Professional Documents
Culture Documents
Fasihi
Fasihi
YALIYOMO
Williady, (2015) Fasihi ni tawi moja wapo la sanaa linalotumia lugha katika
kuwasilisha ujumbe wa mdomo au wa maandishi.
MAANA YA SANAA
(Williady: 2015) Sanaa ni ujuzi au ufundi wenye kuleta manufaa kwa uma.
UMBO LA SANAA
Fasihi Simulizi
Fasihi Andishi
Namna ya uwasilishaji wake. Fasihi simulizi huwasilishwa kwa njia yam domo
wakati fasihi andishi uwasilishwa kwa njia ya maandishi.
Vidato na elimu. Fasihi simulizi haiitaji mtu ajue kusoma ama kuandika,
inamuhitaji mtu mwenye uwezo wa kuzungumza. Fasihi andishi inamhitaji mtu
anayejua kuandika na kusoma.
Idadi ya tanzu. Fasihi simulizi inatanzu nyingi zaidi kuliko fasihi andishi.
Kuhifadhi. Hapo kale fasihi simulizi ilihifadhiwa kichwani, kwa sasa
fasihi simulizi yaweza kuhifadhiwa katika vinasa sauti, kaseti na santuri. Fasihi
andishi yenyewe huifadhi wake ni kwa njia ya maandishi.
1.Fasihi simulizi
Ngano, vigano, hekaya, soga, tarihi, visa, visasili, shajara, istiala, michapo
na mbazi
AINA ZA NYIMBO
Bembezi, nyimbo za mapenzi, nyiso, nyimbo za jadi, nyimbo za harusi, nyimbo
za watoto nyimbo za sifa, nyimbo za kampeni, nyimbo za maombolezo na
nyimbo za chombezi.
A) Dhima na maudhui
C) Kusisimua
D) Urudufishaji
E) Chombezo
F) Nyimbo
Nyimbo zina kazi nyingi katika masimulizi ya hadithi. Moja wapo ya
matumizi hayo ni kama vile kuondoa uchovu kwa wasikilizaji, kuvuta
usikivu, kuwakaririsha hadhira falsafa au lengo kuu la hadithi hiyo.
MAMBO MENGINE
b) Ujenzi wa wahusika
d) Ujenzi wa taswira
2. FASIHI ANDISHI
RIWAYA (NATHARI)
USHAIRI (NUDHUMU)
FANI
Fani ni ufundi unaotumiwa na msanii katika kufikisha ujumbe
uliokusudiwa, fani sio ujumbe bali ni mfano wa kipaza sauti kinachotumika
kufikisha ujumbe.
a) Muundo
b) Mtindo
c) Mandhari
e) Matumizi ya tamathali za
semi(usemi)
e) Wahusika
DHAMIRA
UJUMBE
FALSAFA
MAFUNZO
MIGOGORO
Mgogoro wa nafsi
VI. MTAZAMO
METHALI ZA KISWAHILI
“A”
2. Adui mpende
8. Akiba haiozi
9. Akili ni mali
“B”
“C”
“E”
“F”
“G”
“I”
“J”
“K”
160. Kiwi cha Yule, ni chema cha Yule, hata ulimwengu wishe
“L”
“M”
287. Mnywa maji kwa mkono mmoja, kiu yake I pale pale
0762 – 957493
0768 – 625660
hwilliady@ymail.com
majumbeni@gmail.com
Athari za Ubinafsi
Ubinafsi ni hali au tabia ya mtu au watu wachache kufanya vitendo au vitu
fulani ili kuweza kujinufaisha wao wenyewe bila kujali maisha ya wengine
(Muhura 2009: 81). Katika filamu ya Taswira, ubinafsi unajitokeza kwa
kumuangalia mhusika James ambaye anataka kutumia mali ya urithi kwa
manufaa yake binafsi bila kumshirikisha ndugu yake, Tamala. James anatumia
mali hii na mke wake Jesca, ambapo baadaye anapata fundisho kwa mkewe
Jesca kumkimbia baada ya kumfilisi. Pia ubinafsi unajitokeza kwa kumuangalia
mhusika Dkt Gumbo ambaye alijali maisha yake na ya familia yake tu, bila
kuwajalia wengine, yaani, Tamala na Trace ambao aliwapa ujauzito na
kuwatelekeza. Katika filamu hii ubinafsi unasababisha wahusika wengi
kutelekezwa, kuhangaika kwa mateso na hatimaye wengine kufa. Matokeo ya
ubinafsi wa James na Dkt. Gumbo yanasababisha maisha ya Tamala yawe ya
kuhangaika na kutangatanga, kwani mwishowe Tamala anarudi kijijini na kuishi
maisha ya taabu huku kaka yake (James) akitumia mali ya urithi pamoja na
Jesca, mkewe. Pia ubinafsi wa Dkt Gumbo ulisababisha Trace kufariki dunia.
Usaliti
Usaliti, ambao waweza kuhusisha utapeli na udanganyifu, ni dhamira ambayo
hutawala katika kazi mbalimbali za fasihi kama vile tamthilia, riwaya, hadithi
fupi na filamu. Katika filamu ya Taswira, dhamira hii inajidhihirisha kwa
kuwaangalia Jesca, Dkt. Gumbo, James na Trace. Jesca hakuwa na mapenzi ya
kweli kwa James. Nia yake ilikuwa kumfilisi, kwa kuuza mali zote na
kukimbilia Botswana na wanae, akimwacha James hana kitu. Kwa upande
mwingine, Dkt. Gumbo anamsaliti mkewe kwa kuwa na uhusiano wa
kimapenzi nje ya ndoa. Lakini hata nje pia anaishia kuwatelekeza anaowapa
ujauzito. Kwa mfano, anamtelekeza Tamala baada ya kumpa ujauzito. Vile vile
Dkt. Gumbo anamlaghai Trace kwamba atamsomesha na hatimaye anambaka na
kumtelekeza baada ya kumpa ujauzito.
