You are on page 1of 9

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA


MASWALI YA KUJIPIMA KWA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA

03 MAARIFA YA JAMII NA STADI ZA KAZI

Muda: Saa 1:30 Mwaka : 2021

Maelekezo

1. Karatasi hii ina sehemu A na B zenye jumla ya maswali arobaini na tano (45).

2. Jibu maswali yote katika kila sehemu.

3. Soma maelekezo yote yaliyoko katika fomu maalumu ya kujibia (OMR).

4. Jaza taarifa zote katika fomu ya OMR.

5. Weka kivuli katika kila tarakimu ya Namba yako ya Mtihani kwenye nafasi husika katika fomu ya
OMR.

6. Weka kivuli katika herufi ya jibu sahihi kwa swali la 1 hadi 40 katika fomu yako ya kujibia uliyopewa.
Kwa mfano, kama jibu sahihi ni A weka kivuli kama ifuatavyo:

7. Ukigundua kuwa herufi uliyoweka kivuli si jibu sahihi, futa kivuli hicho kwa umakini kwa kutumia
kifutio safi kabla ya kuweka kivuli katika herufi mpya.

8. Tumia penseli ya HB tu katika kujibu swali la 1 hadi 40, na kalamu ya wino wa bluu au mweusi
kujibu swali la 41 hadi 45.

9. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mtihani.

Ukurasa wa 1 kati ya 9
SEHEMU A (Alama 40)
Jibu maswali yote katika sehemu hii.

Chagua jibu sahihi kisha weka kivuli kwenye herufi ya jibu lililo sahihi katika fomu maalum (OMR) ya
kujibia uliyopewa.
1. Ardhi ni rasilimali ambayo isipotunzwa vizuri inaweza kusababisha hatari katika maisha ya viumbe
hai na rasilimali nyingine. Ipi ni njia bora itakayotumika kutunza rasilimali hiyo kati ya zifuatazo?
A Kuongeza idadi ya wakulima mashambani
B Kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya ardhi
C Kuhimiza wafugaji kuongeza idadi ya mifugo
D Kuwahimiza wananchi kutumia mbolea za viwandani
E Kuhimiza upandaji miti katika maeneo ya wazi

2. Katika sikukuu ya wakulima, kauli mbiu iliyotolewa na Waziri Mkuu ilikuwa ni, “Kilimo ni uti wa
mgongo katika uchumi wa Tanzania”. Kauli mbiu hiyo ina maana gani?
A Ni shughuli inayofanywa na watu matajiri
B Hufanyika kwa kutumia matrekta na majembe ya kukokotwa na ng’ombe
C Ndio shughuli kuu ya uzalishaji mali
D Hufanyika sehemu zenye vyanzo vya maji pekee
E Mazao yanayovunwa huuzwa nje ya nchi

3. Mwalimu Kazimoto alifundisha kuhusu shughuli ya kilimo cha mazao ya biashara kilichofanywa
Tanganyika kabla ya uhuru. Je, wanafunzi walibaini mazao yapi ya biashara?
A Korosho, maharage, mkonge na pareto
B Mahindi, kahawa, chai na pareto
C Kahawa, pareto, mkonge na chai
D Zabibu, kahawa, chai na maharage
E Pareto, korosho, chai na mahindi

4. Wakulima wengi nchini Tanzania hupeleka mazao sokoni kuuza. Ni njia zipi kuu za usafirishaji
zinazotumika?
A Barabara na Reli B Anga na Barabara C Maji na Anga
D Reli na Anga E Maji na Barabara

5. Shughuli za kilimo huweza kuharibu ardhi ikiwa hazikufanyika kwa uangalifu. Ni kwa namna gani
kilimo kinaweza kuharibu ardhi?
A Kwa kutumia mbolea ya asili B Kwa kulima kwa kubadilisha mazao
C Kwa kulima matuta ya kukinga mteremko D Kwa kutumia mbolea za viwandani
E Kwa kupanda miti karibu na shamba

Ukurasa wa 2 kati ya 9
6. Shamba la Bwana Tembo ambalo lipo pembeni ya mlima Pina limepungukiwa na rutuba kutokana na
momonyoko wa udongo. Kama mtaalam wa mazingira ni nini chanzo cha momonyoko huo?
A Shamba kuwa katika mteremko mkali
B Shamba kuwa na miti mingi
C Samadi kuwekwa shambani
D Shamba kupandwa mazao mengi ya mizizi na nafaka
E Mazao kubadilishwa shambani kila mwaka

