You are on page 1of 3

Vitate, Vitawe na Visawe

Baadhi ya maneno ya Kiswahili yanaweza kuwa na maana sawa, maana zaidi ya moja au
matamshi yanayotatiza. Vikundi hivi vitatu ni:

1. Vitate - maneno yanayotatiza kimatamshi. ⇒ Vitate hutatiza kimatamshi


2. Vitawe - maneno yenye maana zaidi ya moja. ⇒ Vitawe hugawanywa kwa matawi au
maana zaidi
3. Visawe - maneno tofauti yenye maana sawa. ⇒ Visawe huwa na maanasawa ''

Vitate

Maneno yanayotatiza kimatamshi.

1. ndoa na doa :
1. ndoa ⇒ kuungana kwa watu wawili na kuishi pamoja kama mume na mke
2. doa ⇒ alama ya uchafu, kasoro au dosari
2. baba na papa :
1. baba ⇒ mzazi wa kiume
2. papa ⇒ mnyama wa baharini
3. fua na vua :
1. fua ⇒ osha nguo, tengeneza vyuma
2. vua ⇒ shika samaki kutoka majini; toa nguo
4. faa na vaa :
1. faa ⇒ inayostahili, inayopaswa
2. vaa ⇒ weka nguo juu ya mwili
5. ngoma na goma :
1. ngoma ⇒ ala ya muziki itoayo sauti inapopigwa
2. goma ⇒ acha kufanya kazi
6. shinda na shida :
1. shinda ⇒ ongoza katika makabiliano, mashindano
2. shida ⇒ taabu au matatizo
7. shindano na sindano :
1. shindano ⇒ makabiliano baina ya watu wawili au zaidi ili kutambua
atakayeongoza
2. sindano ⇒ kifaa kinachotumika kushonea vitu
8. pinga na piga :
1. pinga ⇒ kutokubaliana na jambo fulani
2. piga ⇒ kugonga au kuchapa
9. fahali na fahari :
1. fahali ⇒ ng'ombe wa kiume. pia ndume
2. fahari ⇒ kujivunia, furaha
10. haba na hapa :
1. haba ⇒ kisichokuwa kingi
2. hapa ⇒ mahali karibu

Vitawe
Mano yenye maana zaidi ya moja

1. paa :
1. kwea (enda juu)
2. mnyama wa porini anayefanana na mbuzi
3. sehemu ya juu ya nyumba
2. shinda :
1. kaa au ishi mahali/wakati fulani
2. ongoza katika shindano
3. tupu
3. kaa :
1. sehemu yenye moto ya kuni
2. mnyama wa majini
3. keti chini
4. kuwa mahali fulani kwa muda
4. mbuzi :
1. mnyama anayefugwa kama ng'ombe
2. chombo cha kukunia nazi
5. mlango :
1. ukoo au watu wenye asili smoja
2. sehemu ya kuingia kwenye nyumba
3. kitu kinachotumika kifunga nyumba
6. fua :
1. unda vyombo/vifaa mbalimbali kwa kupiga chuma
2. osha nguo
7. vua :
1. toa nguo kutoka mwilini
2. toa samaki kwenye maji
8. kiboko :
1. mnyama mkubwa wa baharini
2. silaha inayotumika kwa kuchapa au kupiga
9. tembo :
1. aina ya ndovu
2. aina ya pombe

Visawe

Maneno tofauti yenye maana sawa.

1. msichana au banati : ⇒ kijana wa jinsia ya kike


2. mvulana au ghulamu : ⇒ kijana wa jinsia ya kiume
3. fahali au ndume : ⇒ anayesoma, anayefundishwa
4. huzuni au majonzi : ⇒ hali ya kilio na huruma
5. mazishi au matanga : ⇒ shughuli za kumzika marehemu
6. wakati au mwia : ⇒ wakati au muda
7. mtu au mja : ⇒ mnyama atembeaye kwa miguu miwili mwenye uwezo wa kuongea
na kufikiri kimantiki
8. barua au waraka : ⇒ kartasi inayoandikwa na kutumwa ili kuwasilisha ujumbe
fulani
9. siri au faragha : ⇒ jambo lisilopaswa kujulikana na mtu mwengine
10. macho au maninga : ⇒ sehemu za mwili zinazotumika kuangalia na kuona
11. mwangaza au nuru : ⇒ miyale inayowezesha watu kuona vitu

Mungu au Mola au Rabana au Jalali au Rabuka : ⇒ Majina ya Mwenyezi Mungu

You might also like