Udanganyifu unaendelea kujitokeza pale ambapo Trace anamua kujihusisha
katika mapenzi na Sospeter ili aweze kumsingizia ujauzito aliopewa na Dkt.
Gumbo. Tatizo au hali kama hii ya kusingizia ujauzito inajitokeza katika jamii
ya Kitanzania. Wapo wanawake na wasichana ambao wanapewa ujauzito na
kujaribu kuwasingizia watu wengine ili waweze kupata matunzo. Hii hutokana
na kutelekezwa na anayehusika na ujauzito huo. Pia hali ngumu ya maisha
huwafanya wanawake na wasichana hao kufanya udanganyifu kama huo.
Madhara ya usaliti na udanganyifu katika ndoa au uhusiano kwa ujumla
yanaweza kufarakanisha familia kwa kuleta migogoro isiyokwisha na kurudisha
maendeleo nyuma kutokana na kukosa umoja kati ya watu. Kwa jumla, usaliti,
utapeli na udanganyifu katika uhusiano wa kimapenzi hutokea kwa kiwango
kikubwa katika jamii ya Kitanzania. Wapo wasichana wadogo na wanawake
ambao wamekumbwa na kuathirika na hali kama hii, na, imewasababishia
kukata tamaa na hatimaye kujiua wanapoona kuwa hawana pa kukimbilia. Hali
hii inawapata hasa wanawake wa umri mdogo ambao hawawezi kusimama peke
yao, na kwa kiasi fulani inatokea kwa watu wazima pia.
Ubakaji
Kubaka ni kitendo cha kufanya tendo la ngono na mtu bila ridhaa yake. Idadi ya
matukio ya ubakaji inayozidi kuongezeka kuripotiwa kwenye vyombo vya
habari inadhihirisha jinsi ubakaji ulivyo tatizo kubwa katika jamii ya Kitanzania.
Matukio hayo yanahusisha watu wazima wanaobaka watoto wadogo, vijana
wanaobaka vijana wenzao, watu wazima kubaka watu wazima wenzao, na
wanaume (na vijana) wanaobaka vikongwe. Katika filamu ya Taswira ubakaji
unajitokeza pale Dkt. Gumbo anapombaka Trace, na hatimaye, kumpa ujauzito
na kumtelekeza. Matukio ya ubakaji hutokea sehemu nyingi kama sehemu za
kazi na waathirika wengi ni wanawake, ambao huishia kupata mimba na
maradhi. Aidha, wanaume wabakaji hujiongezea nafasi za kupata maambukizi
ya magonjwa ya zinaa. Matatizo haya ya kubakwa, hutokea wakati wa kutafuta
nafasi za ajira, nafasi za masomo au misaada mbalimbali. Pia, upo ubakaji wa
vikongwe na watoto wadogo, ambao, huweza kufanyika kwa ajili ya imani za
kishirikina.
Vile vile, zipo kazi nyingine ambazo zinaonyesha athari za uigaji wa tamaduni
za kigeni. Kwa mfano, katika Wimbo wa Lawino uliotungwa na p’ Okot Bitek
(1975), Lawino ambaye alikuwa akidumisha mila na desturi za Kiafrika
anaonekana kumkosoa Clementine ambaye ameathiriwa na tamaduni za kigeni
kwa kuiga mtindo wa mavazi na nywele na hata kupaka rangi ya mdomo pamoja
na uvaaji kwa ujumla, (u.k. 39). Mwandishi anaonyesha jinsi Clementine,
mwanamke wa kisasa, anavyoiga utamaduni wa Kimagharibi ambapo
anawakilisha wanawake wengi ambao wanaiga mitindo ya uvaaji bila kujali
mila na desturi zao.
Jamii ya Kitanzania inawatarajia wanawake au akina dada kuvaa nguo ndefu ili
kujisitiri, lakini kutokana na utandawazi watu wanaiga utamaduni wa kigeni bila
kuangalia mazingira na madhara yake. Kwa ujumla athari za tamaduni za kigeni
zimeanza toka wakoloni walipoingia nchini Tanzania, tokea utawala wa Wareno,
Wajerumani na Waingereza. Lakini katika miaka ya hivi karibuni, hali hii
imezidi kuongezeka kutokana na utandawazi na kukua kwa teknolojia ya
vyombo vya habari na mfumo wa kijigitali. Kwa jumla, hali hii imeathiri sana
utamaduni wa Mtanzania kiasi kwamba tunashindwa kutofautisha utamaduni wa
Mtanzania ni upi na wa kigeni ni upi. Utamaduni wa Mtanzania umepoteza dira
kutokana na mwingiliano wa tamaduni. Athari hizi za tamaduni za kigeni
zimechangiwa na mataifa yanayoendelea kuiga mambo yanayoendelea katika
mataifa yaliyoendelea. Hii inajitokeza kwa kuangalia suala la utandawazi
ambapo mataifa yanayoendelea hulazimika kuiga mambo ambayo yako nje ya
utamaduni.
Katika jamii ya Kitanzania suala la malezi bora, utu, wema, heshima, hekima
yanatokea katika jamii yetu. Wapo wazazi ambao wanawalea watoto wao katika
malezi mazuri ambayo yanawafanya watoto hao kuwa na heshima na upendo
wa kujali wengine wenye shida. Kwa upande mwingine, wapo wazazi ambao
hawawalei watoto wao katika maadili na kuwasababishia kukosa upendo, moyo
wa kujali wengine na hatimaye kukosa heshima na hekima, kwani mtoto
umleavyo ndivyo akuavyo.
