You are on page 1of 6

Masharti ya Sala

Haya ni baadhi ya masharti ya lazima katika hali ya kawaida kwa sala zote.
(1) Kuwa Muisalmu.
(2) Kuwa na nia ya kutaka kusali sala ile.
(3) Kuwa tohara mwili, kivazi na pahali pakusalia.
(4) Kuvalia kivazi cha kufaa kwa sala.
(5) Pahala pakufaa kusali.
(6) Kusali ndani ya wakati wake.
(7) Kuelekea kibla.

Tafauti ya mwanamme na mwanamke katika kusali


Ni bora nioneshe tafauti hizi mapema kwani maelezo ya sala yatakuwa kwa mwanamme basi
mwanamke atakuwa keshajua yale ambayo hayamuhusu.
(1) Mwanamke hasomi adhana wala iqama. Ni jambo la maana sana kusoma dua baada ya adhana
na iqama kwa wote.
(2) Mwanamke si vyema kusali msikitini na wanaume lakini sala yake haiharibiki ikiwa
hatoiharibu kwa mambo mengine yaharibuyo sala.
(3) Mwanamke anaweza kusalisha wanawake, asiwe mwanamme hata mmoja katika maamuma.
(4) Mwanamke anaweza kusalishwa na mwanamme.
(5) Safu bora ya wanaume ni ile ya mwanzo. Safu bora ya wanawake ni ile ya mwisho. Ikiwa
pana watoto safu yao iwe baina ya wanawake na wanaume.
(6) Mwanamke atajikunjakunja akisali na zaidi wakati wa kusujudu, haibagui mikono yake mbali
na kiwiliwili chake bali anaigandisha., wala hasujudu mbali na magoti akaacha mvungu wa
tumbo.
(7) Mwanamke afunike mwili wote isipokuwa uso na viganja hata kama anasali peke yake.
Mwanamme yeye avaliye vyema katika sala ingawa inatosha kujistiri baina ya kitovu na magoti.
Kitovu na magoti visitiriwe.
(8) Mume akisali safari na mke atasali safari. Akifa mume ugenini mke ataendelea kusali safari
mpaka arejee au aolewe na mume mkaazi.
(9) Mwanamke asitie udhu akiwa pahala anapoonekana na wanaume na hata wanawake ajnabi
kwani hudhihiri baadhi ya viungo vyake. Wala asisali pahala wazi watu wakamuona ila kwa
dharura. Ikiwa hapana cha kujistiri basi aende mbali kidogo iwe ni masafa yanayomstiri.
(10) Ikiwa imamu kakosea na ikabidi mwanamke amzinduwe basi hasemi neno inasemekana
kuwa hupiga kofi dogo nyuma ya kiganja cha kushoto kwa kiganja cha mkono wa kulia. Na Mola
ndiye anayejuwa.
(11) Imamu mwanamke hakai mbele. Hukaa katikati katika safu ya mbele.
(12) Mwanamke anaweza kumsalia maiti, soma sala ya maiti karibu na mwisho wa kitabu hichi
uijuwe ukipata fursa uisali haina taabu.
(13) Mwanamke hasomi sala kwa sauti ya kusikia wengine.
(14) Anapokwenda msikitini, mwanamke asijipambe wala asijitie manukato. Mwanamme afanye
hivyo, lakini asinukie sana.
(15) Wanawake wawe wa mwanzo kutoka msikitini baada ya sala. Wafanye haraka kurudi
majumbani wasipige soga mbele ya msikiti wala wasizurure huku na kule kama wafanyavyo
wengi kule Makka na Madina.
(16) Mwanamke hakai msikitini akiwa na hedhi au nifasi.

Sala za Faridha
(1) Sala ya adhuhuri husaliwa rakaa nne kwa kusoma ndani yake alhamdu tu katika rakaa zote
nne. Siku ya Ijumaa husaliwa sala ya Ijumaa rakaa mbili badala ya adhuhuri.
(2) Sala ya laasiri husaliwa rakaa nne kwa kusoma ndani yake alhamdu tu katika rakaa zote nne.
(3) Sala ya magharibi husaliwa rakaa tatu kwa kusoma ndani yake alhamdu na sura au aya za
Qur-an katika rakaa mbili za mwanzo na kusoma alhamdu tu katika rakaa ya tatu, ya mwisho.
(4) Sala ya isha husaliwa rakaa nne kwa kusoma ndani yake alhamdu na sura au aya za Qur-an
katika rakaa mbili za mwanzo na alhamdu tu katika rakaa mbili za mwisho.
(5) Sala ya alfajiri husaliwa rakaa mbili kwa kusoma ndani yake alhamdu na sura au aya za
Qur-an katika rakaa zote mbili..
(6) Wengine wanasema sala ya maiti ni faridha na sala ya witri ni sunna ya wajib. Mtu akiwa
hakusali sala ya witri lazima ailipe. Na Mola Anajua zaidi.
(7) Sunna ya alfajiri mtu akiikosa anaweza kuilipa baada ya faridha ya alfajiri au baada ya kutoka
jua.

