You are on page 1of 4

PETE YA ORISHA MMILIKI WA BAHARI “ OLOKUN”

Bahari inachukua asilimia 71 ya sehemu ya dunia, na asilimia 97 ya maji ya dunia yapo


baharini, kwasababu hii bahari ina athari kubwa kwa hali ya hewa, halijoto na upatikanaji wa
chakula cha binadamu pamoja na viumbe hai wengine, dunia ina bahari moja tu ambayo kabla
haijatengana na kupewa majina mengi ilikuwa ikiitwa Panthalassa lakini oceanographers yaani
wataalamu wa maswala ya baharini pamoja na tawala za mataifa mbalimbali wakaigawa bahari
katika maeneo manne, bahari ya pacific, atlantic,indian na arctic,japokuwa mwanzoni mwa karne
ya 20 oceangraphers waliita bahari iliyopo kwenye bara la antaktika kama bahari ya kusini na
ulipofika mwaka 2021 watafiti wa national geographic waliitambua bahari ya kusini kama bahari
ya tano.
Licha ya umuhimu wa bahari kwa maisha ya kila kiumbe hai kilichopo duniani lakini bahari
bado ni fumbo kubwa kwa binadamu , pamoja na chunguzi nyingi za muda mrefu zilizofanywa
na wanasanyansi lakini hadi sasa zaidi ya asilimia 80 ya bahari haijawahi kufikiwa na binadamu,
kuchunguzwa wala hata kuonwa na binadamu yeyote, binadamu ameweza kutafiti mwezi , nyota
pamoja na sayari nyingi lakini ameshindwa kuitafiti bahari , wanasayansi wanaamini asilimia 90
ya viumbe vilivyopo baharini bado havijulikani
Kipo kisa cha mtume Muhammad kilichosimuliwa na wanazuoni wa kiislamu kinachowafanya
wengi waamini kuwa makazi ya shetani yapo baharini, walidai mtume Muhammad siku moja
alimuuliza ibn sayaad kuwa anaona nini baharini, na ibn sayaad akajibu anaona kiti cha enzi
katika bahari kikiwa kimezungukwa na wafuasi …na mtume Muhammad akamwambia Ibn
Sayaad kuwa hicho ni kiti cha enzi cha Ibilisi
Leo katika darasa la Maalim shafii the don, tunaingia ndani ya kina kirefu cha bahari, mahali
ambako mwanga wa jua hupenyezi ,ndani ya giza kuu la dunia kwenye ukimya na upweke
pamoja na nguvu ya kiungu, kumtafuta kiumbe aliyefungwa minyororo ya amri na muumba ili
hasira yake isije kuangamiza binadamu aliyekosa maadili, tunaingia kwa baba wa bahari,
mtawala wa kila kilichomo baharini, jina lake anaitwa olokun ,olo likiwa na maana ya mmiliki
na neno “okun” likiwa na maana ya bahari, karibu tumfahamu mmiliki wa bahari pamoja na pete
yake.

