You are on page 1of 13

1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

 Log in Register 

 Forums  General Forums  Jamii Intelligence 

Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch


 Ben Zen Tarot ·  Apr 2, 2021

1 of 14 Next  

Ben Zen Tarot


JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #1

Biblia ina Vitabu 73 lakini isiwe Mpaka wakusoma hivyo 73 tu, Canon ya Vitabu 73
iliapitishwa mwaka 382 na Baraza la Maaskofu wa Roma kuna Vitabu Vilipitishwa vikiwa
Havina Sifa E.g (Waebrania) lakini kuna vitabu havikupitishwa Kuwemo ndani ya Biblia
lakini vikiwa na Sifa, mfano Kitabu cha Henoko, Pengine Mababu waliona "Chakuzushi"
lakini ukweli ni Kwamba kiliandika Aibu nyingi.

Henoko anayedhaniwa kuwa alikuwa ndio mwandishi wa kitabu hiki ni Yule mtoto wa
Yaredi na baba wa Metuselah, ambaye akaja kuwa babu wa Nuhu MWANZO 5:21-23, Ni
Moja ya Mtu anayetajwa kuwa na Mwisho wa Ajabu kwani hakufa, bali alitwaliwa
mbinguni YOSHUA BIN SIRA 44:16, WAEBRANIA 11:5. Maswala Kama haya hupaswi kujadili na
Wale wenye Canon Ya Vitabu 66 kwani watakwambia vitabu hivi havifai "Wanaviita
Apokrifa" Wasijue Hata Baadhi ya Sura za Kitabu cha Zaburi ni Apokrifa na katika Biblia yao
zimo.

Hiki kitabu cha Henoko Hukataliwa na Kanisa Katoliki la Magharibi (Latin Church) kwa
Sababu zake za Msingi Moja ya Sababu ni Kitabu Kukosa Jina la Mwandishi hakika, Lakini
kanisa Katoliki la Mashari la Ethiopia (Orthodox) katika Orodha yao wanakitumia kama
Kitabu cha Muhimu sana. Ni kama Wayahudi wanavyokitumia kitabu kinachoitwa YASHARI
au JASHAR kinachotajwa 2SAMWELI 1:18, Vitabu hivi vina mambo fulani ya kipekee ambayo
wataalamu husema ni siri.

Kitabu Cha Henoko Hutajwa kwa hypingwa Vikali kwa sababu Ndio huonyesha Mtu
JamiiForums uses cookies
mweupe alipata to helpPia
wapi Ujuzi, personalise
huonyeshacontent, tailorcha
Chanzo yourMapepo
experience
naand to keep you logged in if
Wanefili.
you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.
Ukisoma Kitabu cha HENOKO 6:1-8 ni sawa na Ukisoma MWANZO 6:1-8 lakini kuna utofauti
wa Stori za malaika zaidi, Inaonekana katika zama za YAREDI babaye na HENOKO kuna
 Accept
malaika
Learn more…
kama 200 walikubaliana kushuka duniani na Kujichanganya na wanadamu, hapo

https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 1/13
1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

ndipo ambapo YUDA alinakili maelezo ya YUDA 1:6 Malaika walipoona kuna mabinti wa
wanadamu wanavutia/Wazuri MWANZO 6:2 Ndipo wakashauriana "Mwaonaje Tujitwalie
tuwaoe, tuzae nao watoto?" Malaika Kiongozi aliyeitwa SAMYAZA akahofia Labda malaika
wenzie wanaweza Kumsaliti katika mpango huu, Akahimiza malaika kuapa, Wakaapa
kutekeleza. (Henoko 7:3-6)

Kitabu Cha Henoko kinawataja kabisa kwa Majina Viongozi wa Malaika hao waliokuwa
katika Mlima HERMON kwamba ni SEMIAZAZ, ARAKIBA, RAMEEL, KOKABIEL, TAMIEL, RAMIEL,
DANEL, EZEQEEL, BARAQIJAL, ASAEL, ARMAROS, BATAREL, ANANEL, ZAQIEL, SAMSAPEEL, SATAREL,
TUREL, JOMJAEL, SARIEL.

