Professional Documents
Culture Documents
2012
Sumbawanga Ngara
Eng. Stella Martin Manyanya Mb Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
Weka Manispaa yetu sa na Inayovutia ili kila mtu aseme Kwetu ni Sumbawanga
a
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
b
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
UDHIBITI WA MAZINGIRA
SUMBAWANGA NGARA
Novemba, 2012
i
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
YALIYOMO
MAONI YA BAADHI YA WADAU WA SUMBAWANGA NGARA ...............iv VIFUPISHO..ix DIBAJI .................................................................................................... x SHUKRANI ...........................................................................................xii MUHTASARI ....................................................................................... xiv 1. 1.1. 2. 2.1. 2.2. 2.3. 3. 3.1. 3.2. 3.3. 3.4. 4. 5. 5.1. 5.2. 5.3. 5.4. 5.5. 5.6. 5.7. 5.8. 5.9. UTANGULIZI .............................................................................. 1 Utekelezaji wa Pamoja kwa faida ya wote (SMART PARTNERSHIP) ....3 TAARIFA REJEA ......................................................................... 6 Maana ya taka ....................................................................................... 7 Madhara ya taka: .................................................................................. 7 Faida ya taka: ......................................................................................... 8 MALENGO YA MILENIA, DIRA NA SERA ZA TAIFA ............... 9 Malengo ya Milenia .............................................................................. 9 Dira ya Taifa ya Tanzania 2025 ........................................................10 Sera ya Mazingira................................................................................10 Sera ya Maendeleo ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati ya 2003 .....11 HALI HALISI YA HUDUMA YA TAKA SUMBAWANGA......... 12 WADAU WA TAKA .................................................................. 15 Wananchi ..............................................................................................15 Serikali ...................................................................................................15 Wafanyakazi .........................................................................................16 Wafanyabiashara.................................................................................16 Watu wa kujitolea ...............................................................................16 Vikundi na vilabu vya vijana vya Mazingira ..................................16 NGOs, CBOs, Vyama vya Kujitolea, na Jumuia za kijamii ...........16 Makampuni Binafsi ............................................................................ 17 Washirika wa Maendeleo .................................................................. 17
ii
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
iii
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
viii
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
VIFUPISHO
APRM CBO CCM DKT EMA Eng. Mb MDG MSME NGO SME African Peer review Mechanism Community Based Organization Chama cha Mapinduzi Daktari Environmental Management Act Engineer Mbunge Millennium Development Goals Micro, Small and Medium Enterprises Non-Governmental Organization Small and Medium Enterprises
ix
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
DIBAJI
Udhibiti wa uharibifu wa Mazingira hususani udhibiti wa taka