Katika filamu ya Taswira, hali hii inajidhihirisha pale ambapo Dkt. Gumbo
anafanya mapenzi na Tamala na kumsababishia ujauzito, hatimaye kumtelekeza
bila kufuatilia taarifa zozote za mama na mtoto. Hii inasababisha afanye
mapenzi na Trace na kumpa ujauzito bila kujua kwamba ni binti yake. Baadaye
Dkt. Gumbo anamwambia Trace atoe mimba hiyo kwa kuwa eti ingeleta
mgogoro katika ndoa yake. Trace hakubaliani na uamuzi wa Dkt. Gumbo kwa
sababu anajua athari za utoaji mimba. Hii inaonyesha kuwa alikuwa na elimu ya
kutosha kuhusiana na athari za utoaji mimba na anamwambia Dkt. Gumbo kuwa
amtafutie nyumba yake ya kuishi. Baada ya mke wa Dkt. Gumbo kupata taarifa
za ujauzito wa Trace anamlaghai Trace kwa kumpa dawa ambazo anadai kuwa
zingemsaidia katika ukuaji wa mimba. Badala yake dawa hizo ni za kutoa
mimba, na, zinamfanya Trace kupata maumivu makali na baadaye kupelekwa
hospitali na kufanyiwa upasuaji. Katika tukio hilo, madaktari wanafanikiwa
kumuokoa mtoto lakini, kwa bahati mbaya, Trace anapoteza maisha. Kifo cha
Trace kinaonyesha jinsi mabinti wanavyoweza kuhatarisha maisha yao kwa
kujaribu kunywa madawa ya kutoa mimba. Pia, inaonyesha jinsi wasichana
wanavyopata matatizo katika kulea mimba hizo kama vile kukosa matunzo,
kutelekezwa na hatimaye vifo.
Katika jamii ya Kitanzania suala la mimba nje ya ndoa na utoaji mimba
linatokea sana hasa kwa wasichana wa umri mdogo. Kama ilivyolezwa hapo
awali kuwa zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. Wasichana na
wanawake walioathirika na tatizo hilo wamefikia hata kuwatupa watoto
majalalani kutokana na ugumu wa maisha na kutokuwa tayari kubeba mimba
hizo na kutunza watoto. Hii inatokana na kukosa elimu ya kutosha juu ya
kujikinga na mimba nje ya ndoa. Kuhusiana na suala la utoaji mimba, kwa
mfano, wapo madaktari ambao badala ya kuwaelimisha wanawake juu ya athari
za utoaji mimba wao wanakuwa mstari wa mbele kuwashinikiza watoe mimba,
ili madaktari hao, waweze kujipatia kipato kwani utoaji mimba umekuwa kama
mradi kwa baadhi ya madaktari. Hii inaonyesha ukosefu wa maadili kwa baadhi
ya madaktari. Kwa upande wa Tanzania, suala la utoaji mimba siyo halali kwa
mujibu wa sheria. Kutoa mimba ni kosa la jinai ambalo linachukuliwa kama
uuaji. Ipo mijadala mbalimbali iliyofanyika kuhusiana na suala hili, ikiwemo
mijadala ya bungeni. Hii ni katika harakati za kupiga vita utoaji mimba, kwamba
ni kitendo kisichokubalika katika jamii ya Kitanzania. Pia ni kinyume cha haki
za binadamu.
Masuala ya Kijinsia
Dhamira hii imezungumzia nafasi ya mwanamke na mwanaume katika jamii.
Masuala ya kijinsia yanazungumziwa sana katika jamii yetu ya Kitanzania.
Kuhusiana na nafasi ya mwanamke katika jamii, wapo waandishi mbalimbali
ambao wamezungumzia suala la nafasi ya mwanamke katika jamii. Mwanamke
amesawiriwa katika nafasi mbalimbali kutegemeana na mtazamo wa mwandishi.
Vilevile Mke wa Dkt. Gumbo amesawiriwa katika nafasi chanya kwa kuonesha
uwajibikaji wake. Amesawiriwa kama mwanamke anayefanya kazi kwa bidii
kwa kujishughulisha na biashara ya kuendesha kampuni iliyoitwa Kilua
Investment. Mama Sospeter anadiriki kwenda hata, nchi za mbali kutafuta
mawasiliano na malighafi kwa ajili ya kuendeleza kampuni, akiongozana na
mwanae Sospeter. Hii inaonyesha kuwa wanawake wanaweza kufanya shughuli
ambazo wanaume wanafanya.
Kwa upande wa pili, mwanamke katika filamu ya Taswira amesawiriwa katika
nafasi hasi kwa kumwangalia Tamala na Trace. Tamala anatumiwa kama
chombo cha starehe na Dkt. Gumbo kwa kukubaliana kufanya urafiki na,
hatimaye, kuwa na uhusiano ya kimapenzi nje ya ndoa. Katika filamu hii
mwanamke anaonekana kama chombo cha starehe pale Tamala anapopata
ujauzito wa Dkt. Gumbo na kutelekezwa. Vilevile Dkt. Gumbo anajikuta akiwa
na uhusiano kimapenzi na Trace bila kujua kuwa ni binti yake na ambaye pia
Dkt. Gumbo alimkana baada ya kupata ujauzito. Pia nafasi hasi inajidhihirisha
kwa kumuangalia Mke wa Dkt Gumbo, ambaye anaonyesha na roho mbaya na
ya kinyama ya kumdhuru Trace, pale anapompa dawa za hatari za kutoa mimba.