Ikumbukwe hawa hawakuwa malaika Watiifu kwa Mungu, Ni wazi kuwa walikuwa sehemu
Katika wale Walioasi pamoja na shetani, Katika MWANZO 6:2-4 Imewataja kama "WANA
WA MUNGU" hili jina lisikuchanganye maana malaika wote huitwa wana wa Mungu ndio
maana hata Biblia ya asili ya Kiyunani imewaita malaika "ANGELUS ES DEUS" ikimaanisha
malaika wa Mungu No matter Watiifu au Sivyo, Sasa mstari wa 4 katika MWANZO 6
unasema "Basi walikuwepo Wanefili duniani(NEPHILIM THE FALLEN ANGELS) hapo jiulize kwa
nini aseme "DUNIANI" ni kwasababu hapakuwa mahali pao pa asili (2Petro 2:4,YUDA 1:6) Ni
lazima waliyaacha makao yao...

Kitabu cha HENOKO 7:1-6 tunaona haya yafuatayo, Malaika wale 200 Wakiongoza na
SEMJAZA baada ya Kiapo, wanaoa mabinti wanadamu Na Kuwapa Mimba, Hawakuishia
hapo, Katika Sura ya 7 Mstari wa 10 tunaona Malaika hawa waliwafundisha binadamu
Uchawi "sorcery" Wakafundisha Orodha ya Maneno ya Kufufua wafu "incantations"
Wakawafundisha Jinsi ya Kutengeneza Dawa za Kuwatibu kutumia Mitishamba
(pharmacology).

Ilipofika kipindi cha wale mabinti kuzaa Katika sura ya 7:11-14 tunaambiwa Walizaliwa
Viumbe wakubwa kupita hata Binadamu na Malaika (Giants), Walizaliwa wengi Mpaka
Binadamu walichoka Kuwahudumia chakula, Wakaanza kula Wanyama, Ndege na
Samaki, Baadae wakaanza kuwala Binadamu, na Mwisho wakalana wao kwa Wao.

Basi katika Sura ya 8 tunaona Malaika AZAZEL anawaonea huruma Binadamu, Anaanza
kuwafundisha Kutengeneza Silaha, Mapanga (Swords) , Visu, Ngao na Ngao za Vifuani
(BREASTPLATED) hapa ndipo zana za chuma zilipogunduliwa (MWANZO 4:22) TUBALI-KAINI
akiwa wa kwanza kuchukua Ujuzi.

Kupitia Malaika Azazel ndipo Binadamu alipojua Kupigana Vita, Malaika hawakuishia
hapo, Malaika hawa ndio Walifundisha Dada zetu kuvaa Vikuku na Bangili (BRACELETS) Pia
wakafundisha dada zetu kupaka Rangi Kope (BEAUTIFYING OF EYELIDS) na hapa ndipo
Dhambi ya Kuzini kwa matamanio ilianza

Malaika waliendelea Kutoa siri nyingi na Kumpa Binadamu uwezo Ulioshindikana, Kila

https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 2/13
1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

malaika alikuwa na Kitengo chake.

Malaika aliyeitwa SEMJAZA huyu aliwafundisha Binadamu kumiliki Nguvu za Maajabu


kufanya Mambo makubwa, Pia Kutumia Mizizi ya Miti kama Tiba, Kemia Kiujumla. Malaika
ARMAROS alifundisha jinsi ya Kutatua Tatizo litokanalo na Uchawi wa mtu mwingine.
Malaika BARAQIEL huyu aliwafundisha binadamu elimu ya vitu vya Angani "ASTROLOGY"
Malaika kwa jina la KOKABEL akawafundisha binadamu elimu ya Anga ihusuyo mipaka ya
Nyota na maumbo yake "CONSTELLATION" Malaika EZEQEEL akawafundisha Binadamu Juu
ya Mawingu. Malaika ARAQIEL akawafundisha Alama za Kidunia (zodiac elemental
rulerships) ambazo tunaziita Libra, Virgo, Capricon nakadhalika. Malaika SHAMSIEL
akafundisha alama za Jua Na Malaika SARIEL akawapa Kozi za Elimu ya Mwezini.

Kwahiyo Ujuzi wa Binadamu na Mambo machafu yalianzia Juu ya Hawa malaika Bila Ujio
wao Binadamu Angekuwa "Kilaza Mmoja hivi" Basi Baadhi ya Malaika Watiifu walienda
Kumuelezea Mungu juu ya Uchafu uliofanywa na malaika duniani, Hata Mungu aliona
wameipa Mbingu aibu, na Alishindwa Kuwasamehe na aliwafunga vifungo vya milele chini
ya Giza wakingojea hukumu.

Catholic theological reflection.