ngumu na rejea, uzuiaji wa ukataji miti kiholela na uchomaji wa moto katika maeneo yaliyotengwa, uchomaji wa taka na uepukaji wa shughuli za kibinadamu zenye uchangiaji mkubwa katika uharibifu wa mazingira limepewa kipaumbele kuwa ni suala mtambuka. Uchafuzi unaoendana na kusambaa kwa taka ngumu na miminika umeleta athari kubwa kwa viumbe hai ikiwemo binadamu, wanyama wanyonyeshao na wasionyonyesha, wadudu ambao wengine ni muhimu katika maendeleo chanya ya ardhi, kuongezeka kwa mmomonyoko wa ardhi unaosababisha vina vya maji kupungua katika maziwa kama Rukwa na Tanganyika na kukauka kwa baadhi ya mito. Utiririshaji wa maji taka yenye viashiria vya sumu au sumu kamili vinavyotokana na mabaki ya bidhaa za viwandani zimekuwa na athari kwa viumbe hai waishio nchi kavu na majini na kusababisha kupungua kwa wanyama na baadhi ya aina za samaki, na wengine kubadilisha hata ladha yao ya asili. Kwa ujumla wake uharibifu huo umechangia kwa kiwango kikubwa mabadiliko ya tabia nchi hususan, hali ya hewa katika baadhi ya maeneo, na hivyo kubadili uzuri wa asili na kupoteza baadhi ya vivutio. Mfano ni kuhama kwa wanyama na ndege katika maeneo yao ya asili, kukauka kwa maporomoko ya maji na kadhalika. Uharibifu unaoendana na taka umesababisha miji yetu kuwa michafu na isiyovutia, milipuko ya magonjwa kama kuhara na kipindupindu, magonjwa ya ngozi kama upele, kudumaa kwa afya, kimsingi watu kuwa na afya hafu na vifo. Matumizi ya dawa
x
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
xi
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
SHUKRANI
Kwa heshima na unyenyekevu shukrani za pekee zimwendee Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kwa upendo, hekima, kuniamini na kuwa na jicho la Jinsia. Namshukuru Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt Mohammed Gharib Bilal kwa kukubali kutuzindulia Mpango wa Sumbawanga Ngara. Napenda pia kumshukuru Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda (Mb) kwa kukubali kutuzindulia kitabu hiki ambacho ni mwongozo wa kufanikisha Mpango wa Sumbawanga Ngara. Nawashukuru wananchi wa Mkoa wa Rukwa wakiwemo Baba Askofu Kyaruzi, Sheikh Akilimali, Wafanyabiashara, Viongozi wa Taasisi za Umma na Binafsi, Wazee, Wanawake, Vijana pamoja na wadau wengine wote wenye nia njema ya kuhakikisha kuwa mazingira yetu yanakuwa bora na salama na kuwezesha Mpango wa Sumbawanga Ngara kukubalika kuanzia hatua za awali za utekelezaji. Nitakuwa si mwingi wa fadhila endapo sitamshukuru kipekee Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Alhaji Salum Mohammed Chima pamoja na watumishi wote wa Osi ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Mhe. Mathew Sedoyeka, Meya wa Manispaa ya Sumbawanga, Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga ndugu William Shimwela pamoja na Idara yake ya Usa na Mazingira, Osi ya Mganga Mkuu kwa kutaja mmoja Dkt. Temba pamoja na wana Kongano la Sumbawanga Ngara. Namshukuru Mhe, Jaji Pelagia Khaday kwa kutuunga mkono.
xii
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
xiii
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
MUHTASARI
Mpango huu wa Sumbawanga Ngara ulianzishwa mnamo tarehe 12 Januari 2012, chini ya uasisi wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Martin Manyanya (MB) ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar. Siku hiyo Mkuu wa Mkoa, Katibu Tawala wa Mkoa, Watumishi wa Mkoa na Halmashauri ya Manispaa kwa pamoja na wadau wengine ikiwemo Mbunge wa Jimbo la Sumbawanga, Mwenyekiti wa Chama Tawala (CCM) na wananchi wa mitaa ya Hospitali ya Mkoa na Sokoni walihamasisha usa kwa kufagia barabara pamoja na kutoa mchanga katika mifereji iliyopo katika eneo hilo. Mpango huu ulizinduliwa rasmi tarehe 24 Februari na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Mohammed Gharib Bilal kwa kuweka jiwe la msingi kwenye mnara wa Sumbawanga Ngara uliopo kwenye makutano ya barabara ya Nyerere na Two way. Mnara huu umepewa heshima kwa akina mama, kwa ishara ya utamaduni wao (ngoma ya Kingwengwe}, ambayo huchezwa hasa na wanawake, ikizingatiwa kuwa kihistoria mdau mkuu wa usa ni mama.
xiv
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Billal akizindua rasmi mpango wa Sumbawanga Ngara Mkoani Rukwa tarehe 24 Februari, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Billal akigawa vifaa vya usa kwa wadau mara baada ya uzinduzi wa mpango huo tarehe 24 Februari, 2012.
