You are on page 1of 11

1.

0 ANDIKO LA MRADI WA KUTOA MAFUNZO YA KUOTESHA NA KUPANDA


MITI KATIKA WILAYA YA SINGIDA
1.1 Jina la Mradi:
KUTOA ELIMU YA KUOTESHA, KUPANDA MITI NA KUENDELEZA MISITU KATIKA
WILAYA YA SINGIDA KWA AJILI YA KUONGEZA MAZAO YA MISITU, KUONGEZA
UFANISI KATIKA MATUMIZI ENDELEVU YA MISITU NA KUBORESHA MAISHA YA
JAMII KUTOKANA NA MAZAO YA MISITU KWA KIZAZI KILICHOPO NA KIJACHO’

1.2 Jina na Anwani ya Mwombaji:


WIRWANA ASSOCIATION FOR DEVELOPMENT AND EMPOWERMENT (T) LTD
(WAENDELEE)
S.L.P 108, SINGIDA
Barua pepe: wirwanayetu@gmail.com
Simu: 0784 565 576, 0759 770 233

1.3 Jina na sifa ya Mwunganishi:


RAJABU AHMED MUMBEE, Mratibu wa Misitu na Mazingira wa Wilaya. Ni mhitimu
wa Chuo kikuu Cha Kilimo Sokoine(SUA), ana Shahada ya Sayansi za Mazingira na
usimamizi. Ni mfano na kielelezo katika ubunifu wa miradi ya Mazingira na kudhibiti
mabadiliko ya Tabia nchi.

1.4 Mahali Mradi utakapotekelezwa : Wilaya ya Singida

1.5 Eneo la kipaumbele lipendekezwalo: Kutoa elimu kwa wanavikundi na Kuboresha vitalu
vya kuoteshea miche kwa kununua vitendea kazi.

1.6 Aina ya Ruzuku inayoombwa: Ruzuku ya kati.

1.7 Uwezeshwaji unaoombwa: Kuwezesha wawakilishi wa vikundi vinavyosimamia vitalu


vya kuotesha miti kupata mafunzo ya namna ya kuotesha mbegu na kuhudumia miche

1
mpaka kufikia hatua ya kupandwa pamoja na mafunzo ya uhifadhi misitu na mazingira kwa
ujumla. Pia kununua baadhi ya vitendea kazi vya bustani.

1.8 Aina ya uwezeshwaji unaoombwa: Gharama za semina kama usafiri kwa wanasemina na
wawezeshaji, chakula na chai, malazi na kununua vitendea kazi vya bustani za miche.

1.9 Mantiki na uthibitisho wa kuwa na Mradi:


Katika miongo ya hivi karibuni kumekuwa na uharibifu mkubwa wa misitu katika wilaya ya
Singida uliosababishwa na ukataji ovyo wa miti, matumizi mabaya ya ardhi, ufyekwaji na
uchomwaji wa misitu kwa ajili ya kilimo na ukataji wa miti ovyo kwa ajili ya kuni na mkaa. Hali
hii imesababishwa na elimu duni katika jamii kuhusu umuhimu wa kutunza misitu na mazingira
kwa ujumla. Pia ukosefu wa maji, mavuno ya kutosha ya mazao ya chakula, biashara pamoja na
mazao ya misitu ni miongoni mwa matokeo hasi yanayoikabili jamii ya wilaya ya Singida
kutokana na uharibifu huo wa misitu na mazingira.
Kutokana na changamoto hii, taasisi ya WAENDELEE ilianzisha mradi wa kuotesha na kupanda
miti katika eneo lote la wilaya ya Singida mwaka 2015. Mradi huu umelenga kupanda miti kwa
wingi ili kuifanya wilaya ya Singida kuwa ya kijani kwa ajili ya kuongeza mazao ya misitu na
kuongeza ufanisi katika matumizi ya mazao ya misitu kwa kizazi kilichopo na kijacho.

