Professional Documents
Culture Documents
Mchango Wa Waandishi Wa Kazi Za Kubuni Katika Uend
Mchango Wa Waandishi Wa Kazi Za Kubuni Katika Uend
net/publication/337543122
CITATIONS READS
0 5,027
1 author:
SEE PROFILE
All content following this page was uploaded by Ernest Sangai Mohochi on 09 September 2020.
To cite this article: Ernest Sangai Mohochi (2019) Mchango wa Waandishi wa Kazi za Kubuni
katika Uendelezaji wa Kiswahili, Eastern African Literary and Cultural Studies, 5:3-4, 223-238, DOI:
10.1080/23277408.2018.1529851
IKISIRI MANENO
Makala hii ililenga kuchunguza mchango wa waandishi wa waandishi wa kazi za kubuni;
kazi za kubuni katika uendelezaji wa Kiswahili. Hili ushawishi wa kijamii; athari;
lilichochewa na ukweli kuwa waandishi ni miongoni mwa uendelezaji wa Kiswahili;
wanafunzi; walimu
makundi muhimu katika ukuzaji wa lugha, mengine
yakiwa: wanaisim, walimu, watafiti, wachapishaji, na
wapenzi wa lugha. Hata hivyo, waandishi wa vitabu
kuhusu maswala mbalimbali ya kinadharia, pamoja na
uendelezaji wa lugha na fasihi yake ndio wametajwa zaidi.
Mchango wa waandishi wa kazi za kubuni haujaangaziwa
sana. Madhumuni mahsusi ya makala hii yalikuwa
kuchanganua nafasi ambayo waandishi wa fasihi ya
Kiswahili wameipa lugha hii katika kazi zao, pamoja na
jinsi ambavyo nafasi hiyo inachangia katika ukuzaji wa
lugha hiyo. Aidha, maelezo yametolewa kuhusu jinsi
wamechangia kuwaathiri wasomaji wao kuhusu umuhimu
wa Kiswahili. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya
ushawishi wa kijamii inayoshikilia kuwa watu maarufu
wana ushawishi mwingi unaowawezesha kuwaathiri
wengine katika jamii. Waandishi wana sifa hizo na hivyo
wanaweza kuathiri misimamo na mielekeo ya wasomaji
wao kuhusu umuhimu wa lugha ya Kiswahili. Data
ilikusanywa kwa kusoma kazi za kubuni za waandishi
watatu wa fasihi ya Kiswahili walioteuliwa maksudi:
Shaaban Robert, Wallah bin Wallah na Ken Walibora,
pamoja na hojaji iliyotolewa kwa wanafunzi 40 na walimu
8 katika Chuo Kikuu cha Rongo. Vilevile, kazi za waandishi
hao ziliteuliwa maksudi. Matokeo ya utafiti huu
yameonyesha kwamba waandishi hawa wameipa lugha ya
Kiswahili nafasi ya kipekee kama sehemu ya maudhui
katika kazi zao, na wamewachora wahusika wapenzi wa
Kiswahili wanaokitetea Kiswahili, ambao wanawaathiri
wahusika wenzao. Isitoshe, waandishi hawa wameathiri
msimamo wa wanafunzi na walimu wa Kiswahili kuhusu
Kiswahili kutokana na nafasi wanayokipa katika kazi zao.
Makala inahitimisha kuwa, kwa mujibu wa nadharia ya
ushawishi wa kijamii, waandishi ni kundi muhimu katika
jamii lenye ushawishi mkubwa na wanapoendelea
kuithamini lugha ya Kiswahili, watawaathiri wengine wengi
kuwa na msimamo kama huo.