xvi
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
1. UTANGULIZI
Mgaagaa na upwa hali wali mkavu, Mcheza kwao hutuzwa na Mwenye macho haambiwi tazama. Hii ni misemo au methali za wahenga wetu ambazo maana zake hazibadiliki kizazi hadi kizazi. Hivyo, methali hizi zimekuwa chachu iliyoamsha ari ya Osi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kuandika kitabu hiki kinachochochea nafasi ya wananchi katika kujiletea maendeleo. Mara nyingi tumejielekeza kusema kuwa tumeshindwa kufanikiwa katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo katika jamii yetu kwa visingizio mbalimbali. Hayo yanajitokeza zaidi hasa katika siasa za sasa chini ya vyama vingi ambapo malalamiko yamekuwa makubwa kuliko kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu huku hali ya kujitoa katika kuchangia shughuli za maendeleo imeshuka. Mara nyingi majibu ya wananchi na vyombo vyote vya dola katika mapungufu ya kutekeleza majukumu na wajibu wao imekuwa ni kwa ajili ya ukosefu wa fedha, na Serikali imekuwa ndiyo ikitupiwa lawama zaidi kuwa haiwajibiki kwa wananchi, haikusanyi kodi kutoka kwa wafanyabiashara, haina mipango mizuri ya uhifadhi wa mazingira na kila linalowezekana kusemwa ili mradi tu mtu akipata nafasi atasema. Aghalabu si rahisi kusikia taasisi mbalimbali zikiwemo za kibunge kujadili misingi ya matatizo ya wananchi bila kuitupia lawama Serikali, Serikali hii haijali watu, watu wana umaskini wa kutupwa lakini Serikali haijali, watoto wameshindwa kwenda shule kwa sababu ya Serikali, watu wakiona taka ziko barabarani sababu ni Serikali na kadhalika. Katika taarifa ya mwaka 2012 African Peer Review Mechanism (APRM) yaani Mkataba ambao umekubaliwa na nchi wanachama wa Umoja wa Afrika kama mchakato wa kujifanyia tathmini inaeleza kuwa Watanzania wengi wanaamini kuwa Serikali ndiyo inastahili kufanya kila kitu kwa ajili yao. Kama ndivyo basi tuna tatizo kubwa, ni lazima liangaliwe kwa makini.
1
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
Baada ya kujifunza mbinu hii kupitia semina elekezi iliyotolewa na OWM TAMISEMI Chini ya Uongozi wa Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda (Mb) Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisaidiwa na Mhe. Hawa Abdulraman Ghasia (Mb) Waziri OWM - TAMISEMI tarehe 15 mpaka 18 Novemba 2012 kwa Waheshimiwa Wakuu wa Mkoa, Ma RAS na Wakuu wa Wilaya wote, inajidhihirisha wazi kuwa ili kazi hii iwe nyepesi na yenye tija matumizi ya teknolojia kwa ajili ya Sumbawanga Ngara ni muhimu sana. 1. Katika msingi wa kwanza unaosisitiza juu ya matumizi ya teknolojia katika kuharakisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa manufaa ya wote, vitahitajika vifaa kama magari ya taka, vijiko, vihifadhi taka, uchakataji wa taka au taka rejea (recycling) ni muhimu sana. 2. Ubunifu yakinifu wa Ushindani: Katika eneo hili wananchi na taasisi za umma wataendelea kutengeneza utaratibu mzuri wa ushiriki pamoja na Serikali. Uratibu maalum utafanyika wa kuangalia namna shughuli za uhifadhi
3
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya na Katibu Tawala Mkoa huo Alhaj Salum Mohammed Chima wakishiriki kwa vitendo katika usa wa mazingira katika mitaa ya Mji wa Sumbawanga tarehe 12 Januari, 2012.
5
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
2. TAARIFA REJEA
Kabla ya kuendelea kuchambua katika maeneo mengine kuhusu udhibiti wa mazingira na huduma ya taka kwa ujumla ni vema tufahamu pia juu ya mpango wenyewe au mwongozo huu. Mpango wetu: SUMBAWANGA NGARA Kaulimbiu yetu: Mkakati wetu: Weka Manispaa yetu sa na inayovutia ili kila mtu aseme kwetu ni Sumbawanga Uwajibikaji wa pamoja kwa ajili ya mazingira yetu. Tuwe nyumbani, tuwe kazini, hospitali, kwenye nyumba, kwenye maeneo ya umma hata kwenye michezo na popote pale ambapo tupo, usa ni kipaumbele chetu. Tuifanye Sumbawanga ingare kuliko ilivyowahi ku Ngara tangu kuwepo kwake. Kila mtu anaweza akatimiza wajibu wake kwa kuweka mji wake pamoja na maeneo yake yanayomzunguka na pia ahakikishe maeneo ya wazi ni sa. Saidia Manispaa ya Sumbawanga, Makao Makuu ya Mkoa wetu yawe sa kulingana na hadhi yake. Saidia Manispaa hii iwe sa ili iwe mfano kwa wilaya nyingine za mkoa wa Rukwa, Tanzania kwa ujumla na popote Duniani. Sumbawanga Ngara itafanikiwa tu endapo tutakuwa tumefanikiwa kudhibiti taka
6
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
7
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
9
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akiwa pamoja na wafanyakazi wa Osi yake ambao kwa pamoja hushiriki katika usa wa mazingira katika alhamisi ya kila wiki kuzunguka mazingira ya osi hiyo.
