You are on page 1of 6

Sala ya Kuomba Haja au Rukhsa

(1) Mtu akitaka kufanya jambo kubwa au dogo ni bora aombe rukhsa kwa Mungu. Na akihitaji
kitu akitamani amuombe Mungu. Tunatakiwa tumuombe Mungu hata chumvi ya kupikia mara
moja.
(2) Nimemsikia shekhe akisema kuwa ukishakusali sala hii si lazima uambiwe kuwa fanya au
usifanye. Mwenyewe utajua kwa kulitaka lile ulilokusudia au kulikataa yaani utaraghibika
kulifanya au utaona si jema, yaani utahisi. Kuna watu wawili waaminifu kwa nijuavyo mimi
wamesali sala hii na wamepata uwamuzi sahihi, wamefurahi.
(3) Wengine wameona bora kuifundisha sala ya kuomba haja peke yake na sala ya kutaka rukhsa
iwe mbali. Mimi nafupisha kwa maelezo haya haya wewe nuilia lile ulilokusudia.
(4) Ikiwa umekusudia kufanya jambo zuri muombe Mungu akuwafikishe uweze kulifanya
akutilie barka na kheri nyingi ndani yake. Ikiwa jambo hilo halina kheri na wewe akuepushe nalo
asikujaalie kulitenda na akuongoze kwenye jema.
(5) Mtu humuomba Mungu wakati wowote lakini kuna nyakati nyengine nzuri zaidi tutazitaja
baadaye na ni bora kwanza kusali sala hii ikiwa unataka uwe karibu zaidi na kutakabaliwa.
(6) Ni sala ya rakaa mbili. Husaliwa wakati wowote usiokatazwa kusali lakini bora usiku na ni
bora kuisali siku tatu mfululizo.
(7) Ukishamaliza kusali soma dua. Tutaitia hapa aliyotufundisha Mtume S. A. W. tuliyoipata
vitabuni.
(8) Wala si lazima kuitamka hiyo haja yako kwa kiarabu. Mola anajua haja yako kuliko
unavyoijua wewe mwenyewe. Iseme moyoni au kwa kuitamka kwa lugha ujuwayo baada ya dua.
(9) Huu mfano tu, omba utakavyo wala usipange kuwa ntasema nini ntaomba vipi, omba kama
unamuona Mungu mbele yako, yuko mbele yako kweli na kama humuoni yeye anakuona
anakusikia.Taja haja yako kama kuolewa, kuoa, kusafiri, kuuza shamba na kama hayo. Kama haja
yako ni kuolewa na Abdulla.
" Ewe Mola wangu mimi nataka kuolewa na Abdulla basi ikwa ndoa hii ina kheri na mimi
nakuomba unijaalie aniowe ututilie kheri nyingi na barka ndani yake. Na kama haina kheri na
mimi nakuomba isiwe na uniepushe nayo kwa salama na unipe lililonakheri na mimi tena
uridhike nalo Mola wangu". kisha utamsalia Mtume S. A. W. kama tulivyoelekeza.
(10) Umewahipo kuisali sala hii, au hata umefikiripo kuisali. Tia nia ya kuisali usijiweke mbali na
dini yako.
(11) Ukitaka kutamka nia:-

(12) Dua baada ya sala hii:-

Kuomba dua
Hapa ni pazuri kutaja kidogo yahusuyo dua. Tazama kitabu changu kiitwacho Hivi Ndio
Kuabudu cha 1995 ukurasa wa 53 kuna maelezo ya namna ya kuomba dua. Kama huna
nikuletee chako lakini omba dua zako kama kawaida yako usingoje kitabu huenda kikachelewa
kukufika au kisikufike.
* wakati nzuri wa kuomba dua
(1) laylatulqadir (2) usiku wa nusu ya Shaabani
(3) siku ya Arafa (Arafa) (4) laylatiljumaa
(5) kila siku usiku (6) kabla na baada ya sala
(7) baada ya adhana (8) kabla ya iqama
(9) akifuturu ( mfungaji) (10) Mwezi wa Ramadhani
(11) baada ya mawaidha ya dini.
* pahala pazuri
(1) Msikitini Makka (2) Msikitini Madina
(3) Safa na Marwa (4) Msikiti (Beitl Maqdis)
(5) Msikiti wowote (6) Arafa na Muzdalifa
(7) Muna baada ya kupiga mawe .

