Professional Documents
Culture Documents
Askofu/Padre: Uwajalie watu wote paji lako la imani ya kuwa Wewe upo. Utupe
hekima ya kutafuta ukweli katika mambo yote, na kuishi kwa uaminifu katika amri
zako.
Kiitikio: Ee Bwana uibariki nchi yetu.
Askofu/Padre: Uwaongoze viongozi wetu wote ili watimize wajibu na kazi zao
sawasawa.
Kiitikio: Ee Bwana uibariki nchi yetu.
Askofu/Padre: Utufadhili sisi sote kufikia kipeo ulichotutayarishia, yaani kuwa raia
katika ufalme wa mbinguni, unapoishi na kutawala daima na milele.
Wote: Amina.
Padre: Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, kwa moyo wote tunakukabidhi pia
kanisa takatifu katoliki katika nchi zetu. Tunaweka chini ya ulinzi wako wewe Mama
mwajibikaji, kila Jimbo na kila Parokia ili waumini wote wanapokutana pamoja na
wachungaji wao, kwa nguvu ya Roho Mtakatifu, kwa Nguvu ya injili na adhimisho
la Sadaka ya Ekaristi Takatifu, Kanisa takatifu katoliki la Kitume, lake Yesu Kristo.
Padre: Maria Mama yetu, Upokee tendo hili la kuziweka nchi zetu chini ya ulinzi
wako, na utujalie kupata hayo tunayoomba kutoka kwa moyo wa Mwanao, Bwana
wetu Yesu Kristo. Amina.
SALAMU MALKIA
Salamu Malkia, Mama mwenye huruma, uzima, tulizo na matumaini yetu, salamu.
Tunakusihi ugenini hapa sisi wana wa Eva. Tunakulilia tukilalamika na kuhuzunika
bondeni huku kwenye machozi. Haya basi, Mwombezi wetu, utuangalie kwa
macho yako yenye huruma. Na mwisho wa ugeni huu, utuoneshe Yesu, mzao
mbarikiwa wa tumbo lako. Ee mpole, ee mwema, ee mpendelevu, Bikira Maria.
Tuombe:
Ee Mungu, makimbilio na nguvu yetu, uwaangalie kwa wema watu wanaokulilia;
na kwa maombezi ya Bikira Maria mtukufu asiye na kosa, Mzazi wa Mungu, na ya
Mtakatifu Yosefu, mchumba wake, na ya Watakatifu Petro na Paulo Mitume wako,
na ya Watakatifu wote: usikilize kwa Huruma na wema sala tunazokutolea kwa
wongofu wa wakosefu na kwa uhuru na utukufu wa Kanisa, mama mtakatifu.
Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
Amina.