Nguzo za sala
Ni zile ambazo mtu akiziacha bila sababu hata kwa kusahau basi sala huharibika. Nazo ni pamoja
na:-
(1) Nia (2) Kusimama
(3) Takbir ya kuhirimia (4) Alhamdu
(5) Kurukuu (6) Kusujudu
(7) Kukaa kwa tahiyatu (8) Tahiyatu
(9) Salamu.

Nyakati za sala
(1) Adhuhuri huanza mchana pale kivuli chako kinapoanza kurefuka kwani jua lilipokuwa juu ya
utosi wako kilikuwa kifupi umekikanyaga.. Mwisho wa wakati ni pale kitakapokuwa sawa na
wewe mwenyewe.
(2) Hapo huanza laasiri na kuendelea mpaka kutua jua.
(3) Hapo hapo huanza magharibi na kuendele mpaka yaanze kutoweka mawingu mekundu.
(4)Hapo huanza wakati wa isha mpaka thuluthi ya usiku. Maulamaa wengine wanasema mpaka
nusu ya usiku.
(5) Alfajiri huanza kwa kutoka alfajiri na humaliza kwa kuchomoza jua.

Nyakati tatu zilizokatazwa kusali sala yoyote.


(1) Linapoanza kuchomoza jua asubuhi mpaka likamilike kutoka lote.
(2) Linapoanza kutua jua magharibi mpaka likamilike kutuwa lote.
(3) Jua linapokuwa katikati mchana juu ya utosi siku za joto kali isipokuwa sala ya Ijumaa.

Nyakati zisizofaa kusali sala yoyote ila zenye sababu.


(1) Baada ya sala ya laasiri mpaka lituwe jua lote.
(2) Baada ya sala ya alfajiri mpaka litoke jua lote ila sunna ya alfajiri ile kama umeikosa kuisali
kabla.

Nyakati zisizofaa kusali sala yoyote ila baada ya kitendo


(1) Haifai kusali sala isiyokuwa na sababu baada ya kusali witri ila baada ya kulala japo kidogo.
Ikiingia alfajiri anaweza kusali kama kawaida yake.
(2) Haifai kusali sala yoyote ikiwa inasaliwa sala ya faridha jamaa mpaka imalize. Mtu akiwa
anasali sunna pakasaliwa faridha jamaa basi awache sunna aunge jamaa. Ama ikiwa jamaa
yenyewe ni sunna anaweza kusali faridha. Kwa mfano ikiwa watu wanasali taraweh yeye
anaweza kusali isha. Na Mola anajua zaidi.

Nyakati zinazofaa kusali


(1) Nyakati zote ambazo hazikukatazwa zinafaa kusali. Inafaa pia kusali sala zenye sababu
maalum katika nyakati maalum zisizofaa sio zile tatu zilizokatazwa. Ni bora kuweka mifano:-
(1) Inafaa kusali sala ya kupatwa mwezi baada ya sala ya witri. Sala hii ina sababu maalum nayo
ni kupatwa mwezi la si hivyo isingesaliwa au ingeweza kusaliwa wakati mwengine.
(2) Inafaa kumsalia maiti baada ya sala ya laasiri au sala ya alfajiri.
(3) Inafaa kusali baada ya laasiri likishakutua jua lote hata kama hujasali faridha.
(4) Kauli mpya ni kuwa mtu anaweza kusali tahiyatulmasjid ikiwa amesali sunna ya alfajiri
nyumbani.
(5) Inafaa kusali sala ya tawafu laasiri ikwa jua halijaanza kutuwa na baada ya sala ya alfajiri
ikiwa halijaanza kutoka. Ama likianza kutoka mpaka litoke lote na likianza kutua mpaka litue
lote.