7. Shughuli za kibinadamu kando ya mto Matumaini huleta madhara kwa jamii inayouzunguka. Ni
madhara gani yanasababishwa na shughuli za ukataji miti ovyo pembeni mwa mto huo?
A Ukosefu wa maji viwandani
B Uchafuzi wa hewa
C Ardhi kupoteza rutuba
D Kukauka kwa vyanzo vya maji
E Kupungua kwa uvuvi

8. Wazo ni mkulima ambaye anataka kuanzisha kilimo katika eneo ambalo ni nusu jangwa. Kama Afisa
kilimo ni ushauri gani utampa?
A Kulima mazao yanayovumilia ukame
B Kuachana na shughuli za kilimo
C Kulima msimu wa mvua tu
D Kutumia mbolea ya viwandani tu wakati wa kilimo
E Kutumia samadi peke yake wakati wa kilimo

9. Ukiwa ni kiongozi wa klabu ya kutunza mazingira, utampa ushauri gani mtu anaye kata miti ovyo kwa
ajili ya kupata nishati?
A Kutumia nishati mbadala rafiki kwa mazingira
B Kujificha asikamatwe na Maafisa Misitu
C Kuhifadhi vyema mabaki ya miti iliyokatwa
D Kuuza kuni na mkaa kujiongezea kipato
E Kukata miti ya ndani ya misitu ili asijulikane

10. Ni tukio lipi la kihistoria lilitokea Tanganyika mwaka 1926?


A Kuanza kwa Vita Kuu ya Pili ya Dunia
B Kuanzishwa kwa chama cha African Association
C Kuanzishwa kwa Baraza la Bunge
D Uhuru wa Tanganyika
E Kuanzishwa kwa vyama vingi

Ukurasa wa 3 kati ya 9
11. Wanafunzi wa Darasa la Saba katika Shule ya Msingi Mwenge wanapanga safari ya kimasomo
kwenda kuona mabaki ya mifumo ya kilimo cha umwagiliaji iliyotumiwa na watu wa kale. Ni eneo
lipi la kihistoria utawashauri kutembelea?
A Engaruka B Amboni C Isimila
D Olduvai Gorge E Kondoa Irangi

12. Maeneo yafuatayo ya kihistoria yanapatikana Tanzania isipokuwa


A Rusinga B Olduvai Gorge C Engaruka
D Kondoa Irangi E Kaole

13. Historia ya ukombozi wa Tanzania ilianza na vyama vya ustawi wa wafanyakazi kama vile TTACSA
mwaka 1922 kilichobadilishwa kuwa TAA mwaka 1929 na baadae kuwa TANU mwaka 1954. Je, ni
kwa nini TAA ilibadilishwa kuwa chama cha TANU mwaka 1954?
A Kuwaunganisha watu wote katika kudai uhuru
B Kuwa chama cha kisiasa kwa ajili ya wafanyakazi tu
C Kuwaunganisha watu wote kupigana vita vya ukombozi
D Kuunganisha vyama vyote vya siasa katika harakati za ukombozi
E Kuwa chama cha kutetea ustawi wa wakulima

14. Wanafunzi wa Darasa la Sita walirekodi viwango vya jotoridi kuanzia Jumatatu hadi Jumapili kama
ifuatavyo: 200C, 320C, 300C, 240C, 270C, 270C na 220C mtawalia. Je, upi ni wastani wa jotoridi kwa
wiki?
A 200C B 320C C 270C D 26.20C E 260C

15. Umepewa jukumu la kutoa mafunzo kwa wanakijiji wa Kijiji cha Juhudi juu ya fursa mbalimbali za
kibiashara ambazo zinaweza kufanyika katika vipindi mbalimbali vya mwaka. Je, ungewashauri
kufanya biashara ya kuuza miavuli katika kipindi gani?
A Wakati wa Kiangazi B Wakati wa Kipupwe C Wakati wa Vuli
D Wakati wa Masika E Wakati wa Baridi