WASILIANA Ernest Sangai Mohochi smohochi@gmail.com © 2019 Informa UK Limited, trading as Taylor & Francis Group
Eastern African Literary and Cultural Studies is co-published by NISC Pty (Ltd) and Informa Limited (trading as Taylor & Francis Group)
224 E. S. MOHOCHI
Utangulizi
Lugha ni kitu ambacho daima huhitaji kushughulikiwa kwa namna mbalimbali ili
kukiwezesha kutekeleza majukumu yake katika jamii. Hili linachangiwa kwa kiasi
kikubwa na ukweli kuwa lugha hubadilika kwa mpito wa wakati. Ili hili liweze kufa-
nyika kunahitajika juhudi za maksudi kutoka kwa wadau mbalimbali. Miongoni
mwa watu muhimu katika mchakato huu ni waandishi. Makala hii imelenga
kundi hilo la wadau lakini kwa kujikita zaidi katika waandishi wa kazi za fasihi,
huku mjadala ukiegemezwa kwenye nadharia ya ushawishi wa kijamii. Makala
imetangulizwa na mjadala mfupi wa dhana ya ushawishi kwa kuwarejelea wataa-
lamu wachache miongoni mwa wale ambao wameizungumzia. Sehemu ya pili
imemulika athari au ushawishi walio nao waandishi katika jamii. Hii imefuatiwa
na maelezo ya mchango wa waandishi wa fasihi katika uendelezaji wa lugha ya
Kiswahili, ikiwa ni pamoja na uchambuzi wa kazi mahsusi za waandishi watatu
wa fasihi ya Kiswahili ili kuonyesha ni jinsi gani wamekipa Kiswahili nafasi
muhimu katika kazi zao. Inatarajiwa kuwa jambo hili linaweza kutoa hamasisho
na kuchangia kupendwa zaidi kwa lugha hiyo. Pia, maoni ya wanafunzi na
walimu wa Kiswahili kuhusu mchango wa waandishi wa kazi za kubuni katika uen-
delezaji wa Kiswahili umejadiliwa.
Mbinu za Utafiti
Mwandishi alipitia kazi mbalimbali za waandishi wa Kiswahili na kueleza mchango
wa kazi hizo katika uendelezaji wa lugha ya Kiswahili. Katika kufanya hivyo, kundi
la kwanza linahusu kazi za waandishi wa awali ambao walichangia sana ukuzaji wa
fasihi ya Kiswahili. Sehemu ya pili ilihusisha usomaji wa kina wa kazi mahsusi za
waandishi watatu na kuonyehsa zinavyochangia ukuzaji wa Kiswahili katika
ujenzi wa maudhui. Kazi zilizorejelewa ni za Shaaban Robert, Wallah Bin Wallah,
na Ken Walibora. Kazi zao zinazozungumzia Kiswahili ziliteuliwa maksudi na kuja-
diliwa katika makala hii. Aidha, hojaji ilitumiwa kupata data kutoka kwa wanafunzi
228 E. S. MOHOCHI
wa Kiswahili katika Chuo Kikuu cha Rongo pamoja na walimu wa chuo hicho na
shule jirani katika kaunti za Migori na Kisii, magharibi mwa Kenya. Walimu wa
shule jirani waliotumiwa ni wale ambao hufunza Kiswahili kama walimu wa
muda katika Chuo kikuu cha Rongo. Lengo kuu la kutumia hojaji lilikuwa
kupata maoni ya walimu na wanafunzi kuhusu nafasi ya kazi za kubuni katika uen-
delezaji wa Kiswahili, pamoja na athari ya waandishi wa kazi hizo katika maswala
ya ukuzaji wa Kiswahili. Kwa jumla, wanafunzi arobaini na walimu wanane
walishiriki katika utafiti huu. Walimu na wanafunzi walioshiriki ni wale ambao wali-
patikana chuoni Rongo wakati wa kufanyika kwa uchunguzi huu.
unyanyasaji kwa wenyeji, hususan wanyonge katika jamii. Kupitia kwa njia hii, fasihi
inatekeleza majukumu kadhaa likiwemo lile la kuangazia historia ya jamii zetu.