1.10 Malengo ya Mradi na viashiria vya utendaji:

(i) Kutoa elimu na uelewa wa uoteshaji, utunzaji miti na mazingira kwa ujumla kwa jamii
katika maeneo yatakayopandwa miti.

(ii) Kuongeza uoto wa asili utakaombatana na upatikanaji endelevu wa mazao ya misitu.

(iii) Kutoa hamasa ya matumizi endelevu ya misitu na mazao yatokanayo na misitu kama
vile kufuga nyuki.

(iv) Kuongeza mazao yatokanayo na misitu kwa ajili ya kunyanyua kipato kwa jamii.

2
1.11 Matokeo yanayotarajiwa kutoka kwenye Mradi

(i) Kurudisha uoto wa asili uliokuwepo siku na miaka ya nyuma na kuboresha upatikaji wa
mazao ya misitu, nishati,mvua na maji.

(ii) Kuongeza kipato kwa wanajamii wa Singida Vijijini kupitia mazao ya misitu, ufugaji
wa nyuki lakini pia shughuli za kilimo na ufugaji zitaboreka zaidi.

(iii) Kuweka mfumo endelevu wa wanajamii wote wa Singida wa kutunza mazingira kupitia
vikundi mbalimbali kama shule, SACCOS, vijana, akina mama n.k.

(iv) Kuimarika kwa afya na kuondoa maradhi ambayo yanaweza kuzuilika kwa kuimarika
kwa mazingira.

1.12 Watakaonufaika na Mradi:

Mahitaji ya kuendeleleza mazingira ya Wilaya ya Singida ni muhimu kwa wananchi wote wa


Wilaya.

 Wanavikundi 2848 watanufaika moja kwa moja kwa kupata elimu ya uoteshaji na
utunzaji wa bustani za miti.

 Wanufaikaji wasio wa moja kwa moja, hawa ni wananchi wa Wilaya ambao ndiyo
watakuwa wapandaji wa miti na watanufaika kwa kuimarika kwa misitu na mazingira.

Mradi huu utaongeza upatikanaji wa maisha bora kwa wananchi wote kwa uboreshaji wa
mazingira na misitu ambao utaongeza ubora wa maisha.

 Kuongeza vizuizi vya upepo ambavyo kwa namna nyingine vitapunguza mmomonyoko
wa udongo na uharibifu wa mazao.

3
 Kuboresha maisha/kipato cha wanajamii kwa kuuza matunda kama machungwa, maembe
pamoja na mazao mengine ya misitu kwa mfano asali.

 Kuongeza uelewa na ufahamu wa masuala ya mabadiliko ya hali ya hewa kwa wanajamii


na kutoa mchango wa kuimarisha na kupunguza athari dhidi ya mabadiliko ya hali ya
hewa.

1.13 Jumla ya kiasi kinachoombwa kutoka kwenye Mfuko (Sh): 20,000,000


1.14 Michango mingine ikiwemo ya hali na mali (Sh): 1,000,000
1.15 Muda wa kutekeleza Mradi na mwezi utekelezaji utakapoanza:
Mradi wa kuotesha na kupanda miti umeanza toka mwezi August kwa kuanzisha bustani
mbalimbali Wilaya nzima ya Singida na kupatikana miti iliyopandwa kipindi cha 2015/2016 cha
mvua. Mradi uliwezeshwa na wanachama wa asasi na tunategemea kuendelea kuotesha miti kwa
ajili ya kupanda msimu wa mvua wa 2016/2017. Malengo ya asasi ni kuhakikisha uoto unaenea
Wilaya nzima na inakusudia kupanda miti 1,500,000 kila mwaka.

2. Ridhaa
(a). Mapendekezo ya Mkuu wa Taasisi zinazo/inayoomba

Maoni: Mradi wa upandaji miti kwa Wilaya ya Singida umeanza tangu 2015. Hata hivyo mradi
bado unahitaji uwezashwaji wa ruzuku ili kutawezesha kufanikisha malengo na azma ya
kuboresha mazingira na misitu kwa ufanisi zaidi.

