You are on page 1of 69

USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

PASTOR ESKAKA CHAULA 1


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

HAKIMILIKI

Hakimiliki @ Pastor ESKAKA CHAULA

Simu: +255 (0) 718578313

Baruapepe: chaulaeskakaa@gmail.com

Instagram: pastoreskakachaula

Haki zote zipo chini ya Pastor Eskaka Chaula

Huruhusiwi, kunakili, kurudufu au kutumia sehemu ya kitabu hiki bila


idhini ya mwandishi, Kufanya hivyo itakuwa ni ukiukwaji wa haki za
mwandishi. Isipokuwa unaweza kushirikisha kwa kutumia watu wengine
pekee.

Unaweza kuchukua sehemu ndogo ya kitabu hiki kwa ajili ya nukuu na


mafundisho.

@2024.

PASTOR ESKAKA CHAULA 2


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

YALIYOMO
UTANGULIZI ................................................................. 5

PORNOGRAFIA NI NINI? ............................................. 8

KWANINI WATU HUANZA KUTAZAMA PICHA ZA


NGONO ....................................................................... 10

MADHARA YA UTAZAMAJI WA PICHA ZA NGONO17

PUNYETO NI NINI? .................................................... 20

MAMBO MENGINE YA KUJUA KUHUSU PUNYETO


[MASTERBATION] NA KUTAZAMA PICHA ZA NGONO
....................................................................................... 26

MADHARA YA PUNYETO NA KUTAZAMA PONOGRAFIA


....................................................................................... 30

MADHARA YA PUNYETO KWENYE AFYA YA UZAZI


[KIMWILI] ..................................................................... 36

MADHARA YA KUTAZAMA PICHA ZA NGONO NA


KUJICHUA KIROHO ................................................... 38

NATOKAJE KWENYE KUTAZAMA PICHA ZA NGONO NA


KUJICHUA. ................................................................... 43

PASTOR ESKAKA CHAULA 3


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

KWANINI WATU WENGI WANAOMBEWA NA


KUFUNGULIWA KUTOKA KWENYE PEPO LA
PORNOGRAPHIA NA KUJICHUA LAKINI WANARUDI
TENA BAADA YA MUDA. .......................................... 50

UFANYEJE KUTOKA JUMLA KWA UNAYE ANGUKA


ANGUKA? .................................................................... 55

KILIO CHA KIZAZI CHANGU! .................................. 58

NINI KIFANYIKE KUNUSURU HIKI KIZAZI NA


PORNOGRAPHY NA MASTERBATION HASA KWENYE
TAIFA LANGU LA TANZANIA? ................................. 60

MAOMBI YA USHINDI DHIDI YA KUANGALIA


PORNOGRAFIA ........................................................... 62

SHUHUDA ZA BAADHI YA WATU WALIOVUKA JUMLA


KWENYE URAIBU WA UTAZAMAJI WA PICHA ZA
NGONO NA KUJICHUA ............................................ 64

PASTOR ESKAKA CHAULA 4


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

UTANGULIZI
Kijana mmoja alinijia huku akiwa amepoteza tumaini la kushinda jumla
uraibu na kifungo cha uraibu wa ngono. Historia yake kama ilivyo
maelezo yake alianza kusema;

Nikiwa shule ya msingi siku moja niliona marafiki zangu wakiwa na simu
na ni kama kuna kitu wanaangalia kwa shauku huku wakikifurahia. Na nje
ya matamanio [curiosity] ya kibinadamu nikatamani nikatazame nini
wanatazama, bahati mbaya nilipofika walizima simu wakaficha, mmoja
wao akanambia wewe huwa unasema umeokoka, sasa wenzio
wanaangalia watu wanafanya mapenzi.

Niliondoka japo kishingo upande, nilikuwa sijawahi kulala na mwanamke


wala kuona video za watu wakifanya tendo la ndoa, cha kushangaza baada
ya tukio lile shauku na kiu ya kuona watu wakizini iliingia ndani yangu.
Siku moja nikiwa nyumbani nikishika simu ya kaka yangu, nilipoenda
kwenye gallery nikakuta video za watu wapo uchi, nikakumbuka lile
jambo la shuleni, nikadhamiria kuhakikisha naziangalia bila kaka kujua.

Kweli nilifanikiwa kuangalia siku moja kwa muda mrefu maana kaka
alikuwa nazo nyingi sana, na sikuishia kuangalia tu bali nilijikuta kila
nikiangalia najichezea sehemu za siri mpaka nikafika mshindo na huo ndio
ukawa mwanzo wa maisha ya uraibu [addiction] wa kutazama picha za

PASTOR ESKAKA CHAULA 5


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

ngono na kujichua, hata nilipojaribu kuacha nilishindwa kabisa. Mwisho


wa simulizi.

Mwingine anasimulia kwa masikitiko makubwa, Pastor Eskaka, mimi


nilianza nikiwa chuo kikuu nikajaribu kuacha lakini nikashindwa,
nikaambiwa nikiokoka itaisha lakini hata baada ya kuokoka ni kweli kasi
ilipungua lakini kila baada ya muda flani narudia kutazama picha za ngono
na kujichua, mbaya zaidi mimi nimekuwa nikiwasaidia wengine kutoka
kwenye hilo shimo ila mimi nimenasa baba, kiukweli hakuna mtu anayejua
na anayeweza kuamini kuwa napitia haya ,maana hadi wachungaji
wananiamini imekuwa ni dhambi yangu ya sirini ambayo sijui kama
nitaweza kuitua kabisa.

“Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la


mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na
dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika
yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu” (Waebrania 12:1 Biblia
Takatifu)

Mara zote mtu akiokoka kweli hawezi kufurahia kuishi kwenye uchafu wa
ngono, maana dhamiri yake ni hai na ina mhukumu.

PASTOR ESKAKA CHAULA 6


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

“Nami ninajizoeza katika neno hili niwe na dhamiri isiyo na hatia


mbele za Mungu na mbele ya watu siku zote” (Matendo ya Mitume
24:16 Biblia Takatifu)

Aliyeokoka akinaswa na uchafu huu uishia kujilaumu, kujihukumu,


kujichukia na kujiona hafai mbele za uso wa Mungu.

“Habari mbaya ni kuwa uraibu wa kutazama picha za ngono ni


janga la kidunia, na waamini wengi wamejikuta wakikwama katika
vita hii. Takwimu zinashangaza, inaripotiwa kuwa asilimia 50 ya
wakristo wanaume na Asilimia 35 ya wanawake wakristo
wamekwama katika kuangalia picha za uchi angalau mara moja
kila mwezi” [Pastor Gospel Orji, STRAIGHT TALK ON
PORNOGRAPHY]

Kama nawewe ni mhanga wa jambo hili basi umeshika jawabu la


changamoto yako sasa na Bwana Yesu anakwenda kukusaidia kutoka
jumla kwa msaada wa Roho wa Mungu.

Hakikisha unasoma kitabu hiki mpaka mwisho na unahakikisha


kuna mwingine anapata nakala hii ili tukinusuru kizazi hiki na
agenda ya kuzimu ya kuharibu hatima za watu wakuu wa
Mungu.

PASTOR ESKAKA CHAULA 7


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

PORNOGRAFIA NI NINI?
Neno pornografia linatoka kwenye maneno mawili ya kigiriki:

“prostitute” na “I write” or “I record”. ikimaanisha ni ukahaba kwa njia ya


maandishi au maonesho/picha/video.

Kwa kiswahili kisicho rasmi Pornografia kwa lugha nyepesi ni picha au


video za watu wakifanya ngono au ni picha za watu walio uchi.

[Pornography is the image or picture of people having sex or an immoral


position]

Additionally, pornography is the explicit literary or visual depiction of sexual


subject matter; any display of material of an erotic nature.

Mtumishi wa Mungu Pastor Gospel Orji wa kanisa la DUNAMIS, chini ya


maono ya Dr. Paul & Becky Enenche, ameandika kwa urefu sana kwa
habari ya namna ya kushinda pornographia kwenye kitabu chake cha
"straight talk on pornography". Nimefanya rejea ya baadhi ya vitu
kutokea kwenye kitabu chake nlipokuwa naandika kitabu hiki "ushindi
dhidi ya kujichua na pornografia"

Sasa tuendelee kidogo kuangazia kuhusu pornografia na maana zake kwa


mujibu wa watumishi wa Mungu mbalimbali.

PASTOR ESKAKA CHAULA 8


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Kwa mujibu wa mchungaji Pastor Nick Ifeanyi Thomas, Ponografia ni picha


(inaweza kuwa mchoro, picha au video) yenye kusisimua tamaa ya ngono.
“Pornography are images [Paintings, pictures, and videos] that
stimulate sexual lust”

Utagundua pornografia ni moja kati ya agenda ya kuzimu ya kuamsha


tamaa za kimapenzi nje ya utaratibu wa Mungu ili kuwaingiza watu wengi
kwenye utumwa wa uraibu wa porno, kujichua na maisha ya zinaa.

“Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa


porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata
yatakapoona vema yenyewe” (Wimbo Ulio Bora 2:7 Biblia
Takatifu)

“Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa


porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata
yatakapoona vema yenyewe. (Wimbo Ulio Bora 3:5 Biblia
Takatifu)

Nadhani umeelewa kwa upana kidogo kwa habari ya tafsiri au maana ya


pornografia. Najua unaweza kuwa unajiuliza nini kipo nyuma ya watu
hasa kizazi chetu kupenda kutazama picha za ngono, usiache kufatana
namimi kwenye muendelezo wa somo hili.

PASTOR ESKAKA CHAULA 9


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

KWANINI WATU HUANZA KUTAZAMA PICHA ZA


NGONO
Unaweza kushangaa sana ukiwauliza watu sababu za kwanini wanatazama
picha za uchi. Sababu wanazotoa zingine ni za kusikitisha kabisa. Kuna
wengine hata hawaoni hata shida ya kutazama, wanaona ni jambo la
kawaida kabisaa, yaani hata walio kwenye ndoa bado nao ni wahanga wa
kutazama picha za ngono.

