Professional Documents
Culture Documents
Kwa mujibu wa Nurse na Spear (1985) lugha huanzia mahali fulani pamoja
katika kipindi fulani kadri wasemaji wanavyoongezeka na lugha huanza
kubadilika na kuwa ya ana kwa ana. Hivyo kutokana na sababu ya
kutawanyika kunapelekea kutokea kwa lahaja tofautitofauti. Mfano; hawa
wanazuoni wanadai kuwa lahaja za kiswahili zilianzia kaskazini mwa
Mombasa katika eneo la Lamu na kuendelea sehemu nyingine ya pwani ya
Afrika Mashariki na hii ni kutokana na kwamba utafiti wa akiolojia unaonesha
kuwa mbantu wa kwanza kabisa aliishi katika mji wa Lamu. Udhaifu wa
mtazamo huu ni kwamba kama watu hao wametokea katika jamii moja
yenye lugha moja, hivyo ni vipi wanaweza kutambulishwa kutumia lahaja
zao yaani lahaja za kaskazini na lahaja za kusini.