14
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
5. WADAU WA TAKA
Ili mpango huu wa Sumbawanga Ngara kuwa endelevu, ni lazima ushirikishe jamii ya watu wote waishio Sumbawanga pamoja na taasisi zake za kiserikali na binafsi kama ifuatavyo. Pia ni muhimu Suala la Sumbawanga Ngara lifahamike kwa wadau wengine wote wa maendeleo waishio Mkoani Rukwa na nje ya mkoa. Kwa kushirikisha makundi ya wadau wote, umiliki wa mradi huu utakuwa ni wa wote kuanzia chini (grassroot), ngazi ya uwezeshaji hadi Serikali yaani Serikali za Mitaa na Serikali Kuu. 5.1. Wananchi Hawa ni wananchi wa kawaida ambao pia ni wazalishaji wa taka za majumbani (domestic waste). Lakini pia wananchi ni nguvukazi katika kuondoa taka katika maeneo yao yanayowazunguka. Wananchi ndio wanufaika wakuu na wa moja kwa moja au kupitia fursa zinazoambatana na ajira za taka kama vile Usashaji, taka rejea, mbolea na mboji, pamoja na kuchangia huduma ya taka. Wananchi hao wanaweza kuwa ni mtu mmoja mmoja au vikundi vya kijamii, wanawake, wanaume, vijana, wazee, walemavu na kadhalika. 5.2. Serikali Kwa ajili ya kuhakikisha kuwa kunakuwa na Sera nzuri pamoja na sheria zinazosaidia kudhibiti taka. Kwa sasa baadhi ya wadau wakuu katika eneo hili ni Osi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM- TAMISEMI), Wizara ya Osi ya Makamu wa Rais -Mazingira, Ardhi, Afya, Nishati na Madini, Osi ya Mkuu wa Mkoa na Manispaa ya Sumbawanga. Wajibu wao ni pamoja na kuboresha miundombinu ya taka pamoja na vitendea kazi kama magari, vizimba sehemu ya kutupa taka n.k.
15
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
16
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
17
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
6. UCHAMBUZI WA TATIZO
6.1. MKUKUTA Kwa muda mrefu sasa Tanzania imekuwa ikitekeleza Mpango wa kupunguza Umaskini na Kukuza Uchumi (MKUKUTA) ambao juhudi mbalimbali zimetumika katika kutoa elimu pamoja na kuwawezesha wananchi. Katika eneo hili la kuboresha miji, hususan katika eneo la taka ngumu na taka miminika Serikali pamoja na wadau wa maendeleo kama vile Shirika la Kazi Duniani (International Labour Organization ILO) imejaribu kutengeneza mikakati mbali mbali ili kuona kuwa miji inakuwa sa. Lakini nguvu kubwa imekuwa ikielekezwa hasa katika miji mikubwa kama Dar es Salaam, Mwanza na Arusha.