Nakubaliana kabisa na mtumishi wa Mungu Pastor Gospel Orji kutoka


kwenye kitabu cha "straight talk on pornography" baadhi ya sababu za
watu kutazama picha za ngono nimeziainisha hapa chini kwa kuongezea
pia na za kwangu

Shauku [curiosity] ya kutaka kujaribu uzoefu [new


experience] mpya kwenye maisha.

Kuna watu wamejikuta wamenasa kwenye shimo la pornografia baada ya


kujaribu kwa mara moja katika shauku ya kutaka kuona hiki kitu
kinachoitwa picha za ngono kinafananaje! Walipojaribu tu mara moja
mpaka leo wamenasa na hawajui watatokaje hapo.

PASTOR ESKAKA CHAULA 10


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Mara nyingi jambo hili uwakuta vijana walio katika umri wa balehe. Na
wengine walijikuta wananasa baada ya kushawishika na vijana wa umri
wao [peer pressure] kuingia kwenye utazamaji wa picha za ngono.

Ujinga /kukosa maarifa juu ya madhara halisi ya


picha za ngono.

Watu wengi wanao tazama picha za ngono na kuzani ni jambo la kawaida


kwa sababu ya ujinga tu, hawajui madhara halisi kwenye uchumi, kiafya,
kiakili, madhara makubwa kwenye ndoa na mbaya zaidi madhara
makubwa sana kiroho. Bahati mbaya sana ile kwamba hujui madhara ya
pornografia haimaanishi kuwa hayatakupata, kubali ukweli huu utazamaji
wa picha za ngono hauna faida hata moja zaidi ya kukufanya unaswe na
mapepo na kuharibu kila kitu kwenye maisha yako.

Kupata utoshelevu wa kihisia [to get satisfaction


and fulfilment]

Kuna watu wengi wameingia kwenye uraibu huu kwa sababu ya msongo
wa mawazo au kukosa utoshelevu wa kihisia. Mabinti/vijana wengi baada
ya kukosa upendo halisi wa wazazi wao au kwa watu walio tegemea
kupata faraja kwao na ikatengeneza maumivu ya moyo /kihisia, na hii
imefanya watu wengi kuingia kwenye uraibu wa pombe, madawa ya
kulevya na wengine kujichua na kutazama picha za ngono.

PASTOR ESKAKA CHAULA 11


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Upweke [loniliness]

Baadhi ya vijana wakati mwingine hadi wanandoa wengine wanaingia


kwenye uchafu wakidai ni kwa sababu ya upweke muda wote wenzi wao
wanapokuwa wapo mbali nao.

Kujiridhisha na hamu za kingono [To Cure from


sexual urge]

Hisia za kingono kwa mtu sio dhambi, tatizo linakuja pale ambapo hisia
zinaanza kukuendesha [nimeandika vizuri kwenye kitabu, namna ya
kutawala hisia za kimapenzi kabla ya ndoa]

Sasa kuna watu wakipata tu hisia za kingono wanakimbilia kutazama picha


za ngono na kujikuta wamejiridhisha wenyewe au wamejichua.

Kukaa muda mwingi bila kuwa na jambo la


maana la kufanya [idleness]

“An idle mind, they say, is the devil’s workshop” Kuna watu walijikuta
wanapata mawazo ya kutazama huu uchafu kwa sababu ya kukaa muda
mwingi bila kuwa na jambo la maana, shetani akapenyeza wazo tu la
kupekua katika mtandao na wakajikuta wamenasa jumla kwenye huu
uraibu wenye sumu ndani yake.

PASTOR ESKAKA CHAULA 12


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Wengine utazama kwa sababu ya kupata starehe


tu [pleasure/fun]

Nadhani umewahi kusikia mtu anajinasibu kuwa yeye wala sio mzinzi ila
starehe yake ni pombe tu, na wengine hudai starehe yao ni kutazama
picha za ngono.

Watu wengine hudhani kuwa wakitazama picha za ngono basi watatibu


tamaa ya mwili [lust], wasichokijua kutazama picha za ngono ni sawa na
kumwagia petrol kwenye moto wa kuni na unatarajia moto uzimike!

“Pornography can only bring you pressure, not pleasure. Porn will cause you to
burn and boil in the flesh. And, many times, the pressure from porn leads to
self-destruction. Pornography puts people’s emotion and body under pressure”

Mafunzo ya namna ya kushiriki tendo la ndoa

Kuna watu wengi sana [hadi kwenye ndoa] wanao dai kuwa wanaangalia
pornografia ili kujifunza namna ya kuwaridhisha wenzi wao. Bahati mbaya
sana huwa hawajiulizi mwanzilishi wa wazo la porno ni nani?

Je hao wanao cheza porno nani aliwafundisha hizo style? Kama porno ni
kitu cha kawaida unadhani mtu ana akili zake timamu anaweza kuwa tayari
kushiriki tendo la ndoa huku akiwa ana rekodiwa na watu dunia nzima
wamtazame? Wewe unaweza kufanya hivyo?

PASTOR ESKAKA CHAULA 13


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Ndugu yangu hakuna jema unaweza kujifunza na kulipata kwenye picha


za ngono. Nikuulize tu swali dogo, hivi unadhani Adam na Eva ni nani
aliwafundisha kufanya tendo la ndoa? (kujamiana) Maana tunaoma
walipata watoto, unadhani walipataje? Uliwahi kusoma biblia inasema siku
moja Adam/Eva analalamika harizishwi kingono na mwenza wake? Kwa
nini wewe unataka kujifunza kutokea kwa watu walio jaa mapepo, jambo
ambalo ni takatifu kwa ajili ya wanandoa?

“Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba,


akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa
Bwana. Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili" (Mwanzo 4:1-
2 Biblia Takatifu)

Acha akili mbovu ya kwenda kuzoa mapepo na uchafu kutokea kwa


mawakala wa kuzimu kwa kutazama picha za ngono, Mungu ana hekima
sana sana, kwanza hakuna mashindano ya style na kufanya tendo la ndoa
na mme/mkeo, Mungu anawapa akili ya kumjua kila mtu mwenzie na
namna ya kuridhishana bila kushushiana heshima.

“Yafahamu sana hayo nisemayo, kwa maana Bwana atakupa akili


katika mambo yote. (2 Timotheo 2:7 Biblia Takatifu)

Lakini pia Mungu ameweka hekima kwa walimu mbalimbali waliojaa Roho
Mtakatifu, wanaoweza kufundisha jambo hili kwa usafi na utakatifu hasa

PASTOR ESKAKA CHAULA 14


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

pale vijana wanapokuwa wamefikia hatua kubwa sana katika mchakato wa


kuoana au hata baada ya kuoana...!!

Mapepo ya zinaa ni chanzo cha kutazama porno


[Demonic Influence]

Usichokijua ni kuwa tupo nyakati ambazo uzinzi na uasherati [zinaa] ni


moja kati ya agenda ya kuzimu kuharibu hatma za watu.

“Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa" Mathayo 12:39


(Biblia Takatifu)

"Kizazi kibaya na cha zinaa …" Mathayo 16:4 (Biblia Takatifu)

"Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu,


katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi..." Marko 8:38 Biblia
Takatifu)

Na moja kati ya kitengo maalumu kuzimu imekiandaa ni kitengo cha


porno na kujichua.

Kuna watu walianza kwa utashi wao wenyewe kutazama porno ila baada
ya muda hawakuwa na uwezo tena wa kuhitawala miili yao,
wanaendeshwa na pepo wa porno na zinaa kwenye uchafu huu nje ya
maamuzi yao.

PASTOR ESKAKA CHAULA 15


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Hizo ni baadhi ya sababu za watu wengi kuingia kwenye utazamaji wa


picha za ngono. Kwa upana tutaangazia madhara halisi ya utazamaji wa
picha za ngono na kujichua ili tujue pia na namna ya kutoka jumla kwenye
shimo hilo.

PASTOR ESKAKA CHAULA 16


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

MADHARA YA UTAZAMAJI WA PICHA ZA NGONO


PORNO INA ATHIRI UFAHAMU NA AKILI YA
MTAZAMAJI [Porn distorts your reasoning and mental
faculty]

Moja kati ya eneo ambalo lina athirika moja kwa moja kwa utazamaji wa
porno ni eneo la nafsi hasahasa hisia na akili. Kama dhambi zingine za
zinaa zinazo haribu nafsi pia porno ina madhara makubwa sana kwenye
akili ya muhusika.

“Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo


litakalomwangamiza nafsi yake. Atapata jeraha na kuvunjiwa
heshima; Wala fedheha yake haitafutika” (Mithali 6: 32-33 Biblia
Takatifu)

Watu wengi wanao tazama porno wakiwa wawazi watakuelezea kuwa


mara zote akili yao ikiwaza kuhusu ngono inafikiria kupata sawasawa na
kile walichokiona kwenye uchafu wa porno. Hakuna mtu aliye mraibu
wa porno ambaye ufahamu wake na akili yake upo sawa! HAPANA!

PASTOR ESKAKA CHAULA 17


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Porno inadhalilisha utu wa mwanadamu na


kulifanya tendo la ndoa lipoteze heshima yake ya
kiungu [Porn degrades humanity and diminishes the beauty
that God intended for sexuality]

Ukiwa mkweli kama umewahi kuwa mraibu wa porno utagundua kuna


uchafu unafanyika mle ambao kwa mwanadamu wa kawaida ni aibu na
udhalilishaji wa utu wa mwanadamu. Mathalani kijana wa kiume ambaye
ameathirika na porno moyo na utu wake wa ndani unaanza
kutowaheshimu wanawake na unaanza kuwachukulia kama vyombo vya
starehe na ngono.

Yaani mtu akimtazama mwanamke ni kwa ajili ya tamaa za kingono tu, na


sio kuwa mtu wa thamani ambaye wanaweza kuanzisha familia ya kiungu.

“So, porn addiction leads to a negative change of mindset and attitudes.


Christian actor, Terry Crews has this to say about pornography: “It changes the
way you think about people. People become objects. People become body
parts; they become things to be used rather than people to be loved.”

Porno zinaamsha tamaa ya kingono [porno


awake/flames man's sexual lust].