Namna ya Kusali
Sala ya mtu peke yake ya rakaa nne
Sala ya adhuhuri au laasiri au isha..
(1) Simama uelekee kibla usiache nafasi kubwa baina ya miguu. Iwe nafasi kiasi ya urefu wa
unyayo wako. Elekea kibla kwa kifua chako utazame pahala pakusujudia. Fanya hivi kwa sala
zote. Sala za sunna unaweza kusali umekaa lakini thawabu zinapunguwa.
(2) Soma adhana kama haijasomwa hapo. Mwanamke hasomi adhana.
(3) Soma iqama. Mwanamke hasomi iqama.
(4) Soma tawjihi. Madhehebu yetu sala zote zinayo tawjihi hata ya maiti tawjihi ni hii:-

(5)Ikiwa utapenda kutamka nia, hapa ndio pahala pake.


(i) Ya adhuhuri:-

(ii) Ya laasiri:-

(iii) Ya isha:-

(iv) Ya magharibi:-

(v) Ya alfajiri

(6)Soma takbir ya kuhirimia.


Kwa kusoma takbir ya kuhirimia utakuwa umeshaingia ndani ya sala ukifanya lolote la kuharibu
sala basi sala yako itaharibika. Sala zote zinayo takbir hii. Sasa hapa inaanza rakaa ya mwanzo ya
sala zote.

Rakaa ya mwanzo kwa sala zote


(7) Soma audhu ikiwa ilikuwa hujaisoma.
(8) Soma bismillah yote.
(9) Soma alhamdu yote.
(10) Sala ya adhuhuri na laasiri hazina kusoma sura wala aya za Qur-ani. Ama magharibi na isha
na alfajiri hapa ndio pakusoma sura au aya za Qur-an katika rakaa mbili za mwanzo.
(11) Ukimaliza utarukuu na huku unasoma takbir. kamata magoti yako vyema usome
tasbihi hii mara tatu au zaidi.
Kisha simama na huku unasoma samiallahu. mara moja tu. Ukisha kusimama
sawa sawa soma rabbanaa mara moja tu.
(12) Sujudu kwa kuleta takbir. Pinda magoti yaweke juu ya msala , weka mikono kisha weka
kichwa na pua juu ya msala, hakikisha viungo saba vimegusa chini sawa sawa kisha lete au soma
tasbih hii mara tatu.Viungo saba ni kipaji cha uso na pua, viganja viwili , magoti
mawili matumbo ya vidole vya miguu miwili. Viganja uwe umevikunjua, vidole viwe
vimegusana. Uchache wa kusoma tasbih ni mara tatu. Unaweza kuzidisha ukitaka.
(13) Ukisha utakaa kitako kwa takbir. Kalia miguu yako au mguu wa kushoto. Weka mikono juu
ya magoti na utulize viungo vyote.
(14) Sujudu mara ya pili kama sijda ya mwanzo kwa takbir na tasbih. Hapo utakuwa
umeshamaliza rakaa ya mwanzo.
(15) Simama kwa takbir uanze rakaa ya pili.

Rakaa ya pili
(1) Rakaa zote nyengine usisome adhana wala iqama wala audhu wala tawjih. Anza na
bismillahi na alhamdu. Ikiwa ni isha au magharibi au alfajiri basi utasoma sura au aya za Qur-an
baada ya alhamdu.
(2) Rukuu kisha usujudu kama rakaa ya mwanzo ila usisimame utakaa kusoma tahiyatu ya
mwanzo. Ukimaliza ndio usimame kwa ajili ya rakaa ya tatu. Kila ukisujudu au ukisimama lete
takbir.

Tahiyatu ya mwanzo ni hii:-

Rakaa ya tatu
(1) Simama uanze rakaa ya tatu. Umeshajua kuwa rakaa huanza kwa bismillahi ya alhamdu na
humaliza rakaa kwa kumaliza sijda.
(2) Katika sala ya rakaa nne, rakaa ya tatu haina tahiyatu. Simama kwa ajili ya rakaa ya nne.
(3) Kumbuka katika sala ya isha rakaa mbili za mwanzo utasoma sura au aya za Qur-an baada ya
alhamdu.

Rakaa ya nne
(1) Kumbuka kuwa haina kusoma sura baada ya alhamdu lakini inayo tahiyatu. Soma tahiyatu ya
mwisho wenye kujua ile tahiyatu ya zamani wataona tafauti kidogo. Zote zinafaa hii ni nyepesi
na ina dua ndani yake.

Tahiyatu ya mwisho ni hii:-

(2) Toa au soma salamu. Na sala imekwisha.