Wanateolojia wa kanisa husema wazi kuwa inawezekana huu ulikuwa ni mpango wa


Shetani kuharibu Mpango wa Mungu wa MWANZO 3:15 kwa Sababu Mungu alisema
Mkombozi wa Wanadamu atakuwa binadamu Pure na si Malaika na Atazaliwa Pasipo
Dhambi, Na Atazaliwa na Mwanamke, Basi Shetani alipanga kuharibu Vinasaba (Gene) za
Binadamu kwa kuzichanganya na za Malaika Basi basi Kuzaliwa Kwa Mkombozi
kungeshindikana.

Lakini Mungu anajua Zaidi (An omniscient) Ni zaidi ya Malaika (ISAYA 46:9-10) anajua
Mwanzo na Mwisho, Hivyo ndio maana Alifuta Kizazi cha Enzi zakina Nuhu kwa Gharika na
Kubakiza Wanadamu 8 tu.

Sent using Jamii Forums mobile app


kibombonya, mwandende, Adolph hitler jr and 72 others

keisangora
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #2

https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 3/13
1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

Dakika za mwisho kila kitu kitawekwa wazi

Rabbon, Best Tanzania, digba sowey and 16 others

plan z
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #3

Hebu naomba hicho kitabu kama unacho nikisome mwenyewe. Tuma pdf yake humu

whiteskunk, Cleophace makuli, Bill and 4 others

Ben Zen Tarot


JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #4

plan z said: 

Hebu naomba hicho kitabu kama unacho nikisome mwenyewe. Tuma pdf yake humu

https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 4/13
1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

hans jf and ndege JOHN

mikogo mia
M Member

Apr 2, 2021  #5

plan z said: 

Hebu naomba hicho kitabu kama unacho nikisome mwenyewe. Tuma pdf yake humu

Bora hivyo
Icho hapo

Anigrain
Sent using Jamii Forums mobile app
JF-Expert Member

https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 5/13
1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

Apr 2, 2021  #6

"Basi Baadhi ya Malaika Watiifu walienda Kumuelezea Mungu juu ya Uchafu uliofanywa na
malaika duniani" kwahiyo unataka kusema bila malaika kumwambia Mungu asingejua
matendo ya hao malaika?

"Lakini Mungu anajua Zaidi (AN OMNISCIENT) Ni zaidi ya Malaika (ISAYA 46:9-10) anajua
Mwanzo na Mwisho, Hivyo ndio maana Alifuta Kizazi cha Enzi zakina Nuhu kwa Gharika na
Kubakiza Wanadamu 8 tu"

Kupitia hizo paragraph 2 inaonekana kama kuna ukomo wa kuona au kujua mambo Kwa
Mungu, kama anajua zaidi hadi akafuta kizazi cha Nuhu nazani lengo lilikuwa ni kuondoa
kizazi kiovu cha Nuhu na kuleta kizazi kizuri Ila cha ajabu hiki kizazi ndio kibaya kuliko ata
cha Nuhu hivo sidhani kama alijua na hiki kizazi kitakuwa hivi

Kuendelea kumuacha shetani uraiani ili binadamu apambane nae mwenyewe ni Sawa na
kujitekenya mwenyewe na kucheka mwenyewe, kama Baba huwezi kuwatakia mema
watoto wako Kwa kuwaweka chumba kimoja na Nyoka, kuendelea kutuweka zizi moja na
shetani na kutegemea tutakuwa tofauti na kina Nuhu inabidi uwe na akili za Wanyonge
kuamini hili, Kamata shetani funga huko dunia iwe sehemu salama easy tu

Jero_pesa, Jack Daniel, Cicadulina and 51 others

Surya
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #7

Maandiko ya Biblia yanajitosheleza kabisa, na ndio Mungu kataka tusome hayo tu.

Nje na hapo hakuna hekima tena, labda ukajifunze uchawi tu huko nje ya biblia.

Jabrone, Roy Logan, Fabolous and 13 others

kopites
JF-Expert Member

https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 6/13
1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

Apr 2, 2021  #8

Ben Zen Tarot said: 

Biblia ina Vitabu 73 lakini isiwe Mpaka wakusoma hivyo 73 tu, Canon ya Vitabu 73 iliapitishwa
mwaka 382 na Baraza la Maaskofu wa Roma kuna Vitabu Vilipitishwa vikiwa Havina Sifa E.g
(Waebrania) lakini kuna vitabu havikupitishwa Kuwemo ndani ya Biblia lakini vikiwa na Sifa, mfano
Kitabu cha Henoko, Pengine Mababu waliona "Chakuzushi" lakinj ukweli ni Kwamba kiliandika Aibu
nyingi....