PASTOR ESKAKA CHAULA 18


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Porno zinafanya mtu asiridhishwe kingono na


mpenzi mmoja

Mara nyingi walio pitia kutazama picha za ngono watakwambia huwezi


kuishia kutazama aina moja ya video. Kila wakati utatamani uende
utazame watu wa aina, rangi, saizi na mataifa tofauti tofauti na hii
inatengeneza, ndani yako hali ya kutoridhika na mtu mmoja kingono, ndio
maana watu wengi walio tazama ngono waliishia kujichua au kuwa na
zinaa na watu wengi.

Porno ni mlango mkubwa wa kuingia kwenye


kujichua/punyeto [masterbation]

Pornography also encourages masturbation, creating an impure desire for self-


gratification. Someone had said, and I believe it, that pornography exists
primarily for the purpose of masturbation.

Mara nyingi watu wanao tazama picha za ngono, ili kushibisha tamaa ya
ngono iliyo inuka uishia kujichua. Tutaangazia kwa undani kuhusu kujichua
kwenye kurasa zinazofuata.

Porno ni dhambi na inaua mahusiano yako na


Mungu

PASTOR ESKAKA CHAULA 19


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

PUNYETO NI NINI?
Baadhi ya maelezo nimechukua kwenye kitabu cha mtumishi wa Mungu
brother evarist koba "ushindi dhidi ya punyeto" nashauri kila kijana
[na kila mtu akisome] na ikiwezekana watokee watu wanaoweza kukilipia
na ku-print na kukisambaza bure mashuleni, vyuoni, makanisani na kila
eneo, ni moja ya kitabu kizuri sana kwa habari ya kuvuka jumla kwenye
shimo la kujichua/punyeto.

PUNYETO ni hali ya kujiridhisha kingono kwa Mwanamume au


mwanamke kwa kutumia vifaa visivyoasilia kwa ngono kama vile sabuni,
mikono na mafuta, kutumia midoli ya maumbile ya kike au ya kiume na
vinginevyo.

PUNYETO hufanywa na watu/vijana wengi walio makanisani [na


mashuleni] na hata walio kwenye ndoa kwa sababu shetani [na watu
wasio na maarifa sahihi au mawakala wa kuzimu] amewadanganya kuwa
PUNYETO sio dhambi na PUNYETO inakusaidia usifanye uasherati [wao
uiita ngono salama]

Hivyo baadhi hufanya PUNYETO ili kujiepushe kukutana kingono na jinsia


tofauti ili kuepuka magonjwa ya zinaa.

PASTOR ESKAKA CHAULA 20


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Mfano nimewahi kusoma majarida flani yalikuwa maarufu sana hapa


Tanzania wakati nasoma shule ya msingi miaka ya 2006/2007 na tulikuwa
tunaaminishwa yana lengo la kutusaidia. Lakini nilikuja kugundua yalikuwa
yanahamasisha sana zinaa na kujichua, maana walikuwa hawaweki sana
mkazo kwenye kujiepusha na zinaa na kuwa na hofu ya Mungu bali
kwenye kutumia condom kama njia ya kujikinga na mimba lakini pia
kujichua kama njia ya ngono salama na walikuwa wanatuambia kuwa
hakuna madhara yeyote yatokanayo na kujichua na ilipekea vijana wengi
hasa walio kwenye balehe kujikuta wamedumbukia kwenye shimo hilo la
kuzimu la uraibu wa kujichua.

Punyeto/puli/kujilipua/kujichua/kujihudumia/kujimaliza/kujirid
hisha [masterbation] Ni kitendo cha mtu kujichezea kimahaba huku
akivuta hisia za mapenzi kwa mtu ambaye yupo mbali naye hadi
anapomaliza haja zake.

Punyeto kwa wanawake mathalani, mara nyingi ufanywa kwa kutumia


vifaa bandia (artificial) na wengine vifaa halisi kama aina mbalimbali za
matunda ambazo zinafanana na sehemu za siri za kiume! Wengine
wanatumia njia wanazojua wenyewe, lakini wanaume wengi wanatumia
sabuni, mafuta na njia nyingine nyingi wazijuazo wao kwa lengo la
kujiridhisha.

PASTOR ESKAKA CHAULA 21


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

LINAKUJAGA KAMA WAZO TU LA KUJISIKIA KUTAZAMA


PICHA ZA NGONO AU KUJICHUA

Watu wengi ukikaa nao na kuwauliza kwa habari ya kwanini wanashindwa


kujizuia kufanya uchafu huu ilihali wengine wanajua kabisa madhara mengi
ya kutazama picha za ngono na kujichua, wengi watakwambia linakuja
kama wazo kwenye ufahamu na utu wa ndani lenye nguvu kubwa sana
asiyo weza kuipuuza wala kuipinga na anajikuta ameshalitii hilo wazo na
anakuja kuanza kujilaumu mara tu baada ya kuwa amemaliza kujichua.

Watu wengi wasiochokijua ni kuwa hilo sio wazo la kawaida ni sauti


halisi rohoni (ya pepo) mmoja kukupa maelekezo na amri ya
kutazama picha za uchi na kujichua

Mara nyingine ili kuwafanya watu waelewe umuhimu wa kuacha na


kushinda vita dhidi ya uchafu huu uwa nawapa mfano huu kuwa Roho
Mtakatifu akitaka kuonesha nguvu zake au uwezo wake wa kufanya jambo
mfano kuponya anatumia kifaa kinachoitwa mwili wa mwanadamu
aliyetayari, kwa nje sisi tunaona Pastor Eskaka amemuombea mgonjwa
akapona lakini rohoni ni kuwa Mungu ametumia mwili wangu kumponya
mtu.

Ndivyo ilivyo pia ufalme wa giza, jini mahaba [spiritual husband or wife]
likitaka kushiriki tendo la ndoa linamvaa na kumuendesha mtu kwa kumpa

PASTOR ESKAKA CHAULA 22


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

mawazo ya kutazama picha za ngono na kujichua. Kwa msingi huo ukiwa


unajichua maanake umeutoa mwili wako ili pepo autumie kuzini!

Usikubali sasa kuwa mjinga [mtu aliyekosa maarifa] ukiona kuna wazo
linakuja la kutazama picha za uchi au kujichua, sasa unajua kabisa kuna
kiumbe cha rohoni kinataka kutumia mwili wangu kufanya mapenzi, fanya
vita na pepo aliye nyuma ya hilo wazo mpaka atokomee na akuache jumla.

“Maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika


Mungu hata kuangusha ngome;) tukiangusha MAWAZO na kila
kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka
nyara kila fikira ipate kumtii Kristo” (2 Wakorintho 10:4-5 Biblia
Takatifu)

Usisahau haya kuhusu kujichua na picha za utupu

✓ Pornografia na kujichua kunaongozwa na kitengo


maalumu kuzimu cha mapepo ya kuua hatma za watu
wakuu...

✓ Kuna pepo [jini] linalo shughulika na kuwafanya watu


waingie kwenye huo uchafu, ni kiumbe kabisa wa kiroho
ambaye akikuingia anaanza kuiuendesha kwa namna
ambayo yeye anataka kinyume na utashi na maamuzi yako.

PASTOR ESKAKA CHAULA 23


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

“Kwa kuwa amemwamuru yule pepo mchafu amtoke mtu yule.


Maana amepagawa naye mara nyingi, hata alilindwa kifungoni
na kufungwa minyororo na pingu; akavikata vile vifungo,
akakimbizwa jangwani kwa nguvu za yule pepo” (Luka 8:29)

✓ Lakini pia moja kati ya mlango mkubwa wa adui shetani


kupenyeza agenda ya ngono zisizo kuwa za kawaida kwa
binadamu [Demonic Sex] ni kwa kupitia picha chafu za
ngono

“Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao,


waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao. Kwa
maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia
kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele.
Amina. Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata
wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya
asili, wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya
asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa,
wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.
Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu
aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.
Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya;

PASTOR ESKAKA CHAULA 24


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia


mbaya, wenye kusengenya” (Warumi 1:24-29) (Biblia Takatifu)

Kwa sababu ya kuingia kwa ponografia watu wengi wamemezwa kwenye


kujichua/kujiridhisha, wengine wameangukia kufanya ngono na wanyama,
wanaume kuwaingilia wanawake kinyume na maumbile au kufanya ngono
kwa namna za ajabu na wamefika mbali zaidi hadi wanawake kwa
wanawake [usagaji/Lesbianism] au wanaume kwa wanaume [ushonga/
gaysim].

PASTOR ESKAKA CHAULA 25


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

MAMBO MENGINE YA KUJUA KUHUSU PUNYETO


[MASTERBATION] NA KUTAZAMA PICHA ZA NGONO
✓ Kupiga punyeto na kutazama picha za ngono
hakuui[hakumalizi/hakuondoi] hamu ya ngono bali
kunaichochea zaidi.

✓ Kupiga punyeto na kutazama picha za ngono humfanya


mtu kuwaona watu wa jinsia tofauti kuwa vitu au vifaa vya
kujitosheleza kingono tu.

✓ Hatari ya kutazama picha za ngono na kujichua ni kwamba


ni rahisi sana kuanza uchafu huu lakini inaweza kuwa
ngumu sana sana kutoka kwenye uraibu huu hasa ukikosa
msaada mzuri wa kiroho na kiufahamu kutoka kwa walio
vuka au wenye neema ya kuwavusha wengine hapo.

Nilidhani ni wanaume tu, kumbe na wadada wamevamiwa pia

Miaka michache tu hapo nyuma kuna mambo kuyasikia yanafanyika kwa


wanawake ilikuwa ni nadra na jambo la ajabu sana. Hapo nyuma kidogo
ilikuwa ni kwa wanaume tu kusikia wanateseka na kutazama picha za
ngono na kujichua.

PASTOR ESKAKA CHAULA 26


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

lakini kwa kizazi hiki hali ni hatari sana mpaka kwa wadada nao
wamedumbukia na kuzama kabisa kwenye wimbi hili la kujichua na
kutazama picha za utupu...

