You are on page 1of 2

MKATABA WA UPANGAJI

Mkataba huu wa leo tarehe 05/04/2024


BAINA
MOHAMED ALI SALIM wa S.L.P 19180, Dar es salaam (ambaye katika
mkataba huu ataiwa "MWENYE NYUMBA" kwa upande wa kwanza,
NA
ABDIKADIR HASSAN wa mobile No. 0744163208 Dar es Salaam (ambaye
katika mkataba huu ataitwa "MPANGAJI") kwa upande wa pili.
KWA VILE mwenye nyumba anamiliki nyumba No. 18 plot No. 06 Mtaa wa
Pemba/Livingstone, Kariakoo, Wilaya ya Ilala, Dar es salaam (Ambayo
kwenye mkataba huu itaitwa "Nyumba hiyo") na anataka kumpangisha
Mpangaji, ghorofa ya tano apartment Na.1 kwa ajili ya kuishi.
HIVYO MKATABA HUU UNASHUHUDIWA YAFUATAYO:
1. Mwenye nyumba kwa hiari yake amekubali kumpangisha mpangaji
ghorofa ya tano apartment No.1 kwa ajili ya kuishi, na mpangaji hiyari
yake amekubali kupanga nyumba hiyo kwa kipindi cha miezi 12. Kuanzia
tarehe 05/04/2024 mpaka tarehe 04/05/2025. Na amelipa kodi ya miezi
sita.
2. Kodi ya nyumba itakuwa 500,000/= (Laki tano tu) kwa mwezi, na kwa
miezi sita itakuwa Tsh 3,000,000/= (Milioni tatu tu).
3. Mpangaji atatumia nyumba hiyo kwa ajili yakuishi.
MPANGAJI ANAWAJIBIKA KUFANYA YAFUATAYO
i. Kulipa kodi kama alivyokubaliana na mwenye nyumba katika mkataba
huu.
ii. Atalipa gharama za umeme atakaotumia.
iii. Mpangaji haruhusiwi kupangisha mtu mwingine sehemu aliyopanga
bila kupata idhini ya maandishi kutoka kwa mwenye nyumba.
iv. Mpangaji hatafanya matengenezo yoyote kwenye sehemu aliyopanga
bila kupata kibali kutoka kwa mwenye nyumba.
v. Mpangaji atahusika mwenyewe kwenye marekebisho ya kitu chochote
ambacho kitaharibika.
vi. Mpangaji itamlazimu sehemu hiyo aliyopanga pamoja na mazingira
wakati wote, sehemu ya nyumba aliyopanga pamoja na mazingira ya
ndani na nje ni safi na ipo katika hali ya kuridhisha.
vii. Baada ya muda wa mkataba kumalizika iwapo mpangaji atataka
kuendelea au kutoendelea na upangaji katika sahemu hiyo itabidi utoe
taarifa ya mwezi mmoja (1) kabla ya muda wa upangaji haujamalizika
kwa mwenye nyumba na atawalazimu wakubaliane upya na kwa
mkataba. Hali kadhalika na mwenye nyumba itabidi atoe notice ya
mwezi mmoja (1) kwa mpangaji kama ataamua kumtoa.
viii. Kwamba mpangaji atakapomaliza muda wake atakabidhi sehemu
aliyopanga bila ya kuvunja au kuharibu sehemu yoyote ya fremu hiyo.
ix. Mkataba utatawaliwa na sheria za Tanzania.

KWA KUTHIBITISHA MAKUBALIANO HAYA WAHUSIKA


WAMETIA SAINI MKATABA HUU KAMA IFUATAVYO:-
IMETIWA saini hapa Dar es salaam na
MOHAMED ALI SALIM
Ambaye ninamfahamu leo hii tarehe:
____ Mwezi ____ Mwaka _______ _________________________
Saini _____________________________ MWENYE NYUMBA
Anuani____________________________

IMETIWA saini hapa Dar es salaam na


ABDIKADIR HASSAN
Ambaye ninamtahamu leo hii tarehe:
____Mwezi _______Mwaka ______ ________________________
Saini__________________________ MPANGAJI
Anuani________________________

You might also like