Nimekisoma chote hicho kitabu kina siri nyingi sana ambazo hazijulikani

Prince Kesh Jr, fungi06, mtu chake and 2 others

ancillary
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #9

Ben Zen Tarot said: 

Icho hapo View attachment 1740892

Sent using Jamii Forums mobile app

Nimekuja speed nikajua umetuwekea tupate uhondo

fungi06 and Mpinzire

Amigoh
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #10

Ben Zen Tarot said: 

Biblia ina Vitabu 73 lakini isiwe Mpaka wakusoma hivyo 73 tu, Canon ya Vitabu 73 iliapitishwa
mwaka 382 na Baraza la Maaskofu wa Roma kuna Vitabu Vilipitishwa vikiwa Havina Sifa E.g
(Waebrania) lakini kuna vitabu havikupitishwa Kuwemo ndani ya Biblia lakini vikiwa na Sifa, mfano

https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 7/13
1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

Kitabu cha Henoko, Pengine Mababu waliona "Chakuzushi" lakinj ukweli ni Kwamba kiliandika Aibu
nyingi...

Niliwahi kupata dokezo kidogo wa hiki kitabu kupitia jarida moja la mashahidi wa yehova..
itabidi nikitafute nikipitie aisee.
mtu chake, MUME MASKINI and crusader_jr

Kimwakaleli
K JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #11

Ben Zen Tarot said: 

Biblia ina Vitabu 73 lakini isiwe Mpaka wakusoma hivyo 73 tu, Canon ya Vitabu 73 iliapitishwa
mwaka 382 na Baraza la Maaskofu wa Roma kuna Vitabu Vilipitishwa vikiwa Havina Sifa E.g
(Waebrania) lakini kuna vitabu havikupitishwa Kuwemo ndani ya Biblia lakini vikiwa na Sifa, mfano
Kitabu cha Henoko, Pengine Mababu waliona "Chakuzushi" lakinj ukweli ni Kwamba kiliandika Aibu
nyingi....

Aisee umejitahidi mkuu!

whiteskunk, Prince Kesh Jr and Ben Zen Tarot

Lupweko
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #12

Ndio maana ya imani. Huwezi kulazimisha watu wengine waamini katika maandiko fulani,
lakini inawezekana kwako wewe kuamini maandiko hayo. Kama ni kweli unayoyasema,
basi RC waliona hayo maandiko hayaendani na imani yao.

Lakini RC hawajamzuia mtu kuyaamini. Cha ajabu watu wanataka wengine waamini
imani fulani wakati wapo huru kuifuata, na hata katiba za nchi nyingi zinaruhusu tu

whiteskunk, BabaDesi, Fabolous and 4 others

https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 8/13
1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

Shadow7
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #13

Ahsante

zitto junior
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #14

Surya said: 

Maandiko ya Biblia yanajitosheleza kabisa, na ndio Mungu kataka tusome hayo tu.

Nje na hapo hakuna hekima tena, labda ukajifunze uchawi tu huko nje ya biblia.

Hiko kitabu kinatumika na Ethiopian Orthodox ambalo ndio kanisa la Kwanza Afrika hata
kabla RC haijafikiriwa kuanza.

Je unaona nani yupo sahihi hapo? Au inakua halali pale tu mzungu akikiweka kwenye
biblia?

Mfano Wimbo ulio bora una changamoto zote kma book of Enoch ila hakijatolewa and
more so hta makanisani hakifundishwi regularly!! But kingekua nje ya Biblia kama naona
jinsi mngekikejeli.

Mwl Athumani Ramadhani, keisangora, Proved and 11 others

Surya
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #15

zitto junior said: 

Hiko kitabu kinatumika na Ethiopian Orthodox ambalo ndio kanisa la Kwanza Afrika hata kabla RC
haijafikiriwa kuanza.

https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 9/13
1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

Je unaona nani yupo sahihi hapo? Au inakua halali pale tu mzungu akikiweka kwenye biblia?

Mfano Wimbo ulio bora una changamoto zote kma book of Enoch ila hakijatolewa and more so hta
makanisani hakifundishwi regularly!! But kingekua nje ya Biblia kama naona jinsi mngekikejeli

Mimi naujua umuhimu wa agano la kale na muhubiri anatakiwa kulitumia vipi agano la
kale kufundisha neno la Mungu,
Agano jipya pia.

Sasa kama kuna kitu cha muhimu mwanadamu kukijua na hakipo ndani ya biblia kiseme.

Kwasababu biblia inasema laiti kama biblia ingeandika kila alilolifanya Yesu kipindi chake
isinge wezekana ?
Yohana 21:25
[25]Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani
hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa.

