You are on page 1of 1

Seventh-day Adventist Church P. O.

Box 14286 DAR-ES-SALAAM


Tel: + 255 719505811
South-East Tanzania Conference E-mail: utumishikanisani@gmail.com
mgwenyahm@secadventist.or.tz
Headquarters
Youth Ministries

02/4/2024.

Mchungaji wa mtaa,
Wazee wa kanisa,
Viongozi wa Vijana Makanisani na Kanda.

YAH: REFRESHER COURSE KWA MASTERGUIDE NA SYL.

Nawasalimu kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.


Union Ya Kusini Mwa Tanzania imeandaa Refresher Course (Mafunzo maalum) kwa
ajili ya Masterguide na SYL itakayofanyika Mlali-Dodoma tarehe 8-15/12/2024.
Mafunzo haya yatafanyikia nje ya nyumba, hivyo wahusika wajiandae kwa ukambikaji
(Mahema na Chakula).
Wajumbe/Wahusika wa mafunzo haya ni wachungaji wa mitaa, Chaplain wote (Vyuo na
shule),wazee wa makanisa wanaolea idara ya vijana, Wadhamini wa vijana wakubwa,
Masterguide wote waliohitimu (wakiwemo wale waliohitimu zamani na huenda
walishapoteza vyeti vyao), Masteguide & SYL wote mafunzoni (wanaotazamia
kuhitimishwa 2024, walioanza na wanaotarajia kuanza mafunzo), Kupitia refresher
course hii, tutatengeneza tanzi data (DATABASE) ya STU kujua idadi ya Masterguide na
SYL wote waliohitimu. Hivyo ni muhimu kwa Masterguide na SYL waliohitimu kufika
ili kutambulika na kuingizwa kwenye mfumo huo.
Pia tutazindua rasmi kozi mpya ya Club Ministries Training (CMT) ambayo ni mpya
kabisa kwa Masterguide na SYL, sambamba na uzinduzi wa kadi jipya la Masterguide.
Wajumbe watapaswa kulipa shilingi elfu ishirini na tano tu (25,000) kwa ajili ya
kiingilio na bima. Mwisho wa kutoa kiingilio na bima ni tarehe 05/10/2025. Kiingilio
kilipwe kupitia akaunti ya Konferensi (21210032030 – SDA COLLECTION ACCOUNT
– NMB).
Eneo la kukambika liko Km 35 toka PANDA MBILI, njia ya kuelekea Mlali kutokea
barabara kuu ya Dar es salaam kwenda Dodoma.
Maelekezo mengine tutazidi kuwajulisha kwa kadri inavyowezekana.

Ndimi Mtumishi mwenzenu shambani mwa Bwana.

Pr. Mgwenya H. Mugabo


MKURUGENZI WA VIJANA - SEC
Nakala: Maofisa – SEC

You might also like