You are on page 1of 4

KISIMA CHA MAJI

UNA NINI, MWANANGU?


PMC BOKO 18 OKTOBA 2020

UJUMBE
 Kisima ni chanzo cha maji
 Kisima ni mahali zinapotoka baraka zako
 Kisima ni mahali penye hazina yako

ANDIKO KUU
Mwanzo 21:14-19
14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji,
akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka,
akapotea katika jangwa la Beer-sheba. 15 Yale maji yakaisha katika kiriba,
akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja. 16 Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye
kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa
akimkabili, akapaza sauti yake, akalia. 17 Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika
wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri?
Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko. 18 Ondoka,
ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa
kubwa. 19 Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda
akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana.

Kuna nyakati unazopitia ambazo ni ngumu


Kuna majira unayopitia ambayo ni ya shida
Unapitia msimu ambao ni mgumu sana katika maisha yako
Lakini nyakati huja na nyakati hupita
Hakuna mateso yasiyokuwa na mwisho, hilo ulilonalo litapita.
Upo wakati ambao unaishi na kuona tumaini lako linapotea
Kitu ulichokitegemea kinakufa
Mtu uliyemtegemea anakuacha
Mtu uliyemtegemea anakwambia ondoka
Kazi uliyoitegemea unafukuzwa
Duka ulilolitegemea linaungua kwa moto

Mungu ameruhusu tatizo ulilonalo kupima Imani yako


Mungu anataka ulishinde tatizo hilo ili akufanye taifa kubwa
Mungu anataka huyo unayemtegemea asiseme bila yeye usingekuwa hivyo ulivyo
Akuache katika hali duni nay a masikitiko
Akuache akisema hutafika
Akuache akisema hutaweza
Jina lake ni iligibor,
Jina lake ni Adonai,
Njia zake hazichunguziki
Wakati unasema Mungu uko wapi, kwa nini umeruhusu hivyo, Yeye anasema
mwanangu ninataka kukupandisha kutoka utukufu hadi utukufu.

Mwanzo 26:19-22
18 Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za
Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa
kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.
19 Watumwa wa Isaka wakachimba katika lile bonde, wakapata kisima cha maji
yanayobubujika. 20 Wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaka
wakisema, Maji haya ni yetu. Ndipo akakiita jina la kile kisima Eseki, kwa sababu
waligombana naye. 21 Wakachimba kisima kingine, wakagombania na hicho tena.
Akakiita jina lake Sitna. 22 Akaondoka huko akachimba kisima kingine, wala
hicho hawakukigombania. Akakiita jina lake Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa
Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi.
Wapo wanaogombania kazi yako; wakisema nafasi hiyo uliyonayo ni yao.
Wapo wanaogombania ardhi yako; wakisema ni mali yao;
Wapo wanaogombania mchumba wako, hata kama hawakwambia, wakisema
hustahili wewe kumpata huyo.

Usigombane nao waachie hicho kisima, ni Eseki


Nami naamuru Bwana akufanyie nafasi katika familia yako; akupe kisima
ambacho hakuna mtu atakayekigombania; akufanyie nafasi katika maisha yako;
Waliokushusha chini wakuone ukiinuliwa
Waliokufukuza wakuone ukiishi kwako
Waliokukataa wakuone ukipokelewa
Aliyekufukuza kazi akuone ukikaa kwenye kiti kikubwa zaidi
Waliosema umefika mwisho waone ukiruka juu kama tai
Usiwe mtu unayegombana na watu kwa ajili ya vitu na ugomvi huo haushi miaka
yote hata unarithisha watoto wako ugomvi. Huelewani na ndugu yako na watoto
wenu hawaelewani; ugomvi wako na watu wengine usiwarithishe vizazi vyako.

Hata kama ni haki yako achilia; Yakobo alikuwa na haki ya visima ambavyo
Ibrahimu Baba yake alichimba huko Gerari lakini Wafilisti wakavigombania.

Ninaitamka siku ambayo Yesu anakufanyia nafasi, jina la kisima chako ni


Rehobothi, Ndoa yako Rehobothi, Biashara yako Rehobothi, Kazi yako Rehobothi,
Kilimo chako Rehobothi, Ardhi yako Rehobothi.
Ninaweka mhuri wa damu ya mwanakondoo; alama inayothibitisha furaha yako ni
furaha yako, amani yako ni amani yako, afya yako ni afya yako hakuna
wakukunyang’anya.

Ninazidisha furaha yako


Ninazidisha biashara yako
Ninazidisha huduma yako
Ninazidisha afya yako
Ninazidisha siku za

Malaika wa Bwana alipomtokea Hajiri alimwuliza, Una nini, Hajiri?

Isaya 40:28 Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana,


Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.
29 Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.
30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;
31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa
mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu,
wala hawatazimia.

Isaya 43:2 Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito,
haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto
hautakuunguza.

You might also like