16. Wanafunzi wa Darasa la Nne walifundishwa kuhusu vipengele mbalimbali vya hali ya hewa. Ni kundi
lipi linawakilisha vipengele vya hali ya hewa walivyojifunza?
A Jotoridi, udongo, mvua na unyevuanga
B Anga, mwangajua, mgandamizohewa na upepo
C Maji, udongo, jotoridi na mawingu
D Mgandamizohewa, jotoridi, mvua na mwangajua
E Mvua, jotoridi mgandamizohewa na anga

Ukurasa wa 4 kati ya 9
17. Baraka anatafuta msaada wako kumwezesha kujibu swali kuhusu dhana ya “utamaduni”. Je, ni
vielelezo vipi vya utamaduni utakavyompa Baraka ili aweze kuielewa vizuri dhana hiyo?
A Lugha, mila na tohara B Mila, desturi na lugha
C Mila, desturi na miiko D Tohara, mila na desturi
E Lugha, mila na makumbusho

18. Ngoma za asili, uchongaji, uchoraji na maigizo ya jadi ni miongoni mwa mambo ya kitamaduni
yanayovutia watalii. Ni neno gani lifaalo kwa vipengele hivi vya utamaduni?
A Mila B Sanaa C Michezo D Lugha E Miiko

19. Kiongozi kutoka Wizara inayosimamia Utamaduni aliwataka vijana kuacha kushabikia tamaduni za
kigeni na kudharau tamaduni za Kiafrika. Je, nini lengo la ushauri huo?
A Kulinda maslahi ya wageni B Kulinda maslahi ya viongozi
C Kupata fursa ya kutembelea nchi za nje D Kulinda rasilimali za Taifa
E Kufurahia rasilimali za Taifa

20. Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Harambee husisitiza wanafunzi wake kushiriki katika michezo
ya jadi. Lipi kati ya yafuatayo ni lengo lake kuu?
A kukuza kufikiri na kucheza B kuwezesha maamuzi na kuwa mbinafsi
C kukuza kufikiri na kufanya maamuzi D kuongeza uzuri wa nyimbo na kufikiri
E kutanua utawala wa sheria na kufanya maamuzi

21. Fikiria umeteuliwa kuongea na mojawapo ya makundi rika katika jamii yako kuhusu mahusioano
mema miongoni mwao. Lipi kati ya yafuatayo ungelisisitiza?
A Kuheshimiana na kusaidiana B Kusaidiana na kugombana
C Kusalimiana na kudharauliana D Kuheshimiana na kubaguana
E Kuelewana na kuogopana

22. Kama kuna wazazi na watoto, hii ni familia ya awali. Je, familia hii itaitwaje baada ya vifo vya wazazi
wao?
A Familia pana B Familia ya watoto C Familia ya watoto yatima
D Familia tegemezi E Familia ya watoto wa mitaani

23. Ukoloni katika nchi nyingi za Kiafrika ulikuwa na hasara zaidi kuliko faida. Kama mwanahistoria, ipi
unadhani ni athari ya kijamii iliyotokana na ukoloni katika Tanganyika?
A Kusaini mikataba na watawala wenyeji na kuleta mazao mapya
B Kuanzishwa kwa elimu rasmi na kueneza Ukristo
C Kusaini mikataba na watawala wenyeji na kujenga barabara
D Kuanzishwa kwa mazao mapya na kuteua machifu kama watawala
E Kuleta elimu rasmi na kusaini mikataba na watawala wenyeji

Ukurasa wa 5 kati ya 9
24. Nchi nyingi za Afrika kuwa wanachama wa jumuiya mbalimbali inadhihirisha umuhimu wa jumuiya
hizo kwa nchi husika. Unadhani nini kitatokea endapo nchi itavunja uhusiano huo?
A Kutakuwa na maendeleo makubwa katika nchi
B Kushuka kwa uchumi na kudorora kwa amani
C Kutumia bidhaa za nchi nyingine na kukua kwa maendeleo
D Kuongeza wajuzi katika nchi na dunia
E Kupata fursa ya kuungana na mataifa tajiri

25. Mnamo robo ya mwisho ya karne ya 19, Mataifa ya Ulaya yaligombea maeneo ya Afrika kwasababu
walitaka malighafi, masoko, wafanyakazi na sehemu ya kuweka vitega uchumi. Maeneo yafuatayo
yaligombaniwa isipokuwa
A Maeneo ya kando kando ya Bahari au Ukanda wa Pwani
B Maeneo yenye hali ya hewa nzuri na ardhi yenye rutuba
C Maeneo yenye maziwa na mito mikuu
D Maeneo yenye utajiri wa madini na rasilimali nyingine
E Maeneo yenye viwanda vingi vya kuzalisha bidhaa