* wakati mzuri
(1) ndani ya kusujudu (2) ndani ya kufunga
(3) Unapoamka (4) safarini
(6) inaponyesha mvua (6)) unapokunywa maji ya zamzam

Nakumbusha kuwa unaweza kuomba dua wakati wowote pahala popote na katika kitendo
chochote chema. Humu nilimotaja ni afadhali na uwezekano wa kutakabaliwa ni mkubwa zaidi.

Sala ya kupatwa mwezi au jua


(1) Natoa ushauri kuwa uisome sala hii katika kitabu cha sheikh Abu Taib Khalfan Al Tiwani
kiitwacho Qamusi Salaa.Yeye kagusia mila mbaya za zamani juu ya kupatwa mwezi na jua
(kimeandikwa Kiarabu).
(2) Sala hii husaliwa wakati wa kupatwa mwezi au jua. Ndio nikasema ukiipata fursa ya kuisali
usiiwache ni adimu sana. Wanawake husali pia.
(3) Ina rakaa 2 lakini rukuu 4 na alhamdu 4 na sijda 4.
(4) Mtu anaweza kuisali peke yake lakini bora kusaliwa jamaa.
(5) Sala hii kama sunna zote haina adhana wala iqama lakini ni kutoa sauti kwa takbiri ili
kuwaita jamaa kuja kusali. Kila mtu inafaa kuleta hizo takbiri, idadi kubwa.
(6) husali kama sala za kawaida:-
* soma tawjihi
* tia nia moyoni au tamka ukitaka
* soma takbiri ya kuhirimia
* rukuu kama kawaida
*simama baada ya kurukuu, usisujudu kwanza
* soma tena alhamdu na sura fupi kuliko ile ya mwanzo
* rukuu tena mara ya pili kabla ya kusujudu.
* sasa endelea na sala umalize rakaa ya mwanzo.
* simama uanze rakaa ya pili, utarukuu mara mbili vile vile
* na utasoma alhamdu baina ya kurukuu na kurukuu mara ya pili kama mwanzo.
* maliza sala kama kawaida
Utaona ina kurukuu mara nne katika rakaa mbili na alhamdu nne.
(7) Matamko ya nia sala ya kupatwa mwezi:-

(8) Ya kupatwa juwa:-

Sala ya Maiti
(1) Kuna thawabu nyingi sana katika kumsalia maiti. Inasikitisha sana kuwa wengi wetu ingawa
tunakwenda kuzika lakini wachache tunaomsalia. Mashekhe wengi wanasema hii ni faridha
kwani maiti asiposaliwa watu hupata dhambi.
(2) Sala hii tumeifundisha katika vitabu vitatu vyengine kwa hivyo hapa tuaitia kwa ufupi. Vitabu
hivyo ni kiitwacho Sala ya Maiti na chengine Huduma za Maiti na Kitabu cha Hijja na Umra.
Tafadhali visome.
(3) Husaliwa jamaa au hata mtu peke yake. Ina takbiri ya kuhirimia na nyengine tatu. Zote ni nne.
Haina kurukuu wala kusujudu. Ni kusimama tu kwa wanaoweza.
(4) Haina kusoma Qur-an baada ya alhamdu.
(5) Anza sala yako kama kawaida kwa tawjihi na nia. Imamu akileta takbiri ya kuhirimia nawe
ilete. Na hii ndio ya mwanzo.
(6) Soma alhamdu, ukisha msubiri imamu.
(7) Akileta imamu takbiri ya pili nawe ilete, usimtangulie imamu katika takbiri zote.
(8) Baada ya takbiri ya pili (i) Msalie Mtume S A W au (ii) soma alhamdu ya pili. Khiari yako.
Wa zamani wakisoma alhamdu ya pili.
(9) Msubiri imamu akileta takbiri nawe ilete, hii ni ya tatu.
(10) Soma dua. Tutakutilia dua fupi, ukitaka refu utaipata pahala pengine.
kama umesoma alhamdu mbili msalie Mtume S.A.W. katika hii dua. Tutakutilia hapa dua ya
kumsalia Mtume S. A. W. pia kwa ufupi.
(11) Msubiri imamu akileta takbiri ya nne nawe ilete.
(12) Msubiri imamu akitowa salamu nawe maliza sala yako kwa salamu pia. Kasha omba
maghfira na kushukuru, ukiwa na hakika kuwa nawe siku yako haiko mbali.

