Professional Documents
Culture Documents
Vitate Visawe Vitawe
Vitate Visawe Vitawe
Baadhi ya maneno ya Kiswahili yanaweza kuwa na maana sawa, maana zaidi ya moja au
matamshi yanayotatiza. Vikundi hivi vitatu ni:
Vitate
1. ndoa na doa :
1. ndoa ⇒ kuungana kwa watu wawili na kuishi pamoja kama mume na mke
2. doa ⇒ alama ya uchafu, kasoro au dosari
2. baba na papa :
1. baba ⇒ mzazi wa kiume
2. papa ⇒ mnyama wa baharini
3. fua na vua :
1. fua ⇒ osha nguo, tengeneza vyuma
2. vua ⇒ shika samaki kutoka majini; toa nguo
4. faa na vaa :
1. faa ⇒ inayostahili, inayopaswa
2. vaa ⇒ weka nguo juu ya mwili
5. ngoma na goma :
1. ngoma ⇒ ala ya muziki itoayo sauti inapopigwa
2. goma ⇒ acha kufanya kazi
6. shinda na shida :
1. shinda ⇒ ongoza katika makabiliano, mashindano
2. shida ⇒ taabu au matatizo
7. shindano na sindano :
1. shindano ⇒ makabiliano baina ya watu wawili au zaidi ili kutambua
atakayeongoza
2. sindano ⇒ kifaa kinachotumika kushonea vitu
8. pinga na piga :
1. pinga ⇒ kutokubaliana na jambo fulani
2. piga ⇒ kugonga au kuchapa
9. fahali na fahari :
1. fahali ⇒ ng'ombe wa kiume. pia ndume
2. fahari ⇒ kujivunia, furaha
10. haba na hapa :
1. haba ⇒ kisichokuwa kingi
2. hapa ⇒ mahali karibu
Vitawe
Mano yenye maana zaidi ya moja
1. paa :
1. kwea (enda juu)
2. mnyama wa porini anayefanana na mbuzi
3. sehemu ya juu ya nyumba
2. shinda :
1. kaa au ishi mahali/wakati fulani
2. ongoza katika shindano
3. tupu
3. kaa :
1. sehemu yenye moto ya kuni
2. mnyama wa majini
3. keti chini
4. kuwa mahali fulani kwa muda
4. mbuzi :
1. mnyama anayefugwa kama ng'ombe
2. chombo cha kukunia nazi
5. mlango :
1. ukoo au watu wenye asili smoja
2. sehemu ya kuingia kwenye nyumba
3. kitu kinachotumika kifunga nyumba
6. fua :
1. unda vyombo/vifaa mbalimbali kwa kupiga chuma
2. osha nguo
7. vua :
1. toa nguo kutoka mwilini
2. toa samaki kwenye maji
8. kiboko :
1. mnyama mkubwa wa baharini
2. silaha inayotumika kwa kuchapa au kupiga
9. tembo :
1. aina ya ndovu
2. aina ya pombe
Visawe