26. Mwalimu Julius Kambarage Nyerere anatambulika kuwa ni shujaa hapa Tanzania na Afrika kwa
ujumla. Ni nini kinachomfanya atambulike hivyo?
A Alihudhuria vikao vya UNO huko Ulaya
B Alipinga vikali aina zote za ubaguzi wa rangi na kidini
C Alipinga vikali urejeshwaji wa mfumo wa vyama vingi
D Aliwahamasisha Watanganyika kutumia mapambano ya silaha
E Alihamasisha mapinduzi katika kupigania uhuru

27. Kuanzia mwaka 1985 hadi 2015 Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliongozwa na marais watatu. Ipi
ni orodha sahihi ya Marais hao?
A Julius K. Nyerere, Ali H. Mwinyi and Bejamin W. Mkapa
B Julius K. Nyerere, Ali H. Mwinyi na Jakaya M. Kikwete
C Ali H. Mwinyi, Benjamin W. Mkapa na Jakaya M. Kikwete
D Julius K. Nyerere, Abeid A. Karume na John P. Magufuli
E Benjamin W. Mkapa, Jakaya M. Kikwete na John P. Magufuli

28. Mwalimu aliwaambia wanafunzi wake kuwa mistari ya latitudo huwa na mizingo tofauti tofauti
kutegemea na mahali ulipo. Ni mstari upi wenye mzingo mrefu kati ya hii ifuatayo?
A Tropiki ya Kaprikoni B Mzingo wa Aktiki C Mstari wa Ikweta
D Tropiki ya Kansa E Mzingo wa Antaktiki

Ukurasa wa 6 kati ya 9
29. Wakati wa kipindi cha somo la Maarifa ya Jamii mwalimu aliwapa wanafunzi ramani ya Tanzania
yenye vitu vya asili na vilivyotengenezwa na binadamu kwa lengo la kujifunza. Je, hiyo ilikuwa ni
ramani ya aina gani?
A Ramani za takwimu B Ramani za kisiasa C Ramani za kontua
D Ramani za topografia E Ramani za miji

30. Mtalii aliwasili nchini Tanzania kupitia uwanja wa ndege wa Kilimanjaro na kuelekea moja kwa moja
katika hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro bila ya kupokelewa na mwenyeji yeyote. Ni kifaa kipi kati ya
vifuatavyo kilimwezesha kufika huko?
A Skeli B Hali ya hewa C Ramani
D Mwelekeo wa jua E Picha

31. Bahati alichora ramani ya kijiji chao bila kuonesha kipimio cha ramani. Ni adhari ipi atakayoipata
mtumiaji wa ramani hiyo?
A Kushindwa kufahamu mipaka ya kijiji
B Kutofahamu ukubwa halisi wa kijiji
C Kutozitambua alama zilizotumika
D Maudhui ya ramani kutoeleweka
E Mazao ya chakula yaliyo kijijini kutoonekana vizuri

32. Fikiria kuwa umealikwa kama mtaalamu wa mambo ya hali ya hewa kuelezea umuhimu wa tabaka la
ozoni kwa jamii. Je, ungeeleza nini?
A Huzuia kansa ya ngozi B Huzuia mmomonyoko wa udongo
C Huongeza idadi ya watu D Husababisha kutengenezeka kwa mvua
E Huongeza uoto wa asili

33. Rafiki yangu alisafiri kwenda Ulaya kumtembelea shangazi yake kipindi cha likizo. Kulikuwa na
baridi kali iliyoambatana na mchana kuwa mfupi kuliko usiku. Je, hali hiyo inawakilisha msimu upi
wa mwaka?
A Kiangazi B Masika C Kipupwe D Vuli E Mvua

34. Wanafunzi wa Darasa la Tatu walijifunza kuwa, kuna sayari nane zinazounda mfumo wa jua ambazo
baadhi zipo mbali na nyingine zipo karibu na jua. Je, ni Sayari ipi miongoni mwa zifuatazo ipo karibu
zaidi na jua?
A Sumbula B Kausi C Zuhura D Zebaki E Dunia