Tukizingatia kuwa fasihi ina mchango mkubwa pia katika kufunza na kupanua
ufahamu wa lugha maalumu, ni wazi kuwa waandishi hawa wamesaidia pia katika
ufundishaji wa Kiswahili. Kwa mfano, mwandishi wa makala hii aliitumia kazi ya
Ken Walibora ya Ndoto ya Amerika (2001) pamoja na riwaya ya Tumaini (2006)
ya Clara Momanyi katika ufundishaji wa Kiswahili kwa wanafunzi wa kigeni
nchini Marekani. Walimu wengi wa Kiswahili nchini Marekani na maeneo
mengine ughaibuni hutumia kazi mbalimbali za fasihi katika madarasa yao,
hasa kwa wanafunzi wa viwango vya pili na tatu. Ingawa kumekuwa na mjadala
wa muda mrefu miongoni mwa wataalamu kuhusu umuhimu wa fasihi katika
ufundishaji wa lugha, kinachoaminika ni kuwa fasihi husaidia si katika kipengele
cha kuwapa wanafunzi fursa nzuri ya kuelewa mengi zaidi kuhusu utamaduni
wa jamii tu, bali vilevile kuwafahamisha namna mwafaka za kuelezea hisia mba-
limbali. Aidha, fasihi hukuza zaidi matumizi yao ya miundo mbalimbali ya
kiisimu wanayoisoma. Hali hii haibainiki katika mafunzo kwa wanafunzi wa
kigeni tu. Hata katika muktadha wa Kiswahili hapa Afrika Mashariki, usomaji wa
kazi nyingi za kubuni huwasaidia wanafunzi kupanua msamiati wao wa lugha
pamoja na miundo tofauti ya matumizi ya lugha hiyo.
Mwandishi anaisifu lugha ya Kiswahili kwa sababu ya uzuri wake na kusema kuwa
wasioifahamu atawaelimisha kwa njia ya kuimba ili kuisifu lugha hii adhimu.
230 E. S. MOHOCHI
Aidha, anaeleza jinsi ambavyo imemkuza tangu akiwa mtoto hadi sasa ambapo
anaizungumza kwa urahisi katika utu uzima. Inamwezesha sasa kutekeleza shugh-
uli zake zote popote aendapo. Kwa sababu hiyo anailinganisha na manukato.
Labda muhimu zaidi ni kibwagizo kisemacho ‘titile mama litamu, jingine halishi
hamu’. Tukitafakari kauli hii tunaona kuwa kwa kumithilisha lugha ya Kiswahili
na titi, Robert anaonesha umuhimu wake kwetu. Hakuna mtu anayeweza
kupinga, kwa mafanikio, umuhimu wa titi la mama kwa mtoto. Ingawa wapo
ambao siku hizi hawataki kuwapa wana wao titi, ati kwa sababu kunyonywa
kutayaharibu matiti, wataalamu wamesema kuwa hakuna kiwezacho kuchukua
nafasi ya maziwa ya mama kwa mtoto. Isitoshe, twaweza kuangalia uamuzi wa
kutumiwa kwa mfano wa mbwa kwa mapana zaidi. Katika jamii ya wanyama,
mbwa hana hadhi kubwa sana. Wapo wanyama wanaoheshimiwa zaidi, lakini
kwa mwana mbwa hakuna jingine liwezalo kuchukua mahali pa titi la mama.
Vivyo hivyo, japo zipo lugha nyingine, tukumbuke kuwa ni lugha zetu tu
ambazo zinaweza kutimiza hamu. Kwa maana hiyo, kwetu sisi Kiswahili ndiyo
lugha tuwezayo kuitumia kutekeleza shughuli zetu na kuleta maendeleo. Inatubidi
kuiendeleza ili vizazi vijavyo viweze kuendelea kulinyonya titi la mama na kupata
uhondo wake.