Mwanaume katika filamu hii ya Taswira pia amesawiriwa katika nafasi hasi,
hasa kwa kumuangalia mhusika Dkt. Gumbo kwa anaonyesha tabia ya umalaya
ya kujihusisha na mapenzi na wanawake zaidi ya mmoja huku akijua kuwa ana
mke wake ndoa. Hii inajidhihirisha kwa kumuangalia Tamala na Trace ambao
walijihusisha kimapenzi na Dkt. Gumbo mwisho wake walitelekezwa. Pia Dkt.
Gumbo amesawiriwa kuwa mnyanyasaji kwa kumnyanyasa Trace kijinsia, pale
anapombaka. Katika jamii ya Kitanzania wapo wanaume ambao wanafanya
mambo yenye manufaa kwao binafsi na kwa jamii nzima na pia wapo wale
wanaofanya mambo ambayo hayakubaliki kijamii. Wapo wanaume ambao
kutokana na hulka na mienendo yao wamekuwa wakifanya mambo ya ajabu
kama umalaya na kuwasababishia watu wengine matatizo. Wapo wanaume watu
wazima ambao wanajihusisha kufanya mapenzi na wasichana wadogo bila
kuona aibu wakidai kwamba wanakwenda na wakati.
Ukatili
Ukatili ni hali ya kumtendea mtu mwingine kitendo kisichostahili kufanywa kwa
binadamu yeyote yule. Suala la ukatili katika filamu hii linajitokeza pale
ambapo mke wa Dkt. Gumbo alipojaribu kumpa Trace vidonge vya kutoa
mimba. Mke wa Dkt. Gumbo alifanya hivyo, baada ya kugundua kwamba mume
wake ndiye aliyehusika na ujauzito huo, ambao ulisababisha Trace kufariki na
mtoto aliyezaliwa, kupoteza mzazi wake. Mke wa Dkt. Gumbo hakujali utu na
uhai wa mtu, ili mradi lengo lake la kuhakikisha kuwa mimba ile inatoka,
linatimia.
Suala la ukatili katika filamu hii pia, linasababishwa na ushawishi. Hii
inajidhihirisha pale ambapo James anakubali kushawishiwa na mkewe Jesca ili
wamtese Tamala wakati alipokuwa akiishi pamoja nao katika nyumba ya urithi.
Jesca ni wifi mkatili ambaye anamshawishi James afanye ukatili kwa Tamala.
Wote wawili wanamnyanyasa Tamala kwa kumnyima haki za msingi kama
elimu, na anaishia tu kufanya kazi za nyumbani. Pia wakati alipokuwa anaumwa
hawakumjali wala kumpeleka hospitali mpaka alipozimia ndipo walimpeleka
hospitali. Tamala alipopata nafuu alirudi nyumbani akidhani kuwa maisha
yangebadilika lakini haikuwa hivyo. Alipoona kuwa taabu zinazidi na hakuna
dalili za mabadiliko aliamua kuondoka na kwenda kuishi na shangazi yake.
Ushawishi na ukatili wa mawifi katika jamii yetu ya Kitanzania upo na
umekuwa ni tatizo katika kusambaratisha jamii. Filamu hii ya Taswira imeakisi
hali halisi ya mahusiano katika ndoa ambao unasababisha migogoro mbalimbali
katika familia.
Uongozi
Suala la uongozi katika filamu ya Taswira pia, limegusiwa. Katika filamu hii,
uongozi wa kijiji umeonekana ukiwajibika katika kuwasaidia wananchi kutatua
masuala mbalimbali ya kijamii kama vile migogoro na masuala mengine ya
kifamilia na ya kijamii kwa ujumla. Pia uongozi unaozungumziwa katika filamu
hii unasisitiza kufuata na kuheshimu sheria za nchi, hususan sheria za umilikaji
wa ardhi. Hii inajidhihirisha kwa kuwaangalia wahusika Tamala na Baraka
ambao walikwenda kutoa taarifa katika uongozi wa kijiji kuhusu uharibifu wa
mashamba yao uliofanywa na mifugo. Uongozi huo wa kijiji ulifikia uamuzi
kuwa wafugaji wote walipie fidia ya uharibifu wa mazao uliofanyika. Hii
inaonyesha kuwa uongozi wa kijiji pamoja na maamuzi wanayofanya
yanaheshimiwa na wanakijiji.
Umaskini
Umasikini ni hali ya kukosa mali, ufukara na ukata (TUKI 2004). Umaskini ni
miongoni mwa matatizo makubwa yanayozikumba nchi zinazoendelea.
Kutokana na kwamba Tanzania ni miongoni mwa nchi hizo, umasikini
unajitokeza kwa kiasi kikubwa na kuathiri maisha ya watu. Watanzania walio
wengi ni masikini sana mpaka kiasi cha kushindwa kumudu maisha yao na
kuacha urithi wowote wa mali kwa watoto wao (Chiraka 2009:54). Umaskini
umesababisha watu wengi kushindwa kupata huduma muhimu kama elimu,
huduma za kiafya na hata maji. Zipo kazi mbalimbali za sanaa ambazo
zimezungumzia suala la umaskini. Mathalani katika Riwaya ya Shida, Chonya
na Matika wanakutana na hali ngumu ya maisha mpaka wanaamua kwenda
mjini kutafuta maisha. Huko mjini wanakumbana na hali ngumu zaidi mpaka
wanaamua kurudi tena kijijini ambapo wanagundua kuwa elimu ndiyo
mkombozi wa maisha yao. Vilevile katika tamthiliya ya Ngoswe Kitovu cha
Uzembe dhamira ya umaskini ni mojawapo ya dhamira zilizojadiliwa. Hali hii
inajidhihirisha kwa kuangalia malazi pamoja na mavazi ya wahusika.