Kabla sijaenda kueleza kwa undani kwa habari ya madhara


halisi na namna ya kutoka jumla kwenye uchafu huu, ebu ngoja
niwadokezee mabinti na wanawake madhara ya kuendelea
kukaa kwenye shimo la kutazama picha za utupu na kujichua...

✓ Siku ukipata Neema ya kuolewa utasababisha kijana wa


watu [mmeo] aonekane hana uwezo wa kukufurahisha
kwenye tendo la ndoa [nitaelezea mbele ya safari jambo
hili la mengine]

✓ Ukiolewa utakuwa unafurahia zaidi kutazama picha za


ngono na kujiridhisha mwenyewe kuliko kukutana na
mwenzi wako na tendo la ndoa itakuwa kama mzigo au
utumwa vile.

Miaka kadhaa nyuma nilikuwa mahali na mtumishi wa Mungu ninaye


mpenda na kumheshimu sana [mimi nilikuwa bado sijawa mchungaji wa
kusimikwa] tukiwa kwenye huduma ile, tunajiandaa na ibada hivi,
nikamshuhudia akimuombea mama mmoja kwenye simu.

PASTOR ESKAKA CHAULA 27


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Mambo kadhaa nayo yakumbuka na yanayoweza kutusaidia kuelewa hii


pointi, nilikuja kujua kuwa yule alikuwa mke wa mtu wa ndoa, lakini cha
ajabu na kweli alikuwa kila akilala na mme wake ajisikii kuridhika ni mpaka
aende chooni kidogo akatazame picha za utupu na kujiridhisha
mwenyewe ndio walau anahisi kutoshelezwa

Kumbuka anafanya jambo, mmewe akiwa hajui na kiukweli sio kwamba


mumewe alikuwa na tatizo lolote ni vile tu huyu mama alikuwa na pepo
[jini mahaba] kufupisha habari, ile hali ilisababisha kuwe na ugomvi
mkubwa sana kwenye ndoa kati ya mme na mke na kama Bwana
hakuingilia kati nina amini ile ndoa ilivunjika [Japo naamini Bwana
aliwasaidia kuvuka hapo]

✓ Kuna weza kukusababisha uingie kwenye uchafu wa


kusagana [ngono ya wanawake kwa wanawake]

Shetani amepandikiza mapepo ya ushoga na usagaji sana kwenye picha za


ngono, ndio maana ni kawaida kuona movies nyingi ziki-potray mambo
haya kama mambo ya kawaida na baadhi ya serikali za wanadamu
zinazoongozwa na mifumo ya kuzimu kushadadia na kutaka dunia
ilichukue jambo kama jambo la kawaida na kulipitisha kwenye mataifa yao.

PASTOR ESKAKA CHAULA 28


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Sasa mtu akianza kutazama picha za utupu kuna majira atajikuta anaanza
kuvutiwa na za usagaji [au ushoga] na matokeo yake anavaliwa na roho
ya usagaji na ataanza kutamani kujaribu kile ambacho amekiona kwenye
videos na hii ndio maana baadhi ya shule [na vyuoni] kuna usagaji na
ushoga sana.

✓ Utavamiwa na majini mahaba [nimeelezea vizuri


mbele] ambayo yana madhara makubwa sana kwako
binti/mama ikiwepo yatakusumbua sana kwenye eneo la
kupata mtu sahihi wa kukuoa, Kuteseka kuolewa na hatari
zaidi kama nilivyoeleza juu hapo hutafurahia tendo la ndoa
na utajikuta unapitia ndoa yenye magomvi na kutokuelewa
kusiko na sababu za msingi na wakati mwingine utaishia
kuachika au kuomba talaka.

Binti na mama yangu usikubali kuendelea kutumikishwa na


shetani kwenye utumwa wa kutazama picha za ngono na
kujichua wakati msaada wa Mungu wa kukutoa upo.

PASTOR ESKAKA CHAULA 29


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

MADHARA YA PUNYETO NA KUTAZAMA


PONOGRAFIA
MADHARA KINAFSI

✓ Kuingia mikataba na maagano na mapepo ya


ngono.

Kuna watu kwa sababu ya kutazama picha za ngono wamejikuta


wameingia maagano na ulimwengu wa giza. Kuna watu nafsi zao zimezwa
kuzimu kabisa na wamejikuta wana ndoa za kipepo na majini na wengine
mpaka wana watoto kabisa.

Ndio maana sio ajabu sana kuona mtu ambaye yupo addicted na
pornography au kujichua kukwambia kuwa mara kwa mara anaota ana
zini na watu mbalimbali ndotoni na kuna wengine wanaota
wanafungishwa ndoa bahari, wengine wanaota wapo bahari ni mamalkia
na wana watoto wana nyonyesha kabisa.

Tafsiri yake ni kuwa watu hawa tayari wameshaingizwa kwenye maagano


na hizi nguvu za kipepo.

✓ Nafsi yako kutaka kuingia katika kina zaidi kwenye


kuangalia ponografia.

PASTOR ESKAKA CHAULA 30


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Mfano unakutana na mtu ambaye mara ya kwanza shauku yake ilikuwa ni


kuona watu wakizini tu na anajichua anaacha. Baadae kidogo anasema
nikaanza kuwa natamani kutazama mitindo mbalimbali za ngono, na
baadae anasema akahama akaanza kutazama mitindo za ovyo Zaidi.

Baadae mtu huyu akataka aanze kujua hivi video za wanyama na


wanadamu zinafananaje, akaenda mbali zaidi mpaka akaanza kutazama za
watu wa jinsia moja na za binadamu na wanyama mpaka inafikia kipindi
ameathirika kihisia na kisaikolojia.

Kuna baadhi ya video za ponografia akizitazama wala hazimuamshi hisia


zake anakuwa kama ambavyo mimi ningekuwa natazama nyimbo ya injili,
hakuna hisia hata kidogo, na akanambia hii ni takribani kwa mtu yeyote
ambaye ameendelea kuangalia uchafu huu kwa muda mrefu...Dahh!!!

✓ Kutengenezeka kwa picha chafu kwenye ufahamu wa


muhusika.

Moja kati ya mtihani mzito ambao watu walio athirika na utazamaji wa


picha za ngono ni kutofutika kwa picha hizo katika fahamu zao. Unakutana
na kijana mmoja, umemuombea amefunguliwa kabisa na anasema sisikii
ile hamu kabisa baada ya kuombewa lakini anajiskia vibaya maana picha za
yale matukio zimekuwa zikijirudia mara kwa mara na wengine muda flani

PASTOR ESKAKA CHAULA 31


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

baada ya kumfungua hata kama aangalii tena anaweza jikuta anaota mara
kadhaa akiwa pengine anatazama picha za ngono au anazini.

Na kuna mwingine anaweza kuwa hata yuko kwenye maombi na katikati


ya maombi anashangaa zile picha ni kama zinarudi kwenye ufahanu wake
upyaa. Bila shaka moja kati ya njia kadhaa za kutatua kesi hii ni pamoja na
kumuomba Mungu azifute jumla hiyo kumbukumbu, kuendelea kujilisha
neno la Mungu

(Wala msifuate kanuni za dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia
zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza,
na ukamilifu. (Warumi 12:1)

Lakini pia tumia damu ya Yesu kuangusha kila ngome;

“Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi


ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo
katika Mungu hata kuangusha ngome; tukiangusha mawazo na kila
kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka
nyara kila fikira ipate kumtii Kristo” (2 Korintho 10:3-5]

PASTOR ESKAKA CHAULA 32


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

✓ Muunganiko wa nafsi na mapepo na kujikuta


unazini na mapepo yaliyo chukua sura na
maumbo ya watu ndotoni na wengine ni kitu halisi
kabisa wanazini na watu wasio waona.

Ukifatilia kwa makini watu ambao wameathirika na utazamaji wa picha za


ngono na kujichua basi wamekuwa wahanga wakubwa wa mara kwa mara
kuota ndoto wanazini na watu mbalimbali kwenye ndoto.

Na watu wengine imevuka mipaka mpaka mapepo yale yamekuwa ni


viumbe halisi, wakiwajia kabisa mwilini na kushiriki nao tendo la ndoa.

✓ Kupoteza hisia na jinsia tofauti (tendo la ndoa


linapoteza ladha)

Kuna watu hisia na saikolojia yao imeharibiwa kabisa na picha za utupu


na kujichua kwa kiwango ambacho yupo tayari kujichua na kutazama
picha za ngono kuliko kuoa / kuolewa. Na kuna wengine [hata walio
kwenye ndoa] hawana kiu kabisa ya kufanya tendo la ndoa, kwao ni bora
wajichue au waangalie picha za ngono kuliko kukutana kimwili na wenzi
wao. Ni hatari sana lakini ni ukweli.

PASTOR ESKAKA CHAULA 33


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

✓ Kuwa mtumwa wa picha za uchi kihisia.

Mfano kuna watu hawawezi kupata hisia za kushiriki tendo la ndoa ni


mpaka ametazama picha za ngono kwanza.

✓ Kutoridhishwa kihisia na mtu mpaka umevuta


hisia za kuzini na mtu mwingine.

Kuna mtu mmoja amewahi kuniambia kabla Bwana Yesu ajamfungua


kutoka kwenye dhambi za zinaa, alikuwa ili aweze kuridhishwa na mke
wake ni lazima wakati wa mchakato mzima wa tendo la ndoa yeye uwa
anawaza na kuvuta hisia na kutengeneza picha za kuwa analala na
mwanamke mwingine.

✓ Kutaka kujaribu kufanya [practice] kile ambacho


umekitazama kwenye pornographia.

Watu wengi kwa uongo wa shetani wamejikuta wanadai kwamba


wanataka wajifunze aina/mifumo mbalimbali za kufanya mapenzi eti kwa
njia ya kutazama picha za ngono. Baba yangu katika imani Bishop Dickson
Kabigumila huwa anauliza swali hili kuwa, “Adam na Eva ni nani
aliwafundisha namna ya kufanya mpaka wakazaa watoto?”

Kama hakuna mtu wa kuwafundisha then uhitaji watu walio jaa pepo
wachafu wakufundishe namna ya kukutana na mke/mme wako.