Wallah Bin Wallah katika shairi lake “Tutukuze Kiswahii”, linalopatikana katika
diwani ya Malenga wa Ziwa Kuu (1988) ameijadili nafasi muhimu ya Kiswahili
katika jamii. Anatanguliza kwa kusema kuwa atakayoyasema ni ya ukweli. Mion-
goni mwa mambo mengi anayoyaeleza ni kuwa: lugha ni kitu kinachotoa
heshima kwa nchi; ni muhimu kwa watu wote, wakubwa kwa wadogo; ukosefu
wake waweza kukwamisha mambo mengi; Mungu alitubariki Afrika Mashariki
kutupa Kiswahili hivyo tukisambaze, huku na ughaibuni; ni muhimu kisemwe na
kutumiwa kwa ufasaha unaostahili, na juhudi za urekebishaji wa pale palipohari-
bika zifanywe kwa umoja. Kibwagizo chasema ‘Kiswahili kitukuzwe, kwani lugha
ya Taifa’. Shairi hili lilitungwa katika muktadha wa Kenya ambapo wakati huo
Kiwahili kilikuwa ni lugha ya taifa tu. Hata hivyo, yasemwayo na mshairi yanahusu
eneo letu zima la Afrika Mashariki lililo kitovu cha lugha hii. Ni wajibu wetu kuki-
tukuza Kiswahili. Shairi hili lilikuza sana lugha ya Kiswahili na kuathiri msimamo wa
watu kuhusu Kiswahili. Hili lilibainika zaidi wakati idhaa ya redio na runinga ya KBC
(Kenya Broadcasting Corporation) ilipolitumia kutanguliza vipindi vya Lugha Yetu.
Shairi hili liliimbwa kwa mahadhi mazuri na kufahamika kote nchini.
Mwandishi mwingine katika kundi hili ni Ken Walibora. Katika riwaya yake ya
Siku Njema (1996) lugha ya Kiswahili imepewa nafasi muhimu sana na mwandishi.
Awali ya yote, majina ya wahusika wake wengi ni majina yanayohusiana na Uswa-
hili. Haya ni pamoja na: Zainabu, Msanifu Kombo, Salim, Vumilia Binti Abdalla,
Selemani, Bakari, Rashidi, Amina, Zawadi, na Athman. Pia, jina la mhusika mkuu,
lililofahamika zaidi ya hilo Msanifu, la Kongowea Mswahili ni moja kati ya
majina hayo. Pili, amewasawiri baadhi ya wahusika wake kama watu ambao
wanaipenda na kuithamini sana lugha ya Kiswahili. Kwa mfano, Zainabu
Makame, mama yake Kongowea. Mama huyu alikuwa mwimbaji na mtunzi
EASTERN AFRICAN LITERARY AND CULTURAL STUDIES 231
babake, Juma Mukosi, ndiye Amuj Isokum, mwandishi wa diwani maarufu ya Sauti
ya Bara, ambayo aliipenda sana mamake na yeye mwenyewe, na iliyokuwa inafun-
dishwa kwenye shule ya kina Alice na mwalimu Nambuye Pilipili. Kutokana na sifa
hizo za wazazi wake, hasa kuhusiana na lugha ya Kiswahili, si ajabu kuwa Kongo-
wea naye aliibuka kukipenda na kukienzi Kiswahili kweli kweli.
Mwandishi ametumia mifano mingi kuonyesha mapenzi aliyokuwa nayo Kon-
gowea kwa lugha ya Kiswahili; mapenzi ambayo yalisababisha yeye kuja kuitwa
Mswahili, jina ambalo lilikuwa maarufu na kuchukua nafasi ya jina lake halisi,
Msanifu Kombo. Mapenzi ya Msanifu Kombo kwa lugha ya Kiswahili yalianza
mapema sana katika maisha yake. Mwenyewe anasema hivi, “Nilipojua kusoma
nilijikusuru kuzisoma tungo adhimu za Kiswahili nilizopata kukumbana nazo, vita-
buni na magazetini” (uk. 5). Katika ukurasa unaofuata anasema wazi, “Waama,
mambo yanayohusiana na Kiswahili na Uswahili yamenitamia kwa miaka mingi.