Katika filamu hii ya Taswira ipo migogoro mbalimbali iliyojitokeza. Kwa mfano
kuna mgogoro kati ya wakulima na wafugaji. Chanzo cha mgogoro huu ni
wafugaji kuingiza mifugo yao katika mashamba ya wakulima na kusababisha
uharibifu. Baada ya wakulima kuona hali hiyo, wanatoa taarifa katika serikali ya
kijiji na inaamuliwa kwamba wafugaji walipe fidia ya uharibifu wote
uliofanyika. Katika jamii ya Kitanzania ipo migogoro ya ardhi kati wa wakulima
na wafugaji. Kwa mfano, kuna mgogoro wa ardhi baina ya wakulima na
wafugaji wa Kimasai Arusha na Morogoro kiasi cha serikali kuingilia kati kwa
kuwahamishia baadhi ya wafugaji katika mikoa mingine.
Uzazi na Ndoa
Uzazi ni kielelezo cha kuwepo na kukua kwa jamii ya mwanadamu popote pale
ulimwenguni. Ijapokuwa uzazi ni kitambulisho kikubwa cha kuwepo (uhai) na
kukua kwa jamii, mtazamo juu ya jambo hili kwa jamii moja au nyingine
unaweza kufanana au kutofautiana kulingana na mazingira ya jamii. Katika
ontolojia ya Kibantu, uzazi huchukuliwa kama kitu muhimu sana katika asili ya
Wabantu na kinachoweza kuleta mshikamano katika ndoa na ndani familia. Kwa
Wabantu, uzazi ni suala zito na linaheshimiwa na kuthaminiwa katika jamii zao.
Katika jamii za Wabantu kuna sherehe mbalimbali zinazofanywa ambazo lengo
na madhumuni yake ni kuuenzi uzazi. Kwa mfano, sherehe za kuzaliwa na
kumpa mtoto jina zinaashiria kusherehekea kuongezeka kwa ukoo. Hivyo
wanajamii wanasherehekea kwa lengo la kumkaribisha mwanafamilia mpya
katika jamii (Mbiti 1969).
Kwa mtazamo wa Kiafrika, watu wengi huona kuwa ili kuishi pamoja katika
ndoa, kuzaa ni lazima. Wanasahau upande mwingine kuwa kuzaa ni majaliwa ya
Mwenyezi Mungu. Hapa inaonyesha kuwa katika jamii za Kibantu uzazi ni
suala muhimu, na ndio maana katika filamu hii Stella alipatwa na misukosuko
kutokana na tatizo la kutozaa. Hii inaakisi hali halisi ya maisha ya watu katika
jamii ya Kitanzania kwani wapo wanawake wengi wenye matatizo ya uzazi
ambao wananyanyasika katika ndoa zao. Hii imewasababishia matatizo ya
kisaikolojia hatimaye kuvunjika kwa ndoa zao.
Ushirikina na Uganga
Suala hili limejitokeza katika tamthilia kadhaa, mathalani, tamthilia ya
Emmanuel Mbogo, Ngoma ya Ng’wanamalundi na Ibrahim Hussein, Kinjekitile.
Kwa ujumla, ushirikina na uganga kama itikadi za jadi katika tamthiliya hizi
zinasawiriwa kama amali muhimu za jamii zifaazo kutumiwa kutatua baadhi ya
matatizo ya kimaisha. Uchawi na itikadi za ushirikina, vilevile ni tatizo sugu
lenye kukwamisha maendeleo (Mulokozi 1996:210). Zipo imani za aina
mbalimbali lakini imani zinazozungumziwa hapa ni imani za kijadi ambazo
zinahusisha ushirikina au nguvu za mizimu na miungu wengine. Nguvu hizi
kama ilivyoelezwa hapo awali hutumika katika kutatua matatizo mbalimbali ya
kijamii na watu wanaziamini kuwa zinafanya kazi.
Katika filamu ya Vita vya Ushindi, imani za kijadi yaani ushirikina limejitokeza
kwa kiasi kikubwa. Hii inajidhihirisha kwa kumwangalia Mama Fred, Mama
Jane, Jane na mganga Masolosolo. Wahusika wanaamini kuwa nguvu hizi
zinafanya kazi hasa pale walipotaka kuiharibu ndoa ya Fred na Stella kutokana
na tatizo lake la kutozaa. Mama Fred anaona kuwa njia pekee ya kumuondoa
Stella kwenye ndoa ni kutumia ushirikina na uganga. Katika kutimiza hilo
Mama Fred anaamua kwenda kwa mganga ambaye anawapatia dawa ambazo
wanaamini zingefanya kazi. Katika kudhihirisha ushirikina na uchawi wao,
Mama Fred anamtuma Jane kuchukua nguo za ndani za Stella ambazo
zilianikwa kwenye kamba ili waweze kuzifanyia uchawi. Jane anafanya hivyo
na anafanikiwa kuzipata. Hii inaashiria kwamba uchawi unaweza kufanywa kwa
kupitia nguo za mtu. Nia yao kubwa ilikuwa kutaka kumwachisha ndoa yake.
Pia, katika ushirikina wao Mama Fred na Jane wanadiriki kuamka usiku na
kwenda kuwanga chumbani kwa akina Stella. Kutokana na kushika dini, Stella
alikuwa na nguvu za kuweza kupambana na uchawi. Alipata uwezo wa kuwaona
wakati wakiwa wanawanga usiku na kumwamsha mumewe ili aweze
kushuhudia.
Katika jamii wapo watu ambao wanategemea nguvu za uchawi na uganga katika
kutatua matatizo yao mbalimbali. Jamii nyingi hasa zile ziishizo vijijini na
maskini zinaamini sana ushirikina. Pia mijini ushirikina upo kwani baadhi ya
watu wenye nyadhifa zao ambazo wanaamini kuwa nguvu za sihiri zinaweza
kuwasaidia kupata madaraka au wasiondolewe katika madaraka. Hudiriki
kusafiri safari ndefu kwenda kutafuta nguvu za sihiri ili waweze kudumu katika
madaraka. Mbali na viongozi, wapo watu wa kawaida ambao hutumia uganga
katika kutatua matatizo kama magonjwa, mahusiano ya kimapenzi na kadhalika.