PASTOR ESKAKA CHAULA 34


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Na moja kati ya hatari ya uchafu huu ni kutamani kuona mwenzi wako


anafanya kama ulicho kiona kwenye mauchafu. Ndio maana kuna
wanaume wasio na "AKILI" wanaona watu pekee "WASIOJIELEWA"
wanaoweza kufanya uchafu wa kila namna bila kujali utu wao, kikubwa tu
wanachuma pesa ya "JUA" mmoja ni malaya wanao jiuza au nyumba
ndogo.

Kitu wasichokijua ni kuwa wale wanaoigiza kwenye pornografia kwanza


wengi wapo wamemilikiwa na mapepo, wanaendeshwa na pepo wachafu,
pili wale wapo kibiashara zaidi ili wapate pesa ya "WAPUMBAVU"
watakao kuja kuingia internet kutazama uchafu wao so ni lazima wafanye
hata uchafu wa kupita kawaida lakini cha tatu kuna vingine ni editing ya
film makers na sio uhalisia kabisaa.

Usikubali kuendelea kushikwa kwenye shimo refu hili la kuzimu dhamiria


kutoka jumla ndugu yangu...na nakuombea kwa jina la yesu, Bwana akutoe
kwenye huu uteka.

PASTOR ESKAKA CHAULA 35


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

MADHARA YA PUNYETO KWENYE AFYA YA UZAZI


[KIMWILI]
Nimejaribu kufanya utafiti kwa kufatilia wataalamu wa afya na kupata
nafasi ya kuwasaidia kwa neema ya Mungu au kuwasikia waathirika wa
uraibu wa kutazama picha za ngono na kujichua nimegundua kuwa uchafu
huu una madhara makubwa sana kwenye eneo la afya ya uzazi[mwili], na
mtumishi wa Mungu Brother Evarist Koba kwenye kitabu chake cha
"USHINDI DHIDI YA PUNYETO" ameelezea kwa upana sana namimi
nitachukua sehemu ya maelezo yake na nitaongezea ya kwangu pia.

PUNYETO huambatana na madhara makubwa ya kiafya

✓ Ni moja ya chanzo Kikuu cha kupoteza nguvu za kiume,


uume kusinyaa na kukosa nguvu kwa sababu ya kuharibu
misuli na mishipa ya damu ya uume wakati MTU
akijisugua/akijiridhisha

✓ Husababisha mwanamume kutoa mbegu haraka kipindi


cha tendo la ndoa (Premature ejaculation) na
kushindwa kufanya mwanamke kufurahia tendo la ndoa
[zawadi ya mungu kwa wanandoa kwa ajili ya kuimarisha
bond ya ndoa]

PASTOR ESKAKA CHAULA 36


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

✓ Husababisha msongo mkubwa wa mawazo [ATHARI ZA


KISAIKOLOJIA] kwani mara nyingi kila umalizapo tendo
hilo unajuta na kuumia sana na kuapa kwamba hutorudia
tena lakini ikifika mida Fulani "KUJICHUA kama kawa" hali
Hii baadae hupelekea kujiona kama mnyama na
wasiposaidiwa hufikia mahali pa kujichukia kabisa na hii
mara nyingi huwatokea wanawake.

✓ Lakini pia punyeto hupunguza hamu[hisia] ya kufanya


mapenzi [tendo la ndoa] kwa sababu kihisia kunakuwa
hakuna utoshelevu.

PASTOR ESKAKA CHAULA 37


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

MADHARA YA KUTAZAMA PICHA ZA NGONO NA


KUJICHUA KIROHO
Kutazama picha za ngono na kujichua sio tu starehe au tukio la kujisisimua
hisia mara moja bali ni MADHABAHU ya kuzimu ya kuua uhusiano kati
ya mtu na Mungu. Ndio maana eneo la kwanza linalo anza kuathiriwa ni
ukiroho wako [mahusiano yako na Mungu] kwanza.

Yafuatayo ni baadhi ya madhara ya uchafu huo kwenye maisha


yako ya kiroho.

✓ Ina kata na kuua ushirika na mungu.

Unaweza kuigiza mbele za watu wasio yaona maisha yako ya sirini kuwa
uko vizuri na Mungu lakini uwezi idanganya nafsi yako na moyo wako
kujua kuwa ukinaswa na pepo la zinaa unapoteza kabisa hofu ya Mungu
na unagundua hauna ukaribu na Mungu kama ambavyo ulikuwa ujajiingiza
kwenye huo uchafu.

“Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa


wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; lakini maovu yenu
yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu
zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia. Kwa maana
mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na VIDOLE vyenu

PASTOR ESKAKA CHAULA 38


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi


zenu zimenong'ona ubaya” (Isaya 59:1-3 Biblia Takatifu)

Dawa pekee hapo sio kuwaigizia watu kujifanya upo vizuri na Mungu,
wakati umekufa lazima ukubali kurudi upya na kuanza na Bwana na kuitia
huruma na rehema zake zikutoe jumla.

✓ Kuvamiwa na mapepo machafu kama majini


mahaba na mengine yanayo haribu maisha yako.

Kuna watu maisha yao yalianza kupoteza uelekeo mara tu baada ya


kujiingiza kwenye kujichua na kutazama picha za utupu.

“Mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake; Na yeye


abomoaye BOMA, nyoka atamwuma” (Mhubiri 10: 8 Biblia
Takatifu)

Dhambi inaondoa ulinzi wa Mungu kwenye maisha yako hasa ukianza


dhambi za zinaa. Mwenyewe ni shahidi ukiwa haupo vizuri na Mungu
unakuwa huna hata hofu na Mungu lakini kila ulipoanza kuingia kwenye
huu mtego umepoteza ujasiri unahofu hofu kila muda maana roho yako
inaona ukuta[ulinzi] wa Bwana na uvuli wake umeondoja juu yako.

PASTOR ESKAKA CHAULA 39


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

✓ Kupoteza ujasiri wa kuhusiana na mungu kama


baba yako [utapoteza ujasiri wa kuomba]

Kuna tofauti ya kuwa mwombaji wa ratiba na muombaji ambaye unajua


unahusiana na Mungu kama baba na huwa anakujibu maombi yako.
Ukishaanza kuingia kwenye dhambi hizi ule ujasiri wa kumuendea Mungu
kama baba, utagundua unapungua sana sana na wakati nwingine unaisha
kabisa.

“Wapenzi, mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu; na


lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri
zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake” (1 Yohana 3:21-
22 Biblia Takatifu)

✓ Kuingiwa na roho ya zinaa na tamaa isiyo isha.

Anasimulia Mtumishi wa Mungu Brother Evatist Koba kwenye kitabu


chake cha “USHINDI DHIDI YA PUNYETO”

"Kuna kijana alinifata akaniambia kuwa amefikia hatua ya kuweka mikono


yake pilipili ili usiku akiamka asipige punyeto, lakini alishindwa, akawa
anapiga hivyo hivyo na mikono aliyopaka pilipili. Akikaa mwenyewe kuna
muda akimuona tu mwanamke mbegu (semen) zinatoka zenyewe,
anajichua hadi mara sita kwa siku, hizi roho zinatesa watu mnoo, Mungu

PASTOR ESKAKA CHAULA 40


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

alimfungua akaacha kabisa, mapepo yakalipuka siku anaombewa,


yanasema huyu ni mume wetu"

✓ Kuishi chini ya utumwa na utawala wa pepo la


pornographia na kujichua kwa level ya kushindwa
kujitawala hasa linapokuja swala la kufanya
maamuzi ya kuacha [being addicted]

Kutazama picha za ngono kuna sababisha watu wavamiwe na kumilikiwa


na majini mahaba [spiritual husband & wife]. Zaidi ya 99.9999% ya wanao
tazama picha za ngono huwa wanajichua kwa sababu nyuma ya kujichua
kuna jini mahaba linalokuwa limekuoa au kuolewa nawewe.

MADHARA YA MTU KUWA NA PEPO LA JINI MAHABA

✓ Unaweza kuchelewa kuoa au kuolewa [marital delay]

✓ Unaweza jikuta unakosea kosea mahusiano au kila


mahusiano unayoingia yanaishia kwenye uzinzi au
kuvunjika

✓ Kuwa mtu mwenye ugomvi na watu wa jinsia tofauti


[hasira zisizo za kawaida]

PASTOR ESKAKA CHAULA 41


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

✓ Kujikuta unachukia ndoa [hutaki kuolewa au kuoa] bila


sababu ya msingi

✓ Kulalwa na mapepo kwenye ndoto [sexual dreams] na ni


kama vile umelala na mtu na ukiamka ni kama umelala na
mtu kabisaa

✓ Kukosea kuoelewa /kuoa [ili uwe na migogoro na mwenzi


wako, na msipeane tunda ili lenyewe lilale nawewe]

✓ Kutokuridhishwa na mwenzi wako hata afanye nini [ili


ujikute unarudi kwenye kutazama picha za ngono na
kujichua]

✓ Kuwa na ugomvi wa mara kwa mara na mwenzi wako


[unao pelekea kutotaka kushiriki tendo]

✓ Kupoteza hashki ya tendo la ndoa na mwenza wako. [na


hujui kwanini]

✓ Kuwa na ashki na matamanio na mwenzi wako akiwa


mbali lakini akiwa karibu anapoteza mvuto kabisa

✓ Maisha ya uchumi kupigwa na maeneo mengi ya maisha


kuyumba yumba.

PASTOR ESKAKA CHAULA 42


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

NATOKAJE KWENYE KUTAZAMA PICHA ZA NGONO


NA KUJICHUA.
1. Tambua hiyo ni roho kamili chafu [kiumbe cha
kiroho/pepo] na amua kufanya vita nacho

[Usikubali kushindwa mpaka umetoka jumla]

2. Amua kuacha dhambi zote jumla na kuyakabidhi maisha


yako kwa yesu, ili kuziba mwanya wa kuendelea kuwa
miliki ya shetani.

Kuna watu wao wanachotaka tu, ni Yesu awasaidie kuacha kutazama


picha za ngono ila maisha yao wabaki nayo wenyewe na wayaendeshe vile
wanavyo jisikia wao. Sasa ukiwa ujaokoka kwa kumaanisha wewe bado ni
wa shetani na kwa sababu utaendelea kuishi maisha ya dhambi. Basi
shetani atakurudia tena kwa nguvu na kukumiliki tena.