Niliwahusudu wazee wengi wa Tanga kwa umahiri wao katika Kiswahili na
kunga zake za ushairi.” Kwa sababu hiyo, Msanifu alipenda kukaa na wazee mba-
limbali ili aweze kupata maarifa kutoka kwao. Vilevile, alipendelea kusoma vitabu
mbalimbali vya Kiswahili katika maktaba ya umma ya Tanga, jambo analodai lilim-
wezesha kukijua Kiswahili vizuri zaidi ya hirimu zake wengine.
Akiwa katika shule ya msingi, alitunga hadithi “Kongowea Mswahili” ambayo
ilichukua nafasi ya kwanza katika mashindano ya shule za msingi mkoani
Tanga. Huo ndio ulikuwa mwanzo wa jina lake la Kongowea Mswahili akiwa
darasa la sita. Kutokana na weledi alioonyesha shuleni, hasa katika somo la Kiswa-
hili, wenzake walianza kumuita bingwa wa Kiswahili, ingawa yeye binafsi haku-
jiona ama kujichukulia kuwa bingwa. Kongowea alipoletewa habari kuwa
anaitwa na mamake aliyekuwa katika hali mahututi, alikuwa kwenye maktaba
ya umma akisoma Kamusi ya Kiswahili iliyoandikwa na Dr. Ludwig Krapf (uk. 11-12).
Halikadhalika, baada ya kusoma nakala ya gazeti iliyokuwa na habari kuhusu
kifo na mazishi ya marehemu mamake, Kongowea anatoa kauli inayodhihirisha
kuwa hakipendi tu Kiswahili kwa sababu alikijua, bali alikithamini kiasi cha kujali
ni jinsi gani kinavyotumiwa na wengine. Anamsifu mwandishi wa habari ile kwa
sababu ya matumizi mufti ya lugha ya Kiswahili, jambo ambalo anakiri ni nadra
sana katika magazeti mengi ya Kiswahili. Anasema kuwa “waandishi wa habari
na vitabu wanayo dhima ya kuwafundisha wasomaji wao ufasaha na umbuji uta-
kikanao … Mtu anayepima ubora wa Kiswahili kutokana na kile akisomacho katika
magazeti yetu hana budi kukihukumu kuwa lugha dufu na pungufu” (uk. 17). Ken
Walibora amejitokeza na kujibainisha kuwa ni mwandishi anayekithamini Kiswahili
na kuhimiza hali ya kukiendeleza kwa kufuata kaida na kanuni mwafaka za lugha
hii adhimu kwa kupitia kwa kauli za wahusika wake mbalimbali kama vile Kongo-
wea katika Siku Njema, na Amani katika Kidagaa Kimemwozea. Aidha, yeye amefa-
nya kazi katika sekta ya habari kwa muda mrefu, kwa hivyo hali anayoizungumzia
hapa anaielewa barabara.
Kongowea Mswahili pia alikuwa mtunzi wa mashairi ya Kiswahili. Baada ya
mazungumzo ya muda mrefu na Mjomba wake, Kitwana Makame, kuhusu
EASTERN AFRICAN LITERARY AND CULTURAL STUDIES 233
Ulipofika wakati wake kutoka Tanga, miongoni mwa vitu vichache alivyovibeba
katika mkoba wake ni vitabu vitatu: cha hadithi kilichoitwa Shani Kubwa; diwani
ya Sauti ya Bara, pamoja na kamusi ya Kiwahili. Uamuzi huu ni dhihirisho
kuhusu nafasi ya Kiswahili katika maisha yake. Alipoishi na Rashid mjini
Mombasa, alipenda kutumia muda wake wa ziada kwenda katika maktaba ya
umma kusoma vitabu. Aidha, aliandika hadithi fupi na mashairi, baadhi ambayo
yalitokea katika magazeti ya Baraza na Taifa Leo. “Hapana shaka niliandika mno,
lakini ilikuwa kazi iliyonipa furaha isiyomithilika. Niliipenda. Nilipenda kuchangia,
japo kwa akali ndogo, utukufu wa lugha ya Kiwahili.” (uk. 74).