Imefikia hatua mpaka waganga wanajinadi na kujitangaza kwenye magazeti na
mabango ili kuvutia biashara. Kwa hiyo, hii inaonyesha kuwa masuala ya
uganga yamefanywa kama shughuli ya kujipatia pesa. Lakini mwishoni
inaonyesha kuwa nguvu hizo hazidumu kwani watu wanaotegemea sana nguvu
hizi mwisho wake huanguka (hushindwa).
Usaliti
Unyanyasaji wa Kijinsia
Hili ni suala linalojitokeza kwa kiasi kikubwa katika kazi mbalimbali za fasihi
kama vile riwaya, tamthiliya na ushairi. Watunzi wanajaribu kuonyesha hali duni
ya mwanamke katika jamii ya sasa ili kutafuta sababu ya hali hiyo na
kupendekeza ufumbuzi. Baadhi ya waandishi wa tamthiliya wanaogusia suala
hilo ni Muhando, katika Nguzo Mama, Machozi ya Mwanamke, Mulokozi,
katika Mukwawa wa Uhehe, Mazrui, katika Kilio cha Haki na Ebrahim Hussein
Kwenye Ukingo wa Thim. Unyanyasaji wa kijinsia ni suala ambalo linatokea
sana katika jamii zetu za sasa na limekuwa ni chanzo cha matatizo kama
mafarakano katika familia na hata ulemavu. Kwa mfano Jarida la FEMA
(2010:11) linaeleza kuwa unyanyasaji wa kijinsia ni tendo lolote lenye mtazamo
wa jinsia linaloweza kumsababishia mtu adha au kero, madhara na mateso ya
kimwili, kisaikolojia na kingono.
Ujasiri na Uvumilivu
Kutokata tamaa, ujasiri na uvumilivu kunajitokeza kwenye kazi mbalimbali za
fasihi. Kwa mfano katika riwaya ya Watoto wa Mama Ntilie, mhusika Mama
Ntilie anachorwa kuwa mvumilivu, jasiri na asiyekata tamaa ya maisha. Hii
inajidhihirisha kwa jinsi anavyoweza kuvumilia matatizo ya ulevi wa mume
wake bila kukata tamaa. Anaamua kufanya biashara ndogondogo kwa lengo la
kutokomeza umaskini unaoikabili familia yao. Katika riwaya hii pia Kurwa ni
mmoja wa wahusika wavumilivu na jasiri katika kuyakabili matatizo.
Katika filamu ya Vita vya Ushindi, dhamira hii inajidhihirisha kwa kumwangalia
mhusika Stella ambaye anaonyesha ujasiri katika kupambana na changamoto
ambazo zinamkabili. Mbali na kunyanyaswa kutokana na kutozaa, Stella
hakukata tamaa, aliendelea kumuomba Mungu akitegemea kuwa atamsaidia.
Stella aliendelea kuwa mnyenyekevu na mvumilivu mbali na matatizo na
manyanyaso yote aliyoyapata katika ndoa yake kutoka kwa wazazi wa Fred na
Fred mwenyewe. Alivumilia mpaka Mungu (kwa imani yake) alipomjalia kupata
mtoto. Wanawake wengi wamekuwa wakipata matatizo haya katika ndoa zao
lakini wamekuwa wavumilivu ili waweze kutunza watoto na familia kwa
ujumla.
Starehe
Starehe ni hali ambayo mtu au watu hujiliwaza kwa kufanya matendo ambayo
wao hufikiri wanaweza kupata raha au faraja ya namna fulani. Zipo starehe za
aina mbalimbali kama kutumia vinywaji, kujihusisha na masuala ya mapenzi,
kushiriki katika michezo mbalimbali na kadhalika. Starehe hutegemea mtazamo
wa mtu mwenyewe kuwa ni kitu gani anapenda. Kitu fulani kinaweza kuwa
starehe kwa mtu mmoja na kuwa karaha kwa mtu mwingine. Katika filamu hii
ya Vita vya Ushindi suala la starehe linajidhihirisha kwa kumwangalia Fred na
marafiki zake ambao wamekaa baa wakinywa pombe na wanawake
wanaoendesha ukahaba.
Starehe zao hizi zinasababisha mpaka kutafutiana wapenzi. Kwa mfano, Rich
anamtafutia Fred mwanamke wa kustarehe naye wakati anajua fika kuwa Fred
ana mke wake. Fred anaingia katika mkumbo wa kujihusisha kimapenzi na
mwamke wa nje, yaani Wema, kutokana kuchanganywa na wazazi wake kuwa
Stella hafai. Matokeo yake ni kwamba waliishia kufanya starehe na kusahau
familia zao. Kwa kuwa Fred alikuwa ni mcha Mungu hakutarajiwa kunywa
pombe na kujihusisha na masuala ya mapenzi nje ya ndoa. Kwa mtazamo huu
Fred anachukuliwa kuwa ametenda dhambi kwa kukiuka amri za Mwenyezi
Mungu ambazo zinakataza watu kutumia kilevi cha aina yoyote, kutamani na
kuzini na mke wa mtu na kadhalika.