Jina:_HARUNA SUMWA Cheo:_KAIMU MTENDAJI MKUU Muhuri rasmi:_________


Saini:____________________________Tarehe:____________________

(b) Mapendekezo ya Kijiji/ Mtendaji Kata/ Mtaa (ambapo Mradi utakapotekelezwa).


Maoni:______________________________________
Jina:____________________________ Muhuri:________________________
Saini: ____________________________ Tarehe:___________________________
(c) Mapendekezo ya Mkurugenzi wa Halmashauri utakapokuwa Mradi:

4
Maoni:____________________________________________
Jina : __________________________ Muhuri: _________________
Saini:___________________Tarehe:______________________

3.0 MATINI KUU

3.1 Muhtasari wa Mradi


Kwa milongo michache iliyopita Wilaya ya Singida Vijijini imekuwa na ukataji wa miti
usioelezeka, kama matokeo ya matumizi mabaya ya ardhi,
Mradi wa kuotesha na kupanda miti katika wilaya ya Singida umepewa kipaumbele na taasisi
ya WAENDELEE kutokana na hali mbaya ya uharibifu wa misitu na mazingira kwa ujumla
katika wilaya ya Singida. Mradi huu umekusudia kurudisha hali ya uoto wa misitu
iliyokuwepo kabla ya uharibifu holela wa misitu kutokea katika wilaya ya Singida kutokana
na ongezeko la watu na uhitaji mkubwa wa shughuli za kiuchumi kuongezeka. Ukosefu wa
elimu ya uhifadhi wa misitu na mazingira pia vimechangia kwa kiasi kikubwa katika
uharibifu wa misitu na uoto wa asili. Pia mradi huu unatajiwa kusaidia kupunguza na hata
kuondoa msukumo mkubwa wa jamii katika kuvamia maeneo ya hifadhi za misitu na vyanzo
vya maji vilivyobaki kwani kukiwa na miti wananchi watakuwa na uwezo wa kupata
nishati(kuni na mkaa) na mazao mengine ya misitu kama asali kutokana na miti iliyopandwa
na kuepuka kuvamia na kuharibu hifadhi za misitu ya asili. Aidha mradi unatarajiwa kusaidia
kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi kwa kuimarisha hali ya hewa na mazingira. Hivyo
shughuli zingine za kiuchumi pia zitaimarika kutokana na kuimarika kwa mazingira.

5
3.2 Utangulizi
Mradi wa uoteshaji na upandaji miti chini ya asasi ya WAENDELEE ni mradi endelevu ambao
utafanyika kwa muda usiopungua miaka kumi. Mpango wa asasi ni kufikia uwezo wa kuotesha
na kupanda miti 1, 500,000 kila mwaka. Kwa msimu wa kwanza wa mradi (2015/2016) asasi
imefanikiwa kupanda miti 160,000 katika maeneo mbalimbali ya Wilaya kwa kushirikiana na
vikundi/vitalu 13 vilivyoanzishwa wilayani. Kwa msimu wa pili wa mradi (2016/2017) asasi
imefanikiwa kuongeza vikundi/vitalu hadi kufikia 48 ambavyo vinataratajiwa kuotesha miti 1,
300,000
Mradi wa kuotesha na kupanda miti ulianza Agosti 2015 mara tu baada ya taasisi ya
WAENDELEE kuanzishwa na kusajiliwa. Katika kuongeza ufanisi taasisi ya WAENDELEE
kwa sasa inatilia mkazo suala la kuipatia jamii elimu kwa kupitia vikundi na wadau
mbalimbali kwani suala la elimu ni la muhimu na ndio msingi katika kufanikisha malengo ya
mradi huu.
Mradi wa kuotesha na kupanda miti ni endelevu na lengo kuu ni kuifanya Wilaya ya Singida
kuwa ya kijani