Dua Fupi Baada ya Takbiri ya Tatu


Hii ndio fupi, nimeipa namba iwe wepesi kwako kuihifadhi. Watu wengi hawamsalii maiti kwa
kuwa hawakuhifadhi dua. Kama unajua nyengine inafaa.

(mwanamme)
mwanamke)

Unaweza kuikamilisha dua yako kwa kusoma aya ii:-


* (5)
*
*
Hii dua bila ya namba.

*
* *

(13) Ikiwa ulisoma alhamdu mbili, hapa,mwisho wa dua msalie Mtume S. A. W..

(14) Kila ukitaka kumsalia Mtume S.A.W. soma hii au kama hii.

Sala ya maiti kwa ufupi


(1) Tawjih
(2) Takbir
(3) Alhamdu (usisahau bismillahi)
(4) Takbir
(5) Kumsalia Mtume S.A.W. (au Alhamdu ya pili).
(6) Takbir
(7) Dua
(8) Takbir
(9) Salam
Sasa huna sababu ya kuwa usimsalie maiti.
Makosa na Mambo Mengine Mengine
Tumeona makosa mengine ndani ya sala inafaa kuyataja.
(1) Katika rukuu unatakiwa upinde mgongo bila ya kupinda magoti, uwe kama herufu C na
kichwa kimepinda kutazama chini wala sio kusogeza magoti kwa kuyapinda ili uyapate kwa
urahisi. Usiwe zigzag.
(2) Ukisimama kutoka kwenye rukuu usisujudu mpaka usimame sawa sawa. Usifupishe kwa
kusujudu kabla hujasimama sawa sawa.
(3) Unaposujudu kipaji cha uso na pua iguse pakusujudia. Sio kilemba au kofia.
(4) Unaposujudu vidole vya miguu vibane kwenye msala upande wa nyayoni sio kwa juu, wala
miguu isining'inie kama ya sungura.
(5) Unapotoa salamu usiyavute mbele mabega. Kwa nini unafanya hivyo na wewe unawaombea
dua walionyuma yako. Salamu ni dua.
(6) Kujiona mtu yuko peke yake asivalie kikamilifu. Valia kikamilifu na jitie uturi-manukato
kidogo hata kama hakuna wa kumfikia harufu yake.
(7)Usiingie msikitini na simu mfukoni. Ikitokezea ikatoa sauti utawababaisha wengine na wewe
mwenyewe. Ikilia simu na wewe umo katika safu na jamaa ukiizima huenda ukaharibu sala yako
peke yako na usipoizima utaharibu na sala za wenzako pia. Dhamana ya kukosea kwao kwa
kuwababaisha ni juu ya shingo yako. Fanya uamuzi sahihi..
(8) Imamu asikae muda mrefu baada ya adhana awasalishe watu wachawanyike katika ardhi
kutafuta rizki, sio akae nusu saa anasubiri mtu au anasubiri wakati wa kalenda.
(9) Kuadhini iwe kwa wakati kwa sababu wengine hufanya ndio saa yao ya kujizuia kula daku au
kuanza kufutari hata kama si mwezi wa Ramadhani. Na wengine hawasali mpaka wasikie adhana
hata kama wakati umeshaingia.
(9) Jifundishe ujue maana ya kisomo chote katika sala. Uliza japo si sala yote kwa mara moja.au
soma vitabu upate tafsiri. Tafsiri ya alhamdu kama huijui anza leo kujifunza. Tafsiri za Qur-ani
ziko zinapatikana na kama huwezi kupata uliza usijikalie tu. Jishughulishe na dini yako. Mola
Atakusaidia.