Fabolous, Proved, Airo and 3 others

zitto junior
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #16

Surya said: 

Mimi naujua umuhimu wa agano la kale na muhubiri anatakiwa kulitumia vipi agano la kale
kufundisha neno la Mungu,
Agano jipya pia.

Sasa kama kuna kitu cha muhimu mwanadamu kukijua na hakipo ndani ya biblia kiseme.

Kwasababu biblia inasema laiti kama biblia ingeandika


Click kila alilolifanya Yesu kipindi chake isinge
to expand...

Kasome Yuda 6 na 14-15 alafu uniambie ilikua quoted kutoka kitabu gani cha agano la
kale then ukifaham naomba ukaulize kwanini mitume walikisoma alafu sisi tukataliwe?

Mwl Athumani Ramadhani, MTAZAMO, Prince Kesh Jr and 5 others

https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 10/13
1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

Surya
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #17

zitto junior said: 

Kasome Yuda 6 na 14-15 alafu uniambie ilikua quoted kutoka kitabu gani cha agano la kale then
ukifaham naomba ukaulize kwanini mitume walikisoma alafu sisi tukataliwe?

Nikasome wapi. ?

zitto junior
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #18

Surya said: 

Nikasome wapi. ?

Agano jipya.... Yuda mstari wa 6 na 14-15 then unipe mrejesho kuendana na nlichouliza
hapo juu

Mwl Athumani Ramadhani, Amani bm 150 and mtu chake

Surya
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #19

zitto junior said: 

Agano jipya.... Yuda mstari wa 6 na 14-15 then unipe mrejesho kuendana na nlichouliza hapo juu

Nimesoma kitabu hicho cha Yuda.

Lakini point yangu itabaki pale pale, ni mafundisho yapi ya Henoko unayoyalilia wewe
ukitaka yawekwe kwenye biblia.
https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 11/13
1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

Manabii wa zamani walitoa unabii kuwaonya watu wa kipindi kile, si henoko peke yake
alifanya hivo, wapo manabii wengi tu.

Lakini swali linakuja wewe uliyesoma kitabu cha henoko unanizidi nini mimi ambae
sijakisoma. ?

Na kama waliounganisha vitatu vilivyounda Biblia waliona hakifai Roho mtakatifu


aliwaonesha kuwa kimechakachuliwa ? Au si cha muhimu.
Utalazimisha kiwepo kwenye Biblia ?

Kama henoko anamafundisho muhimu sana, tuambie.


Maana mimi najua hata vitabu vya Solomon si vyote vilichukuliwa na kuwekwa kwenye
biblia.

lekumok, Central systemer, Fabolous and 8 others

Surya
JF-Expert Member

Apr 2, 2021  #20

zitto junior said: 

Agano jipya.... Yuda mstari wa 6 na 14-15 then unipe mrejesho kuendana na nlichouliza hapo juu

Pia Mungu anaweza taka wewe ukakisome hicho kitabu.


Ndio sikatai

Lakini usiseme biblia inamapungufu.


Ilivyo ndivyo Mungu ametaka biblia iwe.

Roy Logan, mashinetata and Frank Wanjiru

1 of 14 Next   You must log in or register to reply here.

Similar Discussions

Matukio yanayoonesha uongo kwenye vitabu vya dini


Started by The Evil Genius · Oct 29, 2022 · Replies: 461

https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 12/13
1/5/23, 11:09 AM Sababu za kufichwa kwa kitabu cha Enoch | JamiiForums

Jamii Intelligence

Mungu aliwaadhibu Wanadamu kwa kosa lililoletwa na Malaika wake


Started by FabNXTzqEtcgazfbjjfo · Apr 4, 2022 · Replies: 361
Jamii Intelligence

Amka Muafrika
Started by Mtuache · Oct 6, 2022 · Replies: 18
Jamii Intelligence

Ujuzi dhidi ya Binadamu katika kujifunza


Started by let the caged bird sings · Sunday at 4:57 PM · Replies: 1
Jamii Intelligence

M Hivi ni kwanini Walokole wengi wanamtukana shetani?


Started by mimiamadiwenani · Dec 19, 2022 · Replies: 44
Habari na Hoja mchanganyiko

Share:      

 Forums  General Forums  Jamii Intelligence 

Contact us | Terms | Privacy Policy | Help

https://www.jamiiforums.com/threads/sababu-za-kufichwa-kwa-kitabu-cha-enoch.1854578/ 13/13

You might also like