You are on page 1of 1

Pia akafanya vilevile kuhusu kikombe kisha wao kula chakula cha mangaribi, na kusema: “Kikombe hiki

kinamaanisha agano jipya kwa musingi wa damu yangu, yenye itamwangwa kwa ajili yenu.

waroma 5: 12 Hiyo ndiyo sababu, kama vile kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo
kupitia zambi, na ni vile kifo kilienea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi

waroma 5:19 Kwa maana kama vile kupitia kukosa kutii kwa ule mutu mumoja wengi walifanywa kuwa
watenda-zambi, vilevile pia kupitia kutii kwa mutu mumoja wengi watafanywa kuwa wenye haki

ufunuo 14: 1 Kisha nikaona, na angalia! Mwana-Kondoo amesimama juu ya Mulima Sayuni, na pamoja
naye watu elfu mia moja makumi ine na ine (144000) wenye kuwa na jina lake na jina la Baba yake likiwa
limeandikwa kwenye mapaji ya nyuso zao.

1wakorinto 11:23,24 Kwa maana nilipokea kutoka kwa Bwana kile chenye niliwapatia ninyi pia, kwamba
Bwana Yesu katika usiku wenye angesalitiwa, alichukua mukate,

24 na kisha kutoa shukrani, akauvunja na kusema: “Huu unamaanisha mwili wangu, wenye uko kwa ajili
yenu. Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”

25 Akafanya vilevile na kikombe pia, kisha wao kula chakula cha mangaribi, akisema: “Kikombe hiki
kinamaanisha agano jipya kwa musingi wa damu yangu. Muendelee kufanya hivi, kila wakati wenye
munakikunywa, kwa kunikumbuka mimi.”

2 wakorinto 5:14, 15 Kwa maana upendo wenye Kristo iko nao unatulazimisha, kwa sababu tumefikia
uamuzi huu, kwamba mutu mumoja alikufa kwa ajili ya watu wote; kwa hiyo basi, watu wote walikuwa
wamekufa. 15 Na alikufa kwa ajili ya watu wote ili wale wenye wanaishi wasiishi tena kwa ajili yao
wenyewe, lakini kwa ajili ya ule mwenye alikufa kwa ajili yao na akafufuliwa.

You might also like