Alipofika Kitale na kupata makazi katika kasri la Bi Mercy MacDonald, Mswahili
aliendelea kutunga mashairi na kuyapeleka magazetini, na mengi yalisomwa na
watu katika Baraza na Taifa Leo. Hali hii ilichangia umaarufu wake na kujulikana
na watu wengi kama vile mwalimu wa shule alikosomea Alice, Bintiye Bi Mercy.
Mwalimu wa Alice aliomba kuonana naye wakati Alice aliomba msaada wa
kuchambua diwani ya Sauti ya Bara. Mwalimu Nambuye alimwalika Kongowea
Mswahili kuzungumza na wanafunzi wake kuhusu Kiswahili. Awali alisita sana
ama kumsaidia Alice au kwenda shuleni kwao lakini hatimaye, kutokana na
mapenzi yake kwa Kiswahili, akakubali maombi yote mawili. Haya yalifanyika
baada ya shairi lake, “m’baguano” kupata nafasi ya kwanza katika mashindano
ya utunzi wa mashairi nchini Kenya. Kuhusu mwaliko wa kwenda shuleni kutoa
hotuba, alisema hivi, “ … nitakuja. Nitakuja tu kwa sababu ya utukufu wa Kiswa-
hili.” (uk. 120).
Akijiandaa kwa hotuba yake shuleni Kongowea alisoma vitabu vingi, baadhi
akiwa ametoka navyo Tanga na vingine alivyovinunua mjini Kitale. Mwenyewe
anasema kuwa yalikuwa mazoea yake kununua vitabu vya Kiswahili. Ni wangapi
kati ya walimu na wataalamu wengine wa Kiswahili wawezao kusema kuwa
wana mazoea ya aina hiyo? Japo wapo, si wengi sana. Katika hotuba yake, ‘Mata-
tizo yanayoikabili lugha ya Kiswahili’, Mswahili alieleza mengi muhimu kuhusu Kis-
wahili kabla ya mhusika Kazi Kwisha kuivuruga hotuba yake. Kongowea alitaja
wazi uzuri na umuhimu wa Kiswahili kisha akalalamika kuwa, kwa kiasi kikubwa,
ni sisi wenyewe ambao hatuelekei kukitambua, kukithamini na kukiendeleza
kwa dhati Kiswahili. Aliwatambua na kuwasifu wageni kutoka nje, kama vile:
Lambert, Dr. Krapf, F. Johnson, na Prof. Wilfred Whiteley kwa mchango wao
mkubwa katika kutafiti na kuandika mambo mengi kuhusu Kiswahili. Aliwatanaba-
hisha wasikilizaji wake kuwa jukumu la kuiendeleza lugha hii tukufu ni letu sisi
sote, tuwe wa pwani ama wa bara. Analalamika kuwa waandishi wa Kiswahili
hawana soko kubwa kwa sababu watu hawapendi kusoma vitabu vya Kiswahili.