Kwa ujumla starehe kupita kiasi hasa unywaji wa pombe, umekuwa na madhara
makubwa katika familia mbalimbali. Ulevi umefanya watu kuwa maskini
kupunguza kipato cha familia na kushindwa kuhudumia familia ipasavyo. Ulevi
pia unaweza kusababisha kupoteza maisha kutokana na kunywa pombe kali
kupita kiasi. Madhara mengine ni kama kuvunjika kwa familia, umalaya, ukatili
na unyanyasaji, ukosefu wa maadili katika familia, na kutokuwajibika. Katika
jamii ya Kitanzania matukio kama unywaji wa pombe, wanaume kufanya
uhusiano wa kimapenzi nje ya ndoa yanatokea na kuathiri maendeleo ya jamii
kwa ujumla. Zipo familia zilizosambaratika kutokana na athari za starehe za
kupita kiasi. Starehe pia zimepelekea watu kuathirika na magonjwa yasiyopona
kama UKIMWI.
Utoaji wa Mimba na Mimba Nje ya Ndoa
Kama ilivyoelezwa hapo awali katika filamu ya Taswira, dhamira hii pia
inajitokeza katika filamu ya Vita vya Ushindi. Hii inajidhihirisha pale ambapo
mchumba wa John anamlazimisha John waitoe mimba. John anaonekana
kutokukubaliana na suala hilo. Wanaamua kumuona daktari ambaye anawaeleza
kuwa kutoa mimba ni hatari. Uamuzi wa kwenda kumuona daktari unaonyesha
jinsi John alivyokuwa na uelewa wa kutosha kuhusiana na athari za utoaji
mimba. Pia inaonyesha jinsi baadhi ya madaktari wanavyoweza kutoa ushauri
mzuri kwa kuzingatia maadili ya kazi zao. Ushauri wenye busara huepusha
madhara kwa watu hasa wasichana wanaotaka kutoa mimba.
Ujumbe katika filamu hii ya Vita vya Ushindi ni kuwa watu wategemee nguvu
za
Mungu kupitia dini, katika kutatua matatizo yao ya maisha na siyo kuegemea
nguvu za sihiri (ushirikina na uganga). Mungu ndiye muweza wa kila jambo, na
nguvu zake zinatenda kazi kuliko nguvu za sihiri. Pia filamu hii inatufunza
kuwa subira yavuta heri. Kuvumiliana katika masuala ya ndoa na uzazi ni
muhimu na siyo kumnyanyasa mwanamke. Pia wazazi wanaaswa kuwa wasiwe
na tabia ya kuingilia ndoa za watoto wao wanapoona kuna tatizo la uzazi kwani
Mungu ndiye anayewajalia au kutokuwajalia watu kupata watoto.
Hitimisho
Tamthilia
NA
Henry Kuria, Kimani Nyoike, Gerishon Ngugi na B.M Karutu ni miongoni mwa
wanafunzi wa mwanzo wa Graham Hyslop waliokuwa wakisoma katika shule
ya Alliance High School. Hyslop ni mwingereza aliyekuwa katika utumishi wa
serikali ya kikoloni nchini Kenya. Hyslop alianzisha kikundi cha maigizo kwa
ajili ya askari waliopigana katika vita ya pili ya dunia, miaka ya 1950 alianza
kutunga michezo ambayo iliigizwa na kikundi chake. Michezo yake ya mwanzo
katika lugha ya Kiswahili ni Afadhali Mchawi (1957), na Mgeni Karibu (1957).
Inasemekana kuwa Mwingereza huyu (Graham Hyslop) ndiye mtu wa kwanza
kuleta tamthiliya kwa lugha ya Kiswahili yenye kufuata kanuni zote za Ki-
Arstotle. Mbali na Henry Kuria, wanafunzi wengine wa Hyslop walioandika
tamthiliya kwa Kiswahili ni Kimani Nyoike aliyeandika tamthiliya ya Maisha ni
Nini mwaka 1955, B.M Karutu Atakiwa Polisi mwaka 1957 na Gerishoni Ngugi
Nimelogwa Nisiwe na Mpenzi mwaka 1961.
“Hapo mwanzo Ebrahim Hussein aliathiriwa sana na Bretch katika utunzi wake.
Lakini kadri alivyoendelea kustawi katika uandishi wake wa sanaa za
maonyesho Ebrahim Hussein alianza taratibu kuchanganya jadi za kiafrika kama
vile masimulizi, utambaji, mianzo pamoja na miisho ya kifomula katika uandishi
wake. Hivyo Hussein ndiye mwandishi wa mwanzo kabisa aliyeanza kuzikiuka
taratibu za kiuandishi katika tamthiliya zilizofuata kanuni za ki-aristotle kwa
kuingiza ujadi wa ki-afrika katika kazi zake”.
Muhando (2013);
Nadharia
NADHARIA HUTUMIWA SANA KATIKA UTAFITI
MAANA YA NADHARIA
Anasema kuwa ili kazi ya fasihi ieleweke ni lazima ushiriki wa msomaji uoane
au upatane na maana inayojitokeza katika kazi ya Fasihi.
Kwa hiyo basi , nadharia ya Upokezi hufasili Fasihi kama mchakato wa namna
msomaji na wanavyoathiriana.Uzoefu wa maisha wa msomaji unaweza kutoa
tafsiri tofauti kwa kazi ya fasihi kutoka msomaji mmoja na mwingine.
Ontolojia inaweza kutazamwa kwa namna tatu: kama taaluma, kama falsafa na
kama nadharia. Hivyo kwa kuwa utafiti huu ulichunguza “Mabadiliko ya
kiuandishi kutoka kanuni za Ki-Aristotle kwenda kanuni za jadi ya Ki-Afrika”,
kipengele cha Ontolojia ya Kibantu kinachoweza kutumika katika kazi za fasihi,
tuliona ni vyema kutumia Ontolojia kama nadharia katika utafiti huu, kwani
imewezesha utafiti huu kufikia malengo yake, pia ilihusiana na mada
iliyoshugulikiwa.
Kwa jumla, wataalamu hawa wameeleza mengi juu ya nadharia hii, jambo
lililosisitizwa sanana wataalamu wengi waliojadili nadharia hii ni kuhusu
uchaguzi wa Ontolojia nzuri na namna ya kutumia nadharia hii. Wanasema
Ontolojia nzuri ni ile inayohusisha njia za Kisayansi na kutupatia njia chache na
rahisi ambazo zitaelezea mambo mbalimbali katika ulimwengu. Pia nadharia hii
inatukuza sana Ubantu na kumuona mwafrika kama kiumbe bora mwenye
uwezo wa kubuni na kusimamia mambo yake kwa usahihi. Mbali na kutumia
Ubantu (U-Afrika), nadharia hii inaeleza mambo kadhaa ambayo ni sehemu ya
ufahari kwa waafrika, mambo hayo ni pamoja na dhana ya familia pana,
kuamini uzazi kuwa ndio njia ya uzima wa milele, yenye kuhashiria umuhimu
wa binadamu, na Ugumba ni laana na utupu kwa binadamu, kuabudu katika
Mungu na miungu na kuheshimu Wahenga. Pia huhusisha na imani kuhusu
uchawi, na sihiri, na ndani yake kuna masuala ya uganga. Pia umri kwa waafrika
una nafasi kubwa sana katika jamii na unabeba hekima za mtu.
3.UJUMI (AESTHETICS)
Ujumi ni nini?
AU
ETHOS, ni desturi ama mguso, tabia ama kaida Fulani ndani ya jamii ambazo
hufanya matakwa yahusuyo jamii Fulani tu.
Kabla falsafa mpya ya Aesthetics haijachukua kasi yake, hapo awali masuala ya
hisia yaliwekwa chini ya nadharia ya hisia za akili (mental perception). Dhana
ya ujumi ilitoka kwenye nadharia ya hisia za akili katika karne ya 18 na
kuitwa “Falsafa ya uzuri” au “Falsafa ya sanaa” au yote mawili kwa pamoja.
Baadaye ujumi uliachana na falsafa na kuwa tawi linalojitegemea la elimu.
2. SANAA
Sanaa ni ufundi wa kuunda jambo. Twaweza kuueleza uzuri kupitia sanaa. Sanaa
yaweza kuupambanua uzuri kwa viwango vya juu zaidi kuliko jambo lolote lile.
0762 – 957493
0768 – 625660
hwilliady@ymail.com
majumbeni@gmail.com
moja ya wadau waliochangia sana kuendelea kwa nadharia hii kwa kasi ni
Adrew Dworkin. Mwaka 1976, akiwa katika mji mkuu wa Uingereza, London,
alitoa mapendekezo makali katika kukomesha utawala wa mwanaume kwa
mwanamke, Dworkin anasema: Ili kufanikisha, tunahitaji kubomoa kabisa
muundo wa mihimili ya utamaduni wa jamii kama vile sanaa, kanisa, sheria,
kaya zinazodhibitiwa na baba, jamii na taswira zote za asasi, mila, desturi
ambazo zinamwona mwanamke kuwa mtu ovyo.
“BI MOJA: (kwa Shaabani): Kama ulijua kufika sasa hivi nipe hela ya kanga
bwana meli meli hii hainikosi leo utanipa hela hizo kanga nikakate. Mwezi wa
tatu huu kanga sizijui.
Hana wa kumsaidia
“Wanawake wanne, Dauda, wanne miongoni mwa wabunge mia moja uwiano
gani huu wa kimzaha! Wala hakuna uwakilishaji wa kimkoa” (uk.81)
Kwa upande wa kijamii, mwanamke amekuwa akikandamizwa kwa kupigwa na
mumewe bila sababu zozote za msingi. Hili linajidhihirisha katika riwaya ya
Rosa Mistika iliyoandikwa na Euphrase Kezilahabi (1988) kwa kumtumia
mhusika Zakaria ambaye alikuwa anampiga mkewe bila sababu. Mwandishi
anasema:
“Lete hiyo barua iko wapi? Pamoja na shilingi ulizopewa unafikiri sisi hapa
maskini. Rosa alipigwa tena na tena. Makofi yalikwenda mfululizo hata damu
zikamtoka puani na mdomoni. Baba nihurumie sitarudia tena… Zakaria
hakujali alichukua fimbo na kuongozana na bintiye mpaka chumba cha watoto
hali akinguluma lazima unioneshe barua hiyo unataka kuniletea umalaya wa
mama yako hapa.” (Uk.7)
“BI TANO: Yaani mnasema mimi mvivu siyo nimezunguka mji mzima na zigo
hilo halafu mnaniambia mimi mvivu. Nawaambia watu hawataki kununua au
mnataka niwagawie bure.”
BI NANE: Lakini kwa nini wakatae kununua hivi, mbona vile vya mwanzo
walivinunua? (uk.16).
“…Haa! Shemeji mmerudi kuchukua hata kitanda! Hata sufuria! Nitalala wapi
na nitapikia wapi jamani!” (uk.39)
Kudhihirisha kuwa kuna sifa fulani za kike na uzoefu fulani wa kike katika
uwazaji, hisia, kutathmini, kujiangalia na kuuangalia ulimwengu wao wa nje.
Uzoefu fulani wa kike unajitokeza katika uwazaji na jinsi wanavyousawiri
uhalisi. Kazi ambazo zinamsawiri mwanamke kwa njia chanya, mfano ni riwaya
ya Kiwasifu ya Shaaban Robert Wasifu wa Siti Binti Saad. Kuna mashairi
kadhaa aliyoyatunga mwandishi ambayo yanaendeleza suala hili la uchanya wa
wanawake katika jamii. Mfano wa usawiri wa wahusika linathibitishwa pale
mwandishi anaposema:
Ulitoka shamba,
Kama si sauti,
HITIMISHO