3. Baada ya kuamua toka ndani kutoka jumla na kuokoka


kwa kumaanisha, tafuta msaada wa mtu mwenye nguvu za
kiroho akufungue utoke hapo

PASTOR ESKAKA CHAULA 43


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

“Na kama Shetani ameondoka juu ya nafsi yake, akafitinika,


hawezi kusimama, bali huwa na kikomo. Hawezi mtu kuingia ndani
ya nyumba ya mtu mwenye nguvu, na kuviteka vitu vyake,
asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu; ndipo atakapoiteka
nyumba yake” (Marko 3:26-27 Biblia Takatifu)

4. Amua kujaa moto ndani yako [kwa maombi na neno]

“Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji,


akitafuta mahali pa kupumzika, asipate. Halafu husema, Nitarudi
nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa,
na kupambwa. Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo
wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na
kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko
ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya.
(Mathayo 12: 43-45 Biblia Takatifu)

Njia nyingine ya kushughulika na pepo la masterbation na pornographia


ni kuhakikisha unaacha kulisha moyo wako vitu vinavyo vuta mapepo na
kuua moto wa mungu na kuanza kuilisha roho yako mambo yanayo inua
moto wa Mungu

PASTOR ESKAKA CHAULA 44


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

1. Acha kabisa kutazama/kusikiliza miziki ya kidunia


[iliyo imbwa na watu wasio na roho wa mungu]

“Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote
utakuwa na nuru. Lakini jicho lako likiwa bovu, mwili wako wote utakuwa
na giza. Basi ile nuru iliyomo ndani yako ikiwa giza; si giza hilo” (Mathayo
6:22-23 Biblia Takatifu)

“Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri; au


ufanyeni mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana
kwa matunda yake mti hutambulikana. Enyi wazao wa nyoka,
mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha
mtu huyanena yaujazayo moyo wake. Mtu mwema katika akiba
njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa
mabaya. (Mathayo 12:33-35 Biblia Takatifu)

Comedies/movies zenye mlengo wa ngono na vitendo vya ngono ndani


yake, acha kabisa kuzifatilia kwa usalama wa roho yako. Kimsingi acha
kutazama vitu vyote vinavyo kula muda wako lakini havikuinui kiroho.

PASTOR ESKAKA CHAULA 45


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

2. Epuka mazungumzo mabaya hasa yahusuyo zinaa


na watu hasa marafiki

“Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema” (1


Wakorintho 15:33 Biblia Takatifu)

3. Amua kujiongezea thamani (ku-update standard)


ili uweze kupunguza baadhi ya watu wa ovyo
kwenye maisha yako

“Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala


hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa
wenye mizaha. Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria
yake huitafakari mchana na usiku. Naye atakuwa kama mti
uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake
kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo
litafanikiwa” (Zaburi 1:1-3 Biblia Takatifu)

LAZIMISHA KUINGIA KWENYE MFUMO WA MAISHA


UNAO KUWEKA KARIBU NA MUNGU

1. Maisha ya ibada na kukusanyika na watakatifu


mara kwa mara

PASTOR ESKAKA CHAULA 46


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

“Mwenye haki atasitawi kama mtende, Atakua kama mwerezi wa


Lebanoni. Waliopandwa katika nyumba ya Bwana Watasitawi
katika nyua za Mungu wetu. Watazaa matunda hadi wakati wa
uzee, Watajaa utomvu, watakuwa na ubichi. (Zaburi 92:12-14
Biblia Takatifu)

2. Maisha ya maombi [kwa mwendelezo]

3. Kujizoeza kusoma neno kila siku

4. Kusikiliza watumishi wa mungu [audio au videos]

“Nimedumbukia kwenye uraibu wa kuangalia picha za ngono na


kujichua kwa muda mrefu ni kweli nimeacha lakini je nitakuwa
salama?”

Kuna mtu anaweza kuwa ameanza kujichua tokea akiwa ana umri mdogo
na amejichua kwa muda mrefu sana pamoja na kutazama picha za ngono,
then Mungu akamsaidia kutoka jumla hapo, mashaka yake yakawa je
nitawezaje kuyaepuka madhara yote yatokanayo na kujichua kwa kipindi
chote hicho?

PASTOR ESKAKA CHAULA 47


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

1. Ukiokoka kwa kumaanisha na kuanza kutembea na Mungu, Mungu


atarejesha kila kilichoibiwa na adui kwenye maisha yako [ikiwemo
kuyaondoa madhara pia].

“Neno la Bwana lililomjia Yoeli, mwana wa Pethueli. Sikieni haya,


enyi wazee; Sikilizeni, enyi wenyeji wote wa nchi. Je! Mambo haya
yamekuwako katika siku zenu, Au katika siku za baba zenu?
Waarifuni watoto wenu habari yake, Watoto wenu wakawaambie
watoto wao, Na watoto wao wakakiambie kizazi kingine.
Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige
yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na
madumadu. (Yoeli 1:1-4 Biblia Takatifu)

“Na sakafu za kupepetea zitajaa ngano, na mashinikizo yatafurika


kwa divai na mafuta. Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na
nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa
nililotuma kati yenu. Nanyi mtakula chakula tele na kushiba, na
kulihimidi jina la Bwana, Mungu wenu, aliyewatendea mambo ya
ajabu; na watu wangu hawatatahayari kamwe. Nanyi mtajua ya
kuwa mimi ni katikati ya Israeli, na ya kuwa mimi ndimi Bwana,
Mungu wenu, wala hakuna mwingine; na watu wangu
hawatatahayari kamwe. (Yoeli 2:24-27 Biblia Takatifu)

PASTOR ESKAKA CHAULA 48


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

2. Lakini pia unaweza kutafuta msaada wa maombezi kutoka kwa


mtumishi wa Mungu mwenye neema ya kufungua watu na kila kitu
kitarudi kwenye ukawaida [muujiza wa uumbaji ukatokea, ukabadilishiwa
mfumo mzima wa uzazi kwa nguvu za Mungu]

Mathalani nimeshuhudia mara kadhaa mtu anakuwa ana tatizo la mifumo


ya uzazi kwa sababu ya madhara kujichua kwa muda mrefu lakini baada
ya kuombewa Bwana anarejeza kila kitu kwenye nafasi yake na anapona
kabisa.

Kwa hiyo bado lipo tumaini kwa yeyote ambaye amedhamiria kutoka
jumla na kuwa chombo cha Bwana pia kwa ajili ya kuwatoa wengi kwenye
mashimo hayo na kuishi maisha ya ushuhuda kwa ajili ya Bwana

“Kwani yako matumaini ya mti, ya kuwa ukikatwa utachipuka


tena, Wala machipukizi yake hayatakoma. Ijapokuwa mizizi yake
huchakaa mchangani, Na shina lake kufa katika udongo; Lakini
kwa harufu ya maji utachipuka, Na kutoa matawi kama mche”
(Yoeli 2:7-9 Biblia Takatifu)

PASTOR ESKAKA CHAULA 49


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

KWANINI WATU WENGI WANAOMBEWA NA


KUFUNGULIWA KUTOKA KWENYE PEPO LA
PORNOGRAPHIA NA KUJICHUA LAKINI WANARUDI
TENA BAADA YA MUDA.
Kwa neema ya Mungu nimekuwa nikiwaombea na kuwasaidia watu wengi
sana kutoka kwenye uchafu wa zinaa ikiwepo kuwa watumwa wa kujichua
na kutazama picha za utupu. Lakini cha kushangaza kuna wakati
unamuombea mtu na kumpa maarifa ya namna ya kuvuka jumla kwenye
shimo, anafunguliwa lakini baada ya miezi kadhaa au muda kadhaa
wengine hadi miaka baadae wanakuja wanarudia matapishi hayo na kwa
kweli hali yao ya mwisho inakuwa mbaya sana sana.

Wanaweza kuwa waraibu kuliko hata ulivyo wakuta mwanzo sawasawa


na neno la Bwana

“Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa


kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na
kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya
kwanza. Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya
haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa.
Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa

PASTOR ESKAKA CHAULA 50


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa


amerudi kugaa-gaa matopeni. 2 Petro 2:20-22 Biblia Takatifu)

Mtumishi wa Mungu aliye nifanya nianze kuwaombea watu kwa ujasiri na


kujua lazima wafunguliwe hiki kifungo ni baba yangu katika imani Bishop
Dickson Cornel Kabigumila maana yeye kwenye eneo la Deliverance za
aina zote, Bwana huwa anamtumia kwa namna ambayo mimi natamani
kuwa kama yeye.

Lakini wakati flani nilikutana na mtu ambaye yeye amemuombea namimi


najua kwa uhakika alikuwa amefunguliwa kabisaa na alikaa muda kabisa
bila kurudia uchafu huo wa kujichua, baada ya muda nashangaa ananifata
mimi anasema Brother Eskaka nisaidie nimeanguka tena kwenye kujichua
[bila shaka, nilimsaidia lakini sikumbuki kama alivuka jumla yule ndugu].

Lakini nilibakia na swali kichwani kwanini watu wengine nikiwaombea


wanavuka jumla wanakuja na shuhuda za kudumu lakini watu wengine
wanarudi walikotoka hata baada ya kuombewa muda mrefu na kusaidiwa?
Hizi ni baadhi tu ya sababu [bado naendelea kujifunza], zinazo sababisha
watu warudi nyuma.

✓ Kutokumaanisha kutoka moyoni toba ya kuacha


[bali kuomba toba ili kupata amani ya moyo tu
kwa kipindi flani]

PASTOR ESKAKA CHAULA 51


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Kuna watu baada ya kusikia ukifundisha au wakisoma mahali madhara ya


kujichua, au ametazama picha za ngono ni kama anasikia hukumu ndani
yake. Sasa ili asiendelee kusikia hatia ndani yake, anaamua kuomba toba
au kutafuta mtumishi wa Mungu amuombee tu ili apate ahueni ya moyo
lakini ndani yake kabisa bado ajadhamiria kutoka jumla kwenye jambo
hilo au kuna raha[faida] anaipata kwa kuendelea kufanya hayo mambo.