234 E. S. MOHOCHI
Hitimisho
Makala hii imelishughulikia swala la mchango wa waandishi wa kazi za kubuni
katika uendelezaji wa lugha ya Kiswahili kwa kujikita katika nadharia ya ushawishi
wa kijamii. Sehemu ya mwanzo imeeleza dhana ya ushawishi wa kijamii. Kimsingi
238 E. S. MOHOCHI
imebainishwa kuwa katika maisha yetu ya kila siku, kuna hali nyingi za kuathiriana
baina ya wanajamii. Wapo wanaotuathiri na tunaowaathiri. Mtagusano wetu ume-
jengeka kwenye mahusiano ya kuathiriana. Mjadala wa nafasi ya waandishi katika
jamii, hasa waandishi wa fasihi, umeshughulikiwa. Kwa jumla, imefafanuliwa kuwa
maandishi na waandishi huchangia sana katika maendeleo ya jamii. Hii ni kwa
sababu waandishi huyaweka maarifa katika hali ya kuweza kuwafikia watu
wengi zaidi na hivyo kutoa elimu na burudani miongoni mwa mambo mengine.
Mjadala uliegemea pia mchango wa waandishi wa kazi za kubuni katika uende-
lezaji wa Kiswahili. Makala imejikita katika uchanganuzi wa kazi za waandishi
watatu ili kudhihirisha jinsi waandishi wanavyochangia katika kuikuza lugha.
Katika kulishughulikia hili, makala imezingatia aina mbalimbali za mchango wao
kama waandishi wa kazi za fasihi ya Kiswahili.
Sehemu ya mwisho imejadili maoni ya walimu na wanafunzi wa Kiswahili kuhusu
mchango wa waandishi wa kazi za kubuni katika uendelezaji wa Kiswahili. Imebai-
nika kuwa waandishi wa kazi za kubuni wana umaarufu katika jamii, ambao huwa-
fanya kuwa na ushawishi mkubwa sana. Kutokana na hilo, wana uwezo wa kuathiri
watu wengi. Wanapotokea kuwa watetezi wakubwa wa lugha ya Kiswahili na kuji-
husisha katika uandishi wa kazi katika lugha hiyo na wanaposhiriki katika shughuli
nyingine za kuiendeleza, wanakuwa mawakala muhimu wa lugha yenyewe.
Marejeleo
Abdulaziz, H.M. (1979). Muyaka: 19th Century Popular Swahili Poetry. Nairobi: EAEP.
Aboh, R. (2015). “Talking” Igbo, “Writing” English: Nigerianism in the Concubine, katika A.
Odebunmi & J.T. Mathangwane (wh.), Essays on Language, Communication and Literature in
Africa. Newcastle-upon-Tyne: Cambridge Scholars Publishing. Iliyopakuliwa kutoka from
https://ebookcentral.proquest.com/lib/rucke-ebooks/detail.action?docID = 4648739
Friedkin, N.E. (1998). A Structural Theory of Social Influence. Cambridge: Cambridge University
Press.
Goldsmith, E.B. (2015). Social Influence and Sustainable Consumption. International Series on
Consumer Science, DOI 10.1007/978-3-319-20738-4_2
Mayhew, L.H. (1997). The New Public: professional communication and the means of social
influence. Cambridge: Cambridge University Press.
Mlamali, M. (1980). Al Inkishafi: Sayyid Bin Ali Bin Nasir. Nairobi: Longman.
Momanyi, C. (2006). Tumaini. Nairobi: Vide-Muwa Punlihsres.
Ngugi Wa T. (1986). Decolonising the mind: the politics of language African literature. Nairobi:
Heinemann Educational Publishers.
Ngugi Wa T. (1992). Petals of Blood. Nairobi: East African Educational Publishers.
Robert, S. (2016). “Titi la Mama”, Katika Jahadhmi’s anthology of Swahili poetry. Iliyorejelewa
kutoka http://www.mwambao.com/mashairi.htm
RUC, 01/09/16
Walibora, K. (1996). Siku Njema. Nairobi: Longhorn Publishers.
Walibora, K. (2001). Ndoto ya Amerika. Nairobi: Sasa Sema Publishers.
Walibora, K. (2016). “Lugha Bora”, Shairi ambalo halijachapishwa.
Wallah, B.W. (1988). “Tutukuze Kiswahili”, katika Malenga wa Ziwa Kuu. Nairobi: Heinemann
Kenya Limited.