazo ya kuacha shule, hapana lazima uwe mvumilivu, usiwe na mawazo ya
kushindwa jambo Fulani kutokana na changamoto.
Huna fedha ya kusoma masomo ya ziada (Tuition) unakata tama, huna fedha ya kula
shule unakata tama, unapata alama kidogo unakata tama, hapana pambana. Shida
unazozipata leo ni furaha na faraja ya kesho ila raha uzipatazo leo ni shida na maumivu
ya kesho.
Ukiwa hausomi unalala tu, unakaa kijiweni, unakwenda disko, unashinda na boda
boda, unaona faraja kuwa na wasichana wengi, unaona faraja kudhurula tambua
hiyo ni dalili kubwa ya shida na matatizo ya kesho (ELEWA HIVYO). Hivyo vumilia
shida zote leo ili kesho uepukane nazo.
August 2016
Hayo juu ni mambo ambayo Mtandao wa wanafunzi Tanzania (TSNP) unapendekeza
kuwa mwanafunzi awe nayo katika maisha yake yote ya kitaaluma.
Lakini hayo hayatoshi bila mwanafunzi mwenyewe kutimiza wajibu wake kama ambavyo
TSNP inaendelea kueleza.
MAJUKUMU YA MWANAFUNZI
(STUDENT’S RESPONSIBILITY)
Mtandao wa Wanafunzi Tanzania TSNP unawaomba wanafunzi wote kuzifuata njia hizi,
kuzitii, kuzitekeleza na kuziheshimu.
2. MUDA WA KUPUMZIKA
Mwanafunzi lazima atenge muda wa kupumzika mchana ili kufanya ubongo na akili
yake kuwa imara (Active). Mfano, unarudi kutoka shule, unakula, unaoga kisha
unalala angalau Saa moja na nusu, halafu ukiamka unaweza amua ku relax,
kutembea tembea kidogo au kwenda mazoezini, ukirudi jioni unaweza kula usiku
halafu ukaendelea na ratiba yako ya kujisomea usiku muda wowote ambao
umepanga mwenyewe.
4. KUFANYA MAZOEZI
Pata muda wa kufanya mazoezi hata kwa nusu saa au saa moja, hii itakusaidia
kuwa imara (Active) na kuzidisha kumbukumbu. Hakuna dawa ya akili au ya
kuongeza kumbukumbu bali ni kutekeleza haya kwa moyo wote kama ambavyo
TSNP inavyowashauri.
August 2016
8. KUFUNDISHA WENGINE
Pia TSNP unamuomba na kumshauri mwanafunzi apende pia kuwafundisha
wenzake, hii kwanza itamfanya awe na mahusiano mazuri na wenzake, pili
itamfanya aweze kukumbuka kwa urahisi anachokisoma.
Achana na maneno:-
Sisomi kwa sababu yako.
Nafeli kwa sababu yako.
Unanifanya niwe na mawazo.
Achana na hizi sentensi.
Haya yote ni majukumu ambayo mwanafunzi anapaswa kuyatimiza mbali na walimu. Uhaba
wa walimu na vitabu hizi ni changamoto ambazo zipo tu. Hivyo mwanafunzi katika
kutekeleza haya anapaswa awe “committed” awe amejidhatiti kufanya yote haya. Sasa hivi
kuna notes kila mahali, mitandao ipo, tutumie simu zetu kwa faida. Mfano, “THL” ni progam
ipo playstore unaweza kuidownload halafu unakuta notes za kila somo, na maswali yote
unayoyahitaji.
AU (Reading Strategies)
Mtandao wa wanafunzi Tanzania TSNP umefanya uchunguzi na utafiti kupitia idara yake ya
mafunzo na tafiti (Research development and training department) na kuweza kugundua
njia bora za usomaji ili kufahulu mitihani na masomo kwa mwanafunzi.
Mwanafunzi anatakiwa kusoma kwa lengo la kujifunza na kuelewa (Learnig goals) epuka
kukariri. Kariri panapohitajika ila penda kusoma kwa lengo la kuelewa.
Mara nyingi wengi wanapenda kusoma kipindi cha mitihani au kipindi cha jaribio (test) hii
njia inaitwa “performance goal”. Anapenda kusoma kwa ajili tu ajibu mtihani kwa muda ule,
hii ni hatari sana kwani si rahisi mwnafunzi kufanya vizuri kupitia njia hii, kusoma ni kila siku
na sio kipindi cha mitihani tu.
Kusoma kwa makundi (reading in groups). Hii itasaidia katika kuelewa vitu au mambo
magumu kwa sababu mtakuwa mkichangia mawazo. Anayependa kujifungia chumbai na
kujisomea peke yake kila siku huwa hafanyi vizuri siku zote, ni vizuri pia kusoma na
wenzako. Lakini pia tenga muda wa kusoma peke yako (Individual learning).
KUJISOMEA MWENYEWE
(Individual reading)
Mtandao wa wanafunzi Tanzania unashauri wote kuwa njia bora ya kusoma ni ile inayoitwa
kusoma kwa UMAKINI. Yaani “INTENSIVE READING”. Hii ndiyo njia bora kwani
mwanafunzi lazima asome kwa uangalifu na kwa kuelewa ili aweze kukumbuka.
Njia bora ya kusoma initwa intensive reading. Kusoma kwa umakini, kusoma neno
kwa neno, herufi kwa herufi.
SQ3R ( SQ TRIPPLE R)
I. Survey
II. Question
III. Read
IV. Recall
V. Review
Ili kutumia INTENSIVE READING, lazima mwanafunzi atumie njia hizo tano za SQ3R.
I. TAFITI (SURVEY)
Hapa mwanafunzi achunguze ajue kidato alichopo masomo yako yana topiki zipi,
mfano yupo kidato cha 3 lazima ujue history kidato cha tatu kuna topiki ngapi,
Kiswahili kina topic ngapi, Physics ina topiki ngapi baada ya kufahamu ni topiki
ngapi unapaswa uzisome. Hii itakuwa ni hatua nzuri kwako, kujua nini kifanyike,
wanafunzi wengi wanasoma bila kufahamu, wala hataki ku-survey kujua kuna
“topiki” ngapi hawajui, mwanafunzi wa namna hii ni vigumu na sio rahisi kufahulu.
III. KUSOMA(READING)
August 2016
Baaada ya kufahamu kuwa huwezi kujibu maswali yoyote kutoka topic flani kazi
iliyobaki ni kusoma hiyo topiki au kutafuta mtu akuelekeze yote ili uelewe. Ni
vizuri katika kusoma uwe unasummarize pembeni hii inasaidia kukumbuka vizuri
unachokisoma.
AHSANTE!
August 2016