3.3 Azma na madhumuni ya mradi na matokeo yanayotarajiwa


Azma ya mradii huu ni kuboresha shughuli za uoteshaji miti katika vikundi/vitalu kwa
kuwapatia wawakilishi wa vikundi/vitalu elimu juu ya njia au mbinu sahihi ya uoteshaji miti na
jinsi ya kuitunza mpaka kufikia katika hatua ya kupandwa. Pia watajifunza jinsi ya utunzaji wa
misitu, matumizi endelevu ya rasilimali misitu na utunzaji wa mazingira kwa ujumla wake.
Wawakilishi 96 kati ya wanufaikaji(wanavikundi) 4848 wa moja kwa moja watapata mafunzo
hayo. Aidha mradi huu utasaidia kuboresha vitalu vya kuoteshea miche kwa kuongeza baadhi ya
vitendea kazi katika bustani husika. Mradi utasaidia kuboresha maisha ya jamii kwa kuwapatia,
elimu, ajira katika vitalu na pia ujira katika uuzaji wa miti hiyo.
Mwisho wa mradi tunatarajia kwamba, uzalishaji wa miche ya miti utaongezeka na kuboreka
kutokana na elimu itakayotolewa. Pia elimu juu ya upandaji miti, utunzaji na utumiaji endelevu
wa rasilimali misitu itafika kwa jamii nzima kwa ujumla kupitia wanavikundi watakaopata
mafunzo. Mwisho wa mradi jamii itapata mwamko wa kupanda miti kwa wingi na kuitunza kwa
ajili ya manufaa ya kizazi kilichopo na kijacho.

6
3.4 Mbinu za kutekeleza mradi
Zifuatazo ni mbinu za kutekeleza Mradi.
 Kuwapatia viongozi wa vikundi Mafunzo juu ya usimamizi wa vikundi
vinavyojishughulisha na upandaji wa miti na namna ya kutekeleza sheria ndogo ndogo
za misitu na mazingira.
 Kuwashirikisha viongozi wa Kata zote za wilaya ya Singida pamoja na wataalamu wa
misitu Wilaya juu ya utekelezaji wa mradi ili kuweza kupata michango mbali mbali
kutoka kwao.
 Kuimarisha ushiriki wa vikundi vyote vinavyojihusisha na shughuli za upandaji miti.
 Kushirikiana na uongozi wa vijiji kwa ajili ya kuandaa mpango wa usimamizi wa
Misitu pamoja na sheria ndogo ndogo za Misitu.

3.5 Vichocheo Vikuu vya Mafanikio


Vifuatavyo ni vichocheo vikuu vya mafanikio.
 WAENDELEE inayo mpango wa kuifanya Wilaya ya Singida kuwa ya kijani kwa
kujikita katika utoaji wa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa upandaji wa miti, mpaka
sasa Asasi hii imesaidia katika upandaji wa miti zaidi ya miche 160,000 katika Wilaya
ya Singida. Miti hiyo imepandwa katika taasisi mbali mbali ikiwemo shule za msingi na
Sekondari, Ofisi za vijiji, Zahanati na taasisi za kidini yaani Makanisa na Misiki pamoja
na wananchi. Kutokana na mgawo wa miti hiyo imekuwa kichocheo na hamasa kwa
wananchi katika kutekeleza azma ya mradi kwa ufanisi.
 Kwa mafanikio hayo machache tungependa kuona kila kaya ilioko Wilaya ya Singida
inapata uelewa juu ya umuhimu wa kupanda miti na kuitunza, jambo ambalo litaigeuza
Wilaya ya Singida kuwa ya kijani na kuongeza mazao yatokanayo na misitu na pia
kuondokana na hali ya ujangwa kama ilivyo sasa.

7
3.6 Mpango wa Uperembaji na Tathmini
Asasi ya WAENDELEE itafanya usimamizi na ufutiliaji wa karinbu katika kipindi chote cha
mradi. Ufutiliaji utajumuisha usimamizi sahihi wa fedha ili kufikia lengo la mradi. Tathmini
ya mradi itafanyika kwa parameta halisi na kulinganishwa ili kupata uwiano sahihi wa
mabadiliko yaliyotokana na utekelezaji wa mradi. Mabadiliko hayo yatapimwa kwa
kulinganisha parameta mbalimbali kabla na baada ya mradi kama vile ongezeko la miche
bora, uelewa wa wanavikundi kuhusu elimu ya umuhimu wa uhifadhi wa mazingira n.k.