Na ishara mojawapo ya kuwa mtu huyu ajaamua kutoka ndani ya moyo


wake kutoka jumla ni pale mtu anaomba toba lakini bado anarudi kwenye
mazingira yaleyale ambayo anajua kabisa ndio chanzo cha yeye kuanguka
mfano anarudi tena kwenye mahusiano ya ovyo yanayo chochea hashki
na kuamshana kihisia nje ya ndoa, kuangalia movies zenye maudhui ya
ngono ndani yake na kuishi maisha yale yale yanayo kuangusha kila siku.

✓ Kukubali uongo wa shetani kuwa sio rahisi kutoka


jumla.

Kuna watu wanaombewa na kwa kweli wanafunguliwa lakini shetani


anaendelea kuwasemesha kuwa hauwezi kutoka kirahisi tu, yaani
umejichua miaka kumi na utoke kwa kuombewa mara moja tu. Na
anaanza kuingiza mlango wa hofu ya kurudi tena kwenye uchafu, na hofu
ni moja kati ya mlango mkubwa wa mapepo kumuingilia mtu na kuharibu
maisha yake.

PASTOR ESKAKA CHAULA 52


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

“Maana jambo hilo nichalo hunipata, Nalo linitialo hofu hunijilia”


2Petro 2:25 (Biblia Takatifu)

Mtu amefunguliwa lakini bado yeye mwenyewe ni kama ana subiria ni lini
ataanguka tena na shetani anakuwa anamletea mawazo kila mara asipo
yapinga kwa neno la Mungu basi anaanguka tena.

“Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi


ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo
katika Mungu hata kuangusha ngome;) tukiangusha mawazo na
kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na
tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo” 2 Wakorintho 10:3-5
Biblia Takatifu)

✓ Kutobadili mfumo wako wa maisha ya zamani [ili


kuondoa mazingira ya kurudiwa na pepo]

✓ Kutojua madhara halisi ya kujichua na


pornographia kwenye maisha na hatma yako
[ndio maana unadhani utaendelea kuanguka na
kutubu tu]

Kuna watu wengine kwa sababu hawajaambiwa ukweli wote wa madhara


halisi ya uchafu wa kujichua na utazamaji wa picha za utupu, imekuwa ni

PASTOR ESKAKA CHAULA 53


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

ticket ya kuanguka na kurudi tena [nimeelezea kwa undani madhara ya


uchafu huu]

✓ Kutotambua nafasi ya neema ya Mungu kama


msaada pekee wa kukuvusha hapo

“Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote


imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za
kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika
ulimwengu huu wa sasa” (Tito 2: 11-12 Biblia Takatifu)

Kuna watu wengine kinachowafanya warudi kwenye hizi dhambi ni


KIBURI cha kiroho tu. Yaani mtu anadhani kwa sababu yeye ni mhubiri
au mtu mwenye nafasi flani au kwa sababu yeye anafunga sana na kuomba
basi hawezi kuanguka kwenye uchafu huu, ukweli ni kuwa pamoja na
umuhimu wa mifungo na kuomba, kinachotusaidia tusirudi nyuma ni
kutambua na kuheshimu nafasi ya Neema ya Mungu kutusaidia kuendelea
kukaa salama mbali na maanguko.

Bila Neema ya Mungu hata yule anayedhani hawezi kuanguka ni sekunde


chache tu anaweza kuanguka na kupata aibu kubwa sana.

PASTOR ESKAKA CHAULA 54


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

UFANYEJE KUTOKA JUMLA KWA UNAYE ANGUKA


ANGUKA?
✓ Dhamiria sio tu kutoka kwenye uraibu huo bali
kuacha dhambi zote na kumuishia Yesu [okoka
kwa kumaanisha]

Tuko kwenye kizazi cha ajabu, yani mtu anasema pastor mimi nahitaji
Mungu anisaidie kutoka kwenye kujichua ila hataki kuokoka na anataka
aendelee na maisha yake kama ya zamani. Haupo makini Mimi huwa
nawaambia ukweli huko ni sawa na kujitekenya halafu unacheka
mwenyewe tena, kwa sababu kama nikikutoa pepo sahivi na ukarudi
kwenye maisha yako ya uchafu ya zamani pepo litarudi na hali yako
itakuwa mbaya.

“Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji,


akitafuta mahali pa kupumzika, asipate. Halafu husema, Nitarudi
nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa,
na kupambwa. Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo
wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na
kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko
ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”
Mathayo 12: 43-45 Biblia Takatifu)

PASTOR ESKAKA CHAULA 55


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Sasa watu wengi wanataka Yesu awasaidie kutoka hapo tu, maisha
mengine wamuachie. Unautani! nakuhakikishia baada ya muda utarudi
tena, mpaka siku ukiamua kutoka moyoni kuwa unahitaji maisha yako
yaongozwe na Yesu maisha yako yote yaliyo bakia kwa kumaanisha ndipo
utakuwa kweli salama.

✓ Utoe mwili wako dhabihu kwenye madhabahu


kwa maombi.

Baada ya kuamua kuokoka kwa kumaanisha hakikisha una utoa mwili


kama sadaka[dhabihu] kwa njia ya maombi.

“Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni


miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu,
ndiyo ibada yenu yenye maana” (Warumi 12:1 Biblia Takatifu)

Ingia kwenye chumba cha maombi mwambie Mungu kwanzia leo


nakukabidhi kila kiungo changu macho, mdomo, miguu, mikono, sehemu
za siri n.k kuwa mali yako zitawale ziongoze na zisifanye lolote ambalo ni
aibu na uchafu mbele zako, fanya hivi mara kwa mara na utaona namna
Mungu anakutawala na kuchukua usukani wa mwili wako. Lakini njia
nyingine ya kuutoa mwili wako ni kwa njia ya maisha ya maombi na
mifungo kwa muendelezo, jiwekee utaratibu wa kufunga walau kila juma
siku kadhaa.

PASTOR ESKAKA CHAULA 56


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Wale ambao wamepata Neema ya kunisikiliza au kumsikiliza baba Bishop


Dickson Kabigumila, amekuwa akisisitiza walau ufunge mara tatu kwa
juma, kila juma kwa muendelezo. Hii inaweza kukusaidia usiangushwe
tena na kuzimu kwenye uchafu lakini pia hakikisha umesoma na kufanyia
kazi maelekezo ya namna ya kutoka jumla kwenye uchafu huu.

PASTOR ESKAKA CHAULA 57


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

KILIO CHA KIZAZI CHANGU!


KWANINI KIZAZI HIKI KUMEKUWA NA UTAZAMAJI WA
PICHA ZA NGONO NA KUJICHUA KWA KIWANGO
KIKUBWA SANA.

➢ Ni kutimia kwa unabii wa kizazi cha siku za


mwisho [kizazi cha zinaa & uzinzi]

Kizazi tulichopo ni kizazi cha siku za mwisho na kwa sababu neno la


Mungu haliwezi kusema uongo, tutaendelea kuona uchafu wa zinaa wa
kila namna kwenye hiki kizazi chetu.

"Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha ZINAA ..." (Mathayo


12:39 Biblia Takatifu)

"Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu,


katika kizazi hiki cha UZINZI na dhambi..." (Marko 8:38 Biblia
Takatifu)

Utagundua kwa kadri miaka inavyozidi kwenda mifumo ya dunia hii


inakutengenezea mazingira mepesi sana ya kuingia kwenye zinaa hasa
dhambi za kutazama picha za ngono zinazopelekea watu wengi waingie
kwenye maisha ya utumwa wa kujichua.

PASTOR ESKAKA CHAULA 58


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Si ajabu sana ukaingia mtandao kutafuta mafundisho ya imani lakini


ukakutana na “Ads” zinazokushawishi kwenda kutazama picha za ngono,
ndio aina ya kizazi tulichopo sasa KIZAZI CHA ZINAA[UZINZI] NA
DHAMBI.

Kwenye miziki ya kidunia utagundua kinachofanyika ni nusu ya kuangalia


watu wanazini kabisa, na bado hizo ndio nyimbo zenye soko na ushawishi
kwenye jamii yetu kuliko hata nyimbo zenye watu walio vaa kwa staha.

➢ Mavumbuzi kwa uvuvio wa kipepo [invection by


demonic inspiration]

“Tazama, hili tu nimeliona; Mungu amemfanya mwanadamu


mnyofu, lakini WAMEBUNI MAVUMBUZI MENGI” (Mhubiri 7:29
Biblia Takatifu)

Miaka kadhaa nyuma ilikuwa ni nadra sana kuona watu wanaongelea au


kuangalia pornografia, lakini kwa kadri siku zinaenda kuna watu wana
shirikiana na ulimwengu wa giza kupokea [kuvuviwa na mapepo] baadhi
ya mawazo [ideas] ambazo wao zinawaingizia pesa na kuwafanya maalumu
lakini ni sababu ya uharibifu wa vizazi na vizazi, moja wapo ya jambo hilo
ni watengenezaji na wasambazaji wa filamu za ngono. Kiukweli jambo hili
kwa watu wa rohoni sio jambo la ajabu japo linasikitisha maana ni agenda

PASTOR ESKAKA CHAULA 59


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

ya kuzimu inayotumika sio tu kuua hatma za watu bali kupeleka watu


wengi kuzimu milele.

NINI KIFANYIKE KUNUSURU HIKI KIZAZI NA


PORNOGRAPHY NA MASTERBATION HASA KWENYE
TAIFA LANGU LA TANZANIA?
➢ Elimu itolewe juu ya madhara halisi ya uchafu huu
mashuleni, vyuoni na maeneo mbalimbali yenye
mkusanyiko wa vijana.

