You are on page 1of 2

Saikilojia

Saikilojia ni neno linalotokana na neno la kingereza (psychology)


ambalo asili yake ni neno la kiyunani (psyche) lenye maana ya nafsi
au roho.

Kwa ujumla wake saikolojia ni sayansi inayohusu nafsi au roho na


namna nafsi hii (roho) inavyo fanya kazi.

Vile vile saikolojia inahusu elimu ya ufahamu wa tabia za wanyama


hasa binadamu.

Kwa elimu hii ya saikolojia unaweza kufahamu vyanzo vya tabia flani
kwa binadamu, pia inampa binadamu uwezo wa kujielewa madhaifu
yake na mazuri yake na namna bora ya kuyaepuka (madhaifu) au
kuishi nayo bila kuleta madhara na namna bora ya kuyaendeleza
mazuri aliyonayo.

Wataalamu wa saikolojia siku zote hupenda kufahamu kwa upana


tabia za binadamu kupitia tafiti ikiwa ni pamoja na kufahamu mahitaji
yake, motisha, hamasa zake, hisia zake (mwenendo wa fikra zake na
mihemuko yake).

Hii huwafanya wataalamu wa saikolojia kubuni njia na kutuo ushauri


ambao humfanya (humuwezesha) binadamu kuishi maisha ya furaha
na amani.

Saikolojia ni somo ambali haliepukiki katika maisha ya binadamu.


Nikweli na ni wazi kuwa kila binadamu ni wapekee. Upekee huu
unasababiswa na mambo makubwa mawili ambayo ni ASILI (Nature)
na MAZINGIRA (nurture).

Kutokana na mambo haya mawili, binadamu hujikuta tukitofautiana


kuanzia maumbile yetu hadi tabia zetu. (hata wale ambao
wanachangia baba mmoja na mama mmoja).

Upekee huu pia umetufanya kuwa na utofauti wa hisia (mihemko).

Kwa kuzingatia ukweli kuwa binadamu tunategemeana ili kuendelea


kuishi kwa amani na furaha na kwa mafanikio, ni wazi kwamba
kutegemeana huku kunatokana na utofauti tulio nao.

Jaribu kufikiri, kama binadamu wote tungekuwa na tabia moja,


maumbile yanayo fanana, nguvu zinazolingana, vipaji vinavyo fanana,
hisia zinazo fanana nk. Ni nani angemtegemea mwenzake? Na
kungewa na umuhimu gani wa kuwa na marafiki? Au dunia
ingekuwaje?

Hivyo basi ni kwa uelewa wa elimu ya saikolojia inayotuwezesha na


kutusaidia kuanzisha mahusiano na kuyalinda ili tuendelee kusaidiana
na kushirikiana kupitia mbalimbali za kimaisha.

Pia upatikanaji wa elimu hii ya saikolojia sio kitu kigumu kama watu
wengi wanavyo dhani.

Kuipata elimu hii sio lazima uhudhurie mafunzo maalumu katika chuo
husika kwa sababu maisha yetu kwa asilimia kubwa yametawaliwa na
elimu hii ya saikolojia.

You might also like