Awali ya yote napenda kuwakumbusha wale wanaotaka utajiri juu ya pete na mafuta ya mami
wata , kwa wale wanaotaka kusafisha njia zao za kipato na kujiondolea vifungo vya kimaisha
pamoja na kung’arisha nyota zao usipitwe na mafuta ya awla bulbul, kwa wale wenye kuhitaji
elimu za tiba asili na kufahamu mambo yanayofanyika katika ulimwengu wa siri usithubutu
kupitwa na vitabu vya Maalim shafii the don.
kuwasiliana na Maalim shafii the don usisite kumpigia simu katika nambari yake inayoanza na
+255 692 007 575. Karibu
Olokun ndiye mtawala wa maji na roho wote wa majini, ana mamlaka juu ya vyote vilivyo
ndani na karibu ya maji. Mwenye uwezo wa kutoa mali, afya, na ustawi wa kila nyanja. Olokun
ni Orisha au roho yenye uungu inayosimamia kuingiza roho ulimwenguni na kuziongoza katika
maisha ya baada ya kifo.
Pia anajulikana kama jini wa kifalme mwenye utajiri mkubwa na ana baraza la majini
wanaomshauri akiwemo yemaya , mami wata na oshun ambao mara nyingi hufanya kazi kama
mawaziri wake, Wafuasi wa Olokun wanaamini kuwa roho huyo anaishi chini kabisa ya bahari
mahala ambako hata mwanga wa jua haupenyezi
Olokun huoneshwa kama samaki mtu na wakati mwingine jinsia yake huwa ni tata, wapo
wanaoamini ni mwanamke na wapo wanaoamini ni mwanaume, huenda hii ni kwasababu mara
nyingi humtumia mke wake yemaya kumuwakilisha katika kazi zake, ni jini msiri na asiye
patikana kirahisi rahisi hivyo wengi hawamjui vyema,
kama kila Orisha , Olokun ana asili ya duality yaani uwili ~ anajulikana kama chanzo cha
uzaliwaji wa viumbe hai vyote ikiwemo mimea, na pia anajulikana kama mwenye mamlaka ya
ulimwengu wa wafu. Kama ilivyo kwa dunia, wayoruba walikuwa wakiamini kuwa vitu vingi
asili yake ni baharini na hata mwisho wake kuishia baharini , wayoruba wanaamini pia Mungu
alipoiumba bahari , papo hapo akatokea na mmiliki wa bahari ama kwa jina la kiyoruba Olokun
ambae hasira yake juu ya matendo ya binadamu ndio hupelekea kutokea kwa tsunami.
wanasayansi wa hivi sasa wanaamini kuwa viumbe hai wa kwanza kabla ya binadamu viliibuka
kutokea baharini , majibu ya tafiti zao yanazua mafumbo mengi zaidi na kuwalazimisha
wanasayansi wazidi kutafiti siri za bahari.
Kwa maana hiyohiyo hata binadamu anazaliwa kutoka kwenye tumbo la mama na ndani ya
mfuko wa ujauzito kuna kioevu amniotic au amniotic fluid , majimaji yenye chumvi
yanayomzunguka mtoto na kulinda ukuaji wake hadi kuzaliwa hilo linafanya maji na chumvi
yaonekane kuwa na nguvu ya uumbaji na binadamu ana mahusiano na bahari.
Wayoruba wanaamini chini ya kina cha bahari, lipo eneo ambalo roho ya binadamu ni lazima
ivuke baada ya kufa au kabla ya kuzaliwa, imani hiyo inafanana na imani ya wachina juu ya mto
wa wang chuan uliopo katika ulimwengu wa kiroho, Wayoruba wanaamini Olokun ndio mwenye
mamlaka ya ulimwengu huo.
Wayoruba wanaamini kuwa baada ya Mungu kuumba kila kitu, miungu mingi iliishi mbinguni
lakini Olokun hakuwahi kuiacha bahari na kutimiza majukumu yote aliyopangiwa hivyo Mungu
muumba akampa mamlaka ya juu zaidi kwa baharini kuliko Orisha mwingine yoyote.
Kwakuwa utajiri wa dunia ni sawa na punje ya mchele ukilinganisha na utajiri uliopo
baharini,Olokun anafahamika kama Mungu mkuu wa utajiri kwa tamaduni nyingi za kiafrika na
watu wa jamii tofauti ikiwemo Cuba hufanya maagano na Olokun pamoja na kuvaa Vidani vya
cheni , pete na bangili zilizotengenezwa kwa nishati na roho ya Olokun ili kuvuta utajiri wa
bahari.
Olokun anaonekana kama mmoja wa Waorisha waliostahimili zaidi katika dini ya Kiyoruba,
Olokun ana mtoto ambaye pia ni mungu wa utajiri mwenye kufanya kazi badala ya baba yake,
naye anaitwa Aje Olokun. Roho wote wenye asili ya uzao wa Olokun hawatambulikagi jinsia
kwasababu wanaweza chukua umbile lolote wanalolitaka, hata baba yao Olokun akitokea katika
umbile halisi huvaa vazi lenye rangi za bluu za aina tisa kama samawati,samawati ya
kigiza,samawati ya kifalme,aguamarine nakadharika, kwa ujumla zipo aina 50 za rangi za bluu,
vazi hilo alivaalo Olokun huficha umbile lake na usoni huvaa kinyago , pia Olokun huvaa
mkufu wenye shanga ambao una matumbawe na rangi ya maziwa , kijani kibichi na bluu
iliyokolea. Nambari zake ni saba na tisa.
Wazaliwa wote wa Olokun pia ni Wamiliki wa utajiri wa baharini. Wanaishi kwenye kina kirefu
cha bahari, mahala penye furaha kubwa . Olokun ni Orisha mwenye shauku na amri , ana sifa ya
uvumilivu, nguvu, hasira na hekima, wafuasi wanaomjumuisha Olokun katika maombi yao,
hupewa ulinzi na mwongozo wa kimaisha
Maalim Shafii the don anasema ukimuita Orisha huyu na kufanya naye maagano basi unatakiwa
kujua kuwa sadaka zake hupelekwa baharini kila mwaka . Watu humuita na kuomba ujuzi wa
mambo, kupata afya kutokana na magonjwa, kupata baraka, utajiri nakadharika. Sadaka
anazopendelea ni bukini wanaofanana na bata maji ,bata wa kawaida, njiwa, kanga , nguruwe, na
jogoo lakini pia unaweza kumuahidi unachoweza kukitoa kama sadaka sharti utimize
unachokiapia . Roho wote wa uzao wa Olokun Wanapenda matunda ya aina zote hasa matikiti
pamoja na chakula cha viazi vikuu vilivyopikwa. Maalim anasema ukipewa utajiri wa Olokun
unatakiwa kutimiza ahadi utakazoapa kumpa kama sadaka, kama hutotimiza ahadi yako unaweza
kwenda na maji
Njia nyingine ya kumwita Olokun ni kutandaza leso nyeupe kwenye madhabahu yako. Kisha
weka mdoli wa Olokun au sanamu kwenye leso. Maalim anasema utaweka na unga wa uvumba
wa Yemaya, unga wenye maajabu kwelikweli, kisha unga huo utie kwenye mkaa na uwashe.
Mara tu uvumba ukiwashwa, unaweza kuanza kutoa sadaka yako kwa Olokun.
Maalim pia anasema ukiwa na pete ya Olokun halafu ukiwa na uvumba wa yemaya unaweza
kufanya mambo ya ajabu kwelikweli ila hiyo ni mada ya siku nyingine.
Mara nyingi matambiko ya Olokun hufanyika kila mwaka , sanasana huko nchini Nigeria
pamoja na nchi zenye dini ya Kiyoruba.mfano katika Jimbo la Lagos, hufanya sherehe za
Olokun katika mwezi wa Novemba. Ukienda Edos, katika mji Usonigbe utakuta hekalu kubwa
la Olokun, wao husherehekea na kufanya ibada kuu za Olokun mwishoni mwa mwezi wa
Februari.
Na huu ndio mwisho wa darasa la Maalim shafii the don

You might also like