6.2. Sheria za Mazingira na Taka, Sera Sheria ya Uhifadhi wa Mazingira Tanzania ya mwaka 2004 au kama ilivyoandikwa kwa lugha ya Kiingereza (The Environmental Management Act-EMA 2004) Sehemu ya sita (6) ya sheria inaelekeza wajibu wa mtu yeyote aishiye Tanzania kulinda na kuhifadhi Mazingira. Katika tafsiri neno Mazingira linajumuisha mambo yote yenye mahusiano yanayomzunguka Binadamu zikiwamo hewa, ardhi, maji, hali ya hewa, mwanga, harufu, vionjo, vijidudu au vimelea, shughuli za kilimo, ufugaji, mimea, rasilimali za kiutamaduni na masuala yoye yanayohusiana na shughuli za kiuchumi ikiwemo ujenzi. Waraka wa Waziri wa Nchi Osi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mheshimiwa George Huruma Mkuchika (wakati huo) unaoelekeza juu ya kufuatilia usa wa Mazingira wa mwaka 2012. Pia Waziri wa Osi ya Makamu wa Rais Mazingira
18
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
19
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
20
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
22
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
17. Kutenga maeneo ya shughuli za kiuchumi na kuwapanga wadau kadiri inavyofaa. 18. Kutafuta wafadhili ikiwa ni pamoja na kutafuta maraki wa Manispaa ya Sumbawanga Kiusa. 19. Kuendelea kutoa elimu kupitia sanaa na michezo. 20. Kuhamasisha wadau kuchangia gharama pamoja na kufadhili vikundi vinavyojihusisha na kazi za taka. 21. Kutengeneza maeneo maalum ya bustani na sehemu za kuchezea watoto. 22. Kuweka alama za barabarani. 23. Kuzuia ujenzi holela. 24. Kupata takwimu za miti iliyopo. 25. Kutenga na kuhifadhi maeneo ya vyanzo vya maji. 26. Elimu kwa wanafunzi Sumbawanga Ngara. na kuanzisha vitabu vya
27. Kuzuia kilimo kisichozingatia kanuni bora za kilimo na taratibu za mipango miji. 28. Kuzuia shughuli za uchimbaji wa madini zisizo na kiwango kufuatana na Sheria za Mji na Mazingira. 29. Kuondoa mizoga yote barabarani. 30. Kutumia mbinu zisizo na uharibifu au uchafuzi katika uvunaji wa Kumbikumbi. 31. Kuweka utaratibu wa kupuliza dawa za kuua mazalio ya mbu.
25
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
28
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akishiriki kwa vitendo usa wa mazingira kwa kusasha mitaro katika mji wa Sumbawanga tarehe 12 Januari, 2012.
7.3.
Mduara wa Utekelezaji
7.4. Ukusanyaji wa taka: Katika hatua ya kwanza mtu binafsi, kaya au Taasisi za Umma watakuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa taka kuzunguka maeneo yao au sehemu zisizohitajika zinakusanywa na kuhifadhiwa vizuri kutegemeana na aina ya taka, mfano karatasi, plastiki, chupa za vioo na kadhalika. Katika hatua ya pili taka za hatua ya kwanza zitapelekwa kwenye vituo vya muda kwa kutumia watu binafsi, mikokoteni ya vikundi au magari binafsi na ya makampuni au Taasisi. Katika hatua ya tatu Magari ya manispaa au mawakala wao ndio watahusika katika kuondoa taka hizo na kuzipeleka katika kituo cha kudumu yaani Dampo. Gharama za kazi hiyo zitapangwa kadiri ya taratibu zitakazowekwa na Manispaa.
29
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
8. HITIMISHO
Tumeamua kuanza mpango huu kwa manufaa ya Sumbawanga, Mkoa wetu wa Rukwa na Tanzania nzima kwa ujumla. Naomba sote tudhamirie na tujitoe kuufanikisha mpango huu kwa ustawi wa leo na kesho wa Sumbawanga yetu, Rukwa yetu na Taifa letu. Kama alivyosema yule Mwandishi wa Marekani Hellen Keller kwamba, Peke yetu tunafanya machache, pamoja tunafanya mengi. Tukijitoa sote kufanya kazi kwa bidii, ufahamu na maarifa hata yale yanayoonekana hayawezekani yatawezekana na hata yale yanayoonekana magumu yatakuwa mepesi. Na tuanze sasa safari hii yenye heri na mafanikio tukimuomba Mungu atusaidie. Maandishi haya yatuongezee nguvu ya kuanza safari yetu ya kuhakikisha kuwa Sumbawanga ina Ngara na Halmashauri nyingine za Rukwa zifuate. Tutaendelea kuboresha maandishi haya siku hadi siku, huku tukivuna uzoefu na kuweza kuyaboresha kadiri tunavyojifunza na kupata ushauri mbalimbali hasa ule wa kitaalam. Inawezekana, kila mtu atimize wajibu wake.
31
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
Novemba, 2012
32
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
33
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
Sumbawanga Ngara
Umoja wetu ni Ushindi!
34
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa