Professional Documents
Culture Documents
31 Machi, 2018
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Machi 31, 2018) kwenye Mkutano
Mkuu wa BAKWATA uliofanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma,
ambapo amesisitiza kuwa ni muhimu wasaidizi wa Mufti wakasimamia suala hilo.
“Dini ni taasisi muhimu sana kwa maisha yetu ya kila siku ndio maana Serikali
inaheshimu na kuzitambua dini zote kutokana na mchango wake mkubwa katika
amani ya nchi yetu. Niwaombe viongozi wangu popote mlipo muilinde amani yetu”
Waziri Mkuu amesema amani ni miongoni mwa neema kubwa sana kwa binadamu
na ndio maana wote wanamtambua Mwenyezi Mungu, hivyo wasiruhusu mtu au
kikundi chochote kujaribu kuchafua na kuharibu amani iliyopo nchini.
Waziri Mkuu amesema Mufti wa Tanzania Sheikh Aboubakar bin Zubeiry ambaye
ndiye kiongozi wa Waislamu nchini mara zote amekuwa akisisitiza jambo hilo na
kuwataka waislamu popote walipo watambue kuwa hicho ni chombo chao.
1
“Ni muhimu sana kwa ninyi wasaidizi wa Mufti mlio kusanyika hapa muhakikishe
mnalisimamia hili katika maeneo yenu. Katika hili napenda kuwahakikishia kuwa
Serikali yenu iko pamoja Mheshimiwa Mufti kutekeleza nia hiyo njema.”
Amesema ahadi ya Rais Dkt. Magufuli ni kuwa Serikali anayoiongoza ipo tayari
kusikiliza maoni, ushauri na mapendekezo yeyote kutoka kwa viongozi wa dini .
‘Milango iko wazi saa zote ‘
Ameongeza kuwa yeye si mtaalamu sana kama walivyo Masheikh hao lakini
anakumbuka maneno ya Mwenyezi Mungu ndani ya Qur’ani sura Al Imran aya ya
103 yanayosema “ Shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote na wala
msifarakane”
(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAMOSI, MACHI 31, 2018.