35. Tanzania ni nchi iliyojaaliwa kuwa na madini ya aina mbalimbali. Ni kundi lipi kati ya yafuatayo
hujumuisha madini ya vito?
A Dhahabu, chumvi na chuma B Almasi, rubi na tanzanaiti
C Almasi, dhahabu na chuma D Cobalt, rubi na tanzanaiti
E Chumvi, dhahabu na almasi

Ukurasa wa 7 kati ya 9
36. Wanafunzi wa Darasa la Saba walipewa aina mpya ya vifungo kwa ajili ya mashati yao. Ni kanuni ipi
wanapaswa kuzingatia wakati wa kushona vifungo hivyo?
A Kuchagua uzi wenye rangi tofauti na vifungo walivyopewa
B Kuchagua sindano inayoendana na kitambaa cha shati
C Kuanza kushona mshono wa kushikiza
D Kutumia sindano kubwa kuliko tundu la kifungo
E Kupitisha uzi upande wa juu ya kitambaa cha shati

37. Umemtembelea shangazi yako na kupewa chumba kichafu cha kulala. Ni magonjwa gani unaweza
kuyapata kwa kulala kwenye chumba hicho?
A Kuharisha na kutapika B Kukohoa na kutapika
C Mafua na kifua D Malaria na kifua
E Kuharisha na mafua

38. Bwana Nzima amepanga kusafiri na amedhamiria kufungasha nyama kwa ajili ya safari yake.
Ungemshauri kutumia mojawapo ya njia zipi kuandaa nyama hiyo ili kuzuia kuharibika?
A Kukaanga, kuchemsha na kuchoma B Kuchemsha, kubanika na kukaanga
C Kutokosa, kukaanga na kuchoma D Kuchoma, kukaanga na kubanika
E Kuchoma, kubanika na kupika kwa mvuke

39. Mwalimu wa Stadi za Kazi aliwaongoza wanafunzi kufinyanga chungu na kuwapa mbinu za
kukikausha vizuri. Je, kuna umuhimu gani wa kukikausha chungu hicho?
A Kukifanya kiwe imara B Kukifanya kiwe na rangi nyeusi
C Ili kuweza kukiweka nakshi D Kukifanya kuwa na harufu ya kuungua
E Kukifanya kiwe chepesi

40. Mimi ni mbunifu, mwenye uthubutu na ninajituma katika kutimiza malengo yangu. Je, mimi ni nani?
A Mjasiriamali B Mtu mwenye ujuzi C Mfanyabiashara
D Mnunuzi E Muuzaji

SEHEMU B (Alama 10)

Katika swali la 41-45, andika majibu sahihi katika nafasi zilizoachwa wazi kwenye fomu maalum (OMR)
kwa kutumia kalamu ya wino wa bluu au mweusi.

41. Eleza kwa kifupi tofauti kati ya mjasiriamali mtumishi na mjasiriamali mfanyabiashara?

42. Mlipuko wa volkano katika kijiji cha Kikuu umeleta madhara kwa jamii. Bainisha madhara chanya
mawili ya mlipuko huo.

Ukurasa wa 8 kati ya 9
43. Bi Atupele aliwataka wanafunzi waorodheshe tabia ya nchi ya maeneo waliyotoka. Mmoja wa
wanafunzi alitaja kuwepo kwa mvua nyingi, kiwango cha juu cha jotoridi na uwiano mdogo wa joto
kwa mwaka mzima. Je, eneo hilo lina tabia gani ya nchi?

44. Tabu alitembelea kituo cha hali ya hewa kilichopo uwanja wa ndege wa Mwanza kuchukua takwimu
za hali ya hewa ya eneo hilo, na kuwasilisha takwimu hizo katika Jedwali kama ifuatavyo:

Mwezi J F M A M J J A S O N D
Mvua (mm) 800 800 1000 1200 1000 800 700 900 600 800 900 900
Jotoridi (0C) 18 18 24 28 24 18 16 19 20 18 19 19

(a) Ni mwezi upi ulikuwa na mvua na jotoridi kubwa?


(b) Ni aina ipi ya tabia ya nchi inawakilishwa na taarifa zilizopo kwenye jedwali?

45. Ni kwa nini Chifu Mkwawa alijulikana kama shujaa katika jamii yake?

Ukurasa wa 9 kati ya 9

You might also like