Sala kwa Ufupi


Baada ya kuwa masharti ya sala yametimia yote, na ni pamoja na kuwa na nia ya kusali, ambayo
pia ni nguzo ya sala, na kuwa na nguo zifaazo kusalia, na pahala safi na kuelekea kibla basi kwa
rakaa ya mwanzo simama (kusimama pia ni nguzo katika sala za faridha):-
(1) soma adhana na iqama mwanamme tu, sala za faridha.
(2) soma tawjihi. Kwa sala zote
(3) Soma takbir ya kuhirimia sala zote
(4) soma audhu kama hujaisoma kabla sala zote
(5) soma alhamdu yote pamoja na bismillah sala zote
(6) soma sura au aya za Qur-an tulimoeleza tu
(7) rukuu kwa kukamata magoti ila sala ya maiti
(8) ukimaliza kurukuu simama sawa sawa.
(9) sujudu kwa viungo saba ila sala ya maiti
(10) kaa kitako baada ya sijda
(11) sujudu mara ya pili.
(12) simama kutokana na sijda ya pili.
Rakaa ya mwanzo imemaliza hapa.
(13) Rakaa nyengine zote huanza kwa bismillahi ya alhamdu.
(14) Husomi tena yale yote yaliyo kabla ya alhamdu ya mwanzo.
(15) Katika sala ya rakaa nne, rakaa ya pili siku zote humaliza kwa tahiyyatu ya mwanzo na ile
ya nne humaliza kwa tahiyyatu ya mwisho na salamu.
(16) Katika sala ya rakaa tatu rakaa ya pili siku zote humaliza kwa tahiyyatu ya mwanzo na ile
ya tatu humaliza kwa tahiyyatu ya mwisho na salamu.
(17) Katika sala ya rakaa mbili rakaa ya pili siku zote humaliza kwa tahiyyatu ya mwisho na
salamu.
(18) Sala ya rakaa moja humaliza kwa tahiyyatu ya mwisho na salamu.
(19) Salamu ni moja ya nguzo za sala.
(20) Ikiwa kuna sijda ya kusahau ilete baada ya salamu au kama tulivyofundisha. Sijda maalumu
huja baada ya salamu na pia dua zako nyengine.

Itikafu kwa ufupi sana


(1) Kufanya itikafu ni kukaa msikitini kwa nia ya kufanya ibada kwa kufuata nidhamu maalumu
za itikafu.
(2) Hii ni sunna kubwa kwa vile imetajwa katika Quran pale ilipokatazwa kuwaingilia wanawake
kwa mwenye kufanya itikafu. Na pia Mtume (S.A.W.) na masahaba wake waliifanya.
(3) Nidhamu yake imechukuliwa kutokana na vile ilivyofanywa. Na kwa hivyo kuna khitilafu
ndogo ndogo na kubwa kidogo katika hiyo nidhamu. Na pengine ndio sababu iliyochangia
kupelekea kusahauliwa itkafu au kuwa imehamwa mpaka watu wengi hawaitaji na wengi
hawajapata kuisikia hata mashekhe wakiitaja.
(4) Nidhamu hii ni pamoja na masharti ambayo yasipotimizwa haiwi itikafu na makatazo ambayo
yakifanywa yataiharibu.
(5) Hapa tutaja baadhi kwa ufupi:-
* iwe ndani ya msikiti unaosaliwa jamaa. (kwa Kiibadhi ni sharti).
* iwe mtu amefunga.(kwa Kiibadhi ni sharti).
* iwe usiku na mchana unaofuatia.(Kwa wengine wana rai nyengine).
* usiku uanzie mwanzo kabla jua kutua. Mchana umalize magharibi kwa kutua jua. (na hapa
kuna khitilafu pia).
* iwe hapana kutoka msikitini ila kwa haja kubwa ya lazima.
* achunge mambo ya dini asiwe mwenye kuasi hata kwa maneno.
* ukitoka msikitini bila ya haja kubwa ya kukubalika ukarejea lazima utie nia upya.
* inaharibika kwa maingiliano ya kimwili mke na mume.(kuna khitilafu juu yale yaliyohusu
kitendo hicho ambayo huja kabla.
* ikiharibika lazime irudiwe tena. Ilipwe.
* kuna na mengi mengine. Mengine ya kawaida kama nia na tohara na mengineyo.
Ibada za sunna za kufanya ndani ya msikiti tumeshazitaja kabla. Tazama huko na ni pamoja na
sala za sunna za usiku.
Na yote hayo yana khitilafu za maulamaa. Soma tafauti hizi kwa urefu katika kitabu kiitwacho
Fiqh Sunna Cha Sayyid Saabiq au Qawaid L-islam cha Aljittaly au
chochote kizuri.
(6) Ukitaka kufanya itikafu uliza. Hapa tumetia kwa ufupi sana kukujuilisha kwani kama
nilvyosema wengi hawajui kama kuna itikafu katika kuabudu.) Tunaomba uzinduke nawe ufanye
itikafu inshaallah.
This document was created with Win2PDF available at http://www.daneprairie.com.
The unregistered version of Win2PDF is for evaluation or non-commercial use only.

You might also like