➢ Tumuombe Bwana wa mavuno [Roho wa Mungu]


apeleke watenda kazi mashuleni [msingi na
secondary] na vyuoni wenye moto wa mungu

➢ Wazazi wasiogope kuwa wawazi kwa watoto wao


kuwaeleza ukweli juu ya uwepo wa zinaa na
madhara yake

➢ kusiwepo na uhuru uliopitiliza wa vijana kutumia


simu bila uangalizi wa wazazi hasa waliopo
mashuleni na ikiwezekana waweke vizuizi
(restriction) kwenye access ya baadhi ya programs
kwenye simu

PASTOR ESKAKA CHAULA 60


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

➢ Injili ihubiriwe kwa kasi sana kwa vijana [hasa


shuleni, vyuoni na mitaani]

➢ Watumishi wa Mungu walipe gharama ya kutafuta


nguvu za Mungu za kufungua walio fungwa

➢ Kuwepo na kufundishwa kwa somo la zinaa na


madhara yake na namna ya kutoka mara kwa
mara kwenye maeneo mbalimbali ya
makusanyiko ya vijana

➢ Kurejeshwa kwa hofu ya Mungu kwa vijana wa


kizazi hiki na wana ndoa

PASTOR ESKAKA CHAULA 61


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

MAOMBI YA USHINDI DHIDI YA KUANGALIA


PORNOGRAFIA
KAMA UJAOKOKA, NA UMEFANYA MAAMUZI YA
KUOKOKA ANZA KWA KUKIRI SALA HII KWA SAUTI
KABLA UJAOMBA MAOMBI YA VITA

1. “Baba katika jina la Yesu, nimechoka na maisha ya dhambi,


naomba unisamehe kwa damu yako, maisha yangu uyaongoze
kwanzia leo, naomba unipe ushindi dhidi ya dhambi zote,
nitakufata Yesu siku zote za maisha yangu, ninaamini Yesu ulikufa
na kufufuka ili kunipa ushindi dhidi ya shetani, dhambi na nguvu
zote za giza, kwanzia leo nimeokoka, kwa jina la Yesu.AMINA”.

Hongera umeokoka sasa, naomba unitafute kwa namba yangu,


0718578313

MAOMBI YA USHINDI DHIDI YA PEPO LA KUANGALIA


PICHA ZA NGONO NA KUJICHUA

2. Baba kwa jina la Yesu, naomba unirehemu kwa kuishi maisha ya


dhambi [taja baadhi ya dhambi unazozijua] na kuacha kutembea
kwenye njia yako. Kwa damu yako na rehema [mercy] zako kila

PASTOR ESKAKA CHAULA 62


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

nguvu inayo nifanya ninaswe kwenye shimo la kujichua na


pornography iharibiwe kwa damu ya YESU.

“Nao wakamshinda kwa damu ya mwana-kondoo, na kwa neno la


ushuhuda wao” (Ufunuo 12:11)

Kila mwanamme/mwanamke wa kipepo anayekuja kulala namimi kwenye


ndoto, anayenifanya nitazame picha za ngono na kujichua, aharibiwe kwa
moto wa Roho wa Mungu na damu ya Yesu. Bwana Yesu kwa neema
yako, naomba unisaidie kukaa mbali na uchafu wa ngono wa kila namna,
na niishi maisha ya kukupendeza wewe siku zote za maisha yangu.

“Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote


imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za
kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika
ulimwengu huu wa sasa” Tito 2:11-12 (Biblia Takatifu)

Bwana YESU kwa akili zangu timamu nautoa mwili wangu kama sadaka
na dhabihu kwenye madhabahu ya maombi na neno, uchafu wa ngono
hautatawala kanisa mwili wangu

“Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili
yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo
ibada yenu yenye maana” (Warumi 12:1 Biblia Takatifu)

PASTOR ESKAKA CHAULA 63


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

SHUHUDA ZA BAADHI YA WATU WALIOVUKA JUMLA


KWENYE URAIBU WA UTAZAMAJI WA PICHA ZA
NGONO NA KUJICHUA
USHUHUDA #01

Naitwa Brother E.K nasoma must mwaka wa tatu technical education


civil engineering niliingia kwenye uraibu wa kutazama porno graphy 2021
baada ya kushika simu ya rafiki yangu baada ya kuja chuo nilikuwa
naangalia kwa vipindi kwa mfano naangalia January narudi kuangalia may
kwa sababu kahofu kaMungu kalikuwepo mwaka wa pili nilIjitahidi ila
sikufanikiwa kushinda jumla na ilikuwa hainishitua sana mana darasani
nilikuwa nafanya vizuri namshukuru Mungu amenipa nguvu ya kushinda
moja kwa moja paka sasa.

USHUHUDA #02

Naitwa Brother Y.E, kutoka ABC global mbeya pia ni mwanafunzi wa


udaktari mwaka wa 3 chuo cha UDSM-MCHAS. Mwaka 2016 nikiwa
kidato cha pili nliingia kwenye uraibu wa kutazama picha za uchi na
kusoma hadithi(story) za ngono.

PASTOR ESKAKA CHAULA 64


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

Nilizaliwa kwenye familia ya wazazi waliookoka lakini mambo mengi


nliyokuwa nafanya sirini wasingejua mana nlikuwa mtiifu kwao na Jumapili
tunaenda wote kanisani na hata darasan nlikuwa nafanya vizuri sana.

Chanzo cha kuingia kwenye huo uraibu ni baada ya kaka yangu mmoja
kutembelea nyumbani na nlipochukua simu yake nikaenda sehemu ya
video nikakuta video za Ngono na nlipozitazama tu kuna roho iliniingia.
Mwaka huohuo nlipewa simu na wazazi japo ilikuwa ya buton lakini
iliweza kusearch Google na kuingia Facebook.

Kwahiyo nlikuwa nasearch picha Google na kusoma story za Ngono


Facebook hali yangu ilikuwa mbaya mana nlikuwa siwezi kulala mpaka
nmetazama na kusoma story za Ngono. Mwaka 2017 mwishoni
namshukuru Mungu nlikutana na Neema ya wokovu na huo uraibu
haukuendelea.

Mwaka 2021 baada ya kumaliza kidato cha 6 nlianza nlianza kuona kama
ule msukumo wakutazama picha unarudi na safari hii uliambatana na
tamaa Kali ya macho zaidi nlipofika chuoni mwaka huohuo. Lakini
namshukuru Mungu alinikutanisha na Baba Pst Eskaka Chaula mwaka
2022 na nikatoka jumla kwenye huo uraibu. Kwahiyo kama Bwana YESU
alinitoa mimi nawewe anaenda kukutoa

PASTOR ESKAKA CHAULA 65


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

USHUHUDA #03

BWANA YESU asifiwe naitwa M.l, nasoma chuo kikuu cha Dodoma
UDOM mimi kwa mara ya kwanza kabisa nilitazama picha za uchi ningali
mdogo mno nakumbuka nikama 2007 baada yahapo nilijikuta nikiwaka
tamaa na kwakuwa nyumbani tulikuwa wafugaji basi hali hii ilinipelekea
kubaka ng'ombe, kuku na mbuzi ningali kijana mdogo sana.

Badaye tulihama tulipokuwa tunaishi nikamwamini Yesu 2008 kwa


kweli kidogo nilijitahidi kuacha kujichua lakini badaye nilijikuta tena
kwenye changamoto hii. Kiufupi mimi nimelelewa katika familiya ya
kitumishi kabisa baba yangu ni mchungaji mama yangu ni mwinjilisti lakini
sikuwahi kuwashiliksha hili tatizo. Kuanzia 2016 nilipata simu kubwa
(smartphone) mambo yalizidi kuwa mabaya kwasiku nilijichua marambili
wakati mwingine nikila nilivyo jiskia. Mungu anisamee. Nilipo fika chuo
kikuu shetani alizidi kunitumikisha zaidi. Mchungaji naomba niwe wazi tu
kwani maandiko yanasema ''afichae dhambi hatafanikiwa", mimi
nimtumishi wa Mungu kabisa lakini hili jambo limenitesa sana na limekuwa
kikwazo katika huduma yangu.

Namshukru sana Mungu mwishoni mwa mwezi wa pili mwaka huu 2024
nikiwaka kwenye maombi Roho Mtakatifu aliniongoza kuomba maombi
ya rehema nikimuomba Mungu anipe tu nafasi ya mwisho, kwakweli

PASTOR ESKAKA CHAULA 66


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

namshangaa sana Mungu ameniokoa cha ajabu baada ya siku mbili hivi
kuna mwenzangu tunaishi naye chumba kimoja akaanza kutazama picha
za ngono chumbani tena hadharani kwakutumia PC yake ndipo nilipo
mkemea kwa hasira. Naomba Mungu azidi kunipigania na nimechoka
kutumikishwa na shetani natamani kumtumikia Mungu kwa amani kabisa,
Mungu anisaide.

PASTOR ESKAKA CHAULA 67


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

KUHUSU MWANDISHI

Eskaka Chaula ni mchungaji mkazi wa kanisa la Assembly of Believers


Church [ABC GLOBAL MBEYA CITY], akitumika chini ya mbeba maono
Baba yake na Mkufunzi wake, Askofu wa makanisa ya ABC GLOBAL
Bishop Dickson Kabigumila.

Pastor Eskaka Chaula ameandika kitabu hiki kwa muongozo wa Roho wa


Mungu, kama mchango wake wa kusaidia kizazi hiki na vingi vijavyo,
kumjua Mungu na kuzijua njia za Mungu ili kuishi maisha ya ushindi na
mguso. Pastor Eskaka Chaula amepata Neema ya kuoa mke mwenye akili,
anayesimama naye kwenye maono makubwa ya kuujaza ulimwengu na
maarifa ya Bwana, Evelyn Eskaka Chaula.

Kama umeguswa na kuvushwa mahali kwa kupitia kitabu hiki karibu kwa
ushuhuda au sadaka kwa Tigopesa [+255(0)718578313, Eskaka Chaula],
lakini pia kujifunza neon la Mungu kuhusu kila eneo la maisha nifatilie
kupitia mitandao ya kijamii yote, Facebook, Instagram, Telegram, TikTok
na YouTube account zote kwa jina moja la Pastor Eskaka Chaula.

PASTOR ESKAKA CHAULA 68


USHINDI DHIDI YA KUJICHUA NA PORNOGRAFIA

PASTOR ESKAKA CHAULA 69

You might also like