Salamu hii ikusudie ni dua kwa viumbe wema walioko kulia na kushoto na nyuma yako. Salamu
moja inatosha na ukitoa mbili si vibaya. Salamu ukiitoa peleka uso kwenye bega la kulia na la
kushoto bila kulivuta wala kulinyanyua wala kuchezesha kichwa, haifai.
Sala imekamilika tumshukuru Mola ili atuzidishie neema na rehma.

Sala ya rakaa tatu


Salaya mtu peke yake ya magharibi
(1) Ni kama sala ya isha ila hii ina rakaa tatu.
(2) Utasoma sura au aya katika rakaa mbili za mwanzo baada ya alhamdu..
(3) Tahiyatu ya mwanzo katika rakaa ya pili na ya mwisho katika rakaa ya tatu.

Sala ya Rakaa mbili


Sala ya mtu peke yake ya alfajiri
(1) Ni kama sala ya magharibi au isha ila hii ina rakaa mbili tu. Unasoma sura au aya za Qur-an
baada ya alhamdu katika zote rakaa mbili.
(2) Tahiyatu ya mwisho ni hiyo ya rakaa ya pili.
Sala ya Rakaa mbili
Sala ya Ijumaa husaliwa jamaa
(1) Siku ya Ijumaa husaliwa sala ya Ijumaa badala ya adhuhuri ni lazima sio pendekezo,
isipokuwa mgonjwa sana, mtoto, msafiri, na mwanamke kwa madhehebu yetu sijui mengine ni
vipi. Hawa hawalazimishwi lakini hawazuiliwi wakitaka watasali.
(2) Sala hii ina masharti yake na ni pamoja na kuwa isaliwe jamaa.
(3) Ni kama sala ya alfajiri. Imamu atasoma sura au aya za Qur-an baada ya alhamdu katika zote
rakaa mbili.
(4) Tahiyatu ya mwisho ni hiyo ya rakaa ya pili.
(5) Kabla ya kusali imamu atasoma khutba, ni makosa kusema hata neno moja ikiwa imamu
anakhutubu bali ni wajib kumsikiliza.
(6) Ikiwa hukumuwahi imamu kwa rakaa kamili itakubidi usali na adhuhuri. Na Mola Anajua
zaidi.
(7) Ni sunna siku ya ijumaa kuoga na kujitia manukato- mafuta au krim yenye kunukia kidogo.
Na ni wajibu kuvalia vyema kwa kila ukienda msikitini.
(8) Ukitaka kutamka nia ni hii. Husomwa baada ya tawjih.

Sala ya Jamaa
(1) Unaposali na imamu nuilia kusali na jamaa na kuwa ni amri unaitekeleza.
(2) Usimpite imamu kwa chochote ikiwa kisomo au kitendo, usimtangulie wala usiwe nyuma
sana. Unaweza kujua spidi yake kutoka rakaa ya mwanzo. Ikiwa atasujudu na wewe hujamaliza
kusoma alhamdu basi ana spidi kubwa na wewe itabidi uongeze kidogo. Ikiwa wewe utamgonja
sana hajasujudu baada ya kumaliza alhamdu basi ana spidi ndogo na wewe itakubidi upunguze
spidi.
(3) Wewe utaanza kwa tawjihi na nia kisha utaanza rakaa ya mwanzo na kuendelea kama
unayesali peke yako.
(4) Usisome sura wala aya baada ya alhamdu mote. Msikilize imamu na uzingatie maana ya yote
unayomsikia khasa maana ya Qur-an.
(5) Mfuate imamu vitendo vyote. Usisome samiallahu wewe soma rabbanaa
mote.
(6) Ikiwa imamu ni msafiri akasali rakaa mbili katika sala ya rakaa nne basi wewe kamilisha nne
kama sala ya mtu peke yake. Ama ikiwa nyote ni wasafiri mutamaliza pamoja rakaa mbili
zinatosha.
(7) Ikiwa wewe ni msafiri unasali rakaa mbili katika sala ya rakaa nne ukamuwahi imamu
anayesali rakaa nne katika rakaa mbili za mwisho basi itakubidi usitowe salamu naye, uzisali
rakaa mbili za mwanzo za mtu peke yake ndio utowe salam, utakuwa na wewe umesali nne.
(8) Si makosa kutamka nia kabla ya kuhirimia. Matamko ya nia ni:-
(i) Ya adhuhuri:-

(ii) Ya laasiri:-

(iii) Ya isha

(iv) Ya magharibi:-

(v) Ya alfajiri
This document was created with Win2PDF available at http://www.daneprairie.com.
The unregistered version of Win2PDF is for evaluation or non-commercial use only.

You might also like