3.7 Mpango Endelevu wa Mafanikio ya Mradi


Baada ya mradi kumalizika jamii ya Wilaya ya Singida kwa ngazi ya Kata, Vijiji na Vitongoji
kutakuwa na uelewa juu ya utunzaji wa misitu na umuhimu wa kupanda miti na kuitunza.
Lakini pia mazao ya Misitu yataongezeka kwa sababu jamii itakuwa tayari ilishapata uelewa
wa kutosha juu utunzaji wa misitu na umuhimu wa upandaji miti.

8
Kielelezo cha bajeti ya ruzuku ya kati
Kipengele/Shughuli Kizio Kiasi Gharama ya Jumla ya gharama
kizio sh. Sh.
Mafunzo ya kuotesha na kukuza miche
kwa siku tatu
Nauli ya kwenda na kurudi mtu 96 14,000 1,344,000
Malazi kwa siku tatu mtu 96 21,000 2,016,000
Chakula kwa siku tatu-chai, chakula cha mtu 96 24,375 2,340,000
mchana na usiku
Gharama ya ukumbi wa mafunzo kwa ukum 1 300,000 300,000
siku tatu bi
Gharama ya wakufuzi wa semina kwa mtu 4 450,000 1,800,000
siku tatu
Gharama ya zana za kufundishia-kalamu kala 100 500 50,000
mu
Gharama ya ya zana za kufundishia- Dafta 100 1,500 150,000
madaftari ri
Jumla ndogo ya 40% ya awamu ya mwanzo ya mradi 8,000,000
Gharama ya vifaa/vitendea kazi kwa
vikundi 48 vinavyotarajia kuotesha
miche zaidi-viriba na mbegu

Gharama ya kununua viriba kwa vikundi kilo 294.6 10,000 2,946,000


48
Gharama ya kununua mbegu aina ya kilo 24 55,000 1,320,000
gravelia
Gharama ya mbegu aina ya miti maji kilo 12 30,000 360,000
Gharama ya mbegu aina ya mijohoro kilo 24 20,000 480,000
Gharama ya mbegu aina ya machungwa kilo 24 35,000 840,000

9
Gharama ya kufuata mbegu mtu 1 54,000 54,000
Dodoma(kwenda na kurudi,chakula na
malazi ya siku moja)
Jumla ndogo ya 30% ya awamu ya pili ya mradi 6,000,000
Gharama ya kufanya ufuatiliaji na
tathmini - kutembelea vikundi 48
wilayani kwa siku 14
Gharama ya usafiri kwa siku 14 mtu 3 420,000 1,260,000
Gharama ya chakula kwa siku 14 mtu 3 84,000 252,000
Gharama ya mawasiliano kwa siku 14 mtu 1 78,000 78,000
Posho kwa wafuatiliaji kwa siku mtu 3 1,120,000 3,360,000
14@80,000
Gharama ya kuandika ripoti ya vikundi mtu 3 150,000 450,000
48
Posho ya waandishi wa ripoti mtu 3 200,000 600,000
Jumla ndogo ya 30% ya awamu ya 6,000,000
mwisho ya mradi
JUMLA KUU 20,000,000
OMBI KUTOKA MFUKO 19,000,000
MICHANGO MINGINE
MCHANGO WA 1,000,000
MWOMBAJI

10
Mpango kazi wa mradi
Malengo SHUGHULI 7 8 9 10 11 12 1 2 3 4
MAHSUSI
Uhabarisho wa 
mradi
Mafunzo ya 
kuotesha,
kupanda, kutunza
miti pamoja na
kuhifadhi misitu
Kununua vifaa 
vya bustani za
miche na
kukabithi kwa
vikundi
Ufutiliaji na 
kufanya tathmini
ya mradi
Kuandika ripoti 
ya mradi

11

You might also like