You are on page 1of 4

MKATABA WA KUPANGISHA CHUMBA

BAINA YA

MALIDAVIS INVESTMENT LTD

(MPANGISHAJI)

NA

………………………………………………

(MPANGAJI)
Huuu ni mkataba wa leo ……………………. mwezi ………………….mwaka 20……………
BAINA YA
MALIDAVIS INVESTMENT LTD S.L.P 669, ARUSHA , (ambaye kwa minajili ya mkataba
huu atajulikana kama "mpangishaji') kwa upande mmoja.
NA
……………………………………………………………….mwenye namba ya simu ……………………….
(ambaye kwa minajili ya mkataba huu atajulikana kama "MPANGAJI" Kwa upande
mwingine.
WAHUSIKA WA MKATABA HUU WANAKUBALIANA KAMA IFUATAVYO:
1.0 MAELEZO YA NYUMBA
1.1 Sehemu ya nyumba inayopangishwa ni chumba chenye choo pamoja na
sehemu ya kupikia, katika nyumba namba 4 iliyopo Njiro Seminari, block
C1, kwa mjibu wa mkataba huu kitajulikana kama CHUMBA.
1.2 Kwamba, MPANGISHAJI anampangishia mpangaji kwa ajili ya Makazi na
kwamba taratibu za kupangisha nyumba zinazofahamika kisheria zifuatwe.
1.3 Kwamba,Mpangaji haruhusiwi kumpangishia mtu mwingine ila tu
ataitumia kwa matumizi yaliyoainishwa kwenye kipengele 1.2 Hapo juu.
2.0 MALIPO YA KODI YA PANGO KWA MWENYE NYUMBA
2.1 Kodi ya pango kwa kipindi cha kuanzia tarehe …………………. Hadi tarehe
…………………. ni shilingi ……………………….. na mpangaji atalipa kiasi hicho
kabla ya kusaini mkataba.
2.2 Mpangaji atawajibika kulipa gharama za umeme anaotumia pamoja na
kuchangia gharama za maji, ulinzi na usafi kama itakavyopangwa.
2.3 Mpangaji ataweka kiasi cha kodi ya mwezi mmoja kama dhamana, ambacho
kitarudishwa siku anakabidhi chumba kama hakuna uharibifu wowote
uliofanywa na mpangaji. Kama kuna uharibifu wa chumba au vifaa
vilivyopo chumbani au kwenye mazingira uliofanywa na mpangaji, basi
kiasi cha dhamana kitatumika kufidia uharibifu huo na kama uharibifu ni
mkubwa kuliko kiasi cha dhamana, mpangaji atalazimika kuongeza kiasi
cha pesa kufidia gaharama za uaharibifu.
3.0 MDA WA MKATABA
3.1 Mkataba ni wa miezi …… unaoweza kuongezwa baada ya pande zote
kuridhia. Mkataba unaweza kuvunjwa kwa kutoa taarifa mwezi mmoja
kabla au kulipa kodi ya mwezi mmoja kwa upande unaokusudia kuvunja
mkataba.

4.0. MAJUKUMU YA MPANGAJI


Mpangaji anaweka ahadi kwamba atakuwa na majukumu yafuatayo katika
kipindi chote cha mkataba huu:
4.1 Kumlipa mwenye nyumba kodi ya pango anayopaswa kulipa kwa
kuzingatia masharti yaliyoko kwenye kipengele cha 2 chaa mkataba huu.
4.2 Mpangaji atatakiwa kutunza nyumba ikiwa ni pamoja na kufanya usafi na
kuhifadhi /kutunza mazingira yawe katika hali nzuri, iii nyumba iwe katika
mazingira mazuri na endelevu yanayofaa kwa matumizi ya mwanadamu.
4.3 Kumruhusu mwenye nyumba au wakala wake kuingia kwenye eneo la
nyumba aliyopangishiwa kwa lengo la kuangalia na kufanya marekebisho
wakati wowote baada ya mwenye nyumba kutoa taarifa kwa mpangaji.
4.4 Kulipa bili zote za maji (maji safi na maji taka), taka, usafi, umeme na
gharama nyingine zote ambazo anapaswa kulipa kwa muda wote wa
mkataba isipokuwa tu zile ambazo mwenye nyumba anapaswa kulipa kwa
mujibu wa sheria.
4.5 Kutoa taarifa kwa wakati kwa mwenye nyumba kuhusu tatizo lolote lililoko
kwenye jengo ambalo ni jukumu au wajibu wa mwenye nyumba
kulishughulikia iii mwenye nyumba aweze kulifanyia kazi.
4.6 Kuwa mwangalifu na mwadilifu katika kutekeleza mkataba huu na
kuhakikisha kwamba hataacha deni lolote analodaiwa wakati wa kukabidhi
chumba kwa mwenye nyumba.
4.7 Kutosumbua wapangaji wengine kwa kelele zozote au tabia zingine
zinazokera
4.8 Kutumia nyumba kwa matumizi ya kuishi tu na si matumizi mengine
yeyote.
5.0 MAJUKUMU YA MWENYE NYUMBA
5.1 Mwenye nyumba atakuwa na jukumu la kuhakikisha kuwa chumba kiko
katika mazingira mazuri yanayofaa kwa matumizi ya makazi kabla
mpangaji kuingia kwenye chumba katika kutekeleza mkataba huu.
5.2 Kuingia na kukagua hali ya chumba, lakini katika kufanya hivyo mwenye
nyumba hatasababisha usumbufu usio wa lazima kwa mpangaji.
5.4 Kufanya marekebisho ambayo watakubaliana na mpangaji na
kushughulikia matatizo yaliyowasilishwa kwake na mpangaji.

6.0 MASHARTI YA KUZINGATIA


6.1 Mpangaji hatoruhusiwa kufanya marekebisho yoyote ya nyongeza katika
jengo analopangishiwa bila kupata ruhusa ya maandishi kutoka kwa
mwenye nyumba na endapo atafanya hivyo bila ruhusa ya mwenye jengo
atakuwa amekiuka mkataba na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
6.2 Bila kuathiri masharti ya kipengele cha 6.1 hapo juu mpangaji anaweza
kufanya marekebisho madogo ambayo sio jukumu la mwenye nyumba
kwa mfano kuweka balbu iliyoungua.

Mpangishaji……………………………………………. Mpangaji:……………………………………………...

You might also like